Sunday 1 December 2019

Halmashauri Ya Jiji La Dodoma Yaanza Kutekeleza Agizo La Rais La Kuwalipa Fidia Wananchi Waliopisha Eneo La Jeshi.

Na.Faustine Gimu Galafoni ,Dodoma
Halmashauri ya jiji la Dodoma imeshaanza kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli alilotoa Nov.25 mwaka huu la kulipa fidia kwa wananchi  1526 wanaopisha eneo la Jeshi la Wananchi Jijini Dodoma.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jana  Nov.30,2019  jijini Dodoma  mkurugenzi wa jiji la Dodoma Godwin Kunambi amesema kiasi kinachotakiwa kulipwa kwa wananchi hao ni Tsh.Bil.3.399  na ukubwa wa eneo zima  ni ekari elfu tano  na eneo linalopaswa kulipwa fidia ni ekari  elfu 3 mia 4 na 31 na kinachotakiwa kwa wanufaika  ni kufungua akaunti za benki huku uhakiki ukiendelea.

Aidha,Bw.Kunambi amesema ofisi ya mkurugenzi  jiji la Dodoma imeshaanza kuwasaidia wananchi kusaidia kufungua akaunti za benki na kuanzia wiki ijayo wananchi wataanza kulipwa fedha zao.

Ikumbukwe kuwa Nov.25,2019 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.John Pombe Magufuli wakati akiweka jiwe la Msingi eneo la Jeshi la Ulinzi alitoa agizo kwa  halmashauri ya jiji la Dodoma kuwalipa fidia wananchi  1526 wanaopisha mradi wa eneo la jeshi la Ulinzi.


Share:

Sekta Ya Ardhi yatakiwa Kupewa Kipaumbele Katika Mipango Ya Maendeleo Nchini

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara Eng. Stellah Manyanya amezitaka idara mbalimbali za Serikali kuipa kipaumbele sekta ya ardhi katika mipango ya maendeleo inayofanyika nchini.

Eng. Stellah Manyanya ameyasema hayo wakati akifungua Mkutano mkuu wa sita wa Mwaka wa Wataalaamu wa Mipangomiji ulioanza tarehe 27 hadi 29 Novemba 2019 jijini Dodoma.

Eng. Stellah Manyanya amesema, kumekuwepo na miradi mingi nchini inaanzishwa na Serikali inatumia gharama kubwa katika kuikamilisha matokeo yake imekuwa haitumiki na wakati mwingine inaingiliana na shughuri nyingine za kijamii hali inayopelekea kuzuka kwa migogoro katika jamii.

Akitolea mfano Jengo la Machinga Complex  lililopo Ilala Jijini Dar es Salaam, Eng. Stellah Manyanya amesema kuwa kutokuwepo kwa mipango kina ya muda mrefu na utafiti duni ndio chanzo kikubwa hadi leo hii jengo hilo kushindwa kufikia lengo walilojiwekea la kuwa saidia wafanyabiashara wadogowadogo kuwa na sehemu yao ya kufanyia shughuri zao.


Share:

Elimu Ya Umeme Kwa Wasioona Yaipa Tanesco Taswira Mpya

SHIRIKA la Umeme Nchini TANESCO limeendesha semina maalum inayohusu masuala ya Umeme kwa wanachama wa chama cha wasioona  Tanzania (TLB)  mkoani Morogoro.

Akizungumza wakati wa uzinduzi  wa warsha hiyo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro  Loata Ole Sanare amesema kuwa Tanesco  imeonyesha mfano mzuri wa kuigwa kwa kutoa elimu hiyo kwa watu wa kundi  maalum katika jamii.

Alisema pia kupitia hili shirika limetoa taswira kuwa mashirika ya Umma yanafuata muelekeo wa Raisi John Pombe Magufuli ambae ni  Raisi wa wanyonge na kwa kujali wateja wake hata wa Makundi maalum kwa kutoa elimuYa Umeme itakayowasaidia katika maisha yao ya kila  siku.

Mkuu huyo wa Mkoa  amewataka wasioona kutokuwa wanyonge kwakudhani kuwa  Serikali haiwatambui na kusema kuwa Serikali ipo pamoja nao na kuwakaribisha katika ofisi za Mkoa, muda wowote watakapokua na changamoto zozote.

Naye Kaimu meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) mkoa wa Morogoro William Masome amesema Kuwa TANESCO chini ya Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Tito Mwinuka imetambua umuhimu wa watu wenye Ulemavu wa kutoona kupatiwa elimu ya Umeme ili waweze kutambua fursa  zitokanazo na umeme zitakazoweza kuwainua kiuchumi lakin pia kuwafundisha jinsi ya kutumia umeme vizuri (matumizi Bora ya umeme)ili wasilipe gharama kubwa
Kwenye kununua Umeme.

Naye kwa upande wake Mratibu wa idara ya maendeleo, Vijana na Chipkizi toka TLB , Bw.Kiongo Itambu ameishukuru TANESCO kwa kuwapatia elimu hiyo Maalum ambayo itawasaidia hasa katika kujiepusha na matukio ambayo yanaweza kuathiri usalama wao.

Alisema kwani wameshajua athari za kukaa karibu na miundombinu ya umeme  na  kuahidi kushirikiana na TANESCO katika kuwafichua wanaolihujumu Shirika kwa kuiba umeme na kuharibu miundombinu ya Shirika.

Aidha Bw. Kiongo alimuhakikishia Mkuu wa mkoa kuwa wao kama watu wenye ulemavu ni kama watu wengine, ni mara chache kusikika wasioona ikiwa na sifa ya kuliibia shirika la umeme na watakuwa mabalozi wa kuhakikisha Tanesco haiujumiwi ili kukuza kipato chake kwa maendeleo ya Shirika na Taifa kwa ujumla

Mwisho.


Share:

Chama cha Walimu Tanzania Kujenga Kiwanda Cha Mikate Lishe Simiyu

Na Stella Kalinga, Simiyu RS
Chama cha Walimu Tanzania (CWT) kinatarajia kujenga kiwanda cha mikate lishe kupitia kampuni yao inayosimamia Maendeleo ya Walimu ya biashara (TDCL), katika eneo la Ng’hami wilayani Maswa mkoani Simiyu.

Akimkabidhi  Katibu wa Chama cha Walimu Nchini, Mwl. Deus Seif hati ya kiwanja chenye ukubwa wa hekari mbili (2), Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe amesema wilaya imetoa kiwanja hicho bure, ikiwa ni moja ya njia ya kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya viwanda ambapo kumhakikishia upatikanaji wa malighafi ya kiwanda hicho (viazi lishe)

“Tumejipanga kuzalisha viazi lishe vya kutosha vitavyotumika kama malighafi ya kiwanda hiki na tayari wakulima wamepewa mbegu za viazi hivyo, niendelee kuwakaribisha CWT wilayani Maswa, kama kuna uwekezaji mwingine mnahitaji kufanya karibuni, hata kama ni tawi la benki yenu ile ya walimu tunawakaribisha sana,” alisema Dkt. Shekalaghe.

Kwa upande wake Mkuu wa mkoa wa Simiyu amesema kukamilika kwa kiwanda hicho kutasaidia kupunguza tatizo la ukosefu wa lishe ambalo limekuwa ni changamoto kwa  Mkoa wa Simiyu.

Aidha, Mtaka amesisitiza Mkuu wa Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashautri na wataalam wa kilimo wahakikishe mbegu ya viazi lishe inapatikana kwa wingi ili wananchi wanapohitaji waipate

 Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania(CWT) Taifa, Mwl. Deus Seif amesema chama hicho kinaunga mkono sera ya Tanzania ya Viwanda huku akibainisha kuwa ujenzi wa kiwanda hicho utaenda haraka kwa kuwa tayari kampuni ya CWT inayosimamia miradi imeshaanza kulifanyia kazi suala hilo.

Ameongeza kuwa pamoja na kujenga kiwanda cha mikate lishe, chama hicho pia kinatarajia kuchukua uwakala katika Kiwanda cha Chaki cha Maswa ili kusambaza chaki zinazozalishwa wilayani humo katika shule zote nchini.


Share:

Kampeni Ya Elimu Kwa Mlipakodi Kuanza Kesho Dar

Na Veronica Kazimoto, Dar es Salaam
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), inatarajia kuanzisha Kampeni ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi katika Mkoa wa Dar es Salaam itakayodumu kwa siku 13 kuanzia kesho tarehe 2 hadi 14 Desemba, 2019.

Akizungumzia kampeni hiyo leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Idara ya Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo amesema kuwa lengo ni kutoa elimu kuhusu masuala mbalimbali ya kodi pamoja na kusikiliza malalamiko, changamoto na kupokea maoni kutoka kwa wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla.

"Kampeni hii ni mwendelezo wa kampeni ambayo imemalizika katika Mikoa ya Morogoro na Pwani na sasa tunaingia katika Mkoa wa Dar es Salaam tukiwa na lengo la kuwaelimisha walipakodi na wananchi masuala yanayohusu kodi, kupokea maoni yao, kusikiliza changamoto na malalamiko ili tuweze kuyatafutia ufumbuzi", alisema Kayombo.

Kayombo ameongeza kuwa kampeni hiyo itaambatana na huduma ya usajili wa wafanyabiashara wapya wasiokuwa na Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi yaani TIN.

"Pamoja na kutoa elimu ya kodi, kupokea maoni na kusikiliza changamoto za walipakodi pia tutatoa huduma ya usajili wa walipakodi wapya ambapo tutawapatia cheti cha Namba ya Utambulisho wa Mlipakodi tukiwa na dhumuni la kupanua wigo wa walipakodi hapa nchini", aliongeza Kayombo.

Mkurugenzi Kayombo amebainisha maeneo ambayo yatafikiwa katika kampeni hiyo kuwa ni Ilala, Kinondoni, Temeke na Kariakoo na itafanyika kwa njia ya semina katika vituo vilivyopangwa kwenye maeneo hayo pamoja na kuwatembelea walipakodi katika biashara zao yaani duka kwa duka.

MWISHO.


Share:

WENYEVITI WAPYA WA VIJIJI NA VITONGOJI JIMBO LA KISESA MKOA WA SIMIYU WAAPISHWA, MBUNGE MH. LUHAGA MPINA AWATAKA WAKATAMBUE MAHITAJI YA WANANCHI, KUTANGAZA MAFANIKIO YA RAIS DK. JOHN POMBE MAGUFULI

 Wenyeviti wa Vijiji, Vitongoji na wajumbe wao kutoka Jimbo la Kisesa wilayani Meatu Mkoa wa Simiyu wakila kiapo cha utii  kwenye hafla iliyofanyika Mwandoya Makao Makuu ya Jimbo la Kisesa.
 Wenyeviti wote wa Vijiji vya Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu wakiwa katika picha ya pamoja muda mfupi baada ya kuapishwa.
 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Ikigijo Kata ya Mwabusalu Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Itinje Kata ya Itinje Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo

  Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Lingeka  Kata ya Lingeka Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha  Matale Kata ya Tindabuligi Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha  Mbugayabahnya Kata ya  Mbugayabahnya Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo

 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Mwashata  Kata ya  Mwabuma Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
 Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Ntobo  Kata ya Kisesa  Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
  Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Nyanza  Kata ya Mwakisandu  Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo
Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha Semu  Kata ya Isengwa  Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo

Wajumbe wa Serikali ya Kijiji cha  Ming’ongwa Kata ya Sakasaka  Jimbo la Kisesa Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu baada ya kula kiapo

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumapili December 1















Share:

Saturday 30 November 2019

SERIKALI YAANZA MCHAKATO WA KUPANDIKIZA FARU WEUPE NCHINI KWA MARA YA KWANZA


Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.Khamis Kigwangala  akiwa na baadhi ya wasanii wa muziki na filamu katika hifadhi ya Burigi Chato

Na Ashura Jumapili - Malunde 1 blog 

WIZARA ya Maliasili na Utalii ipo katika mchakato wa kupandikiza Wanyama zaidi wa aina mbalimbali katika hifadhi mpya ya Taifa ya Burigi Chato wakiwemo Faru weupe ili iweze kuwa kivutio kwa watalii mbalimbali ambao wameanza kutembelea hifadhi hiyo.

Akiongoza zoezi la utalii wa kutembea kwa miguu akiwa amefuatana na wasanii wa muziki na filamu katika hifadhi hiyo, mpya iliyopo katika mikoa ya Kagera na Chato Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.Khamis Kigwangala amesema kwa mara ya kwanza Serikali ya Tanzania imeamua kupandikiza Faru weupe katika hifadhi ya Burigi Chato.

Alisema utatifi bado unaendelea wa kuangalia namna ambavyo Faru hao weupe wataweza kuishi katika hifadhi hiyo kwa sababu hawakuwahi kuwepo kabisa hapa nchini.

Alisema ,Asili ya Faru weupe wanazaliana kwa wingi na kwa haraka hivyo wakipandikizwa katika hifadhi hiyo watasaidia sana kukuza idadi ya Faru weupe katika nchi na pia kuendelea kuwahifadhi kwa faida ya dunia nzima.

Pia alisema utafiti wa kupandikiza Faru weusi katika hifadhi hiyo umekamilika na malisho yapo ya kutosha na kudai kuwa asili ya hifadhi ya Burigi Chato ni nchi ya Faru historia inaonyesha kulikuwa na Faru wengi.

Alisema pia wamesha peleka familia moja ya Simba kutoka hifadhi ya Serengeti Mkoani Mara na kudai kuwa bado wapo kwenye uzio na wataachiwa rasmi baada ya wiki mbili.

 Msanii wa filamu Steven Mengele maarufu kama (Steve Nyerere) alisema hifadhi ya Burigi Chato ilichelewa sana lakini awamu ya tano imewekezekana chini ya msimamizi wake Khamis Kigwangala na wizara nzima ya maliasili na utalii.

Mengele,alisema Burigi Chato ndio mbuga ya kwanza yenye Twiga warefu na weusi pia ina kila vivutio alivyowahi kuviona.

Single Mtamabile,maarufu kama (Rich )alisema kutembelea hifadhi unapata uzoefu mkubwa sana katika mambo ya uhifadhi wa mazingira na utalii.

“Sisi wenyewe tulikuwa tunaona ni kawaida lakini tulipofika katika hifadhi hii ya Burigi Chato tumeona na kujifunza vitu vingi katika masuala ya Utalii”,alisema Mtambalike.

Alisema kujenga tabia ya kutembelea hifadhi za Taifa unakuwa unalinda asili yako na rasiliamali za nchi kwa kufika kujifunza na kuelewa namna ya kuendelea kutunza na kuhifadhi mazingira.
Share:

Picha : SHIRIKA LA FIKRA MPYA LAENDESHA KONGAMANO KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA




Shirika lisilo la kiserikali liitawalo Fikra Mpya la Mkoani Shinyanga, linalofanya shughuli ya kutoa elimu ya kujitambua kwa mtoto wa kike, limeendesha Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanafunzi wa kike kutoka Shule za Sekondari Nane Mjini Shinyanga.


Kongamano hilo limefanyika leo Novemba 30, 2019, kwenye ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Ualimu mjini Shinyanga (Shycom), na kuhudhuriwa na wadau mbalimbali wa maendeleo, wakiwemo maofisa ustawi jamii, maendeleo, dawati la jinsia kutoka polisi, walimu, pamoja na wazazi.

Mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya Leah Josiah, amesema wameendesha Kongamano hilo kwa wanafunzi wa kike, ili kutoa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia, ikiwemo kutokomeza tatizo la mimba na ndoa za utotoni, ambalo limekuwa likizima ndoto za wanafunzi walio wengi.

Amesema wameendesha Kongamano hilo kama sehemu ya kuadhimisha siku 16 za kupinga Ukatili wa kijinsia, ambayo ilianza kuadhimishwa Novemba 25 mwaka huu na itahitimishwa Desemba 10, kwa kufanya mijadala mbalimbali ya kujadili namna ya kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto na wanawake.

“Shirika letu tumeamua kuendesha Kongamano hili la kupinga vitendo ya ukatili wa kijinsia kwa wanafunzi wa kike, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha siku 16 za kupinga ukatili wa kijinsia, ambapo tunajadili kwa pamoja na wanafunzi ili kupata suluhu ya kutokomeza ukatili na wanafunzi wapate kutimiza ndoto zao,” amesema Josiah.

“Mkoa wetu wa Shinyanga na Kanda ya ziwa inatajwa kuongoza kwa vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto na wanawake, ambapo takwimu zinaonyesha kuanzia Januari hadi Juni 2019 kanda ya ziwa inaongoza kwa asilimia 38, ikifuatiwa na mikoa ya nyanda juu kusini asilimia 32, Pwani asilimia Tisa (9),

“Kanda ya kaskazini asilimia Tisa (9), Kanda ya Kati asilimia Saba (7), pamoja na Kanda ya Magharibi asilimia Tano (5),”ameeleza Josiah.

Naye mgeni Rasmi kwenye Kongamano hilo Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Kamara Beda, akimwakilisha mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, amewataka wanafunzi wanapokuwa wakifanyiwa vitendo vya ukatili wasikae kimya, bali watoe taarifa ili wahusika wapate kuchukuliwa hatua na kukomesha vitendo hivyo.

Nao baadhi ya wanafunzi akiwemo Mariamu Charles kutoka Shule ya Sekondari Mwasele, wameshukuru kuendeshwa kwa Kongamano hilo, ambalo wamedai limewasaidia kuwapatia upeo namna ya kupinga vitendo ya ukatili wa kijinsia, pamoja na wapi pa kwenda kutoa taarifa hizo.


TAZAMA MATUKIO KATIKA PICHA HAPA CHINI

Mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya Mkoani Shinyanga Leah Josiah akizungumza kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia leo Jumamosi Novemba 30,2019. Picha zote na Marco Maduhu - Malunde 1 blog

Mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya Mkoani Shinyanga Leah Josiah akizungumza kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Mgeni Rasmi Afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Kamara Beda akimwakilisha mkuu wa wilaya ya Shinyanga Jasinta Mboneko, akizungumza kwenye Kongamano la Kupinga ukatili wa kijinsia.

Wanafunzi wakiwa kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Wanafunzi wakiwa kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Wanafunzi wakiwa kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Wageni waalikwa wakiwa kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Mratibu kutoka Shirika la Women Fund Tanzania Mkoani Shinyanga Glory Mbia, akifungua mjadala wa kujadili juu ya vitendo vya ukatili wa kijinsia na kutafuta suluhu ya kuvitokomeza.

Mwenyekiti wa baraza la watoto manispaa ya Shinyanga Rose Matiku akichangia mada kwenye Kongamano hilo la kupinga ukatili wa kijinsia.

Afisa wa Jeshi la Polisi kutoka dawati la Jinsia wilaya ya Shinyanga Joseph Christopher, akichangia mada kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia, wakwanza kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya Leah Josiah.

Mzazi Aida Luben akichangia mada kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Mwandishi wa habari Isack Edward kutoka Radio Faraja, akichangia mada kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia namna vyombo vya habari vinavyosaidia kutoa elimu ya kutokomeza matukio hayo.

Mwanafunzi Verynice Busanga kutoka Shule ya Sekondari Mwasele, akichangia mada kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Mwanafunzi Mariam Charles kutoka Shule ya Sekondari Mwasele akichangia mada kwenye Kongamano hilo la kupinga ukatili wa kijinsia.

Awali wanafunzi wakiingia kwa maandamano kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa Kijinsia.

Mgeni Rasmi afisa tawala wa wilaya ya Shinyanga Kamara Beda akipokea maandamano kwenye Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Wageni waalikwa wakiwa na mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya wakipiga picha ya pamoja mara baada ya kumaliza Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.

Wageni waalikwa, wanafunzi pamoja na mkurugenzi wa Shirika la Fikra Mpya ,wakipiga picha ya pamoja mara baada ya kumaliza Kongamano la kupinga ukatili wa kijinsia.


Picha zote na Marco Maduhu- Malunde 1 Blog
Share:

SIMBA SC YAMTIMUA KOCHA PATRICK AUSSEMS

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger