Friday, 25 October 2019
SERIKALI, SIDA, UNESCO WAANZA MAANDALIZI YA RIPOTI YA KITAIFA UANUAI WA KITAMADUNI
WANAWAKE WAPEWA MBINU ZA KUSHINDA UCHAGUZI
Serikali yaagiza waliokimbia na Bilioni 1.2/= za Wakulima Mtwara wakamatwe
SHIRIKA LA LIFEWATER INTERNATIONAL LAZINDUA MRADI WA MAJI MKOANI SHINYANGA
Shirika la Lifewater International lenye makao yake makuu nchini Marekani limezindua mradi wa maji mkoani Shinyanga, ambapo katika awamu ya kwanza utatekelezwa katika kata tatu za Mwantini, Mwamala pamoja na Mwalukwa zilizopo katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.
Uzinduzi wa mradi huo wa maji umefanyika leo, Oktoba 25, 2019 kwenye ukumbi wa mikutano wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga ambapo Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko, akimwakilisha mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack.
Akizungumza kwenye uzinduzi wa mradi huo,Mboneko amelipongeza Shirika la Lifewater International, kwa kuanzisha mradi wa maji mkoani Shinyanga ambao utaanza kutekelezwa kwenye kata hizo tatu za halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, ambazo zinakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji safi na salama.
Amesema Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli inasisitiza sana upatikanaji wa maji kwenye maeneo mengi ili wananchi waweze kuondokana na adha ya ukosefu wa maji safi na salama, pamoja na kuugua magonjwa yatokanayo na matumizi ya maji ambayo siyo salama kiafya, na kubainisha mradi huo upo sehemu sahihi.
“Tunalishukuru sana Shirika hili la Lifewater International kwa kutuletea mradi huu wa maji mkoani Shinyanga, na kuanza kutekelezwa kwenye halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, ambapo tunaomba mradi huu pia ufike na kwenye maeneo mengine ambayo yana shida ya maji safi na salama ikiwemo wilaya ya Kishapu,”amesema Mboneko.
Naye Mkurugenzi wa Shirika la Lifewater International Tanzania Devocatus Kamara, amesema mradi huo kwa kuanza utatekelezwa kwenye kata hizo tatu za halmshauri ya wilaya ya Shinyanga, ambazo ni Mwantini, Mwamala na Mwalukwa , na baada ya hapo utapanuka kwenye maeneo yote ya mkoa wa Shinyanga na mikoa mingine, ambayo inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama na usafi wa mazingira.
Amesema mradi huo utadumu kwa muda wa miaka mitatu kuanzia mwaka 2020 hadi 2024 na utagharimu kiasi cha Shilingi za kitanzania 4,286,070,528, ambao utajenga visima vipya virefu vya maji safi na salama na kuvikarabati vibovu, kujenga na kuhamasisha ujenzi wa vyoo bora, kuboresha usafi wa mazingira, na utahamasisha na kuhimiza ushiriki wa jamii kikamilifu ili kuhakikisha uendelevu wa mradi.
Kwa upande wake,Meneja wa Shirika Lifewater International mkoa wa Shinyanga Benety Malima, amesema kuwa katika maeneo ambapo maji ya ziwa Victoria yamekwishafika, watafanya utaratibu wa kuendelea kuyasambaza katika maeneo yanayokusudiwa.
Pia amesema maeneo ambayo yatapitiwa na mradi huo wa maji, ni sehemu za shule, zahanati, pamoja na kwenye makazi ya watu, ambapo mradi huo umelenga kufikia watu 100,000.
TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko, akizindua mradi wa maji wa Shirika la Lifewater ambao utatekelezwa mkoani Shinyanga na kuanza kutekelezwa kwa awamu ya kwanza katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga katika Kata tatu za Mwantini, Mwamala na Mwalukwa, ambao utadumu ndani ya miaka mitatu (2020-2024). Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Shirika la Lifewater International Tanzania Devocatus Kamara, akielezea namna mradi huo wa maji utakavyofanya kazi Mkoani Shinyanga.
Katibu Tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela, akiwataka watumishi wa Serikali kutoa ushirikiano kwenye utekelezaji wa mradi huo wa maji.
Wajumbe wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.
Wajumbe wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.
Wajumbe wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.
Wajumbe wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.
Uzinduzi ukiendelea.
Wajumbe wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.
Kushoto ni Meneja wa Lifewater International mkoa wa Shinyanga Benety Malima akiwa kwenye kikao cha uzinduzi wa mradi wao wa maji.
Katibu Tawala wa wilaya ya Shinyanga Boniphace Chambi akichangia mada kwenye kikao cha uzinduzi wa mradi wa maji kutoka Shirika la Lifewater Internationali.
Kaimu Meneja wa Wakala wa Maji Vijijini mkoa wa Shinyanga (Ruwasa) Malwa Kisibo,akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi huo wa maji.
Kaimu meneja wa wakala wa maji vijijini wilaya ya Shinyanga (Ruwasa) Emaeli Nkopi, akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi huo wa maji.
Kaimu Afisa afya mkoa Mussa Makungu akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi huo wa maji kutoka Shirika la Lifewater International.
Kaimu Afisa afya halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Gibril Mongi akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.
Kaimu mganga mkuu wa halmshauri ya wilaya ya Shinyanga Bashiri Salumu akizungumza kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.
Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Edward Maduhu, akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi maji kutoka Shirika la Lifewater Intenational.
Wajumbe wakipiga picha ya pamoja na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko aliyekaa kwenye kiti katikati mara baada ya kumaliza kuzindua mradi wa maji kutoka Shirika la Lifewater International.
Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog.
Job vacancy at USAID (GHSC TA-TZ) Project, HIV/AIDS Supply Chain Advisor
Job Vacancies at USAID Global Health Supply Chain Program – Tanzania (GHSC TA-TZ) Project, 2019 The Global Health Supply Chain Program – Technical Assistance – Tanzania (GHSC-TA-TZ) project, supported by the United States Agency for International Development (USAID), provides expert technical assistance to Tanzania to strengthen country supply chain systems across all health elements, e.g., malaria, family planning… Read More »
The post Job vacancy at USAID (GHSC TA-TZ) Project, HIV/AIDS Supply Chain Advisor appeared first on Udahiliportal.com.
Mahakama Kuu Yakubali ACT- Wazalendo Kujiunga Kwenye Kesi Kuhusu Ukomo Wa Urais
Assistant Accountant CUM Sales Job at Firstlink Safaris Limited
Position: Assistant Accountant CUM Sales Job Description REPORTS TO: Branch Supervisor Role Purpose statement: Supporting the finance department, accountant, and management team by completing routine clerical and accounting tasks. Preparing budgets, maintaining reports, and completing basic bookkeeping and accounting duties for the company. Key Accountabilities and Responsibilities: Preparing financial documents such as invoices, bills, and accounts payable and… Read More »
The post Assistant Accountant CUM Sales Job at Firstlink Safaris Limited appeared first on Udahiliportal.com.
Tour Coordinator/Guide Job at Fastlink Safaris Limited
Position: Tour Coordinator/Guide Job Description REPORTS TO: Branch Manager The tour coordinator’s job begins long before the tour itself. A tour coordinator interacts with managers, booking agents and publicists to develop a calendar of events with locations, dates and times. This calendar provides the groundwork for organizing travel and transportation and accommodations. The tour coordinator is also responsible… Read More »
The post Tour Coordinator/Guide Job at Fastlink Safaris Limited appeared first on Udahiliportal.com.
Serikali Yaelekeza Kukamilika Kwa Ujenzi Wa Kiwanda Ili Kukuza Soko La Mifugo Nchini
Waziri Mkuu: Biashara Kati Ya Tanzania Na Urusi Iratibiwe
Wapinzani Wapinga Mpango wa Nyuklia Rwanda
Muswada huo wa ujenzi wa nguvu za nyuklia ulipitishwa bungeni Rwanda ukipingwa na wabunge wawili pekee.
Lakini Serikali ya Rwanda inasema teknolojia ya nyuklia itaifaa kwa matumizi ya kutengeneza nishati, dawa na matumizi mengine ya amani.
-BBC
Job vacancy at The Association of African Higher Education Financing Agencies (AAHEFA)
VACANCY ANNOUNCEMENT – AAHEFA CEO The Association of African Higher Educaton Financing Agencies (AAHEFA), is an apex body of Higher Education Financing Agencies with Headquarters in Dar es Salaam. AAHEFA is an umbrella body of Higher Education Financing Institutions that deal with issuance of loans, bursaries/grants and scholarships to Higher Education students as well as recovery/ collection of… Read More »
The post Job vacancy at The Association of African Higher Education Financing Agencies (AAHEFA) appeared first on Udahiliportal.com.
Programme Assistant Job at UNESCO,
Programme Assistant Job Title: Programme Assistant (Only candidates with authorisation to work in Tanzania are eligible to apply) OVERVIEW OF THE FUNCTIONS OF THE POST Under the overall authority and direct supervision of the Head and Representative of UNESCO Dar es Salaam Office, the Programme Assistant is tasked with the delivery of a range of office, financial and… Read More »
The post Programme Assistant Job at UNESCO, appeared first on Udahiliportal.com.
Project Manager Job at Africa Academy for Public Health
Project Manager The Africa Academy for Public Health (AAPH) is an independent organization registered in Tanzania with the mission to address public health priority challenges in sub-Saharan Africa through innovative scientific evidence, training and capacity building and knowledge translation. AAPH is currently implementing different health and nutrition research studies in 6 regions within Tanzania mainland and would like… Read More »
The post Project Manager Job at Africa Academy for Public Health appeared first on Udahiliportal.com.




























