Sunday 28 November 2021

Tanzia : NGULI WA PICHA TANZANIA RAMADHANI TONGE AFARIKI DUNIA




Mzee Ramadhani Tonge ambaye aliwahi kuwa mkufunzi wa masuala ya picha katika vyuo vya uandishi wa habari jijini Dar es Salaam amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Amana, Ilala  Jijini  Dar es Salaam na mwili wake utasafirishwa kwenda Morogoro kwa ajili ya mazishi.

Kwa nyakati tofauti, Mzee Tonge alitoa huduma ya ukufunzi katika Chuo cha Uandishi wa Habari cha Times School of Journalism (TSJ) cha Ilala Shariff Shamba jijini Dar es Salaam.

Pia aliwahi kuwa mkufunzi Dar es Salaam School of Journalism kilichopo Ilala, Sharrif Shamba na kuhudumu SHIHATA, Idara ya Habari MAELEZO na kwingineko kama mpiga picha.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBA 28,2021


Magazetini leo Jumapili November 28 2021







Share:

Saturday 27 November 2021

RAIS YOWERI MUSEVENI WA UGANDA AANZA ZIARA YA SIKU TATU TANZANIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na mgeni wake Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam leo tarehe 27 Novemba 2021 kwa ajili ya ziara ya Kitaifa ya siku tatu hapa nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni akimtambulisha ujumbe aliofuatana nao mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam leo tarehe 27 Novemba 2021 kwa ajili ya ziara ya Kitaifa ya siku tatu hapa nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakisalimiana na Wasanii wa vikundi vya ngoma mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam leo tarehe 27 Novemba 2021 kwa ajili ya ziara ya Kitaifa ya siku tatu hapa nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam leo tarehe 27 Novemba 2021 kwa ajili ya ziara ya Kitaifa ya siku tatu hapa nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama na mgeni wake Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakati nyimbo za mataifa mawili (Tanzania &Uganda na ule wa Afrika Mashariki) zikipigwa katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam leo tarehe 27 Novemba 2021 mara baada ya Rais wa Uganda Mhe. Museveni kuwasili nchini.
Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni, akikagua Gwaride la JWTZ nara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam leo tarehe 27 Novemba 2021 mara baada ya Rais wa Uganda Mhe. Museveni kuwasili nchini.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na mgeni wake Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni wakati alipowasili katika Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam leo tarehe 27 Novemba 2021 mara baada ya Rais wa Uganda Mhe. Museveni kuwasili nchini.
**


Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni amewasili nchini kwa Ziara ya Kitaifa ya siku 3 yenye lengo la kuimarisha uhusiano baina ya nchi yake na Tanzania kufuatia mualiko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Jijini Dar es Salaam, Mhe. Rais Museveni amekagua gwaride la heshima lililoandaliwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa ajili yake pamoja na kupigiwa mizinga 21.

Mhe. Rais Museveni alipowasili Ikulu Jijini Dar es Salaam amefanya mazungumzo na mwenyeji wake Mhe. Rais Samia pamoja na kuzungumza na vyombo vya habari kuhusu masuala mbalimbali ya uhusiano na ushirikiano wa nchi hizi mbili.

Katika mazungumzo yake na vyombo vya habari, Mhe. Rais Samia amesema Tanzania inaridhishwa na uhusiano mzuri na wa kindugu uliopo kati yake na Uganda na kusisitiza kuwa uhusiano huo utaendelea kudumishwa.

Mhe. Rais Samia amesema yeye na Rais Museveni wamewaelekeza Mawaziri wa Kisekta kukutana mara kwa mara kwa ajili ya kutatua changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika maeneo yao ili kuendelea kuimarisha ushirikiano huo.

Pia, Mhe. Rais Samia amesema Uganda ni nchi ya pili kwa uwekezaji hapa nchini kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, ambapo Uganda imetoa ajira 2,150 kwa watanzania. Mhe. Rais Samia ameahidi kwamba Tanzania itaendelea kuwekeza zaidi nchini Uganda ili kukuza zaidi kiwango cha biashara.

Mhe. Rais Samia amesema kwa lengo la kuimarisha biashara kati ya nchi mbili hizo, wamekubaliana kushughulikia kwa pamoja vikwazo visivyokuwa vya kikodi na kuviondoa.

Amesema, katika mazungumzo yake na Mhe. Rais Museveni wamekubaliana kukuza biashara na uwekezaji kati ya nchi hizo mbili kwa kuwa bado kuna fursa nyingi za kibiashara hususan katika sekta za viwanda, kilimo, uvuvi, huduma za kijamii, utalii pamoja na usafirishaji.

Vilevile, Mhe. Rais Samia amemshukuru Mhe. Rais Museveni pamoja na Serikali ya Uganda kwa uamuzi wa kuendelea kutumia Bandari ya Dar es Salaam kupitisha shehena mbalimbali za mizigo ikiwemo itakayotumika katika ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi mkoani Tanga nchini Tanzania.

Mhe. Rais Samia pia amemuomba Mhe. Rais Museveni kuridhia Mamlaka ya Bandari nchini kufungua ofisi yake ya uratibu Jijini Kampala, Uganda kwa ajili ya kusogeza karibu huduma za Bandari kwa wateja waliopo Uganda.

Aidha, Mhe. Rais Samia amesema Serikali ya Tanzania na Uganda zimekubaliana kujenga viwanda vya kutengeneza chanjo ya UVIKO 19 pamoja na magonjwa mengine ikiwa ni jitihada za kupambana na kuenea kwa magonjwa hayo.

Mhe. Rais Samia amemshukuru Mhe. Rais Museveni kwa uamuzi wa kujenga Shule ya Msingi Museveni yenye Mtaala wa Kiingereza wilayani Chato mkoani Geita na kueleza kuwa hatua hiyo ni ishara ya upendo, undugu na uhusiano mzuri kati ya nchi hizo mbili.

Kwa upande wake Mhe. Rais Museveni amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa mualiko wa kuja kutembelea Tanzania katika ziara hiyo ambayo amesema inazidi kuimarisha uhusiano wa kindugu baina ya mataifa hayo uliokuwepo kwa muda mrefu.

Mhe. Rais Museveni amesema wamekubaliana kuwa Serikali zote mbili zitaendelea kusimamia mradi wa ujenzi wa Bomba la kusafirisha mafuta ghafi la Afrika Mashariki kutoka Hoima Uganda hadi Tanga nchini Tanzania na kuhakikisha unakamilika kwa wakati na kuleta manufaa yaliyokusudiwa.

Jaffar Haniu

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.
Share:

BENKI YA NBC YATOA MSAADA WA MIFUKO 920 YA SARUJI UJENZI WA MABWENI SHULE YA KIRIBA MUSOMA


Makabidhiano ya saruji yakiendelea

Na Mussa John Mara

Benki ya NBC imetoa mifuko mia 920 ya saruji yenye thamani ya shilingi milioni 21 katika shule ya sekondari Kiriba iliyopo halmashauri ya wilaya ya Musoma Mkoani Mara ili kuunga juhudi za wananchi za ujenzi wa mabweni mawili ya wasichana na wavulana.

Akizungumza wakati wa kukabidhi saruji hiyo Meneja wa NBC Tawi la Musoma Sophia Lyimo alisema lengo la NBC ni kutoa msaada kwa jamii inayowazunguka na ni jambo wamekuwa wakilifanya hivyo kutolewa kwa saruji hiyo ni kuhakikisha wanaunga mkono jitihada za wananchi kwa ajili ya ujenzi wa mabweni katika shule hiyo.

Lyimo alisema kuwa kutokana na changamoto ya wanafunzi wanaosoma katika shule hiyo kutembea umbali mrefu imewalazimu kuungana na serikali ya Mhe. Rais Samia Suluhu iliyotoa kiasi cha shilingi Milioni sitini (60) kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vitatu vya madarasa na wananchi kuamua kujenga mabweni hivyo saruji hiyo itasaidia sehemu flani kufikia kiwango wananchi wanachokihitaji.


“Lengo letu ni kuhakikisha ndoto za watoto hawa zinafikiwa nakumuunga Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan katika utoaji wa elimu bora kwa hiyo tunakabidhi mifuko hii ya saruji kwani furaha ya NBC nikuona watoto wanaondokana na changamoto hasa katika swala la elimu”,alisema Lyimo.

Mkuu wa shule ya Sekondari Kiriba Mtani Shadrack Paul ameipongeza Benki ya NBC kwa namna ilivyoguswa katika kuchangia shule hiyo ambayo pia inatarajia kufungua kidato cha tano na sita mwaka 2022 hivyo kukamilika kwa mabweni hayo itasaidia mabinti ambao wanatembea kilomita zaidi ya 10 kwenda na kurudi shule.

“Hatuwezi kumsahau mbunge wa jimbo hili Profesa Sopeter Muhongo kwa namna ambavyo anatushirikisha kuhakikisha jambo hili linakamilika kama inavyotakiwa binfasi nimefarijika sana kwa msaada huu kutoka NBC bado tunahitaji wadau wengine wajitoe kusaidia kama walivyofanya Benki hii tulituma maandiko na leo wametupokea ni msaada mkubwa ambao unaungana na nguvu za wananchi kufikia malengo zaidi”, Hamisi Magoti Diwani wa kata ya Kiriba.


Aidha baadhi ya viongozi wa vijiji vitatu wanaoshiriki katika ujenzi wa mabweni hayo ikiwemo Bwai Kumsoma ,Bwai Kwitururu pamoja na Kiriba wamesema msaada huo utakuwa chachu kwa wananchi kujitokeza kwa wingi kuongeza nguvu kazi katika eneo la mradi ambapo wamesema watahakikisha saruji hiyo inasimamiwa na kufanya kazi iliyokusudiwa.
Share:

RAIS SAMIA ATEUA VIONGOZI MBALIMBALI, YUMO BALOZI OMBENI SEFUE






RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa viongozi wafuatao:-

Mosi, amemteua Balozi Ombeni Yohana Sefue, Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Uongozi (Uongozi Institute). Balozi Sefue anachukua nafasi ya Dkt. Stergomena Tax ambaye ameteuliwa kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Novemba 27, 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais (Ikulu), Jafar Haniu, uteuzi huo umeanza tarehe 24 Novemba, 2021.


Pili amemteua Balozi Mathias Meinrad Chikawe, Mwenyekiti na Mkurugenzi Mwenza wa Kampuni ya Uwakili ya FMD Legal Consultants and Advocates kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni ya Tanzania and Italian Petroleum Refining Company Limited (TIPER).


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Novemba 27, 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais (Ikulu), Jafar Haniu, uteuzi huo umeanza tarehe 24 Novemba, 2021.


Tatu amemteua Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe, Katibu Mkuu Mstaafu – TAMISEMI kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF).


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Novemba 27, 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais (Ikulu), Jafar Haniu, uteuzi huo umeanza tarehe 16 Novemba, 2021.


Nne amemteua Prof. Ephata Elikana Kaaya kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Kilimanjaro (KCMUCo), Kilimanjaro kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Taasisi ya Saratani Ocean Road.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Novemba 27, 2021 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais (Ikulu), Jafar Haniu, uteuzi huo umeanza tarehe 15 Novemba, 2021.
Share:

TPSF NA PSFU WAANDAA KONGAMANO KUJADILI FURSA ZITAKAZOPATIKANA KWENYE MRADI WA BOMBA LA GESI

Waziri wa Nishati Mhe.January Makamba akizungumza katika kongamano la Mafuta na Gesi lililoandaliwa na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania pamoja na Taasisi ya Sekta Binafsi Uganda kujadili ni namna gani wanaweza kunufaika na mradi wa Bomba la gesi. Kongamano hilo limefanyika leo JJkatika ukumbi wa JNICC Jijini Dar es Salaam. Naibu Waziri wa Nishati Mhe. Stephen Byabato akizungumza katika kongamano la Mafuta na Gesi lililoandaliwa na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania pamoja na Taasisi ya Sekta Binafsi Uganda kujadili ni namna gani wanaweza kunufaika na mradi wa Bomba la gesi. Kongamano hilo limefanyika leo JJkatika ukumbi wa JNICC Jijini Dar es Salaam.

Wadau wa Gesi wakifuatilia kongamano la Mafuta na Gesi lililoandaliwa na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania pamoja na Taasisi ya Sekta Binafsi Uganda kujadili ni namna gani wanaweza kunufaika na mradi wa Bomba la gesi. Kongamano hilo limefanyika leo JJkatika ukumbi wa JNICC Jijini Dar es Salaam. Waziri wa Nishati Mhe.January Makamba akipata picha ya pamoja na baadhi ya wadau wa gesi nchini katika kongamano la Mafuta na Gesi lililoandaliwa na Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania pamoja na Taasisi ya Sekta Binafsi Uganda kujadili ni namna gani wanaweza kunufaika na mradi wa Bomba la gesi. Kongamano hilo limefanyika leo JJkatika ukumbi wa JNICC Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

*****************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Taasisi ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF) kwa kushirikiana na taasisi ya sekta binafsi ya nchini Uganda (PSFU) wameandaa Kongamano la pamoja la Mafuta na gesi ili kujadili Mradi wa Bomba la Gesi kuona ni namna gani wanaweza kunufaika.

Akizungumza katika Kongamano hilo Waziri wa Nishati Mhe.January Makamba amesema kupitia kongamano hilo litatoa elimu kwa Watanzania na sekta binafsi kwa nchi yetu.

"Mradi huu unauwezo mkubwa hasa kuchangia katika uchumi wa nchi yetu, unauwezo wa kuchangia katika ajira pamoja na kutujengea uwezo kama Watanzania katika sekta hii". Amesema Waziri Makamba.

Amesema katika kila eneo ambalo bomba hilo limepita kuna fursa za ajira mbalimbali kama vile makambi, ulinzi, chakula, usafirishaji, ujenzi na ajira nyingine nyingi.

Aidha amesema Tanzania ina mradi mwingine wa kuchakata gesi mkoani Lindi ambao wameanza mazungumzo kati yao na wawekezaji.

"Kupitia mradi huu, Tanzania na Uganda zinaenda kubadilika kwa kiasi kikubwa kwa maana ya Uchumi wake na masrahi wananchi wa nchi hizo mbili". Amesema

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Sekta Binafsi (TPSF) Bw. Francis Nanai amesema gharama za utengenezaji wa mradi huo zaidi ya dola za Kimarekani 3.5 Bilioni lakini ukiangalia mnyororo mzima wa thamani umezidi dola za Kimarekani Bilioni 20 ambazo zinakaribia tirioni 45.

Amesema wamekutana kufahamu na kueleimishana kuhusu mradi hasa faida zake kwenye suala la ajira.

"Tutaangalia ni namna gani Watanzania wanaweza kunufaika kuhusiana na huu mradi moja kwa moja au kupitia mambo mengine ya kibiashara ". Amesema Bw.Nanai.
Share:

KOFFI OLOMIDE APIGWA STOP KUFANYA TAMASHA RWANDA



Wanaharakati wa haki za wanawake nchini Rwanda wamelipiga ‘stop’ tamasha la mwamba wa Rhumba wa Congo, Koffi Olomide kwa tuhuma za ubakaji na unyanyasaji wa kingono anazokabiliwa nazo katika Mahakama za Ufaransa.


Mwezi Desemba, Mahakama ya Paris nchini Ufaransa itatoa uamuzi wa rufaa iliyoombwa kwa mashtaka dhidi ya Le Grand Mopao Mokonzi ambaye alipatikana na hatia ya kuwanyanyasa kijinsi wanenguaji wake wanne wa zamani.


Juliette Karitanyi, mwanaharakati mjini Kigali, Rwanda anasema kumruhusu Koffi kutumbuiza nchini Rwanda itakuwa ni kutoheshimu waathiriwa wa unyanyasaji wa kingono.


Hata hivyo, baadhi ya watetezi wa Mopao Mokonzi kwenye mitandao ya kijamii wanasema hakuna msingi wa kisheria wa kumzuia kutumbuiza nchini Rwanda.
Share:

KIJANA ABEBA BANGO KUMSAKA BABA YAKE



Benson Kirobi, anayemtafuta Baba yake
**
Kijana mmoja nchini Kenya aitwaye Benson Kirobi, anamtafuta Baba yake aitwaye Benson Obote, ambaye hajawahi kumuona tangu azaliwe na kusema kwamba baba yake huyo alikuwa mwanajeshi na alitumwa nchini Sierra Leone kufanya kazi na hakuwahi kurudi tena.

Kufuatia hali hiyo Kirobi, aliamua kushika bango na kutembea nalo kwenye Jiji la Nairobi, akimtafuta mzazi wake huyo, ambapo wakati akifanyiwa mhojiano na Tuko swahili, alisema kwamba kwamba ameamua kufanya hivyo kwa kuwa kila mmoja hutamani kuwa karibu na watu anaowapenda.

"Baadhi ya watu walikuwa wakinitupia jicho kali, ishara kwamba kamwe hawakukubaliana na hatua yangu, hata hivyo nilihisi kuna wale ambao walinitia moyo kimya kimya, kila mmoja wetu anatamani kuwa na wale anaowapenda, ninaamini kwa kukutana naye, nitaelewa vyema kwa nini niko jinsi nilivyo,” amesema Kirobi

Kirobi amesema kwamba baba yake alipoondoka nchini, mama yake alikuwa mjamzito na huenda hakuwa anafahamu hali ya mke wake huyo na kwamba mama yake Kirobi alipomuulizia aliambiwa kwamba askari wengi waliokuwa kwenye oparesheni hiyo waliuawa vitani.
Share:

TAASISI ZA FEDHA ZAHIMIZWA KUTOA MIKOPO KWA WAVUVI NA WAFANYABIASHARA WA DAGAA


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akionja dagaa waliokuwa wanakaangwa katika mwalo wa Igombe ambapo amezisihi taasisi za kifedha pamoja na Halmashauri kutoa mikopo kwa wafanyabiashara hao wa dagaa ili waweze kuboresha mazingira na mitaji yao kwa kuwa biashara hiyo inalipa. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mhe. Hassan Masala.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akizungumza na Wavuvi katika mwalo wa Kayenze wilayani Ilemela mkoani Mwanza mara baada ya kusikiliza kero zao ambapo ameendelea kuwasisitiza kutumia zana sahihi za uvuvi.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akimuangali samaki aina ya sangara mwenye uzito zaidi ya kilo 40 wakati alipotembelea Kampuni ya Y & P inayozalisha barafu na kugandisha samaki Jijini Mwanza. Mhe. Ulega amewahimiza wamiliki wa Kampuni hiyo kuongeza kasi katika kukamilisha taratibu zilizobaki ili waanze kuchakata samaki.


Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mwanza, Dkt. Anthony Diallo akizungumza na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega wakati alipotembelea Ofisi za CCM Mkoa kwa ajili ya kusaini kitabu cha wageni. Kuanzia kushoto ni Katibu wa CCM Mkoa, Ndg. Julius Peter akifuatiwa na MNEC, Ndg. Jamal Babu.

.................................................................................

Taasisi za kifedha nchini zimehimizwa kutoa mikopo kwa wavuvi na wafanyabiashara wa dagaa kwa kuwa zao hilo lina tija kiafya na kiuchumi.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega wakati alipotembelea mwalo wa Igombe wilayani Ilemela mkoa wa Mwanza baada ya kufika kwenye moja ya banda linalotumika kukaangia dagaa na kukutana na wafanyabiashara hao.

Naibu Waziri Ulega amesema kuwa umefika wakati wa taasisi za kifedha pamoja na Halmashauri kuanza kuliangalia kundi hilo ambalo likiwezeshwa litaweza kuwahakikishia watanzania kuondokana na utapiamlo lakini pia kuongeza kipato kwa wahusika na taifa kwa ujumla.

“Dagaa ni zao la kimkakati kutokana na umuhimu wake kiafya na kiuchumi ndio maana tunaendelea kuzihamasisha taasisi za kifedha kuwakopesha wavuvi na wafanyabiashara wa dagaa ili waweze kuvua dagaa wengi kwa kutumia zana za kisasa, kuwahifadhi katika mazingira mazuri na kusafirishwa katika maeneo mbalimbali ya ndani na nje ya nchi,” alisema Naibu Waziri Ulega

Halmashauri kupitia mikopo ya asilimia 10 inayotokana na makusanyo ya mapato ya ndani zimeshauriwa kuanza kuliangalia kundi hilo linalojishughulisha na mnyororo wa thamani wa dagaa kwanza kwa kuwakopesha ili waweze kuboresha mazingira wanayofanyia kazi kuanzia kwenye utengenezaji wa vichanja kwa ajili ya kuanikia dagaa, kukaangia hadi kwenye maghala ya kuhifadhia.

Lakini pia Naibu Waziri Ulega amewasihi wafanyabiashara hao kuwa waaminifu hasa kwenye urejeshaji wa mikopo kwani kumekuwepo na tatizo la baadhi ya vikundi kusumbua kwenye urejeshaji wa mikopo waliyopatiwa. Vilevile amewataka kuzingatia ubora katika uandaaji wa dagaa hao ili wanapopelekwa sokoni kusiwe na tatizo lolote.

Pia amewataka wataalam kutoka katika Halmashauri kuwa jirani na wafanyabiashara hao ili wawasaidie katika kuwashauri namna ya kupanga mipango yao itakayowasaidia waweze kujinyanyua kiuchumi.
Share:

SERIKALI YASIKIA KILIO CHA MTATURU SINGIDA MASHARIKI

...............................................................

Mkandarasi wa Wakala wa Umeme Vijijini (REA),kutoka Kampuni ya M/s Central Electrical ameanza kazi ya kutawanya nguzo za umeme katika Tarafa ya Mungaa jimbo la Singida Mashariki.

Akizungumza baada ya kukagua uanzaji wa kazi ya usambazaji kwenye maeneo ya Kitongoji Cha Sie Kijiji Cha Mungaa,Katibu wa mbunge wa jimbo hilo Nicodemus Mwaya ameishukuru serikali kwa kutimiza ahadi yake.

"Tunaishukuru serikali kwa kusikia kilio Cha mbunge wetu Miraji Mtaturu,haya ni matunda yake,mara kadhaa amekuwa akiikumbusha serikali kupitia maswali anayouliza na michango anayoitoa bungeni,lakini pia amefuatilia wizarani Ili kuweka msukumo wa utekelezaji,tunamshukuru sana,

"Niahidi tu katika kipindi hiki ambacho Mbunge wetu anatekeleza majukumu mengine ya kibunge nje ya jimbo, mimi Katibu wake na viongozi wengine wa Chama Cha Mapinduzi CCM wilaya,na diwani tutakuwa tunapita mara kwa mara Ili kuona namna kazi inavyoendelea,lengo letu ni kuhakikisha dhamira ya serikali ya kufikisha umeme kwenye kila Kijiji inafikiwa,"aliongeza.

Singida Mashariki #MaendeleoKipaumbeleChetu#
Share:

Senior Grants and Compliance officer at FHI 360

Senior Grants and Compliance officer    FHI 360 is a nonprofit human development organization dedicated to improving lives in lasting ways by advancing integrated, locally driven solutions. Our staff include experts in Health, Education, Nutrition, Environment, Economic Development, Civil Society, Gender, Youth, Research and Technology; creating a unique mix of capabilities to address today’s interrelated […]

This post Senior Grants and Compliance officer at FHI 360 has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Senior Cargo Sales and Services Executive at Qatar Airways

Senior Cargo Sales and Services Executive    Qatar Airways  Dar es Salaam About the job We are pleased to announce an incredibly exciting opportunity to join our Cargo Sales team in Dar Es Salaam as Senior Cargo Sales and Services Executive. Accountabilities   Assist on all customer/client phone calls, telexes, e-mails with all information related […]

This post Senior Cargo Sales and Services Executive at Qatar Airways has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

PAKUA APP MPYA YA MALUNDE 1 BLOG....IMEBORESHWA ZAIDI KUKUPA RAHA YA HABARI NA MATUKIO BURE KWENYE SIMU YAKO


Toleo Jipya Kabisa la App ya Malunde 1 blog, Kama unayo kwenye simu Pakua Upya mtu wangu...  Bofya mara Moja <<Hapa>>
Toleo Jipya Kabisa la App ya Malunde 1 blog, Kama unayo kwenye simu Pakua Upya mtu wangu...  Bofya mara Moja <<Hapa>>
Toleo Jipya Kabisa la App ya Malunde 1 blog, Kama unayo kwenye simu Pakua Upya mtu wangu...  Bofya mara Moja <<Hapa>>

Habari Njema Wasomaji wa Malunde 1 blog !! Ili kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio  ya ukweli na uhakika kwa wakati yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla tunakushauri kupakua/ kudownload Aplikesheni ya Malunde 1 blog

Usikubali kupitwa na habari na Matukio yanayotokea… Pakua leo App ya Malunde 1 blog


Tembea na dunia kiganjani mwako kiulaini kabisa.

Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. 


Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install

https://bit.ly/2Qb7qyF

Usikubali kukosa habari kizembe..Pakua app yetu Mpya ya Malunde1 blog Sasa

Toleo Jipya Kabisa la App ya Malunde 1 blog, Kama unayo kwenye simu Pakua Upya mtu wangu...  Bofya mara Moja <<Hapa>>



Share:

Assistant Lecturer – Economics at Mzumbe University

POST: ASSISTANT LECTURER-ECONOMICS – 1 POST POST CATEGORY(S): BANKING, ECONOMICS AND FINANCIAL SERVICES EMPLOYER: Mzumbe University APPLICATION TIMELINE: 2021-11-25 2021-12-08 DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. Undergo an induction course in pedagogical skills for those who have not acquired them; ii. Carry out lectures; conduct tutorials, seminars and practicals for undergraduate programmes; iii. Prepare and present case studies; iv. […]

This post Assistant Lecturer – Economics at Mzumbe University has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Artisan II – Motor Vehicle Mechanics at Mzumbe University

POST: ARTISAN II-MOTOR VEHICLE MECHANICS – 1 POST POST CATEGORY(S): ENGINEERING AND CONSTRUCTION EMPLOYER: Mzumbe University APPLICATION TIMELINE: 2021-11-25 2021-12-08 DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. Performs more challenging machinery jobs under close supervision, ii. Collects and takes care of tools and equipment, iii. Perform routine technical cleaning of the workshop environments iv. Carries-out minor repairs and maintenance of […]

This post Artisan II – Motor Vehicle Mechanics at Mzumbe University has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Program Manager at Tech Mahindra

Program Manager   Tech Mahindra  Dar es Salaam, The ideal candidate will be comfortable outlining and planning all aspects of work related to a given project such as budget, timelines and teams. They will have strong communication skills that enable them to effectively communicate with all relevant teams. This individual should be able to foresee […]

This post Program Manager at Tech Mahindra has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Senior Project Manager at Tech Mahindra

Senior Project Manager   Tech Mahindra  Dar es Salaam, About the job – 10+ years of experience in managing and controlling large projects – Experience in Utilities and GIS domain – Experience in running minimum2 large GIS projects – Lead efforts in driving the project implementation and ensuring that all roadblocks are tracked and removed […]

This post Senior Project Manager at Tech Mahindra has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger