Thursday 28 November 2019

Video Mpya : PUMARIO - MY LOVER LOVER

Video mpya ya Msanii Pumario inaitwa My Lover Lover

Share:

MSHINDI WA PROMOSHENI YA TIGO CHEMSHA BONGO APATIKANA


Mtaalam wa Huduma za ziada-Tigo, Fabian Felician na Jehud Ngolo- Afisa Mwandamizi Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania. wakimpigia simu Shaban Khamis Ali,mkaazi wa Zanzibar, mshindi wa promosheni ya Tigo Chemsha bongo
Mtaalam wa Huduma za ziada-Tigo, Fabian Felician na Jehud Ngolo- Afisa Mwandamizi Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania. wakimpigia simu Shaban Khamis Ali,mkazi wa Zanzibar, mshindi wa promosheni ya Tigo Chemsha bongo

****
Droo ya mwisho ya promosheni ya ‘Tigo Chemsha Bongo’ imefanyika jijini Dar es Salaam ambapo mkaazi wa Zanzibar, Shabani Khamis Ali (48) amejishindia gari mpya aina ya Renault KWID yenye thamani ya 23m/-. Khamis akiongea baada ya kupigiwa simu na Mtaalam wa Huduma za Ziada kutoka Tigo, Fabian Felician, kumfahamisha kuwa ameibuka mshindi, alisema anayo furaha kufanikiwa kuwa miongoni mwa washindi kupitia promosheni hiyo kwa kujishindia gari mpya. 

“Sikutegemea kabisa kuwa ningeibuka mshindi katika promosheni hii, Habari hizi naziona kama ndoto kwangu, nashukuru Tigo kwa kunifungia mwaka vizuri na kutimiza ndoto yangu ya kumiliki gari, kwani itanisaidia katika mizunguko yangu ya kibiashara “alisema kwa furaha. 

Mtaalam wa Huduma za Ziada kutoka Tigo, Fabian Felician, alimpongeza mshindi huyo na kutumia fursa hiyo kuwashukuru wateja wote wa kampuni ambao walishiriki na baadhi yao kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo zawadi za fedha taslimu ambayo yalitolewa na kampuni hiyo. 

“Tunayo furaha kubwa katika kipindi hiki tunachoelekea katika msimu wa sikukuu kumpata mshindi wetu wa gari ya aina Renault Kwid,yenye thamani ya 23m/-, gari hili ni jipya kabisa, baada ya kumpata mshindi taratibu zengine zitafata ili tuweze kumkabidhi Shaban Khamis Ali gari lake jipya. Tunawashukuru wateja wetu kutoka nchini pote walioshiriki kwenye promosheni hii ya miezi mitatu ambayo imemalizika mwishoni mwa mwezi wa Novemba 2019”. alisema Felician. 

Aliongeza kuwa, promosheni hii ambayo ilianza jijini Mwanza katika msimu wa Tigo Fiesta 2019-Saizi Yako  imepata mafanikio makubwa kutokana na wateja wengi kujitokeza kushiriki na baadhi yao kufanikiwa kujishindia zawadi(fedha taslim) mbalimbali na hivyo Tigo kufanikisha lengo lake ambalo lilikuwa ni kuwashukuru wateja kwa kuiunga mkono kampuni kupitia kununua bidhaa zake mbalimbali. 

Kwa kumalizia Felician aliwashukuru wateja wote wa Tigo kwa kuendelea kuunga mkono kampuni na kuahidi kuwa promosheni mbalimbali za kunufaisha wateja wa kampuni hiyo zinatendelea kubuniwa katika siku za usoni.


Share:

Jumuiya ya Afrika Mashariki yasaini mkataba wa EURO milioni 10 na umoja wa nchi za Ulaya Ili Kusaidia Kuimarisha Usalama

Jumuiya ya Afrika  Mashariki imesaini mkataba wa EURO milioni 10  na umoja wa nchi za Ulaya  kwa ajili ya kuimarisha ulinzi na usalama katika nchi uanachama wa jumuiya hiyo.
 
Mkataba huo umesainiwa  jana katika ofisi za makao makuu ya jumuiya hiyo  na Katibu mkuu wa jumuiya ya Afrika Mashariki ,Liberat Mfumukeko  na Balozi  wa umoja wa nchi za Ulaya Tanzania ,Manfredo Fanti.
 
Akizungumza wakati wa kusaini mkataba huo ,Katibu mkuu wa EAC ,amesema kuwa, fedha hizo zimetolewa na jumuiya ya umoja  huo ili kuziwezesha nchi wanachama kukabiliana na changamoto ya usalama ambayo imekuwa na kikwazo kikubwa Cha maendeleo katika nchi hizo.

Ameshukuru jumuiya hiyo kwa msaada huo ambao umekuja muda muafaka na kuongeza kuwa, jumuiya hiyo itaendelea kushirikiana kwa ukaribu Sana katika nyanja mbalimbali za maendeleo.
 
Hata hivyo ,Mfumukeko amesema kuwa,jumuiya hiyo ya nchi za Ulaya wamekuwa washirikiana kwa muda mrefu na jumuiya hiyo ambapo katika kipindi cha miaka mitano wamekwisha kutoa kiasi Cha EURO milioni  85 .

“Umoja wa Ulaya wamekuwa washirika muhimu katika kusukuma mbele ajenda ya mtangamano wenye lengo la kuwawezesha kiuchumi, ipo miradi mbalimbali ambayo imefadhiliwa na EU tangu mwaka 2007 ambayo imekua na matokeo chanya kwa wananchi wetu.

“Programu hii ambayo tumeizindua itasaidia kupunguza nafasi ya kushamiri kwa uhalifu unaovuka mipaka ya nchi moja kwenda nyingine ambayo unaweza kutishia mchakato wa mtangamano, pia itasaidia kuendeleza sera na utekelezaji wake, uwajibikaji kisiasa na uimarishaji wa taasisi,” amesema Mfumukeko. 

 
Kwa upande wake ,Balozi wa jumuiya ya umoja wa Ulaya nchini Tanzania,Manfredo Fanti amesema kuwa, wataendelea kusaidia jumuiya hiyo katika maswala mbalimbali ya maendeleo .
 
“Tumekuwa tukisaidia jumuiya ya Afrika Mashariki katika miradi mbalimbali tangu mwaka 2007 ambayo imeleta manufaa makubwa kwa wananchi wa nchi hizo na kuondokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili.”amesema Balozi huyo.


Share:

CHAMA CHA WAAJIRI ATE: KUJISAJILI WCF NI LAZIMA SIO HIARI

NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
MKURUGENZI Mtendaji wa Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), Dkt. Aggrey Mlimuka amewaambia waajiri nchini kuwa kujisajili na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi sio hiari bali ni lazima.
Dkt. Mlimuka ameyasema hayo Alhamisi Novemba 28, 2019 jijini Dar es Salaam wakati akifungua mafunzo ya siku moja yaliyoandaliwa na ATE na kuwaleta pamoja waajiri kutoka sehemu mbalimbali nchini ili kujifunza kuhusu masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi.
“Naomba tuelewane toka mapema, siyo hiari kujiunga na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi hilo ni takwa la kisheria Mfuko huu uko pale kisheria na ni vema likaeleweka mapema.”Alisema Dkt. Mlimuka
Alisema Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) kiko kwa maslahi ya waajiri lakini pia kwa maslahi ya waajiriwa (wafanyakazi) kwani wameajiriwa ili kufanya shughuli mbalimbali na wanaweza kuumia au kupatwa na madhara yoyote wakati wakitekeleza majukumu yao na ndio maana upo Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi ambao umeundwa maalum kushughulikia masuala hayo.
“Niwashukuru sana viongozi wa WCF  kwa kuja hapa leo kutupatia mafunzo,  sisi waajiri tutanufaika vya kutosha na mafunzo haya ambayo yataweza kujibu maswali yaliyo mengi kutokana na changamoto mbalimbali.” Alibainisha Dkt. Mlimuka.
Alisema,hapo zamani malipo ya Fidia kwa Mfanyakazi aliyeumia yalikuwa kidogo sana, na ndio maana Serikali ikaanzisha Mfuko huu ambao umesaidia sana katika kutatua changamoto zilizokuwa zikitukabili kutokana na masuala ya Fidia.
Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF),  Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Dkt. Abdulsalaam Omary alisema, Waajiri wanao wajibu wa kuhakikisha usalama wa wafanyakazi wao unapewa umuhimu wa kwanza na ndio maana WCF inatoa elimu mara kwa mara.
“Ifahamike kuwa sisi WCF wajibu wetu wa msingi ni kulipa fidia stahiki na kwa wakati kwa mfanyakzi aliyeumia, kuugua au kufariki wakati akitekeleza wajibu wake wa kazi… kusajili na kupokea michango kutoka kwa waajiri walio katika sekta ya umma na binafsi Tanzania Bara, lakini pia tunalo jukumu la kisheria la kukuza mbinu za kuzuia ajali na vifo kazini kwa kutoa elimu kwa waajiri lakini pia wafanyakazi wenyewe na hiki ndicho tunachokifanya hapa leo.” Alisema Dkt. Omary wakati akiwasilisha mada yake ya namna ya kudai Fidia.
Washiriki hao walipatiwa mafunzo mbalimbali yakiwemo Sheria iliyoanzisha Mfuko, Kujisajili na jinsi ya kuwasilisha michango WCF na namna ya kuwasilisha madai ya Fidia, lakini pia Mafao yanayotolewa na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), Dkt. Aggrey Mlimuka, akitoa hotuba ya ufunguzi wa mafunzo kuusu masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi yaliyotolewa kwa Waajiri kutoka sehemu mbalimbali nchini na kufanyika jijini Dar es Salaam Novemba 28, 2019.
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE), Dkt. Aggrey Mlimuka (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. Abdulsalaam Omary, mara baada ya kutoa hotuba.
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. Abdulsalaam Omary, akizungumza mwanzoni mwa mafunzo ya siku moja kuhusu masuala ya Fidia kwa Wafanyakazi kwa wanachama wa Chama Cha Waajiri Tanzania (ATE) jijini Dar es Salaam Novemba 28, 2019.
 
 Bw, Deo Ngowi kutoka kitengo cha Sheria Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), akiwasilisha mada kuhusu Sheria iliyoanzisha Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi.
 Bw.Pascal Rischard kutoka Kitengo cha Usajili na Uwasilishaji Michango WCF, akiwasilisha mada kuhusu namna ya kujisajili na kuwasilisha michango kupitia Portal ya WCF
Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini, Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Dkt. Abdulsalaam Omary,
Meneja Madai Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF), Bi. Rehema Kabongo, akiwasilisha mada kuhusu Mafao yatolewayo na WCF.

 Baadhi ya washiriki w asemina wakifuatilia mafunzo hayo.
 Baadhi ya washiriki w asemina wakifuatilia mafunzo hayo.
 Baadhi ya washiriki w asemina wakifuatilia mafunzo hayo.
 Maafisa wa juu wa WCF, kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano, Bi. Laura Kunenge, Bw. Deo Ngowi kutoka Kitengo cha Sheria na Bw. Pascal Richard kutoka Kitengo cha Usajili na Uwasilishaji Michango WCF
Baadhi ya washiriki w asemina wakifuatilia mafunzo hayo.
Share:

Marekani Yawaunga mkono waandamanji Hong Kong, China Yatishia Kulipiza Kisasi

Rais wa Marekani Donald Trump amesaini muswada wa kuunga mkono vuguvugu la maandamano ya kudai demokrasia mjini Hong Kong na kuwa sheria licha ya pingamizi kutoka kwa serikali ya China. 

Sheria hiyo ambayo iliungwa mkono kwa sauti moja bungeni, inahitaji Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani kuthibitisha angalau kila mwaka kwamba uhuru wa Hong Kong haukutatizwa. 

Bunge la Marekani pia limepitisha muswada wa pili - ambao Rais Trump pia ameusaini - unaopiga marufuku usafirishaji na uuzaji wa silaha za kudhibiti maandamano ya umma kwa vikosi vya usalama vya Hong Kong kama vile, mabomu ya kutoa machozi, dawa ya pilipili, risasi za mpira pamoja na bunduki za kutoa mshtuko wa umeme. 

China ilimuonya Trump wiki iliyopita kuwa itachukua hatua za kulipiza kisasi iwapo atasaini miswada hiyo na kuwa sheria.


Share:

Nafasi 62 za Kazi TANESCO | Wanahitajika watu wa Customer Care

Nafasi 62 za Kazi TANESCO | Wanahitajika watu wa Customer  Care 
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

👉Mwisho wa Kutuma maombi ni; 11/12/2019
👉Elimu ni  Diploma ya Marketing, Public Relations au  Business Administration 
👉Mwenye Elimu Kidogo ya Computer atapewa Kipaumbele
👉Uzoezi ni Mwaka mmoja
▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬▬

==>>Kujua namna ya kutuma maombi <<INGIA HAPA>>


Share:

Tanzania Mwenyeji wa Mkutano wa JPC na Namibia




Share:

MBUNGE BALOZI ADADI AISHUKURU SERIKALI KUWASAIDIA KUWEKA LAMI KWENYE MJI WA MUHEZA

 MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu akizungumza wakati wa halfa ya utiliaji saini  ya kati ya Halmashauri ya Muheza na Mkandarasi wa Kampuni ya ujenzi ya SIMAC Limited kutoka Dar kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara za mita 800 kwenye mji huo kwa kiwango cha lami kulia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Nassib Mbaga na kushoto ni Meneja wa Tarura wilaya hiyo Mhandisi Joseph Kahoza
 Mkurugenzi wa Halmashauri ya Muheza Nassib Mbaga akizungumza wakati wa halfa hiyo kushoto ni Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kulia ni Katibu  wa CCM wilaya ya Muheza Mohamed Moyo 
 Meneja wa Tarura wilaya hiyo Mhandisi Joseph Kahoza akizungumza wakati wa halfa hiyo kulia ni Mbunge wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajab
 MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu akimkabidhi nyaraka na michoro mkandarasi wa kampuni ya ujenzi SIMAC LTD kutoka Dar Felix Chawe mara baada ya kusaini nae mkataba kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara za mita 800 katika mji wa Muheza
 
 MBUNGE wa Jimbo la Muheza kushoto Balozi Adadi Rajabu (aliyevaa suti) akisisitiza jambo kwa mkandarasi wa ujenzi huo mara baada ya kutembelea eneo ambalo ujenzi huo utafanyika 
 MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu kushoto akimsikiliza Katibu wa CCM wilaya ya Muheza Mohamed Moyo kulia wakati walipotembelea barabara ya sokoni wilayani humo 


MBUNGE wa Jimbo la Muheza (CCM) Balozi Adadi Rajabu ameishukuru serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Magufuli kuwasaidia kuweka lami baadhi ya barabara zilizopo kwenye mji huo.

Huku akiwataka wananchi wilayani humo kumpa ushirikiano mkandarasi ambaye anatekeleza ujenzi huo ili aweze kutekeleza kazi yake kwa wakati kutokana na kwamba amepewa muda wa miezi saba. 


Balozi Adadi aliyasema hayo wakati wa halfa ya utiaji wa saini kati ya kati ya Halmashauri ya Muheza na Mkandarasi wa Kampuni ya ujenzi ya SIMAC Limited kutoka Dar kwa ajili ya kuanza ujenzi wa barabara za mita 800 kwenye mji huo. 


Alisema kwamba utiliaji saini huo umeonyesha namna serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuhakikisha inaboresha miundombinu kwenye miji mbalimbali hapa nchini.

Mbunge huyo alisema kwamba barabara ni kilomita ya pili ambayo itaanzia Kilimanjaro Bar, Darajani, relini mpaka hospitali ya Teule Muheza na baadae kufika mpaka kwenye kipande ambacho kinatumika na wananchi kwenye maeneo ya karibu na soko la Muheza.

“Serikali ya awamu ya tano imeweza kutusaidia kuweka lami ni jambo kubwa na la faraja kubwa kwetu hivyo kwa sababu lami itawekwa kwenye mji wetu hakikisheni mnapa ushirikiano na niwaombe msimpe vikwazo vya namna yoyote ile “Alisema Balozi Adadi. 


Awali akizungumza wakati wa halfa hiyo Meneja wa Tarura wilaya ya Muheza Mhandisi Joseph Kahoza alisema kwamba mkandarsi aliyekabidhi mkataba huo ni wa barabara za mita 800 kwa ajili ya kuweka lami kwa mji wa muheza.

Alisema mkandarasi huyo ataanza kufanya kazi hiyo kuanzia barabara ya Kilimanjaro darajani, relini mpaka teule ambao utakuwa na thamani ya milioni 386 huku akieleza barabara nyengine ya mita 200 zinazokarabatiwa mjini humo zitatumia zaidi ya milioni 60..

Naye kwa upande wake Mkandarasi wa kampuni ya ujenzi SIMAC LTD kutoka Dar Felix Chawe ambao wamekabidhiwa barabara hiyo alisema kwamba anajisikia furaha kupata nafasi ya ujenzi huo huku akihitaji ushirikiano na kuhaidia kufanya kazi kwa uwezo wake wote na maelekezo yaliyopo kwenye mkataba.

Mwisho.
Share:

Baada ya Rais Magufuli Kupiga Marufuku Halmashauri Kukopa, Waziri Jafo Awapa Wiki Moja Wakurugenzi Kumpa Taarifa Za Mikopo

Na.Alex Sonna/FullShangwe
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo,amezitaka halmashauri zote nchini kutoa taarifa Ofisini kwake  juu ya uchukuaji wa mikopo kutoka mabenki ya kibiashara.

Agizo hilo Mhe.Jafo amelitoa leo ofisini kwake jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Mhe. Jafo amesema kuwa wale wote waliochukua mikopo na hawajaanza kuitumia wairudishe haraka ipasavyo kwani Taasisi zote za Serikali zikiwemo mamlaka za Serikali za Mitaa hazitakiwi kuchukua mikopo kutoka mabenki ya kibiasha.

“Hayo ni maelekezo kutoka katika walaka wa Barua ya Katibu Mkuu Hazina barua ya tarehe 13 /12/2016 barua yenye kumbu kumbu namba CBC.155/233/01 kuwa taasisi zote za serikali na mamlaka za serikali hazipashi kuchukua mkopo kutoka benki za kibiashara” Amesisitiza Mhe.Jafo

Aidha  Mhe.Jafo amesema kuwa halmashauri yoyote itakayo wasilisha taarfa zisizo sahihi itachukuliwa hatua za kisheria.

“Hivyo wito wangu kwa  halmashauri hizo ni kuwasilisha taarfa sahihi kulingana na mikopo waliyo chukua kwani udanganyifu wowote utakao bainika kuwa kuna mikopo ya kimashaka mashaka ambayo haikufuata taratibu sahihi ofisi itachukua hatua mbali mbali za kisheria” amesema Mhe. Jafo

Hata hivyo Mhe.Jafo amemtaka Katibu Mkuu OR-TAMISEMI Mhandisi Joseph Nyamhanga kusimamia  wakurugenzi wake wote kuhakikisha wanafanya kazi kwa kanuni , sheria na taratibu za kazi zinavyowataka kufanya kazi ili kufikia malengo yanayotakiwa katika utendaji wao.

Jafo amesema kuwa baada ya halmashauri zote kuwasilisha taarfa hizo katika ofisi za TAMISEMI itafanya tathimini na kutoa maelekezo baada ya kupima taarfa zilizo wasilishwa.


Share:

Upembuzi Yakinifu Ujenzi wa Reli ya Kuunganisha Tanzania na Rwanda Wakamilika

Tanzania na Rwanda zinakamilisha mchakato wa ujenzi wa reli itakayounganisha mataifa hayo mawili ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Hayo yamesemwa  Jana Jumatano November 27, 2019 na Rais Magufuli wakati akizungumza na wananchi wa Isaka Mkoani Shinyanga.

“Nimeshazungumza na Rais Kagame (Paul wa Rwanda) kuhusu utekelezaji wa mradi huu, upembuzi yakinifu umekamilika. Kinachofanyika sasa ni kutafuta fedha,” alisema Rais Magufuli. 

Reli hiyo itakayounganishwa na ile ya kati itaanzia bandari kavu ya Isaka wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.

Mradi huo ambao tayari hatua ya upembuzi yakinifu umekamilika utarahisisha usafirishaji wa mizigo kutoka bandari kavu ya Isaka kwenda nchi jirani.


Share:

Scholarship Mpya Kwa Watanzania | Commonwealth Shared Scholaships Tenable In The United Kingdom 2020

1.0 Call for Applications
The General public is hereby informed that, the Government of United Kingdom has opened a new Commonwealth Shared Scholarship to eligible Tanzanians to pursue Masters Studies in the United Kingdom for the academic year 2020. Interested candidates are highly encouraged to apply under the following six themes:-

1.Science and technology for development;
2.Strengthening health systems and capacity;
3.Promoting global prosperity;
4.Strengthening global peace, security and governance;
5.Strengthening resilience and response to crises; and
6.Access, inclusion and opportunity.

Further details on the eligible study Programmes can be accessed through the following link

2.0 Mode of Application
The online application system can be reached through the following link:<<BOFYA HAPA>>

Before making an online application you are advised to read the following guidelines found in the following link: <<CLICK HERE TO DOWNLOAD PDF>>

3.0 Submission
All applications must be submitted by 16.00 (GMT) on 18th December 2019 
 
Note:
It is important that applicants should read and understand all instructions when filling the application forms, attach all the required documents such as certified copies of academic certificates, transcripts, and birth certificates and submit them online through the above link.


Share:

Zaidi Ya Wakulima 500,000 Wamejengewa Uwezo Chini Ya Mfumo Shirikishi Wa Udhibiti Ubora Kwa Ajili Ya Soko La Ndani Na La Jumuiya Ya Afrika Mashariki

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Nchi mbalimbali Duniani zinajadili na kuweka mikakati ya kuendeleza kilimo-hai. Mwaka 2010, Umoja wa Afrika kupitia Marais wake, ulipitisha Azimio la mpango na mkakati wa kilimo-hai kuelekea ajenda yake ya miaka 50 ijayo (Agenda 2063), na kuzitaka nchi zote kuchukua hatua kutekeleza azimio hilo.

Katika kufikia azimio hili la Umoja wa Afrika, Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na wadau imefanikiwa kuwa na Sera ya Kilimo iliyohusisha kilimo-hai kwa upana wake na uwekezaji kwenye viwanda vinavyo chakata mazao ya kilimo-hai.

Hii inaenda sambamba na jitihada za Serikali ya awamu ya tano chini ya Mheshimiwa Rais John Pombe Joseph Magufuli ya kutaka Tanzania ifikie uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025 kupitia sera ya viwanda. Ambapo kumeanzishwa dawati la kilimo-hai katika idaya ya Maendeleo ya Mazao ili  kufikia idadi ya wakulima  na wafugaji 149,000 waliothibitishwa na kuingia katika fursa ya masoko ya bidhaa za kilimo-hai kimataifa, wanaozalisha kwenye eneo la hekta takribani 278,000.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyasema hayo jana tarehe 26 Novemba 2019 wakati akifungua kongamano la kitaifa la kilimo-hai la siku mbili linalofanyika Jijini Dodoma na kuongeza kuwa zaidi ya wakulima 500,000 wamejengewa uwezo chini ya mfumo shirikishi wa udhibiti ubora (participatory guarantee system - PGS) kwa ajili ya soko la ndani na la Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Ameongeza kuwa kilimo-hai Duniani katika mataifa mbalimbali kinakua kwa kasi kubwa. Inakadiriwa kuwa soko la bidhaa na mazao ya kilimo-hai duniani ni wastani wa Euro 89 bilioni ambapo hiyo ni fursa kubwa kwa kwa Tanzania kwani ni nchi ya tatu kati ya tano barani Afrika zinazoongoza kwa kuwa na eneo na idadi kubwa zaidi zilizo thibitishwa katika mfumo huo wa kilimo-hai, ikiongozwa na Uganda na Ethiopia na kufuatiwa na Kenya na Jamhuri ya Kidemokrsi ya Kongo (DRC).

Waziri Hasunga amesema kuwa kufuatia kupitishwa kwa mtaala mpya unaojumuisha stadi na programu za kilimo-hai katika vyuo vya mafunzo ya kilimo na vyuo vikuu kikiwemo SUA, inatarajiwa idadi hiyo ikiongezeka mara dufu. Vyama vikuu vya ushirika – KCU, KNCU na KDCU pamoja na makampuni kama Biore, Biosustain, Biolands na OLAM  wamewezesha nchi yetu kufikia mafanikio hayo.

Pia, ametoa mwito kwa wadau wa kilimo-hai nchini kufanya kazi kwa karibu na Wizara na Taasisi zake na Serikali yote kwa ujumla ili kwa pamoja kuwezesha upatikanaji wa uhakika wa chakula na lishe na masoko utakao boresha maisha ya watanzania walio wengi kwenye sekta ya kilimo.

Amesema kuwa baadhi ya changamoto katika kuendeleza kilimo-hai nchini ni pamoja na uhakiki (certification) wa mazao hayo kuwa ya kilimo hai, fedha kwa ajili ya uwekezaji katika kilimohai kibiashara, kutoyafikia masoko maalumu (niche market) hususani katika nchi za Ulaya kutokana na kutokidhi vigezo vya masoko hayo na tishio la mabadiliko ya tabianchi ambayo ni fursa katika kuendelea kilimohai nchini.

Waziri Hasunga amewahakikishia wadau wote waliohudhuria katika mkutano huo kuwa Wizara ya kilimo itaendelea kushirikiana nao kwa karibu hivyo wasisite kuwasilisha mapendekezo yao wakati wowote ili Serikali iyashughulikie kwa maslahi ya kuendeleza kilimo-hai nchini.

Kadhalika, amewasihi wadau wote kupitia kongamano hilo, kujadili na kuzitafutia ufumbuzi changamoto hizo ili kuweza kuongeza uzalishaji kupitia kilimo-hai.



Share:

Waziri Ummy Asema Serikali Inaendelea Na Mchakato Wa Kuboresha Sera Mpya Ya Afya

Na.Faustine Gimu Galafoni.Dodoma
Waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mhe. Ummy mwalimu amesema serikali inaendelea na mchakato wa kuboresha sera mpya ya afya  ili kuimarisha huduma  za afya nchini badala ya kuendelea na sera iliyopo kwasasa ambayo imepitwa na wakati.
 
Waziri Ummy amesema hayo  jana Nov.27,2019 jijini Dodoma wakati akifungua Kongamano  la sita la   afya nchini  lijulikanalo  “TANZANIA HEALTH SUMMIT “ambapo pamoja na mambo mengine ameendelea kusisitiza  dhamira yake ya kuwasilisha bungeni muswaada utakao lazimisha kila mtanzania kuwa na bima ya Afya.
 
Waziri Ummy amesema Sera ya Afya ya Mwaka 2017 imejikita zaidi katika masuala ya tiba na si kinga hivyo Sera Mpya ya mwaka 2019/2020 itajikita zaidi katika Masuala ya kinga kwani kinga ni bora kuliko tiba.

Aidha ,Waziri Ummy amesema katika sera Mpya ya Afya ya Mwaka 2019/2020 itaangalia mktadha wa kuwafikia wananchi huduma ya Afya yaani Afya kwa wote kwa kuangalia vigezo muhimu vya uhitaji  tofauti ya na sera ya iliyopo ambapo inasema zahanati kila kijiji bila kuangalia mzigo wa Magonjwa ama geografia ya eneo husika.

Kwa upande wake Rais wa Kongamano la Afya nchini Tanzania, Dokta Omary Chillo  amesema Lengo la kongamano hilo ni kujadili changamoto mbalimbali zilizopo katika sekta ya afya na namna ya kukabiliana nazo ili kuleta ufanisi zaidi katika utendaji kazi.

Kongamano la sita la Afya Mwaka 2019 limeanza Nov.27 hadi  28,2019  huku likiandaliwa na Taasisi  sita ambazo ni  Wizara ya Afya Tanzania,Wizara ya Afya  Upande wa Zanzibar ,Ofisi ya Rais TAMISEMI ,Tume ya Huduma za kijamii ya Kikristo,Baraza la Waislam Tanzania[BAKWATA]  na Tindwa Medical Services   na kaulimbiu ni ufanisi na Matokeo katika utoaji wa huduma za Afya.

Mwisho.


Share:

Benki Ya Biashara Na Maendeleo Mashariki Na Kusini Mwa Afrika Yaleta Neema Kwa Wafanyabishara Wa Tanzania

Na Josephine Majura, Dar es Salaam
Benki ya Biashara na Maendeleo Mashariki na Kusini mwa Afrika (TDB), imeahidi neema kwa Wafanyabiashara nchini kwa kuwapatia mikopo nafuu itakayowawezesha kusafirisha na kuuza bidhaa za kilimo nje ya nchi

Hayo yameelezwa na Mwakilishi wa Rais wa Benki ya Biashara na Maendeleo Mashariki na Kusini mwa Afrika (TDB), Bw. Lloyd Muposhi, wakati ujumbe wa Benki hiyo uliopo nchini kwa ziara ya kikazi, ulipokutana na  kufanya mazungumzo na  Wafanyabiashara wanaojihusisha na uuzaji wa mazao hayo nje ya nchi ikiwemo  nafaka, chai, kahawa na katani.

Bw. Muposhi, ameeleza kuwa mazungumzo kati ya pande hizo mbili yalikua mazuri yenye kujenga ambapo kwa mwaka ujao wa fedha ameahidi benki hiyo itawawezesha wafanyabishara ama sekta binafsi kimtaji ili waweze kukuza mitaji yao na kufanya biashara ya ushindani na yenye tija.

Kwa upande wake Mkurenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), Bw. Edwin Rutageruka ameishukuru Wizara ya Fedha na Mipango kwa kuratibu mkutano huo na kuwakutanisha Wafanyabiashara na Uongozi wa Benki ya Biashara na Maendeleo ambapo wamepata muda wakubadilishana uzoefu na kujadili mambo mbalimbali zikiwemo changamoto mbalimbali zinazokabili usafirishaji wa bidhaa nje ya nchi, uzoefu wa kufanya biashara pamoja na ukosefu wa mitaji.

Bw. Edwin alisema changamoto kubwa iliyopo kwa Wafanyabiashara wa ndani ni ukosefu wa mitaji kwa kuwa ni gharama kubwa  kusafirisha bidhaa kwenda nje ya nchi hivyo iwapo TDB wataanza kutoa ufadhili kwa Wafanyabiashara wa Tanzania watakuwa wamewasaidia sana kuondokana na tatizo hilo.

Naye mmoja wa Wafanyabiashara walioshiriki katika mkutano huo Mkurugenzi wa ALASKATANZANIA, Bi. Jennifer Bash ameipongeza Serikali kwa kuandaa mkutano huo kwani umetoa fursa ya kubadilishana uzoefu kati ya Wafanyabiashara hao na uongozi wa benki hiyo.

Alieleza kuwa changamoto kubwa inayowakabili Wafanyabiashara wengi ni uhaba wa fedha na mitaji hivyo mkutano huo umetoa mwanga kwao kwa kuwa wamezungumza mambo mengi ambayo iwapo yatatekelezwa yatapunguza ombwe lililopo la ufanisi wa biashara kwa wafanyabiashara wengi.

Mkutano huo umefanyika Dar es Salaam ambapo ulihusisha Uongozi kutoka Benki ya Biashara na Maendeleo Mashariki na Kusini mwa Afrika (TDB), Wataalamu kutoka Wizara ya Fedha na Mipango na Wataalamu kutoka Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE).


Share:

Rais Magufuli apiga marufuku halmashauri kukopa benki.

Rais Magufuli amewapiga marufuku Wakurugenzi  Watendaji wa Halmashauri zote nchini kuacha  mara moja kukopa fedha kwenye taasisi za fedha kwa madai ya kufanya miradi ya maendeleo.

Ametoa kauli hiyo Jumatano Novemba 27, 2019 wilayani Bukombe mkoani Geita wakati akihutubia mkutano wa hadhara, Rais Magufuli amewaagiza iwapo wapo ambao wameshachukua fedha hizo kuzirudisha na kuvunja mikataba waliyoingia.

“Kama kuna mkurugenzi yeyote amekopa fedha azirudishe, mwenye mamlaka ya kukopa kwa niaba ya Serikali ni paymaster general wa Serikali ambaye ni Wizara ya Fedha pekee.”

“Anayekopa ajiandae kutoka. Naamini Wakurugenzi wamenielewa, nimepita Kahama Mkurugenzi ananiambia anataka kukopa kutoka TIB (Benki ya Uwekezaji Tanzania) kwa ajili ya kujenga stendi, haiwezekani fedha za wananchi kuchezewa, ovyo”  alisema Rais Magufuli




Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Alhamisi November 28























Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger