Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli anasikitika kutangaza kifo cha Katibu Mkuu Kiongozi Mhe. Balozi John William Kijazi kilichotokea leo Februari 17,2021 saa 3:10 usiku akiwa katika Hospitali ya Benjamini Mkapa Jijini Dodoma alikokuwa anapatiwa matibabu.
Rais Magufuli amesema taratibu za mazishi ya marehemu Balozi Kijazi zitatangazwa baadae.
0 comments:
Post a Comment