Friday 3 January 2020
Thursday 2 January 2020
JAMAA WAWILI WAFIKISHWA MAHAKAMANI BAADA YA KUIBA POMBE
Jamaa wawili wamefikishwa mahakamani Jumanne ,Disemba 31, 2019 baada ya kukashifiwa kwa kuiba chupa sita za pombe aina ya Jameson.
Daniel Mbugua na Cliff Obonyo ambao ni wafanyakazi wa kampuni ya Mitchel Cot wanasemekana kutekeleza kitendo hicho Disemba 17, wakiwa mtaani Embakasi.
Pombe hiyo ni ya thamani ya KSh 15,000.
Washukiwa hao wanasemekana kuficha pombe hiyo kwenye gari la kampuni ambalo husafirisha mizigo na bidhaa.
Wawili hao walikana mashtaka dhidi yao na kuachiliwa kwa dhamana ya KSh 20,000 kila mmoja. Kesi dhidi yao itasikizwa tena Aprili 28, 2020.
JAMAA ANYWA MIKOJO YA WANAWAKE LITA MOJA NA NUSU
Jamaa mmoja nchini Uganda aliyetambulika kwa jina la Ismail Dholaga mwenye miaka 35, amelazimika kunywa lita moja na nusu ya mikojo ya wanawake ili kurejesha fahamu baada ya kulewa tilalila.
Ismail Dholaga ambaye anafanya kazi ya udereva wa pikipiki (bodaboda) alilazimishwa kufanyiwa kitendo hicho na wakazi wa eneo la mji wa Iganga, baada ya kukutwa akiwa amelewa na wapita njia.
Wakazi wa eneo hilo na wapita njia walikusanya mikojo ya wanawake waliokuwepo kwenye tukio, ikapatikana lita moja na nusu, mmoja wa wanawake waliotoa huduma hiyo amesema “Tulifaulu kupata lita moja unusu ya mkojo na kumlazimisha kunywa kama huduma ya kwanza”.
Hata hivyo huduma hiyo haikufanikiwa ndipo maafisa wa polisi walifika na kumkimbiza katika hosptali iliyokuwa karibu.
Picha : HIACE YAGONGA BAISKELI IKIKWEPA GARI NA KUJERUHI SHINYANGA MJINI
Watu watatu wanaelezwa kujeruhiwa baada ya gari aina ya Hiace yenye namba za usajili T 836 DEB ikitokea Kishapu kwenda Shinyanga Mjini kumgonga mwendesha baiskeli na kutumbukia mtaroni wakati ikikwepa gari aina ya Toyota Harrier yenye namba za usajili T726 DFM.
Ajali hiyo imetokea majira ya saa 12 jioni leo Alhamis Januari 2,2019 katika eneo la Pepsi ‘Ushirika’ barabara ya Shinyanga – Mwanza.
Kwa Mujibu wa mashuhuda wa ajali hiyo wameiambia Malunde 1 blog kuwa dereva wa Hiace akitokea Kishapu alikuwa anajaribu kumkwepa dereva wa gari aina ya Toyota Harrier aliyeingia kwenye njia isiyo yake ndipo Hiace ikamgonga mwendesha baiskeli ambaye ni miongoni mwa waliojeruhiwa wakiwemo wale waliokuwa ndani ya Hiace na wamekimbizwa katika hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Shinyanga.
Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga likiongozwa na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Shinyanga (RTO) Anthony Gwandu wamefika eneo la tukio na tayari gari aina ya Harrier inashikiliwa katika kituo cha polisi.
Taarifa kamili tutawaletea hivi punde.
Gari aina ya Hiace yenye namba za usajili T 836 DEB ikiwa kwenye mtaro baada ya ajali - Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Gari aina ya Hiace yenye namba za usajili T 836 DEB na baiskeli eneo la ajali
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blo
MWANAMKE AFARIKI DUNIA BAADA YA KUPIGWA NA MME WAKE
Na Amiri Kilagalila-Njombe
Jeshi la polisi mkoani Njombe linamshikilia ndugu Josphat Mtega (24) mkazi wa Ramadhani mjini Njombe kwa tuhuma za kumsababishia kifo mkewe kilichotokana na ugomvi.
Akizungumza na vyombo vya habari ofisini kwake,kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamis Issa amesema mtuhumiwa huyo anashikiliwa na jeshi la polisi kutokana na kugombana na mkewe Angelina Sanga (24) ambapo inadaiwa alimpiga na hivyo kumsababishia majeraha makubwa yaliyosababisha kifo chake.
Kamanda amesema mara baada ya ugomvi huo, Angelina alisafirishwa hadi hospitali ya Ikonda iliyopo wilayani Makete ambapo baada ya kufikishwa katika hospitali hiyo uchunguzi wa kitabibu ulibaini kuwa dada huyo alionekana amevunjika mkono na sehemu mbali mbali za mwili wake zilionekana zimeshambuliwa vibaya.
Amesema mwanaume huyo anaendelea kushikiliwa na jeshi la polisi kwa uchunguzi zaidi huku taratibu za kisheria zikiendelea.
WATOTO 4 WAFA MAJI NJOMBE
Na Amiri Kilagalila-Njombe
Jeshi la polisi mkoa wa Njombe limesema kwa nyakati tofauti watoto wanne mkoani humo wamepoteza maisha kutokana na maji.
Akizungumza na vyombo vya habari mkoani humo kamanda wa polisi Hamis Issa amesema,mtoto wa kwanza aliyefahamika kwa majina ya Alpha Pilla (6) mkazi wa mtaa wa Kibendange mjini Makambako na mwanafunzi wa shule ya Makoga akiwa akicheza 25-12-2019 alitumbukia kwenye dimbwi la maji yaliyotuama ambayo hutumika kwa shughuli za uchimbaji mchanga na kusababisha kifo chake.
Kamanda amesema tukio jingine ni la mtoto Shani Belevete (8) huko kijiji cha Msimbazi kata ya uhambule wilaya ya Wanging’ombe alikutwa ametumbukia ndani ya kisima cha maji na mpaka watu kutafuta ngazi alikutwa amekwishafariki.
Amesema tukio jingine linahusisha vifo vya watoto wawili Joel Kutika (6) na Abromovich Hosea (3) huko kijiji cha Saja wilayani Wanging’ombe mnamo tarehe 1-1-2020 walikufa maji katika mto Bokelo uliopo kijijini hapo huku kiini cha tukio hilo kikiwa ni wazazi kutokuwa makini na watoto wao wanapokuwa wanacheza.
Aidha kamanda wa polisi ametoa wito kwa wazazi kuwa makini na watoto huku jeshi hilo likianza kuchukuwa hatua kwa mzazi yeyote asiyekuwa makini kuhakikisha ulinzi wa watoto na kusababisha vifo vya uzembe.
Mahakama Yamgomea Kabendera Kuhudhuria Ibada ya mazishi ya mama yake.
Mahakama ya Kisutu imetupilia mbali ombi la Erick Kabendera kwenda kutoa heshima za mwisho kufuatia kifo cha mama yake mzazi.
Hakimu Janeth Mtega amesema mahakama haina mamlaka ya kutoa ruhusa hiyo, na mtuhumiwa hana fursa ya kukata rufaa kupinga uamuzi huo.
Maombi hayo yaliwasilishwa na mawakili wake wakiongozwa na Jebra Kambole.
Kwa upande wake Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alitoa pole kwa Erick kufiwa na mama yake ambapo licha ya pole hizo, upande wa mashtaka ulipinga ombi hilo kwa madai ya kuwa hoja za upande wa utetezi hazikuwa na mashiko.
Kesi imeahirishwa hadi Januari 13.
Mwili wa Verdiana Mujwahunzi (80), mama mzazi wa mwandishi wa habari nchini Tanzania, Erick Kabendera aliyefariki dunia Desemba 31, 2019 katika Hospitali ya Rufaa Amana jijini Dar es Salaam utagwa kesho Ijumaa Januari 3, 2019 Chang’ombe Dar es Salaam kisha kusafirishwa kwenda Bukoba mkoani Kagera kwa maziko yatakayofanyika Januari 6, 2020.
Hakimu Janeth Mtega amesema mahakama haina mamlaka ya kutoa ruhusa hiyo, na mtuhumiwa hana fursa ya kukata rufaa kupinga uamuzi huo.
Maombi hayo yaliwasilishwa na mawakili wake wakiongozwa na Jebra Kambole.
Kwa upande wake Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon alitoa pole kwa Erick kufiwa na mama yake ambapo licha ya pole hizo, upande wa mashtaka ulipinga ombi hilo kwa madai ya kuwa hoja za upande wa utetezi hazikuwa na mashiko.
Kesi imeahirishwa hadi Januari 13.
Mwili wa Verdiana Mujwahunzi (80), mama mzazi wa mwandishi wa habari nchini Tanzania, Erick Kabendera aliyefariki dunia Desemba 31, 2019 katika Hospitali ya Rufaa Amana jijini Dar es Salaam utagwa kesho Ijumaa Januari 3, 2019 Chang’ombe Dar es Salaam kisha kusafirishwa kwenda Bukoba mkoani Kagera kwa maziko yatakayofanyika Januari 6, 2020.
Picha : MGOGORO WA MAKINIKIA YA ALMASI MWADUI WAIBUKA KISHAPU, MKUTANO WA WACHIMBAJI WAPIGWA STOP…MADIWANI WAZIMIWA SPIKA
Diwani wa kata ya Maganzo, Lwinzi Mbalu Kidiga ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madiwani wa kata zinazozunguka mgodi wa Mwadui akiwatangazia wananchi kuhusu taarifa za kuzuiwa kwa mkutano wao.
Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Katika hali isiyotarajiwa mkutano wa wananchi wanaozunguka mgodi wa almasi wa Williamson Diamond LTD ‘Mgodi wa Mwadui’ ulioandaliwa na Madiwani wanaozunguka mgodi huo kujadili hatima ya Masalia ya mchanga wa madini ya almasi ‘Makininikia’umepigwa marufuku dakika chache kabla ya mkutano kuanza ambapo ghafla viti viliondolewa huku spika zikizimwa wakati diwani wa Maganzo Lwinzi Kidiga akizungumza.
Tukio hilo limetokea leo Alhamis Januari 2,2020 majira ya saa sita mchana ambapo madiwani wa kata zinazozunguka mgodi huo pamoja na wananchi waliokusanyika katika soko la kata ya Maganzo ‘Mji wa Maganzo’ wilayani Kishapu mkoani Shinyanga kutakiwa kutawanyika mara moja kwa madai kuwa ni ‘Order’ Agizo kutoka juu.
Tukio la kuzuiwa kufanyika mkutano ni kielelezo cha mgogoro uliozuka kati Wachimbaji wadogo wanaozunguka mgodi wa Mwadui na Chama cha Wachimbaji Madini mkoa wa Shinyanga ‘Shinyanga Region Miners Association – SHIREMA’ siku chache baada ya Mgodi wa Williamson Diamond Ltd kuamua kutoa mchanga wa Makinikia ya Almasi bure kwa wachimbaji wa wadogo wa madini.
Katika kikao hicho ambacho kilihudhuriwa pia na Waziri wa Madini Dotto Biteko baada ya wachimbaji kuomba wapewe makinikia ili kuondoa mgogoro kati yao na mgodi ambapo SHIREMA walipewa jukumu la kusimamia utaratibu mzuri wa kugawa mchanga huo.
Akitoa taarifa kwa wananchi kuhusu kusitishwa kwa mkutano huo,wakati tayari viti na meza kuu vikiwa vimetolewa,Diwani wa kata ya Maganzo, Lwinzi Mbalu Kidiga ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madiwani wa kata zinazozunguka mgodi wa Mwadui, ghafla spika zilizimwa na watu ambao hawakujulikana mara moja.
Kidiga alisema wameahirisha kufanya mkutano huo kutokana na Amri kutoka juu iliyowataka waahirishe mkutano huo vinginevyo watawekwa ndani.
Alisema chanzo cha kuzuiwa kufanya mkutano ni watu wachache waliojipanga kuhujumu uchumi wa watu wa Maganzo ili wapate asilimia za chini huku akibainisha kuwa yeye kama diwani hakubali.
“Ndugu wananchi mmeiona sura hapa, sura ya hapa haijakaa vizuri tulikuwa tumetoa viti kwa ajili ya mkutano wa hadhara lengo na madhumuni ilikuwa ni kuzungumza changamoto zilizopo katika hata hii na kata za jirani.Mkutano wetu ulikuwa ni mzuri tu wa kupeana habari haukuwa na ashki yoyote.Lakini cha kushangaza hapa meza zimetolewa,huu mkutano umeahirishwa..kwa Kiswahili kingine Tumezuiwa”,ameeleza Kidiga.
“Nimezuiwa lazima niseme ukweli..Huu mkutano wangu upo ndani ya kisheria na nina mamlaka ya kuitisha mkutano bila kuuliza kwa mtu yeyote,sheria na katiba ya nchi inanilinda. Kwa Order kutoka Juu mkutano huu nimeambiwa nisifanye mara moja..Sasa mara moja maana yake huwezi kuuliza lakini wanasema chelewa chelewa mwishowe ukweli utaonekana.
“Sisi hapa ni wakweli,tunataka tuzungumze ukweli na ukweli wenyewe ni kutetea watu walio chini wapate maslahi siyo waingilie watu wachache,hiyo biashara haipo.”,alisema Kidiga huku akishangiliwa na wananchi.
“Mmetuchagua kwa ajili ya kusimamia haki zenu siyo baadhi ya watu wanufaike,hiyo biashara haipo..Tumezuiwa sawa,sisi tuko chini ya sheria hakuna mtu aliye juu ya sheria lakini ilikuwa halali yetu tufanye mkutano huu na madiwani wa kata jirani, tulikuwa tumepanga tuzungumzie kuhusu Makinikia basi.
Tumeambiwa tukifanya mkutano tutawekwa ndani na tukiendelea ku – force udiwani ndiyo basi tena. Ndani tutakwenda kwani waliomo ndani siyo watu?. Tukiwekwa ndani basi Rais Magufuli atakuja kutuwekea dhamana. Nilitaka niseme hilo ili msisambae kienyeji kwani tuliwaita kwenye mkutano na wengine mmetoka mbali”,alieleza Kidiga.
Kidiga alisema SHIREMA imekuwa ikifanya vikao vyake na kufanya mambo bila kuwashirikisha madiwani wa kata zinazozunguka mgodi wa Mwadui akidai kuwa haina nia nzuri ya kuwasaidia wachimbaji wadogo wa madini wilayani Kishapu.
Hata hivyo baada ya mkutano huo uliokuwa umezungukwa na askari polisi wakiongozwa na Mkuu wa Kituo cha Polisi wilaya ya Kishapu kuahirishwa,Madiwani wanaozunguka mgodi wa Mwadui,waliamua kufanya mkutano na waandishi wa habari ‘Press Conference’ ili kueleza lengo la mkutano wao.
Katibu wa Jumuiya ya Madiwani wanaozunguka mgodi wa Mwadui Abdul Ngolomole ambaye ni Diwani wa Kata ya Songwa (CCM) alisema hawakubaliani na kitendo cha SHIREMA kumpatia Mkandarasi anayesafirisha mchanga wa madini kutoka Mwadui asilimia 75 ya mauzo ya almasi na wachimbaji wadogo kupewa asilimia 15.
“Tunataka Mkandarasi wa kusafirisha makinikia atangazwe hadharani kupitia zabuni kwani mkandarasi aliyepo sasa ni Mkandarasi wa mfukoni ambaye ni Junior Construction ya Mbunge wa Kishapu Suleiman Nchambi,ni mkandarasi ambaye amebuniwa na SHIREMA ,huyu ni mtu mkubwa sana, mamlaka zipo lakini kwanini hazisemi?. Sisi tunapotaka kufanya mkutano kuwaeleza wananchi ukweli tunaonekana tunataka kuzuia maslahi ya watu flani”,alisema Ngolomole.
“Baada ya kulalamikia hizo asilimia 15 SHIREMA wameongeza asilimia kwamba mchimbaji mdogo apate asilimia 37.5 ambayo haiwasaidii wanyonge.Sisi madiwani tumekubaliana wananchi wapate zaidi ya asilimia 60 ili kuwasaidia wanyonge,ndicho anachokitaka Mhe. Rais John Pombe Magufuli kwani hajatoa Makinikia haya ili wachache wanufaike nayo”,alifafanua Ngolomole.
“Sisi madiwani tunawataka wananchi wasikubali kufanya kazi chini ya SHIREMA kwani inanyonya wananchi wamejiwekea fedha kwenye makinikia haya na wamekuwa wakiwatoza wachimbaji wadogo shilingi 200,000/= tena bila risti ili wapewe usajili SHIREMA. Tunataka wananchi wapewe mamlaka ya kuchagua viongozi wa kuwasimamia kutoka kwenye vikundi vyao vya uchimbaji”,alisema Ngolomole.
“Tumezuiwa kufanya mkutano kwani inaonekana tunaingilia maslahi ya watu binafsi.Kwenye mkutano tulitaka tuwaeleze wananchi mapendekezo ya madiwani na kupokea maoni ya wananchi kuhusu makinikia”,alisema.
Ngolomole alimuomba Rais Magufuli wakati anatoka kwenye mapumziko yake Chato mkoani Geita apitie Maganzo kukutana na wachimbaji wadogo wa madini ili kutatua mgogoro huo wa makinikia.
Kwa upande wake diwani wa kata ya Mwadui Luhumbo Paul Magembe, William Luhende Jijimya wa kata ya Mondo walisema hawapo tayari kuona wananchi wananyonywa na hawatarudi nyuma huku wakimuomba Rais Magufuli kuwasaidia wachimbaji wadogo wa madini wilayani Kishapu.
Nao wananchi waliozungumza na waandishi wa habari,akiwemo Ramadhani Amani,Bala Masanja na Hamis Sizya walisema zoezi la kupewa makinikia lilitolewa bila asilimia hivyo wanashangaa kuona baadhi ya viongozi wanatumia fursa hiyo kujipatia kipato na kuomba serikali kujali wanyonge.
Kufuatia malalamiko yaliyotolewa na wananchi pamoja madiwani kuhusu SHIREMA,Viongozi wa Chama cha Wachimbaji Madini mkoa wa Shinyanga (SHIREMA) ambao ni Hamza Tandiko (Mwenyekiti) na Gregory Kibusi (Katibu) walikataa kuzungumza na waandishi wa habari wakidai kuwa watatoa taarifa kuhusu Makinikia kwenye kikao chao na vikundi vya wachimbaji wadogo wa madini Januari 3,2020.
ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Diwani wa kata ya Maganzo, Lwinzi Mbalu Kidiga ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madiwani wa kata zinazozunguka mgodi wa Mwadui akishangaa baada ya spika kuzimwa wakati akiwatangazia wananchi kuhusu taarifa za kuzuiwa kwa mkutano wao katika Soko la Maganzo wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga leo Januari 2,2020. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Katibu wa Jumuiya ya Madiwani wanaozunguka mgodi wa Mwadui Abdul Ngolomole ambaye ni Diwani wa Kata ya Songwa (CCM) akiwaomba wananchi kuwa watulivu baada spika kuzimwa baada ya kuzuiwa kufanya mkutano wa hadhara.
Katibu wa Jumuiya ya Madiwani wanaozunguka mgodi wa Mwadui Abdul Ngolomole ambaye ni Diwani wa Kata ya Songwa (CCM) akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari 'Press Conference' baada ya kuzuiwa kufanya mkutano wa hadhara uliolenga kujadili kuhusu Makinikia ya almasi yaliyopo katika Mgodi wa Mwadui.
Katibu wa Jumuiya ya Madiwani wanaozunguka mgodi wa Mwadui Abdul Ngolomole akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari.
Diwani wa kata ya Maganzo, Lwinzi Mbalu Kidiga ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Madiwani wa kata zinazozunguka mgodi wa Mwadui akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari 'Press Conference' baada ya kuzuiwa kufanya mkutano wa hadhara uliolenga kujadili kuhusu Makinikia ya almasi yaliyopo katika Mgodi wa Mwadui.
Kulia ni William Luhende Jijimya wa kata ya Mondo akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari 'Press Conference' baada ya kuzuiwa kufanya mkutano wa hadhara uliolenga kujadili kuhusu Makinikia ya almasi yaliyopo katika Mgodi wa Mwadui.
Diwani wa kata ya Mwadui Luhumbo Paul Magembe akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari 'Press Conference' baada ya kuzuiwa kufanya mkutano wa hadhara uliolenga kujadili kuhusu Makinikia ya almasi yaliyopo katika Mgodi wa Mwadui.
Mchimbaji mdogo wa madini akizungumza na waandishi wa habari.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Upande wa Jamhuri wakataa Kabendera kumzika Mama yake...Mahakama Kuamua
Upande wa Serikali umempa pole Mwandishi wa Habari, Erick Kabendera kwa kufiwa na Mama yake mzazi, Verdiana Mujwahuzi huku ukipinga maombi yake ya kutaka ashiriki Ibada ya mazishi ya mama yake.
Hayo yamebainika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakati Kabendera anayekabiliwa na kesi ya utakatishaji fedha alipofikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya kesi yake.
Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon amemueleza Hakimu Mkazi, Janeth Mtega kwamba Jamhuri inampa pole Kabendera kwa kufiwa na Mama yake mzazi.
“Hata sisi tuna masikitiko makubwa na tunampa pole nyingi Kabendera kwa kufiwa na Mama yake mzazi, lakini mahakama isifungwe mikono kwa maombi yaliyowasilishwa ya kutaka kushiriki msiba,”amesema Wankyo.
Wankyo amedai kuwa maombi ya Kabendera kupitia mawakili wake yamewasilishwa wakati ambao si sahihi kwa sababu mahakama haina mamlaka na pia Mkurugenzi wa Mashitaka hajaipa kibali ya kusikiliza kesi hiyo.
“Katika macho ya kisheria mahakama yako haina mamlaka, hata sisi tuna masikitiko makubwa lakini mahakama isifungwe mikono,” amesema.
Kuhusu mwenendo wa kesi, upelelezi unaendelea na shauri limefika hatua nzuri ya maelewano baina ya mshitakiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Mashitaka (DPP).
Kukataliwa kwa Kabendera kushiriki mazishi ya Mama yake, kumeibuka kutokana na maombi aliyoyatoa Kabendera kupitia Mawakili wake akiwemo Jebra Kambole.
Wakili Kambole amedai wanaiomba mahakama hiyo imruhusu Kabendera akashiriki Ibada ya Mazishi ya Mama yake mzazi katika Kanisa la Roman Katoliki lilipo Changombe majira ya mchana.
Kambole ameieleza mahakama kuwa suala la kushiriki sala ya mwisho ya msiba ni haki ya Binadamu, suala la faragha.
“Kushindwa kuudhuria maziko ya Mama yake tutakuwa tumemuadhibu adhabu kubwa tena kwa kuangalia uhusiano wa mshitakiwa na mama yake mzazi kwani alikuwa akimuuguza na ni vizuri akatoa heshima ya mwisho,”ameeleza.
Wakili Jebra amedai kuwa ni muhimu kwa Kabendera kushiriki kwa sababu Mama mzazi ni mmoja, akifa anaagwa mara moja.
“Jamhuri haitaathirika kwa lolote kwa sababu mshitakiwa atakuwa chini ya ulinzi na ibada itakuwa mchana kanisani na Temeke sio mbali na gerezani, tunaomba akatoe heshima ya mwisho,” ameomba.
Baada ya kutoa hoja hizo, Hakimu Mtega ameahirisha kesi hiyo hadi saa 8:45 mchana kwa ajili ya kutoa uamuzi kama Kabendera ashiriki Ibada ya mazishi ya Mama yake mzazi ama lah.
Waandamanaji waondoka eneo la ubalozi wa Marekani, Iraq
Waungaji mkono wa makundi ya kijeshi nchini Iraq yanayoungwa mkono na Iran ambao waliovamia maeneo ya viunga vya ubalozi wa Marekani na kurusha mawe katika maandamano ya siku mbili wameondoka jana(01.01.2020).
Hatua hiyo imewezekana baada ya Marekani kupeleka vikosi vya ziada na kutishia kuchukua hatua dhidi ya Iran. Lakini wachambuzi wa masuala ya kisiasa wanaonya kuwa hali hiyo inaweza kuwa na athari za kudumu katika sekta tete ya usalama nchini Iraq pamoja na mahusiano ya kidiplomasia.
Waandamanaji , ambao wamekasirishwa na mashambulizi ya anga ya vikosi vya jeshi la Marekani dhidi ya kundi linaloungwa mkonom na Iran la Hezbollah ambapo kiasi ya watu 25 waliuwawa, walirusha mawe katika jengo la ubalozi wakati wanajeshi wa jeshi la Marekani waliokuwa katika mapaa ya jengo hilo wakifyatua mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya.
Ilipofika mchana , wengi walionekana kutii wito wa kujiondoa kutoka katika eneo hilo, uliotolewa na kundi la wanamgambo wa Kishia linaloongoza vikundi vya umma vya mapambano PMF, ambalo lilisema ujumbe wa waandamanaji tayari umesikika.
Vijana walitumia matawi ya miti ya mitende kufajia mtaa mbele ya eneo la ubalozi wa Marekani. Wengine walikusanya vifaa hivyo na magari yaliwasili kuvichukua.
Maandamano hayo yameonesha mabadiliko mapya katika kivuli cha vita kati ya Marekani na Iran vinavyotokea katika eneo la mashariki ya kati. Rais Donald Trump ambaye anakabiliwa na kampeni ya uchaguzi mwaka 2020, ameishutumu Iran kwa kuchochea ghasia hizo.
Ametishia siku ya Jumanne kuchukua hatua dhidi ya iran lakini alisema baadaye kuwa hataki vita.
Makamu ya rais katika taasisi ya Charles Koch anayehusika na utafiti na sera Will Ruger amesema hatua Marekani inazochukua kuibinya Iran hazitafanyakazi:
Ametishia siku ya Jumanne kuchukua hatua dhidi ya iran lakini alisema baadaye kuwa hataki vita.
Makamu ya rais katika taasisi ya Charles Koch anayehusika na utafiti na sera Will Ruger amesema hatua Marekani inazochukua kuibinya Iran hazitafanyakazi:
"Moja ya matatizo hapa ni kwamba sio tu shambulio la roketi la jeshi la Marekani ndio lililochochea mzozo huu, lakini pia kile tulichoshuhudia jana katika ubalozi wa Marekani mjini Baghdad, nafikiri hii inaonesha kwamba kampeni kubwa ya shinikizo ambayo utawala wa Trump umekuwa ukitumia dhidi ya Iran haifanyikazi kupunguza wasi wasi. Na haifanyi Iran kutulia. Badala yake inaleta uhasama na changamoto nyingi kwa mahusiano."
Iran , ikiwa katika hali mbaya ya kiuchumi kutokana na vikwazo vya kuumiza vilivyowekwa na Trump, imekana kuhusika.
Ghasia hizo zilitokana na mashambulizi ya anga siku ya Jumapili dhidi ya vituo vya kundi la Kataib Hezbollah kwa kulipiza kisasi kwa mashambulizi ya makombora ambayo yalisababisha kifo cha mkandarasi wa Marekani kaskazini mwa Iraq wiki iliyopita.
Ghasia hizo zilitokana na mashambulizi ya anga siku ya Jumapili dhidi ya vituo vya kundi la Kataib Hezbollah kwa kulipiza kisasi kwa mashambulizi ya makombora ambayo yalisababisha kifo cha mkandarasi wa Marekani kaskazini mwa Iraq wiki iliyopita.
Marekani imesema wanadiplomasia wako salama na inapeleka mamia ya wanajeshi wa ziada katika eneo hilo.
Wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani imesema jana kuwa waziri wa mambo ya kigeni Mike Pompeo ameamua kuahirisha ziara yake kwenda Ukraine, Belarus , Kazakhstan, Uzbekistan, na Cyprus na kubakia mjini Washington ili kufuatilia hali nchini Iraq.
-DW
Wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani imesema jana kuwa waziri wa mambo ya kigeni Mike Pompeo ameamua kuahirisha ziara yake kwenda Ukraine, Belarus , Kazakhstan, Uzbekistan, na Cyprus na kubakia mjini Washington ili kufuatilia hali nchini Iraq.
-DW
Polisi adaiwa kukatwa sehemu za siri na mkewe
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linamshikilia Flora Adamu (23), mkazi wa Shinyanga Mjini, kwa tuhuma za kumkata mumewe sehemu za siri, ambaye ni askari Polisi mwenye Namba H, 8980 Pc Kazimiri, kwa madai ya kumtuhumu kutokuwa muaminifu katika ndoa.
Imeelezwa kuwa mtuhumiwa huyo alimtuhumu mumewe kuwa ana nyumba ndogo.
Akizungumza na wanahabari, Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga, Deborah Magiligimba, alisema tukio hilo limetokea Desemba 28 mwaka jana, majira ya saa 6:30 usiku wakati wanandoa hao wakiwa wamelala.
Alisema wakiwa wamelala, ghafla Flora aliamka na kuanza kumnyatia, huku akiwa ameshika kitu chenye ncha kali kisha kumkata mumewe sehemu za siri na kumjeruhi vibaya.
“Baada ya askari huyu kukatwa uume wake alikimbizwa kwenye Hospitali ya Rufani ya Mkoa wa Shinyanga ili kupatiwa matibabu ya haraka, ambapo alilazwa kwa muda wa siku mbili kisha kuruhusiwa kurudi nyumbani kuendelea kujiuguza kidonda,” alisema Kamanda Magiligimba.
“Chanzo cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi, ambapo mwanamke alikuwa akimtuhumu mume wake kuwa ana nyumba ndogo, ndipo akaamua kuchukua kitu chenye ncha kali kisha kuanza kuukata uume wa mumewe na kumjeruhi vibaya,” aliongeza.
Aidha, kamanda huyo alisema Jeshi la Polisi linamshikilia mwanamke huyo, na kwamba uchunguzi ukikamilika, atafikishwa mahakamani.