Monday 29 November 2021

Grant Officers -12 Job Opportunities at Deloitte

Grant Officers 12 positions   Grants Officer (Ref: C3HP/GO/12-21) Background Deloitte Tanzania has been awarded a contract to implement a Comprehensive Client-Centered Health Program HIV/TB LOC (C3HP) in Southern regions in Tanzania. This is a five year project (November 9, 2021 to September 30, 2026) funded by the American People through USAID aiming at supporting the […]

This post Grant Officers -12 Job Opportunities at Deloitte has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 29, 2021

 











Share:

Sunday 28 November 2021

GULAM HAFEEZ MUKADAM ATAJA MIRADI INAYOTEKELEZWA KATA YA MJINI SHINYANGA...AKEMEA WANAOMBEZA RAIS SAMIA


Diwani wa Kata ya Mjini Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Gulam Hafeez Mukadam akizungumza kwenye mkutano wa hadhara leo.
Diwani wa Kata ya Mjini Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Gulam Hafeez Mukadam akizungumza kwenye mkutano wa hadhara leo
Diwani wa Kata ya Mjini Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Gulam Hafeez Mukadam akizungumza kwenye mkutano wa hadhara leo
Diwani wa Kata ya Mjini Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Gulam Hafeez Mukadam akiwa kwenye mkutano wa hadhara leo

***
Na Mwandishi wetu - Malunde 1 blog
Diwani wa Kata ya Mjini Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mhe. Gulam Hafeez Mukadam amepongeza jitihada zinazoendelea kufanywa na Rais  wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha za kutekeleza miradi ya maendeleo katika kata hiyo.


Mukadam amebainisha hayo leo Jumapili Novemba 28,2021 wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye mtaa wa Buzuka aliouitisha kwa ajili ya kuwashukuru wananchi wa kata hiyo kwa kumchagua kwa kura nyingi uchaguzi uliopita huku akitoa taarifa za miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika mitaa mbalimbali ya kata hiyo.

Amesema wakati wa siasa umekwisha  hivyo nivyema wananchi wakajikita kufanya kazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo huku akiwaomba wakazi wa kata hiyo kuendelea kumuombea na kumpongeza Rais Samia kwa kazi anazofanya badala ya kubeza kazi zake ,waondoe wasiwasi na waendelee kumuamini kwa kazi zake.


“Siku ya uchaguzi mkuu Oktoba 28 mwaka jana, mlinipigia kura nyingi za ushindi, na kunifanya niwe diwani wenu kwa awamu nyingine tena, ambapo naahidi kuendelea kuwapigania kwa kueleza changamoto zinazoikabili kata ya Mjini na nyinyi mnaona namna barabara zinavy jengwa kwa kiwango cha lami ,ujenzi wa mitaro ,ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa shule za msingi na sekondari hivyo ni vyema muendelee kuniamini na kumuunga mkono Rais Samia ili aendelee kutoa fedha za kutekeleza miradi mbalimbali katika kata yetu, amesema Mukadam.

“Mnachopaswa kufanya kwa sasa ni kumpongeza Rais Samia pamoja  na kukemea vikali baadhi ya watu wanaobeza kazi zake ili aendeleze yale mazuri anayo endelea kuyafanya kwa maslahi ya taifa na hasa akina mama msimuangushe Rais Samia ”,ameongeza.

Pia amesema ataendelea kuwaletea maendeleo wananchi kama alivyofanya kwenye awamu iliyopita, na kuibadilisha Shinyanga kuwa Jiji, ambapo Kata hiyo ya Mjini ndiyo kitovu cha mkoa wa Shinyanga.

Hata hivyo amewasisitiza wananchi kujitokeza kupata chanjo ya Uviko 19  kwani ni salama na kuepukana na uvumi wa watu akieleza kuwa hata  yeye tangu amechanja yuko vizuri na anaendelea kuchapa kazi.
Share:

WANUFAIKA TASAF WATAKIWA KUWA NA MTAZAMO WA KUJIKWAMUA KIUCHUMI


Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Uswisi Bi.Patricia Danzi ,akizungumza na wanufaika wa mpango wa kusaidia kaya masikini (TASAF) katika kijiji cha Wilunze wilaya ya Chamwino wakati wa ziara ya kujionea Maendeleo ya mpango huo kwa wananchi wa kijiji hicho. 


Balozi wa Uswisi Nchini Tanzani Bw.Didier Chassot,akiwaeleza wanufaika wa mpango wa kusaidia kaya masikini (TASAF) katika kijiji cha Wilunze wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma jinsi Serikali ya Uswisi inavyoendelea kuisaidia Tanzania katika sekta mbalimbali wakati wa ziara ya kujionea Maendeleo ya mpango huo kwa wananchi wa kijiji hicho. 


Mkurugenzi wa wilaya ya Chamwino Dk Semistatus Mashimba,akitoa taarifa ya wanufaika katika miradi ya TASAF katika Halmashauri yake namna wakazi walivyonufaika katika kijiji cha wilunze. 


Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF, Ladislaus Mwamanga,akizungumza na wanufaika wa mpango huo huku akiwataka wananchi kuendelea na kuwekeza katika miradi yao ya kimaendeleo kupitia Miradi ya TASAF mara baada ya kutembelea wanufaika katika kijiji cha Wilunze wilaya ya Chamwino kujionea Maendeleo ya mpango huo. 


Mwenyekiti wa kijiji cha Wilunze Bw.Amos George Chindole,akitoa neno la shukrani kwa Viongozi na wadau wa TASAF kwa kuweza kutembelea na kujionea maendeleo ya Mpango huo katika kijiji cha Wilunze wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma. 


Wakazi wa Kijiji cha Wilunze wakiwa katika mkutano wa hadhara wakati wa viongozi na wadau wa Mfuko wa Mendeleo ya Jamii TASAF wakizungumza mara baada ya kutembelea na kujionea maendeleo ya Mpango huo katika kijiji hicho. 


Muonekano wa ujenzi wa barabara za ndani ya kijiji zilizoanza kujengwa na wanaufaika kwa kutumia zana za mikono 


Viongozi wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii TASAF Pamoja na wadau wakikagua mradi wa Barabara uliojengwa na Wanufaika wa TASAF ,inayounganisha Kijiji cha jirani . 


Mnufaika wa Mfuko wa Mendeleo ya Jamii TASAF, Mkazi wa kijiji cha Milunze wilayani Chamwino Mkoani Dodoma Bi.Moreni Erenesti,akielezea jinsi alivyoweza kunufaika na mfuko huo. 


Mnufaika wa Mfuko wa Mendeleo ya Jamii TASAF,Luzy Agustino,akizungumzia jinsi alivyonufaika na mfuko huo kwa kuwa na makazi yake na malengo yake ya baadae nikujenga nyumba kubwa na Kuendela kusomesha waototo wake ambaye pia anajishughulisha na ujasiliamali (wa kwanza kushoto) ni Balozi wa Uswisi Nchini Tanzani Bw.Didier Chassot (wa pili kutoka kushoto) ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Uswisi, Patricia Danzi. 


Picha ya Pamoja ya wadau na viongozi wa Mfuko wa maendeleo ya Jamii TASAF baada ya kutembea na kujionea miradi mbalimbali inayotekelezwa na TASAF katika kijiji cha Wilunze wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma. 

........................................................ 

Na.Alex Sonna,Chamwino 

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Uswisi, Patricia Danzi amewataka wanufaika wa Mpango wa kusaidia kaya masikini (TASAF) kuwa na mtazamo wa kujikwamua na umaskini. 

Danzi ametoa kauli hiyo wakati walipowatembelea wanufaika wa Mfumo wa Maendeleo ya Jamii TASAF katika kijiji cha Wilunze wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma. 

Mkurugenzi huyo amesema kupitia ubalozi wao nchini Tanzania utaendelea kusaidia kuwezesha mambo ambayo yatakuwa kichocheo cha kimaendeleo . 

''Serikali ya Uswisi itaendelea kuimraisha ushirikiano na uhusiano wa muda mrefu wa zaidi ya miaka 40 na Tanzani katika nyanja mbalimbali za kimaendeleo ikiwemo Sekta ya Afya,Elimu pamoja na kusaidia juhudi za Serikali katika mapambano ya kuondokana na umaskini na kuinua kipato cha wananchi''amesema Danzi 

Pia ameeleza kuwa Uswisi itaendelea na jitihada zake za kutoa misaada mbalimbali kwa Tanzania ili kunusuru Kaya Maskini. 

Danzi amesema kuwa amefurahi kuwasikia wanufaika wakisema kwa uwazi sana, mara nyingi ni vigumu kuongea kuhusu maisha yao, lakini mkiwa na jitihada katika kufanya Kazi mtajitoa kwenye hali ya umaskini. 

“Naomba mfanye kazi kwa bidii na maarifa hasa wenye nguzu za kufanya kazi na mjitahidi kujiwekea akiba kwa kidogo mnachopata,”amesema Danzi. 

Kwa upande wake Balozi wa Uswisi Nchini Tanzani Bw.Didier Chassot,amesema kuwa Uswisi na Tanzania wamekuwa na mahusiano mazuri na sasa wanasherekea miaka 40 ya ushirikiano . 
''Nawaomba walengwa mtumie vizuri fedha mnazopata ili ziweze kuwasaidia nyie pamoja na familia zenu hivyo Kupitia TASAF tutaendelea kushirikiana na Tanzania''amesema Chassot 

Awali ,Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Maendeleo ya Jamii-TASAF, Ladislaus Mwamanga,amesema katika awamu ya kwanza ya mpango wa kunusuru Kaya maskini zaidi ya laki mbili zimefanikiwa kubadilisha hali ya maisha yao hivyo kuondokana na Umaskini. 

Hata hivyo Mwamanga ameipngeza wilaya ya Chamwino kwa kutekeleza vyema mpango huo ikiwamo utoaji wa ajira za muda mfupi ambapo yamechangia mabadiliko makubwa kwa wanufaika. 

“Kutokana na matokeo mazuri mliyoonesha ndio maana mmepata ugeni huu kutoka Uswisi, niwaambie wametoa Uswisi ni wadau wa maendeleo ambao wametoa msaada mkubwa na wametupatia Sh.Bilioni 41,”amesema. 

Amesema Rais Samia Suluhu Hassan ana shauku ya kuona wananchi wanaondokana na umaskini. 

Naye, Mkurugenzi wa Wilaya ya Chamwino, Dk.Semistatus Mashimba amesema kijiji cha Wilunze ni mojawapo ya wanufaika katika miradi ya Tasaf ambacho kinawalengwa 193 na tayari Sh.Milioni 45.1 zimetolewa kwa walengwa kwa mujibu wa mwongozo. 

Mmoja wa wanufaika hao, Ruth Kalulu amesema mpango huo umewasaidia kwa kiasi kikubwa kujikwamua kiuchumi kwa kuanzisha ufugaji kwa kuwa mumewe alimkimbia na kumuacha na watoto wanne. 

Amesema kwasasa amefanikiwa kujenga nyumba ndogo ya kuishi na familia yake huku ufugaji ukimuingizia kipato kinachosaidia kulipa ada na michango ya watoto shuleni.
Share:

SIMBA SC YAICHAPA RED ARROWS FC MABAO 3-0 KOMBE LA SHIRIKISHO

 


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Simba Sc imefanikiwa kuwachapa Red Arrows Fc ya nchini Zambia kwa mabao 3- katika mchezo ambao ulichezwa kwenye uwanjja wa Benjamini Mkapa Jijini Dar es Salaam.

Licha ya uwanja kujaa maji Simba Sc ilicheza kandanda safi na kufanikiwa kuondoka mapumziko wakiwwa na faida ya mabao mawili yaliyofungwa na Benard Morrison pamoja na Meddie Kagere.

Kipindi cha pili kilianza Simba Sc ikionekana bado inahitaji magoli zaidi licha jya kuwa mbele kwa mabao mawili ambapo dakika 79 ilifanikiwa kupata bao  la tatu kupitia tena kwa nyota wao Benard Morrison .

Simba inahitaji ushindi wowote ama sare katika mchezo ujao ili waweze kufuzu hatua ya makundi kombe la Shirikisho ambapo Red Arrows watakuwaa nyumbani kwenye mchezo huo.



Share:

WAZIRI PROF. MKENDA : SEKTA YA KILIMO INACHANGIA 26% YA PATO LA TAIFA NA KUTOA AJIRA KWA 58%

 Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda

Na Dotto Kwilasa-Malunde 1 Blog, DODOMA.


SEKTA ya kilimo imeajiri asilimia 58 ya Watanzania ikilinganishwa na asilimia 90 wakati wa uhuru, hali inayoashiria kukuza uchumia na kuongeza pato la Taifa.


Hayo yameelezwa leo Jijini Dodoma na  Waziri wa Kilimo Prof. Adolf Mkenda wakati akiwasilisha taarifa ya mafanikio ya wizara yake kwa kipindi cha miaka 60 ya Uhuru.


Amesema mchango wa sekta ya kilimo kwenye pato la Taifa umekua kutokana na  hatua mbalimbali za kuimarisha sekta ya kilimo hapa nchini na kusaidia kuongeza  pato la Taifa kwa  asilimia 26.


Licha ya hayo ameeleza kuwa Serikali imechukua hatua katika kuimarisha uzalishaji wa alizeti na chikichi hapa nchini ili kukabiliana na changamoto ya upatikanaji wa mafuta nchini kwa kupunguza uagizaji toka nje.


"Katika kipindi cha miaka 60, Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kuimarisha sekta ya kilimo hapa nchini,matokeo ya hatua hizo ni Taifa kujitosheleza kwa chakula na kuzalisha ziada inayouzwa nje ya nchi,"amesema. 


Akizungumzia mikakati ya Serikali kwa sasa Katika kuongeza tija kwenye kilimo,Prof.Mkenda ameeleza kuwa imejikita katika kuimarisha tafiti, huduma za ugani, kuongeza upatikanaji wa mbegu bora, kuimarisha kilimo cha umwagiliaji na masoko. 


Ameeleza kuwa Serikali imeweka mikakati ya kuhakikisha upatikanaji wa mbolea hapa nchini unakuwa wa uhakika kwa kuvutia wawekezaji kuja kujenga Viwanda ikiwemo kile kinachojengwa hapa Dodoma kitakachozalisha tani laki sita kwa mwaka.


"Kupitia mikakati hii tani milioni 18 za mazao zitazalishwa na ziada ni tani milioni 3,ni hatua nzuri kwani wakati wa kupata uhuru tulikuwa tunazalisha tani 1 ya mpunga kwenye ekari 1 na sasa tani 2.3 hadi 4 kutokana na maboresho kwenye sekta ya kilimo,"amesema Waziri huyo.


Sambamba na hayo amezungumzia utoshelevu wa chakula nchini kuwa kwa sasa ni asilimia 126  ikilinganishwa na wakati tunapata uhuru ambapo Tanzania ilikuwa inaomba msaada wa chakula kutoka mataifa tajiri.


"Mwanzoni kabisa tulikuwà tunaomba chakula mataifa tajiri kama Marekani lakini Sasa hilo halipo tunajitegemea wenyewe na sisi kama Serikali tunaweka msukumo zaidi katika kuimarisha ushirika hapa nchini ili kuwasaidia wakulima kupata manufaa zaidi kiuchumi,"amesema. 


Kadhalika Waziri Mkenda amesema huduma za ugani zimeimarishwa zaidi katika kipindi hiki na tayari Serikali inaendelea kuwapatia vitendea kazi ikiwemo pikipiki 2000 ambazo zitatolewa Januari, 2022 na kwamba  86 tayari zimeshatolewa.

Share:

ANGOLA WAENDELEZA UBABE KWA ZANZIBAR, CANAF 2021


Wachezaji wa Angola (jezi nyekundu) wakikabiliana na wachezaji wa Zanzibar (jezi ya kijani mpauko) kwenye mchezo wa CANAF 2021 uliochezwa leo, Novemba 28,2021 jijini Dar es Salaam ambapo Angola imeshinda 12-0.


Timu za Uganda (jezi nyekundu) na Timu ya Siera Leon (jezi nyeupe) wakiimba nyimbo zao za Taifa wakati wa mechi ya mashindano ya CANAF 2021 leo Novemba 28, 2021

*************************

Na. John Mapepele



Mabingwa watetezi wa Mashindano ya Afrika kwa mchezo wa Mpira wa Miguu kwa wenye Ulemavu CANAF 2021 timu ya Angola leo, Novemba 28, 2021 wameonyesha kwamba wao ni mabingwa wa dunia katika mchezo huu baada ya kuichabanga Zanzibar dazani moja kwa nunge kwenye Uwanja wa Uhuru mjini Dar es Salaam.



Katika kipindi chote Angola waliutawala mchezo huo kutokana na uzoefu mkubwa wa wachezaji wao wanaocheza katika mashindano ya kimataifa.



Kipindi cha kwanza tayali Angola ilikuwa inaongoza kwa magoli sita kwa nunge na katika kipindi cha pili wakaongeza magoli mengine sita na kufanikiwa kupata ushindi wa dazani moja kwa sifuri dhidi ya timu ya Zanzibar.



Magoli ya Angola yamefungwa na Kufula Hilario, Aharo Francisco, Joachim Sabino, Chiarere Jord na Pacincia Fblio.





Wakati huo huo katika mchezo mwingine, Timu ya Siera Leon imeibamiza mabao 3- 0 ambapo bao la kwanza limefungwa katika dakika ya 15 na mshambuliaji Kuroma Ctbassy na goli la pili limefungwa dakika ya 18 ya kipindi cha kwanza na goli la tatu dakika ya 43 kipindi cha pili na Lumeh Foday.



Mchezo huo ulitawaliwa na mvua kubwa hali iliyosababisha kushindwa kuendelea na kwa muda baada ya kipindi cha kwanza cha mchezo kumalizika kutokana na maji kujaa katika uwanja.



Mashindano haya yamezinduliwa rasmi jana Novemba 27 na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa na yatakamilika Disemba 4, 2021.

Share:

MARY MASANJA AKUTANA NA BODI YA MAENDELEO YA RWANDA


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amekutana na watendaji wa Bodi ya Maendeleo ya Rwanda kwa lengo la kujifunza uwekezaji kwenye Utalii wa Mikutano katika kikao kilichofanyika Kigali- Rwanda.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akizungumza na watendaji wa Bodi ya Maendeleo ya Rwanda alipowatembelea kwa lengo la kujifunza uwekezaji kwenye Utalii wa Mikutano katika kikao kilichofanyika Kigali Rwanda.


Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Utalii kutoka Wizara ya Maliasili na Utalii, Philip Chitaunga (kulia) akizungumza katika kikao kati ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) na watendaji wa Bodi ya Maendeleo ya Rwanda kuhusu uwekezaji kwenye utalii wa mikutano kilichofanyika katika ofisi za bodi hiyo Kigali nchini Rwanda.


Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) akipokea zawadi kutoka kwa Naibu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Maendeleo ya Rwanda, Ariella Kageruka mara baada ya kikao cha kujadili uwekezaji kwenye Utalii wa Mikutano kilichofanyika katika ofisi za Bodi ya Maendeleo ya Rwanda Kigali nchini Rwanda.


Kaimu Mkurugenzi, Idara ya Utalii,Wizara ya Maliasili na Utalii, Philip Chitaunga akipokea zawadi kutoka kwa Mkuu wa Idara ya Udhibiti wa Utalii, Bodi ya Maendeleo ya Rwanda, Emmanuel Nsabimana mara baada ya kikao cha kujifunza uwekezaji kwenye Utalii wa Mikutano kilichofanyika katika ofisi za Bodi ya Maendeleo ya Rwanda Kigali nchini Rwanda.


Ujumbe wa Tanzania ukiongozwa na Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) (katikati) katika picha ya pamoja na watendaji wa Bodi ya Maendeleo ya Rwanda mara baada ya kikao cha kujifunza uwekezaji kwenye Utalii wa Mikutano kilichofanyika katika ofisi za Bodi ya Maendeleo ya Rwanda Kigali nchini Rwanda.

****************************

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) leo amekutana na watendaji wa Bodi ya Maendeleo ya Rwanda kwa lengo la kujifunza kuhusu uwekezaji katika Utalii wa Mikutano.

Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Bodi ya Mikutano ya Rwanda ,Kigali.

Amesema kuwa Bodi hiyo imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuvutia watalii wa mikutano kwa kushirikiana kwa karibu na Sekta Binafsi.

“Kwa mfano kuna ukumbi mkubwa wa mikutano unaomilikiwa na Serikali unaendeshwa na Sekta Binafsi na umefanikiwa kuvutia watalii wengi” ameongeza Mhe. Masanja.

Amesema kupitia ujuzi uliopatikana katika kikao hicho, Tanzania itaenda kuutumia ili kutangaza na kuvutia watalii wa mikutano kutoka ndani na nje ya nchi na hatimaye kuikuza Sekta ya Utalii.
Share:

Video Mpya : NG'WANA SALA - POMBE NI TAMU


Hii hapa video mpya ya Msanii Ng'wana Sala inaitwa Pombe Tamu...Itazame hapa


Share:

Ngoma Matata ya Walevi : MSANII MEZA - WALWA



Kama kawaida ya Malunde1 blog kukuweka karibu na wasanii wa nyimbo za asili.Leo ninayo ngoma mpya kali ya asili kutoka kwa msanii wa Nyimbo za asili Meza kutoka Ilola Shinyanga vijijini inaitwa 'Walwa' (pombe).


Wimbo huu ni maalumu kwa walevi,umetengenezwa katika studio za Passmedia zilizopo mjini Kahama mkoani Shinyanga.


Tazama ngoma hii ya walevi hapa chini..ni balaa sana
Share:

SERIKALI YAIAGIZA TAKUKURU KUWA WAKALI KUSIMAMIA FEDHA ZA MIRADI ZILIZOTOLEWA NA RAIS SAMIA


Naibu Waziri wa nchi,Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi na Utawala bora Deo Ndejembi akifunga Mkutano wa mwaka wa wakuu wa Takukuru Jijini Dodoma.
Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU,Kamishna wa Polisi Salum Rashid Hamduni akizungumza wakati wa kufunga Mkutano wa mwaka wa wakuu wa Takukuru Jijini Dodoma.
Viongozi wakuu wa Takukuru kutoka mikoa 28 nchini wakiwa katika picha ya pamoja katika mkutano wao wa Mwaka wenye lengo la kutathmini utendaji kazi.


Na Dotto kwilasa, Malunde 1 blog_Dodoma

SERIKALI imeiagiza Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini (TAKUKURU) kufuatilia,kusimamia na ikibidi kuwa wakali katika fedha zilizotolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya shule na vituo vya afya.

Hatua hii imekuja ikiwa ni siku chache tangu Rais Samia azindue Mpango wa Serikali kuinua uchumi na kukabikiana na ugonjwa wa virusi vya Corona kwa kutumia mkopo wa fedha wa shilingi Trilioni 1.3 uliotolewa na Shirika la Fedha Duniani (IMF) na kutoa onyo Kwa watendaji kuzielekeza fedha hizo kwenye malengo yaliyokusudiwa.


Naibu wa nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora, Deogratius Ndejembi amesema hayo jana Wakati akifunga mkutano mkuu wa mwaka wa wakuu wa TAKUKURU jijini Dodoma na kusema kuwa kuna viashiria vya rushwa katika fedha hizo huku akidai kuna maeneo tofali linafuatwa umbali wa kilomita 150 wakati kuna uwezekano wa kupatikana kwa urahisi.

Ndejembi amekosoa pia uamuzi wa baadhi ya watendaji kuchukua muda mrefu kwenye ushindani wa zabuni na kushindwa kukidhi mahitaji muhimu ya muda wa utekelezaji wa miradi ndani ya miezi tisa kuanzia sasa na kubainisha kuwa hali hiyo huenda ikawa ni kiini cha rushwa, uzembe, upendeleo, pamoja na uwezo mdogo wa mzabuni.

“Nawaagiza TAKUKURU nendeni mkasimamie fedha za miradi zilizotolewa na Rais, kuna viashiria vya rushwa katika fedha hizo ,maeneo mengine tofali linafuatwa umbali wa kilomita 150 mtu mmoja anapewa tenda za kununua matofali,kuna maeneo mengi ujenzi umesimama ukiuliza unaambiwa nondo zimeisha,hapa kuna viashiria vya rushwa,niwaombe sana mfuatile na muwe wakali,”amesema.

Aidha,Naibu waziri huyo ameitaka TAKUKURU kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu madhara ya rushwa ikiwa ni pamoja na kuwa na mipango ya katika kuzuia zaidi ili kuleta faida.

“Tusimame imara tuwadhibiti watumishi wanaofanya kazi kwa mazoea simamieni rushwa na mmomonyoko wa maadili huku mkizingatia utoaji wa haki,”amesema.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU,Kamishna wa Polisi Salum Rashid Hamduni,amesema katika Mkutano huo wa siku tatu uliohusisha viongozi wa Taasisi hiyo kutoka mikoa 28 wameweza kutathmini utendaji wao na kujadili namna Bora ya kuongeza ufanisi wa mapambano dhidi ya rushwa.

"Kwa muda wa siku tatu tumejifunza mengi kupitia mada mbalimbali za misingi ya maadili na mashauri ya kinidhamu,yote haya ni kuhakikisha chombo hiki kinakuwa cha mfano, kwa ujumla kila mmoja wetu amépata tiba anayostahili,"amesema Mkurugenzi huyo.

Sambamba na hayo amesema Taasisi hiyo inaendelea kufanya tafiti kubaini njia bora za kuziba mianya ya rushwa na kwamba kwa kipindi cha mwaka 2020 hadi 2021 jumla ya shilingi billioni 29.3 ziliokolewa na kwamba billion 11 .2 ziliokolewa kwa mfumo wa fedha taslim na utaifishaji mali huku kiasi cha bilioni 18 zilidhibitiwa kabla hazijatumika.

Ameeleza miradi ya kimaendeleo 1,188 yenye thamani ya billion 714.17 katika sekta ya afya maji elimu ziliweza kufatiliwa na kuona makosa ambayo wameyachukulia hatua.

“Tumejifunza namna ya kudhibiti hisia hasi na mahusiano kazini,hali hii itatupa nguvu zaidi ya kuzuia vitendo vya rushwa na kuongeza kushirikisha jamii pamoja na kuwafikisha watuhumiwa Mahakami kwa kushirikiana na ofisi ya Taifa ya mashtaka", amefafanua.

Vile vile ameeleza kuwa jumla ya majalada 1,053 yalichunguzwa na kukamilishwa huku majadala 339 yaliwasilishwa kwa Mkurugenzi wa mashitaka kuomba kibali cha kuwafikisha mahakani esi mpya zilipatikana 542, na kesi 541 zilitolewa uamuzi ambapo Jamhuri iliweza kushinda kesi 345.
Share:

WAKANDARASI MIRADI YA UMEME VIJIJINI WAAGIZWA KUANDAA MPANGO KAZI


Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo akizungumza na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini katika Mkoa wa Pwani (hawapo pichani), akiwa katika ziara ya kazi wilayani Bagamoyo, mwishoni mwa juma.

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy (wa tatu-kulia), akifafanua jambo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo (wa pili-kushoto), Mjumbe wa Bodi Oswald Urassa (wa kwanza-kushoto) na wataalam kutoka REA na TANESCO, wakati Ujumbe huo ulipokuwa katika ziara ya kazi wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani, mwishoni mwa juma.

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo akiwa amefuatana na Mjumbe wa Bodi, Oswald Urassa, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy, watalaam kutoka REA na TANESCO pmaoja na mkandarasi kutoka kampuni ya Sinotec, wakikagua mradi wa kusambaza umeme katika maeneo yaliyo pembezoni mwa miji, Kitongoji cha Dagaza wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani mwishoni mwa juma.

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo (katikati), Mjumbe wa Bodi Oswald Urassa (kushoto) na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy (kulia), wakiwa katika kikao na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini katika Mkoa wa Pwani (hawapo pichani). Viongozi hao walikuwa katika ziara ya kazi wilayani Bagamoyo, mwishoni mwa juma.

Msimamizi wa miradi ya umeme vijijini, Kanda ya Mashariki, Mhandisi Balisidya Myula akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo, Mjumbe wa Bodi Oswald Urassa na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy (hawapo pichani). Viongozi hao walikuwa katika ziara ya kazi mkoani Pwani, mwishoni mwa juma.

Wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini Mkoa wa Pwani, wakiwa katika kikao na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo, Mjumbe wa Bodi Oswald Urassa na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy (hawapo pichani). Viongozi wa REA walikuwa katika ziara ya kazi kukagua utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini, wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani, mwishoni mwa juma.

******************************

Na Veronica Simba, REA - Pwani

Wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini wametakiwa kuandaa mpango kazi unaoainisha kazi zote wanazofanya pamoja na muda wa kuzikamilisha kwa kila hatua.

Sambamba na hilo, wameagizwa kila mmoja kuwasilisha mpango kazi wake kwa viongozi wa eneo anakotekeleza Mradi akiwemo Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya, Mbunge, Diwani, Mwenyekiti wa Kijiji na Ofisi ya TANESCO ili kurahisisha ufuatiliaji wa utekelezaji wa miradi hiyo.

Wito huo umetolewa mwishoni mwa juma na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Wakili Julius Kalolo, ambaye alifuatana na Mjumbe wa Bodi Oswald Urassa pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini, Mhandisi Hassan Saidy, wakiwa katika ziara ya kazi wilayani Bagamoyo, Mkoa wa Pwani.

“Hili ni agizo kwa wakandarasi wote wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini nchini kote. Kila mmoja awasilishe mpango kazi wake kuanzia sasa hadi pale mradi utakapokamilika,” alisisitiza Wakili Kalolo.

Vilevile, Ujumbe huo wa REA ulitoa maagizo kwa wakandarasi kuhakikisha wanajenga uhusiano mzuri na jamii katika maeneo wanakotekeleza miradi.

Akifafanua kuhusu agizo hilo, Mkurugenzi Mkuu wa REA aliwataka wakandarasi kuwaelekeza wafanyakazi na vibarua wao kutumia lugha nzuri wakati wakiwasiliana na jamii, kulipia kwa wakati huduma zote zinazotolewa na wananchi pamoja na kujiepusha na vitendo mbalimbali vilivyo kinyume na maadili ikiwemo mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi pamoja na mabinti wadogo.

Aidha, viongozi hao waliwaelekeza wakandarasi kuhakikisha wanatumia vifaa vyenye ubora katika kutekeleza miradi hiyo kwani serikali haitahusika kulipia gharama ya kubadili vifaa vitakavyokaguliwa na kuthibitika kuwa havina ubora unaotakiwa.

“Mkandarasi atakayeagiza na kutumia vifaa visivyo na ubora, atambue kuwa atabeba gharama ya kuvibadilisha,” alisisitiza Mhandisi Saidy.

Naye Mjumbe wa Bodi, Oswald Urassa aliwasisitiza wakandarasi kuhakikisha wanakamilisha miradi wanayotekeleza kwa muda ulioafikiwa katika mikataba yao na kuongeza kuwa wazingatie ubora unaotakiwa.

“Wakandarasi wakumbuke kuwa hatutaongeza muda wa kukamilisha miradi hiyo hivyo wajipange kwelikweli,” alisema Urassa.

Katika hatua nyingine, viongozi hao wa REA waliwaasa wananchi kutunza miundombinu ya umeme iliyopo katika maeneo yao kwani serikali inatumia fedha nyingi kuijenga, hivyo uharibifu wake ni hasara kwa serikali na wananchi wa eneo husika.

Katika ziara hiyo, viongozi hao walikagua utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini wilayani Bagamoyo, hususan mradi wa kusambaza umeme katika maeneo yaliyo pembezoni mwa miji maarufu kama mradi wa Peri-Urban.

Pia, walifanya kikao pamoja na wakandarasi wanaotekeleza miradi ya umeme vijijini katika Mkoa wa Pwani na kujadiliana maendeleo ya utekelezaji wa miradi hiyo pamoja na kutoa maelekezo yanayohusu ukamilishwaji wake kwa wakati.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger