Friday, 25 October 2019

SERIKALI, SIDA, UNESCO WAANZA MAANDALIZI YA RIPOTI YA KITAIFA UANUAI WA KITAMADUNI

 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akisalimiana na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos mara baada ya kuwasili kwenye warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg.
 Afisa Mtendaji Mkuu COSOTA ambaye pia ni Mtaalamu wa Taifa wa mradi unaolenga kutekeleza makubaliano ya UNESCO ya mwaka  2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Tamaduni Anuwai, Bi. Doreen Sinare akitambulisha meza kuu (hawapo hewani) wakati wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo akitoa hotuba kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe wakati wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
 Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos akitoa salamu za UNESCO wakati wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg akitoa salamu za SIDA wakati wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akimkabidhi Afisa Mtendaji Mkuu COSOTA na Mtaalamu wa Taifa wa mradi unaolenga kutekeleza makubaliano ya UNESCO ya mwaka  2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Tamaduni Anuwai, Bi. Doreen Sinare cheti cha ushiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg (kushoto) pamoja na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (kulia).
 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akimkabidhi  Bw. Maximilian Chami kutoka Tume ya Taifa ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (NATCOM-Unesco) cheti cha ushiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg (kushoto) pamoja na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (kulia).
 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akimkabidhi Meneja wa Programu wa Taasisi ya Culture and Development East Africa (CDEA), Bw. Mandolin Kahindi cheti cha ushiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg (kushoto) pamoja na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (kulia).
 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akimkabidhi Mwakilishi kutoka COSOTA Bw. Zephania Lyamula cheti cha ushiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg (kushoto) pamoja na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (kulia).
 Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo (katikati) akimkabidhi Afisa Uhusiano wa Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), Bi. Mwamini Mohamed cheti cha ushiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO kwa ufadhiliwa wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam. Wanaoshuhudia tukio hilo ni Balozi wa Sweden nchini Mh. Andres Sjoberg (kushoto) pamoja na Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bw. Tirso Dos Santos (kulia).
Baadhi ya washiriki wakiwasilisha kazi za vikundi wakati wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
 Baadhi ya washiriki waliohudhuria warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.
Mgeni rasmi Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu Tanzania Dr. Kiagho Kilonzo katika picha ya pamoja na washiriki wa warsha ya mafunzo ya kuwajengea uwezo wadau mbalimbali wa sekta ya Ubinifu, Utamaduni na Sanaa katika uandaaji wa taarifa ya kitaifa ya makubaliano ya UNESCO ya mwaka 2005 ya Ulinzi na Ukuzaji wa Vielelezo vya Utamaduni Anuwai iliyoratibiwa na UNESCO na kufadhiliwa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Sweden (SIDA) iliyofanyika kwenye Hotel ya Courtyard Protea jijini Dar es Salaam.


Na Mwandishi Wetu
SERIKALI ya Tanzania kwa kushirikiana na Shirika la Utamaduni, Elimu, Utamaduni na Sayansi la Umoja wa Mataifa (UNESCO) wamezindua mafunzo ya kuandaa ripoti ya kitaifa ya Mkataba wa UNESCO wa mwaka 2005.

Mkataba huo ambao serikali ya Tanzania umetia saini mwaka 2011 unazungumzia kulinda na kuendeleza uanuai wa kujieleza kiutamaduni.

Kwa mujibu wa matakwa ya mkataba huo kila baada ya miaka mine mataifa yanayotakiwa kuandika taarifa kuelezea utekelezaji wa mkataba huo. Mengi ya mataifa ikiwamo Tanzania haijawahi kuandika  taarifa hiyo.

Kwa kawaida taarifa hiyo ni mchanganyiko wa taarifa za serikali na wadau wengine wakiwemo wa taasisi zisizo za kiserikali (AZAKI).

Fedha za kufanyia mafunzo hayo na kuandika taarifa zimetolewa na Sweden kupitia Mfuko wake wa Maendeleo (SIDA) chini ya uratibu wa UNESCO.

Taarifa hiyo ikishakamilika inatarajiwa kujadiliwa na wadau na kupelekwa serikalini ambako nako itapitiwa na kufikishwa UNESCO.

Akisoma hotuba ya ufunguzi wa mafunzo hayo kwa niaba ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dk. Harrison Mwakyembe Kaimu Katibu Mkuu wa Bodi ya Filamu nchini Dk. Kiagho Kilonzo, alisema kwa sasa Tanzania ipo tayari kwa taarifa hiyo ndio maana imeunda kamati na kuanza mafunzo.

Kamati hiyo ya kuandika Ripoti inaongozwa na Robert Mwampembwa ambaye ikisimamiwa na Doreen Sinare, Ofisa mtendaji Mkuu wa COSATA ambaye ndiye mtaalamu wa mradi.

Kwa mujibu wa Balozi wa Sweden nchini Andres Sjoberg, ufadhili wa taifa hilo kwa nchi 16 zinazotakiwa kuandika utekelezaji wa mkataba huo umelenga kuhakikisha kuwa kuna uhuru wa wasanii kujieleza kiutamaduni na hasa wanawake.

Alisema kwa sasa dunia sio kijiji bali kutokana na mifumo ya upashanaji wa habari kuzidi kuimarika dunia imekuwa ni moja na hivyo masuala ua kujieleza yanabaki kuwa wazi kila mahali.

Naye Dk. Harrison Mwakyembe alisema kwa sasa Tanzania iko vizuri kutokana na kuridhia mkataba huo wa 2005 ambao lengo lake kubwa ni kutengeneza fursa kwa wasanii kuwa karibu na soko la dunia.

Aidha alisema kwamba nia kubwa ya makubaliano hayo ni kulinda uanuai wa kujieleza kiutamaduni na hivyo kutengeneza mazingira ya kukua kwa utamaduni kwa manufaa ya watu wote.

Kwa mujibu wa Dk. Mwakyembe ni matarajio yake kwamba ifikapo Aprili mwakani taarifa hiyo itakuwa imekamilika na tayari kutumika na tasnia ya utamaduni na ubunifu na dunia pia.

Naye Mkuu wa Ofisi na Mwakilishi wa UNESCO Dar es Salaam, Tirso Dos Santos,  alisema kwamba taarifa ya Tanzania itaunganishwa na mataifa mengine ili kuelezea dunia inavyoendelea katika kutekeleza matakwa ya mkataba.

"Sote tunajua kwamba Tanzania ni kitovu cha ubunifu na hasa kwa kuwa na matamasha mbalimbali hali inayodhirisha umuhimu wa mradi huu kwa ajili ya maendeleo maendelevu ", alisema mwakilishi huyo wa UNESCO ambapo aliyataja matamasha makubwa ya filamu nchini ikiwamo ya ZIFF na Azam kama moja ya uanuai wa utamaduni.
Share:

WANAWAKE WAPEWA MBINU ZA KUSHINDA UCHAGUZI


Mwezeshaji wa Mafunzo Bw. Henry Kigodi akifafanua jambo katika mafunzo 
Mwezeshaji Gratiana Rwakibarila akiwa anaeleza namna ya kuboresha mbinu za kampeni 
Washiriki wa mafunzo wakiwa katika vikundi vya mijadala 
WANAWAKE wa wilaya ya Songea mkoani Ruvuma waliotia nia ya kugombea uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika nchini Tanzania, Novemba 24, 2019 toka vyama vya siasa wamepewa mbinu za kushinda uchaguzi huo kwa wingi na kishindo.

Wanawake 64 wamepewa mafunzo na Shirika lisilo la Kiserikali la Tanzania Gender Networking Programme (TGNP Mtandao) la Dar es Salaam, kwa lengo la kuwajengea uwezo wanawake waliotia nia katika kinyang’anyiro cha Uchaguzi wa serikali za mitaa wakiwa na moto wao wa "Wanawake wakati wa kuongoza ni sasa".
Mwezeshaji wa Mafunzo hayo toka TGNP Mtandao, ambaye ni Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Mwalimu Nyerere Dar es Salaam, Bw. Henry Kigodi amesema: TGNP Mtandao imejikita kusaidia wanawake ambao wametia nia katika kugombea nafasi mbalimbali ili kukidhi hitaji la kupata viongozi wanawake wengi ambao kwa kipindi kirefu hushindwa kufanikiwa kwa sababu mbalimbali ikiwa ni pamoja na kukosa mbinu za kampeni na kukabiliana na mfumo dume. 

Bw. Kigodi alisema wanawake wakipata uongozi huwa makini katika maamuzi, kutekeleza na kusimamia shughuli za kimaendeleo kwakuwa wanawake huwa wanakabiliwa na changamoto nyingi za kimaendeleo katika vitongoji, vijijiji na mitaa yao. “Wanawake ndiyo wanaohangaika na changamoto za ukosefu wa maji, huduma za afya na Malezi lakini wao ndiyo hushiriki kwa kiwango kikubwa katika shughuli za uzalishaji mali kama kilimo na hawafaidi matunda yake,” alisema Kigodi.

Naye, mwezeshaji Mwenza Gratiana Rwakibarila, alisema ni vema wanawake wakatambua kuwa wana uwezo mkubwa katika kuongoza jamii na hivyo wanawajibu mkubwa katika kuhakikisha wanapata mbinu za kushinda nafasi walizoziomba kwa kupewa mafunzo ya kujijengea uelewa wa pamoja juu ya ushiriki katika uchaguzi.

Vilevile alisema, wanawake lazima wajengewe uelewa wa dhana za jinsia ili kuwawezesha watia nia kuzihusisha na masuala ya uchaguzi, kujadili umuhimu katika ushiriki wa wanawake katika kampeni na uchaguzi. Aidha, Gratiana alisema mafunzo hayo yatawaboreshea mbinu zao za mikakati na mbinu za kampeni wakati wa uchaguzi.

Jumla ya vyama vitano vya siasa vinashiriki mafunzo hayo, vyama hivyo ni ADA- TADEA, CCM, CHADEMA, CUF na TLP. 

Washiriki wamesisitizwa kuwa wakishinda wayaangalie maendeleo kwa mtazamo wa kijinsia na kupambana na sera potofu za kijinsia.
Kwa mujibu wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo (MB), maandalizi ya awali ya uchaguzi wa serikali za mitaa yamekamilika kwa kuzingatia kanuni za Uchaguzi wa serikali za Mitaa wa Mwaka 2019 Ibara ya 4 (13).
Share:

Serikali yaagiza waliokimbia na Bilioni 1.2/= za Wakulima Mtwara wakamatwe

Na Mwandishi Wetu
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni ameliagiza Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara kuwakamata  Viongozi wa Vyama vya Msingi vya Ushirika wanaotuhumiwa kukimbia na  Kiasi cha Shilingi Bilioni 1.2/= za wakulima ambazo ni madeni ya Korosho.

Ametoa kauli hiyo leo wakati akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Newala  katika Mkutano wa Hadhara uliofanyika Viwanja vya Stendi Kuu baada ya kupokea Ripoti ya Jumla ya Madeni wanayodai wakulima katika Wilaya za Mtwara, Masasi, Nanyumbu, Newala na Tandahimba.

“Nilivyofika hapa Mtwara jambo la kwanza lilikuwa kumuuliza Kamanda wa Polisi wa hapa juu ya utekelezaji wa agizo la Mheshimiwa Rais alilolitoa siku za hivi karibuni alipokuwa ziara na kuagiza kukamatwa kwa viongozi wawili wa vyama vya msingi vya  ushirika  wanaodaiwa fedha za korosho na wakulima, ameniambia walitekeleza agizo na hao viongozi  wawili tayari wameanza kulipa hizo fedha,” amesema Masauni

Akizungumza baada ya kupokea ripoti ya madeni kwa Wilaya zote za Mkoa wa Mtwara Naibu Waziri Masauni amelitaka Jeshi la Polisi kuwakamata viongozi wengine katika wilaya zilizobakia za Mtwara, Newala, Masasi, Nanyumbu na Tandahimba ambazo katika taarifa ya jumla ya mkoa inaonyesha takribani Shilingi Bilioni 1.2 bado zinadaiwa na wakulima hao kutoka kwa viongozi wa vyama hivyo.

“Mheshimiwa Rais kwenye ziara yake aliishia wilaya ya Masasi lakini katika ripoti hapa inaonyesha katika wilaya zingine wakulima pia wanadai fedha zao ambacho ni kiasi kikubwa,nakuagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara kuwakamata viongozi wengine katika wilaya zilizobakia na hakikisha kiasi hicho cha fedha cha wakulima hao kinalipwa,” amesema Masauni

Katika taarifa hiyo iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara,Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Blasius Chitanda inaonyesha jumla ya Vyama vya Ushirika 61 bado vinadaiwa na wakulima katika wilaya za Mtwara, Masasi, Tandahimba na Newala kuanzia Msimu wa Korosho wa Mwaka 2015/2016 hadi 2017/2018.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti katika mkutano huo baadhi ya wakulima wanaodai fedha zao waliiomba serikali kuhakikisha wanalipwa haki yao kwani madeni hayo yamechukua muda mrefu hali inayopelekea kuzorotesha shughuli zao za kuchumi huku familia zao zikipata taabu kutokana na fedha zao kutopatikana kwa wakati.


Share:

SHIRIKA LA LIFEWATER INTERNATIONAL LAZINDUA MRADI WA MAJI MKOANI SHINYANGA




Shirika la Lifewater International lenye makao yake makuu nchini Marekani limezindua mradi wa maji mkoani Shinyanga, ambapo katika awamu ya kwanza utatekelezwa katika kata tatu za Mwantini, Mwamala pamoja na Mwalukwa zilizopo katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga.


Uzinduzi wa mradi huo wa maji umefanyika leo, Oktoba 25, 2019 kwenye ukumbi wa mikutano wa mkuu wa mkoa wa Shinyanga ambapo Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko, akimwakilisha mkuu wa mkoa wa Shinyanga Mhe. Zainab Telack.

Akizungumza kwenye uzinduzi wa mradi huo,Mboneko  amelipongeza Shirika la Lifewater International, kwa kuanzisha mradi wa maji mkoani Shinyanga ambao utaanza kutekelezwa kwenye kata hizo tatu za halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, ambazo zinakabiliwa na uhaba mkubwa wa maji safi na salama.

Amesema Serikali ya awamu ya Tano chini ya Rais John Pombe Magufuli inasisitiza sana upatikanaji wa maji kwenye maeneo mengi ili wananchi waweze kuondokana na adha ya ukosefu wa maji safi na salama, pamoja na kuugua magonjwa yatokanayo na matumizi ya maji ambayo siyo salama kiafya, na kubainisha mradi huo upo sehemu sahihi.

“Tunalishukuru sana Shirika hili la Lifewater International kwa kutuletea mradi huu wa maji mkoani Shinyanga, na kuanza kutekelezwa kwenye halmashauri ya wilaya ya Shinyanga, ambapo tunaomba mradi huu pia ufike na kwenye maeneo mengine ambayo yana shida ya maji safi na salama ikiwemo wilaya ya Kishapu,”amesema Mboneko.

Naye Mkurugenzi wa Shirika la Lifewater International Tanzania Devocatus Kamara, amesema mradi huo kwa kuanza utatekelezwa kwenye kata hizo tatu za halmshauri ya wilaya ya Shinyanga, ambazo ni Mwantini, Mwamala na Mwalukwa , na baada ya hapo utapanuka kwenye maeneo yote ya mkoa wa Shinyanga na mikoa mingine, ambayo inakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama na usafi wa mazingira.

Amesema mradi huo utadumu kwa muda wa miaka mitatu kuanzia mwaka 2020 hadi 2024 na utagharimu kiasi cha Shilingi za kitanzania 4,286,070,528, ambao utajenga visima vipya virefu vya maji safi na salama na kuvikarabati vibovu, kujenga na kuhamasisha ujenzi wa vyoo bora, kuboresha usafi wa mazingira, na utahamasisha na kuhimiza ushiriki wa jamii kikamilifu ili kuhakikisha uendelevu wa mradi.

Kwa upande wake,Meneja wa Shirika  Lifewater International mkoa wa Shinyanga Benety Malima, amesema kuwa katika maeneo  ambapo maji ya ziwa Victoria yamekwishafika, watafanya utaratibu wa kuendelea kuyasambaza katika maeneo yanayokusudiwa.

Pia amesema maeneo ambayo yatapitiwa na mradi huo wa maji, ni sehemu za shule, zahanati, pamoja na kwenye makazi ya watu, ambapo mradi huo umelenga kufikia watu 100,000.

TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI


Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko, akizindua mradi wa maji wa Shirika la Lifewater ambao utatekelezwa mkoani Shinyanga na kuanza kutekelezwa kwa awamu ya kwanza katika halmashauri ya wilaya ya Shinyanga katika Kata tatu za Mwantini, Mwamala na Mwalukwa, ambao utadumu ndani ya miaka mitatu (2020-2024). Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog

Mkurugenzi wa Shirika  la Lifewater International Tanzania Devocatus Kamara, akielezea namna mradi huo wa maji utakavyofanya kazi Mkoani Shinyanga.

Katibu Tawala wa mkoa wa Shinyanga Albert Msovela, akiwataka watumishi wa Serikali kutoa ushirikiano kwenye utekelezaji wa mradi huo wa maji.

Wajumbe wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.

Wajumbe wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.

Wajumbe wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.

Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.

Wajumbe wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.

Uzinduzi ukiendelea.

Wajumbe wakiwa kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.

Kushoto ni Meneja wa Lifewater International mkoa wa Shinyanga Benety Malima akiwa kwenye kikao cha uzinduzi wa mradi wao wa maji.

Katibu Tawala wa wilaya ya Shinyanga Boniphace Chambi akichangia mada kwenye kikao cha uzinduzi wa mradi wa maji kutoka Shirika la Lifewater Internationali.

Kaimu Meneja wa Wakala wa Maji Vijijini mkoa wa Shinyanga (Ruwasa) Malwa Kisibo,akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi huo wa maji.

Kaimu meneja wa wakala wa maji vijijini wilaya ya Shinyanga (Ruwasa) Emaeli Nkopi, akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi huo wa maji.

Kaimu Afisa afya mkoa Mussa Makungu akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi huo wa maji kutoka Shirika la Lifewater International.

Kaimu Afisa afya halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Gibril Mongi akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.

Kaimu mganga mkuu wa halmshauri ya wilaya ya Shinyanga Bashiri Salumu akizungumza kwenye uzinduzi wa mradi wa maji.

Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Shinyanga Edward Maduhu, akichangia mada kwenye uzinduzi wa mradi maji kutoka Shirika la Lifewater Intenational.

Wajumbe wakipiga picha ya pamoja na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko aliyekaa kwenye kiti katikati mara baada ya kumaliza kuzindua mradi wa maji kutoka Shirika la Lifewater International.

Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog.


Share:

Job vacancy at USAID (GHSC TA-TZ) Project, HIV/AIDS Supply Chain Advisor

Job Vacancies at USAID Global Health Supply Chain Program – Tanzania (GHSC TA-TZ) Project, 2019 The Global Health Supply Chain Program – Technical Assistance – Tanzania (GHSC-TA-TZ) project, supported by the United States Agency for International Development (USAID), provides expert technical assistance to Tanzania to strengthen country supply chain systems across all health elements, e.g., malaria, family planning… Read More »

The post Job vacancy at USAID (GHSC TA-TZ) Project, HIV/AIDS Supply Chain Advisor appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Mahakama Kuu Yakubali ACT- Wazalendo Kujiunga Kwenye Kesi Kuhusu Ukomo Wa Urais

Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imekubali ombi la Chama cha ACT-Wazalendo kujiunga kama washtakiwa kwenye kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na Dezydelius Mgoya, maarufu kama Mkulima, kuhusu ukomo wa urais.

Uamuzi huo ulitolewa jana na Jaji Dk. Benhaj Masoud baada ya kusikiliza maombi ya ACT-Wazalendo kujiunga na kesi hiyo kwa sababu wana maslahi nayo.

Wakili wa ACT-Wazalendo, Jebra Kambole, alidai kuwa mteja wake ameomba kujiunga kwa sababu ni chama kilichosajiliwa na kimeshiriki katika uchaguzi.

Pia alidai kuwa chama hicho kina wanachama Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar kwa mujibu wa matakwa ya kisheria na kikatiba.

Mgoya alifungua kesi hiyo chini ya kifungu cha 4 cha sheria ya utekelezaji haki na wajibu, sura ya 3 ya mwaka 1994 chini ya Ibara ya 30(3) ya Katiba ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977.

Kwa mujibu wa hati ya madai ya kesi hiyo, Mgoya anahoji Ibara ya 40(20) ya Katiba ambayo imeweka ukomo wa mihula miwili tu ya miaka mitano mitano ya uongozi katika nafasi hiyo ya urais.

Hivyo anaiomba mahakama hiyo itoe tamko na tafsiri ya maana sahihi na athari za masharti ya ibara hiyo.Pia anaiomba mahakama itoe tafsiri ya maana dhahiri ya masharti ya Ibara ya 42(2) ya Katiba kwa kuhusianisha na masharti ya Ibara za 13, 21 na 22 za Katiba hiyo.

Kadhalika, Mgoya anaiomba mahakama itoe tafsiri ya maana ya Ibara hiyo ya 40(2) kwa kuhusianisha na Ibara ya 39 ya Katiba.

Credit:Nipasahe


Share:

Assistant Accountant CUM Sales Job at Firstlink Safaris Limited

Position: Assistant Accountant CUM Sales Job Description REPORTS TO: Branch Supervisor Role Purpose statement: Supporting the finance department, accountant, and management team by completing routine clerical and accounting tasks. Preparing budgets, maintaining reports, and completing basic bookkeeping and accounting duties for the company. Key Accountabilities and Responsibilities: Preparing financial documents such as invoices, bills, and accounts payable and… Read More »

The post Assistant Accountant CUM Sales Job at Firstlink Safaris Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Tour Coordinator/Guide Job at Fastlink Safaris Limited

Position: Tour Coordinator/Guide Job Description REPORTS TO: Branch Manager The tour coordinator’s job begins long before the tour itself. A tour coordinator interacts with managers, booking agents and publicists to develop a calendar of events with locations, dates and times. This calendar provides the groundwork for organizing travel and transportation and accommodations. The tour coordinator is also responsible… Read More »

The post Tour Coordinator/Guide Job at Fastlink Safaris Limited appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Serikali Yaelekeza Kukamilika Kwa Ujenzi Wa Kiwanda Ili Kukuza Soko La Mifugo Nchini

Na. Edward Kondela
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel ameuelekeza uongozi unaosimamia ujenzi wa kiwanda cha kusindika nyama cha Eliya kinachojengwa katika Wilaya ya Longido Mkoani Arusha kuhakikisha unakamilisha ujenzi wa kiwanda hicho mapema mwanzoni mwa mwaka 2020 ili kiweze kuleta tija kwa taifa na wafugaji wanaoishi katika Mkoa wa Arusha, mikoa ya jirani na nchi ya jirani ya Kenya.

Prof. Gabriel amesema hayo jana (24.10.2019) mara baada ya kutembelea ujenzi wa kiwanda hicho akiwa pamoja na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Longido na kukuta tayari ujenzi wa kiwanda umefikia asilimia 90 ambapo mitambo mbalimbali imeanza kufungwa katika kiwanda ambacho kitakuwa na uwezo wa kuchinja ng’ombe 500 kwa siku na mbuzi takriban Elfu Mbili kwa siku.

Katibu mkuu huyo ametoa wito kwa wadau wa mifugo kujipanga vizuri namna ya kutumia fursa ya uwepo wa kiwanda hicho ili wafugaji na wafanyabiashara waweze kuuza mifugo katika kiwanda hicho ambacho kitaongeza ajira na kukuza sekta ya mifugo nchini.

Awali akizungumza na wakuu wa idara na vitengo wa Halmashauri ya Wilaya ya Wilaya ya Longido kabla ya kutembelea ujenzi wa kiwanda hicho, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel amepokea maoni ya namna ya kudhibiti vitendo vya kutorosha mifugo mipakani hali inayochangia kuikosesha serikali mapato ambapo elimu imesisitizwa kwa watu wanaoishi mipakani.

Prof. Gabriel amesema Wizara ya Mifugo na Uvuvi inazidi kuchukua maoni ya namna ya kuhakikisha vitendo vya utoroshaji wa mifugo hususan katika mpaka wa Namanga ambao ni kati ya mipaka ya nchi za Tanzania na Kenya vinadhibitiwa ili kuhakikisha mapato ya serikali hayapotei pamoja na kusimamia  viwanda vya kusindika nyama kikiwemo cha Eliya kinachotarajia kukamilika mapema mwaka 2020 kinapata mifugo ya kutosha kutoka Mkoa wa Arusha na mikoa ya jirani ili kusindika nyama katika kiwanda hicho.

Mwisho.


Share:

Waziri Mkuu: Biashara Kati Ya Tanzania Na Urusi Iratibiwe

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameutaka ubalozi wa Tanzania nchini Urusi uratibu mipango ya wafanyabiashara wa Urusi wanaokusudia kuja nchini kuwekeza kwa kuwaunganisha na Taasisi na Wizara husika ili waweze kuwekeza mitaji yao kwa kuzingatia maslahi ya Taifa.

Ametoa agizo hilo jana (Alhamisi, Oktoba 24, 2019) baada ya kugundua uwepo wa wafanyabiashara wengi wa Urusi wanakusudia kuja Tanzania kwa ajili ya kuangalia maeneo ya uwekezaji pamoja na kutafuta wafanyabiashara wa Kitanzania watakaoungana nao katika uwekezaji wanaokusudia kuufanya.

“Tayari miadi imekwishawekwa ya kuwakaribiasha wawekezaji wa Urusi kuja Tanzania kwa ushawishi wa kwangu mwenyewe pamoja na ushawishi wa wafanyabiashara wa Tanzania, hivyo nisingependa wafanyabiashara hao wasumbuliwe au kukatishwa tamaa katika kutimiza nia yao hiyo.” Waziri Mkuu alisisitiza.

Alisema Mkutano baina ya Wakuu wa nchi na Serikali kutoka Mataifa ya Afrika na Urusi uliomalizika jana Oktoba 24, 2019 ulilenga kujenga uhusiano mzuri zaidi katika nyanja mbalimbali hususani za kiuchumi.

Akizungumza baada kumalizika mkutano huo kwenye ukumbi wa Olympic Park wa Sochi nchini Urusi, Waziri Mkuu alisema Urusi imeutumia mkutano huo kueleza bayana maeneo ambayo wako tayari kushirikiana na Afrika katika kuwekeza kwa faida ya pande zote mbili.

Waziri Mkuu aliyataja maeneo hayo kuwa ni pamoja na uuzaji wa zana za kilimo kama vile matrekta, sekta ya mafuta na gesi pamoja na madini, Ujenzi wa miundombinu hasa reli, masuala ya elimu hasa utoaji wa nafasi za mafunzo nchini humo.

Alisema kwa upande wake Tanzania imejinadi vizuri ikIngozwa na yeye mwenyewe kwani alifanya mazungumzo na viongozi wa makampuni zaidi ya manane ya Urusi ili kuyashawishi yawekeze nchini na yote yalikubali kufika Tanzania mapema iwezekanavyo.

“Viongozi wa makapuni yote niliyopata nafasi ya kuzungumza nao wamesema wako tayari kuja nchini ili waweze kufanya mazungumzo na Serikali pamoja na wafanyabiashara wazalendo ambao wako tayari kuungana na wafanyabiashara hao katika kuwekeza nchini Tanzania.”

Waziri Mkuu alisema viongozi hao walimueleza maeneo ambayo wao wanaamini kuwa wanafanya vizuri na wangependa kupata kibali cha kuwekeza Tanzania baada ya mazungumzo yao na Serikali. Pia walieleza ni kwa namna gani Taifa litanufaika na uwekezaji wao.

Alisema, tayari wafanyabiashara binafsi 18 wa Tanzania walijitokeza kushiriki katika Mkutano huo na walifanya kazi kubwa na nzuri ya kuwahabarisha wenzao wa Urusi kuhusu mazingira mazuri ya kuwekeza yaliyopo nchini hasa baada ya Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais, Dkt. John Pombe Magufuli kuondoa kero, kanuni na taratibu ziliokuwa zikiyafanya mazingira ya uwekezaji kuwa magumu.

Awali, akizungumza kwenye Mkutano baina ya Wakuu wa nchi na Serikali kutoka mataifa ya Afrika na Urusi, Waziri Mkuu alisema kwa sasa Tanzania ni nchi sahihi kwa uwekezaji kwa wanaotaka kuwekeza barani Afrika kwani imedhamiria kukuza uchumi wake na kufikia wa kati ifikapo 2025 kwa kupitia sekta ya viwanda. Pia ni nchi yenye amani na utulivu.

 “Nchi yetu imejaliwa kuwa na maliasili nyingi ambazo vilele ni malighafi kwa viwanda kama vile mazao ya kilimo, misitu, bahari, maziwa, madini na mbuga za wanyama ambazo ni kivutio cha watalii,” alifafanua Waziri Mkuu.

Leo Oktoba 25, 2019 Mheshimiwa Majaliwa ataondoka nchini Urusi kwenda nchi ya Azerbaijan ambako pia atamwakilisha Rais Dkt. John Pombe Magufuli katika Mkutano wa Nchi zisizofungamana na upande wowote. Mkutano huo ni wa siku mbili.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Wapinzani Wapinga Mpango wa Nyuklia Rwanda

Nchi ya Urusi imeahidi kusaidia baadhi ya mataifa ya Afrika kujenga uwezo wake wa kutumia teknolojia ya nyukilia.

Hayo yamejitokeza katika mkutano baina ya Urusi na wakuu wa mataifa 40 ya Afrika uliomalizika huko Sochi nchini Urusi.

Rwanda ni miongoni mwa mataifa yanayotarajiwa kunufaika kwa ushirikiano huu. Hata hivyo,mpango huo umeanza kupata upinzani kutoka chama cha upinzani.

Kiongozi wa chama cha upinzani cha Green nchini Rwanda, Frank Habineza  amepinga mpango wa nchi yake kujenga kiwanda cha nyuklia kwa ushirikiano na Urusi akisema utakuwa na athari mbaya kwa wananchi.

Akizungumza na BBC, Habineza amesema wao hawakuunga mkono ushirikiano huo baina ya serikali ya Rwanda na Urusi kutokana na athari zake.

"Kulikuwa na mapatano ya Vienna kuhusu maswala ya nyuklia, na wakati huo huo Rwanda ilisaini mapatano mengine na Urusi kuanzisha kiwanda cha nyuklia hapa Rwanda. Mapatano ya Vienna yalikuwa kama kupalilia njia ya hayo ya Urusi kuanza kutekelezwa."

"Bungeni sisi hatukupigia kura mswada huo kwa sababu tuliona kwamba bado ni mapema kwa nchi ya Rwanda kujiingiza katika kuidhinisha matumizi ya nishati ya nyuklia kwa sababu sehemu zote kulikojengwa nyuklia kumekuwa na athari mbaya kwa wananchi na kwa mataifa yenyewe" amefafanua.

Muswada huo wa ujenzi wa nguvu za nyuklia ulipitishwa bungeni Rwanda ukipingwa na wabunge wawili pekee.

Lakini Serikali ya Rwanda inasema teknolojia ya nyuklia itaifaa kwa matumizi ya kutengeneza nishati, dawa na matumizi mengine ya amani.


-BBC


Share:

Job vacancy at The Association of African Higher Education Financing Agencies (AAHEFA)

VACANCY ANNOUNCEMENT – AAHEFA CEO The Association of African Higher Educaton Financing Agencies (AAHEFA), is an apex body of Higher Education Financing Agencies with Headquarters in Dar es Salaam. AAHEFA is an umbrella body of Higher Education Financing Institutions that deal with issuance of loans, bursaries/grants and scholarships to Higher Education students as well as recovery/ collection of… Read More »

The post Job vacancy at The Association of African Higher Education Financing Agencies (AAHEFA) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Programme Assistant Job at UNESCO,

Programme Assistant   Job Title: Programme Assistant (Only candidates with authorisation to work in Tanzania are eligible to apply) OVERVIEW OF THE FUNCTIONS OF THE POST Under the overall authority and direct supervision of the Head and Representative of UNESCO Dar es Salaam Office, the Programme Assistant is tasked with the delivery of a range of office, financial and… Read More »

The post Programme Assistant Job at UNESCO, appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Project Manager Job at Africa Academy for Public Health

Project Manager  The Africa Academy for Public Health (AAPH) is an independent organization registered in Tanzania with the mission to address public health priority challenges in sub-Saharan Africa through innovative scientific evidence, training and capacity building and knowledge translation. AAPH is currently implementing different health and nutrition research studies in 6 regions within Tanzania mainland and would like… Read More »

The post Project Manager Job at Africa Academy for Public Health appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Ijumaa October 25























Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger