Friday 14 July 2023

WIZARA YA MALIASILI NA UTALII YAIBUKA KIDEDEA MAONESHO YA 47 YA SABASABA

...
Wizara ya Maliasili na Utalii imeibuka Kidedea kwenye Maonesho ya 47 ya Kimataifa ya Biashara (Saba Saba) Jijini Dar es Salaam na kukabidhiwa tuzo na  Rais wa zanzibar na Mwenyekiti wa Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ally  Mwinyi ambaye alikuwa Mgeni rasmi katika ufungaji wa Maonesho hayo. 


Akielezea Tuzo hiyo ya Banda bora na mashuhuri upande wa Wizara na Taasisi, Mwenyekiti wa Maonesho ya Saba Saba Wizara ya Maliasili na Utalii, Bw. Filex John, amesema ni Matokeo chanya ya Uongozi mzuri wa Wizara hiyo pamoja na kazi nzuri iliyofanywa na Watumishi wa Wizara hiyo ya utoaji huduma kwa Kiwango cha juu kwa wote waliofika kwenye Banda hilo. 

Bw. John amewashukuru wadau  na wananchi  wote waliojitokeza kupata huduma kwenye Banda hilo la Maliasili, pamoja na ushirikiano waliotoa katika kuhakikisha Maonesho hayo yanakuwa na Mafanikio Makubwa.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger