Saturday, 14 October 2023
𝗧𝗨𝗞𝗢 𝗧𝗔𝗬𝗔𝗥𝗜 𝗞𝗨𝗦𝗛𝗜𝗥𝗜𝗞𝗜𝗔𝗡𝗔 𝗡𝗔 𝗦𝗘𝗞𝗧𝗔 𝗕𝗜𝗡𝗔𝗙𝗦𝗜: 𝗲-𝗚𝗔
Na Mwandishi Wetu.
Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA), imeahidi kushirikiana na Benki ya NMB ili kuimarisha, kukuza na kuendeleza ujuzi na vipaji kwa vijana wa Kitanzania wabunifu na wale wanaosoma fani ya TEHAMA, katika Vyuo Vikuu mbalimbali nchini, kupitia programu maalum ya mafunzo kwa vitendo inayotolewa na e-GA kupitia Kituo chake cha Utafiti, Ubunifu na Uendelezaji wa Serikali Mtandao (eGOVRIDC).
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na Mkurugenzi Mkuu wa e-GA Mha. Benedict Ndomba, wakati wa kikao cha pamoja kati ya e-GA na Benki ya NMB kilichofanyika katika Makao Makuu ya ofisi za e-GA jijini Dodoma, kwa lengo la kujadili namna taasisi hizo zinavyoweza kushirikiana katika maeneo mbalimbali ya teknolojia.
Maeneo hayo ni pamoja na utafiti, matumizi ya teknolojia za kisasa, kuvumbua vipaji na kuviendelea kwa wavijana wabunifu wa Kitanzania, pamoja na kutoa fursa kwa vijana wavumbuzi na wabunifu ikiwa ni sehemu ya kuendeleza Sekta ya TEHAMA nchini.
Ushirikiano huo unatarajiwa kuongeza na kukuza fursa za ajira kwa vijana sambamba na kuimarisha uhusiano mzuri kati ya Serikali na sekta binafsi kwenye eneo la TEHAMA, alisema Ndomba .
“e-GA imekuwa ikishirikiana na Vyuo Vikuu mbalimbali nchini katika kuwapata vijana wenye ujuzi, hivyo makubaliano hayo kati ya e-GA na NMB ni muendelezo wa ushirikiano mazuri uliopo kati ya e-GA na wadau mbalimbali wa TEHAMA”, alifafanua Ndomba.
Aliongeza kuwa, katika kikao hicho taasisi hizo zimekubaliana kushirikiana na kuandaa mkataba wa makubaliano (MOU) ambapo baada ya kukamilika kwa mkataba huo, pande zote mbili zitakutana na kujadiliana namna ya utekelezaji wa makubaliano hayo.
“e-GA imekuwa ikiwatengeneza vijana wanaoshiriki programu maalum ya mafunzo kwa vitendo pamoja na utaratibu wa kujitolewa (interns and volunteering) kupitia kituo chetu cha utafiti na ubunifu, kwa kuwajengea uwezo zaidi ili kwenda sambamba na soko la ajira pamoja na mabadiliko ya sayansi na teknolojia yanayoibuka kila siku”, alisema Ndomba.
Aidha, Ndomba aliishukuru Benki ya NMB kwa kuona umuhimu wa kutengeneza wataalamu wazawa wa TEHAMA kupitia programu hiyo na kuwa, e-GA ipo tayari kushirikiana na benki nyingine zenye dhamira ya kuijenga Tanzania ya kidijitali katika sekta zote za serikali na binafsi.
Naye Meneja eGovRIDC Dkt. Jaha Mvulla alisema, e-GA ipo tayari kushirikiana na Benki ya NMB katika maeneo mbalimbali yanayolenga kukuza matumizi ya TEHAMA nchini ikiwemo eneo la rasilimali za miundombinu na vifaa vya TEHAMA vya kufanyia mazoezi na majaribio, ubunifu hasa maeneo ya teknolojia mpya, kujenga uwezo na uzoefu kwa vijana, mafunzo kwa vitendo, utafiti na machapisho, maonesho, mashindano mbalimbali ya kidigitali kwa ajili ya kuvumbua vipaji, na maeneo mengine yanayohusiana na jitihada za Serikali Mtandao na teknolojia za kifedha.
“e-GA ipo tayari kufanya kazi na NMB kupitia programu maalumu ya mafunzo kwa vitendo inayoendeshwa na eGovRIDC, ili kuchochea ubunifu katika matumizi ya teknolojia mpya zinazoibuka duniani ikiwemo Akili Bandia (AI), Machine Learning, Blockchain na matumizi yake kama vile kujenga ulewa wa teknolojia kama za Digital Currency na FinTech, Utengenezaji wa mifumo (System Development) kwa ajili ya kutatua changamoto zetu nchini na usalama mtandaoni (Cyber Security)”, alisema Dkt.Jaha.
Mkuu wa Kitengo cha Rasilimali Watu- Kituo cha Taaluma NMB Bi. Joanitha Rwegasira alisema kuwa, Benki ya NMB imeandaa programu hiyo ili kuongeza idadi ya vijana wabobezi kwenye masuala ya TEHAMA watakaofanya kazi katika sekta za umma na binafsi kwa lengo la kukuza taifa la kidijitali.
Programu hiyo itasaidia kufanya majaribio ya teknolojia mpya zinazoibuka ikiwemo Sarafu ya mtandaoni na kutoa suluhu kwenye maeneo mbalimbali yenye changamoto katika utendaji kazi na utoaji wa huduma kwa wananchi ikiwemo matishio ya usalama mtandaoni, ubunifu wa mifumo n.k, alisema Rwegasira
Aidha, aliishukuru Mamlaka kwa kuonyesha utayari wa kushirikiana na NMB na kwamba watatumia fursa hiyo katika kuhakikisha wanaboresha huduma za kibenki hususani huduma zinazotolewa kidijitali.
Friday, 13 October 2023
MRADI KITUO CHA KUPOZA UMEME CHALINZE WAFIKIA ASILIMIA 84.3
Na Mwandishi wetu,Pwani.
*Asisitiza Watanzania wanataka umeme*
*Atoa Pongezi kwa wafanyakazi kwenye mradi huo
*TANESCO wapongezwa kwa hatua ya ujenzi*
Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme wa Msongo wa kilovoti 400/220/132/33 wa kituo cha Chalinze umefikia asilimia 84.3 na hivyo kuleta matumaini ya kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme.
Hayo yameelezwa leo Oktoba 12, 2023 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko alipotembelea na kuzungumza na wafanyakazi wa kituo hicho cha Chalinze Mkoani Pwani, kujionea maendeleo ya ujenzi wa mradi huo.
"kwa sasa ujenzi umefikia asilimia. 84.3 na unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 31 Disemba, 2023. Mradi huu unakwenda kupunguza changamoto ya umeme kwa kiasi kikubwa hususan katika mkoa huu wa Pwani," amesema Dkt. Biteko.
Ameongeza kuwa, mara baada ya Mradi huo kukamilika, kituo hicho kitakuwa na uwezo wa kupokea Megawatt 2115 kutoka katika Bwawa la kuzalisha Umeme wa Maji la Julius Nyerere na kitasambaza Megawati 850 kwenye mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam na Pwani na kuimarisha hali ya upatikanaji umeme katika mikoa hiyo.
Akizungumza na wafanyakazi wanaofanya kazi katika mradi huo amewataka wafanye kazi kwa bidii kwa kuwa Serikali imewapa ushirikiano ili mradi huo ukamilike kwa wakati.
Meneja wa Mradi wa kituo hicho Mhandisi Newton Livingstone Mwakifwamba amesema kuwa Serikali imetoa ushirikiano mkubwa katika utekelezaji hususan katika mazingira mazuri ya wafanyakazi. Amesema mradi huo utakamilika kwa muda uliopangwa ifikapo mwezi Desemba 2023.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema toka kuanza kwa mradi huo hakuna changamoto iliyojitokeza kukwamisha mradi huo. Amempongeza Dkt. Biteko kwa kutembelea mradi huo kujionea maendeleo yake.
Naye, Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora amesema kuwa, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa katika utekelezaji wa mradi huo na kusisitiza kuwa mradi utakapokamilika utakua ni msaada mkubwa wa mkoa wa Pwani.
Mradi huo ulianza rasmi tarehe 6 Septemba, 2021 ambapo kazi za ujenzi zilianza tarehe 11 Oktoba, 2021 na unahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka JNHPP hadi Chalinze pamoja na kituo cha kupoza umeme na kusafirisha umeme kuelekea mikoa ya kaskazini kwa kuingizwa Kenya Gridi ya Taifa.
Ziara hiyo ilihudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mipango na Uwekezaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Decklan Mhaiki, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Halima Okash na Viongozi Mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Pwani na Watumishi wa mradi huo
KAMISHNA BENEDICT WAKULYAMBA AKAGUA MRADI WA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE
Thursday, 12 October 2023
SERIKALI KUONGEZA WODI MAALUM 100 ZA UANGALIZI WA WATOTO NJITI




TEA YASHIRIKI MAONESHO YA ELIMU YA WATU WAZIMA KIBAHA
MRADI KITUO CHA KUPOZA UMEME CHALINZE WAFIKIA ASILIMIA 84.3
Na Mwandishi wetu,Pwani.
*Asisitiza Watanzania wanataka umeme*
*Atoa Pongezi kwa wafanyakazi kwenye mradi huo
*TANESCO wapongezwa kwa hatua ya ujenzi*
Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme wa Msongo wa kilovoti 400/220/132/33 wa kituo cha Chalinze umefikia asilimia 84.3 na hivyo kuleta matumaini ya kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme.
Hayo yameelezwa leo Oktoba 12, 2023 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dkt. Doto Biteko alipotembelea na kuzungumza na wafanyakazi wa kituo hicho cha Chalinze Mkoani Pwani, kujionea maendeleo ya ujenzi wa mradi huo.
"kwa sasa ujenzi umefikia asilimia. 84.3 na unatarajiwa kukamilika ifikapo tarehe 31 Disemba, 2023. Mradi huu unakwenda kupunguza changamoto ya umeme kwa kiasi kikubwa hususan katika mkoa huu wa Pwani," amesema Dkt. Biteko.
Ameongeza kuwa, mara baada ya Mradi huo kukamilika, kituo hicho kitakuwa na uwezo wa kupokea Megawatt 2115 kutoka katika Bwawa la kuzalisha Umeme wa Maji la Julius Nyerere na kitasambaza Megawati 850 kwenye mikoa ya Morogoro, Dar es Salaam na Pwani na kuimarisha hali ya upatikanaji umeme katika mikoa hiyo.
Akizungumza na wafanyakazi wanaofanya kazi katika mradi huo amewataka wafanye kazi kwa bidii kwa kuwa Serikali imewapa ushirikiano ili mradi huo ukamilike kwa wakati.
Meneja wa Mradi wa kituo hicho Mhandisi Newton Livingstone Mwakifwamba amesema kuwa Serikali imetoa ushirikiano mkubwa katika utekelezaji hususan katika mazingira mazuri ya wafanyakazi. Amesema mradi huo utakamilika kwa muda uliopangwa ifikapo mwezi Desemba 2023.
Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Pwani Abubakar Kunenge amesema toka kuanza kwa mradi huo hakuna changamoto iliyojitokeza kukwamisha mradi huo. Amempongeza Dkt. Biteko kwa kutembelea mradi huo kujionea maendeleo yake.
Naye, Mbunge wa Jimbo la Chalinze Mhe. Ridhiwani Kikwete ambaye ni Naibu Waziri Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora amesema kuwa, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya kazi kubwa katika utekelezaji wa mradi huo na kusisitiza kuwa mradi utakapokamilika utakua ni msaada mkubwa wa mkoa wa Pwani.
Mradi huo ulianza rasmi tarehe 6 Septemba, 2021 ambapo kazi za ujenzi zilianza tarehe 11 Oktoba, 2021 na unahusisha ujenzi wa njia ya kusafirisha umeme kutoka JNHPP hadi Chalinze pamoja na kituo cha kupoza umeme na kusafirisha umeme kuelekea mikoa ya kaskazini kwa kuingizwa Kenya Gridi ya Taifa.
Ziara hiyo ilihudhuriwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mipango na Uwekezaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Decklan Mhaiki, Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo Mhe. Halima Okash na Viongozi Mbalimbali wa Chama cha Mapinduzi mkoa wa Pwani na Watumishi wa mradi huo




































.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)
.jpg)