Sunday 25 October 2020

MAGUFULI AUNGURUMA MANYARA AKINADI SERA ZA CCM NA KUOMBA KURA...."VIJANA WANASEMA TUMETOBOA...NA KWELI TUMETOBOA KIMAENDELEO..TUSIKUBALI KUCHONGANISHWA"




NI MAGUFULI DAY: Siku mbili kuelekea Uchaguzi Mkuu, Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli ameendelea kuwafikia Mamilioni kwa Mamilioni ya Watanzania na Kunadi Sera, Ilani ya CCM na kuomba kura kwa Wananchi na Leo ni Zamu ya Manyara ambako amefanya Mkutano Mkubwa uliofana sana pale Babati na haya ndiyo aliyoyazungumza Kwenye Mkutano huo.
#KuraKwaMagufuli2020#T2020JPM

Waziri Mkuu mstaafu Mzee Fedrick Sumaye akizungumza nakumuombea kura mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM Rais Dk. John Pombe Magufuli katika mkutano huo.
Waziri Mkuu mstaafu Mzee Fedrick Sumaye akiwa ameketi na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Rodrick Mpogolo wakishiriki katika mkutano huo wa kampeni uliofanyika mjini babati. 
Picha mbalimbali zikionesha maelfu ya wananchi wakiwa wanamsikiliza mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Rais Dk. John Pombe Magufuli wakati alipokuwa akiwahutubia wananchi hao kwenye uwanja wa Kwaraa mjini Babati.
Share:

Majaliwa: Serikali Hainunui Korosho, Inasadia Upatikanaji Wa Masoko


MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa amesema Serikali hainunui korosho wala mazao mengine bali inaweka mazingira mazuri ya upatikanaji wa masoko.

“Serikali hainunui korosho, Serikali hainunui pamba, wala hainunui chai au kahawa. Kazi ya Serikali ni kutengeneza fursa ili wanunuzi waje. Mtu asitumie zao la korosho ili kujipatia umaarufu wa kisiasa,” amesema.

Ametoa kauli hiyo leo (Jumapili, Oktoba 25, 2020) wakati akizungumza na wakazi wa kata za Likongowele na Kibutuka wilayani Liwale ambako alienda kumuombea kura mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli, mgombea ubunge wa jimbo la Liwale, Bw. Zuberi Kuchauka na madiwani 20 wa kata za jimbo hilo.

“Mwaka 2018, kuna wafanyabiashara waliungana na wakagomea kununua korosho kwa sh. 1,800. Rais Dkt. Magufuli akasema hakuna kununua korosho za wakulima kwa bei hiyo, ndipo akatoa sh. bilioni 900 ili zitumike kununua korosho kwa bei isiyopungua sh. 3,000 kwa kilo.”

“Fedha hizo zimetumika kuwalipa wakulima, wasafirishaji, wenye magunia, kulipia usimamizi wa maghala na sasa imebakia kuwalipa Halmashauri ambao wanadai ushuru wa asilimia 5, na hao ni Serikali wenzetu kwa hiyo watalipwa tu. Kama kuna wakulima waliobakia ni mmoja mmoja sana, hao wanafuatiliwa na Wizara husika.”

Amesema korosho siyo zao pekee lililoathiriwa na kuporomoka kwa bei bali mazao mengine kama pamba, chai, kahawa na tumbaku nayo yameathiriwa na kushuka kwa bei mwaka huu.

“Korosho ni miongoni mwa mazao ya kimkakati nchini yaliyokosa soko msimu uliopita baada ya mataifa ya Ulaya kufunga mipaka yao kutokana na ugonjwa wa corona na hivyo wanunuzi hawawezi kuja nchini.”

“Korosho, pamba, tumbaku, chai na kahawa hayakuwa na bei nzuri kutokana na corona si vinginevyo. Serikali hainunui mazao, kazi yake ni kutengeneza mazingira mazuri ya soko asije mtu akawadanganya na kutumia bei za mazao ili apande chati kisiasa,” alionya.

Akitoa mfano, Mheshimiwa Majaliwa amesema: “Bei ya pamba imeshuka kutoka sh. 1, 200 hadi sh. 800 kwa kilo; kahawa imeshuka kutoka sh. 1,800 has sh. 1,200 kwa kilo, na tumbaku imeshuka kutoka sh. 1,700 hadi sh. 1,400.”

“Wanunuzi wakubwa wa korosho wanatoka China, Singapore, Vietnam na India. Hawa wenzetu sasa hivi bado wameelemewa na ugonjwa huu, hawawezi kutoka na kusafiri. Tuwaombee nchi zao ziondokane na corona ili na sisi tuweze kufanya biashara na nchi nyingine,” alisisitiza.

(mwisho)


Share:

Sekta ya mawasiliano ya simu ilivyo nguzo muhimu kuleta mabadiliko ya kiuchumi Tanzania


Dunia inaendelea kushuhudia maabadiliko makubwa ya kiteknolojia sehemu mbali mbali kwa kasi ya ajabu. Sehemu kubwa ya matunda ya teknolojia mfano matumizi ya simu mkononi ambayo yapo sasa, yasingeweza hata kufikirika mwanzoni mwa karne ya 21.

Ukweli usiopingika ni kwamba, kadiri maendeleo ya teknolojia yanavyozidi kupanuka, ndivyo matumizi ya mtandao wa intaneti yatakavyoongezeka. Kwa mfano, takwimu zilizotolewa na Mkutano wa Umoja wa Mataifa wa Biashara na Maendeleo zinaonesha kuwa matumizi ya data yameongezeka toka 46,000GB kwa sekunde mwaka 2017 na yatafikia 150,700 GB kwa sekunde mwaka 2022.

Vijana wanatajwa kuwa kundi lililo katika nafasi ya kunufaika zaidi na maendeleo haya ya kiteknolojia kutokana na uharaka wao katika kuweza kuitumia teknolojia.

Tanzania kama ilivyo nchi nyingine nayo inaendelea kunufaika na maendeleo haya ya kiteknolojia yanayoshamiri kote duniani. Tanzania imeshuhudia mabadiliko makubwa ya kidijitali huku watu wakitumia fursa hiyo kukuza biashara zao na kuendesha maisha.  

Kwa mfano, katika robo ya pili ya mwaka huu wa 2020, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetangaza kuwa matumizi ya jumla ya fedha kwa njia ya simu yameendelea kuongezeka ambapo jumla ya akaunti zilizosajiliwa kutuma na kupokea fedha kwa njia ya simu zimeongezeka kutoka milioni 27 mwezi Aprili hadi milioni 29 milioni mwishoni mwa Juni.
Ukuaji huu wa huduma ya fedha kwa njia ya simu umekuwa muhimu sana kwa namna ambavyo watu wanatumia na kuhifadhi fedha zao.

Maendeleo haya yote yanatokana na jitihada zilizofanywa kuwekeza katika sekta hii na wadau mbalimbali. Mfano mzuri ni Tigo Tanzania ambapo huduma ya fedha ya Tigo (Tigo Pesa) imewapatia wateja wake huduma yenye kasi na njia ya kuaminika ya kuweka na kutoa/kutuma fedha, pamoja na faida nyingine lukuki za kuingia katika mfumo rasmi wa kifedha bila urasimu.
 
Ama kwa hakika, sekta hii ya mawasiliano ya simu Tanzania imeonesha kuwa ina uwezo wa kuleta mabadiliko chanya katika nchi kupitia teknolojia.

Tukiwa tunafurahia na kutumia matunda ya sekta hii, tuendelee kuunga mkono sekta kwa kuendelea kuwa na sera rafiki na bora ili sekta hii izidi kukua na kuleta tija zaidi kwenye jamii na uchumi wa Tanzania kwa ujumala.


Share:

IGP Sirro aonya vikundi vilivyopanga kufanya vurugu Arusha.


Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Simon Sirro amesema jeshi lake limepata taarifa za kuwepo kwa baadhi ya vikundi vichache katika Jiji la Arusha vyenye nia ya kuharibu amani siku ya uchaguzi na kutoa onyo kali kwe wote wenye mpango huo.

IGP Sirro ametoa kauli hiyo Jijini Arusha baada ya kuzungumza na askari polisi zaidi ya 700 watakaosimamia mchakato wa uchaguzi unaotarajiwa kufanyika nchini kote Jumatano ijayo.

Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi pia ametumia fursa hiyo kuwaomba wananchi wa Mkoa wa Arusha kuendelea kuimarsha amani na utulivu siku hiyo ya uchaguzi.


Share:

HAYA NDIYO ALIYOYAZUNGUMZA MAJALIWA AKINADI JPM LEO MKOANI LINDI


 Mjumbe wa Kamati kuu ya CCM Ndugu Kassim Majaliwa ameendelea na Mikutano yake ya Kampeni Kunadi Sera na Ilani ya CCM Kisha kuomba kura. Na Leo Jumapili amefanya Mkutano Mkubwa wa Kampeni Wilayani Liwale Mkoani Lindi na haya ndiyo aliyoyazungumza Kwenye Mkutano huo Mkubwa. Liwale inasema ilikosea na Sasa wametubu, Oktoba 28 wanaenda na CCM tu kwa maendeleo na si ubabaishaji tena.

#KuraKwaMagufuli2020#T2020JPM
Share:

OFISI YA CHADEMA KANDA YA SERENGETI ILIYOPO SHINYANGA MJINI YANUSURIKA KUCHOMWA MOTO

Share:

Benard Membe Azungumzia Kuhusu Barua Inayosambaa Mitandaoni


Mgombea wa Urais kupitia chama cha ACT Wazalendo, Bernard Membe, ametoa sababu ya kuandika barua iliyokuwa ikisambaa mitandaoni ikieleza kuhusu kujitoa kwenye kinyanganyiro cha Urais wa Tanzania bara.


Membe kupitia ukurasa wake wa Twitter leo, amethibitisha kuwa barua hiyo iliyosambaa mitandaoni kuwa ni ya kweli na yeye ndiye aliyeandika barua hiyo.

“Barua inayosambaa ya tarehe 24/9 ya kujiondoa kwenye mbio za Urais ni ya kweli, niliandika baada ya kutofautiana na msimamo wa Viongozi wangu wa kutaka nimuunge mkono Tundu Lissu. Hata hivyo barua hiyo ilikataliwa kwa sababu maneno " msimamo wa viongozi wangu" yanawatia hatiani.” amesema Bernard Membe

Aidha katika barua hiyo inayosambaa iliyoelekezwa kwa mwenyekiti wa chama hicho Maalim Seif, na Katibu Mkuu wa cha hicho , Membe aliahidi kujikita katika kuwasaidia madiwani na wabunge wote wa chama hicho.
 





Share:

Majaliwa: Sh. Bilioni 5.26 Zanunua Dawa Lindi


MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa amesema katika kipindi cha miaka mitano, Serikali imetumia sh. bilioni 5.26 kwa ajili ya ununuzi wa dawa kwenye Manispaa ya Lindi.

“Serikali imetoa shilingi bilioni 5.26 ambapo kati ya hizo, shilingi bilioni 4 zilikuwa za Hospitali ya Rufaa ya Sokoine na shilingi bilioni 1.26 zilitolewa kwa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi kwa ajili ya ununuzi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi. Fedha za ununuzi wa dawa kwa mwezi, ni wastani wa shilingi milioni 21,” alisema.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumamosi, Oktoba 24, 2020) wakati akizungumza na wakazi wa mji wa Lindi na vitongoji vyake waliofurika kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika jana kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi.

Akielezea kuhusu uboreshaji wa sekta ya afya, Mheshimiwa Majaliwa alisema katika Manispaa ya Lindi, kuna magari matano ya kubeba wagonjwa kwa ajili ya vituo vya afya Mjini, Mnazimmoja, Kitomanga, Milola na Rutamba.

Mheshimiwa Majaliwa ambaye yuko mkoani Lindi kumuombea kura mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli, alitumia fursa hiyo kuwanadi mgombea ubunge wa jimbo la Lindi, Bi. Hamida Abdallah na wagombea udiwani wa kata 20 za jimbo hilo.

Kuhusu sekta ya maji, alisema sh. bilioni 50 zimetolewa kwa ajili ya miradi mikubwa ya maji ikiwemo ujenzi wa skimu ya pampu Mtutu, skimu ya pampu Cheleweni, Narunyu, Tandangongoro na Muungano na kwamba zimesaidia kuongeza upatikanaji wa maji kwenye mji wa Lindi.

“Fedha hizo zimetumika pia kwa ajili ya mradi wa maji safi na usafi wa mazingira Lindi Mjini (Mradi wa Maji Ng'apa) na kwenye mradi wa maji Ng'apa kijijini na usambazaji mtandao wa mabomba,” alisema.

Alisema sh. bilioni 1.26 zilitolewa kwa ajili ya miradi mingine ya maji ikiwemo ya kuchimba visima virefu katika maeneo ya Jangwani, Nanyanje, Kitumbikwela, Nachingwea, Kitunda, Likotwa, Mtange, Tulieni, Mitumbati, Mayani na Ngongo-Nanenane.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa alisema mkoa wa Lindi utanufaika zaidi kwa sababu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimeamua kuanzisha kitivo cha kilimo mkoani humo. “Taratibu zimeshakamilika na tumewapa ekari 150 katika eneo la Ngongo ili waweze kujenga kitivo cha kilimo,” alisema.

Leo Mheshimiwa Majaliwa anaendelea na kampeni kwenye jimbo la Liwale.

(mwisho)


Share:

SERIKALI YAKABIDHI BAISKELI 103 KWA WAHUDUMU WA AFYA IKUNGI

 

 Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo akikabidhi usafiri wa Baiskeli na Vipaza sauti kwa Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii wilayani hapo juzi kama nyenzo muhimu zitakazowasaidia. kurahisisha utekelezaji wa majukumu yao.

Hafla ya makabidhiano ikiendelea.
Afisa Lishe na Mratibu wa Huduma za Jamii wilayani hapo, Agnes John akisoma taarifa fupi ya Mradi wa Boresha Lishe kwenye Halmashauri ya Ikungi.
Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii wakiwa na baiskeli na vipaza sauti muda mfupi baada ya kukabidhiwa.
Mwonekano wa Baiskeli hizo.

Mkuu wa Wilaya Mpogolo akiendesha hafla hiyo.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Ikungi (DAS), Winfrida Funto (katikati) akifuatilia kwa makini makabidhiano hayo, kulia ni Afisa Tarafa, Josephine Kadaso na DC Mpogolo.

Hafla ikiendelea.

Afisa Mradi wa Boresha Lishe kutoka shirika la SEMA, Hudson Kazonte akizungumzia tija ya mradi huo na namna usafiri huo wa baiskeli utakavyopunguza changamoto ya utoaji huduma.


Na Godwin Myovela, Ikungi

SERIKALI kwa kushirikina na Umoja wa Nchi za Ulaya na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) imetoa jumla ya baiskeli 103 kwa wahudumu wote wa afya ngazi ya jamii sambamba na ‘vipaza sauti’ vyenye idadi kama hiyo wilayani hapa, lengo ni kuwapunguzia changamoto ya usafiri wakati wakitekeleza majukumu yao.

Katika kuboresha afya ya uzazi na lishe, kupitia mradi wa ‘Boresha Lishe’ serikali kupitia halmashauri ya Ikungi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, wakiwemo mashirika yasiyo ya kiserikali ya ‘SEMA’ na ‘RECODA’ imeazimia kupunguza udumavu wa siku 1000 za mtoto-yaani tangu kutungwa kwa mimba hadi anapofikisha miaka 2.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi baiskeli hizo ofisini kwake jana, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo aliwataka waliokabidhiwa baiskeli hizo kuhakikisha wanazitunza na zinatumika kwa malengo kusudiwa.

“Niwasihi muwe waangalifu na mzitunze baiskeli hizi, serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki kwenye sekta ya afya hususani kwenye eneo hili la afya ya uzazi na lishe, azma ikiwa ni kuhakikisha tunaondoa kabisa kiwango cha utapiamlo wa udumavu kutoka asilimia 7 mpaka 0,” alisema Mpogolo.

Aidha, aliyashukuru mashirika na nchi wahisani wanaoendelea kushirikiana na serikali katika kutekeleza mradi wa Boresha Lishe kwa vijiji 43 kuzunguka Ikungi huku akisisitiza ni mradi wenye tija kwa makundi yote ya jamii wilayani hapo, na hasa akinamama wajawazito, wanaonyonyesha na watoto chini ya miaka miwili.

Naye Afisa Lishe na Mratibu wa Huduma za Jamii wilayani hapo, Agnes John, alisema Halmashauri ya Ikungi ina jumla ya Kata 28 na Vijiji 101 vyote vina wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii, na wote wamepatiwa mafunzo ya msingi ya awali ya afya ya uzazi na lishe.

Halmashauri ya Ikungi ina jumla ya wakazi 329,520, ambapo watoto chini ya miaka mitano ni 58,707, na wanawake wenye umri wa kuzaa (miaka 15-49) wanafikia 22,884.

“Mafanikio tuliyoyapata mpaka sasa ni kujikwamua mapema kwenye rangi nyekundu, kwa miaka miwili mfululizo mpaka sasa viashiria vyote vinavyohusiana na huduma za wahudumu wa afya ngazi ya jamii vina alama ya kijani kuashiria tunafanya vizuri,” alisema John.

Aidha, mratibu huyo alisema hata kiwango cha utapiamlo wa udumavu kimepungua kutoka asilimia 7 mpaka asilimia 5, wakati kimkoa ni asilimia 29.8. Alisema ukondefu umepungua kutoka asilimia 1 hadi kufikia 0.4, wakati kimkoa ni asilimia 4.7.

 

Share:

MGOMBEA URAIS DK. MAGUFULI ANAENDELEA NA KAMPENI ZA UCHAGUZI LEO MANYARA

Tukiwa na siku 2 kuelekea Jambo letu, kazi ya Kuendelea na kukutana na Wananchi wa Kila sehemu kueleza Sera na Ilani bora ya CCM inaendelea na Leo Oktoba 25, 2020 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli ataunguruma Mkoani Manyara. Watanzania tuna Jambo Letu haswa.

#KuraKwaMagufuli2020
#T2020JPM

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi October 25
















Share:

Saturday 24 October 2020

LIVE: Rais Magufuli Akizindua Safari Za Treni Dsm - Tanga -Arusha.


 LIVE: Rais  Magufuli Akizindua Safari Za Treni Dsm - Tanga -Arusha.




Share:

Nchi Za Afrika Zahimizwa Kushikamana Ili Kuondokana Na Utegemezi


Nchi za Afrika zimehimizwa kushikamana katika masuala ya maendeleo, biashara na uwekezaji ili kuondokana na utegemezi jambo litakaloliwezesha Bara hilo kufanya mambo yake kwa uhuru bila kuingiliwa na mataifa mengine ya nje kwa kisingizio cha demokrasia na haki za binadamu.
Kauli hiyo imetolewa Jijini Dar es Salaam na Kiongozi wa Mabalozi wa nchi za Afrika hapa Tanzania Dkt. Ahamada El Badaoui Mohamed wakati Mabalozi hao walipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ikiwa ni utaratibu wa kukutana na Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania kwa lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo na Tanzania.

Kiongozi huyo wa Mabalozi hapa nchini ambaye pia ni Balozi wa Visiwa vya Comoro amesema njia pekee ya Afrika kutoingiliwa katika mambo yake ya ndani ni kuhakikisha kuwa bara hilo linaweka mikakati madhubuti itakayowezesha bara hilo kujitegemea.

"Njia pekee ya Afrika kutoingiliwa katika mambo yake ya ndani ni kuhakikisha kuwa sisi kama waafrika tunaweka mikakati madhubuti itakayowezesha bara letu kujitegemea kwa umoja, mshikamano wetu wenyewe," Amesema Dkt. Mohamed

Nae Balozi wa Kenya hapa Nchini Mhe. Dan Kazungu amesema kikao hicho cha mabalozi wa Afrika na Prof. Kabudi hususani katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, umewawezesha mabalozi hao kufahamu namna Tanzania ilivyojiandaa kutekeleza demokrasia na kuwataka waafrika kujivunia nchi zao na kuwa wazalendo.

"MKutano wa leo umetuwezesha sisi mabalozi wa Afrika tunaowakilisha nchi zetu hapa Tanzania kufahamu namna Tanzania ilivyojiandaa kutekeleza demokrasia na kuwataka waafrika kujivunia nchi zao na kuwa wazalendo," Amesema Balozi Kazungu.   

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameitumia fursa hiyo kuwaeleza Mabalozi hao namna Tanzania inavyoheshimu na kukuza diplomasia na mahusiano baina ya nchi za Afrika,kulinda demokrasia na haki za binadamu lakini pia kutumia fedha zake katika kuleta maendeleo ya watu na vitu jambo lililoiwezesha Tanzania kuingia katika nchi za uchumi wa kati kabla ya muda uliotarajiwa.  

"Waheshimiwa Mabaalozi napenda kuwahakikishia kuwa Tanzania inaheshimu na imedhamiria kukuza diplomasia na mahusiano baina ya nchi za Afrika, kulinda demokrasia na haki za binadamu pamoja na kuhakikisha kuwa inatumia fedha zake za ndani katika kuleta maendeleo ya watu na vitu jambo lililoiwezesha Tanzania kuingia katika nchi za uchumi wa kati kabla ya muda uliotarajiwa," Amesema Prof. Kabudi.  

Mkutano huo uliohudhuriwa Mabalozi 15 na wawakilishi wa Balozi 8 walitumia fursa hiyo kumuombea Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Baba wa Taifa hayati Julius Kambarage Nyerere kama Baba wa demokrasia Barani Afrika pamoja na kuuombea uchaguzi mkuu wa Oktoba 28.

Mabalozi waliohudhuria katika mkutano huo ni Balozi wa Visiwa vya Comoro, Mhe. Ahamada El Badaoui Mohamed, Balozi wa Msumbiji, Mhe. Patricio Clemente, Balozi wa Namibia, Mhe. Theresia Samaria, Balozi wa Somalia, Mhe. Mohammed Abdi, Balozi wa Morocco, Mhe. Abdelilah Benryane, Balozi wa Zambia, Mhe. Benson Chali.

Wengine ni Balozi wa Burundi, Mhe. Gervais Abayeho, Balozi wa Kenya, Mhe. Dan Kazungu, Balozi wa Ethiopia, Mhe. Yonas Yosef Sanbe, Balozi wa Misri, Mhe. Mohamed Gaber Mohamed Abdulwafa, Balozi wa Angola, Mhe. Sandro De Oliveira, Balozi wa Malawi, Mhe. Chembe Mnthali, Balozi wa Saharawi, Mhe. Mahayub Buyema, Balozi wa Rwanda, Mhe. Meja Jenerali, Charles Karamba pamoja na Balozi wa Algeria, Mhe. Ahmed Djelal.

Wawakilishi waliowakilisha Balozi nane ni Bw. Jaafar Nasir Abdalla kutoka Ubalozi wa Sudan, Mr. Sizwe Ernest Mayoli kutoka Ubalozi wa Afrika Kusini, Balozi William Wani Ruben kutoka Ubalozi wa Sudani Kusini, Bibi. Bintu Bwala Ekikor kutoka Ubalozi wa Nigeria, Bw. Kamal Krista kutoka ubalozi wa Libya, Bw. Adjanga Bissa Benjamin kutoka ubalozi wa DRC, Bibi. Musekura Esezakutoka ubalozi wa Uganda pamoja na Bw. Chrispen Chibuwe kutoka Ubalozi wa Zimbabwe.


Share:

TUMA second round selected applicants 2020/2021

The Tumaini University Makumira TUMA second round selected applicants 2020/2021 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Tumaini University Makumira (TUMA) for the 2020/2021 academic year second round application window. The Tumaini University Makumira TUMA second round applications and […]

The post TUMA second round selected applicants 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger