Friday, 16 December 2016

MWANAFUNZI ALIYEFUKUZWA CHUO CHA UDOM KWA KUONGOZA MGOMO ARUDISHWA CHUO AMALIZIE MASOMO



MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dodoma imetengua uamuzi wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom) ya kumfukuza mwanachuo Phillip Mwakibinga na kuamuru arudishwe ili kumalizia masomo yake.
Uamuzi huo ulitolewa jana na Naibu Msajili wa Mahakama Kuu, John Chaba kwa niaba ya Jaji Awadhi Mohamed aliyekuwa akisikiliza shauri hilo.
Mwakibinga alikuwa akisoma Shahada ya Kiswahili mwaka wa tatu wakati akisimamishwa na alikuwa Waziri Mkuu wa Kitivo cha Sayansi ya Jamii. Katika uamuzi huo, mahakama ilisema mlalamikaji hakupewa nafasi ya kusikilizwa na hivyo kukiuka haki ya asili ya mlalamikaji. Pia mlalamikaji hakupewa haki ya kusikilizwa na hakuandikiwa mashtaka rasmi.
“Baraza liliegemea upande moja bila kumhoji wala nafasi ya kusikilizwa na kujitetea,” alisema. 
Mwakibinga alifukuzwa Udom Januari 14, mwaka jana, kwa madai ya kuongoza mgomo ambapo siku hiyo baraza la chuo lilikaa na kumfukuza bila kupewa nafasi ya kusikilizwa.
Alifungua kesi Mahakama Kuu Kanda ya Dodoma kutaka mahakama kutengua uamuzi huo. Kwa mujibu wa wakili wa Mwakibinga, Elias Machibya alisema awali waliomba ruhusa ya kufungua kesi na wakapewa Februari 5, mwaka jana wakiomba kutengua maombi ya baraza la Chuo Kikuu cha Dodoma.
“Tulipata kibali cha kufungua kuomba kutengua maamuzi ya Chuo Kikuu cha Dodoma kwa kumfukuza,” alisema.
Alizitaja sababu kuu tatu za kupinga mwanafunzi huyo kufukuzwa chuo kuwa ni pamoja na kutopewa nafasi ya kusikilizwa, hakuna hatua za nidhamu zilizochukuliwa, walimfukuza wakidai aliwahi kuhusika na migomo ya nyuma.
Alidai barua ya kumfukuza ilisainiwa na Profesa Shaban Mlacha.
Januari 14, mwaka jana uongozi wa Udom ulimfukuza Mwakibinga ambaye wakati huo alikuwa Waziri Mkuu wa Serikali ya wanafunzi, Kitivo cha Sayansi ya Elimu ya Jamii, na kupewa barua ya kusimamishwa kutokana na kosa la kuhamasisha mgomo.
Uongozi huo ulisema Mwakibinga amefukuzwa kabisa kwa kuwa alishawahi kujihusisha na mgomo wa mwaka 2010/2011 akafukuzwa lakini akakata rufaa na kuomba msamaha kwenye Kamati nidhamu.
“Baada ya kukata rufaa Kamati ikamuonea huruma ikamrudisha kabla ya kurudi alitakiwa aje na kiapo kutoka kwa mwanasheria kwamba hatajihusisha na mgomo tena lakini akarudia tena kosa hilo."

Mwakibinga amesema amefurahia uamuzi huo kwani ndio sababu ya msingi ya kufungua kesi na mahakama imetenda haki. Alisema anasubiri barua ya hukumu ambayo itatoka kesho ndipo taratibu zake za kurudi chuo zitakapoanza.
Share:

Thursday, 15 December 2016

HAYA HAPA MAJINA KIDATO CHA SITA WALIOCHAGULIWA JKT AWAMU YA PILI 2016

 BOFYA JINA LA KIKOSI HAPO CHINI  KUANGALIA MAJINA JA VIJANA WA MUJIBU WA SHERIA AWAMU YA PILI  2016  

BULOMBORA JKT-KIGOMA                           RWAMKOMA JKT -MARA                  MSANGE JKT-TABORA

KANEMBWA JKT-KIGOMA                                         MTABILA-KIGOMA                      RUVU JKT-PWANI

MAKUTUPORA JKT- DODOMA                           MGAMBO JKT-TANGA              MARAMBA JKT- TANGA

MAFINGA JKT- IRINGA                                                                                MLALE JKT -RUVUMA


Share:

New AUDIO | Mwasiti - Kaa Nao | Download

Share:

New AUDIO | Mwasiti - Kaa Nao | Download

Share:

New AUDIO | P Square Ft Akon - Bedroom | Download


Share:

New AUDIO | QChief - Sungura | Download


Share:

Official VIDEO | Mr Nay - Sijiwezi | Watch/Download


Share:

New AUDIO[Official] | Diamond Platnumz Ft. Neyo - Marry You | Download

Share:

New AUDIO | Msaga Sumu - Tatizo Nyota | Download


Share:

Batch 10 allocations for SUA Students receiving loan in Academic year 2016/2017

Share:

VIDEO: Prof. NDALICHAKO AKITOA UFAFANUZI KUHUSU TANGAZO LA AJIRA ZA WALIMU LILILOTEWA IVI KARIBUNI - Majibu ya serikali kuhusu wanaosubiri ajira za ualimu

 
December 15 2016 Waziri wa
Share:

Selemani Msindi - "Afande sele" Ajitoa ACT-WAZALENDO na Kusema hatojihusisha na Siasa Tena


Image may contain: 4 people, people smiling, people standing
Share:

BREAKING NEWS:TANGAZO LA AJIRA MPYA ZA WALIMU WA SAYANSI NA HISABATI SHULE ZA SEKONDARI NCHINI 2016

Image result for SERIKALI YA TANZANIA  
TANGAZO KWA UMMA
SERIKALI INATARAJIA KUAJIRI WALIMU WA MASOMO YA SAYANSI NA HISABATI KWA SHULE ZA SEKONDARI NCHINI.

AJIRA HII NI KWA WALIMU WA DIPLOMA NA DIGRII WALIOHITIMU MAFUNZO YA SAYANSI NA HISABATI MWAKA 2015.

WAHITIMU HAO WANATAKIWA KUWASILISHA NAKALA ZA VYETI VYAO VYA ELIMU SEKONDARI (KIDATO CHA NNE NA SITA) NA TAALUMA YA UALIMU KWA AJILI YA UHAKIKI.

NAKALA HIZO ZIWASILISHWE KUPITIA EMAIL info@moe.go.tz KUANZIA LEO HADI TAREHE 16/12/2016(IJUMAA).

YEYOTE AMBAYE VYETI VYAKE HAVITAHAKIKIWA HATAFIKIRIWA KATIKA UAJIRI.
TANGAZO HILI LINAPATIKANA KATIKA TOVUTI YA NACTE,TCU,NECTA,MOE NA TAMISEMI.

imetolewa na:
Katibu Mkuu
Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
Share:

Wafuasi wa CUF watwangana ngumi Mahakamani

Share:

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI DEC 15 2016

https://mpaper.s3-us-west-2.amazonaws.com/mpaper_1481747951_5851adefb650a/mpaper_1481747951_5851adefb650a.jpg
Share:

Aliyetobolewa macho uso kwa uso na Scorpion mahakamani,Atoa U shahidi Jinsi Alivyo Shambuliwa na Kuporwa

Share:

Kauli ya CHADEMA kufuatia kutoweka kwa kada wao Bwana Ben Sanane

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema hadi sasa hakijui alipo msaidizi wa Mwenyekiti wa chama hicho, Ben Saanane.

Kimevitaka vyombo vya dola, kuchukua hatua za haraka kuhakikisha msaidizi huyo anapatikana haraka. 
Saanane inadaiwa alitoweka katika mazingira ya kutatanisha tangu Novemba 18, mwaka huu. Juhudi za kumtafuta katika vituo vya polisi, hospitalini na vyumba vya kuhifadhia maiti, zimefanyika bila mafanikio.

Kauli hiyo imetolewa na Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, Tundu Lissu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Saanane ambaye hajulikani aliko. 
Alisema hata wao hawajui alipo, hawafahamu kama yuko hai au ameshikiliwa mahali. Kwamba wanachokijua ni kwamba hawajui aliko.

“Katika mazingira haya, tunaiomba serikali na vyombo vyake vya ulinzi, ituambie kama imemkamata na inamshikilia Ben Saanane tuanzie hapo…lakini kama hawajamkamata na hawamshikilii, serikali na vyombo vyake watueleze mawasiliano yake ya mwisho yalikuwa lini, na nani, wapi na yalihusu nini,” alisema.

Alisema kwa kuwa serikali ndiyo yenye udhibiti wa mipaka yote nchini, iwaeleze kama kuna rekodi yoyote inayoonesha Ben aliondoka nchini kwa kupitia mipaka hiyo, kama ni mipaka ya nchi kavu, majini au viwanja vya ndege.

Katika hatua nyingine, alisema pamoja na majibu hayo, lakini pia wanaitaka serikali pamoja na vyombo vyake vya dola, kufukua miili ya watu waliokufa katika mto Ruvu na ifanyiwe uchunguzi ili wajulikane watu hao ni akina nani, ili isije kuwa miongoni mwa watu hao ni Saanane.

Lissu alisema kuwa mawasiliano ya mwisho kati ya Saanane na Mbowe, yalikuwa ni Novemba 14, mwaka huu wakati Saanane akiwa Dar es Salaam na mwenyekiti huyo akiwa Dodoma.

“Alimwambia mwenyekiti uko wapi, akamwambia nakwenda kwenye maziko ya Samuel Sitta, mawasiliano ya mwisho ni ya tarehe 14 Novemba,” alisema Lissu.

Alisema pamoja na kwamba Saanane alikuwa ni msaidizi wa Mbowe katika masuala ya kisiasa na kijamii, lakini hakuwa akitembea na mwenyekiti huyo na kwamba shughuli zake alikuwa akifanyia katika Makao Makuu ya chama hicho.

Lissu alisema kuwa wapo watu wanahoji inawezekanaje Mwenyekiti hajui mahali alipo msaidizi wake, lakini wanapaswa kufahamu kuwa Mbowe hakuwa akitembea na Saanane.

Alisema baada ya maziko ya Sitta, viongozi wote wa chama hicho walikuwa wakizunguka katika mikoa mbalimbali kwa ajili ya kufanya shughuli za chama, lakini katika kipindi chote hicho, mwenyekiti huyo hakuwa na msaidizi wake huyo, kwa kuwa hatembei naye na si jambo la ajabu.

“Baada ya hizi ziara, tulienda nchi za nje…katika kipindi chote hiki Mwenyekiti hakuwa na Ben na vilevile nataka niweke hii vizuri, Mwenyekiti hakupata wasaa wa kusema Ben yuko wapi, kwa sababu hatembei naye, hayuko naye muda wote.”
 “Sasa kuna watu wanaosema Mwenyekiti ndiye anayejua, atuambie yuko wapi, Mwenyekiti hajui, mimi sifahamu aliko Ben, tungekuwa tunafahamu tungeshasema,” alisema.

Alisema kwa mara ya kwanza alipigiwa simu na mdogo wake Ben, aliyemtaja kwa jina la Dorice Desemba 4, lakini hakumpata na alimtumia ujumbe kumwambia kuwa kaka yao Ben amepotea, hawajui aliko na alikuwa akitaka ushauri ambapo alimjibu waliripoti jambo hilo polisi na kwenye vyombo vya habari.

Alisema si kwamba wamenyamaza kimya, kwa kuwa wanajua alipo msaidizi huyo na kwamba watu wanaodai hivyo si sahihi. 
Alitaka mtu yeyote mwenye taarifa kuhusu Saanane alipo, azitoe taarifa hizo hadharani, polisi, kwenye chama, vyombo vya habari au kwa ndugu zake.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger