Sunday, 13 November 2022

WANAHISA NICOL WASIFU KAMPUNI YAO

Mwenyekiti wa Kampuni ya Uwekezaji NICOL, Dk. Gideon Kaunda akizungumza na wanahisa wa kampuni hiyo kwenye Mkutano Mkuu wa nane uliofanyika siku ya Jumamosi jijini Dar es Salam Wanahisa wa Kampuni ya Uwekezaji NICOL wakifuatilia majadiliano yaliyokuwa kwenye mkutano mkuu wa nane wa kampuni hiyo uliofanyika siku ya Jumamosi jijini Dar es Salaam. Mmoja wa wanahisa wa kampuni ya uwekezaji NICOL, akichangia jambo wakati wa mkutano mkuu wa mwaka wa kampuni hiyo ambapo pamoja na mambo mengine ulipitisha gawio la Sh 20 kwa kila hisa Mwenyekiti wa Kampuni ya Uwekezaji NICOL, Dk. Gideon Kaunda akizungumza na wanahisa wa kampuni hiyo kwenye Mkutano Mkuu wa nane uliofanyika siku ya Jumamosi jijini Dar es Salam

*********************

Na Mwandishi Wetu

KAMPUNI ya Uwekezaji ya NICOL imepata faida ya shilingi bilioni nne na imepitisha gawio la Sh bilioni 1.2 kwa wanahisa wake litakalotolewa mwezi ujao.

Gawio hilo lilipitishwa siku ya Jumamosi katika maazimio ya Mkutano Mkuu wa nane wa mwaka wa wanahisa uliofanyika kwa njia ya video kwenye mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza, Mbeya na Arusha.

Akizungumza mara baada ya mkutano huo, Ofisa Mtendaji Mkuu wa NICOL, Erasto Ngamilaga, alisema Mkutano Mkuu ambao umefanyika ni takwa la kisheria kwa makampuni kama hayo kufanya na wanahisa wake wote.

Alisema kwenye mkutano huo wamehudhuria wanahisa wa mikoa ya Mwanza, Mbeya, Arusha na Dar es Salaam ambapo wale wa mikoani walifuatilia mkutano huo kupitia mtandao.

Alisema kwenye mkutano huo wamepata fursa ya kuwaeleza wanahisa namna kampuni ilivyopata faida ya Sh bilioni nne kabla ya kodi na Sh bilioni 3.8 baada ya kodi.

Alisema wanahisa wamepitisha gawio la Sh 20 kwa kila hisa ambayo itaanza kulipwa 15.12.200 na kwamba ni ongezeko la gawio la Sh 17 ambalo lilishalipwa kwenye mahesabu ya mwaka 2021.

“Wanahisa wamefurahi sana kuona kampuni inafanya vizuri na sisi viongozi tumewaaahidi kuweka mikakati mizuri zaidi kuhakikisha kampuni inazidi kusonga mbele na kupata faida kubwa zaidi siku za usoni,” alisema Ngamilaga



Mwenyekiti wa Bodi ya NICOL, Dk. Gideon Kaunda, alisema kampuni hiyo imekuwa ikitoa gawio kila mwaka na aliishukuru bodi mpya kwa kuwekeza sehemu mbalimbali hasa kwenye hati fungani za serikali.

Alisema kampuni hiyo imewekeza asilimia 30 ya uwekezaji wake kwenye hati fungani na ndiyo sababu kampuni hiyo imeendelea kupata faida mwaka hadi mwaka na kuwapa gawio zuri wanahisa wake .

Alisema wanahisa wa NICOL nchi nzima wanafikia 30,000 na wamesambaza sehemu za mikutano ili kuwafikia wanachama wengi badala ya kulazimika kuja Dar es Salaam kwenye mKutano Mkuu wa mwaka.

“NICOL inapenda kuona wanahisa wake wanapata gawio kila mwaka na kweli kampuni imefanya vizuri na gawio limeongezeka kutoka Sh 17 na sasa tutalipa sh 20 kiwango ambacho kampuni zingine zimeshindwa kufikia na tunadhani mwakani tutazidi kuongez gawio kubwa zaidi kwa wanahisa wetu,” alisema

Mwanahisa Mutamwega Mugaywa, alisema anashukuru kuona kampuni ya NICOL imesimama na kuonyesha matumaini makubwa kwa wanahisa wake.

“Nifuraha kubwa kuona NICOL inabeba uchumi na nawashauri watu wengine waje wanunue hisa zao mapema NICOL kwasababu kuna faida nyingi kuwa mwanahisa wakampuni ya wazalendo,”

“Nawapongeza viongozi kwa kusimamia vizuri Kampuni na sasa tunapata gawio zuri nawashauri wengine nao wachangamkie hisa za kampuni yetu,” alisema

Mwanahisa mwingine, Suzana Masele alimongeza Mwenyekiti wa Bodi ya kampuni hiyo, Dk. Gieon Kaunda kutokana na anavoisimamia kampuni hiyo na menejimenti nzima.

“Nampongeza kwani anavyoisimamia vizuri kamouni utadhani ni kampuni yake binafsi ukiangalia ilipokuwa huko nyuma ilikuwa kama imekufa lakini mwenyekiti wa sasa anajua anachofanya na tunaelekea pazuri zaidi,” alisema
Share:

MTANZANIA MZALENDO ALIYEWAPELEKA ZAIDI YA WATANZANIA 2000 MAREKANI KUTUNUKIWA CHETI CHA HESHIMA

Bishop Dr Suleiman Elisha Mjumbe na katibu wa Bodi (TWWT) kushoto akimkabidhi cheti Dr Nathanael Kigwila Kulia kwake, Kushoto kwa ni Mke wa Kigwila Bi Gloria Kigwila pamoja na mtoto wao Enock Kigwila. Octavian Mutayoba Katibu Mtendaji TWWT, kulia, akimkabidhi Dr Nathanael Kigwila kofia pamoja na Tshirt kwa ajili ajili ya ubalazo wa Taasisi hio nchini Marekani

****************************

Mwakilishi wa waziri wa mambo ya ndani ya nchi Bishop Dr Suleman Elisha leo hii amemtunuku Bishop Dr Nathanael Kigwila cheti cha heshima kutambua mchango wake kwa taifa kama mtanzania anayeishi Nchini marekani cheti hicho kimetolewa katika hafla za kuhitimisha mafunzo ya kiroho na uzalendo yaliyofanyika kwa takribani siku nne katika ukumbi wa kanisa la The Growing Mission Church (GMC) lililopo Mapinga Pwani.

Halfa hio imeuzuiliwa na viongozi mbalimbali wa Taasisi ya TWWT akiongoza Dr Ezekiel Kyogo ambaye ni mwenyekiti wa Taasisi ya wananchi wazalendo na mratibu msaidizi wa polisi makao makuu ya polisi Dodoma Octavian Mutayoba katibu mtendaji TWWT na Ayubu Musa afisa mahusiano wa TWWT.

Taasisi ya Wananchi Wazalendo Tanzania (TWWT) imemtunukia Bishop Nathaniel Kigwila Mtanzania anayeishi Nchini Marekani kwa kutambua kazi mbalimbali ambazo amekuwa akizifanya nchini pamoja na kukaribisha wawekezaji kutoka nchini Marekani .

Akizungumza wakati wa kuhitimisha mafunzo Dr Ezekiel Kyogo amesema ni watanzania wachache wanaoishi nchi za nje na wanakumbuka kuwekeza nyumbani nchini Tanzania kama alivyofanya Dr Nathanael Kigwila, kutokana na mchango wake huo taasisi hiyo pia imemteua Bishop Kigwila kuwa balozi wa Taasisi hiyo nchini Marekani ili kuendelea kuhamasisha uzalendo na kuipenda Tanzania.

Dr Nathanael Kigwila ameishi nchini marekani kwa Zaidi ya miaka 30 na katika kipindi hiko amefanikiwa kupeleka Zaidi ya watanzania 2000 kupata mafunzo mbalimbali, Pamoja na kupeleka wanafunzi hao Nchini Marekani pia Bishop Kigwila amefanikiwa kuleta wawekezaki ambao wamewekeza katika Dawa za binadamu kwa kujenga viwanda katika mkoa wa Pwani pamoja na kupeleka dawa hizo katika jeshi la Zanzibar KMKM, Uwekezaji wa kilimo cha viungo unaoendelea katika kijiji cha Mkange Halmashauri ya Chalinze wilaya ya Pwani uliojiri Zaidi ya watanzaia 50 pia Kiwanda cha kusaga unga kilichopo eneo la mlingotini Mkoani Pwani, sambamba na hayo Dr Nathanael Kigwila anahudumia Zaidi ya watoto yatima 150 wakishirikiana na wawekezaji na makanisa kutoka nchini Amerika.

Tunamshukuru Mungu alieyetufanikisha kufanya hivyo, kila mtu ana kitu na kusudi la kufanya ambalo Mungu ameliweka katika maisha yetu, tutaendelea kujitahidi kutumia nguvu na nafasi ambazo Mungu ametupa kuendelea kusaidia watu wengi Zaidi ameongea Bishop Nathanael baada ya hafla hiyo.

Bishop Dr Nathanael Kigwila ambaye pia ni mchungaji kiongozi wa kanisa la GMC ndiye aliyeratibu mafunzo hayo ya kiroho kwa viongozi mbalimbali wa makanisa kutoka katika madhehebu mbalimbali. Mafunzo hayo yalidumu kwa siku 4 yaliongozwa na wakufunzi mbalimbali kutoka nchini Tanzania, Kenya na Marekani.

Wakufunzi hao ni pamoja na Mwinjilisti Terry L Anderson, Jonathan Yergin, Anne Yergin and Trent Radbil kutoka kanisa la Wildwood Baptist lililopo Jimbo la Atlanta nchini Marekani, wakufunzi wengine ni Dr Anne Kiteme kutoka Kenya, Bishop Deo Lubala na Bishop Charles Gadi, Pamoja na Dr Ezekiel Kyogo.

Wakufunzi hao wamefundisha mambo mengi yanayohusu uongozi wa viongozi wa kiroho katika kuhamasisha jamii kupata mabadiliko chanja, pamoja na mafundisho hayo Dr Ezekiel Kyogo amefundisha somo la uzalendo kwa kipindi chote cha mafunzo na kumtaja Dr Nathanael Kigwila kama mfano wa kuigwa na watanzania wengi kwa kuipenda na kuitangaza nchi yake.

Obedi Mwakipiti mshiriki na mwimbaji katika mafunzo hayo amewasifu wakufunzi hao kutoka nchi mbalimbali na kusema wameongeza kitu kikubwa sana katika maisha yake, amejifunza namna sahiihi ya kusoma na kuielewa biblia pamoja na namna nzuri ya kuishi na watu wenye mitazamo ya Imani tofauti.

Kwa upande mwengine, Jackline Lukosya Mshiriki katika mafunzo hayo amejifunza mambo mengi yakiwemo malezi ya familia hasa kushirikiana kati ya baba na mama somo lililofundishwa na Dr Ezekiel Kyogo pamoja na hayo amemsifu Dr Nathanael Kigwila kuwa kuwa mpambanaji katika masuala ya kiroho na katika uwekezaji nchini Tanzania.

Dr Nathanael Kigwila ametoa wito kwa watanzania waliopo nje ya nchi kuendelea kukumbuka nyumbani na Zaidi kuendelea kuwekeza nchini Tanzania, pia Dr Kigwila ameiomba serikali kufanikisha suala la Uraia pacha ambao utamuwezesha mtanzania aneyeishi nje ya nchi kufanya mambo Mengi.

Share:

PURA YATOA UELEWA MASUALA YA MAFUTA NA GESI KWA MAMLAKA ZA UTOAJI VIBALI KWA RAIA WA KIGENI

Timu ya Wataalamu kutoka Mamlaka Zinazohusika na Utoaji wa Vibali vya Kazi na Ukazi Kwa Raia Wa Kigeni Wanaokuja Kufanya Kazi Katika Miradi Mbalimbali Nchini Wakitembezwa Katika Mitambo ya Kuchakata Gesi Asilia Iliyopo Madimba Mkoani Mtwara. Wengine Katika Picha ni Wataalamu kutoka GASCO, Wataalamu Kutoka PURA, Wataalamu Kutoka NEEC na Taasisi ya UONGOZI.

Sehemu ya Wataalamu kutoka Ofisi Zinazohusika na Utoaji wa Vibali Vya Kazi na Ukazi Wakipatiwa Maelezo Kutoka kwa Meneja wa Kitalu cha Mnazi Bay kutoka kampuni ya Maurel and Prom, Bw. Laurent Jars mara baada ya Timu hiyo Kufika Eneo Hilo kwa Ziara ya Kikazi.


Wataalamu kutoka Ofisi Zinazohusika na Utoaji wa Vibali Vya Kazi na Ukazi Wakipatiwa Maelezo Kutoka kwa Mtaalamu kutoka Kiwanda cha Saruji cha Dangote kuhusu miundombinu ya kujaza gesi asilia kwenye magari inayomilikiwa na Kiwanda hicho

**********************

Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imefanikisha ziara maalum kwa mamlaka zinazohusika na utoaji wa vibali vya kazi na ukazi kwa raia wa kigeni wanaokuja nchini kufanya kazi katika miradi mbalimbali ikiwemo miradi ya mafuta na gesi asilia.

Ziara hiyo iliyofanyika hivi karibuni ililenga kuzijengea uelewa mamlaka husika kuhusu shughuli za utafutaji, uendelezaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia nchini.

Mamlaka hizo ni Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora), Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu) na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi (Idara ya Uhamiaji).

Ziara ilihusisha kutembelea miundombinu ya kuzalisha na kuchakata gesi asilia iliyopo eneo la Mnazi Bay Mtwara inayoendeshwa na kampuni ya Maurel and Prom na mitambo ya kuchakata gesi asilia inayoendeshwa na GASCO (kampuni tanzu ya Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania - TPDC) iliyopo eneo la Madimba Mtwara.

Ziara pia ilihusisha kutembelea miundombinu ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia na kituo cha kujaza gesi asilia kwenye magari kinachomilikiwa na Kiwanda cha Saruji cha Dangote pamoja na mradi wa kusambaza gesi asilia majumbani katika eneo la Bandari - Mtwara, mradi uliotekelezwa na unaoendeshwa na GASCO.

Akizungumza mara baada ya ziara, mjumbe kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Bw. Suleiman R. Seng'enge alisema kuwa ziara hiyo imekuwa na manufaa makubwa kwa kuwa imeongeza wigo wa uelewa kuhusu masuala ya mafuta na gesi, jambo ambalo litasaidia wakati wa kuchakata maombi ya vibali kwa raia wa kigeni wanaotaka kufanya kazi katika miradi ya mafuta na gesi asilia nchini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa Wazawa na Uhusishwaji wa Wadau, Bw. Charles Nyangi alisema kuwa, ziara hiyo itasadia katika utekelezaji wa matakwa ya kisheria ya ushiriki wa watanzania katika shughuli za mafuta na gesi asilia nchini.

Kwa mujibu wa Sheria ya Petroli ya mwaka 2015, wakandarasi wanaotekeleza miradi ya mafuta na gesi asilia nchini wanapaswa kutoa kipaumbele cha ajira kwa watanzania kabla ya kuajiri raia wa kigeni. Aidha, Sheria hiyo pia inataka wakandarasi hao kutoa kipaumbele kwa huduma na bidhaa zinazopatikana nchini kabla ya kuagiza bidhaa hizo kutoka nje ya nchi.

Miongoni mwa majukumu ya PURA kwa mujibu wa Sheria hiyo ni kusimamia masuala ya ushiriki wa watanzania katika shughuli za utafutaji, uendelezaji na uzalishaji wa mafuta na gesi asilia nchni.
Share:

HESLB YAFUNGUA DIRISHA LA RUFAA KWA SIKU SABA


************************

*Kuwa wazi kwa siku saba (07) hadi Novemba 20

*Wanafunzi 68,422 wa mwaka wa kwanza wapangiwa mikopo hadi sasa

Jumapili, Novemba 13, 2022

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetangaza leo (Jumapili, Novemba 13, 2022) imetangaza kufunguliwa kwa dirisha la rufaa ili kutoa fursa kwa wanafunzi ambao hawakuridhika na viwango vya mikopo walivyopangiwa kuwasilisha taarifa za uthibitisho ili kuongezewa viwango vya mikopo kulingana na uhitaji wao.

Muda wa kuwasilisha rufaa

Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB, Abdul-Razaq Badru (pichani) amesema dirisha hilo la rufaa litakuwa wazi kwa siku saba (07) kuanzia leo, Novemba 13 hadi 20 mwaka huu na kuwa rufaa kutoka kwa wanafunzi zinapaswa kuwasilishwa kwa njia ya mtandao.

“Hadi leo (Novemba 13, 2022), tumeshawapangia mikopo wanafunzi wa mwaka wa kwanza wapatao 68,422 na tunafahamu kuwa kuna wanafunzi ambao kwa sababu mbalimbali, hawakukamilisha nyaraka muhimu kuthibitisha uhitaji wao, dirisha la rufaa ni fursa kwao,” amesema Badru.

Kwa mujibu wa Badru, lengo ni kutoa mikopo kwa wanafunzi wapya 71,000 katika mwaka wa masomo 2022/2023 na kuwasihi wanafunzi wanaowasilisha rufaa kusoma na kuzingatia maelekezo yaliyopo kwenye mfumo wa kuwasilisha rufaa.

Malipo ya fedha kwa waliopangiwa

Kuhusu malipo, Badru amesema HESLB fedha zilianza kutumwa vyuoni hata kabla ya wanafunzi kufika vyuoni na kuwa kazi hiyo ni endelevu na kuwashauri wanafunzi waliopangiwa mikopo kufika kwa maafisa mikopo wa vyuo vyao ili kukamilisha taratibu za kupokea fedha.

“Pale mwanafunzi anapoona amepangiwa mkopo kupitia yake ya SIPA (Student’s Individual Permanent Account), basi afike kwa afisa mikopo wa chuo chake ambaye yupo palepale chuoni ili awasilishe taarifa zake za benki na kupokea fedha,” amesema Badru.

Shukrani kwa vyuo, serikali za wanafunzi

Wakati huohuo, Badru amezishukuru taasisi za elimu ya juu na serikali za wanafunzi kwa ushirikiano wanaoipatia HESLB ambao umeendelea kuimarisha ufanisi katika kuwahudumia wanafunzi wanaonufaika na mikopo ya elimu ya juu inayotolewa na Serikali kupitia HESLB.

“Kwenye huu mnyororo wa kuwahudumia wanafunzi, uongozi wa vyuo, serikali za wanafunzi na jumuiya yao ya TAHLISO ni wadau muhimu … na wamekuwa wakitupatia ushirikiano mkubwa, tunawashukuru sana,” amesema Badru.

HESLB ilianzishwa mwaka 2005 ikiwa na majukumu makuu mawili, kutoa mikopo kwa wanafunzi wahitaji wa elimu ya juu na kukusanya mikopo iliyoiva ambayo imetolewa na serikali kutoka mwaka 1994/1995.

Imetolewa na:

BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

DAR ES SALAAM

Jumapili, Novemba 13, 2022

Taarifa hii pia inapatikana kwenye tovuti www.heslb.go.tz na mitandao ya kijamii ya twitter na Instagram kwa anuani ya ‘HESLB Tanzania’
Share:

Saturday, 12 November 2022

MAAFISA AFYA MKOA WA DAR ES SALAAM WAPATIWA MAFUNZO YA UFUATILIAJI WASHUKIWA WA UGONJWA WA EBOLA.


*****************

Na Mwandishi Wetu - Dar es Salaam

Wizara ya Afya imeendesha mafunzo kwa Maafisa Afya 100 wa Mkoa wa Dar es Salaam kwaajili ya ufuatiliaji wa tetesi au washukiwa ambao wametoka katika nchi ambazo zinamaambukizi ya Ebola.

Akizungumza katika Mafunzo hayo leo Novemba 12,2022 Jijini Dar es Salaam Mtaalamu wa Magonjwa kutoka Wizara ya Afya Dkt.Biseko Palapala amesema mafunzo hayo ni kuwaweka wataalamu utayari endapo ikatokea mlipuko wawe na uwezo wa kufuatilia wale wote ambao watashukiwa ambao ni wasafiri watakaoingia nchini wakiwa na maambukizi ya virusi vya Ebola.

"Tunawapa ili kuwajengea uwezo kwasababu siku zote ugonjwa unatakiwa utambulike mapema pamoja na kutambua yule ambaye alikuwa na dalili za ugonjwa amekutana na watu gani ili kusudi wale watu wafuatiliwe kupunguza usambazaji wa ugonjwa". Amesema Dkt.Palapala.

Amesema Tanzania ni moja ya nchi ambazo ipo katika hatari ya kupatikana na maambukizi ya Ebola kwasababu inapakana na nchi ya Uganda ambayo tayari virusi vimeshaeneo nchini humo.

Aidha amesema Tanzania na Uganda ni nchi ambazo zinamuingiliano hivyo ili kuweza kupunguza kasi ya maambukizi ya ugonjwa lazima wafuatilie wale ambao wamekutana na yule mtu ambaye anamaambukizi.

Amesema mafunzo ni ya siku tano ambapo siku tatu za mwanzoni watakuwa wanatoa mafunzokwa maafisa afya lakini pia siku mbili watakuwa wanafundisha wale ambao watahusika na jamii moja kwa moja.

Amesema mafunzo hayo pia yanaendelea kutolewa katika mikoa mingine ikiwemo mkoa wa Kagera ili kusudi wataalamu waliopo kwenye mikoa mingine waweze kupatiwa uwezo ili kupambana na maambukizi ya Ebola.

Kwa upande wake Afisa Afya wa Jiji la Dar es Salaam, Bi.Siriel Killeo Amesema "mafunzo haya yamenijengea uwezo na utayari wa kuweza kufuatilia endapo kutakuwa na tatizo lolote la Ebola nchini kwasababu bila ya kuwa na utayari wakati janga likitokea inakuwa ni shida".

Nae Afisa Afya wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw.Ally Kasembe amesema fursa waliyoipata wataenda kuitumia vizuri katika utekelezaji kwani elimu ambayo wamepatiwa ni bora na huenda ikaleta faida kubwa hapo baadae kwa maana haifahamiki kama maambukizi hayo yanaweza kuingia nchini ama la, hivyo tahadhari ni muhimu.
Share:

NDALICHAKO AMPONGEZA PROF MJEMA WA CBE

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako akimkabidhi cheti mmoja wa wahitimu kwenye mahafali ya 57 ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE) Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako akikata utepe kuzindua jingo la maktaba la Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), kabla ya mahafali ya 57 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye viwanja vya chuo hicho jijini Dar es Salam ambapo wahitimu 1,065 walitunukiwa vyeti vya ngazi mbalimbali.Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako akizungumza kwenye Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), katika mahafali ya 57 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye viwanja vya chuo hicho jijini Dar es Salam ambapo wahitimu 1,065 walitunukiwa vyeti vya ngazi mbalimbali. Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Exaud Kigahe akizungumza kwenye mahafali ya 57 ya Chuo cha Elimu ya Biashara (CBE), leo Jumamosi
Sehemu ya wahitimu wa Chuo cha Elimu ya Biashara CBE wakiwa kwenye mahafali yao leo Jumamosi

*********************

Na Mwandishi Wetu

SERIKALI imevitaka vyuo kuzingatia mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi vyuoni ili kuondoa malalamiko kutoka kwa waajiri kwamba wahitimu wengi wanahitimu bila kuwa na ujuzi unaohitajika kwenye soko la ajira.

Hayo yamesemwa leo Jumamosi na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Profesa Joyce Ndalichako, wakati akizungumza kwenye mahafali ya 57 ya chuo hicho yaliyofanyika kwenye viwanja vya chuo hicho jijini Dar es Salam ambapo wahitimu 1,065 walitunukiwa vyeti vya ngazi mbalimbali.

Alisema hali hiyo imekuwa ikisababisha na mafunzo mengi kufanyika kwa madharia bila vitendo na alipongeza chuo cha CBE kwa kuanzisha program ya uanagenzi ambapo mwanafunzi anasoma nusu ya masomo chuoni na nusu akiwa sehemu ya kazi.

“Malalamiko ni kwamba wahitimu wengi wanatoka vyuoni wakiwa na ujuzi ule ambao siyo unaohitajika kwenye soko la ajira na soko linahitaji rasilimali kazi ambayo vyuo havitoi kwa ukamilifu wake kutokana na kukosekana kwa mafunzo ya vitendo,” alisema

“Ndiyosababu naipongeza CBE kwa kuanzisha program ya uanagenzi ambayo mwanafunzi anakua darasani kwa asilimia 50 na anakuwa sehemu ya kazi kwa asilimia 50 na kwa kufanya hivi unatatua changamoto iliyokuwepo ya kuwa na wahitimu ambao hawana ujuzi sawasawa,” alisema

Alipongeza pia kuanzishwa kwa program atamizi kutoa nafasi kwa vijana kuatamia ujuzi wao kwamba vyuo vingine kama Mzumbe, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) na Chuo Kikuu cha Kilimo Sokoine (SUA) vimeshaanzisha program kama hizo.

Alisema kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu inatoa mafunzo ya uanagenzi ili kuhakikisha kama kuna kitu kimepungua kwa mwanafunzi kabla ya kuhitimu anapata ujuzi kwa vitendo kwa udhamini wa serikali.

Alisema serikali katika mwaka wa fedha wa 2021/2022 ilitenga Sh bilioni 9 ambazo ziliwezesha vijana zaidi ya 62,000 kupata mafunzo ya uanagenzi na katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 kwaajili ya kuendelea kutoa mafunzo ya uanagenzi.

Alimpongeza Profesa Emmanuel Mjema kwa kazi nzuri aliyoifanya akiwa mkuu wa chuo hicho kwa kipindi cha miaka 10 kwani chini yake chuo kimepata mabadiliko makubwa kitaaluma kwani alikipokea kikiwa katika hali mbaya.

“Wanafunzi mmefanya kazi nzuri sana kufaulu mitihani yenu na pia napenda kuwapongeza wazazi kwa kuwasomesha wanafunzi hawa nanapenda kuwaambia kwamba hawajapoteza kitu kwasababu hakuna urithi mzuri unaoweza kupita elimu hapa duniani,” alisema

Profesa Ndalichako aliwataka wahitimu hao kutumia elimu waliyopata kwa manufaa yao wenyewe na kwa jamii kwani ulimwengu wasasa unahitaji watu wenye ujuzi na wenye upeo wa kisasa wenye uwezo wa kutatua changamoto zinazoikabili jamii.

Alisema kukua kwa kwa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano ni kubwa sana hivyo inahitaji watu waendelee kujielelimsisha kwasababu mambo yanaenda yakibadilika siku hadi siku.

“Wahitimu msichoke kujielimisha na wala msidhani mmefika mwisho kwasababu dunia inakwenda kwa kasi sana na unachokijua leo baada ya mwaka au miaka miwili unaweza kukuta kimebadilika kabisa kwa hiyo endeleeni kutafuta maarifa kulingana na mabadiliko yanayojitokeza,” alisema
Share:

AMUUA MAMA YAKE KISA KAPEWA CHAKULA KIDOGO

 


Familia moja kutoka kijiji cha Bomeroka huko Kitutu Chache kaunti ya Kisii nchini Kenya inaomboleza ajuza aliyeuawa na mwanawe.

Jamaa huyo mwenye umri wa miaka 34, anayesemekana kuwa mraibu wa dawa za kulevya, aliripotiwa kupandwa na mori baada ya kuhisi kuwa kiasi cha chakula alichotengwa kilikuwa kidogo.

Kulingana na mfanyakazi wa shambani wa nyumba hiyo, mshukiwa alitaka kula chakula chote cha mchana ambacho kilikuwa kimetayarishwa kwa ajili ya familia nzima.

Marehemu alipomsihi asichukue chakula chote, alinyakua panga na kumrukia mara moja akamkata mkono.

“Alitaka kuchukua chakula chote mamake alipomtaka awafikirie ndugu zake ambao walikuwa bado hawajala, alipandwa na mori na hapo mara moja akamjeruhi vibaya kwa panga,” alisema mfanyakazi huyo.

Mwanamke huyo alikata roho kutokana na kuvuja damu nyingi akikimbizwa hospitalini.


Chanzo: TUKO.co.ke
Share:

EWURA, RC DENDEGO WAHAMASISHA UTALII RUAHA




BAADHI ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), wakiwa katika hifadhi ya Ruaha iliyopo mkoani Iringa baada ya kutembelea na kujionea utalii lwa ndani leo Novemba 11,2022.


Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa EWURA ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Mhandisi Modeatus Lumato,(katikati) akiwa Hifadhi ya Ruaha iliyopo Mkoani Iringa ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani.Wengine ni Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Ndani Baptista Mgaya ( kushoto) na kulia ni Meneja TEHAMA wa Mamlaka hiyo ambao ni wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi.


SEHEMU ya Wanyama waliopo katika Hifadhi ya Ruaha iliyopo Mkoani Iringa.


BAADHI ya Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA),wakiwa katika picha ya pamoja ndani ya hifadhi ya Ruaha iliyopo mkoani Iringa baada ya kutembelea na kujionea utalii wa ndani leo Novemba 11,2022.

.................................................

Na Mwandishi Wetu-IRINGA

Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Leo 11 Nov 2022, wamezuru Hifadhi ya Wanyama Ruaha kujionea vivutio mbalimbali na kuchangia ukuaji wa mapato yatokanayo na utalii nchini.

Wajumbe hao ni miongoni mwa wadau walioshirikiana na uongozi wa Mkoa wa Iringa kufanya ziara hiyo iliyoongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Halima Dendego kwa lengo la kuhamasisha watanzania kujiwekea desturi ya kutembelea hifadhi hiyo na vivutio mbalimbali vinavyopatikana mkoani humo.

Akizungumzia wakati wa ziara hiyo, Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa EWURA, ambaye ndiye Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Mhandisi Modestus Lumato amesema wajumbe wa Baraza wameona ni vyema kuunga mkono jitahada za Mkoa wa Iringa na za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan katika kuhamasisha na kutangaza utalii.

"Sisi wajumbe wa Baraza baada ya kutembelea hifadhi hii ya Ruaha, tutakuwa mabalozi katika kutoa hamasa kwa wenzetu tuliowawakilisha ili hata wasipokuja wakiwa kazini, waweze kuja na familia zao hapa," ameeleza Mhandisi Lumato

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe,Halima Dendego, amesema "Niwaeleze tu kwamba, mkoa wetu wa Iringa kwa kushirikiana na mikoa ya Nyanda za Juu Kusini tumejipanga na kujizatiti kufungua utalii wa ndani, hivyo niwaombe watanzania wenzetu tuunge mkono kwenye hili."

Naye Mjumbe wa TUGHE Tawi la EWURA Bi .Stephania Bachubire, ameeleza kufurahishwa kwake na ziara hiyo na ametumia fursa hiyo na kuiomba Menejimenti ya EWURA kuandaa ziara kama hiyo kwa wafanyakazi wote.

Hifadhi ya Ruaha ina uoto asili wa kuvutia, ikiwamo mto Ruaha wenye viboko wengi na mamba sanjari na wanayama wengine kama tembo, chui, simba,nyati, ngiri,twiga, pundamilia, na wanyama jamii ya swala.

Wajumbe wapatao 60 wa Baraza la Wafanyakazi wa EWURA pamoja na wajumbe wa TUGHE wameshiriki ziara hiyo.
Share:

WADAU WATAKA KITABU CHA SAMIA KUTAFSIRIWA KWA LUGHA YA KISWAHILI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.


Na Dotto Kwilasa,DODOMA

BAADA ya uzinduzi wa kitabu cha Rais Samia Suluhu Hassan,baadhi ya wadau wa lugha ya kiswahili wameshauri kitabu hicho kutafsiriwa kwa lugha ya kiswahili ili kuyafikia makundi yote.

Hatua hiyo imekuja baada ya kitabu hicho kilichopewa jina la "Continuity with Vision the Roadmap to Success for President Samia Suluhu Hassan"kuzinduliwa juzi jijini Dodoma na waziri wa elimu,Sayansi na Teknolojia Prf.Adolf Mkenda kwa niaba ya Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa . 

Mmoja wa wadau hao Hosea Steven ameeleza kuwa umuhimu wa kitabu hicho utazingatiwa  endapo kitayafikia makundi yote yakiwemo yale ya pembezoni.

"Tunafahamu kuwa kitabu hiki ni muhimu hasa katika maendeleo ya uchumi wa nchi yetu,tunategemea kuona Kila mwananchi anasapoti kazi za Rais wetu Kupitia hiki kitabu na ili kufikia malengo hayo lazima pia kiandikwe kwa lugha ya wengi,"amesisitiza .

Naye mmoja wa wanafunzi wa Chuo kikuu cha mipango na maendeleo vijijini Ayub Makali amesema kitabu cha Continuity with Vision the Roadmap to Success for President Samia Suluhu Hassan kinakwenda kujibu maswali ya Watu wengi na makundi mbalimbali kuhusu hoja nyingi zilizomo kwenye jamii.

Amesema  kitabu hicho kimetumia muda mchache kuandikwa kutokana na ukweli kwamba Rais wa awamu ya Sita amekuwa Mtendaji kwani kwa Kipindi kifupi ameweza kufanya mengi.

Awali akiongea katika Uzinduzi huo mkuu wa chuo cha Mipango na Maendeleo Vijijini Profesa Hozen Mayaya amesema  Rais ametekeleza kwa ufanisi miradi ya kimkakati na kutoleta mfano ushiliki wa filamu ya Royal tour ambao umeongeza idadi ya watalii wanaokuja kutembelea nchini na kazi kubwa ya wananchi ni kuendelea kumuombea.

Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Umoja wa Vyuo vya Mashariki na Kusini mwa Afrikia ( ESAURP) Ruta Mutakyawa alitumia nafasi hiyo kusema  kuwa walisimamia uandishi na uchapishaji wa kitabu hicho ambapo kitabu kina kurasa 624 ,sura 29.

Mbali na hayo ameeleza  kuwa kitabu hicho  kimewashirikisha wadau 45 waliotoka vyuo vya elimu ya juu, mashirika ya umma na asasi za kiraia.

Katika uzinduzi huo Waziri wa Elimu Profesa Aldof Mkenda ameipongeza ESAURP ambao ndio wamechapisha kitabu hicho kwa uandishi na uchapishaji wa vitabu vingi ambavyo vimekuwa vikifundisha na kuelimisha jamii.

Amesema,Serikali kupitia wizara hiyo ipo mbioni kuanzisha mfuko rasmi wa kuwasaidia waandishi mahiri wa vitabu huku akiwataka  waandishi wote nchini kuchangamkia fursa zinazotolewa ili kutoanmaaandiko makini yatakayoleta tija kwennye jamii.

Waziri Mkenda amesema katika uongozi wa Rais Samia  umuhimu wa uandishi umeonekana na Serikali kuona haja ya kufanya kwa vitendo kwa kuanzisha tuzo ya Mwalimu Nyerere  ili waandishi nguli na mahili kuweza kushiriki na kujipatia tuzo hizo

" Katika kitabu hiki nimeona kimeandikwa na waandishi wengi na ndani yake kinavitu vingi niitake jamii ya watanzania kukisoma na kujua mambo mengi yanayohusu utendaji wa Rais Samia,"amesema.

Kutokana na hayo mmoja wa Mwandishi wa kitabu hicho Profesa Ted Maliyamkono alisema kulikuwa na kila sababu ya kuandika kitabu hicho kwa kushirikisha watu mbalimbali ili kuwaeleza watanzania na dunia kwa ujumla mambo mengi na mazuri yanayofanywa na Rais wa awamu ya sita Samia Suluhu Hassan.

Amesema katika kitabu hicho walizingatia mambo muhimu ya Kisera na sio kufanya tathmini ya utawala wake na kuwataka wananchi wasione udhaifu  wa kitabu.

Vilevile alitaja  lengo kuu la chapisho hilo kuwa ni kuchangia uboreshaji wa Sera serikaini.

" Ndani ya kitabu hiki kinaonyesha Rais Samia amekuwa wa kwanza kutembelea nchi nyingi tofauti na wengine  ili kufunga njia zilizofungwa na milango ya biashara,pia amekuwa Rais wa kwanza kufanya Royal tour na amekuwa Mtendaji wa vitendo na sio wa maneno," amesema Mwandishi huyo .

Amefafanua kuwa katika utawala wa Rais Samia amekuwa Rais wa kwanza kuteua mawaziri wawili Wanawake katika Wizara mbili ambazo hazikuwahi kuongozwa na wanamke enzi na enzi ambazo ni Wizara ya Ulinzi na Wizara  ya Mambo ya Nje.

"Rais Samia pia ameendeleza kazi yote iliyoachwa na Rais wa awamu ya tano hayati John Magufuli na kuhakiki Katiba mpya na kuona atashughulikia kwa namna gani na kwa wakati ulio sahihi,"amesema


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI NOVEMBA 12,2022



punde!







Share:

Friday, 11 November 2022

Video Mpya : MABAWA WISE - SHANGINGI

Huu hapa wimbo mpya wa Mabawa Wise unaitwa Shangingi
Share:

Ngoma Mpya : MASOKOLINO - TABIA

Hii hapa ngoma ya Masokolino inaitwa Tabia
Share:

Video Mpya : IDDY MASEMPELE - NATUNTOLA

Hii hapa ngoma mpya ya Msanii Iddy Masempele inaitwa Natuntola (Sitamuoa)
Share:

HII NDIO TIBA YA KWELI YA UGONJWA WA KIFUA KIKUU (TB)

Share:

MAJAMBAZI WAVAMIA NA KUAMURU WAPIKIWE KUKU KWANZA KABLA YA KUIBA

 
Wenyeji wa Kitengela wamelilia asasi za usalama kuwanusuru kutokana na utovu wa usalama unaoendelea kuwakosesha usingizi kila kukicha.


Wenyeji hao wameripoti kuwa majambazi wanaowavamia wana tabia za kiajabu, kwani huwalazimisha kuwapikia mlo kabla ya kuwaibia majumbani mwao.

Mkaaji wa kijiji cha Noonkopir Nchini Kenya alisimulia jinsi simu yake ilivyotwaliwa na kuamrishwa kupika sima na kitoweo cha kuku na majambazi waliomvamia.

Agatha Njogu aliiambia jarida la Nation.africa kuwa alipoendelea kuwapikia wavamizi hao, mmoja wao alikuwa akiwafuatilia yeye na wanao huku wengine wakizidi kuchokora nyumba na kuiba.

"Hawakuwa na haraka. Ni uvamizi uliopangwa kwa makini,” Njogu aliiambia the Nation. Wenyeji wamelaumu ongezeko la visa vya ujambazi, kwa utepetevu wa maafisa wa usalama eneo hilo.

Wanadai kwamba maafisa wa kituo kidogo cha polisi cha Noonkopir, hujitokeza kwa saa chache hata ingawa wanahitajika kwa dharura.

"Tuliamua kuweka kituo kidogo cha polisi kwa sababu ya visa vya uhalifu kwenye mtaa wetu. Ila maafisa kwenye kituo hicho huwekwa kwa saa chache kisha huondoka," mzee wa kijiji cha Noonkopir village Clement Njung'e alinukuliwa akisema.




Via: Tuko news
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger