Thursday, 5 December 2019

Video Mpya : NGELELA - MOTO GWA MBELELE

Nakualika kutazama video ya Manju Ngelela inaitwa Moto Gwa Mbelele...Itazame hapa chini

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi December 5























Share:

Wednesday, 4 December 2019

Video : MDEMA NGELELA - BHUHABHI NVA


Tazama video ya Msanii Mdema Ngelela inaitwa Bhuhabi Nva.




Share:

MKURUGENZI AZIMIA BAADA YA KUBANWA NA WAZIRI JAFO


Na Sharon Sauwa, Mwananchi 

Mkurugenzi wa kampuni ya Scol Building Contractors Limited ameanguka na kuzirai mbele ya Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo baada ya kubanwa kuhusu ucheleweshaji wa ujenzi wa barabara ya Martin Luther hadi Swaswa mjini Dodoma.

Tukio hilo limetokea leo Jumatano Desemba 4, 2019 baada ya Jafo kutembelea ujenzi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilomita nane iliyotakiwa kukamilika Agosti lakini ukaongezwa muda hadi Oktoba, 2019. Alizirai baada ya kuelezwa na Jafo kuwa kusuasua kwake kutasababisha asipewe kazi nyingine za ujenzi wa barabara.

Kutokana na kuchelewa huko mkandarasi huyo amekatwa Sh80 milioni na Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (Tarura).

Licha ya kujitetea kuwa wamejenga katika miradi mingi nchini ikiwemo katika jimbo la Kisarawe ambalo mbunge wake ni waziri huyo wa Tamisemi, waziri huyo alikataa na kubainisha kuwa uwezo wa kampuni hiyo ni mdogo.

Baada ya hoja hiyo kupanguliwa na Jafo, mkurugenzi huyo alijitetea kuwa anakwamishwa na upatikanaji wa malighafi.

“Si watu wengi wanaweza kutumia hii nyenzo, hili jiwe hili linatoka Lugoba, Sisi tunataka tufanye kazi nzuri,” alijitetea mkurugenzi huyo.


“Umeshatembelea kazi za wenzako ukafanya ulinganisho ,” amehoji Jafo na huku mkurugenzi huyo akikosa jibu.

Hali hiyo ilimfanya Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk Binilith Mahenge kusema inawezekana kuna kinachomfanya kuchelewesha kazi, ndio maana anashindwa kusema ukweli.

“Katika sehemu ambayo sina shaka na mkurugenzi wangu, mhandisi wa Mkoa wa Dodoma wala mkuu wangu wa Mkoa ni eneo hili la usimamizi wa miradi kwa sababu miradi inaenda vizuri sana,” amesema Jafo.

Jafo amesema katika mradi huo changamoto ipo kwa mkandarasi, akibainisha kuwa Dodoma wamejenga barabara nyingi zimekamilika katika muda mfupi.

“Injinia kuna miradi mingine mmempatia hapa Dodoma,” amehoji Jafo na kujibiwa kuwa hakuna miradi mingine aliyopewa.

Alitoa agizo kwa viongozi wa Dodoma kutompatia mradi mwingine mkandarasi huyo huku akitilia shaka kasi yake ndogo na ubora wa barabara.

Jafo aliagiza mkandarasi huyo kuendelea kukatwa fedha hadi kazi itakapokamilika, kwamba ujenzi wa barabara hiyo unatakiwa kukamilika Desemba 30, 2019.

“Hizo blablaa zako za kokoto zinatoka mbali na nini sitaki kuzisikia, wenzako wote wanatengeneza barabara wanatoa wapi. Labda huna mtaji. Wakazi wa hapa wameteseka sana na madimbwi ndio maana tukasema tuunganishe hii barabara,” amesema Jafo.

Waziri huyo amesema ikiwa mradi huo hautakamilika Desemba 30 atawapiga marufuku wataalam wake wote kumpa kazi nchini.

“Wewe unakuja hapa ndio injinia ama mkurugenzi mbona sikuelewi. Ikifika tarehe 30 kazi hii isipokamilika hamtapata kazi yoyote nchini,” amesema Jafo na ghafla mkurugenzi huyo akaishiwa nguvu na kuanguka na Jafo kumtaka asimame na kusisitiza kuhusu Serikali kutotaka kufanya kazi na Mkandarasi mbabaishaji.
Chanzo - Mwananchi

Share:

JAMAA ALIYEIBA CHUPI 100 ZA WANAWAKE TOFAUTI TOFAUTI AKUTWA AMEVAA MBILI



Mwanaume mmoja mwenye tabia ya Wizi wa nguo za ndani za wanawake, anayejulikana kwa jina la Mukoshi Chipukosia (36), kutoka kijiji cha Hirumbi nchini Kenya, amekamatwa na kufikishwa kwa Mjumbe wa Nyumba Kumi kwa kosa la kuwaibia wanawake nguo za ndani 'chupi' 100 na kukutwa amevaa mbili.

Kwa mujibu wa Mjumbe wa Nyumba Kumi amesema, mwizi huyo amekutwa hadharani akiwa amevaa nguo hizo, wakati anajaribu kuiba zingine kwenye kamba na ndipo Mbwa wa ulinzi wa eneo hilo akaanza kubweka na kumshtua mmiliki.

Aidha mmoja wa wamiliki wa nguo hizo amesema, alikuwa anachunga Ng'ombe ghafla akasikia Mbwa wake anabweka na alipoenda akamkuta mwizi huyo anaiba.

"Tumechoshwa na hii tabia, anachofanya sio tabia nzuri, anaiba nguo za ndani za wanawake pekee, kwanini isiwe na za wanaume, kila mara anatuibia sisi tu inatushangaza ni aina gani ya wizi huu bora angeiba Kuku, Mbuzi au Ng'ombe ila sio nguo za ndani imetushtua sana" amesema mmoja wa waathirika wa wizi huo.

Pia mwizi huyo amejitetea kwa kusema yeye ni maskini, hana pesa za kununua nguo za ndani za kiume kwa hiyo ilikuwa inamlazimu kuiba na kuahidi kuwa hatorudia tena.

Chanzo ni Tuko News na K24 Tv.
Share:

COSTECH YATOA MAFUNZO YA HAKI MILIKI KWA WABUNIFU WALIOSHINDA MASHINDANO YA UBUNIFU


Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendeleshaji na Uhaulishaji wa Teknolojia (COSTECH) Dkt.Athuman Mgumia katika akieleza waandishi wa habari lengo la mafunzo hayo
Mshauri wa masuala ya mambo ya hakimiliki bunifu, kutoka Kituo cha uendelezaji na uhaulishaji wa teknolojia katika Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Bi.Judith Kadege akifafanua juu ya umuhimu wa haki miliki bunifu.
Mhandisi Kennedy Mwakatundu (wa pili kushoto),Mbunifu ambaye ametengeneza mashine ya kusafisha fukwe za bahari akizungumza.
Mbunifu wa kitanda cha kuweka kwenye gari la wagonjwa ambacho kinajiendesha chenyewe, Mhandisi Diana Kaijage (wa kwanza kulia) akizungumza.

Wabunifu nchini wametakiwa kujua jinsi ya kulinda bunifu zao ili zisiweze kuibiwa sambamba na kujua njia wanazoweza kuzitumia kwa kujua aina gani ya miliki bunifu zinazohitajika kwa bunifu zao.

Akizungumza wakati wa mafunzo ya Haki Miliki kwa wabunifu 60 walioshinda kwenye mashindano ya sayansi na teknolojia na Ubunifu yaliyotolewa na Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Mshauri wa masuala ya mambo ya hakimiliki bunifu, kutoka Kituo cha uendelezaji na uhaulishaji wa teknolojia katika Tume ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH), Bi.Judith Kadege alisema Wao wapo kwa ajili ya kuwajengea uwezo na kuwashauri wadau tofauti katika sekta ya utafiti na ubunifu nchini lengo ni kukuza teknolojia zaidi na kupanua Wigo wa kufikia kimataifa zaidi.

Alisema elimu ya miliki bunifu inasaidia kujua haki za wabunifu kabla ya kuanza kubuni kitu ambacho wanakifikiria.

“Yote hayo tunafundisha ili kulinda ile miliki bunifu yake isije ikaibiwa, au ikatumiwa ndivyo sivyo bila ya idhini yake ama kibiashara au kwa matumizi mengine,” alisema.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Uendeleshaji na Uhaulishaji wa Teknolojia katika Tume hiyo, Dkt.Athuman Mgumia alisema Mafunzo yataeasaidia wao kujua namna ya kumiliki bunifu zao pamoja na kuboresha teknolojia na kufika kwa Jamii.

Aidha Mhandisi wa Mitambo ambaye ni mbunifu aliyebuni mashine ya kusafisha Fukwe za bahari Kennedy Mwakatundu, alikiri kuwa Kama Wabunifu kuna vitu haviwalindi kisheria lakini kwa Mafunzo hayo wataweza kujua haki zao kisheria.

“Mafunzo haya yametujengea uelewa Mpana wa namna ya kujua sheria inasemaje hasa katika kulinda bunifu zetu hivyo tutaweza kuomdokana na kuibiwa kazi zetu”Alisema

Hata hivyo wabunifu hao waliomba mafunzo hayo yawe yanatolewa hata kwenye ngazi za chini kwa watoto wadogo ili wakue wakiwa wanauelewa wa namna ya kujua teknolojia zilivyo na wao wanaweza kuwa na ubunifu gani katika jamii.

Share:

Scholarship Mpya Kwa Watanzania | Commonwealth Shared Scholaships Tenable In The United Kingdom 2020

1.0 Call for Applications
The General public is hereby informed that, the Government of United Kingdom has opened a new Commonwealth Shared Scholarship to eligible Tanzanians to pursue Masters Studies in the United Kingdom for the academic year 2020. Interested candidates are highly encouraged to apply under the following six themes:-

1.Science and technology for development;
2.Strengthening health systems and capacity;
3.Promoting global prosperity;
4.Strengthening global peace, security and governance;
5.Strengthening resilience and response to crises; and
6.Access, inclusion and opportunity.

Further details on the eligible study Programmes can be accessed through the following link

2.0 Mode of Application
The online application system can be reached through the following link:<<BOFYA HAPA>>

Before making an online application you are advised to read the following guidelines found in the following link: <<HAPA>>

3.0 Submission
All applications must be submitted by 16.00 (GMT) on 18th December 2019 
 
Note:
It is important that applicants should read and understand all instructions when filling the application forms, attach all the required documents such as certified copies of academic certificates, transcripts, and birth certificates and submit them online through the above link.


Share:

WATU SITA WAFARIKI DUNIA, 30 HAWAJULIKANI BAADA YA MAKAZI YAO KUSOMBWA NA MAPOROMOKO YA UDONGO UGANDA

Picha ya maporomoko yaliyotokea mwaka 2010, nchini Uganda.

Watu sita wamefariki na watu wengine zaidi ya 30 hawajulikani waliko baada ya makazi yao kusombwa na maporomoko ya udongo katika wilaya ya Bududa, Mashariki mwa Uganda.

Karibu kila mwaka, watu wengi hupoteza maisha baada ya makazi yao kusombwa na maporomoko ya matope katika wilaya ya Bududa, Mashariki mwa Uganda.

Watu wapatao 30 bado hawajulikani walipo baada ya mkasa huo.

Kiongozi wa juu wa eneo hilo ameviambia vyombo vya habari kuwa watu kadhaa bado wamefukiwa na mwili mmoja pekee umepatikana mpaka sasa.

Hata hivyo, Kamishna kutoka idara ya kukabiliana na majanga, Martin Owur, amenukuliwa akisema miili mitatu imepatikana Bududa na mingie mitatu katika wilaya ya jirani Sironko, huku watu 47 wakiwa hawajulikai walipo na nyumba 38 zikiwa zimeharibiwa.
Barabara nyingi za Bududa zimefurika maji, hali inayofanya zoezi za uokoaji kuwa gumu.

Maporomoko ya matope yalifuatiwa na mvua kubwa iliyonyesha mfululizo kwa saa tano.

Serikali bado inafanya juhudi ya kuwahamisha watu 140 katika vijiji vipya.

Mwaka jana, watu 51 walipoteza maisha na zaidi ya watu 850 walikosa makazi baada ya maporomoko hayo kukumba eneo hilohilo.

Mvua kubwa isiyo ya kawaida katika eneo la Afrika Mashariki iliwaua watu zaidi ya 200 na zaidi ya watu milioni moja wengine. Nchini Kenya, zaidi ya watu 130 wamepoteza maishaa kutokana na mafuriko yaliyotokea tangu mwezi Oktoba.

Watabiri wa hali ya hewa wameonya kuwepo kwa mvua kubwa mpaka mwishoni mwa mwezi Disemba.
Chanzo - BBC
Share:

MKUU WA MKOA WA KAGERA APIGA MARUFUKU MISHIKAKI


Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia jenerali Marco Gaguti, akichangia damu.
Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia jenerali Marco Gaguti akifagia katika soko kuu 
Na Ashura Jumapili - Malunde 1 blog 
MKUU wa Mkoa wa Kagera Brigedia jenerali Marco Gaguti,amewapiga marufuku wanendesha pikipiki (bodaboda ) kuendesha pikipiki bila kuvaa kofia ngumu (Helmet )sanjari na kubeba abiria zaidi ya mmoja (mshikaki ) na badala yake wazingatie sheria za usalama barabarani.

Brigedia Jen. Gaguti,alipiga marukufu hiyo wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya miaka 58 ya uhuru na miaka 57 ya Jamhuri wakati akiongea na wananchi wa Manispaa ya Bukoba wakiwemo waendesha pikipiki Mkoani Kagera.

Alimuagiza kamanda wa jeshi la polisi mkoani humo (RPC ) Revocatus Malimi ,kuhakikisha suala ya kutii sheria bila shuruti lina kuwa endelevu kwa kusimamia sheria na kanuni za usalama barabarani.

Alisema ahakikishe wanasimamia masuala ya leseni za udereva,uvaaji wa kofia ngumu (elements ),kuacha kubeba mishikaki na mwendo kasi.

Alisema akikamatwa bodaboda na kosa la kubeba mishikaki na abiria pia wachukuliwe hatua kwa kuwekwa mahabusu na mambo mengine yaendelee.

"Haiwezekani kumuadhibu bodaboda pekee yake wakati na abiria wanavunja sheria kwa kupanda pikipiki wawili na kutokuvaa kofia ngumu",alisema mkuu huyo wa Mkoa.

Alisema mwezi Novemba mwaka huu walifanya msako kwa mkoa mzima wa kurejesha nidhamu kwa bodaboda pamoja na utii wa sheria bila shuruti.

"Sitaki kuona bodaboda wanabeba mishikaki,wanavunja sheria sa usalama barabarani na kutokuvaa kofia ngumu mimi ndiyo mlezi wenu niko tayari kushirikina na nyie lakini mfuate sheria za usalama barabarani",alisema.

Hata hivyo mkuu huyo wa mkoa alisema endapo bodaboda watajisajili na kutambulika yuko tayari kuwadhamini ili wapewe pikipiki zao na waachane na masuala ya mikataba ili waweze kilipa kidogokidogo.

Mwendesha bodaboda,Abdumajid Almas alisema kuwa suala la mkuu wa mkoa amelipokea vizuri kwa sababu lilikuwa limeshakuwa na changamoto.

Almas alisema kumekuwa na maegesho ya pikipiki ya kiholela bodaboda hawatambuliki ndiyo maana wateja wanalalamika mara kwa mara kuibiwa simu,mikoba vitu mbalimbali ikiwemo na wizi wa bodaboda.

Katika uzinduzi huo mkuu wa mkoa wa Kagera amezindua kwa kufanya usafi maeneo ya soko kuu la Bukoba akiwa na kamati ya ulinzi na usalama mkoa sanjari na kuchangia damu katika hospitali ya rufaa ya Bukoba.
Share:

KIJANA WA MIAKA 22 ATUPWA JELA MIAKA 30 KWA KUMBAKA MWANAMKE WA MIAKA 27



Mahakama ya Wilaya ya Pangani mkoani Tanga, imemuhukumu Kijana Mahadi Elias maarufu kwa jina Maiko, mwenye umri wa miaka 22 mkazi wa Kijiji cha Stahabu wilayani humo, kifungo cha miaka 30 jela kwa tuhuma za kumbaka mwanamke mwenye umri wa miaka 27.

Hukumu hiyo imetolewa Jana Disemba 2, 2019, na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama hiyo Joel Mnguto, ambapo Maiko amehukumiwa kwenda jela miaka 30 na kutakiwa kumlipa fidia mwanamke huyo ya Shilingi laki tatu kwa kosa la kufanya kitendo cha ubakaji huku akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Inadaiwa Maiko alitenda kosa hilo April 5, 2019, majira ya usiku, katika kijiji cha Sange, baada ya kumvamia mwanamke huyo chumbani alikokuwa amelala na kisha kumuingilia kimwili bila ridhaa yake, huku akimuwekea kisu shingoni na kumtisha kuwa asipokubali atamuuwa kwa kumchinja.

Awali mtuhumiwa alikana kosa hilo ambapo upande wa mashtaka ulilazimika kuleta mashahidi 11 ili kuthibitisha kosa hilo, ambapo pamoja na mshtakiwa kujitetea, ushahidi ulipokamilika mtuhumiwa alikutwa na hatia.
Share:

CHADEMA Wafunguka Baada Ya Sumaye Kutangaza Kukihama Chama Hicho

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimesema kuwa kimeshtushwa na kauli za  mwanachama wake ambaye ni Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye aliyetangaza kukihama chama hicho.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam uliofanyika leo, Sumaye ametangaza kujitoa Chadema huku akitoa tuhuma mbalimbali kwa  mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe.

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa CHADEMA, John Mrema amesema kuwa chama hicho hakikuwa na taarifa za mkutano huo uliofanyika leo  na kwamba wameona barua tu mitandaoni kama ilivyokuwa kwa wananchi wengine.

Mrema amesema wamezipokea taarifa za Sumaye kuondoka Chadema na kama mwanachama yoyote ameacha pengo kwenye chama hicho,  kwamba watatafuta namna ya kuziba pengo hilo.

“Hatuna taarifa za makundi kwenye chama chetu l kama anavyodai Sumaye, labda kama yeye alikuwa na kundi.  Sumaye alikuwa mjumbe wa kamati kuu ya chama alikuwa na nafasi ya kutoa taarifa hiyo na kama kweli ipo ingefanyiwa kazi.

Kuhusu uchaguzi wa chama hicho unaoendelea, Mrema amesema katiba ya Chadema hairuhusu mgombea kupita bila kupingwa,  kama mgomba ni mmoja lazima apigiwe kura ya ndio au hapana.


Share:

Zitto Kabwe Akana Kufanya Mazungumzo Yoyote na Sumaye

Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe amesema hawajafanya mazungumzo yoyote na waziri mkuu mstaafu, Frederick Sumaye ambaye leo mchana Jumatano Desemba 4, 2019 ametangaza kuwa si mwanachama wa Chadema.

Zitto ametoa maelezo hayo saa chache baada ya Sumaye kumaliza kuzungumza na waandishi wa habari na kueleza sababu za kujiondoa Chadema, moja ikiwa ni hali ya sintofahamu iliyoibuka katika uchaguzi wa uenyekiti Kanda ya Pwani ambao alipigiwa kura 48 za hapana kati ya 76.

Katika ukurasa wa mtandao wake wa kijamii wa Twitter, Zitto amesema;  "Nipo Mahakamani tangu asubuhi mpaka sasa nikiendelea na kesi ya uchochezi dhidi yangu. Ninasikia tumetajwa tajwa kuhusu Mzee Sumaye. Itoshe kusema kuwa Chama cha @ACTwazalendo  hakina mazungumzo yeyote na Waziri Mkuu huyo Mstaafu. Nashauri apewe nafasi ya kupumzika kama alivyoomba

Sisi kama chama tumehuzunishwa na uamuzi wa Mzee Sumaye kupumzika Siasa. Ilikuwa ni tunu katika upinzani kuwa na Waziri Mkuu Mstaafu katika ngazi zake za Uongozi. Bila shaka tutachota maarifa na uzoefu wake kama mwenyewe alivyoruhusu. Chama chetu kinaheshimu na kuthamini Wastaafu 

 Kwa upande wangu nawatakia kila la kheri wenzetu wa CHADEMA katika Uchaguzi wao unaoendelea. Dhamira yetu ya kuunganisha nguvu ya Vyama vya upinzani ili kukabiliana na CCM haina mashaka. Mara baada ya Uchaguzi wa wenzetu tutaendelea na mazungumzo ya ushirikiano na Uongozi mpya"


Share:

Kauli Ya Humphrey Polepole Baada Ya Sumaye Kung'oka CHADEMA

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amemwambia Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye kuwa alimueleza asingeweza kupata kazi ya kushauri chama chochote cha siasa kama angekuwa nje ya Chama Cha Mapinduzi.

Polepole ametoa kauli hiyo saa chache baada ya Waziri Mkuu Mstaafu Frederick Sumaye kutangaza kujiondoa ndani ya CHADEMA kwa kile alichokidai kuwa hakuna demokrasia ya kweli.

Polepole ameandika; Mzee nilikwambia, kazi ya ushauri hutaipata ukiwa nje ya CCM wenzako wanaotushauri na tunazingatia ushauri wao kwasababu tunawaheshimu, ni wana CCM na kiitikadi tuko pamoja. Sasa umebaki bila Itikadi. Ile ni mali ya Mtu ni yake, nilikwambia mwache, ona sasa unahama mara ya pili
🙆🏽‍♂️



Share:

Baada ya Sumaye, Kigogo Mwingine CHADEMA Atangaza Kujiuzulu

Mratibu wa CHADEMA  Kanda ya Pwani, Casmir Mabina amewasilisha barua makao makuu ya chama hicho ya kujiuzulu nafasi hiyo kutokana na yaliyotokea kwenye uchaguzi wa kanda hiyo ambayo yamemfanya aliyekuwa mgombea uenyekiti, Fredreck Sumaye atangaze kukihama chama hicho.

Mabina ameeleza uamuzi wake huo leo Jumatano Desemba 4, 2019 katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

“Haya Mambo yametokea ndani ya eneo langu la kazi na kwa maana hiyo leo Jumatano nimewasilisha barua ya kujiuzulu nafasi yangu.

"Nitabaki kuwa mwanachama mwaminifu wa chama chetu na nitakuwa tayari kutoa ushirikiano wowote utakaohitajika.” Amesema


Share:

TAKUKURU wampa siku 10 mkandarasi kukamilisha mradi

Na Alex Sonna, Chemba.
Mkuu wa taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa(TAKUKURU) Mkoa wa Dodoma, Sosthenes Kibwengo, amemuagiza Mkandarasi wa Kampuni ya JUAN, inayotekeleza mradi wa Maji wa Kelema Kuu, katika Kijiji Cha Kelema Balai Wilayani Chemba, Mkoa wa Dodoma, kuhakikisha ndani ya siku kumi mradi huo uwe umekamilika.

Mradi wa Maji wa Kelema Kuu wenye thamani ya shilingi milioni Mia mbili ishirini na tatu,(milioni 223) na ulianza kutekelezwa tangu mwaka 2014 na ulikamilika lakini ikitoa maji zaidi ya wiki mbili tu, kwa kutandikwa mabomba yakiyochini ya kiwango na kuamuriwa mkandarasi huyo kutandika mabomba mengine yenye viwango.

Mkuu huyo wa TAKUKURU ametoa maagizo hayo Mara baada ya kutembelea mradi huo na kuagiza ndani ya siku kumi mradi huo uwe umekamilika na wananchi waanze kupata huduma ya maji Safi na salama ambayo wameikosa kwa mda mrefu.

“Tumetoa siku hizo kumi kwa hawa wakandarasi wakamilishe kwa sababu mvua zikizidi watapata visingizio na Kama unavyoona Kuna sehemu wamechimba na Kutokana na mvua mtaro unafukiwa na tope,” amesema Kibwengo.

Akitoa ufafanuzi baada ya kufanya uchunguzi wao amesema walichokibaini ni kwamba yaliyonunuliwa kuweka katika mradi huo yenye PN 6 badala ya 12.5 kama zilivyoidhinishwa katika mkataba wa kutekeleza mradi hio.

Amesema siku hizo walizotoa hakutakuwa na msamaha wowote kwa kampuni hiyo kwasababu ni uzembe na udanganyifu uliofanywa na mkandarasi huyo kinachotakiwa ni wao kufanya kazi jaraka iwezekanavyo hasa ukizingatia mitaro tayari imechimbwa.

Naye Mhandisi wa wakala wa maji vijijini (RUWASA) wilayani Chemba Robert Mganga amesema kazi iliobakia ni nyepesi sana hivyo wiki moja inatosha kukamilisha kufanya utandikaji hio wa mambomba.

“Hakuna.kazi ngumu hapa sema hii kampuni inaleta uzembe,tuko nao pamoja hivi sasa kuhakikidha wanakamilisha,”amesema Mganga.

Kwa upande wa Mwenyekiti wa kitongoji cha Ndoroboni amesema kitongoji hiko kina shida ya maji inayopelekea wakazi wa eneo hilo kuuafuata kijiji cha Kelema Balai kama mili mbili kutoka Kelema Kuu.

Ameiomba serikali kwa kishirikiana na serikali ya mtaa kusimamia mradi huo ukamilike wakazi waweze kupataaji safi kwa ajili ya matumizi yakila siku  amesema wakazi wengine hudhindwa kwenda umbali mrefu na badala yake wanatumia maji ya mabwawa ambayo ni machafu.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa kampuni ya Juan Mhandisi Inocent Benard amesema wakazi wa eneo hilo wategemee mwezi huu kupata maji kutokana na kuwa watakamilisha ndani ya siku ambazo wametakiwa kukamilisha.


Share:

Ahukumiwa Jela Miaka 30 Kwa Kumbaka Bibi wa Miaka 60

Mahakama ya Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza, imemuhukumu mkazi wa Kijiji cha Nange, Shabo Marando (47) kwenda jela miaka 30 kwa kosa la kubaka bibi wa miaka 60.

Mahakama hiyo mbele ya Hakimu Mfawidhi Esther Malick, ilitoa hukumu hiyo baada ya kupitia ushahidi wa upande wa mashtaka uliokuwa na mashahidi wanne.

Malick akisoma hukumu ya kesi hiyo ya jinai namba 87 ya mwaka 2019, akichambua ushahidi wa shahidi wa tatu, Dk Judith  Kiwango wa hospital ya wilaya, ambaye alimfanyia uchunguzi bibi huyo, alisema alimkuta na michubuko sehemu za siri pamoja na manii.

Shahidi wa pili ambaye ni Sama Luheka (34), mkazi wa Kitongoji cha Igokelo, Kijiji cha Nange, alisema Julai 9 mwaka huu huko Igokelo baada ya kusikia kelele katika vichaka alikwenda eneo hilo na kumkuta mtuhumiwa akimbaka bibi huyo.

Naye bibi huyo aliyebakwa, kwenye ushahidi wake alidai kuwa anamfahamu mtuhumiwa kuwa ni mkazi wa kijijini kwake.

Alidai siku ya tukio alikuwa shambani akikusanya kuni na mtuhumiwa alifika na kusalimiana na mara akamkamata kwa nguvu na kumvutia kichakani na kumbaka.

Katika utetezi wake, mtuhumiwa huyo alidai kuwa mlalamikaji ni shemeji yake, alimpa eneo la kulima na siku ya tukio alikamatwa na wananchi baada ya kuwa amechota maji ya kumwagilia nyanya zake kwa madai kwamba dimbwi alilochota maji lilishazuiwa na kwamba si kweli kwamba alimbaka shemeji yake.


Share:

BREAKING NEWS : Sumaye aondoka Rasmi CHADEMA

Waziri Mkuu mstaafu Fredrick Sumaye leo Desemba 4, 2019 ametangaza kuondoka CHADEMA.

Akiongea leo kwenye mkutanao wake na waandishi wa Habari, Sumaye amesema ameamua kufanya hivyo kutokana na figisu alizofanyiwa baada ya kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Chama Taifa.

Ameeleza kuwa alitaka kugombea nafasi ya Uenyekiti ili kuondoa dhana iliyopo miongoni mwa watu kua nafasi ya Mwenyekiti ndani ya CHADEMA ni ya Freeman Mbowe na haiguswi.


==>>Hapo chini kuna nukuu ya mambo aliyayasema leo;


"Lile tangazo lililotoka jana, ilikuwa ni kweli kutoka kwenye Ofisi yangu lakini halikutengenezwa kwa lengo lile kwa hiyo naomba mliache kama lilivyo.
 
"Najua kuna mambo mengi yameandikwa juu ya kikao hichi kwa watu ambao wanajifanya wapiga ramli, ila naomba muyapuuze, ila yakweli ni haya nitakayoongea

"Kanda ya Pwani nilipata habari kuna watu walinifuata nigombee Uenyekiti Kanda, nongwa ilikuja baada ya mimi kuamua kugombea Uenyekiti Taifa, ila lengo la kwanza nilitaka kuondoa hisia kuwa ndani ya CHADEMA hakuna demokrasia ya kweli


"Niliwaambia wajumbe kuwa mkifanya kama mlivyotaka kufanya, nitauthitibitishia umma kuwa ndani ya CHADEMA hakuna demokrasia ya kweli, au kiti cha Mbowe kina utaratibu mwingine.

“Nafasi ya Mwenyekiti Mbowe haiguswi mimi nilitaka kuonesha kuwa hilo sio kweli lakini nilikuwa najidanganya nimefanyiwa figisu kwenye uchaguzi wa kanda kisa niligusa kiti cha Uenyekiti Taifa

“Mbowe aliwahi kutupa nasaha kuwa tusiionje sumu kwa kuilamba, na mimi siwezi kuigusa sumu kwa kuilamba leo natangaza rasmi kuwa sitoendelea kugombea kwenye nafasi ya Uenyekiti Taifa CHADEMA.

“Nimefedheheka sana kwa kitendo kilichofanywa hasa kwa kujua nimefanyiwa hivi kwasababu ya kukigusa kiti cha Uenyekiti Taifa.

“Kama wakubwa wameamua kuwashawishi wapiga kura wangu wa Kanda ya Pwani hata kwa kuwaficha Hotelini, hii maana yake naambiwa Sumaye akufukuzae akuambii toka.

"Baada ya kutafakari kwa kina, ustaarabu unasema toka sasa hutakiwi, wako watakaosikitika nimelazimika kujiondoa CHADEMA kutoka leo hii, mimi sio Mwanachama wa CHADEMA na sijiungi na chama chochote, ila niko tayari kutumika na chama chochote

“Najua katika kujikosha yatakuwepo maneno Kama kapewa fedha na CCM au ACT n.k, kama nilipokuja CHADEMA nilipewa pesa basi na safari hii nimepewa fedha ingawa sijui na nani maana sijiungi na Chama chochote

“Na kama nilikuja CHADEMA kwa hiari yangu bila kupewa pesa basi na safari hii sijapewa pesa na sitopewa pesa maana sijiungi na Chama chochote, mimi sijawahi kuwa Kibaraka wa Mtu wala Kikundi na hata siku moja sito kuwa hivyo


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger