Sunday 30 August 2020
UHURU NA WAJIBU WA VYOMBO VYA HABARI KURIPOTI UCHAGUZI MKUU TANZANIA
Maalim Seif achukua fomu ya kuwania Urais Zanzibar
TUNDU LISSU KUTUA SHINYANGA MJINI JUMATANO KUZINDUA RASMI KAMPENI ZA UCHAGUZI CHADEMA KANDA YA SERENGETI
KANGOYE ATAKA WENYEVITI WA MITAA, MABALOZI NA VIJANA KUENDELEZA MSHIKAMANO WAGOMBEA CCM WASHINDE KWA KISHINDO
INTERNSHIP Opportunities at Envision Africa – Tanzania, TEACHERs
Teacher – Internship Job Description Envision Africa is a social enterprise dealing with innovative and effective ways in empowering youths to learn, thrive and succeed in personal and professional life.Envision Africa provides necessary tools, resources and opportunities for students and mid careers professionals to identify and communicate career interests and transferable skills for personal and […]
The post INTERNSHIP Opportunities at Envision Africa – Tanzania, TEACHERs appeared first on Udahiliportal.com.
Accountant at Afroil Investment Limited
Overview We, Afroil Investment Limited an oil marketing company based in Dar Es Salaam, Tanzania fully licensed and incorporated on 23rd October 2008 is currently looking for dynamic result oriented individual to fill the following position ( Women are highly preferred). Job Title: Accountant Reports to: Finance Manager Department: Finance. JOB PURPOSE To facilitate accurate and timely entry […]
The post Accountant at Afroil Investment Limited appeared first on Udahiliportal.com.
NYOTA WA FILAMU YA BLACK PANTHER CHADWICK BOSEMAN AFARIKI DUNIA
DC TANO MWERA: "SERIKALI IMEPIGA HATUA KWENYE HUDUMA ZA AFYA BUSEGA"
ALAT YAZITAKA HALMASHAURI KUHESHIMU FEDHA ZA MIRADI YA MAENDELEO
Saturday 29 August 2020
Serikali yaahidi milioni 200 kujenga madarasa DIT Myunga
SERIKALI kupitia Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dk Leonard Akwilapo imeahidi kutoa sh milioni 200 kwaajili ya ujenzi wa madarasa matano katika Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), Kampasi ya Myunga ikiyoko Wilaya ya mkoani Songwe.
Ahadi hiyo ilitolewa jana na Dk Akwilapo alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa bwalo la chakula lililojengwa kwa fedha zilizotolewa na serikali kupitia wizara hiyo.
"Nilikua naongea na mkuu wa Taasisi hapa kwamba nikiwapa milioni 200 so mtajenga madarasa matano ili Hawa wanafunzi wasirundikane kwenye darasa moja," alisema Dk Akwilapo.
Ahadi hiyo ilikuja kufuatia ombi la wanafunzi la kuomba serikali kuboresha niundombinu ya kujifunzia ikiwa ni pamoja na madarasa, uwanja wa michezo na vifaa vya michezo pamoja na gari la kwaajili ya kwenda kwenye mafunzo viwandani.
Dk Akwilapo alisema anaamini kwa fedha hizo DIT itajenga madarasa mazuri yenye ubora unaofaa kwa kutumia wataalamu wa ndani wa Taasisi hiyo.
Aidha katika tukio hilo, Dk Akwilapo aliahidi pia kumlipia ada mwanafunzi wa pili TEHAMA, Nozen Mkubwa ambaye alikuwa na changamoto ya ulipaji ada Jambo ambalo lilikuwa likimkwamisha katika masomo yake.
Akizungumzia ujenzi wa bwalo hilo, aliipongeza Taasisi hiyo kwa usimamizi mzuri wa rasilimali fedha uliofanikisha kukamilika ujenzi huo kwa asilimia 100.
Kwa upande wake Mkuu wa Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam, Profesa Preksedis Ndomba alishukuru serikali na Katibu Mkuu huyo kwa msaada ambao umekuwa ukitolewa na serikali kupitia wizara hiyo na kuahidi kuendelea kusimamia vema miradi inawekezwa na serikali katika Taasisi.
Mkurugenzi wa Kampasi ya DIT Myunga, Dk Frank Lujaji alishukuru kwa msaada wa kijana Nozen kulipiwa ada ambapo alitoa wito pia kwa Taasisi nyingine kusaidia vijana wenye changamoto za kupata ada kwani wengi Wana uwezo wa kimasomo pamoja na nia ya kusoma.
TIC yasema Milango ipo wazi kwa Wawekezaji Tanzania
KISHINDO DODOMA DK.MAGUFULI ATAJA ATAYAKAYOANZA NAYO
*Kununua ndege nyingine mpya tano kuimarisha usafiri wa anga nchini
Na Said Mwishehe, Michuzi TV-Dodoma
CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) kimezindua rasmi kampeni zake katika uchaguzi mkuu mwaka huu huku mgombea wake wa urais Dk.John Magufuli akitumia nafasi hiyo kuelezea mambo kadhaa yenye tija kwa Taifa hili iwapo watapata ridhaa tena ya kipindi cha miaka mitano ijayo.
Dk.Magufuli ambaye ametumia nafasi huyo kuzungumzia Ilani ya Uchaguzi Mkuu yaCCM ya mwaka 2020-2025 amewaomba Watanzania wa vyama vyote, dini zote na makabilia yote kuhakikisha wanakipa ushindi Chama chake ili kuendeleza yale ambayo wameyaanza katika miaka mitano ya kwanza.
Katika ufunguzi huo wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma na kuhudhuriwa na maelfu ya wananchi wa Jiji hilo na mikoa jirani ,Dk.Magufuli ametoa hotuba iliyojitosheleza kwa kuelezea hatua kwa hatua mambo ambayo Serikali yake imefanya na yale wanayotarajia kuyafanya iwapo watapewa ridhaa ya kushika dola.
Mgombea huyo wa CCM ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema katika miaka mitano ya kwanza wamefanya mambo makubwa yakiwemo ya kurudisha nidhamu katika utumishi wa umma.
Pia kukomesha rushwa, kudhibiti rasilimali za nchi ili ziwanufaishe Watanzania pamoja na kuboresha huduma mbalimbali za kijamii ikiwemo sekta ya afya,elimu, maji, barabara, usafiri wa anga na sekta nyingine muhimu.
“Katika miaka mitano ya kwanza ya uongozi wetu tumejitahidi kwa kadri ya uwezo wetu na sasa tunakuja kwenu tena watanzania kuomba ridhaa yenu mtupe tena miaka mitano mingine.
“Ili tuendelee na kazi ya kuwatumikia maana hatuna hakika kama mkiwapa wengine wataweza kuifanya kazi hii nzuri ambayo tumeianza na tunataka kuimalizia,”amesema Dk.Magufuli
Hata hivyo ameeleza alivyofurahishwa na na wananchi wa Dodoma kwa kujitokeza kwa wingi katika uzinduzi huo wa kampeni, hivyo amewaahidi atakapochaguliwa kazi ya kwanza akiwa madarakani itakuwa ni kuendelea kulijenga Jiji la Dodoma.
“Wananchi wa Jiji la Dodoma ambako ndiko makao makuu ya Serikali niwahakikishie tutaendelea kuijenga Dodoma, tutajenga uwanja mkubwa wa michezo ambao utawezesha wananchi wengi kuingia na kutosha tofauti na uliopo sasa,”amesema.
Pia amesema katika Jiji la Dodoma utajengwa uwanja mkubwa wa ndege wa kilometa tatu na hivyo ndege zote kubwa zitatokea Dodoma kwenda nchi za Ulaya kwani fedha zipo na Tanzania ni tajiri.
Hata hivyo amesema mwaka2015 Watanzania walitaka mabadiliko na hivyo baada ya kuingia madarakani walianza kufanya mabadiliko makubwa katika maeneo mbalimbali yakiwemo ya kusimamia uwajibikaji , kudhibiti mianya ya upotevu wa makusanyo ya fedha yatokanayo na kodi.
Ameongeza katika mabadiliko hayo Serikali anayoingoza ilisimama imara kuhakikisha sekta za ajira zinaimarishwa ili kuotoa ajira kwa Watanzania.” Tutahakikisha zinapatikana ajira milioni 8 ili kukuza uchumi kupitia ajira hizo.”
Pamoja na kuwepo kwa mambo mbalimbali ya kimaendeleo ambayo watafanya baada ya kuchaguliwa kwa mara nyingine tena, Dk.Magufuli amesema wataendelea kuimarisha usafiri wa anga kwa kununua ndege nyingine mpya tano.
Kati ya ndege hizo mbili zitakuwa za masafa marefu,mbili za masafa ya kati na ndege moja itakuwa ya mizigo.Kwa sasa tayari kuna ndege mpya nane na hivyo itafanya kuwa na jumla ya ndege 11.
DK.JOHN MAGUFULI AAHIDI KUENDELEA KUIMARISHA SEKTA YA NISHATI YA UMEME
MGOMBEA urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 28,2020 Dk.John Magufuli amesema katika miaka mitano ijayo iwapo Chama Cha Mapinduzi(CCM) kitapata ridhaa ya kushika dola wataendelea kuimarisha sekta ya nishati.
Akizungumza leo Agosti 28, mwaka2020 katika Uwanja wa Jamhuri wakati wa uzinduzi wa kampeni za CCM ,Dk.Magufuli amesema wataingiza megawati 5000 za nishati ya umeme katika gridi ya Taifa ikiwa ni mkakati wa kuhakikisha kunakuwa na umeme wa uhakika.
Dk.Magufuli amesema kumekuwepo na mkakati kabambe wa kuimarisha sekta ya nishati ya umeme na licha ya uwepo wa miradi mikubwa ya umeme iliyotekelezwa, kazi inayoendelea sasa ni ujenzi wa bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere.
Kwa upande wa sekta ya afya,Dk.Magufuli amesema kwa kipindi cha miaka mitano wamefanikiwa kujenga zahanati 1,198, Hospitali za Wilaya tisa, vituo vya afya 487, Hospitali za Mikoa 10, Hospitali za Rufaa katika kanda tatu huku pia watumishi wa sekta hiyo 14,479 wakiongezwa.
Amefafanua kwamba bajeti ya imeongezeka kutoka Sh.bilioni 31 hadi Sh.bilioni 270 na tumenunua magari mapya ya wagonjwa 117.Pia amesema wamepunguza safari za rufaa nje ya nchi kwa wagonjwa wa moyo, figo, ubongo na saratani.
“Katika kuimarisha sekta ya afya nchini tuliamua kusomesha madaktari bingwa katika fani mbalimbali ndani na nje ya nchi.Hivyo tunayo sababu ya kuomba miaka mitano mingine ili tuendelee na kazi ambayo tulianza miaka mitano iliyopita,” amesisitiza.
Kuhusu sekta ya madini, Dk.Magufuli amefafanua usimamizi mzuri uliopo umeiwezesha sekta hiyo kukua kwa asilimia 17.7.”Mapato yatokanayo na madini yameongezeka kwa kiwango kikubwa kwani hapo awali yalikuwa Sh.bilioni 168 katika mwaka 2014 hadi mwaka 2015 na sasa yamefikia Sh.bilioni 528.
“Tumeendelea kuboresha sheria kwani sheria mpya ya madini inaeleza kwa kila mgodi ambao utaanzishwa nchini kwetu serikali itakuwa na hisa ya 16,”amesema Dk.Magufuli na kufafanua kutokana na usimamizi mzuri Watanzania wamekuwa wakinufaika na madini yaliyoko katika nchi yao.
Ametumia nafasi hiyo kuzungumzia sekta ya elimu ambapo amegusia elimu bure ambayo inatolewa na Serikali na kufafanua kuwa Sh. Trilioni 1.09 zimetumika kusomesha watoto.
Pia amesema katika kipindi cha miaka wamejenga shule mpya za msingi 905, sekondari 228,wamekarabati shule kongwe 73, mabweni 253 na wameongeza madawati na walimu sambamba na kuangalia maslahi yao.
Ametumia nafasi hiyo kuwaambia Watanzania kipindi hiki cha kampeni za uchaguzi mkuu, wagombea wengi watapita kwa wananchi kunadi sera zao , kikubwa ni kuwasikilisa na kisha kufanya uamuzi sahihi Oktoba 28 mwaka huu ambayo ndio siku ya kupiga kura.
“Niwaombe tu wasikilizeni wagombea wote wataokuja kwenu na baada ya hapo mfanye uamuzi sahihi kwa kuchagua viongozi ambao wataleta maendeleo ya nchi yetu.CCM tunayo sababu ya kupewa dhamana ya kuongoza nchi kwasababu nia yetu ni kuendelea kuleta maendeleo.”
DK.HUSSEIN MWINYI AAHIDI KUENDELEZA PALE ALIPOISHIA RAIS MOHAMED SHEIN ZANZIBAR
Na Said Mwishehe,Michuzi TV
MGOMBEA Urais wa Serikali ya Mapinduzi Sanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)Dk.Hussein Mwinyi amesema akichaguliwa kuwa Rais wa Serikali hiyo atahakikisha anafanya kazi kwa kasi kubwa ya kuendeleza pale ambapo ameishia Dk.Mohamed Ali Shein.
Dk.Hussein Mwinyi ameyasema hayo leo Agosti 29 ,2020 wakati akitoa salamu za wananchi wa Zanzibar katika uzinduzi wa kampeni za mgombea Urais wa Chama hicho Dk.John Magufuli ambapo amesema hakika Dk.Shein amefanya kazi kubwa ya kuleta maendeleo,hivyo akipata nafasi ataendeleza kuanzia pale ambapo Rais Shein ameishia.
"Zanzibar wanasema wako tayari kuwachagua viongozi wa ngazi zote katika uchaguzi mkuu mwaka huu kuanzia Rais , Wabunge, Wawakilishi,Madiwani na Viti maalum.Ilani ya CCM imetekelezwa vizuri kwa pande zote na inatoa nafasi CCM kushinda.
"Nitafanya kazi ya kuendeleza pale alipoishia Rais Dk.Shein ambaye amefanya mambo nengi na nitafanya kazi kwa kubwa sana,"amesema Dk.Hussein Mwinyi na kusisitiza kwamba atasimama imara kuleta maendeleo.
Hata hivyo amesema kwamba hakuna sababu ya kubweteka na badala yake wanachama wa CCM na mashabiki wa Chama hicho kufanya kampeni ya nguvu na hatimaye kushinda kwa kishindo na ni matumaini yake ushindi utakuwa mkubwa kuliko wakati wowote.
Wakati huo huo Dk.Hussein Mwinyi ametumia nafasi hiyo kuwaomba wananchi kujiepusha na vurugu ambazo zinaweza kusababisha uvunjifu wa amani huku akifafanua tayari kuna baadhi ya watu wameanza kutoa kauli ambazo zinaonekana kuhatarisha amani ya nchi.
*Hivyo niwaombe wananchi wote tujiepushe na vurugu.Kuna wanasiasa wameanza kutoa kauli ambazo zinaashiria uvunjifu wa amani, tujiepushe na watu hao wasikuwa na nia njema na Taifa letu,"amesema Dk.Hussein Mwinyi.
Awali wakati anazungumza na wananchi waliohudhuria uzinduzi huo wa kampeni za mgombea urais wa CCM, Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Dk.Mohamed Ali Shein amesema kabla ya kutambulisha Dk.Hussein Mwinyi amesema Watanzania tunayo kila sababu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu kwani nchi yetu imepiga hatua ya maendeleo.
"Ndugu wananchi leo tunazindua kampeni yetu na mimi nimetakiwa kumtambulisha mgombea urais Zanzibar Dk.Hussein Mwinyi ambaye jina lake ni maarufu.Ni mzalendo mkubwa kwa nchi yake,ni daktari bingwa na tunaamini ataendelea kuimarisha Muungano, Umoja na mshikamano,"amesema Dk.Shein wakati anamuelezea Mgombea huyo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
UWANJA WA JAMHURI DODOM KUMEANZA KUNOGA MAPEMA...CCM WANA JAMBO LAO
Na Said Mwishehe,Michuzi TV
KUMEANZA kunoga mapema Uwanja wa Jamhuri Mjini Dodoma!Ndivyo unavyoweza kuelezea jinsi ambavyo idadi kubwa ya wananchi wakiwemo wana CCM ambavyo wamejitokeza uwanjani hapo kushuhudia uzinduzi wa kampeni za mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi Dk.John Magufuli.
Ratiba inaonyesha wananchi walianza kuingia uwanjani saa 12 asubuh. Lakini hadi saa tatu uwanja ulishaanza kufurika kuanzia majukwaa yote na katikati ya uwanja vikundi mbalimbali vilionekana wakipiga jaramba huku wengine wakiendelea kuingia uwanjani hapo.
Hali hiyo pengine haikufikiriwa kwa kuwa wasanii walipoanza kutumbuiza saa mbili asubuh tayari mashabiki wao(wananchi)walikuwa tayari kuwashangilia kinyume na matarajio pengine uwanja ungefurika nyakati za mchana.
Aidha, ni dhahiri wanaCCM pamoja na wananchi wengine wasio makada wa chama hicho hawakutaka kuwa sehemu ya wale watakaohadithiwa au kuangalia kwenye runinga na mitandao ya kijamii kile kitakachotokea Uwanja wa Jamahuri.
Michuzi TV na Michuzi Blog imeshuhudia msusuru wa umati mkubwa wa wananchi ukiendelea kuingia uwanjani hapo huku wale ambao wameshafika uwanjani wakiendelea kupata burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya,wanamuziki wa dansi, waigizaji na kila aina ya wasanii kuhakikisha kila aina ya burudani inapatikana.
Hata hivyo wakati wananchi hao wa Jiji la Dodoma pamoja na Wana CCM hao wakiendelea kupata buradani za nguvu ambazo kwa lugha ya mjini wanaita burudani Konki wapo wananchi wengine ambao wameonekana kuwa makini wakisoma majarida,vipeperushi pamoja na gazeti la Uhuru ambalo ni gazeti la Chama Cha Mapinduzi(CCM) ambayo yanaelezea maendeleo na mafanikio makubwa ambayo Serikali ya Awanu ya Tano chini ya Rais Dk.John Magufuli imeyapata katika miaka mitano ya kwanza.
Aidha, uelewa mpana wa wananchi kuhusu mambo makubwa yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk. John Magufuli kipenzi cha Watanzani imekuwa karata ya turufu kwa CCM wakati wakianza kampei zao leo jijini Dodoma ambako pia ndio makao makuu ya nchi na chama hicho.
Ukweli kazi kubwa na nzuri iliyofanywa na Serikali itamsaidia kwa kiasi kikubwa mgombea wa CCM kunadi Ilani ya Chama chao kwa urahisi na kuongeza mawili matatu bila ya kutumia nguvu nyingi kuongeza ahadi.