maderw

Baadhi ya madereva wa mabasi katika stendi kuu ya Mabasi
yaendayo Mkoani na nchi jirani Ubungo,wakishangilia wakiwa na mabango yao yenye  jumbe : “Mabomu tumeyazoea! Tanzania bila madereva haiwezekani! muda huu wakiwa wamejikusanya wakimsubiria Waziri Mkuu Mizengo Pinda afike kuongea nao kufikia suluhu
Mgomo wa madereva umeibuka tena leo Mei 4 baada ya mabasi na magari ya mizigo kugoma tena kwa mara ya pili kwa lengo la kushinikiza kutatuliwa madai yao ambayo awali baadhi ya viongozi wakuu wa Serikali walijaribu kutatua mgogoro wao ambapo hata hivyo  hawakufikia suluhu.
Kwa hali ya leo Mei 4, Madereva hao wanashinikiza kuonana na  Waziri Mkuu Mizengo Pinda ndipo wafikie muafaka wao.  Hata hivyo, Modewji blog imeweza kushuhudia misululi ya wananchai wakitembea kwa miguu kuelekea makazini na sehemu mbalimbali za miangaiko yao ambapo wengi wa wananchi hao baadhi yao walikuwa wakipanda usafiri wa bajaji, Pikipiki na hata baiskeli ilimradi kufika waendapo.
Maeneo mengi ya vituo vya mabasi kumekuwa na misululu mengi ya abiria ambao wamekosa tumaini licha ya wengine kupanda Pikipiki na wengine kutembea kwa miguu.

Ubungo: Madereva waamuliwa kurudisha nauli za abiria

Katika kile kinachoelezwa kuondoa usumbufu, jeshi la Polisi limeamua kuwatangazia wenye mabasi kuakikisha wanarudisha nauli za abiria waliokwisha wakatisha tiketi.  Modewji blog imeshuhudia tangazo hilo lililokuwa likitolewa na jeshi la Polisi waliokuwa ndani ya gari laa POLISI. Hata hivyo licha ya tangazo hilo abiria na wenye mabasi hawajachukua hatua yoyote ya kufanya hivyo zaidi ya kuangaliana!.
11193285_836675069702699_3932901606451902215_n (2)
Moja ya basi lililokuwa limeegeshwa karibu na mlango wa kutokea baada ya awali kutaka kuondoka na kuishia mlaangoni..!
10995390_836674983036041_6712997597855015801_n
 Hali ilivyo muda huu nje ya Mabasi Ubungo!

BONYEZA HAPO CHINI KUANGALIA PICHA ZAIDI