Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, SACP Peter Kakamba, amefariki dunia
usiku wa kuamkia leo baada ya kuugua maradhi ya tumbo, Jeshi la Polisi
limethibitisha.
Akizungumza na Mwananchi Digital, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Singida, Mayala Towo amesema Kamanda Kakamba amefia hospitali ya Taifa
Muhimbili, jijini Dar es Salaam.
Mwananchi Digital iliwasiliana na Kaimu Kamanda Towo kupata uthibitisho
wa taarifa zilizosambazwa kupitia mitandao ya kijamii mapema leo kuwa
SACP Kakamba ameaga dunia, baada ya kukosa ushirikiano kutoka kitengo
cha mawasiliano cha Makao Makuu ya Jeshi la Polisi, jijini Dar es
Salaam.
Taarifa iliyokuwa inasambazwa kupitia mtandao wa WhatsApp mapema
asubuhi, ilimnukuu Inspekta wa Jeshi la Polisi (IGP) Ernest Mangu
akisema: “IGP anasikitika kutangaza kifo cha Kamanda wa Polisi Mkoa wa
Singida SACP Peter Kakamba kilichotokea usiku wa saa nne katika
Hospitali ya Muhimbili DSM.
Kamanda Kakamba alikuwa amelazwa hospitalini hapo kwa maradhi ya tumbo alikuwa amefanyiwa operesheni hivi karibuni.”
Kwa mujibu wa Towo, mwili wa marehemu Kakamba utawasili Singida kwa
ajili ya kuagwa kabla ya kusafirishwa kwenda nyumbani kwao mkoani Rukwa
kwa ajili ya maziko.
Ndugu
zangu kama ambavyo tunakumbuka Tarehe 10/09/2016 majira ya saa 9 na
dakika 27 Alasiri maeneo ya Kanda ya ziwa hasa Mkoani Kagera kulitokea
tetemeko la ardhi linalokadiriwa kuwa na ukubwa wa 5.9 katika vipimo vya
Richter ambapo Kitovu cha
Ndege iliyobeba watu 81 wakiwemo wachezaji wa klabu ya soka ya
Chapecoense kutoka Brazil imeanguka wakati ikikaribia kutua katika mji
wa Medellin nchini Colombia, mamlaka zathibitisha.
Taarifa kutoka eneo la tukio zinaarifu kuwa watu 76 wamefariki dunia huku watano wakipona.
Maofisa
wa uwanja wa ndege wa Medellin wamesema wachezaji wa Chapecoense
waliokuwa kwenye ndege hiyo walikuwa safarini kwenda kucheza fainali ya
Copa Sudemericana dhidi ya Atletico Nacional ya Medellin, Colombia.
Kutokana na ajali hiyo, mechi baina ya timu hizo iliyokuwa ichezwe kesho imeahirishwa hadi itakapotangazwa tena.
WANAFUNZI 526,653 sawa na asilimia 94.8 ya waliofaulu mtihani wa darasa
la saba mwaka huu, wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwakani
katika shule za sekondari za serikali katika awamu ya kwanza huku 28,638
wakishindwa kupangiwa shule katika awamu ya kwanza.
Kati ya wanafunzi hao, wasichana ni 268,052 sawa na asilimia 94.5 ya
wasichana waliofaulu na wavulana ni 258,601 sawa na asilimia 95.2 ya
wavulana waliofaulu. Wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani wa darasa
la saba mwaka 2016 walikuwa 795,739, huku 244 wakifutiwa matokeo ya
mtihani kutokana na udanganyifu.
Katika mkutano wake na waandishi wa habari jana mjini hapa, Waziri wa
Nchi, Ofisi ya Rais anayeshughulikia Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa (Tamisemi), George Simbachawene alisema wanafunzi waliochaguliwa
wamegawanyika katika makundi manne likiwemo la shule za bweni kwa wenye
ufaulu mzuri ambao waliochaguliwa ni 900 wavulana 480 na wasichana 420.
Alisema kwa shule za bweni za ufundi waliochaguliwa ni 1,005, shule za
bweni kawaida ni 780, shule za bweni kwa wenye ulemavu ni 723 na shule
za kutwa wanafunzi waliochaguliwa ni 523,245. Alisema jumla ya wanafunzi
3,408 sawa na asilimia 0.6 wamechaguliwa kwenda sekondari za bweni.
Jumla ya watahiniwa 555,291 walifaulu sawa na asilimia 70.36 ya
wanafunzi waliofanya mtihani, kati yao wasichana ni 238,753 sawa na
asilimia 51.1 na wavulana 271,538 sawa na asilimia 48.9.
Ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.52 ukilinganisha na asilimia 67.84 kwa
mwaka 2015. Simbachawene alisema katika uchaguzi huo, wanafunzi 28,638
hawakuchaguliwa katika awamu ya kwanza, na kuitaja mikoa ambayo
wanafunzi wamebaki ni Dar es Salaam (18,820), Arusha (4,752), Songwe
(1,465), Kigoma (1,208), Manyara (1,141), Lindi (608), Mbeya (406) na
Katavi (238).
Aidha, waziri huyo alisema kati ya wanafunzi 1,060,588 walioanza darasa
la kwanza 2010, wanafunzi waliosajiliwa kufanya mtihani wa darasa la
saba mwaka 2016 ni 795,739 sawa na asilimia 75 ya wanafunzi
walioandikishwa wakiwemo wasichana 422,562 sawa na asilimia 53.1 na
wavulana 373,177 sawa na asilimia 46.9 ya waliosajiliwa.
Akizungumzia udanganyifu, alisema watawavua madaraka kwa waliokuwa
waratibu elimu kata na walimu wakuu, kuwashitaki mahakamani na kupeleka
mashauri yao Tume ya Utumishi ya Walimu, baada ya udanganyifu kuongezeka
ambako watahiniwa 244 wamefutiwa matokeo mwaka 2016 ikilinganishwa na
wanane wa mwaka jana.
Alizitaja shule zilizohusika kwenye udanganyifu huo ni Shule ya Tumaini
na Little Flower za Sengerema mkoani Mwanza, Mikahamakumi iliyopo
Sikonge, Tabora ambazo ni za binafsi, wakati za serikali ni Kondi
Kasandalala iliyopo Sikonge, Tabora, Qash iliyopo Babati na St Getrude
iliyopo Madaba mkoani Ruvuma.
Aidha, alisema 10 bora za serikali ni Kazunzu iliyopo Halmashauri ya
Buchosa (Mwanza), Mwanahegele ya Maswa (Simiyu), Huruma ya Mbinga
(Ruvuma), Kabanga ya Ngara (Kagera), Butumba B (Jiji Mwanza), Masoko ya
Kilwa (Lindi), Lyambamgongo ya Bukombe (Geita), Kilimani ya Geita
Vijijini, Magufuli ya Chato na Nkome ya Geita Vijijini, Geita.
Alisema shule 10 zilizofanya vibaya ni Chohelo ya Mvomero (Morogoro),
ambayo ni ya mwisho kitaifa ikifuatiwa na shule za Iloliento, Longido
(Arusha), Mwalebi na Nchilila Meatu (Simiyu), Magingi ya Mvomero, Kilole
ya Lushoto, Tanga, Zege ya Korogwe, Tanga na shule tatu za Lubchi,
Kitengo na Mgata za Morogoro vijijini.
Kama utahitaji kuangaliziwa jina lako/AU la ndugu yako kwa "usahihi" na "kasi ya ajabu" (ambapo utajibiwa ndani ya mda mfupi) kama umechaguliwa kujiunga na jkt na kambi uliyopangwa. tafadhali fanya yafuatayo;