Sunday 25 February 2024

AJALI YA MAGARI MANNE YAUA WATU 15 ARUSHA

...

Watu kumi na tano wamefariki dunia katika ajali iliyohusisha lori na magari mengine madogo matatu katika eneo la by Pass Ngaramtoni wilaya Arumeru Mkoa wa Arusha.


Akitoa taarifa hiyo katika eneo la ajali Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha kamshna msaidizi mwandamizi wa Polisi SACP Justine Masejo amesema ajali hiyo imetokea Februari 24,2024 muda wa saa 11 jioni ambapo illmehusisha lori na magari madogo matatu katika eneo la Ngaramtoni Wilaya ya Arumeru Mkoa wa Arusha.

Kamanda Masejo amesema wanaendelea na uchunguzi wakina ajali hiyo ili kubaini chanzo halisi cha ajali hiyo.


Aidha amewaomba wananchi kufika katika hosptali ya rufaa ya mount Meru kutambua miili ya waliofariki katika ajali hiyo.

Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger