Friday 1 November 2019

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro asimamia Zoezi la wanafunzi Watoro kuchapwa viboko mbele ya wazazi wao

...
Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Julius Mtatiro jana Alhamisi  alisimamia zoezi la  kucharazwa viboko wanafunzi 3 ambao ni watoro sugu katika Shule ya Msingi Ligoma iliyoko wilayani humo ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kupambana na utoro sugu, nidhamu za wanafunzi na mimba za utotoni Tunduru.

Mkuu huyo wa wilaya  alimtaka mwalimu Mkuu wa shule hiyo kuwachapa viboko vinne wanafunzi hao na kuagiza  wapewe adhabu nyingine zisizohusiana na viboko, ikiwa ni pamoja na kuchimba visiki.

Baada ya viboko hivyo, aliwauliza wanafunzi hao lini wataanza kwenda shule na mmoja alijibu kuwa ataripoti Jumatatu,hata hivyo, mkuu huyo wa Wilaya alisema wote wanapaswa kuripoti leo.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger