Wednesday, 10 July 2019

MTANDAO WA 4G WA TIGO KUWANUFAISHA WAKAZI WA KIBAIGWA-DODOMA


Mkurugenzi wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya Tigo Kanda ya Kaskazini, Aidan Komba (wa tatu kutoka kulia), akishirikiana na Diwani wa Kata ya Kibaigwa, Richard Kapinye, kukata utepe kuashiria uzinduzi rasmi wa mnara wa mtandao wa 4G uliozindulliwa jana katika Mji wa Kibaigwa Wilaya ya Kongwa, Mkoani Dodoma.
Diwani wa Kata ya Kibaigwa Wilaya ya Kongwa, Mkoani Dodoma, Richard Kapinye akizungumza wakati wa uzinduzi wa rasmi wa mnara wa 4G wa kampuni ya Tigo katika eneo hilo.
Baadhi ya wakazi wa Mji wa Kibaigwa Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma, walishiriki katika hafla ya uzinduzi wa mnara wa huduma ya 4G ya kampuni ya mawasiliano ya Tigo.

---
Katika jitihada zake za kuboresha mawasiliano na kurahisisha maisha ya watanzania kupitia teknolojia ya kidigitali, kampuni ya mawasiliano ya Tigo, imezindua mnara wa mawasiliano wa 4G katika mji wa Kibaigwa mkoani Dodoma.

Akiongea wakati wa hafla ya uzinduzi huo uliohudhuriwa na wakazi wa mji huo, Mkurugenzi wa Tigo kanda ya kaskazini, Aidan Komba, alisema uboreshaji wa mtandao kutoka 3G kwenda 4G unatarajiwa kufungua fursa mpya za kibiashara ambazo zitakuza maendeleo ya kiuchumi katika eneo hilo.

“Kwa kuzingatia kwamba Kibaigwa ina shughuli nyingi muhimu za kiuchumi hususani za kilimo na ufugaji na pia ni kiunganishi muhimu na maeneo mengine ya nchi, sasa ni wakati wa wakazi wa Kibaigwa na vitongoji jirani kutumia Intaneti yenye kasi zaidi ili kuendeleza biashara na shughuli mbalimbali za kiuchumi,” alisema Komba.

Uzinduzi huu unaenda sambamba na ofa maalum kwa ajili ya wateja watakaobadili laini zao kwenda mtandao wa 4G. Wateja hawa watazawadiwa kifurushi cha 4GB cha Intaneti ya bure itakayotumika ndani ya siku 7.

Vilevile, wateja watakaonunua kifurushi chochote cha intaneti kwenye mitandao uliyoboreshwa kutoka 2G kwenda 3G watazawadiwa MB100 kila wanaponunua kifurushi.

Pia kufuatia uzinduzi huu, wateja sasa wataweza kunufaika na huduma mbalimbali za kibunifu kutoka Tigo kama vile “Saizi Yako” ambayo inawapatia wateja ofa mbalimbali za SMS, Intaneti na kupiga simu kulingana na mahitaji na matumizi ya mteja. Kwa mfano mteja anayetumia dakika nyingi zaidi kuliko Intaneti na SMS atapata kifurushi cha dakika za muda wa maongezi. Mteja anayetumia zaidi Intaneti kuliko dakika za maongezi na SMS atapata kifurushi cha Intaneti kinachoendana na matumizi yake.

Tigo inaendelea kuwekeza kwenye teknolojia ya kisasa hususani 4G+ ili kukidhi mahitaji makubwa ya data na Intaneti yenye kasi kutokana na ongezeko la matumizi ya simu janja za bei nafuu.
Share:

Waziri Mbarawa Afungua Mkutano Wa Bodi Za Maji Za Mabonde




Share:

Serikali Yapokea Gawio La Shilingi Bilioni 1 kutoka Benki ya Posta Tanzania (TPB)

Na Saidina Msangi na Farida Ramadhani, WFM, Dodoma
Serikali imepokea gawio la Shilingi Bilioni 1 kutoka Benki ya Posta Tanzania (TPB) linalotokana na faida ya uwekezaji wake wa asilimia 83 ya hisa  katika Benki hiyo katika mwaka wa fedha 2018/19.

Hafla ya makabidhiano ya Hundi kifani ya gawio hilo imefanyika jijini Dodoma, kati ya Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb) ambaye alipokea kwa niaba ya Serikali, na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Benki hiyo Dkt. Edmund Mndolwa.

Akizungumza katika hafla hiyo Dkt. Mpango aliipongeza Benki hiyo kwa kutoa gawio kwa Serikali, na kuahidi kuwa fedha hizo zitatumika katika shughuli mbalimbali za maendeleo nchini.

“Utoaji huu wa gawio ni kiashiria tosha kwa Serikali kuwa Benki inazidi kukua na kuwapa moyo watanzania na wawekezaji kuwa TPB inatoa huduma bora katika jamii”, alisema Dkt. Mpango.

Aliitaka Benki hiyo kuongeza wigo wa utoaji huduma ili kuwafikia wananchi hususani waishio vijijini pamoja na kutoa elimu kwa wananchi hao kuhusu umuhimu wa  kuweka akiba, kukopa sambamba na kurejesha mikopo kwa wakati.

“Riba katika benki zetu bado ni kubwa taasisi za fedha zione namna ya kuzipunguza sambamba na kutoa mikopo kwa kuzingatia kanzidata ya wakopaji ili kuepuka mikopo chechefu.”, alisisitiza Dkt. Mpango.

Aidha, Dkt. Mpango ameiagiza Benki hiyo kuendelea kuwapa wanawake  kipaumbele katika upatikanaji wa huduma za fedha na mikopo ili waweze kuendesha shughuli za maendeleo.

Pia Dkt. Mpango aliiagiza  TPB kusimamia uadilifu kwa watumishi wake na kuwa makini na kutoa taarifa za  miamala yenye mashaka ili kuzuia utakasishaji wa fedha haramu.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TPB Dkt. Edmund Mndolwa alisema kuwa gawio hilo ni sehemu ya faida ya Sh. Bilioni 17.2 kabla ya kodi ambayo Benki yake imeipata katika mwaka wa fedha 2018/19. Pia ameeleza kuwa Benki hiyo itaendelea kutoa huduma bora ili kukidhi mahitaji ya wanahisa wake na wananchi kwa ujumla.

Aidha, Dkt. Mndolwa aliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa utendaji mzuri ambao umeiwezesha Benki hiyo kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa weledi na kuahidi kuendelea kushirikiana nayo ili kukuza uchumi wa nchi.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumatano 10 July





















Share:

Tuesday, 9 July 2019

Picha : RAIS MAGUFULI AZINDUA HIFADHI YA TAIFA YA BURIGI CHATO MKOANI GEITA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla pamoja na viongozi wengine wakivuta utepe kuashiria uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla katika picha ya pamoja na viongozi mbalimbali, Wakuu wa mikoa, Viongozi wa Vyama vya Siasa, Dini pamoja na Mabalozi mara baada ya kuzindua Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Chato kabla ya kuzindua Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Mkuu wa Mkoa Mstaafu wa Mkoa wa Kagera Meja Jenerali Mstaafu Salum Kijuu mara baada ya kumkabidhi Hundi ya Shilingi milioni kumi , kama shukrani katika mchango wake alioutoa katika utunzaji wa wa hifadhi mbalimbali ikiwemo Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wafanyakazi wa TANAPA wakati akielekea kwenda kuzindua Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiondoka mara baada ya kuzindua Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita.
Wakuu wa Mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Mara na Simiyu wakijadiliana jambo wakati wa sherehe za uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama wakati Wimbo wa Taifa ukipigwa kabla ya kuanza kwa sherehe za uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikagua Kikosi cha Jeshi Usu la kukabiliana na vitendo vya Ujangili pamoja na kulinda hifadhi za taifa kabla ya kuanza kwa sherehe za uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi (Burigi -Chato National Park) ilioyopo Chato mkoani Geita.
Kikosi cha Jeshi Usu cha kukabiliana na Vitendo vya Ujangili pamoja na kulinda hifadhi za Taifa kikipita mbele ya Amiri Jeshi Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya ukaguzi katika sherehe hizo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Tuzo ya Hifadhi bora ya Serengeti ambayo imekuwa ya kwanza katika Bara la Afrika kwa mwaka 2019 kutoka kwa Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia sanamu ya Baba wa Taifa Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere yenye ujumbe maalum kuhusu umuhimu wa utunzaji wa mazingira ya wanyama pori.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimshukuru Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla mara baada ya kumkabidhi Sanamu hiyo ya Baba wa Taifa. Rais Dkt. Magufuli ametoa maelekezo kuwa Sanamu hiyo aliyokabidhhiwa ijengewe eneo zuri katika hifadhi hiyo ya Burigi Chato ili watalii wakija waweze kumjua zaidi Muasisi wa Taifa letu Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. PICHA NA IKULU
Share:

Naibu Spika Ataka Misingi Ya Utafiti Kufuatwa Katika Uchapishaji Na Utangazaji Wa Taarifa

NAIBU Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson amesema misingi ya utafiti ni jambo muhimu na la msingi litakalopaswa kuzingatiwa katika uchapishaji na  utangazaji wa taarifa mbalimbali ili kuweza kulinda misingi ya amani iliyopo nchini.

Akizungumza leo Jumanne (Julai 9, 2019) Jijini Dar es Salaam katika Kongamano maalum la siku ya Amani lililoandaliwa na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) katika Maonesho ya 43 ya Biashara ya Kimataifa Dar es Salaam (DITF), Dkt. Tulia alisema uchapishaji na utangazaji wa taarifa yoyote haina budi kuwa na tija katika taifa.

Dkt. Tulia alisema katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na utamaduni uliozoeleka wa kutangaza na kuchapisha taarifa mbalimbali katika jamii kupitia vyombo vya habari pasipo na kuzingatiwa kwa misingi ya utafiti hatua inayoweza kuleta migongano isiyo na tija kwa taifa.

“Serikali ya Awamu ya Tano tunaona inatekeleza miradi mikubwa ya maendeleo, ikiwemo mradi wa umeme katika Mto Rufiji, sni wajibu wetu kulinda misingi ya amani iliyopo ili tuone matunda ya miradi hii katika nchi yetu” alisema Tulia.

Aidha Dkt. Tulia alisema ni wajibu wa misingi ya utafiti ikazingtiwa katika taaluma mbalimbali ikiwemo ya uandishi wa habari kwani wapo baadhi ya watu wanaofikiri kuwa wanaweza kuandika na kutangaza habari pasipo na kusomea taaluma hiyo, jambo ambalo si la kweli kwa kuwa uandishi wa habari ni taaluma nyeti na muhimu kama zilivyo taaluma nyingine.

Aliongeza kuwa ni wajibu wa Watanzania wote kusoma vitabu mbalimbali vilivyoandikwa na waasisi wa taifa vikiwemo vitabu vya Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere ambavyo vimekuwa na wingi wa maarifa na  maelekezo yanayopaswa kuzingatiwa ili kuweza kujenga taifa lenye umoja, upendo na mshikamano.

Naye Mkuu wa Chuo cha Uandishi wa Habari na Mawasiliano Zanzibar, Imane Duwe alisema mfumo wa soko huria nchini yameleta mabadiliko makubwa katika tansia ya habari na mawasiliano ikiwemo matumizi ya mitandao ya kijamii, ambayo imekuwa imeleta hamasa kubwa kwa makundi mbalimbali ya kijamii ikiwemo vijana.

“Hapo awali mwandishi wa habari alipokuwa akitumwa kazi na mhariri wake ni lazima arudi na atoe taarifa kwa mkuu wake pamoja na habari au taarifa hiyo kuweza kufanyiwa uhariri kabla ya kuchapishwa na kutangazwa lakini kwa sasa hali ni tofauti kidogo, kwani tukio lolote linaweza kutumwa wakati huo huo kupitia vyombo vya kisasa zaidi vya mawasiliano” alisema.

Aliongeza kuwa vyombo vya habari vya zamani ikiwemo Magazeti, Redio na Televisheni kwa sasa navyo vimeingia katika ushindani mkubwa wa soko kwani kwa upande wao pia wameanzisha mitandao mbalimbali ya kijamii ili kuweza kuwa na njia za kisasa zaidi za mawasiliano.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Joseph Butiku alisema ni wajibu wa Viongozi na Watanzania wajenge utamaduni wa kuheshimu tunu na misingi mikuu ya amani nchini ikiwemo Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, misingi ya Azimio la Arusha ambayo iliasisiwa na Hayati Baba wa Taifa  Mwalimu Julius Nyerere.

Aidha aliongeza kuwa ili kuweza kujenga Taifa lenye misingi bora ya amani ni wajibu wa Serikali kupitia Viongozi kuwa na  matumizi na usimamizi bora wa rasilimali za taifa na kuhakikisha zinawanufaisha  wananchi wote pamoja na kuweka misingi imara katika ulinzi rasilimali hizo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Amani Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum alisema Tanzania inaweza kufikia na kufanya mapinduzi makubwa katika sekta ya viwanda iwapo Viongozi wataweka mkazo katika usimamizi wa rasilimali watu yenye kutambua umuhimu wa kulinda amani, weledi, uzalendo na kujiamini.

“Moja ya Nguzo muhimu katika kufikia uchumi wa viwanda ni mfanyakazi, hivyo ni wajibu kila mwenye dhamana hiyo kutimiza wajibu wake huku akiogopa kufanya vitendo vya ufisadi kwani hata katika vitabu takatifu vimezungumzia ufisadi ni jambo baya sana”  alisema Sheikh Salum.

MWISHO


Share:

Benki Ya Maendeleo Ya Afrika Kuipandisha Daraja Tanzania

Na Saidina Msangi na Josephine Majura, WFM, Dodoma
Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) inatarajia kuipandisha daraja Tanzania kutoka katika hadhi ya kunufaika na Mfuko wa Maendeleo wa Benki (ADF) hadi kuwa na hadhi itakayoiwezesha Tanzania kuweza kupata rasilimali fedha zaidi kupitia dirisha la African Development Bank (ADB) la Benki ya Maendeleo ya Afrika.

Endapo Tanzania itafanikiwa kupandishwa hadhi, nchi itaweza kunufaika na ongezeko la fedha kutoka Benki ya Maendeleo ya Afrika kutoka Dola za Marekani milioni 350 kwa mwaka hadi Dola za Marekani milioni 812 kwa mwaka.

Hayo yamesemwa Jijini Dodoma na Mwakilishi Mkazi wa Benki hiyo Dr. Alex Mubiru alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Isdor Mpango, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Fedha na Mipango-Treasury Square.

Katika mazungumzo hayo, Dr. Alex ameeleza kuwa hatua hiyo ya kupandishwa hadhi ama kupandishwa daraja inatokana na uchumi wa nchi kufanya vizuri hususani katika maeneo ya kasi ya ukuaji wa uchumi na kuwa na deni himilivu.

“Hatua hiyo itaiwezesha Tanzania kupata fedha zaidi kutoka katika Benki hiyo na kuwezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo na vipaumble kwa Serikali” Alisisitiza Bw. Mubiru.

Mwakilishi Mkazi wa Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB), Bw. Alex Mubiru, amesema kuwa benki hiyo inajivunia kufanya kazi na Tanzania ambayo ni miongoni mwa nchi Waasisi wa Benki hiyo.

Katika mazungumzo yao, Dkt. Mpango ameeleza kuwa Serikali inajivunia kufanya kazi pamoja na Benki ya AfDB kwa kuwa benki hiyo imekuwa na masharti rafiki katika upatikanaji wa mikopo.

Dkt. Mpango amesema kuwa Benki hiyo ina mtazamo chanya katika maendeleo ya watu na kuwa dira katika mipango ya maendeleo na kuahidi kushirikiana nao vyema katika kukuza uchumi wa nchi.

Aidha, Waziri Mpango ameipongeza benki hiyo kwa kukubali kutekeleza miradi ya Ujenzi wa Barabara ya Mzunguko Dodoma (km110.2) kwa kiwango cha lami pamoja na ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Dodoma (Msalato) na kubainisha kuwa uamuzi huo ni mzuri kwani licha ya Dodoma kuwa ni Makao Makuu ya nchi lakini pia miundombinu hii itaunganisha na kuchochea ukuaji wa uchumi na biashara katika mikoa mingi nchini pamoja na nchi jirani.


MWISHO.


Share:

Serikali kujenga uwanja mkubwa wa mpira Chato

Serikali imetangaza kujenga uwanja mkubwa wa mpira wilayani Chato, mkoani Geita ili kukuza sekta ya michezo nchini na kuvutia watalii na wawekezaji. 

Uwanja huo unatarajiwa kuwa wa pili kwa ukubwa baada ya wa Benjamin Mkapa ulipo jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Nishati Medard Kalemani amesema hayo wakati akihutubia sherehe za uzinduzi wa Hifadhi ya taifa ya Burigi-Chato na kueleza kwamba uwanja huo utaitwa Chato Stadium na ujenzi wake unatarajiwa kuanza hivi karibuni.

"Hivi karibuni tunajenga Uwanja wa mipra Chato Stadium ambao utatumika sana katika kuhamasisha Wawekezaji na hasa Watalii wanaotoka nje ya nchi yetu" amesema Waziri Medard Kalemani.


Share:

VIJANA WAUANA KWA MAPENZI

Kijana Fadhili Abdallah Mkunguja {23} mkazi wa Kijiji cha Ruchemi, Kata na Tarafa ya Milola, Mkoa wa Lindi, amefariki dunia baada ya kushambuliwa kwa kukatwa shingoni na kitu chenye ncha kali na mwenzake aitwae Issa Khalifa Mtumwa (20) katika ugomvi uliotokana na wivu wa kimapenzi.

Baadhi ya mashuhuda wa tukio hilo, wameeleza kuwa mauaji hayo yamefanyika wakati wananchi kijijini hapo wakiwa katika sherehe za ngoma ya unyago, ambapo wamesema marehemu alikuwa na mahusiano ya kimapenzi na mchumba wa Issa Khalifa, aitwae Hawa Hamadi {15} na kufanikiwa kupata nae Mtoto mmoja.

"Issa na huyo Hawa ni mtu na mchumba wake, wanaishi nyumba moja kupika na kupakua na wamefanikiwa kupata mtoto wao mmoja", ameeleza mmoja wa mashuhuda ambao hawakutaka jina lake kutajwa.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji wa Kijiji cha Ruchemi, Ally Mussa Mkalola, amekiri kuwepo kwa taarifa hizo na yeye akizipokea kutoka kwa wasamalia wema kuwa mchumba wa Hawa amekutwa akiwa na Fadhili Abdallah wakielekea kichakani.

Mkalola amesema taarifa hiyo ilimfanya Issa kupandwa na hasira na kuamua kuwafuatilia huku akiwa ameshika panga mkononi, kwa ajili ya kwenda kumshambulia Fadhili ambaye kwa wakati huo alidaiwa kuwa na mchumba wake.

"Kitendo cha kumkuta Fadhili ameketi na mchumba wake pale chini ya mti, hakuuliza alichokifanya ni kumshambulia shingoni yule mgoni wake, huku yule msichana akitimua mbio kuelekea nyumbani kwao", amesema Mkalola.

Kamanda wa Polisi mkoani Lindi, ACP Prodansiana Protas alipoulizwa kuhusiana na mauaji hayo, amethibitisha kutokea na kueleza kuwa wanaendelea kumtafuta mtuhumiwa Issa Khalifa, ili sheria ichukue mkondo wake.
Chanzo - EATV
Share:

AUA MTU KWA KUSIKILIZA MUZIKI


Kushoto ni marehemu na kulia ni mtuhumiwa wa kesi ya mauaji

Michael Adams, Mkazi wa nchini Marekani anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kesi ya mauaji ya kijana mwenye umri wa miaka 17, kwa kumpiga na kumkaba hadi kufariki kwa sababu ya kusikiliza muziki.

Polisi wamesema tukio hilo limetokea katika eneo la Circle K , Peoria ave lililopo nchini Marekani, na mtuhumiwa mwenyewe Michael Adams amekiri kufanya tukio hilo na amewaambia maofisa wa polisi sababu ni marehemu alikua anacheza na kusikiliza muziki wa rap.

“Kijana huyo alikua anasikiliza muziki wa rap, na aina ya muziki huo unamfanya yeye kutokuwa salama na ameshambulia watu wengi ambao wanasikiliza muziki huo”, amesema mtuhumiwa huyo.

Aidha mwanasheria wa mtuhumiwa huyo amesema amemtetea mteja wake kuwa alikua anasumbuliwa na ugonjwa wa kiakili na aliachiwa kutoka jela siku 10 zilizopita kabla kufanya tukio hilo.

“Walimuachia kurudi mtaani bila ya kumpima afya yake, tiba na hata kumuwekea ulinzi. Huko ni kushindwa kwa idara hiyo na inatakiwa kufanyiwa marekebisho”.
Share:

Rais Magufuli Aitaka Wizara ya Maliasili Iweke a mikakati kuongeza watalii

Rais Magufuli ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kuweka mikakati madhubuti ya kuongeza watalii nchini ambao ametaja baadhi ya malalamiko ambayo amekuwa akiyapata kupitia ripoti ya robo mwaka na kiitaka wizara hiyo kuhakikisha inafanya kazi masuala hayo.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jumanne Julai 9, wilayani Chato mkoani Geita katika uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi – Chato yenye ukubwa wa kilometa za mraba 4,702.

“Ninatoa wito kwa Wizara ya Maliasili na Utalii kuendelea kujipanga na kuweka mikakati madhubuti ya kuongeza watalii nchini, miongozi mwa malalamiko ambayo nimekuwa nikiyapata ni pamoja na gharama za utalii kuwa juu, usafi kwenye hoteli na mengine mengi hivyo hamna budi kufuatilia mambo hayo,” amesema.

“Ninawasihi kuwa na utaratibu wa kufanya kaguzi mara kwa mara lakini pia wekeni mikakati ya kujenga uwezo wa waongoza watalii na kuhakikisha wote wanatambuliwa rasmi maana kuna wengine wanadanganya watalii, hakikisheni hifadhi zetu zinakuwa na mchanganyiko mzuri wa vivutio,” amesema.

Aidha amewataka watanzania kujega utamaduni wa kutembelea vivutio vya ndani hasa katika maeneo ya hifadhi zinazowazunguka ili kuiongezea nchi kipato na kukuza uchumi wa nchi ambapo ameitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kuweka gharama nafuu kwa watalii wa ndani ili kuwezesha zoezi hilo.

“Ninahimiza Wizara kuendelea kuhamasisha utalii wa ndani ikiwemo kwa kuweka gharama za nafuu pia kwa watanzania ninawasihi kujenga utamaduni wa kutembelea vituo vyetu vya utalii pia tuanzisha hifadhi ndogo ndogo za kufuga wanyama pori,” amesema.

“Mimi ninafikiria kuanzisha hifadhi ndogo lakini nitafuga wale wanyama ambao ni wapole nisije nikajikuta nimekuwa kitoweo huko ndani, ninasisitiza Wizara hakikisheni mnaangalia gharama kwa wazawa zinakuwa chache,” amesema.


Share:

Mwakyembe Atoa Onyo Kwa Wanaosambaza Picha za Ajali Mitandaoni

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe amewaonya watu wanaopiga picha kwa simu mara tu zinapotokea ajali na kusambaza mitandaoni.

Mwakyembe ametoa onyo hilo leo Jumanne Julai 9, wakati wa shughuli ya kuaga miili ya wafanyakazi wa Azam Media waliofariki jana Julai 8, katika ajali ya gari kati ya Shelui na Igunga na kuongeza kuwa Sheria ya Makosa ya Mitandao inazuia kufanya hivyo.

"Niwaombe Watanzania tuendeleze utamaduni wa utu ndugu zetu wanapopata ajali, niwaombeni acheni tabia ya kupiga picha na kurusha kwenye mitandao, sheria ya mitandao inakataza, hatutazungumza tena hili ni onyo la mwisho" - Waziri Mwakyembe


Share:

Rais Magufuli .Ampongeza Faru Rajabu

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli, amempongeza faru Rajabu, ambaye ni mtoto wa Faru John, kwa juhudi zake za uzalishaji na kuzidi kuongeza idadi ya faru hadi kufikia faru140, katika hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Rais Magufuli ameyabainisha hayo leo Julai 9, wakati wa Uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi, iliyopatikana mara baada ya mapori matatu ya akiba kuunganishwa, likiwemo pori la Burigi, Biharamulo na Kimisi Wilayani Chato Mkoani Geita.



"Mwaka 2014 kulikuwa kuna tembo 43,330 lakini hivi sasa baada ya kuanzisha kikosi cha kupambana na ujangili wamefikia zaidi ya 60,000 faru hawakuwepo kabisa ila sasa wamefikia 163 ", amesema Magufuli.
 
''Hakuna budi kupongeza kazi kubwa na nzuri iliyofanywa na faru rajabu, mtoto wa faru John naambiwa kwasasa amezalisha watoto 40, nadhani wajina wangu john alikuwa hajitumi vizuri'


Share:

Iran Yasema Italipa Kisasi kwa Uingereza

Mnadhimu mkuu wa majeshi ya ulinzi nchini Iran Meja Jenerali Mohammad Bagheri amesema leo kwamba, hatua ya Uingereza kuikamata meli yake ya mafuta nje ya eneo la Gibraltar haitapita bila majibu. 

Kwa mujibu wa shirika la habari la Tasnim Bagheri amesema kukamatwa kwa meli hiyo ya mafuta ya Iran chini ya misingi ya visingizio vya kutengenezwa, hakuta pita bila kujibiwa na itakapolazimika Tehran itatoa jibu sahihi. 

Jeshi la majini la Uingereza liliingia katika meli hiyo, Grace 1, nje ya pwani ya Gibraltar siku ya Alhamis na kuikamata kuhusiana na shutuma kwamba inavunja vikwazo kwa kupeleka mafuta nchini Syria. 

Iran imetaka kuachiwa mara moja kwa meli hiyo ya mafuta, wakati kamanda huyo wa jeshi la mapinduzi la Iran ametishia siku ya Ijumaa kukamata meli za Uingereza kwa kulipa kisasi.


Share:

RAIS MAGUFULI AMPONDA KIAINA WA JINA WAKE 'JOHN' KWA UZEMBE KUZALISHA

Rais wa Tanzania, John Magufuli amesema tangu kuanzishwa kwa kikosi kazi cha kupambana na ujangili mwaka 2016 idadi ya wanyama hapa nchini imeongezeka.

Magufuli amesema hayo leo Jumanne Julai 9 mwaka 2019 wakati wa uzinduzi wa Hifadhi ya Taifa ya Burigi-Chato mkoani Geita.

"Mwaka 2014 kulikuwa kuna tembo 43,330 lakini hivi sasa baada ya kuanzisha kikosi cha kupambana na ujangili wamefikia zaidi ya 60,000 faru hawakuwepo kabisa ila sasa wamefikia 163 hatuna budi kumshukuru Faru Rajabu mtoto wa Faru John," amesema Magufuli.

"Inaonekana yule Faru wajina wangu (John alikuwa hajitumi vizuri) huyu mtoto wake nimeambiwa mpaka sasa amekwisha zalisha 43," amesema Rais Magufuli huku akitabasamu.
Na Ephrahim Bahemu, Mwananchi
Share:

Waziri Lugola aagiza Polisi kuwakamata wanaowapa mimba Wanafunzi

Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola, amelitaka Jeshi la Polisi  wilayani Bunda, mkoani Mara, kuwakamata wazazi wanaowatumia wanafunzi katika shughuli za kilimo na mifugo na kuwasababishia kukatisha masomo yao.

Pia Waziri Lugola amewaagiza Polisi hao kuwakamata watu wanaowarubuni wanafunzi wa kike na kuwasababishia kukatisha masomo kwa kuwapa mimba.

Waziri Lugola, ametoa kauli hiyo akiwa wilayani Bunda katika  ziara ya kutembelea miradi ya maendeleo ndani ya jimbo lake la Mwibara, ambapo amesema kuwa lazima Watoto waendelezwe kielimu ili iwaletee manufaa kwao na kwa taifa.

“Nina taarifa baadhi ya wazazi uwatumikisha Watoto wao kufanya shughuli za kilimo, kulima dengu, pamoja na kuwatumia katika kuchunga mifugo, hii haikubaliki, wazazi lazima muwajibike kwa kutowatendea vema watoto,” alisema Lugola na kufafanua;

“Kuvunja sheria za nchi kwa kutompa elimu mtoto ni kosa, hivyo, wazazi wanaotumikisha Watoto shughuli za uchumi wa wazazi hao,hakika tutawakamata, OCD (Kamanda wa Polisi Wilaya), akikisheni mnawakamata wazazi ambao wanawatumia Watoto katika shughuli zao binafsi na pia kusababisha utoro katika shule zetu.”

Pia Lugola aliwahoji wanafunzi wa Shule ya Msingi Karukekere, Kata ya Namuhura, Wilayani humo, kuwa wanataka Serikali iwafanyie nini wazazi wao ambao wanawakatisha masomo, hata hivyo,wanafunzi hao walisema wazazi wao washitakiwa kwa kutowapa haki zao za msingi.

Alisema ili kupunguza utoro ndani ya Jimbo hilo, aliwataka wazazi kufuatilia elimu ya watoto wao, kwa kuhakikishe wanakua na daftari ambalo wanafunzi hao wataenda nalo shuleni, na Mwalimu atasaini baada ya mwanafunzi huo kufika shuleni na pia atasaini kabla ya muda wa kuruhusiwa kwenda nyumbani, hatua hiyo itapunguza zaidi utoro katika jimbo lake.


Share:

Taasisi Za Kidini Na Jumuiza Kijamii Katika Mikoa Ya Mbeya, Iringa, Njombe, Rukwa Na Songwe Kuhakikiwa Kuanzia Tarehe 15 Julai, 2019




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger