Saturday 28 September 2019

RAIS WA AFRIKA KUSINI CYRIL RAMAPHOSA AMTEUA ALIYEKUWA GAVANA WA BENKI KUU TANZANIA PROF. BENNO NDULU KUWA MSHAURI WAKE WA MASUALA YA KIUCHUMI


Rais Cyril Ramaphosa  wa Afrika Kusini amemteua Prof. Benno Ndulu kuwa miongoni mwa watu 18 wanaounda Baraza la kumshauri Rais huyo katika masuala ya uchumi litakaloanza kufanya kazi kuanzia Oktoba 01, 2019.



Baraza hilo lililotangazwa jana na Rais Ramaphosa litakuwa na kazi kubwa ya kuhakikisha uhusiano mzuri na uthabiti katika utekelezaji wa sera ya uchumi na kuhakikisha kuwa Serikali inaweza kujibu mabadiliko ya hali ya uchumi

Baraza linajumuisha viongozi wa ndani na nje ya Afrika Kusini watakaotoa mawazo ya kiuchumi, wakimshauri Rais na Serikali kwa upana zaidi, kuwezesha maendeleo na utekelezaji wa sera za uchumi zinazochochea ukuaji wa umoja

Pamoja na Prof. Benno Ndulu, wengine ni Prof. Mzukisi Qobo, Prof. Dani Rodrik, Prof. Mariana Mazzucato, Mamello Matikinca-Ngwenya, Dkt. Renosi Mokate, Dkt. Kenneth Creamer, Prof. Alan Hirsch, Prof. Tania Ajam, Dkt. Grové Steyn, Wandile Sihlobo, Dkt. Liberty Mncube, Prof. Fiona Tregenna, Prof. Haroon Bhorat, Ayabonga Cawe, Prof. Vusi Gumede, Dkt. Thabi Leoka na Prof. Imraan Valodia


Prof. Benno   Ndulu alikuwa Gavana wa Benki Kuu Tanzania tangu 2008 hadi 2018 baada ya Rais John Magufuli kumteua Profesa Florens Luoga kushika nafasi hiyo.


Share:

KAMPUNI BINAFSI YA ULINZI SGA YATOA MAFUNZO YA USALAMA BURE


Mkurugenzi Mkuu wa kampuni ya SGA Security, Eric Sambu (kushoto) akizungumza jijini Dar Es Salaam leo wakati wa kuadhimisha miaka 35 ya kutoa huduma za ulinzi nchini. Kulia ni Meneja wa Wateja na Mawasiliano wa kampuni hiyo, Aikande Makere.

Kampuni ya ulinzi, SGA Security, imetoa mafunzo ya bure ya usalama kama sehemu ya utoaji wa huduma kwa jamii na kuwazawadia watumishi wake wa muda mrefu ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 35 ya kuwepo nchini Tanzania.

Wiki iliyopita kampuni hiyo ilitoa mafunzo kwa wateja wake wakubwa juu ya mbinu mbalimbali za kisasa za kupambana na changamoto za kiusalama.

Semina hiyo kwa wateja wake ilifanyika Ijumaa Septemba 27 jijini Dar es Salaam na mafunzo yaliongozwa na wataalam waliobobea kwenye masuala ya usalama ambapo zaidi ya mameneja 80 wa usalama wa makampuni makubwa na mabenki nchini walihudhuria.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa SGA, Eric Sambu, alisema kwamba kampuni hiyo ya ulinzi imeamua kutoa huduma kwa jamii kama sehemu ya kusheherekea mafanikio yake nchini.

SGA pia imetoa mafunzo ya usalama kwenye shule 12 za msingi mkoani Dar es Salaam ambapo wanafunzi zaidi ya 2,000 walinufaika. Mafunzo hayo yalikua juu ya majanga ya moto, huduma ya kwanza, mazingira, afya na usalama kwa ujumla.

Ikiwa ina watamushi zaidi ya 5,800, nchini Tanzania, SGA kwa sasa ndio kampuni kubwa ya ulinzi nchini.

Katika shughuli za kuadhimisha miaka 35 nchini, kampuni pia imeanzisha ‘Club 20’ ambao wanachama wake ni watumishi walioitumikia kampuni kwa zaidi ya miaka 20. 

SGA aliwatuza watumishi 16 waliotumikia kampuni kwa muda mrefu ambao pia wamefikia muda wa kustaafu.

Wakati huo huo, mwakilishi kutoka jeshi la polisi nchini ameipongeza SGA kwa kujali maslahi ya watumishi wake na kuongoza kwa mfano, akisema kwamba kampuni nyingi binafsi za ulinzi hazifuati miongozo iliyotolewa kuhusiana na mafunzo, usimamizi, ukaguzi na mishahara.

Amezitaka kampuni nyingine za ulinzi kuiga mfoano wa SGA.

Ikiwa ina waajiriwa zaidi ya 80 waliotumikia kampuni kwa zaidi ya miaka 20 kwenya biashara ya faida kubwa, SGA ina kila sababu ya kusherehekea, amesema Sambu. SGA pia ina watumishi takribani 2,200 walioajiriwa kwa zaidi ya miaka 10.

“SGA ni kampuni ya kwanza binafsi ya ulinzi kuingia Tanzania na imedhihirisha kwamba kuwajali watumishi wake ni muhimu kwa mafanikio ya kampuni,” Sambu amesema.
Watumishi wa SGA wakishiriki kwenye Siku ya Usafi Duniani kama sehemu ya kuadhimisha miaka 35 ya kuwepo nchini Tanzania

“Kampuni mama ina watumishi za ya 18,000 na suala la muhimu kwetu ni watu. Tumewekeza sana katika utoaji wa mafunzo na tunahakikisha kwamba mishahara yetu inaongoza kwenye soko kama sehemu ya kuwapa motisha watumishi wetu,” aliongeza.
Amesema kwamba kampuni anaadhimisha miaka 35 ya utoaji huduma nchini Tanzania huku ikiwa inakua siku hadi siku, hususan katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Ameeleza zaidi kwamba mafanikio ya kampuni yameletwa na watumishi wake ambapo amesema ni waaminifu, waadilifuna wachapa kazi kwa bidii.

“Matukio ya hivi karibuni kwenye mazingira ya kibiashara nchini yamekuwa kama fursa ya kujifunza na kuwawezesha wafanyakazi wetu kwenda sambamba na matakwa ya wateja,” ameongeza.

“Kila mara tunajipanga upya katika utendaji wetu, huku tukiwekeza kwenye teknolojia na watumishi wetu kuhakikisha kwamba hakuna jambo linaloharibika,” amesema Sambu.

SGA ni kampuni kongwe binafsi ya ulinzi Tanzania, ikiwa imeanza kazi mwaka 1984 kama Group Four Security. Inatoa huduma mbalimbali zikiwemo za walinzi, usalama wa kielektroniki, huduma za dharura na usafirishaji wa fedha.

“Tuna magari 224 na vituo 12 mikoani na watumishi wanaojituma, tuna miundombinu ya kutosha kuwahudumia wateja popote pale nchini,” Sambu amesema.

Menaja Rasilimali Watu wa SGA, Ebenezer Kaale, alisema kwenye tukio hilo kwamba watumishi wengi walioajiriwa kwa miaka mingi wanafanyakazi kwenye idara ya kusafirisha fedha, idara nyeti inayohitaji uadilifu na nidhamu ya hali ya juu.

Ikiwa ina mafanikio makubwa kwenye huduma za fedha, ambapo kampuni imehodhi asilimia 90 ya soko, watumishi kwenye idara wanastahili pongezi kwa mafanikio hayo.

Meneja wa Mahusiano ya Wateja, Aikande Makere, amesema kwamba kazi za SGA zitarahisishwa ikiwa wateja wanaenda na wakati kwa kufahamu mbinu za kisasa za kupambana na changamoto za kiusalama.

Mwisho







Share:

KANISA KATOLIKI LATOA TAHADHARI JUU YA MATAPELI WANAOTUMIA JINA LA ASKOFU MKUU RUWA'ICHI


Katibu  Mkuu wa Jimbo Kuu la Katoliki Dar es Salaam, Frank Mtavangu, ametoa tahadhari ya kuwepo kwa ukurasa wa facebook bandia ambao unatumiwa na matapeli kuomba fedha huku wakitumia jina la Askofu Mkuu wa jimbo hilo Yuda Rwai’chi.

Taarifa iliyotolewa na katibu huyo jana jijini Dar es Salaam ilisema matapeli hao wamekuwa wakidai kuwa wanaomba mchango kwaajili ya ujenzi wa makazi ya malezi ya wajane, yatima na wakongwe.

“Napenda kuwatahadharisha kuwa kuna matapeli wamefungua akaunti ya Facebook kwa jina la Askofu Mkuu Yuda Thadei Rwai’chi akaunti hii ni ya kitapeli inayotumia jina la “Askofu Ruwai Chi”.

“Inaomba watu wachangie ujenzi wa makazi kuu ya malezi ya wajane, yatima na vikongwe ikiomba michango itumwe kwenye namba ya simu,”alieleza Mtavangu.

Alisema Askofu hatumii akaunti hiyo na hajawahi kuomba michango ya namna hiyo kwa njia hii na akaunti hiyo sio yake .


Share:

TCRA YASHUSHA RUNGU KWA TV ZA MTANDAONI...MILLARD AYO,WATETEZI TV NA KWANZA TV


Kamati ya maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imetoa adhabu kwa televisheni za mtandaoni kwa kukiuka misingi ya uandishi wa habari na utangazaji na kushindwa kuchapisha sera na mwongozo kwa watumiaji.

Chaneli za mtandaoni zilizokumbwa na rungu hilo ni Watetezi Tv, Millard Ayo na Kwanza Tv ambayo imepewa adhabu ya kufungiwa kwa miezi sita.

Akisoma uamuzi wa kamati Makamu mwenyekiti Joseph Mapunda amesema Kwanza Tv wamekutwa na kosa la kukiuka misingi ya uandishi wa habari na kanuni za utangazaji kwa kuchapisha habari iliyolenga kupotosha.

Amesema kupitia ukurasa wake facebook Kwanza tv iliweka video iliyobebwa na kichwa cha habari Dk Gwajima apata ajali.

Mapunda amesema kwa makusudi habari hiyo haikutaja jina la kwanza la Dk Gwajima hivyo kuzua taharuki hasa ikizingatiwa kuna mtu mwingine maarufu anayetumia jina hilo

Pia Kwanza Tv ilikutwa na kosa la kutochapisha sera na mwongozo kwa watumiaji wake jambo linalowapa uhuru wa kuweka maudhui yoyote bila kujali athari zinazoweza kujitokeza.

Kwa makosa hayo mawili kamati ilifikia uamuzi wa kuifungia Kwanza Tv kwa muda wa miezi sita.

Kosa la kutochapisha mwongozo kwa watumiaji wamekutwa nalo pia Millard Ayo na Watetezi Tv ambao wote wametozwa faini ya Sh5 milioni na kupewa onyo.


Share:

Mfanyakazi CRDB Afikishwa Mahakamani kwa kumuibia mteja zaidi ya milioni 100

Ofisa  wa benki ya CRDB tawi la Ubungo,Andrew Babu(27)na wenzake watatu ambao ni Wafanyabiashara wamefikishwa katika Mahakama  ya Hakimu Mkazi Kisutu,jijini Dar  wakikabiliwa tuhuma za Uhujumu Uchumi ikiwamo kula njama,kugushi tembo kadi, wizi na kutakatisha zaidi ya Mil 100.
 
Mbali na Babu, washitakiwa wengine ni William Sige, Justina Boniphas na Ally Tatupa ambao wote wanakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi namba 101/2019.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon aliwasomea mashtaka yao Alhamisi Septemba 26, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama hiyo, Agustina Mbando.


Hakimu Mmbando ameahirisha kesi hiyo hadi  Oktoba 10, 2019 itakapotajwa tena.

Washtakiwa wote walirudishwa rumande kutokana na shtaka la utakatishaji fedha kutokuwa na dhamana.


Share:

Tutahakikisha Malighafi Zinazohitajika Viwandani Zinapatikana

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Songwe
Serikali imesema kuwa inaimarisha mikakati yake ili kuwa na uwezekano wa kuwa na malighafi toshelevu katika viwanda vyote nchini.

Ifahamike kuwa malighafi nyingi zinazotumika viwandani asilimia kubwa zinatokana na sekta ya kilimo hivyo moja ya mkakati madhubuti ni kusimamia kwa weledi sekta hiyo ili kuwa na malighafi nyingi na za kutosha.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyasema hayo  jana tarehe 27 Septemba 2019 wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la Vwawa Mkoani Songwe.

Alisema kuwa miongoni mwa majukumu muhimu ya Wizara ya kilimo ni kuimarisha Mchango wa sekta ya kilimo ili wakulima waweze kuongeza uzalishaji na tija.

"Ni lazima tuhakikishe kuwa watu wanazalisha kwa ajili ya biashara sio chakula pekee na gharama wanazotumia ni lazima wahakikishe zinarudi ili waone faida ya kilimo" Alikaririwa Mhe Hasunga

Waziri Hasunga ameeleza kuwa serikali kupitia wizara ya kilimo ina jukumu la kuhakikisha umasikini unapungua kwa kuongeza uzalishaji kwa wakulima ili kilimo kiendelee kuingiza fedha nyingi za kigeni na kuchangia kwa wingi pato la Taifa.

Kadhalika ametaja Mikakati mingine ya wizara ya kilimo kuwa ni pamoja na  Pembejeo (Mbegu bora, Mbolea, na Viuatilifu) kufika kwa wakati kwa wakulima ambapo amesisitiza kuwa wananchi wanapaswa kununua mbegu Bora kwani  zinaweza kukinzana na magonjwa na nyingi zinastahimili ukame.

Kuhusu masoko ya mazao ya wakulima waziri Hasunga amesema kuwa wizara yake imekuja na mkakati maalumu wa kuanzisha kitengo cha masoko kitakachokuwa na majukumu ya kubainisha masoko ya mazao mbalimbali ya wakulima.

"Ni lazima kufanya biashara kisasa kwa kujua mahitaji ya soko kabla ya kuzalisha mazao ya kilimo ili wakulima wanapozalisha tayari wawe wanajua watauza wapi mazao yao" Alisisitiza Mhe Hasunga

Katika mkutano huo uliohudhuriwa na mamia ya wananchi ambao ni wakazi wa mamlaka ya mji mdogo wa Vwawa na ameneo ya jirani, Waziri Hasunga amewataka wananchi kuendelea kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli katika kuimarisha ufanisi wa shughuli za maendeleo katika Jimbo la Vwawa na Taifa kwa ujumla.

MWISHO.


Share:

Wadau Maonesho Ya Geita Watembelea Mgodi Wa GGM

Wadau mbalimbali wanaoshiriki Maonesho ya  Pili ya Teknolojia na Uwekezaji kwenye Sekta ya Madini jana  Septemba 27, 2019, wametembelea Mgodi wa Dhahabu wa GGM unaomilikiwa na Kampuni ya Anglo Gold Ashanti. 

Ziara hiyo imelenga katika kujifunza kuhusu namna shughuli za uchimbaji na uzalishaji wa Madini ya Dhahabu unavyofanyika mgodini hapo huku lengo kuu likiwa kuona teknolojia mbalimbali zinazotumika katika uchimbaji wa madini.
 
Aidha, mbali na kujifunza kuhusu uzalishaji na uchimbaji, wadau hao wameelimishwa kuhusu masuala mazima kuhusu namna mgodi huo unavyoshughulikia masuala ya mazingira, usalama na afya mgodini.

Akizungumzia masuala ya jamii, Afisa anayehusika na Masuala ya Mahusiano na Jamii mgodini hapo Musa Shunasu, ameeleza mgodi huo umekuwa ukitoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo,  kufadhili miradi mbalimbali, pia kwa kushirikiana na Wizara ya Madini umeanzishwa mgodi wa mfano wa Lwamgasa unaolenga katika kutoa mafunzo kwa wachimbaji wadogo ili waweze kuchimba kwa tija. 

Aidha, mgodi huo umesaidia jamii katika masuala mengine mbalimbali yakwemo ya elimu na afya
 
Akijibu hoja kuhusu madai mbalimbali ya wananchi kuhusu masuala ya fidia amesema kwamba mwananchi yoyote katika eneo linazunguka mgodi huo ama aliye mbali ya eneo hilo anaruhusiwa kuwasilisha malalamiko yake kwa mgodi.
 
Kwa mujibu wa Shunasu, kampuni hiyo ina zaidi ya migodi 16 maeneo mbalimbali duniani, huku hapa nchini ulianza shughuli za uzalishaji mwaka 2000.
 
Amesema Dira ya kampuni hiyo ni kuchimba dhahabu kuwa kampuni inayoongoza kwa uchimbaji, usalama, mazingira na jamii.


Share:

Serikali Yatoa Onyo Kali Kwa Watendaji Kata

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaonya baadhi ya Watendaji Kata na askari nchini ambao wamekuwa wakishindwa kuzifikisha sehemu husika kesi za watu waliowapa ujauzito wanafunzi na amesema watakaobainika watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Ameyasema hayo jana jioni (Ijumaa, Septemba 27, 2019) wakati akihutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika uwanja wa Ilula Sokoni, kata ya Nyalumbu wilayani Kilolo akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Iringa.

“Wanafunzi bado wanaendelea kupewa ujauzito na kukatishwa masomo yao huku watu waliohusika na vitendo hivyo wakishindwa kuchukuliwa hatua stahiki kwa sababu baadhi ya watendaji na askari wamezikalia kesi zao na kushindwa kuwafikisha polisi.”

“Watoto wa kike lazima walindwe ili wamalize masomo yao waje kulitumikia Taifa lao. Serikaliimeweka sheria kali ya kumlinda mtoto wa kike lengo ni kumuwezesha amalize masomo yake ili aweze kujikwamua kiuchumi na aondokane na utegemezi.”

Waziri Mkuu alisema watoto wa kike wanatakiwa kuheshimiwa katika jamii na adhabu iliyowekwa na Serikali ni kifungo cha miaka 30 jela kwa mtu atakayemuoa, kumpa ujauzo na hata ukikutwa naye nyumbani kwako, katika nyumba ya wageni.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewataka wananchi hususan waishio vijijini wasikubali kurubuniwa na kugawa ardhi yao kwa watu mbalimbali wanaofika kwenye maeneo yao na kutaka wauziwe ardhi bila ya kuzihusisha mamlaka husika.

“Eneo lenu hili la Ilula ni zuri hivyo msikubali kurubuniwa kuuza ardhi yenu kwa sababau inathamani kubwa. Viongozi wa Kata na Vijiji hakikisheni mnaratibu vizuri na muandae mpango wa matumizi bora ya ardhi ili kuepuka migogoro.”

Waziri Mkuu alisema wananchi hao wanatakiwa wawe makini na ardhi na mamlaka zinazohusika na ardhi lazima zihusishwe katika ugawaji wa ardhi kwa sababu wakigawa hovyo watasababisha vijana wao hapo baadaye wakose maeneo ya kilimo.

Akizungumzia kuhusu uboreshwaji wa huduma za afya, Waziri Mkuu ameahidi ujenzi wa kituo cha afya katika kata ya Ilula ili kuwapunguzia wananchi kutembea umbali mrefu hadi Iringa mjini kwa ajili ya kufuata huduma hizo.

Alisema kituo kitakachojengwa kitakuwa na chumba cha kujifungulia, chumba cha maabara kwa ajili ya vipimo mbalimbali, huduma za mama na mtoto, mapasuaji, wodi ya wanaume na wanawake, aliwataka wananchi waendelee kuwa na imani na Serikali yao.

Waziri Mkuu alisema suala la kuboresha na kusogeza huduma mbalimbali za kijamii kwa wananchi zikiwemo za afya limepewa kipaumbele na Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli ambaye anataka kuona wananchi wakiwa na afya nzuri ili waweze kushiriki ipasavyo katika shughuli zao za kimaendeleo.

Kabla ya kuhutubia wananchi kwenye mkutano wa hadhara, Waziri Mkuu alikagua ujenzi wa mradi wa maji Ilula na kuweka jiwe la msingi. Pia, Waziri Mkuu alikagua shughuli za ukarabati wa chuo cha Maendeleo ya Wananchi  Ilula.

Awali, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Josephat Kandege aliwahimiza wananchi hao wajiunge katika Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF) ili wawe na uhakika wa kupata huduma za matibabu ya bure wao na familia zao.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Happi alisema kuwa awali eneo la Ilula lilikuwa linakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo yam ogogoro ya ardhi ambayo kwa kushirikiana na watendaji wenzake walifanikiwa kuitatua.

 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Jumamosi September 28






















Share:

Friday 27 September 2019

Amo training centre tanga Joining instruction 2019/2020

This article contains information on Fomu za kujiunga Chuo cha Afya Amo training centre tanga – Joining instruction Amo training centre tanga Pdf Joining instructions and Admission Letter for Amo training centre tanga Amo training centre tanga Joining instructions and Admission Letter describing the campus and detailing the services and facilities that the College provides for students. Details… Read More »

The post Amo training centre tanga Joining instruction 2019/2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Marekani Kutoa Dola Za Marekani Milioni 120 Kupambana Na Ugonjwa Wa Seli Mundu (Sickle Cell)

Tanzania ni miongoni mwa baadhi ya Nchi zinazotarajiwa kunufaika na kiasi cha dola za Kimarekani milioni 120 zilizotengwa na Serikali ya Marekani kwa ajili ya utafiti wa kupambana na ugonjwa wa  seli mundi (sickle cell).

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Afya wa Marekani Admiral Brett Giroir wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi jijini New York Nchini Marekani.

Admiral Brett ameutaja mkutano wake na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi kama mwanzo mpya wa ushirikiano baina ya Tanzania na Marekani na kuongeza kuwa Nchi yake ina nyenzo zote ikiwemo teknolojia ya kupambana na maradhi ya seli mundu ili kuboresha Maisha ya watoto wanaozaliwa na ugonjwa huo.

Ameongeza kuwa katika siku za hivi karibuni Tanzania imekuwa ikipiga hatua chanya katika kuimarisha masuala mbalimbali ya afya za wananchi wake na kwamba ni azma ya Marekani kuona kuwa ugonjwa wa seli mundo unapata tiba.

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi amesema utafiti na hatimae tiba ya maradhi hayo ya seli mundu kwa kiasi kikubwa itainufaisha Tanzania kutokana na kushika nafasi ya tatu katika Bara la Afrika na ya nne duniani kwa kuwa na wagonjwa wengi wa seli Mundu.

Ameongeza kuwa Tanzania na Marekani zitashirikiana katika kufundisha na kujengeana uwezo wa namna ya kupambana na maradhi ya seli mundu lakini pia kutafuta fedha zitakazowezesha upatikanaji wa dawa ya seli mundu kutokana na ukweli kuwa dawa za ugonjwa huo kwa Tanzania ni miongoni mwa dawa muhimu yaani essential drugs ili iweze kuwafikia wananchi wengi na kwa bei nafuu.

Amezitaja Nchi zilizo na idadi ya watoto wengi wanaozaliwa na ugonjwa wa seli mundu ambapo kwa Afrika Tanzania ni ya tatu baada ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Nigeria nay a nne duniani baada ya India.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki
New York,Marekani


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa, Dalili zake Hizi Hapa..Makala
51 minutes ago

Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kulundia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.


Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.


Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.


Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.


Ugojwa huu wa ngiri unaweza kutibika

Mpate mpenzi wako unayempenda na kumfunga mume,mke mpenzi asitoke kwa mwingine .

Kwa Ushauri na Msaada wa Wasaliana na 
0747100745


Share:

Marekani kupeleka wanajeshi 200 na mifumo ya ulinzi eneo la Ghuba

Mvutano kati ya Marekani na Iran huenda ukaongezeka baada ya Washington kutangaza kuwa inatuma vikosi zaidi vya kijeshi katika eneo la ghuba huku Tehran ikiitaka Saudi Arabia ithibitishe madai kuwa Iran iliishambulia miundombinu ya mafuta ya nchi hiyo.

Wizara ya Ulinzi ya Marekani imesema jana kuwa inapeleka wanajeshi 200 pamoja na mifumo ya kujilinda dhidi ya makombora ili kuimarisha ulinzi wa Saudi Arabia.

Uamuzi huo wa Marekani ambao unajumisha pia kupelekwa kwa rada nne za kijeshi unafuatia mashambulizi ya Septemba 14 kwenye miundombinu ya kuzalisha mafuta nchini Saudi Arabia.

Marekani, Ufaransa, Ujerumani, Uingereza na Saudi Arabia kila moja  zimeilaumu Iran kuhusika na mashumbulizi hayo. 

Iran kwa upande wake imekanusha madai ya nchi hizo na jana Alhamisi rais wa nchi hiyo Hassan Rouhani ametaka utolewe ushahidi kuthibitisha kuwa Tehran ilikuwa nyuma ya hujuma hizo.


Share:

Job Opportunity at AAN Associates, Senior Evaluation/Child protection Expert

Job Opportunity at AAN Associates, Senior Evaluation/Child protection Expert Senior Evaluation/Child protection Expert  AAN Associates is looking for Tanzania based senior Child Protection Expert for a consulting/evaluation opportunity. Evaluation criteria and questions The evaluation criteria are mainly for five areas recommended by the OECD-DAC. Scope 13 regions of Tanzania Time period: from December 2012 to August 2019 Requirement… Read More »

The post Job Opportunity at AAN Associates, Senior Evaluation/Child protection Expert appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Job Opportunity at UN/UNHCR, Protection Associate

Protection Associate  The Protection Associate reports to the Protection Officer. He/she monitors protection standards, operational procedures and practices in protection delivery in line with international standards and provides functional protection support to information management and programme staff. The Protection Associate is expected to coordinate quality, timely and effective protection responses to the needs of populations of concern and… Read More »

The post Job Opportunity at UN/UNHCR, Protection Associate appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Aga Khan University Jobs, Assistant Professors/Lecturers

Assistant Professors/Lecturers in Assessment, Measurement and Evaluation in Education Chartered in 1983, Aga Khan University (AKU) is a private, autonomous and self-governing international university, with 13 teaching sites in 6 countries over three continents (www.aku.edu). An integral part of the Aga Khan Development Network (www.akdn.org), AKU provides higher education in several disciplines, carries out research pertinent to the countries… Read More »

The post Aga Khan University Jobs, Assistant Professors/Lecturers appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

CRM Project Coordinator – Jumia (Full Time) – Tanzania

CRM Project Coordinator – Jumia (Full Time) – Tanzania Jumia Group Intro Jumia is Africa’s leading internet group, with already over 3,000 employees in more than 14 African countries and huge successes such as Jumia, Jumia Travel, Jumia Food, Jumia Deals, Jumia House, Jumia Jobs and Jumia Services. It is led by top talented leaders offering a great… Read More »

The post CRM Project Coordinator – Jumia (Full Time) – Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger