Sunday 29 September 2019

Kituo Cha Uchenjuaji Dhahabu Jema Afrika Chapewa Onyo La Mwisho

Waziri wa Madini Doto Biteko ametoa Onyo la Mwisho la Kukifungia Kituo cha Uchenjuaji Dhahabu cha Jema Afrika kilichopo Wilayani Kahama.

Hatua hiyo inafuatia kubainika kwa jaribio la wizi wa dhahabu uliofanywa na baadhi ya wafanyakazi wa  kituo hicho kutaka kuiba dhahabu ya mteja.

Akizungumzia tukio hilo, Waziri Biteko amewataka wamiliki wa kituo hicho kuandika barua ya kuweka makubaliano na Serikali ya kutojirudia tena kwa vitendo  vya wizi kituoni hapo.

‘’Ni jicho la huruma tu  tukiwapeleka mahakamani mali zenu zitataifishwa. Tunajua mmewekeza mitaji yenu na mna mikopo.  Nilishamwambia mmiliki kuwa kituo  chako kina rekodi ya wizi. Rais anawapenda, anawapigania ili watanzania wamiliki uchumi wa madini lakini mnamuangusha kwa kutofuata taratibu,’’ amesisitiza Waziri Biteko.

Amewatahadharisha wamiliki wa vituo vya uchenjuaji nchini kuhusu wizi wote wa dhahabu  unaofanyika na kuwasisitiza kwamba, unafahamika na kuwataka  wote wanaojihusisha na vitendo hivyo  kujiepusha  na  kwa wale wasiotaka kufanya kazi zao kwa  uaminifu watafute biashara nyingine.

Mbali na kutembelea kituo hicho,  pia, Waziri Biteko  na ujumbe wake  wametembelea Kituo Kidogo cha  Ununuzi   wa dhahabu kilichopo katika eneo la Wachimbaji wadogo wa Mwime  ambapo amewapongeza kwa kufuata taratibu na Sheria na kuwataka kufanya kazi zao kwa amani.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga  Zainab Taleck amesema  Mkoa huo unahitaji wawekezaji lakini walio waaminifu.

Ameongeza kuwa, wizi na udanganyifu katika kiwand cha uchenjuaji Jema Afrika ulibainiwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama na kutumia fursa hiyo kuwatahadharisha wote wasiofuata taratibu kuwa serikali inawaona na itawafikia.

Katika ziara hiyo, Waziri Biteko pia ameongozana na Naibu Waziri wa Madini Stanslaus Nyongo, Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Shinyanga, Kamishna wa Madini Mhandisi David Mulabwa na Watalaam kutoka Tume ya Madini.

Aidha, ziara hiyo imefanywa wakati ambapo wizara na wadau wengine wa madini wanashiriki Maonesho ya Pili ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini Mkoani Geita yanayotarajiwa kuhitimishwa Septemba 29, 2019.

Ziara hiyo imefanyika Septemba 28, 2019


Share:

CHANJO ITAKAYOMALIZA MAAMBUKIZI MAPYA YA VIRUSI VYA UKIMWI 'HIV' KUZINDULIWA

Kituo cha udhibiti wa magonjwa na maambukizi kimeannza kuifanyia kazi chanjo ya virusi vya Ukimwi ambayo itasaidia kumaliza maambukizi mapya ya HIV nchini Kenya, kulingana na gazeti la Daily Nation nchini Kenya.

Chanjo hiyo kwa jina HPTN-081 ni kinga inayohusisha protini ya damu inayoweza kupigana dhidi ya virusi vya HIV.

Akizungumza wakati wa maadhimisho ya 40 ya kituo hicho kwa ushirikiano na Kenya mjini Kisumu siku ya Ijumaa, Mkurugenzi mkuu wa kituo hicho nchini Kenya Marc Bultery alisema kwamba utafiti utahakikisha kuwa chanjo hiyo inaweza kusambazwa hadi maeneo mengine.

Tayari tumemailiza vipimo vyetu vya awamu tatu za chanjo hiyo na tunaelekea katika kupiga hatua kubwa zaidi ambazo zinaweza kwa kamili kuzuia virusi vya HIV, alisema Bultery.

''Tunaangazia wanawake kwasababu ni miongoni mwa makundi yalio na hatari kubwa ya kuambukizwa'', alinukuliwa na Daily Nation akisema.

Daktari Bultery pia alisema kwamba kituo hicho kitasaidia katika mpango wa afya kwa wote nchini Kenya UHC.

''Ni lengo letu kuhakikisha kuwa makundi yote yanaweza kupata matibabu ya bure ikiwemo makundi yaliobaguliwa kama vile wapenzi wa jinsia moja'', alisema bwana Bultery.

Naibu mjumbe maalum wa Marekani nchini Kenya Eric Kneedler alisema kwamba serikali ya Marekani imejizatiti kusaidia mpango wa afya kwa wote ikiwa miongoni mwa ajenda nne za serikali.

''Lengo ni kuona kwamba serikali ya Kenya inakuwa kutoka katika taifa linalotarajia kufaidika hadi taifa lililofaidika'', alisema bwana Kneedler.

Sherehe hizo za maadhimisho zilifanyika kukumbuka mafanikio yakituo hicho nchini Kenya kwa kipindi cha miaka 40.

Baadhi ya ufanisi huo ni pamoja na chanjo ya malaria iliozinduliwa hivi karibuni ambayo imeifanya Kenya na mataifa mengine ya Afrika kufaidika.

Chanjo ya HIV yaonyesha matumaini miongoni mwa binadamu

Chanjo hiyo yenye wezo wa kuwalinda watu duniani kutokana na virusi hivyo ilionyesha matumaini.

Tiba hiyo inayolenga kutoa kinga dhidi ya virusi kadhaa, ilitoa kinga ya HIV katika majaribio yaliofanyiwa watu 339, kulingana na utafiti mmoja uliochapishwa katika jarida la Lancet.

Pia iliwalinda tumbili dhidi ya virusi vinavyofanana na HIV.

Majaribio zaidi tayari yamefanywa kubaini iwapo kinga iliotolewa inaweza kuwalinda watu dhidi ya maambukizi ya HIV.

Takriban watu milioni 37 duniani wanaishi na virusi vya ya HIV au Aids na kuna takriban visa vipya milioni 1.8 kila mwaka.

Lakini licha ya kupiga hatua dhidi ya HIV , tiba yake na chanjo haijapatikana.

Dawa kwa jina Prep ni nzuri katika kuzuia maambukizi ya HIV lakini ikilinganishwa na chanjo inafaa kutumiwa mara kwa mara, hata kila siku ili kuzuia virusi hivyo kuzaana .

Uvumbuzi wa chanjo yake umekuwa changamoto kubwa kwa wanasayansi , kwa sababu kuna aina nyingi za virusi vyake vinavyopatikana katika maeneo kadhaa ya dunia.

Lakini kwa chanjo hii wanasayansi wameweza kutengeneza vipande vya tiba vinayoendana na aina tofauti za virusi vya HIV.

Matumaini ni kwamba inaweza kutoa kinga bora zaidi dhidi ya aina tofauti za virusi vya HIV vinavyopatikana katika maeneo mbali mbali ya dunia.

Washirika kutoka Marekani, Uganda, Afrika Kusini na Thailand walipewa chanjo nne katika kipindi cha wiki 48.

Mchanganyiko wa chanjo hizo ulisababisha kutokea kwa kinga ya HIV na wakaonekana wako salama.

Wanasayansi pia waliwafanyia utafiti kama huo tumbili ambao hawana maambukizi ya HIV ili kuwalinda dhidi ya kuambukizwa virusi vinavyofanana na HIV.

Chanjo hiyo ilionyesha kwa inaweza kuwalinda asilimia 67 ya tumbili 72 kutopata ugonjwa huo.

Wanasayansi waliwafanyia majaribio watu walio kati ya umri wa miaka 18 hadi 50 ambao hawakuwa na HIV na walikuwa na afya.

''Matokeo haya yanawakilisha hatua kubwa iliyopigwa'', alisema Dan Barouch , Profesa wa matibabu katika chuo kikuu cha matibabu cha Havard na kiongozi wa utafiti huo.

Hatahaivyo Profesa Barouch pia ametahadharisha kwamba matokeo hayo yanafaa kuchanganuliwa na tahadhari.

Ijapokuwa chanjo hiyo ilifanikiwa kuimarisha kinga ya watu waliojitolea kufanya majaribio hayo, haijulikani iwapo itatosha kukabiliana na virusi hivyo na kuzuia maambukizi.

''Changamoto katika kutengeza chanjo ya HIV ni nyingi, na uwezo wa kuziimarisha kinga haimaanishi kwamba chanjo hiyo itawalinda binaadamu dhidi ya maambukizi ya HIV'', aliongezea.


Share:

ROBERT MUGABE AZIKWA NYUMBANI KWAKE

Aliyekuwa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe amezikwa nyumbani kwake huko Zvimba.

Kiongozi huyo wa zamani aliiongoza nchi yake kujipatia Uhuru lakini baadaye akashutumiwa kwa kukiuka haki za kibinaadamu na kuharibu uchumi wa taifa lililokuwa likinawiri.

Alifariki akiwa na umri wa miaka 95 nchini Singapore mapema mwezi Septemba. Jeneza lake lililokuwa na rangi ya shaba lilishushwa kaburini.

Robert Mugabe alikuwa amezungukwa na mkewe Grace, watoto na watu wa karibu wa familia yake. Ni marafikize wachache wa zamani waliohudhuria mazishi hayo.

Alizikwa katika eneo la nyumba ya familia yake. Ni wachache ambao wangedhania mtu mwenye haiba kama yake angezikwa na watu wachache.

Baadhi wanasema kwamba ilikuwa taarifa yake ya mwisho ya kisiasa. Kitu ambacho kitakumbukwa katika historia ni kwamba Mugabe alikuwa mchezaji wa chess ambaye hakukubali kushindwa

Wakati alipopinduliwa mwezi Novemba aliondoka bila kutaka. Amezikwa mbali na marafikize ambao anaamini walimsaliti.

Baada ya kifo chake familia yake ililamika hadharani kuwa haikushauriwa kuhusu mipango ya mazishi yake ya kitaifa.

Katika taarifa familia hiyo iliilaumu serikali kwa kutumia nguvu kupanga mazishi ya Mugabe katika makaburi ya mashujaa kinyume na "matakwa yake [Mugabe]".

Taarifa hiyo aidha ilisema kuwa ombi lake la mwisho lilikua la mke wake , Grace Mugabe, kutoondoka kando ya jeneza lake hadi atakapozikwa.
Familia yake inasemekana kughabishwa na jinsi kiongozi huyo alivyong'olewa madarakani na mshirika wake, wa zamani Rais Mnangagwa, miaka miwili iliyopita- halia mbayo huenda imesababisha mvutano kuhusu mahali atakapozikwa.

Bw. Mnangagwa alipendekeza kiongozi huyo azikwe Heroes Acre.

Mugabe, alikua Rais wa kwanza wa Zimbabwe baada ya nchi hiyo kupata uhuru 1980.

Miaka ya awali ya uongozi wake, alisifiwa kwa kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya na elimu kwa Waafrika walio wengi

Lakini baadae utawala wake ulikumbwa na mzozo mkubwa wa kiuchumi na ukandamizaji wa wapinzani wake.

Alikuwa madarakani kwa karibu miongo minne kabla ya kuondolewa kupitia mapinduzi ya kijeshi mwaka 2017 na wadhifa wake kuchukuliwa na Rais wa sasa Emmerson Mnangagwa.
Je Mugabe ni nani?

Robert Mugabe alikuwa rais wa kwanza wa Zimbabwe

Mwaka 1980, Bw Mugabe alishinda uchaguzi na kuwa waziri mkuu.

Mwaka 1982 aliushutumu upinzani kwa kujaribu kupindua serikali.

Maelfu ya watu waliuawa alipolituma jeshi lake lililopata mafunzo Korea Kaskizini, kuwakandamiza maadui zake.

Mwaka 1987,alibadilisha katiba ili imruhusu kuwa rais na kuongeza mamlaka yake.

Uchumi ulidororeka baada ya mwaka 2000…

Wakati Mugabe aliagiza kunyakua mashamba yaliomilikiwa na watu weupe yaliyokuwa kinara katika uchumi.

Mfumuko wa bei ulipelekea sarufi ya taifa kuwa bila thamani na hali nchini humo ikazidi kudororeka.

Baada ya uchaguzi wa mwaka 2008, Mugabe alilazimika kugawanya mamlaka na kiongozi wa upinzani Morgan Tsvangirai.

Japo kulikuwa na ghasia dhidi ya wafuasi wa Bw Tsvangirai katika kampeni za uchaguzi.

Ndoa yake na Grace Mugabe ,anayemzidi kwa maika 40, yaweza kuwa iliyomponza, Wengi walikasirishwa na Grace kuandaliwa kuwa mrithi wake.

Mugabe aliapa kuwa Mungu peke yake ndio angeweza kumtoa madarakani.
Chanzo - BBC
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili Septemba 29




Share:

Saturday 28 September 2019

ZESCO UNITED WAICHAPA YANGA 2-1 , LIGI YA MABINGWA AFRIKA

Na mpiira, umekwisha, Yanga inaondolewa rasmi kwenye mashindano ambapo itacheza Shirikisho na Zesco inaingia hatua ya makundi.

Dak ya 90+4, Zesco wanacheza kwa akili ya kumaliza dakika zilizoongezwa.
Dak ya 90, Moro anapewa kadi nyekundu kwa kucheza madhambi, sasa Yanag wamebaki pungufu. Dakika nne za nyongezwa zinaoneshwa na Mwamuzi wa mezani.

Dak ya 85, Kamusoko anapiga faulo, inaokolewa.
Dak ya 84, faulo nyingine karibu kabisa na eneo la hatari mwa Yanga inapigwa na Zesco. Kamusoko anaonekana na mpira. Muda huo Ally Ally anatoka na Kalengo anaingia kuchukua nafasi yake.
Dak ya 83, Maybin Kalengo anaokena akiandaliwa, bila shaka anataka kuingizwa kuchukua nafasi ya mtu mwingine.
Dak ya 82, hali inakuwa ngumu sasa kwa Yanga, wanapaswa kusawazisha ili mechi iongezwe dakika 30 za ziada.

Dak ya 78, Makame anaizawadia Zesco bao la pili kwa kujifunga, sasa ni 2-1.
Dak ya 69, Yanga wanakosa utulivu wa kutengeneza bao la pili, ni baada ya krosi safi kupigwa engo ya kushoto mwa uwanja lakini inakosa wa kuifanyia kazi.
Dak ya 69, kina nyingine kwa Zesco kipindi hiki cha pili, inapigwa na inaokolewa.
Dak ya 63, Metacha anaanza tena upya.
Dak ya 62, hatari nyingine inatokea katika lango la Yanga, mipira yao ya vichwa inashindwa kufanya walichodhamiria. 

Dak ya 59, Zesco wamekuwa wakifanya mashambulizi mengi japo yamekuwa yakikosa utulivu na ubora wa Yanga eneo la ulizi unakuwa vizuri.
Dak ya 56, Faulo nyingine inapigwa kuelekezwa Yanga, pigwa pale Yanga wanaokoa, unatanguliwa mbele kwake Sadney, unamkuta kipa Banda, anaanza upya.
Dak ya 54, faulo inapigwa na Yanga wanaokoa, wakati huo mchezaji mmoja wa Yanga ameodondoka.
Dak ya 54, Kelvin Yondani anapewa kadi ya njano kwa kucheza madhambi, inakuwa kadi ya nne katika mchezo huu, Yanga wana tatu na Zesco moja.

Dak ya 51, Zesco sasa wanamiliki, mpira anakwenda kwake Kamusoko, hatari kule, Yanga wanaokoa, ilikuwa hatari aisee.
Dak ya 49, Yanga wanafanya shambulizi jingine lango ni mwa Zesco lakini linashindwa kuzaa matunda.
Dak ya 49, Ally Ally anarusha mpira kuelekea Zesco baada ya kutolewa nje.
Dak ya 48, mpira upo kwake Mnata hivi sasa, anaanzisha upya.
Dakika 45 za kipindi cha pili kimeanza

MAPUMZIKO: ZESCO 1-1 YANGA

Dak ya 43, Zesco wanapata faulo karibu kabisa na eneo la penati, ni baada ya Ally Ally kucheza sivyo, wakati huo kuna mchezaji wa Yanga ameanguka chini.
Dak ya 42, Zesco wanajaribu kusaka lango la Yanga kwa nguvu lakini mabeki wake wanapambana kuwazuia, wameongeza kasi.
Dak ya 41, Mpira unarushwa kuelekezwa Yanga.

Dak ya 39, Yanga wanapata kona, inapigwa lakini inashindwa kuzaa matunda.
Dak ya 37, ni faulo, kadi nyingine na ya pili kwa Yanga inenda kwa Moro baada ya kucheza madhambi.
Dak ya 35, Zesco wnafanya shambulizi jingine, Kamusoko anao mpira, Yanga wanaokoa.
Dak ya 34, Yondani anafanyiwa faulo na mpira unapigwa kuelekea Zesco United.
Dak ya 30, Yanga wanakosa nafasi nyingine, inakuwa kona, anakwenda kupiga Sibomana, kwake Sadneeeey, gooli, wanasawazisha.

Dak ya 27, Kaseka anapata kadi ya njano kwa kucheza madhambi, ni kadi ya kwanza kwa dakika 45 za kwanza.
Dak ya 24, Goooli, Zesco wanapata bao la kwanza kupitia kwa Jesse Were akifunga kwa kichwa.
Dak ya 22, Zesco wanazidi kutawala, mpira unarushwa kuelekezwa langoni kwao.
Dak ya 21, Zesco wanaonekana kutawala eneo la kati, wakipambana kusaka namna ya kuipenya ngome ya Yanga.
Dak ya 20, Zesco wanarusha mpira kuelekea Yanga, ni faulo tena Akumu anachezewa, hapana ni offside, Yanga wanacheza.

Dak ya 19, Kamusoko anapiga lakini mabeki wa Yanga wanaokoa.
Dak ya 18, Zesco wanapata faulo, anaenda kupiga Kamusoko, ni kushoto kidogo, mita chache karibu na eneo la hatari.
Dak ya 16, Kaseke anapasiana na Ally Ally kulia kwenye kona ya kulia mwa kibendera lilipo lango la Zesco lakini wanashindwa kuwa watulivu na wapinzani wanauchukua.
Dak ya 14, mlinda mlango wa Zesco Jacob Banda anaonekana akituliza mpira kwa madaha, ni dalili za kupoteza muda ikiwa ni dakika za mapema.
Dak ya 12, Levy Mwanawasa hakuna watu, idadi ndogo ya mashabiki inaonekana.

Dak ya 11, Sadney Urikhob anatoa mpira nje ambao kama angeutuliza vizuri ungeweza kuwa na faida kwa Yanga.
Dak ya 10, ni goli-kiki, kipa Mtacha anonekana akiwaambia jambo wachezaji wake.
Dak ya 09, Tshishimbi anatoa mpira nje, unarushwa kuelekezwa Yanga.
Dak ya 09, Yanga wanafanya shambulizi kali lakini umakini wa kumalizia kambani unakosekana.
Dak ya 08, bado mchezo haujawaa na utulivu kwa timu zote mbili.

Dak ya 07, kona nyingine wanapata Zesco united, wanapiga na Yanga wanaokoa, Lamine Moro anapiga kichwa.
Dak ya 06, Zesco wanapata kona ya kwanza.
Dak ya 05, Tshishimbi anapata nafasi ya kutengeneza shambulizi lakini mabeki wa Zesco wanakuwa mahiri, wanamzuia.
Dak ya 04, faulo inapigwa kuelekezwa katika lango la Yanga.
Dakika 45 za kwanza zimeanza katika uwanja wa Levy Mwanawasa, Ndola, Zambia.
Share:

PICHA: Nyoka Mkubwa Avamia Mkutano wa Waziri Mkuu.....Askari Polisi Aliyemdhibiti Apewa Zawadi

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amemzawadia  Askari Polisi PC Alphonce Daniel Mwambenga sh. 200,000 kutokana na ujasiri wake wa kumdhibiti kwa kumkanyaga nyoka mkubwa aliyekuwa akieleakea jukwaa kuu wakati Waziri Mkuu akihutubia katika Kilele cha Wiki  ya Viziwi Duniani kwenye Uwanja wa Kichangani, Kihesa mjini Iringa, Sepotemba 28, 2019. 

 Kitendo hicho kilifanyika kimyakimya hivyo hapakuwa na taharuki yoyote .  Pichani, Mheshimiwa  Majaliwa akimkabidhi Mwambenga fedha hizo. Wapili kulia ni Mke wa Waziri Mkuu, Mama Mary Majaliwa, kushoto ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Stella Ikupa na kulia  ni Naibu Katibu Mkuu, Wizara y a Elimu, Sayansi na Tekinolojia, Dkt.Avemaria Semakafu.  Wa tatu kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Happy na wa nne kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Dkt. Abel  Nyamkahanga.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Share:

Waziri Mkuu Majaliwa Azindua Urasimishaji Wa Lugha Ya Alama Tanzania

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na lugha moja ya alama ili kuwezesha mawasiliano ya watumiaji wa lugha hiyo, hivyo itaendelea kusimamia uendelezaji, usanifu na urasimishaji wa Lugha ya Alama ya Tanzania, ambao ameuzindua leo(Jumamosi, Septemba 28, 2019).

Amesema hatua hiyo itawezesha utoaji wa elimu katika ngazi mbalimbali pamoja na kuboresha mawasiliano katika jamii na tayari imetoa mafunzo ya lugha hiyo awamu ya kwanza kwa walimu 82 wa shule za Sekondari nchini na kwamba zoezi hilo ni endelevu.


Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Septemba 28, 2019) wakati akihutubia wananchi kwenye kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Viziwi Duniani katika Uwanja wa Kichangani – Kihesa, wilayani Iringaakiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Iringa.

Kaulimbiu ya siku ya Viziwi Duniani kwa mwaka huu inasema “Haki ya Matumizi ya Lugha ya Alama kwa wote”. Kaulimbiu hiyo inalenga kuondoa vikwazo vya mawasiliano miongoni mwa Watanzania ambao ni Viziwi.

“Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo imeanza kurasimisha Lugha ya Tanzania, kutayarisha vifaa vya kufundishia Lugha ya Alama ya Tanzania na kufundisha walimu katika shule za Msingi na Sekondari nchini. Mchakato huo utachukua muda wa takribani miaka miwili kukamilika.”

Amesema Serikali itahakikisha kuwa lugha ya alama ya Tanzania inatambulika na kutumika kikamilifu kama chombo cha mawasiliano miongoni mwa Viziwi nchini ili kuwawezesha kushiriki katika shughuli mbalimbali za ujenzi wa Taifa lao.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli imedhamiria na inatekeleza kwa dhati jitihada za kutoa kipaumbele kwa Watanzania wanyonge ambao hawakuwa wakinufaika ipasavyo na rasilimali za nchi.

“Serikali yenu sikivu inatambua vikwazo vya aina hiyo na inatekeleza maelekezo ya Ilani ya CCM ya 2015/2020, ambayo inaielekeza Serikali ihakikishe watu wenye ulemavu wanapata elimu kwa kupata vifaa maalumu na kushiriki katika shughuli za kijamii.”

Hivyo, Waziri Mkuu amesema Serikali ya Awamu ya Tano itaendelea kuwekeza kwenye miundombinu na mazingira rafiki yatakayowawezesha watu wenye ulemavu kwenda wanapotaka, kutumia vyombo vya usafiri na kupata habari kama walivyo wengine. Amesema katika ofisi yake ataajiri mkalimani wa lugha za alama.

Amesema Serikali itaendelea kuboresha mahitaji maalumu ya watu wenye ulemavu kwa kuwawezesha kupata taarifa mbalimbali kwa urahisi kwa kutumia lugha ya alama, alama mguso, maandishi ya nukta nundu, maandishi yaliyokuzwa au njia nyingine zinazofaa.

Waziri Mkuu amesema Serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo imeanza kurasimisha Lugha ya Tanzania, kutayarisha vifaa vya kufundishia Lugha ya Alama ya Tanzania na kufundisha walimu katika shule za Msingi na Sekondari nchini. Mchakato huo utachukua  takribani miaka miwili kukamilika.

“Serikali kwa kutambua umuhimu wa kuwa na shule maalumu ya Serikali ambayo inahudumia watoto wenye mahitaji maalumu imeanza ujenzi wa Shule Maalumu Patandi katika Mkoa wa Arusha. Shule hiyo inatarajiwa kuchukua wanafunzi 600 wa Msingi na Sekondari na itagharimu sh. bilioni 2.8.”

Kadhalika, Waziri Mkuu amesema katika mapitio ya Kanuni za Maudhui ya Vyombo vya Habari, Kanuni za mwaka 2011, Serikali imeingiza kipengele kipya kinachovitaka vyombo vyote vya habari kuwa na wakalimani wa lugha ya alama kwa vipindi muhimu. Baadhi ya vyombo vya habari ikiwemo Shirika la Habari Tanzania (TBC) vimekuwa vikitekeleza agizo hilo.

“Napenda kutumia maadhimisho haya kuagiza vyombo vyote vya habari kuhakikisha kwamba agizo hili linatekelezwa ipasavyo. Serikali kwa upande wake itaendelea kuhakikisha kuwa haki na mahitaji ya Watu wenye Ulemavu vinapatiwa ufumbuzi kama ilivyoainishwa katika Sheria ya Watu wenye Ulemavu Na. 9 ya Mwaka 2010.”

Amesema anajua ajua changamoto wanazokumbana nazo viziwi wanapotaka kupata huduma mbali mbali katika vituo vya kutolea huduma za afya, mahakama, vituo vya polisi, nyumba za ibada na maeneo mengine muhimu kwa kuwa hayana wakalimani wa lugha ya alama.

Waziri Mkuu ametoa wito kwa taasisi zote za Serikali na binafsi zihakikishe zinakuwa na wakalimani wa lugha ya alama. “Pia naagiza kwamba mitaala ya vyuo vya Afya, Polisi, Mahakama na vinginevyo ihakikishe inazingatia kuongeza kozi ya Lugha ya Alama kama somo la lazima. Hii itasaidia kuzalisha watalaamu wa lugha ya alama ambao wataweza kuwahudumia wenzetu viziwi ipasavyo.”

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) Nidrosy

Mlawa ameishukuru Serikali kwa kuwaamini watu wenye ulemavu na kuwateuwa kushika nafasi mbalimbali za uongozi, lakini waomba iongeze nafasi za ajira kwa watu wenye ulemavu ili nao waweze kujikwamua kiuchumi na kusaidia Taifa.

Pia, ameiomba Serikali iwe na wakalimani wa lugha za alama kwa ajili ya kuwawezesha watu wenye ulemavu waweze kupata taarifa zinazolewa na viongozi wao. Wameomba Serikali ikamilishe mchakato wa urasimishaji wa Lugha ya Alama ya Tanzania. WaziriMkuu amesemamaombi na mapendekezo yao ni ya msingi na muhimu kwa maisha ya Viziwi. Lengo la Serikali ni kuboresha huduma zetu kwa Viziwi hapa nchini.

Maadhimisho hayo yamehudhuliwa na Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais- TAMISEMI Josephat Kandege, Naibu Waziri - Ofisi ya Waziri Mkuu-Kazi, Vijana, Ajira na wenye UlemavuStela Ikupa, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, Dkt. Ave Maria Semakafu pamoja na viongozi wa CHAVITA.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Waziri Lugola Awakatalia Waliopewa Uraia Makazi Ya Wakimbizi Kushiriki Uchaguzi Serikali Za Mitaa Nchini

Na Mwandishi Wetu, Katavi
WAZIRI wa Mambo ya ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amesema wananchi waliopewa uraia katika Makazi ya Wakimbizi ya Katumba, Ulyankulu na Mishamo nchini hawatashiriki kugombea na kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni, kwa kuwa maombi yao bado yanafanyiwa kazi.

Akijibu maombi ya raia hao waliopo Kata ya Katumba, Mkoani Katavi, Waziri Lugola alisema maombi yao wanayo na Serikali inayafanyia kazi kwa ukaribu zaidi, hivyo wanapaswa kuwa wavumilivu kusubiri majibu yao.

“Serikali inawajali, inawathamini, na pia maombi yenu tunayo, na tunayafanyia kazi kwa ukaribu zaidi kwa kuwa Serikali ya Rais Dkt. Magufuli ni sikivu, naomba muendelee kusubiri bila kuwa na uharaka wowote,” alisema Lugola.

Akisoma hotuba ya wananchi hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Ndui Station, Diwani wa Kata hiyo, Seneta Baraka alisema wananchi hao wanakabiliwa na changamoto mbalimbali zikiwemo kutopata haki ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa mwaka huu 2019.

“Ombi letu kwako mheshimiwa Waziri ni kuturuhusu kufanya uchaguzi katika mazingira haya sawa na ilivyofanyika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, ikiwa haiwezekani basi ombi letu na  changamoto zitatuliwe na tupewe fursa ya kufanya uchaguzi mara baada ya changamoto hizo kutatuliwa,” alisema Baraka.

Baraka alisema raia hao walimuomba Waziri huyo, kubalidilisha hadhi ya eneo la Katumba, Mishamo Mkoani Katavi, na Ulyankulu Mkoani Tabora, kuwa na hadhi ya Serikali ya Mitaa kwa kuwa hadhi ya makazi ya wakimbizi inawanyima fursa nyingi za kimaendeleo.

Maombi mengine waliyoyatoa kwa Waziri huyo ni kukamilisha mchakato wa uraia kwa vijana wao uliofanyika mwaka 2017, wakidai kuwa Serikali ilikamilisha mchakato wa uraia wa awamu ya kwanza uliofanyika mwaka 2007, wapo ambao maombi yao hayajakamilika hadi sasa.

Pia waliomba usajili wa laini za simu kwa wenzao ambao hawajakamilisha mchakato wa uraia ili waweze kupata vitambulisho vya taifa.

Akijibu changamoto hizo, Waziri Lugola aliwaambia raia hao maombi hayo yapo mezani kwake na Serikali inayafanyia kazi kwa ukaribu na watapewa majibu mara watakapomaliza kuyafanyia kazi.

Kwa ombi la usajili wa laini za simu, Lugola alisema hiyo ni haki yao kupata vitambulisho, nakuwaahidi kuwa suala hilo litashughuliwa kwa kuwa zoezi hilo ni endelevu.

Kwa upande wake, Mkazi wa Kata hiyo ambaye alikimbia vita mwaka 1972 akitokea nchini Burundi, Zephania Mshinga ambaye ana umri wa miaka 84, alisema Tanzania ni nchi salama, na pia hayupo tayari kuiacha nchi hiyo ambayo ina amani, utulivu, na watu wakarimu.

“Msiombee vita jamani, nilifika hapa Tanzania mwaka 1972 wakati Burundi kulipokuwa na vita, nashukuru nimepewa uraia na kama nikinyang’anywa uraia huu sina mahali pa kwenda, siwezi kurudi nilipotoka maana miaka mingi imepita, sasa ni mkazi wa hapa, naishukuru Serikali ya Tanzania,” alisema Mshinga.

Waziri Lugola yupo Mkoani Katavi kwa ziara ya siku tano ya kikazi, akikagua miradi ya maendeleo, kuzungumza na askari na watumishi wa Wizara yake, pamoja na kusikiliza kero za wananchi katika mikutano ya hadhara mkoani humo.


Share:

Ongeza Nguvu Za Kiume, Maumbire Madogo Pamoja Na Tiba Mbalimbali

MASISA 3 POWER nidawa ya mitishamba iliyotengenezwa kwa muundo wa vidonge na unga  , Huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80)   Inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii)  inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa  tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoazaidi ya maratatu (3)bila hamu kuisha wara kuhisi kuchoka na  itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dk 20-40

SUPER MONGERA  Hurefusha na kunenepesha maumbile madogo yaliosinyaa. Matatizi haya huchagizwa ama husababishwa na tumbo kuunguluma na kujaa gesi,ngili, kisukari, presha korodani moja kuvimba au kuingia ndani nk yote haya yanatibika kabisa na kupona kwa mad mfupi sana,

Pia ninadawa ya vidonda vya tumbo miguu kuwaka moto na kupata nganzi, maumivu ya mgongo na kiuno 

Ni DR CHIPUPA  pekee mwenye uwezo wa kumrudisha mume , mke ,mchumb.

Kwa nini uhangaike na matatizo ya uzazi;   ninadawa ya uzazi kwa pandezote mbili, kupunguza unene kitambi ( nyama uzembe)        kuondoa makovu mwilini, kuzuia mimba kuharibika,kusafisha nyota,  kuzuia majini wachafu, pete ya bahati,

 wasiliana na DR. CHIPUPA 

Call+255 0673878343

watsap +255 0620510598

Huduma hii inakufikia popote ulipo


Share:

Iran yaikosoa Marekani kwa kumyima ruhusa waziri wake wa mambo ya Nje Javad Zarif kumtembelea hospitalini Balozi wa Iran

Iran imeikosoa Marekani kwa uamuzi wa kikatili wa kumzuia waziri wake wa mambo ya kigeni Javad Zarif kumtembelea hospitalini Balozi wa Iran kwenye Umoja wa Mataifa Majid Takht Ravanchi anaetibiwa ugonjwa wa saratani mjini New York. 

Zarif anahudhuria mkutano wa kilele wa hadhara kuu ya Umoja wa Mataifa mjini humo. 

Shirika la habari la kitaifa nchini humo IRNA limemnukuu naibu waziri wa mambo ya kigeni Abbas Araghchi akisema Marekani imeligeuza suala hilo la kibinaadamu kuwa la kisiasa. 

Wizara ya mambo ya kigeni ya Marekani imesema itamruhusu iwapo Iran itamuachia huru mmoja wa raia wengi wa Marekani wanaodaiwa kushikiliwa kimakosa nchini Iran. 

Mwezi Julai Marekani ilitangaza kumzuia waziri huyo kuingia nchini humo, ikiwa ni miongoni mwa vikwazo vyake dhidi ya taifa hilo.

-DW


Share:

Kiboko Ya Maumbile Madogo Na Nguvu Za Kiume

*NGETWA MIX*/
√Hii ndio dawa bora ya mitishamba kiboko ya maumbile Madogo(KIBAMIA) Hurefusha na kunenepesha maumbile  mafupi pia  yaliyoingia ndani kutokana na kitambi ama kuathirika na punyeto

*📌SUPER MORINGA MIX*/
Ni dawabora ya nguvu za kiume yenye mchanganyiko wa miti shamba 10 yenye maajabu yafuatayo:/
🔖(1)Inatibu upungufu wa nguvu za kiume mara dufu na kuimarisha misuri   ilio legea na kusinyaa wakati wa tendo la ndoa/
🔖(2)Kuongeza hamu ya tendo kukufanya uweze kurudia tendo hadi mara tatu bila kuchoka
🔖(3)Itakufanya uchelewe kufika kileleni dk 15-30 kwa tendo la Kwanza na utakuwa na uwezo wa Kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3-4 bila hamu kuisha na inatibu kabisa/
.
*MATATIZO HAYA HUSABABISHWA NA*/
🔖(1)Tumbo kujaa gesi, na kuunguruma chini ya kitovu/
🔖(2) Choo kuwa kama Cha mbuzi/
🔖(3)Ngiri/
🔖(4)Kama umejichua sana punyeto/
🔖(5)Kisukari/
🔖(6)Presha ya kupanda na kushuka/
🔖(7)Vidonda vya tumbo,/
.
Na haya yote husababisha/
📍Kuishiwa kwa nguvu za kiume 📌/
. _______________________
Bado hujachelewa dawa hizi ni mpya kabisa  ni tofaut na ulizo wahi kutumia pia zimeonesha mafanikio kwa watu wengi sana/

Pia tuna tibu  KISUKARI,PRESHA,VIDONDA VYA TUMBO N.K/
._______________________
DR .SELEMANI OMARY ANAPATIKANA  DAR ES SALAAM , PIA UNAWEZA KULETEWA POPOTE ULIPO  NDANI NA NJE YA NCHI .SIMU NO:/
*📞+255788468114*


Share:

Serikali Yatoa Muda wa Wiki Moja kwa Kiwanda cha kutengeneza saruji cha Dangote kuwasilisha taarifa ya utendaji kazi TIC

NA.MWANDISHI WETU
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Uwekezaji Mhe. Angellah Kairuki ametoa muda wa wiki moja kwa Kiwanda cha kutengeneza saruji cha Dangote kuwasilisha taarifa ya utendaji ambazo kwa zaidi ya miaka miaka mitatu hawajaziwasilisha Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) kama sheria na taratibu za nchi zinavyoelekeza.

Waziri Kairuki ambaye aliongozana na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt. Angeline Mabula Katika ziara yake ya kutembelea, kukagua maeneo mbalimbali ya uwekezaji na kuongea na wawekezaji na wafanyabiashara wa Mkoa wa Lindi septemba 27,2019 ameuelekeza uongozi wa kiwanda hicho kuhakikisha kila baada ya miezi sita wanawasilisha taarifa za kiutendaji TIC.

Waziri Kairuki aliwaeleza masikitiko yake viongozi wa kiwanda hicho kwa kutowasilisha taarifa za utekelezaji wao ikiwemo zinazohusu historia ya mradi, mipango ya upanuzi, kodi wanazolipa, faida pamoja na changamoto wanazokabiliana nazo na ushauri wao.

"Nimesikitishwa sana na suala hili la kutopeleka taarifa zenu TIC ambapo inafahamika suala hilo ni la kisheria na lazima litekelezwe kwa wakati,hivyo kuanzia sasa nimewapa wiki moja mhakikishe taarifa hizo zinawasilishwa haraka,"alisisitiza Waziri Kairuki.

Aidha amewapongeza Dangote kwa uwekezaji huo mkubwa pamoja na kuanza ujenzi wa mradi wa kuzalisha umeme wao wenyewe megawati 25 ambao megawati 5 zitaingia kwenye gridi ya taifa.

Amewataka wawekeze na maeneo mengine siyo kwenye saruji tu na kuagiza TIC kupitia mikataba ya utendaji ya wawekezaji wote mahiri kuona ni wapi wanaweza kuwekeza zaidi.

Wakiwa Mkoani Lindi Waziri Kairuki na Mhe. Mabula walitembelea mgodi wa madini ya uno (graphite) uliopo katika Kijiji cha Matambalale Kusini Wilaya ya Ruangwamkoani Lindi na kuona shughuli za awali za mradi huo ambapo Meneja wa kampuni ya Lindi Jumbo inayochimba madini hayo Bw Paul Shauri amesema mgodi utajengwa kwa muda wa miezi tisa na wanatarajia kuwekeza zaidi ya dola za kimarekani milioni 30.

Akiongea mgodini hapo Dkt.Mabula ameziagiza Halmashairi zote vijiji vyenye maeneo ya uwekezaji kufanya zoezi la kuandaa mpango wa matumizi ya ardhi watenge maeneo ya uwekezaji wayahaulishe yawe mali ya kijiji ili mwekezaji akipatikana watimize masharti mengine tu.

"Hakuna sababu ya mwekezaji kuanza kuhangaika na mambo madogo kama hayo ambayo yanampotezea wakati ni lazima halmashauri zijipange ili kumwekea mwekezaji mazingira mazuri avutiwe kuwekeza"alisema Dkt.Mabula

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa Hashim Mgandilwa akiwakaribisha Mawaziri hao amesema Serikali ione kuna sababu ya kuharakisha ujenzi wa miundombinu ikiwemo barabara za wilaya hiyo kwani kuna makampuni mengi makubwa yameonesha nia ya kuwekeza.

Amesema wilaya hiyo pia inakabiliwa na changamoto ya mipaka ya asili na kwamba suala hilo tayari linaendelea kutatuliwa kwa viongozi na watendaji kutoa elimu kwa wananchi.


Share:

Tanzania Yasaini Mkataba wa Kupinga Matumizi ya Nyuklia.....Yapongezwa kwa kulinda amani ukanda wa maziwa makuu

Tanzania imesaini mkataba wa kupiga marufuku matumizi ya silaha za nyuklia, na kuifanya kuwa miongoni mwa nchi 60 zilizosaini na 32 zilizoridhia mkataba huo Duniani

Utiaji saini wa mkataba huo umefanywa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi, kwenye mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa nchini Marekani

Profesa Kabudi amesema kwa kusaini mkataba huo Tanzania inaunga mkono jitihada zote za kupiga marufuku matumizi ya silaha za nyuklia, ikiwa ni sehemu ya kuufanya ulimwengu kuwa mahali salama pa kuishi

Hata hivyo Prof. Kabudi amesema Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haikatai na inaunga mkono matumizi ya amani ya nguvu za nyuklia kama sehemu ya dawa, kuhifadhi vyakula na uzalishaji wa nishati miongoni mwa matumizi mengine chini ya uangalizi madhubuti wa shirika la kimataifa la nguvu za atomiki.

Ameongeza kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imechukua hatua hiyo ikitiliwa maanani kuwa zipo nchi zenye silaha za nyuklia takribani 14 elfu na zimetenga bajeti kubwa kwa ajili ya kuimarisha silaha hizo na kutoa wito kwa mataifa hayo kujenga imani kwa mataifa mengine na kwamba matumizi ya silaha hizo si njia sahihi na salama za kuihakikishia dunia amani na usalama. 


Katika hatua nyingine, Umoja wa Mataifa umeipongeza  Tanzania kwa mchango wake wa kulinda amani katika ukanda wa maziwa makuu na kuahidi kushirikiana na Tanzania katika kuzuia matukio yanayosababishwa na misimamo mikali.

Pongezi hizo zimetolewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Plamagamba John Kabudi ambapo pia katika mazungumzo hayo wamegusia masuala ya maendeleo katika ukanda wa maziwa makuu, ikiwa ni pamoja na hali ya kisiasa ya Burundi na usalama katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Katibu Mkuu Antonio Guterres amesema umoja huo unatambua mchango na jitihada za Tanzania na kuongeza kuwa Umoja huo upo tayari kushirikiana na Tanzania katika jitihada zake za kuzuia matukio yanayosababishwa na misimamo mikali.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na 
0747100745


Share:

Kutana na Mohamedi Buruhani Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH .....Anauwezo wakufanya Dua mbalimbali Na Kutafsiri Ndoto

Kutana  na Mtabibu Mwenye KUBRI kutoka kwa ALLAH Mohamedi Buruhani Mtabibu wa Nyota za Binadamu  Mwenye UWEZO Kubaini tatizo lako Pindi tu Utakapo Fanya Mawasilino Kupitia Wasaa Husika..

JE UNASUMBULIWA NA Mapenzi? (Umeachwa na Umpendae,Awe Mume,Mke na Bado unampenda?Na  Umejaribu Sehemu nyingi Bila Mafanikio?Wasilina na Mohamed Buruani Ujione muujiza wa Papo kwa Papo.. 

Anauwezo WA KURUDISHA MAHUSIANO NA KUIMARISHA NDOA YAKO . Umekimbiwa na Mumeo,mkeo au Mpenzi na anaishi na mtu mwingine? Muone akutatulie ..Atamfanya Atimize Ahadi zote kwa Muda Mfupi.

Mohamed Buruhan Anatumia Jina la Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo lako..

Anatibu kwa Kutumia  Vitabu vya QUR-AN, Anatafsiri Ndoto. ,KUSAFISHA NYOTA, Mvuto wa Mwili na BIASHARA, ...MIGUU Kufa GANZI na mengi zaidi (+255  715971688 au (+255  756914036

NB: TIBA KWA DINI ZOTE NA IMANI ZOTE...


Share:

Mkurugenzi Apewa Saa Nne Kusitisha Mkataba Wa Ujenzi

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa muda wa saa nne kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa Himid Njovu awe ameandika barua ya kusitisha ujenzi wa ukumbi wa mikutano na sherehe katika eneo la shule ya msingi Gangilonga.

Amesema maeneo yote ya taasisi za elimu nchini hayaruhusiwi kujengwa miradi ambayo haihusiani na masuala ya elimu, hivyo amtaka mkurugenzi huyo kusitisha mkataba na mtu aliyemkodisha eneo hilo na kisha alizungushie uzio kwa matumizi ya shule.

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumamosi, Septemba 28, 2019) wakati akizungumza na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa, Halmashauri ya Manispaa ya Iringa na Madiwani wa Halmashauri hizo akiwa katika siku ya tano ya ziara yake ya kikazi mkoani Iringa.

“Mkurugenzi kafute mikata yote ya ujenzi wa miradi katika eneo la shule ya Gangilonga pamoja na shule ya Wilolesi kwa sababu maeneo hayo hayaruhusiwi kujengwa miradi isiyohusiana na elimu. Eneo hilo lisafishwe na ujengwe uzio.”

Kwa upande wake, Mwanasheria wa Manispaa ya Iringa Nocholous Mwasungura amesema aliandaa mkataba wa kupangisha eneo kwa maelekezo ya Kamati ya Fedha, ambapo Waziri Mkuu alimuuliza kwa nini hakuwashauri kuhusu suala hilo kwa sababu tayari Serikali ilishatoa waraka wa kuzuia jambo hilo.

Pia, Waziri Mkuu amemwagiza Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Happi ofisi ya ardhi ya Manispaa ya Iringa kutokana na kuwepo kwa malalamiko mengi kutoka wananchi juu ya Afisa Ardhi ambaye anadaiwa kujigawia viwanja vingi pamoja na kugawa kiwanja kimoja kwa mtu zaidi ya mmoja.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Happi aliwaonya watumishi hao kutojihusisha na vitendo vya rushwa na matumizi mabaya ya madaraka pamoja na kuacha chuki, ubinafsi na roho mbaya na badala yake washikamane na wafanye kazi wa bidii.

Naye,Mkuu wa wilaya ya Iringa, Richard Kasesera aliiomba Serikali izisaidie halmashauri za wilaya hiyo vyombo vya usafiri kwa sababu magari mengi ni chakavu hali inayosababisha Mkurugenzi wa Manispaa awe anaomba lifti kwake. Waziri Mkuu amewataka waombe kibali cha ununuzi wa magari na watumie fedha zao za ndani.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Waziri Jafo Atoa Onyo.....Awataka Wakurugenzi Wawe Makini na Wasimamie matumizi sahihi ya fedha za Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Na. Angela Msimbira OR -TAMISEMI
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote nchini kuhakikisha wanasimamia kwa weledi fedha zilizotengwa kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Ameyasema hayo jana wakati akifungua semina ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa Makatibu Tawala wa Mikoa, Wakurugenzi  wa Halmashauri na Wasimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa  iliyofanyika katika Ukumbi  wa Auditoriumn, Chuo Kikuu cha Dodoma, Jijini Dodoma.

Mhe. Jafo amesema kuwa hatasita kuwachukulia hatua Wakurugenzi ambao wataenda kinyume na utaratibu wa matumizi ya fedha zilizotengwa kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kwa kuwa kukuika miongozo iliyotolewa na Serikali katika matumizi sahihi ya fedha hizo.

Mhe. Jafo ameonya matumizi yasiyofaa kwa fedha zilizotengwa kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa na kusisitiza kuwa fedha hizo ni za moto, hivyo matumizi yake yanahitaji kufuata miongozo na taratibu zilizowekwa na Serikali.

Ameendelea kusema kuwa ni marufuku kwa Mkurugenzi kutumia fedha za uchaguzi kinyume na agenda ya uchaguzi na kusisitiza haja ya fedha hizo kutumika kwa wakati.

“Naomba niwape tahadhari, katika matumizi ya fedha ya uchaguzi, fedha hizi za uchaguzi zinazokuja ni kwa ajili ya uchaguzi, naomba mtu asidanganyike wala kurubunika kwa lolote katika mchakato huu wa uchaguzi, katika fedha za moto hizi fedha za moto” Amesisitiza Mhe. Jafo

Mhe. Jafo amesema kuwa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa inasimamia kwa karibu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa hivyo ni matumaini kuwa matumizi ya fedha za uchaguzi zitaenda kama ilivyokusudiwa kwa kufuata miongozo ya matumzi ya fedha hizo.

Amesema kuwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri nchini  ndio wenye dhamana ya kusimamia matumizi sahihi ya fedha zilizotolewa na Serikali kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, kinyume na hapo anapaswa kujibu hoja zitakazojitokeza za kushindwa kusimamia fedha hizo vizuri.

Kuhusu wasimamizi wa uchaguzi, Mhe. Jafo amewasihi kutekeleza makujukumu yao kwa weledi na kuhakikisha ratiba ya uchanguzi inafuatwa huku akiwataka kutambua kuwa wasimamizi wamebeba dhamana kubwa katika kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa kuzingatia Demokrasia.

“ Natamani sana mlioteuliwa kuwa wasimamizi wa uchaguzi mwende vizuri mpaka mmalize vizuri kwa mujibu wa kanuni zetu. Mheshimiwa Rais anatamani nchi yake ikatekeleze demokrasia vizuri na ndio maana mnaona ameweza kuwezesha kila eneo kwa lengo kuwa uchaguzi uende ukafanyike vizuri”. Amesema Mhe. Jafo

Amesema Uchaguzi wa Serikali za Mitaa nchini ni muhimu kwa kuwa maisha ya watu yanaanzia katika vitongoji, mitaa na vijiji vyenu, mustakabali wa kuchakata maendeleo lazima uanze katika ngazi husika ambayo uchaguzi huu unaenda kuwapata viongozi na  hawawezi  kupatikana kama wasimamizi wa uchaguzi mtashindwa kufanya kazi yenu vizuri.

Wakati Huohuo, Mhe Jafo amewataka Makatibu Tawala wa Mikoa ambao ndio waratibu wakuu wa uchaguzi kuhakikisha wanafuatilia kwa karibu kila tukio na kuwataka wasikubali kuharibiwa kazi.

 “Makatibu Tawala wa Mikoa wao ni waratibu wakuu wa Uchaguzi katika Halmashauri zao kipindi hiki mna kazi kubwa sana ya kuhakikkisha huko chini mambo yanaenda vizuri na wala msikubali hata kidogo mtu awaahiribie kazi”. Amesisitiza Mhe. Jafo

Awali, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhandisi Joseph Nyamhanga, ameeleza kuwa kikao hicho kinalenga kukumbushana majukumu ya uchaguzi huo na kuna matukio mbalimbali yaliyopo katika tangazo la uchaguzi yanayopaswa kutekelezwa.

Mhandisi Nyamhanga amesema OR-TAMISEMI imeshakamilisha maandalizi yote muhimu ya uchaguzi huo na nyaraka mbalimbali zimeandaliwa na kusambazwa ikiwemo kanuni na muongozo wa uchaguzi huo.

Amesema tayari  imeratibu upatikanaji wa fedha na tayari zimeshatumwa kwenye Sekretarieti za Mikoa yote na anaamini zimeshatumwa kwenye Halmashauri kwa ajili ya maandalizi.

Aidha, Nyamhanga alisema katika uchaguzi wa mwaka huu inakadiriwa kuwa na vituo vya kupigia kura 110,000.




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger