Sunday 7 June 2020

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 7,2020






Share:

Saturday 6 June 2020

Ngoma Mpyaaa!!! NYANDA MADIRISHA OBHADO 'MALIGANYA' - STAREHE

Nakualika kutazama Video ya wimbo mpya wa Nyanda Madirisha Obhado ' Maliganya' (Shikomba Bhulolo) kutoka Kahama Mkoani Shinyanga inaitwa Starehe...Ngoma hii imetengenezwa katika Studio za Hardtone.
Tazama video hapa chini
Share:

Jobs at Bunda Municipal council- Public service recruitment secretariat (PSRS)

Jobs at Bunda Municipal council- Public service recruitment secretariat (PSRS)  

The post Jobs at Bunda Municipal council- Public service recruitment secretariat (PSRS) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Government Jobs at Geita- Public service recruitment secretariat (PSRS)

Jobs at Geita- Public service recruitment secretariat (PSRS)  

The post Government Jobs at Geita- Public service recruitment secretariat (PSRS) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Picha : BONANZA LA MICHEZO LA MAVETERANI KANDA YA ZIWA LAUNGURUMA UWANJA MPYA WA 'FRESHO COMPLEX' SHINYANGA


Maveterani kutoka Mikoa ya Mwanza (Mwanza Starehe Veterani), Tabora (Unyanyembe Veterani) na Shinyanga (Ammo Veterani /Jeshi Veterani na Shinyanga Veterani) wamekutana katika Bonanza la Michezo lililoandaliwa na Kampuni ya Fresho Investment Company Limited kwa ajili ya kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali kuhamasisha wananchi wafanye mazoezi ili kujenga afya zao pamoja na kushuhudia uwanja mpya wa Fresho Complex.

Bonanza hilo limefanyika leo Jumamosi Juni 6,2020 katika Uwanja Mpya wa Kisasa uliopewa jina la ‘Fresho Complex’ unaojengwa na Kampuni ya Fresho Investment Company Ltd katika eneo la Ugweto kata ya Ibadakuli katika Manispaa ya Shinyanga ambapo mgeni rasmi alikuwa Kamanda wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kanda ya Shinyanga, Kanali Justas Kitta.

Akifungua Bonanza hilo katika uwanja huo ulioanza kutumika leo, Kanali Kitta ambaye ni miongoni mwa Wachezaji wa Timu ya Jeshi Veterani alimpongeza Fredy Shoo kuwekeza katika sekta ya Michezo kwa kujenga uwanja wa Mpira wa miguu 

“Mimi nikiwa Mwanamichezo,Mkuu wa taasisi ya serikali, nikupongeze sana ndugu yangu Fresho kwa kazi kubwa uliyoifanya. Hii umejenga ni hospitali, itatibu magonjwa mengi badala ya mtu kwenda hospitali kupata dawa atapata hapa. Magonjwa nyemelezi tutayaondoa kwenye kiwanja hiki”,amesema Kanali Kitta.

“Michezo ni afya na michezo inaleta ushirikiano ndiyo maana tumefika hapa kama watu tunaothamini michezo. Ukifanya michezo ni tiba ya magonjwa mengi hasa ukizingatia kuwa sasa tupo katika Mapambano dhidi ya ugonjwa wa Corona kama Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli alivyosema kuwa Michezo ni tiba mbadala katika magonjwa mbalimbali na hata hili gonjwa la Corona”,ameeleza Kanali Kitta.

“Tukipata watu watatu wanne kwa Shinyanga hii nafikiri Kimichezo tutapiga hatua kubwa sana.Kwa hiyo nikutie moyo ndugu yangu endelea,na ningependa katika mkoa wetu tuwe na mabonanza kama haya kila mwezi tuhamasishe watu wapende michezo ili kuondokana na magonjwa mbalimbali kwani michezo ni afya”,ameongeza.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kampuni ya Fresho Investment Company (1999) Ltd, Fredy Shoo amesema lengo la kufanya Bonanza hilo la michezo ni kuendelea kuiunga mkono serikali ya Rais John Pombe Magufuli katika juhudi zake za kutaka Watanzania wawe na afya nzuri na kuweza kupiga vita ugonjwa wa Corona ambapo watu wanaofanya mazoezi wana uwezakano mkubwa wa kushambuliwa na Virusi vya Corona.

Aidha Shoo amesema lengo la kujenga uwanja wa michezo wa ‘Fresho Complex’ ni kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Magufuli katika kufanya watu wakiwemo ,wafanyakazi wa viwandani na serikalini wawe na afya nzuri kwa kufanya mazoezi.

“Tumeanza kujenga uwanja huu mwaka 2017 baada ya ziara ya Rais Magufuli mkoani Shinyanga, tulihamasika kuwa, pamoja na kwamba tunaendelea kujenga viwanda vingine,tumeona tujenge kiwanda cha afya ili kuunga mkono serikali. Pamoja na kwamba ninawekeza katika viwanda nimeona pia niwekeze katika uwanja wa michezo”,amesema Shoo.

“Kingine kilichonisukuma pia kuwekeza katika ujenzi wa uwanja ni kutokana na kwamba mimi ni mchezaji wa Veterani. Wengi wakisikia Veterani wanadhani ni wale wachezaji ambao walikuwa wanacheza katika timu kubwa wakawa wamestaafu. Mimi sikuwahi kucheza Klabu yeyote ya mashindano ya Ligi lakini najiita Veterani kwa sababu ni mchezaji ninayecheza mwenye umri mkubwa”,ameongeza Shoo.

“Niliona tukiwa na uwanja huu Watu wenye umri mkubwa katika eneo hili tutakuwa tunafanya mazoezi katika uwanja huu. Na kutokana na agizo la Mheshimiwa Rais kuwa wananchi wafanye mazoezi siku za Jumamosi,hivyo siku za Jumamosi uwanja huu tutautoa bure ili wananchi wafanye mazoezi hapa”,amesema.

Mkurugenzi huyo amesema pamoja na kwamba uwanja huo utakuwa wa kibiashara lakini siku za Jumamosi atatoa bure kwa siku ambazo serikali imesema ni za mazoezi ili kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano kuhamasisha mazoezi kwa wananchi.

Shoo amesema uwanja huo bado haujazinduliwa rasmi kwa sababu unaendelea kujengwa na bado haujapewa jina rasmi lakini kwa sasa unatambulika kama Fresho Complex ambapo michezo mbalimbali itafanyika humo.

Meneja wa Uwanja wa Fresho Complex, Ombeni Kweka
ambaye ndiye aliyebuni ramani ya uwanja huo amesema umekamilika kwa asilimia 25 na unatarajiwa kukamilika kwa asilimia 100 kati ya mwaka 2022 na 2023 ukijumuisha bustani ya matunda, barabara ya kiwango cha lami, hoteli ya nyota tano, ukumbi wenye uwezo wa kuchukua watu 1,000, eneo la kuogelea (Swimming pool) kwa ajili ya watoto na watu wazima.

“Uwanja wetu ni bora na wa kisasa,una mandhari nzuri, hakuna wa mfano kwa Kanda ya Ziwa, katika eneo la kuchezea (pitch) kuna mfumo wa mabomba yanayomwagilia maji kutoka chini na mfano hii tunaiona Ulaya, lakini pia Ujenzi wa majukwaa ukikamilika utakuwa na uwezo wa kubeba watazamaji 18,000 waliokaa na wengine kama 2,000 watakaosimama.

“Tumeanza kuujenga mwaka 2017 upana wake kwa eneo la kuchezea ni 68 kwa 110, sehemu zingine ambazo hazijakamilika ni eneo la kukimbilia (run away), bwawa la samaki, gym na vyumba vya kubadilishia nguo,” amesema.

Katika Bonanza la Maveterani wa timu ya Ammo Veterani/Jeshi Veterani, Mwanza Starehe Veterani,Unyanyembe Veterani na Shinyanga Veterani zilishuhudiwa mechi 12 ambapo kila timu ilicheza michezo mitatu.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Fresho Investment Company (1999) Ltd, Fredy Shoo akichezea timu yake ya Shinyanga Veterani akiwa amevaa jezi namba 8 ameonesha makali yake baada ya kupachika bao moja katika ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mwanza Veterani.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kamanda wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kanda ya Shinyanga, Kanali Justas Kitta akifungua Bonanza la Michezo lilokutanisha pamoja Maveterani kutoka Mikoa ya Mwanza (Mwanza Starehe), Tabora (Unyanyembe Veterani) na Shinyanga (Ammo Veterani /Jeshi Veterani na Shinyanga Veterani) katika Uwanja Mpya wa Kisasa uliopewa jina la ‘Fresho Complex’ unaojengwa na Kampuni ya Fresho Investment Company Ltd katika eneo la Ugweto kata ya Ibadakuli katika Manispaa ya Shinyanga leo Jumamosi Juni 6,2020 . Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kamanda wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kanda ya Shinyanga, Kanali Justas Kitta akiipongeza Kampuni ya Fresho Investment Company Ltd kujenga Uwanja wa Michezo katika eneo la Ugweto kata ya Ibadakuli katika Manispaa ya Shinyanga.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Fresho Investment Company (1999) Ltd, Fredy Shoo akielezea lengo la kufanya Bonanza hilo la michezo kwa kukutanisha Timu za Maveterani ambapo amesema ni kuendelea kuiunga mkono serikali ya Rais John Pombe Magufuli katika juhudi zake za kutaka Watanzania wawe na afya nzuri na kuweza kupiga vita ugonjwa wa Corona ambapo watu wanaofanya mazoezi wana uwezakano mkubwa wa kushambuliwa na Virusi vya Corona.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Fresho Investment Company (1999) Ltd, Fredy Shoo akielezea lengo la kujenga uwanja wa michezo wa ‘Fresho Complex’ ambapo alisema ni kuunga mkono juhudi za Serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Magufuli katika kufanya watu wakiwemo ,wafanyakazi wa viwandani na serikalini wawe na afya nzuri kwa kufanya mazoezi.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Fresho Investment Company (1999) Ltd, Fredy Shoo akiwakaribisha wakazi wa Shinyanga na maeneo mengine kuutumia uwanjwa wa Fresho Complex . Amesema "Pamoja na kwamba uwanja huo utakuwa wa kibiashara lakini siku za Jumamosi atatoa bure kwa siku ambazo serikali imesema ni za mazoezi ili kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano kuhamasisha mazoezi kwa wananchi".
Meneja wa Uwanja wa Fresho Complex, Ombeni Kweka akielezea kuhusu Uwanja wa Fresho Complex. Amesema ujenzi wa uwanja huo wa kisasa,wenye mandhari nzuri,unatarajiwa kukamilika mwaka 2023 ukiwa una uwezo wa kubeba watazamaji zaidi ya 20,000.
Muonekano wa uwanja wa Fresho Complex wakati wa Bonanza la michezo lililokutanisha Maveterani kutoka Kanda ya Ziwa (Tabora, Shinyanga na Mwanza).
Muonekano wa uwanja wa Fresho Complex wakati wa Bonanza la michezo lililokutanisha Maveterani kutoka Kanda ya Ziwa (Tabora, Shinyanga na Mwanza).
Mechi ya Kwanza : Mchezo kati ya Unyanyembe Veterani kutoka Tabora na Jeshi Veterani (wenye jezi nyeupe) ukiendelea ambapo walitoka kwa kufungana bao 3-3.
Mchezo kati ya Unyanyembe Veterani kutoka Tabora na Jeshi Veterani (wenye jezi nyeupe) ukiendelea
Mchezo kati ya Unyanyembe Veterani kutoka Tabora na Jeshi Veterani (wenye jezi nyeupe) ukiendelea.
Dawati la ufundi timu ya Jeshi Veterani

Wachezaji timu ya Mwanza Starehe Veterani (wenye jezi za njano na kijani) na wachezaji wa Shinyanga Veterani wakijiandaa kuanza mechi ya awamu ya kwanza.
Wachezaji timu ya Mwanza Starehe Veterani (wenye jezi za njano na kijani) na wachezaji wa Shinyanga Veterani wakisalimiana kabla ya mechi ya kwanza kuanza.
Wachezaji timu ya Mwanza Starehe Veterani  wakiwa katika picha ya pamoja.
Wachezaji wa Shinyanga Veterani wakiwa katika picha ya pamoja. Wa pili kulia waliosimama ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Fresho Investment Company (1999) Ltd, Fredy Shoo.
Mchezo kati ya Mwanza Starehe Veterani (wenye jezi za njano na kijani) na Shinyanga Veterani ukiendelea katika Uwanja wa Fresho Complex ambapo Shinyanga Veterani iliibuka mshindi kwa kuichapa Mwanza Starehe Veterani magoli 3-2.
Kulia ni Mchezaji wa Timu ya Shinyanga Veterani, Mkurugenzi wa Kampuni ya Fresho Investment Company (1999) Ltd, Fredy Shoo akiwa amevaa jezi namba 8. Katika mchezo huo alifanikiwa kupachika bao 1 na kuifanya Shinyanga Veterani ipate ushindi wa magoli 3-2.
Mchezo kati ya Mwanza Starehe Veterani (wenye jezi za njano na kijani) na Shinyanga Veterani ukiendelea katika Uwanja wa Fresho Complex ambapo Shinyanga Veterani iliibuka mshindi kwa kuichapa Mwanza Starehe Veterani magoli 3-2.
Mchezo kati ya Mwanza Starehe Veterani (wenye jezi za njano na kijani) na Shinyanga Veterani ukiendelea katika Uwanja wa Fresho Complex ambapo Shinyanga Veterani iliibuka mshindi kwa kuichapa Mwanza Starehe Veterani magoli 3-2.
Hatari katika lango Shinyanga Veterani...Mchezaji wa Mwanza Starehe Veterani akiipatia goli timu yake kwa njia ya penalti.
Dawati la ufundi Timu ya Shinyanga Veterani
Dawati la ufundi Timu ya Mwanza Starehe Veterani.
Mashabiki wakiwa uwanjani wakifuatilia mechi.
Waandishi wa habari na Afisa kutoka Kampuni ya Fresho wakifuatilia mechi uwanjani
Mashabiki wakiwa uwanjani.
Mashabiki wakishuhudiwa kabumbu uwanjani
Mashabiki wakishuhudiwa kabumbu uwanjani
Mashabiki wakishuhudiwa kabumbu uwanjani
Mashabiki wakishuhudiwa kabumbu uwanjani
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

Shule Zote Na Vyuo Vikuu Nchini Kenya Kuendelea Kufungwa Hadi Mwezi Wa Tisa Kwa Madai Ya Kukabiliana na Corona

Rais Uhuru Kenyatta ametangaza kuendelea kufungwa kwa  shule na vyuo vikuu nchini Kenya hadi Septemba Mosi mwaka huu ambapo vitafunguliwa tena.

Akilihutubia taifa kutoka ikulu ya rais jijini Nairobi rais Kenyatta anasema kuwa amechukua hatua hiyo ili kulinda maisha ya wanafunzi na  walimu haswa kutokana na idadi kubwa ya maambukizi aya COVID 19 yanayoendelea kupanda.

Rais Uhuru kenyatta aidha ametangaza kuongezwa kwa muda wa marufuku ya kutoka nje kwa mwezi mmoja zaidi amri iliyotangazwa na serikali kudhibiti maambukizi ya Corona ila muda wa utekelezwaji wake ukibadilishwa na kuanza saa tatu usiku hadi saa kumi alfajiri.


Share:

Fisi Watajwa kuhararisha Maisha Ya Wanawake Wanaokwenda Kuchota Maji

SALVATORY NTANDU
Ukosefu wa huduma ya Maji safi na Salama kwa Wakazi kata ya Ngogwa katika Halmashauri ya Mji wa Kahama mkoani Shinyanga umetajwa kuhatarisha Maisha ya  wanawake  kutokana na baadhi yao kujeruhiwa na wanyama aina ya fisi pindi wanapokwenda kuchota maji kwenye visima vilivyopo umbali wa kilomita 6 nyakati za alfajiri.

Kauli hiyo imetolewa June 5 Mwaka huu na Diwani wa Kata ya Ngogwa,Kamuli Mayunga wakati akizungumza na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kahama iliyotembelea Mradi wa Maji Safu wa Ngogwa-Kitwana unaojengwa na Mamlaka za Maji, SHUWASA, KUWASA na RUWASA.

Alisema kuwa Kumekuwa na Matukio mengi ya wanawake kushambuliwa na wanyama hao ambao wanapatikana kwa wingi katika eneo hilo kutokana na kuwepo kwa milima mingi na kusema kuwa kukamilika kwa mradi huo utaweza kutokomeza matukio hayo sambamba na magonjwa ya homa za matumbo.

“Tunashukuru ujio wa Mradi huu miaka miwili iliyopita tulipoteza wanawake wawili kwa kushambuliwa na fisi hadi kufariki dunia wakati wakienda kuchota Maji nyakati za alfajiri,Tunaipongeza serikali kwa kusikiliza kero hii ya kumtua mama ndoo kichwani,”alisema Kamuli.

Celina Paulo ni Mkazi wa kijiji cha Nyamela alisema kuwa fisi wamekuwa kikwazo kwao pindi wanapokwenda kuchota Maji asubuhi na kuiomba Serikali kuhakikisha wanakamilisha Mradi huo kwa wakati ili kuwaondolea adha hiyo ili kundelea na shughuli zingine za uzalishaji Mali.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Shinyanga (SHUWASA) Flaviana Kifizi alisema Mradi huo umekamilika kwa asilimia 95 na utagharimu shilingi bilioni 2.4 na utakamilika mwezi Agosti Mwaka huu na unatarajia kunufaisha zaidi ya wakazi 1000 wanaoishi pembezoni mwa Halmashauri hiyo.

“Ujenzi wa Matanki Mawili ya Ngogwa na Kitwana umekamilika na kwa sasa tunatarajia kuanza kulaza mabombo ili kuruhusu maji kuanza kutumiwa na wananchi,pia tutajenga vituo 13 vya kuchotea maji ambayo yatawawezesha wananchi kupata huduma za maji safi na salama ambayo itakuwa suluhisho la wao kutembea umbali Mrefu kutafuta huduma hiyo,”alisema Kifizi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa wilaya ya Kahama,ambaye ndio Mkuu wa wilaya hiyo Anamringi Macha alisema kuwa serikali ya awamu ya Tano Chini ya Dk John Pombe Magufuli imedhamiria kitatua kero zote za wananchi hususani ya Maji kwa kuhakikisha wanapata maji safi na salama.

“Katika mradi huu niwaombe wananchi msiweke vikwazo pindi watakapoanza kuchimba mitaro ya kupitisha Mabomba kwani hakuna mtu atakayelipwa fidia,tutoe ushirikiano ili kufanikisha mradi huu kwa wakati na tuendelee na shughuli za uzalishaji maji kupita huduma ya maji,”alisema Macha.

MWISHO.


Share:

Maonesho Ya 44 Kimataifa Ya Biashara Ya Dar Es Salaam (44th DITF) Kuanzia Tarehe 1 – 13 Julai, 2020 Katika Uwanja Wa Maonesho Wa Mwl. J.K. Nyerere

Wizara ya Viwanda na Biashara kupitia Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) inapenda kuwataarifu Taasisi za Umma, Sekta Binafsi, Jumuiya za Wafanyabiashara na Wananchi wote kwa ujumla kuwa inaendelea na maandalizi ya Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam yanayotarajiwa kuanza tarehe 1 hadi 13 Julai, 2020 katika Uwanja wa Maonesho wa Mwl. J. K. Nyerere, Barabara ya Kilwa, Dar es Salaam. 

Lengo la Maonesho haya ni kutoa fursa ya kutafuta masoko ya mazao na bidhaa za kilimo, viwanda na huduma nchini. Kauli Mbiu ya Maonesho ya 44 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (DITF) ni “Uchumi wa Viwanda kwa Ajira na Biashara Endelevu” ikilenga kutambua mchango wa Sekta ya Kilimo na Viwanda katika kuzalisha ajira na kujenga biashara endelevu.
 
Uratibu wa Maonesho unazingatia kanuni za Afya kwa lengo la kuhakikisha kuwa Uwanja wa Maonesho unakuwa salama kwa Waoneshaji na Watembeleaji kwa kuchukua hatua zote stahiki za kujikinga na maambukizi ya COVID-19.
 
Ili kuendana na hali halisi na kufikia wigo mkubwa zaidi wa Wazalishaji na Wanunuzi, Mikutano yote ya ana kwa ana ya Wafanyabiashara (B2B) itaandaliwa na kuratibiwa kwa njia ya mtandao. Lengo la Mikutano hii ni kuimarisha upatikanaji wa masoko endelevu ya bidhaa na huduma. 

Aidha, ili kurahisisha utembeleaji wa Maonesho, watembeleaji watapata fursa ya kununua tiketi kupitia simu za mikononi. Vilevile, Watembeleaji kutoka ndani na nje ya nchi watapata fursa ya kutembelea Maonesho kupitia mtandao (Live streaming and virtual exhibition). Kutakuwa pia Banda Maalumu litakalo tangaza bidhaa za kilimo yakiwemo mazao ya kimkakati.
 
Wizara ya Viwanda na Biashara inatoa wito kwa Wafanyabiashara, Wamiliki wa Viwanda vyote nchini, Wakulima, Taasisi za Umma, Halmashauri za Wilaya na Taasisi Binafsi kushiriki katika Maonesho haya ili kuongeza wigo wa masoko ya bidhaa za kilimo, viwanda, mifugo, uvuvi na madini zinazozalishwa nchini na kuhamasisha Wananchi kupenda bidhaa zinazozalishwa hapa nchini.
 
Imetolewa na;
Innocent L. Bashungwa (Mb.)
WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA


Share:

RC Gaguti Atoa Siku 7 Kurejeshwa Kwa Shilingi Milioni 224.

Na Allawi Kaboyo.
Mkuu wa Mkoa Kagera Brigedia Generali Marco Gaguti ametoa siku 7 kwa watumishi wa halmashauri ya wilaya Biharamulo waliokusanya fedha na kushindwa kuzipeleka Banki wawe wamezipeleka kabla hatua kali za kinidhamu hazijachukuliwa dhidi yao.

Gaguti ametoa agizo hilo wakati wakikao cha baraza la madiwani wa halmashauri hiyo lililolenga kujibu hoja za mthibiti mkuu wa hesabu za serikali CAG ambazo miongoni mwazo ni makusanyo ya fedha Zaidi ya shilingi milioni 224 ambazo hazikupelekwa bank.

Amesema kuwa licha ya halmashauri hiyo kufanya vizuri na kupata hati safi bado suala la ukusanyaji wa mapato ni changamoto ambapo ameongeza kuwa wapo watendaji ambao wanakusanya fedha lakini hawazipeleki Banki na kupelekea halmashauri kuendelea kuandamwa na mzimu wa kutofikia malengo ya ukusanyaji wa mapato ya ndani.

“CAG ametoa hoja mbalimbali kuhusu halmashauri hii na nyingi zinalalia masuala ya fedha, natoa siku saba kwa watendaji ambao wamehusika na kutopelekwa fedha hizi wawe wamezirejesha mara moja na kwenye hili sitanii kabisa tutakuja kuonana wabaya kwenye fedha za umma.” Amesema Gaguti.

Aidha amemuomba mwenyekiti wa halmashauri hiyo kuitisha kikao kingine maalumu ambacho kitakuwa na agenda za kuangalia mwenendo mzima wa watumishi ndani ya halmashauri hiyo ili hatua husika ziweze kuchukuliwa pale itakapostahili.

“Mwenyekiti nataka kabla ya baraza hili kumaliza muda wake niitiwe kikao kingine mahususi kwaajili ya madiwani pamoja na watumishi wote ili kuweza kuchukua hatua nyingine za kinidhamu kwa watumishi ambao wameonyesha vitendo vya ubadhilifu wa fedha za umma lakini na mienendo mibaya.” Alisisitiza Mkuu wa mkoa.

Kwaupande wao madiwani wakichangia kwa nyakati tofauti kwenye hoja za hizo za CAG wameitaka halmashauri kumalizia miradi mbalimbali ambayo wananchi tayari wameshaweka nguvu zao hasa vumba vya madarasa ili kusaidia watoto kusomea katika mazingira ambayo ni mazuri na salama kwaajili ya maisha yao ya baadae.

Madiwani hao wamesama kuwa halmashauri hiyo inatatizo la uhaba wa watendaji Zaidi ya 30 wa vijiji suala linalopelekea ukusanyaji wa mapato kuwa hafifu kwakuwa wanaopewa jukumu la kukusanya wengi wao hawana elimu juu ya mashine za pos zinazotumika kukusanyia mapato na kufanya kuwa changamoto ya kudumu.

Halmashauri ya wilaya Biharamulo ni miongoni mwa halmashauri 8 zinazouunda mkoa wa Kagera ambayo kwa kipindi cha miaka minne mfurulizo imepata hati safi licha ya kuwa na changamoto ya kufikia lengo la ukusanyaji wa mapato ya ndani hali ambayo mkuu wa mkoa ameagiza ishugulikiwae mara moja.


Share:

Nchi Za Nordic Zaahidi Kuendeleza, Kuimarisha Uhusiano Wake Na Tanzania

Nchi za NORDIC ambazo ni Norway, Sweden, Finland na Dernmark zimeahidi kuendelea kushirikiana na Tanzania na kuhakikisha kuwa Tanzania inasonga mbele katika maendeleo yake kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Akiongea wakati wa maadhimisho ya wiki ya Nordic jijini Dar es Salaam, Balozi wa Norway nchini, Mhe. Elisabeth Jacobsen amesema kuwa nchi za Nordic zimeadhimisha wiki ya Nordic nchini Tanzania na zimejadili masuala ya malengo ya maendeleo endelevu ambapo pamoja na mambo mengine, wametumia wiki ya Nordic kuendeleza uhusiano na ushirikiano mkubwa uliopo kati ya Nordic na Tanzania.

"Wiki ya Nordic inatoa fursa ya kushirikiana na kujifunza mambo mbalimbali yakiwemo ya kijamii, kisiasa na kichumi pamoja na kupata uzoefu wa maendeleo kutoka kwa kila mmoja wetu," Amesema Balozi Jacobsen.

Ameongeza kuwa, nchi za Nordic zimejidhatiti kufanya kazi kwa karibu na Tanzania ili kuhakikisha kuwa Tanzania inasonga mbele katika maendeleo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) akiongea mara baada ya kukabidiwa mpira ulioandikwa malengo 17 ya maendeleo endelevu ikiwa ni ishara ya kuhamasisha maendeleo ya Tanzania, Balozi wa Norway nchini amesema kuwa mpira huo ni ishara ya ushirikiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na nchi za Nordic.

"Ushirikiano wetu (Tanzania) na nchi za Nordic ni wa muda mrefu kabla ya uhuru na hata baada ya uhuru. Tumekuwa tukifurahia ushirikiano wetu na nchi za Nordic na umekuwa ukimarika kila wakati, ni matumaini yetu sisi kama serikali kuwa uhusiano utaendelea kuimarika zaidi," amesema Dkt. Ndumbaro    

Mwezi Novemba 2019, ulifanyika Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa Afrika na Nordic, ambapo pamoja na mambo mengine, mkutano huo uzikutanisha nchi za Afrika na Nordic na kutoa fursa ya kujadili masuala mbalimbali yakiwemo, elimu, kilimo biashara na uwekezaji.


Share:

Aliyekuwa bosi wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD) ashtakiwa kwa Makosa Matano Likiwemo la Kutakatisha Fedha

Waliokuwa vigogo wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD) nchini Tanzania jana wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam na kusomewa mashtaka matano yanayowakabili katika Namba 46 ya mwaka 2020.

Watuhumiwa hao waliofikishwa mahamani na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ni aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya Dawa (MSD) Laurien Bwanakunu na aliyekuwa Mkurugenzi wa Lojistiki wa MSD, Byekwaso Tabura.

 
Wakili wa Serikali, Faraji Nguka akiwasomea mashtaka washtakiwa hao, alidai kuwa kati ya Juai 1, 2016 na Juni 30, 2019 maeneo mbalimbali ya jiji na mkoa wa Dar es Salaam, wakiwa watumishi wa umma, kwa pamoja walitengeneza genge la uhalifu kwa ajili ya kujipatia faida.

Katika shtaka la pili inadaiwa kuwa kati ya Julai 1, 2016 na Juni 20, 2019, washtakiwa wote kwa pamoja waliisababishia MSD hasara ya Sh 3,816,727,112.75.

Shtaka la tatu ambalo linamkabili Bwanakunu ni matumizi mabaya ya madaraka, ambapo inadaiwa kuwa kati ya Julai 1, 2916 na June 30, 2019 katika maeneo ya Keko wilaya ya Temeke mkoa wa Dar es Salaam, kwa makusudi alitumia nafasi yake kulipa kiasi cha Sh 3,816,727,112.75 kwa wafanyakazi wa MSD kama nyongeza ya mishahara na posho, bila ruhusa ya Katibu Mkuu Utumishi, na hivyo kuisababishia mamlaka hiyo hasara ya kiasi hicho cha fedha.

Katika shtaka la nne, washtakiwa wote wanadaiwa kati ya Julai 1, 2016 na Juni 30, 2019 katika maeneo ya tofauti ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa pamoja waliruhusu uhifadhi mbaya wa vifaa tiba, uliosababisha vifaa hivyo kuharibika, hivyo kuisababishia MSD hasara ya Sh 85,199,879.65 

Shtaka la tano linalowakabili washtakiwa hao ni utakatishaji fedha, ambapo inadaiwa kati ya Julai 1, 2016 na Juni 30, 2019 katika maeneo ya Keko Wilaya ya Temeke Mkoa wa Dar es Salaam, wote kwa pamoja walijipatia Sh 1,603,991,095.37 wakijua fedha hizo ni zao la uhalifu, ambao ni kuongoza genge la uhalifu.

 Washtakiwa hao hawakurusiwa kujibu chochote, kwa sababu mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo. Hakimu Kabate aliahirisha kesi hiyo hadi Juni 18, 2020.


Share:

Marekani na Iran wabadilishana wafungwa

Iran na Marekani wamebadilishana wafungwa kwa mara nyingine licha ya mvutano mkubwa kati ya nchi hizo mbili hasimu, ishara kwamba mataifa hayo mawili yanaweza kufikia maelewano ya kudumu.

Michael White, askari wa zamani wa kikosi cha wanamaji cha Marekani aliyekamatwa mwezi Julai 2018 nchini Iran, atakuwa "hivi karibuni na familia yake Marekani," Donald Trump amesema kwenye ukurasa wake wa Twitter, ambaye amesema amezungumza na mateka huyo wa zamani , ambaye kwa sasa yuko nchini Uswisi, na "hivi karibuni atakuwa njiani kulekrea nchini Marekani".

"Asante Iran, hii inaonyesha kuwa mkataba unawezekana!", ameongeza rais wa Marekani, bila hata hivyo kutoa maelezo zaidi, huku akiahidi kuendelea kujikita na "kuachiliwa huru kwa raia wote wa Marekani wanaoshikiliwa Mateka katika nchi za kigeni"- jambo ambalo limeendelea kukaribishwa na Wamarekani wengi kwa kipindi cha miaka mitatu.

Baada ya tangazo kuhusu Bw. White, Tehran imesema kwamba mwanasayansi wa Iran, Majid Tahéri, aliyekuwa anazuiliwa nchini Marekani "kwa madai yasiyoeleweka", ameachiliwa na serikali ya Washington.

Majid Tahéri alikanusha mashtaka dhidi yake kuhusu ubadhirifu wa kifedha mwezi Desemba, na pia alishtakiwa kwa kutuma zana ya kiufundi nchini Irani kwa kukiuka vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran, lakini jaji wa Marekani aliagiza kuachiliwa kwake huru Alhamisi wiki hii

-RFI


Share:

Ubora wa Mazingira yetu ndio Uhai na Ustawi Wetu - Zungu

Na Lulu Mussa
Dodoma
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mussa Azzan Zungu amesema suala la mabadiliko ya tabianchi halitambui mipaka ya kijiografia wala ya kisiasa, hivyo, juhudi za kukabiliana na changamoto hii zinahitaji ushirikiano wa pamoja baina ya Jumuiya za Kimataifa.
 
Hayo ameyasema jana Jijini Dodoma katika kilele cha Siku ya Mazingira Duniani ambapo ameitaka jamii ya watanzania kuendelea kulinda mazingira kwa mustakabali wa maendeleo endelevu.
 
Amebainisha kuwa nchi yetu ni Mwanachama wa Jumuiya za Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira za kikanda na za Kidunia, hivyo inatekeleza Sera na Sheria za mazingira kuendana na makubaliano na maazimio yanayofikiwa katika Jumuiya hizo kwa kadri inavyowezekana. 
 
“Nchi yetu ni Mwanachama wa Mkataba wa Kimataifa wa kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi unaojulikana kama Mkataba wa kulinda mazingira wa Paris (Paris Agreement).  Katika kutekeleza Mkataba huu, Nchi wanachama zimekubaliana kupunguza uzalishaji wa gesijoto kwa pamoja na kuongeza juhudi za kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi” Zungu alisisitiza.
 
 Amesema kuwa Tanzania imeandaa miradi ya kimkakati kwa lengo la kupunguza uzalishaji wa gesijoto ikiwa ni pamoja na ujenzi wa reli ya kisasa (Standard Gauge) na ujenzi wa bwawa la uzalishaji wa umeme wa megawati 2115 (Mwalimu Nyerere Hydropower – Stieglers Gorge). 
 
“Malori na mabasi hutumia dizeli ambayo huzalisha gesijoto aina ya hewa ukaa.  Reli ya kisasa inayojengwa haitatumia dizeli bali itatumia umeme ambao unatokana na nguvu ya maji, pia kwa kujenga bwawa la umeme la Mwalimu Nyerere tutaongeza kiasi kikubwa cha umeme unaozalishwa kwa nguvu ya maji, na kupunguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya gesi asilia na dizeli katika uzalishaji wa umeme” Zungu alisisitiza.

Amebainisha kuwa umeme wa uhakika utakaozalishwa na Bwawa la Mwalimu Nyerere utasaidia wananchi walioko vijijini na mijini kupata nishati ya uhakika na kwa gharama nafuu na hivyo kupunguza kwa kiasi kikubwa ukataji wa miti kwa ajili ya kupata nishati ya kuni na mkaa. Jitihada hizi zitachangia kwa kiasi kikubwa kwenye hifadhi ya mifumo asilia ya kimaumbile/bioanuai. 
 
Awali Waziri Zungu amewatunuku vyeti Wakaguzi wa Mazingira 22 kutoka Wilaya za Mkoa wa Dodoma ambao walishiriki mafunzo yalitolewa na Ofisi ya Makamu wa Rais pamoja na Baraza la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira NEMC.

Siku ya Mazingira Duniani huadhimishwa tarehe 5 Juni kila mwaka. Kaulimbiu yam waka huu ni  ”Tutunze Mazingira: Tukabiliane na Mabadiliko ya Tabianchi”.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger