Friday 10 July 2020

Picha : EMMANUEL NTOBI, SALOME MAKAMBA WARUDISHA KWA KISHINDO FOMU KUGOMBEA UBUNGE SHINYANGA MJINI KUPITIA CHADEMA

Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Wanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Emmanuel Ntobi (aliyekuwa diwani wa Kata ya Ngokolo na Mwenyekiti CHADEMA mkoa wa Shinyanga) na Salome Makamba (aliyekuwa Mbunge wa Viti Maalum) wamerudisha kwa kishindo Fomu za kuomba kugombea nafasi ya ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini leo Ijumaa Julai 10,2020.

Makada hao wa CHADEMA wamewasili katika Ofisi za CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini wakisindikizwa na misafara ya wafuasi wa CHADEMA waliokuwa wanaendesha magari na pikipiki huku wakiwa wamebeba bendera za chama hicho sambamba na matarumbeta ya hapa na pale.

Mara baada ya kuwasili katika ofisi za CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini, watia nao walikabidhi fomu za kuomba ridhaa ya kuchaguliwa na chama chao kugombea ubunge jimbo la Shinyanga Mjini kisha wakapata nafasi ya kuelezea mbele ya wanachama wa CHADEMA malengo yao ya kuomba chama kiwapitishe kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.

Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala amesema zoezi la kurudisha fomu kwa wanachama wa CHADEMA waliotia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini ni leo Ijumaa Julai 10 saa 10 kamili jioni.

“Zoezi linalofanyika leo ni kupokea fomu za wanachama wetu waliojitokeza kuomba kugombea nafasi ya Ubunge katika Jimbo la Shinyanga ambapo majina ya waliojitokeza yatajadiliwa katika mkutano wa chama na atapatikana mgombea mmoja”,amesema Ndatala.

Ameyataja majina ya wanachama wa CHADEMA waliochukua fomu kugombea ubunge katika Jimbo la Shinyanga Mjini kuwa ni Emmanuel Ntobi, Samson Ng’wagi, Mchungaji Jilala Fumbuka, Nicholaus Luhende, Hassan Salim pamoja na Zainab Kheri Zena Gulam wanaowania nafasi ya Ubunge Viti Maalum.

Ndatala amesema zoezi la wanachama wa CHADEMA kurudisha fomu za kugombea ubunge jimbo la Shinyanga Mjini limeenda sambamba na kumdhamini Tundu Lissu kuwa mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CHADEMA.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mwanachama wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Emmanuel Ntobi (aliyekuwa diwani wa Kata ya Ngokolo na Mwenyekiti CHADEMA mkoa wa Shinyanga) akiwasili katika ofisi za CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini leo Ijumaa Julai 10,2020 wakati akirudisha fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea ubunge jimbo la Shinyanga Mjini. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akizungumza wakati wa kupokea fomu za wanachama wa CHADEMA waliojitokeza kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akizungumza wakati wa kupokea fomu za wanachama wa CHADEMA waliojitokeza kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Emmanuel Ntobi kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Emmanuel Ntobi kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akionesha fomu ya Emmanuel Ntobi kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Emmanuel Ntobi akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Emmanuel Ntobi akieleza sababu zilizomsukuma kuomba  chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Emmanuel Ntobi akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Emmanuel Ntobi akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Samson Ng'wagi kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Samson Ng'wagi kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Samson Ng'wagi akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Salome Makamba akiwasili katika ofisi za CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini kurudisha fomu ya  kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Salome Makamba kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Salome Makamba kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Salome Makamba akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Salome Makamba akieleza sababu zilizomsukuma kuomba chama chake kimpe ridhaa ya kugombea  Ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Katibu wa CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini Joseph Ndatala  akipokea fomu ya Zena Gulam kuwania nafasi ya Ubunge Viti Maalum Jimbo la Shinyanga Mjini.
Mtia nia kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini kupitia CHADEMA  Zena Gulam akieleza sababu zilizomsukuma kugombea  Ubunge Viti Maalum Jimbo la Shinyanga Mjini.
Awali Makada wa CHADEMA wakiendelea na shamra shamra nje ya ofisi za CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini.
Awali Makada wa CHADEMA wakiendelea na shamra shamra nje ya ofisi za CHADEMA Jimbo la Shinyanga Mjini.
Msanii Mussa Jumanne akitoa burudani wakati makada wa CHADEMA wakirudisha  fomu kuomba kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Msanii Mussa Jumanne akitoa burudani wakati makada wa CHADEMA wakirudisha  fomu kuomba kugombea ubunge Jimbo la Shinyanga Mjini.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

Tanzania, China Zaahidi Kuendeleza Ushirikiano, Kukuza Maendeleo

Tanzania na China zimeahidi kuendeleza ushirikiano wa kidiplomasia ili kuhakikisha kuwa nchi hizo zinakuwa na maendeleo endelevu.  
 
Makubaliano hayo yamefanywa na Balozi wa China nchini, Mhe. Wang Ke, wakati alipokutana kwa mazungumzo na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Wilbert Ibuge leo jijini Dar es Salaam.
 
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Jenerali Ibuge amesema kuwa wamejadili masuala mbalimbali ikiwemo suala la namna ya kutekeleza nia ya Viongozi Wakuu wa nchii za China na Tanzania (Rais wa China, Mhe. Xi Jinping pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. John Joseph Pombe Maufuli) ya kupunguza madhara yatokanayo na ugonjwa wa COVID 19 ikiwemo kufutiwa na kusamehewa madeni. 
 
Naishukuru Serikali ya China kwa uhusiano na ushirikiano ambao imekuwa ikionesha kwa Tanzania. Uhusiano huo umeendelezwa na viongozi wa pande zote mbili ambao umekuwa ukiimarika siku hadi siku na kuahidi kuwa serikali ya Tanzania itaendela kudumisha ushirikiano wake wa kidiplomasia kati yake na China.
 
Pamoja na mambo mengine, mazungumzo yalijadili masuala ya biashara na uwekezaji, mradi wa nyumba 25 za wataalum wa Afya zilizopo Osterbay jijini Dar es Salaam.
 
Kwa upande wake Balozi Wang Ke pamoja na mambo mengine, ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa jitihada ilizochukua katika kukukuza uchumi wake hadi kufikia uchumi wa kati, pamoja na mapambano dhidi ya COVID 19.
 
"Leo nimekutana na Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje, Balozi Brigedia Jenerali Ibuge na kuongea mambo mbalimbali ya ushirikiano na tunaipongeza Serikali ya Tanzania kwa jitihada  ilizochukua katika kufanya kazi kwa bidii na kukuza uchumi wake hadi kufikia uchumi wa kati, pamoja na hatua ilizochukua katika kupambana na janga la COVID 19 ambapo tumefurahishwa kuona janga la COVID 19 limeisha," Amesema Balozi Ke.
 
Balozi Ke ameongeza kuwa wamekubaliana katika maongezi hayo pia kuendeleza ushirikiano wa kufanya kazi kwa pamoja kwa manufaa ya mataifa mawili (Tanzania na China) ili kuhakikisha uhusiano na ushirikiano unazidi kukua na kuimarika.
 
 Tanzania na China zimekuwa zikishirikiana katika sekta za kilimo, biashara na uwekezaji, miradi ya mikopo nafuu na misaada, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Uchukuzi, Afya, Utalii na utamaduni.  
 
China na Tanzania zilianzisha mahusiano rasmi ya kidiplomasia mwaka 1964.


Share:

Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt Hussein Mwinyi Asisitiza Ushirikiano

Mgombea Urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt Hussein Mwinyi amesisitiza ushirikiano na mshikamano ndani ya chama hicho wakati huu wa kuelekea uchaguzi mkuu mwezi oktoba mwaka huu.

Amesema ushirikiano na mshikamano ndio utakaokiwezesha chama hicho kupata ushindi wa kishindo katika uchaguzi mkuu ujao kwa pande zote mbili za muungano.

Dkt Mwinyi ameyasema hayo jijini Dodoma mara baada ya kutangazwa mshindi kwa kupata kura 129 kati ya kura zote zilizopigwa na wajumbe wa halmashauri kuu ya CCM Taifa jijjni Dodoma.

Dkt Mwinyi amewashinda Shamsi Vuai Nahodha aliyepata kura 16 na Dkt Khalid Salim Mohamed aliyepata kura 19.


Share:

Mwanasheria Akaro-Simba Richmond Achukua Fomu Ya Kugombea Urais Kupitia CHADEMA

Mwanasheria Akaro-Simba Richmond  amechukua fomu ya kugombea Urais wa Tanzania, kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)
 

Simba amekabidhiwa fomu hiyo leo Ijumaa tarehe 10 Julai 2020 katika Makao Makuu ya Chadema, Kinondoni jijini Dar es Salaam na  Mkurugenzi wa Uchaguzi Chadema  Reginald Munisi
 
Mtia nia huyo anakuwa wa saba ndani ya Chadema kugombea Urais wa Tanzania, tangu zoezi hilo lianze tarehe 4 Julai 2020. Zoezi hilo litafungwa tarehe 19 Julai mwaka huu.


Share:

Tatizo la kuishiwa nguvu za kiume na maumbile kusinyaa limekuwa tatizo kwa wanaume wengi.

Tatizo la kuishiwa nguvu za kiume na maumbile kusinyaa limekuwa tatizo kwa wanaume wengi.
 ___________________

==>Yajuwe matatizo yanayosababisha upungufu wa nguvu za kiume
___________________

👉(1) Ngiri ya kupanda na kushuka
👉2.Korondani moja kuvimba
👉3.Tumbo kuunguruma kujaa gesi
👉4.Kisukari
👉5.Presha
👉6.Kiuno kuuma
👉7.Kutopata choo vizuri

Ipo Dawa  ya asili ya nguvu za kiume yenye kutibu matatizo kwa wakati mmoja
 ___________________
Pia tunatibu kisukari siku (14) vidonda vya tumbo siku (30), Miguu kufa ngazi, kuwaka moto . 

👉Je umeachwa? Na mke /mume,mchumba na bado unampenda ? Kunamtu unamtaka unashindwa kumwambia? 

Wasiliana na mtalam, humvuta mume, mke,mchumba na mtu yeyote  unayemtaka katika mahusiano na kumfanya atimize unachohitaji kutoka kwake na kumfunga asiwe na mtu mwingine zaidi yako hata kama yupo mbali atakutafuta mwenyewe na kutmiza ahadi zenu .
 ___________________
Wasiliana nae kwa Simu: CALL / WHATSAPP : 0747100745
 



Share:

Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM Kuwa Mgombea Wa Urais wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania

Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM  umempitisha Dkt John Magufuli  kuwa mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa ndiye mwanachama pekee aliyejitokeza kuchukua fomu.

Endelea Kuwa Nasi kwa taarifa zaidi


Share:

Breaking News: Dkt Hussein Mwinyi Apitishwa na CCM kuwa mgombea wa Urais wa Zanzibar

Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM  umempitisha Dkt Hussein Mwinyi kuwa mgombea wa Urais wa Zanzibar baada ya kupata kura 129 sawa na asilimia 78.65 akiwashinda Shamsi Vuai Nahodha  na Dk Khalid Salim Mohamed


Share:

BREAKING: CCM Wamsamehe Na Kufuta Adhabu ya Katibu mstaafu wa CCM Abdulrahman Kinana

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimemsamehe Katibu Mkuu Mstaafu wa chama hicho Abdulrahman Kinana na kumfutia adhabu ya miezi 18 aliyokuwa akiitumikia.

Tangazo hilo limetolewa jijini Dodoma na Mwenyekiti wa CCM Taifa Rais John Magufuli wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya chama hicho kinachoendelea jijini Dodoma baada ya kuomba ridhaa ya wajumbe wa kikao hicho ambao nao wameridhia Kinana asamehewe.

Rais Magufuli amesema Mzee Kinana ameonekana kujutia makosa aliyokuwa ameyatenda na kuomba msamaha, hivyo ni vema akasamehewa ili aungane na wanachama wenzake katika kukijenga chama.

Tayari Mzee Kinana ametumikia adhabu hiyo kwa muda wa miezi minne.


Share:

Waziri Lukuvi Apokea Msaada Wa Compyuta 10 Kutoka Benki Ya Azania

Na Munir Shemweta, WANMM DODOMA
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amepokea msaada wa Kompyuta 10 zenye thamani ya milioni 12 kutoka Benki ya Azania.

Msaada huo ulipokelewa leo tarehe 10 Julai 2020 katika ofisi za ardhi mkoa wa Dodoma na kushuhudiwa na viongozi mbalimbali wa Wizara akiwemo Katibu Mkuu Mary Makondo.

Akizungumza baada ya kupokea msaada huo, Waziri Lukuvi aliishukuru Benki ya Azania kwa msaada huo alioueleza kuwa utasaidia sana kwenye huduma za sekta ya ardhi hasa katika ofisi za ardhi za mikoa zilizoanzishwa hivi karibuni.

Alisema, benki ya Azania imekuwa ikiunga mkono jitihada za Wizara kusaidia vifaa na kuzitaka taasisi nyingine kuiga mfano wa Benki ya Azania katika kusaidia juhudi za serikali kusogeza huduma za ardhi karibu na wananchi.

Kwa mujibu wa Lukuvi, hivi sasa wizara yake baada ya kuanzisha ofisi za ardhi katika mikoa inafanya jitihada mbalimbali kuhakikisha ofisi hizo zinakuwa na vifaa vya kutosha kwa lengo la kuwawezesha watendaji wa ofisi hizo kufanya kazi kwa ufanisi.

Kwa upande wake Meneja wa Benki ya Azania mkoa wa Dodoma Makalla Mbura alimueleza Waziri wa Ardhi kuwa msaada uliotolewa moja ya juhudi za benki hiyo kusaidia jitihada mbalimbali zinaziofanywa na wizara ya ardhi kwenye sekta ya ardhi.

Makalla aliongeza kwa kusema kuwa, benki hiyo itaendelea kuunga mkono jitihada za wizara katika masuala mbalimbali ya huduma za sekta ya ardhi kwa kutoa msaada pale unapohitajika.


Share:

BREAKING: Majina Matatu Yaliyopitishwa na Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM Kwa Ajili ya Kugombea Urais Zanzibar

Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM  umepitisha majina matatu ya wagombea Urais wa Zanzibar, ambao ni ;

1.Dk Khalid Salim Mohamed,
2. Dkt Hussein Ali Mwinyi na 
3. Shamsi Vuai Nahodha.

Wagombea walikuwa 31, Lakini waliopitishwa Tano bora Urais Zanzibar  walikuwa ;

1.Prof. Makame Mbarawa
2.Dkt.Khalid Salum Mohamed
3.Shamsi Vuai Nahodha
4.Dkt.Hussein Mwinyi
5.Khamis Musa Omar

Mkutano bado unaendelea ambapo litapendekezwa jina moja kati ya hayo matatu. Endelea kuwa nasi


Share:

LIVE: Ufunguzi wa Kikao Cha Halmashauri Kuu ya CCM- Kujadili Mgombea Urais Zanzibar

LIVE: Ufunguzi wa Kikao Cha Halmashauri Kuu ya CCM- Ukumbi wa White House Dodoma


Share:

Wabunge Wawili CCM Wahojiwa TAKUKURU

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Dodoma, imewahoji wabunge wawili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaomaliza muda wao, Livingstone Lusinde (Mtera) na Peter Serukamba (Kigoma Kaskazini) kwa tuhuma za kuhusika kugawa rushwa kwa wajumbe ili waweze kuungwa mkono kugombea tena ubunge.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Dodoma, Sostenes Kibwengo, alithibitisha kushikiliwa na kuhojiwa wabunge hao wakihusishwa na tuhuma za rushwa kwa kushawishi wajumbe ili waweze kuwania tena ubunge katika majimbo yao.
 
Kibwengo alidai kuwa Julai 7, mwaka huu majira ya mchana, waliwakamata watu 20 ambao ni wanachama wa CCM wakiwa nyumbani kwa Lusinde eneo la Mvumi, Wilaya ya Chamwino.

Alidai uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba watu hao na wengine waliofanikiwa kutoroka walifika nyumbani kwa mbunge huyo kupatiwa fedha ili wamsaidie wakati wa vikao vya uchaguzi.

Kibwengo alithibitisha pia kushikiliwa na kuhojiwa kwa Serukamba kwa tuhuma za kutoa rushwa kwa wanachama wa CCM ili kushawishi mambo yanayohusina na uchaguzi.

Alisema Serukamba pia ni mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa na pia ni mtia nia ya ubunge katika Jimbo la Kigoma Kaskazini.


Share:

Watuhumiwa Wa Bangi mkoani Arusha Wafikishwa Mahakamani

Wakulima wawili wakazi wa Mwandeti jijini Arusha, wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka ya kujihusisha na biashara ya dawa za kulevya aina ya bangi yenye uzito wa zaidi ya kilo 1,200.

Washtakiwa hao Seuli Mollel na Losieku Mollel, walifikishwa jana mahakamani hapo na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya.

Katika hati ya mashtaka iliyosomwa mahakamani hapo na wakili wa Serikali mbele ya Hakimu Mkazi, Gwantwa Mwankuga alidai watuhumiwa hao wanashtakiwa chini ya kifungu cha sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya sura ya 95 ya sheria za Tanzania.

Inadaiwa kuwa, Juni 2020 katika Kijiji cha Longilong wilayani Arumeru mkoani Arusha, mshtakiwa Seuli alikutwa na kilo 649.5 za dawa ya kulevya aina ya bangi huku mshtakiwa Losieku akikutwa na kilo 728.9 za dawa hizo za kulevya.

Washtakiwa hawakuruhusiwa kujibu chochote kwa kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka kisheria kusikiliza kesi za uhujumu uchumi ambazo husikilizwa Mahakama Kuu au mahakama za chini kwa kupatiwa kibali kutoka kwa DPP.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Julai 22, 2020 itakapokuja kwa ajili ya kutajwa, watuhumiwa wamerudishwa rumande.


Share:

Majina Matatu Ya Wagombea Urais Zanzibar Kujadiliwa Leo

Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi jana ilikutana jijini Dodoma na kufanyia kazi taarifa ya Kamati Kuu Maalum ya Visiwani Zanzibar, kupokea taarifa kutoka Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM na taarifa ya Kamati ya Usalama wa Maadili ya CCM Taifa kuhusiana na makada wa Chama hicho wanaoomba kusimamishwa kuwania Urais Zanzibar.

Kamati Kuu imependekeza majina matatu ya wagombea wa urais Zanzibar kwa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC).

Hata hivyo, majina hayo yatawekwa wazi leo Julai 10,2020 katika kikao cha NEC kwa wajumbe kwa ajili ya kupiga kura kumchagua mwanachama mmoja kwa nafasi hiyo.

Akitoa taarifa kuhusu kikao hicho leo, Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Humphrey Polepole, alisema mapendekezo hayatakuwa wazi na kuwataka watu waendelee kuwa wanyenyekevu na watulivu.

“Ukifanya mchezo tu kesho(leo) tunafanya utaratibu mwingine, kwa hiyo kesho(leo) kwenye NEC tutawaambia wajumbe ni wakina nani kamati kuu imewapeleka NEC… wana CCM tuendelee kuwa watulivu,”alisema.

Aidha, Polepole alisema pamoja na mambo mengine kikao hicho kimetoa pongezi kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Zanzibar kwa kuimarisha uchumi wa Taifa licha ya kupitia katika kipindi kigumu cha ugonjwa wa corona.


Share:

Waziri Jafo amuondoa Meneja wa TARURA Arusha kutokana na kutokutoa taarifa za miradi ya maendeleo Inayofanywa na Serikali

Na.Angela Msimbira ARUSHA
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Mhe. Selemani Jafo amemuagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara za Vijijini  na Mijini Mhandisi Victor Seif kumuhamisha mara moja aliyekuwa Meneja wa Tarura Jiji la Arusha  na kumpangia kazi nyingine  ya kiwango cha chini

Ametoa maagizo hayo jana wakati alipokuwa kwenye ziara ya kikazi ya kukagua Miradi ya maendeleo  inayotekelezwa katika Halmashauri ya Jiji la Arusha, Mkoani Arusha

Mhe. Jafo alisema ameamua kumuhamisha Mtumishi huyo kutokana na kutokutoa taarifa  za miradi ya maendeleo yanayofanywa na Serikali , jambo ambalo linasabisha  Serikali ionekane inashindwa kutimiza  majukumu yake ya kuleta maendeleo kwa wananchi

Amewaagiza watendaji  wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha  wanasimamia miradi ya maendeleo na kutoa  taarifa kuhusu utekelezaji wa miradi ya maendeleo ili wananchi waweze kuijua na kutambua kuwa miradi hiyo imefanywa na Serikali

“Watendaji  wote nchini  mnawajibu wa kuhakikisha mnasimamia miradi ya Maendeleo kwa weledi mkubwa ili iweze kukamilika kwa wakati na kuitangaza kwa wananchi ili iweze kuijua, kuitunza na kuithamini miradi hiyo.” Amesisitiza Mhe. Jafo

Aidha Mhe. Jafo  amewaagiza watendaji wote nchini ambao wamepewa dhamana ya kuwahudumia wananchi watimize majukumu yao kikamilifu ili kutatua kero za wananchi kwa wakati na kuleta maendeleo kwa jamii.


Share:

Mfanyakazi Wa Ndani Auawa Baada ya Kuwaua Kwa Mapanga Watoto Wawili wa Bosi Wake

NA MWAMVUA MWINYI, PWANI
MFANYAKAZI wa kazi za ndani mwanaume,Yasin Abdala (35), Kitongoji cha Kivungwi Kwazoka ,Kata ya Vigwaza Chalinze,Bagamoyo mkoani Pwani ameuwawa na wananchi wenye hasira kali baada kuwauwa watoto wawili wa bosi wake ,kwa kuwakatakata mapanga. 
 
Aidha marehemu pia amemjeruhi mama wa watoto hao Sada Salehe (28) kwa kumshambulia sehemu mbalimbali za mwili na kukimbizwa kituo cha afya Mlandizi kwa matibabu zaidi
 
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kamanda wa polisi mkoani Pwani Wankyo Nyigesa alieleza ,tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Julai 9  nyumbani kwa Wema Senzie.
 
Alisema, mtuhumiwa ameuwawa na wananchi waliokwenda kumkamata baada ya kukimbia alipokuwa amehifadhiwa kwenye ofisi ya Kijiji.
 
Wankyo ,aliwataja Watoto hao aliowaua ni Abubakary Makolo (6) mwanafunzi wa darasa la kwanza shule ya msingi Kwazoka na mdogo wake Rehema Makolo (5) mwanafunzi wa shule ya awali Kwazoka.
 
“Mtuhumiwa baada ya kukamatwa alihifadhiwa ofisini hapo kwa ajili ya kupelekwa kwenye vyombo vya sheria lakini alivunja mlango na kukimbia na walipomkamata walimshambulia kwa silaha za jadi na kusababisha kifo chake,” alisema Wankyo.
 
Wankyo alibainisha, chanzo cha mauaji hayo kinachunguzwa na polisi ila awali kabla ya tukio hilo mtuhumiwa alikuwa na ugomvi na mama wa watoto hao.
 
Miili ya marehemu imehifadhiwa  kwenye kituo cha afya Mlandizi ,kusubiri taratibu za mazishi.


Share:

Rais Magufuli Afanya Uteuzi Wa Wakili Mkuu wa Serikali na Naibu Wakili Mkuu wa Serikali.

Rais Magufuli amemteua Gabriel Malata kuwa Wakili Mkuu wa Serikali akichukua nafasi ya Julius Mashamba.


Kabla ya uteuzi Malata alikuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali.

Aidha, Rais Magufuli amemteua  Boniface Luhende kuwa Naibu Wakili Mkuu wa Serikali akichukua nafasi ya Malata.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger