SERIKALI imepanga kununua ndege za kisasa ili kuimarisha ulinzi katika Hifadhi za Taifa nchini.
Hayo
yamesemwa jana na Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Meja
Jenerali Gaudence Milanzi wakati akihojiwa na kipindi maalumu cha
TUNATEKELEZA kinachorushwa hewani na kituo cha Televisheni ya Taifa
(TBC1).
Meja
Jenerali Milanzi anasema Serikali imeweka mfumo maalumkatika kulinda
hifadhi zilizopo na ili kuweza kukabiliana na ujangili unaojitokeza
katika hifadhi mbalimbali nchini.
“Sekta
ya Utalii nchini inachangia pato la taifa kwa takribani asilimia 17.5
na kutoa ajira kwa zaidi ya watumishi milioni 3 katika sekta mbali mbali
ya utalii nchini, hivyo ni vyema tukaweka mikakati madhubuti katika
kulinda vyanzo vilivyopo” alisema Meja Milanzi.
Aidha,
alisema kuwa Serikali itaendelea kuwachukulia hatua kali za kisheria
watu wote watakaobainika kujihusisha na ujangili pamoja na biashara ya
magogo ili kulinda hifadhi za Taifa na kuweza kuvutia watalii nchini.
Aidha
Meja Jenerali Milanzi aliitaka jamii kwa ujumla kuona umuhimu wa
kutumia nishati mbadala ili kulinda misitu iliyopo kwa kutunza mazingira
na hifadhi za taifa.
Mbali
na hayo Meja Jenerali Milanzi alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi
zinazovutia watalii wengi kutoka Marekani na Uingereza hivyo kuwataka
wananchi kuzingatia sheria na kanuni zinazosimamimia Hifadhi za Taifa
ili kuzudi kuvutia watalii nchini.
KAMANDA wa
Polisi wa kikosi cha usalama Barabarani Mohammed Mpinga ametoa wito kwa
madereva wote ikiwemo madereva wa Serikali na Mashirika ya Umma
kuzingatia sheria za Usalama Barabarani.
Kamanda
Mpinga ameyasema hayo leo jijini Dar es salaam wakati alipokuwa
akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa kampeni ya kitaifa
ya “Abiria paza sauti” inayotarajiwa kuzinduliwa tarehe 28 Novemba,
mwaka huu.
Kamanda
Mpinga alisema kumekuwa tabia ya baadhi ya madereva hususani wa
Serikali na mashirika ya umma ya kutofuata sheria za usalama barabarani
kwa kuendesha magari kwa mwendokasi, na kuwaonya kuwa sheria ni msumeno
na inapaswa kufuatwa na kila mtu.
“Kumekuwa
na madereva hasa wa magari madogo kusafiri kwenda maeneo mbalimbali ya
nchi huku wakiwa hawana uzoefu wa kuendesha umbali mrefu na hivyo
kupelekea uvunjifu wa sheria za barabarani kwa kuendesha kwa mwendokasi
na kusababisha ajali” alifafanua Kamanda Mpinga.
Akifafanua
zaidi Kamanda alisema uzoefu unaonyesha kuwa katika kipindi hiki cha
kuelekea mwisho wa mwaka kumekuwa na ongezeko kubwa la magari
barabarani, na hivyo kuwataka wananchi kuzingatia sheria za barabarani
ili kuweza kupunguza ajali za barabarani.
Kwa
upande wake Kaimu Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Mabalozi wa Usalama
Barabarani, Jackson Kalikumtima alisema lengo la kampeni ya Paza Sauti
ni kuhamasisha ushiriki kamilifu wa wananchi katika kukabiliana na ajali
kwa kuchukua hatua stahiki bila ya uwepo wa askari.
Pia
alisema kuwa kampeni hiyo imelenga kubadili tabia na mtazamo wa
madereva kuhusu usalama barabarani ili waendeshe kwa kuzingatia sheria
bila shuruti na kubadili mtazamo wa wananchi kuhusu usalama barabarani
ili watambue kuwa usalama barabarani ni jukumu la kila mmoja.
Naye Mwanasheria
wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, (ASP), Deus Sokoni alisema
mkakati wa kupunguza ajali barabarani katika kampeni hiyo umelenga
katika kutoa elimu kwa jamii ili kuona suala la usalama barabarani ni
jukumu la kila mmoja na si jukumu la Polisi pekee.
“hakuna
asiyetumia barabara duniani, hatutaki ajali tunataka kuishi salama,
hivyo kila abiria anawajibu wa kutunza na kutii sheria za barabarani “
aliongeza Mwanasheria huyo.
Mwenyekiti wa Chama
cha Kutetea Abiria Taifa (CHAKUA), Hassan Mhanjama aliwataka abiria
wote nchini hususani wanaotajaria kusafiri mwishoni mwa mwaka
kuwasiliana na Mamlaka ya Usafirishaji SUMATRA pindi watakapopandishiwa
nauli mbali na taratibu zilizopo
Mbeya. Muuguzi wa Hospitali ya Mkoa wa Mbeya anayedaiwa kumkamshifu
Junes Elias, mkazi wa Mbozi mkoani Songwe na Rais John Magufuli
ametambuliwa.
Mganga mkuu wa hospitali hiyo, Dk Gloria Mbwille alisema muuguzi huyo
ametambuliwa na kwamba tume imeundwa kuchunguza tuhuma zinazomkabili.
Hata hivyo, alikataa kuzungumzia zaidi kuhusu muuguzi huyo wala kumtaja
jina akisema taarifa zaidi zitatolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Amos
Makalla baada ya tume kukamilisha uchunguzi huo. Juzi mchana, Junes
alimueleza Makalla kwamba alifika hospitalini hapo Novemba 22 asubuhi
akitokea wilayani Mbozi.
Alisema baada alifuata taratibu za kufungua kadi kwa gharama ya Sh5,000
kwa ajili ya kutaka matibabu ya mtoto wake, Joyce Asifiwe (9), lakini
alikashfiwa kwenye dirisha la dawa akiambiwa ataisoma namba kwa
kumchagua Rais Magufuli.
Alisema baada ya kumuona daktari aliandikiwa dawa za kwenda kuchukua kwenye dirisha ambako ndiko alikotolewa maneno ya kashfa.
“Kwenye dirisha hilo nilimkuta muuguzi mmoja ambaye aliniambia kwamba
dawa zote zinauzwa. Hapa hakuna dawa za bure, si mlimchagua Magufuli,
sasa mtaisoma namba,’’ alisema akidai kumnukuu aliyemtaja kuwa ni
muuguzi.
Baada ya kumsikiliza malalamiko hayo, Makalla aliagiza mganga mkuu
aitwe, lakini ilielezwa alikuwa safarini, hivyo kaimu wake, Dk Ismail
Macha alifika.
Makalla alimueleza Dk Macha kwa kifupi yaliyojiri kutoka kwa mlalamikaji
huyo na kumtaka waongozane hadi hospitalini na kuwaita wauguzi
waliokuwa zamu Novemba 22 dirisha la dawa ili amtambue mhusika na
achukuliwe hatua jambo ambalo limefanyika.
CUBA: Rais wa zamani wa Cuba, na kiongozi wa Chama cha Kikomunisti cha
nchini humo, Fidel Alejandro Castro Ruz amefariki dunia leo akiwa na
umri wa miaka 90.
Mufti
Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakari Zuber jana amekabidhiwa ripoti ya
awali iliyoandaliwa na tume ambayo ameiunda kwa ajili ya kufanya
uchunguzi na kuzibainisha mali zote za Baraza kuu la Waislamu
Tanzania (BAKWATA).
Akizungumza
wakati wa kumkabidhi ripoti hiyo, Mwenyekiti wa tume hiyo Sheikh
Abubakari Khalid Hajj alisema kuwa ripoti hiyo imefanyika kwa muda wa
miezi mitatu licha ya kukumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ufinyu
wa muda.
Aidha
aliwambia wanahabari kuwa uchunguzi huo umehusisha ufuatiliaji wa mali
za Bakwata katika Mkoa wa Dar es salaam pekee,ikiwemo majengo,viwanja,
pamoja na kupitia mikataba mbalimbali ili kujiridhisha kama imefuata
taratibu za kisheria.
Akizungumza
mbele ya wanahabari mara baadi ya kupokea ripoti hiyo Mufti Mkuu wa
Tanzania Sheikh Abubakari Zuber alisema kuwa ataipitia ripoti hiyo ili
kujua yale yaliyobainishwa na tume yake, na kuahidi kuyafanyia kazi
mapema iwezekanavyo.
Hata
hivyo Mufti huyo ameiongezea muda wa miezi mitatu tume hiyo ambayo ina
jumla ya wajumbe wanane kwa ajili ya kukamilisha kuandaa ripoti ya mkoa
wa Dar es salaam kabla ya kuhamia mikoa mingine kwani zoezi hilo
litafanyika nchi nzima.
Wataalamu
mbalimbali wa sekta ya afya, sasa wataanza kusajiliwa na kupewa leseni
zitakazowatambulisha na zitakuwa na masharti maalumu.
Hayo
yamesema na Mganga Mkuu wa Serikali, Profesa Muhammad Kambi jana
Jumatano jijini Dar es salaam, wakati akifungua mkutano wa mwaka wa
Chama cha Wafiziotherapia (APTA).
Alisema
serikali imeanza mchakato wa kuipitia upya Sheria ya Madaktari wa
Tanganyika, ambayo itaongezwa sharti hilo pamoja na kuundwa kwa bodi
maalumu itakayosimamia maadili ya watumishi hao.
“Lakini
hivi sasa kuna taaluma nyingi ndani ya hii fani, kwa mfano ninyi
wataalamu wa fiziotherapia. Mpo lakini sheria haiwatambui, kwa maana
hiyo inakuwa vigumu hata kuwafuatilia. Ndiyo msingi wa kuipitia upya
sheria hii,” alisema.
“Katika
sheria mpya itakayoboreshwa, kila mtumishi atatakiwa kukata leseni.
Kila mtumishi atatakiwa kujiendeleza kielimu, kuongeza ujuzi ili aendane
na wakati uliopo kwa sababu mambo yanabadilika, kile ulichosoma jana
unahitaji kujifunza zaidi,” alisema.
Aidha
Kambi alisema tayari maboresho ya sheria hiyo yameshawasilishwa katika
Kamati ya Baraza la Mawaziri ya Katiba na Sheria na imeshapitiwa.