Sunday 2 June 2019

RC MONGELLA AZINDUA RASMI MATUMIZI YA MIFUKO MBADALA "BEI ITASHUKA"


Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akionyesha mifuko mbadaya ambayo ni rafiki kwa mazingira inayopaswa kutumika.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akizungumza kwenye zoezi la kuhamasisha katazo la Serikali kuhusu uzalishaji, usambazaji na matumizi ya mifuko (vibebeo) ya plastiki kuanzia leo Juni 01, 2019.

Mongella ametumia fursa hiyo kuwatoa hofu wananchi wanaodhani inauzwa kwa gharama kubwa akisema nayo itashuka bei kama ilivyokuwa mifuko ya "Rambo" ambayo wakati inaanza kutumika ilikuwa ikiuzwa kwa gharama kubwa na baadae ikashuka.

Zoezi hilo limefanyika katika eneo la Soko Kuu jijini Mwanza na kwenda sambamba na uzinduzi rasmi wa matumizi ya mifuko mbadala ambapo wananchi na wafanyabiashara wamehimizwa kuendelea kusalimisha mifuko ya plastiki katika ofisi mbalimbali ikiwemo Serikali za Mitaa.

Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Wilaya Nyamagana, Dkt. Philis Nyimbi amewahimiza wananchi wa Wilaya hiyo kuwa watiifu kutekeleza katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki na kutumia mifuko mbadala ambayo ni rafiki kwa mazingira.
Naibu Meya wa Jiji la Mwanza, Bhiku Kotecha amesema utekelezaji wa zoezi hilo utazingatia sheria hivyo wananchi waondoe hofu kwani zoezi hilo halitamuonea mtu yeyote na kwa wale ambao bado wana mifuko ya plastiki waendelee kuipeleka katika ngazi husika kama ilivyoelekezwa.
Afisa Mkaguzi kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Abel Sembeka akizungumza wakati wa zoezi hilo ambapo amesema matumizi ya mifuko ya plastiki iliyozuiliwa ni ile inayohusisha vibebeo kama vile "Rambo" na kwamba mifuko ya plastiki ya vifungashio kama karanga, binzari na miwa bado haijazuiliwa.
Katibu wa Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Nyamagana, akitoa salamu zake kwenye zoezi hilo ambapo amesema Serikali itasimamia katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki kwa kuzingatia sheria hivyo wananchi wasiwe na wasiwasi juu ya Serikali yao sikivu.
Viongozi mbalimbali mkoani Mwanza wakifuatilia zoezi la kuhamasisha katazo la Serikali kuhusu uzalishaji, usambazaji na matumizi ya mifuko (vibebeo) ya plastiki.
Wananchi na wadau mbalimbali wa mazingira wakifuatilia zoezi hilo.
Wadau wakiwa kwenye zoezi hilo.
Viongozi wa dini, wafanyabiashara wadogo na wananchi wakifuatilia zoezi hilo.
Wananchi na viongozi mbalimbali wa dini wakinyoosha mikono kuunga mkono katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akionyesha mifuko mbadaya ambayo ni rafiki kwa mazingira inayopaswa kutumika.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akigawa mifuko mbadala kwa baadhi ya viongozi jijini Mwanza ili kuhamasisha matumizi ya mifuko hiyo.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akimsikiliza mmoja wa akina mama wanaouza mifuko mbadala jijini Mwanza ambapo Mongella amesema baada ya muda mfupi ujao, mifuko hiyo itaanza kuuzwa kwa gharama nafuu baada ya wafanyabiashara wakubwa kumaliza taratibu za kuitoa bandarini.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akigawa mifuko mbadala kwa baadhi ya wananchi jijini Mwanza ili kuhamasisha matumizi ya mifuko hiyo.
Meneja wa kiwanda cha Falcon kilichopo jijini Mwanza akionyesha baadhi ya bidhaa ikiwemo mbao zinazotengenezwa kwa kutumia mifuko ya plastiki ambapo amewahamasisha wananchi kukusanya mifuko hiyo na kwenda kuiuza kiwandani hapo badala ya kuitapanya ovyo na kuharibu mazingira.
Baadhi ya wajasiriamali wakisalimisha mifuko ya plastiki kwenye zoezi hilo ambapo kampuni ya kufanya usafi ya GreenWestPro ilitumia zoezi hilo kuhamasisha wananchi na wafanyabiashara kusalimisha mifuko ya plastiki.
Zoezi la kusalimisha mifuko ya plastiki likiendelea jijini Mwanza.
Wananchi wameshauriwa kusalimisha mifuko ya plastiki katika ngazi husika ikiwemo ofisi za Serikali za Mitaa badala ya kuitapanya ovyo na hivyo kuhatarisha mazingira.
Kampuni ya GreenWestPro ni mdau mkubwa wa mazingira ambapo inafanya shughuli zake za usafi na utunzaji wa mazingira katika majiji matatu nchini ambayo ni Dar es salaam, Mwanza na Dodoma.
Kampuni ya GreenWastePro imetumia fursa hiyo kuhamasisha wananchi kuachana na matumizi ya mifuko (vibebeo) ya plastiki na kujikita kwenye matumizi ya mifuko mbadala ambayo ni rafiki kwa mazingira.
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili June 2




Share:

Tamisemi: All girls who passed Form four will Join Form Five or Technical Colleges

Form Five selection, Selection form five 2019/2020 , form five selection 2019/20 first selection form five 2019 pdf tamisemi form five selection 2019 form five second selection 2019/2020 post form five 2019, necta form five selection 2019, www.tamisemi.go.tz form five selection, form 5 selection 2019 pdf download, form five second selection 2019/20

Tamisemi: All girls who passed the Form 4 to  join Form Five, Technical Colleges

Minister of State President’s Office Regional Administration and Local Government Hon. Seleman Jafo said all the girls who succeeded in the Fourth Form exam in 2018 last year have been selected to join the Form five with various technical colleges in the country.

Jafo, he made the same statement today in Dodoma while announcing students selected to join Form Five with vocational education colleges in the year of study that will begin in July, 2019.

“I would like to announce to you the good news that, for this year all the successful girls have been selected to join the Form five with various technical universities, of which a total of 45,816 girls.

Given the performance of the Fourth Form candidates for 2018, from grade one to third, he said 113,825 candidates among them are 47, 779 and 66,046 boys equal to 31.76 percent of all candidates who did the test.

In another phase, the Minister Jafo has called on the councils, especially those of the science and mathematics studies to complete Form five and six classes by March, 2020, which cited Councils as Kyerwa DC, Kilindi DC, DC, Handeni DC, Malinyi, Mtwara DC, Momba DC, Nanyumbu DC and Nanyamba DC, urging Regional Heads and District Heads and Directors of Local Government Authorities to manage closely and ensure the Government’s mandate for each of them and the Formula School is being fulfilled.

Last Minister Jafo has asked all selected students to take into account all the necessary precautions in the case of their final pre-deadline especially for those who are to join the prestigious universities (NACTE).

“We have given a date from 09 June, 2019 to 30 August to have all agreed to join the technical colleges and will fail to do so their positions will be filled with other students.” Said Jafo Minister.

President TAMISEMI’s office has been tasked with the responsibility of overseeing the election of five Formal students and technical colleges from 2014 after the announcement of the Fourth Form Outcomes.

Source: Tamisemi

YOU MAY ALSO LIKE

MORE NEWS ABOUT FORM FIVE SELECTIONS AND JOINING INSTRUCTIONS

The post Tamisemi: All girls who passed Form four will Join Form Five or Technical Colleges appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Saturday 1 June 2019

[FULL PDF DOWNLOAD] Form Five selection 2019

[FULL PDF DOWNLOAD] Form Five selection, Selection form five 2019/2020 , form five selection 2019/20 first selection form five 2019 pdf tamisemi form five selection 2019 form five second selection 2019/2020 post form five 2019, necta form five selection 2019, www.tamisemi.go.tz form five selection, form 5 selection 2019 pdf download, form five second selection 2019/20

Students selected to join form five and Technical Colleges 2019/20 academic year

 

GOOD NEWS!!: YOU CAN NOW EASILY FIND YOUR NAME (FORM FIVE SELECTION NAMES 2019) IN THE PDF FILE ATTACHMENT BELOW, SINCE IT IS NOW AVAILABLE AT UDAHILIPORTAL.COM

CLICK HERE TO ACCESS FULL PDF FILE- FORM 5 SELECTION 2019

 

MORE NEWS ABOUT FORM FIVE SELECTIONS AND JOINING INSTRUCTIONS

The post [FULL PDF DOWNLOAD] Form Five selection 2019 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano 2019

Share:

Yanafunguka Fasta : ORODHA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA TANO 2019

Share:

Breaking : HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO, ELIMU YA KATI NA VYUO VYA UFUNDI 2019

Share:

WAVUTAJI SIGARA HATARINI KUSHINDWA KUSHIRIKI TENDO LA NDOA


Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani na Upasuaji Harisson Chuwa kutoka Hospitali ya Agakhan, amesema miongoni mwa madhara yanayosababishwa na matumizi ya Tumbaku ni wanaume kushindwa kushiriki tendo la ndoa kutokana zao hilo kuathiri zoezi la kusukuma damu mwilini.

Akizungumza kwenye kipindi cha Supamix cha East Africa Radio, Dr Chuwa amesema mbali na wanaume kudai mfumo wa maisha, ikiwemo lishe bora hupelekea kukosa nguvu za kiume lakini pia matumizi ya Sigara na mazao ya Tumbaku, hupunguza nguvu za kiume.

"Madhara mengine ya matumizi ya tumbaku inaweza kusababisha mwanaume kushindwa kushiriki tendo, kwa sababu mishipa ya damu inashindwa kufanya kazi vizuri, ndiyo maana tunasingizia tuna upungufu wa nguvu za kiume, lakini si kweli ni mfumo wa maisha tu wa uvutaji wa sigara" amesema Dr Chuwa.

Aidha Dr Chuwa amesema kuwa "moshi wa sigara una madhara kwa mvutaji mwenyewe na aliyekuwa naye karibu, madhara yanaanzia kwenye saratani ya mapafu, hii ndiyo saratani inayosababishwa na 95% ya matumizi ya sigara, ndiyo maana utakuta wake, waume au watoto wa watu wanaovuta sigara wanapata saratani hii"

Madhara mengine yanayoweza kutokana na matumizi ya tumbaku ni mtoto anapokuwa tumboni, moshi wa sigara unaweza kumuathiri kukua kwa mapafu yake, anaweza kupata pumu na mapafu yanaweza kujaa makamasi, na wakati mwingine inamfanya ashindwe kupumua.

Chanzo- EATV
Share:

ATUPWA JELA MIAKA 30 KWA KUKUTWA NA BANGI


Mkazi wa Kijiji cha Majengo, Kata na Tarafa ya Mtama, Wilaya ya Lindi Ramadhani Haji Juma, amehukumiwa kwenda gerezani kutumikia kifungo cha miaka 30, baada ya kupatikana na hatia ya kujihusisha na madawa ya kulevya aina ya Bangi yenye uzito wa Kilo 7.8 kinyume cha sheria.

Hukumu hiyo imetolewa na Hakimu wa Mahakama ya Wilaya ya Lindi, Liliani Rugalabamo,baada ya Mshtakiwa kukiri kosa lililomkabiri bila ya kulazimishwa.

Baada ya mshitakiwa kukiri kosa, Hakimu Rugalabamo alimuuliza mshtakiwa kama anazo sababu zitakazoishawishi Mahakama isimpe adhabu kali, Ramadhani Haji Juma aliomba asipewe adhabu kali, akidai ni mkosaji wa mara ya kwanza na alilazimika kujiingiza kwenye Biashara hiyo kwa lengo la kujipatia riziki ya kila siku.

"Mh,Hakimu naiomba Mahakama yako tukufu inisamehe na sitarudia kufanya kosa la aina hii tena kushiriki kazi hii "Amesema Ramadhani.

Kufuatia utetezi huo, hakimu Rugalabamo alirejea kwa Mwanasheria wa Serikali, Yahaya Gumbo iwapo anazo kumbukumbu za makosa ya zamani kwa mshtakiwa na kujibu hana, huku akiiomba mahakama impatie adhabu kali ili iwe fundisho kwake na wengine walio na tabia ya aina hiyo.

Hakimu Rugalabamo akimpatia mshitakiwa adhabu katika kesi hiyo Namba 41/2019, alipinga utetezi huo kwa kusema hauna mashiko, kwani zipo njia nyingi za halali kama vile kuitumia ardhi iliyopo kuzalisha mali, yakiwemo mazao ya chakula na biashara ili kuondokana na umasikini.
Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya June 1




Share:

Friday 31 May 2019

WADAU WAANZA KUJITOKEZA KUMSAIDIA BINTI ANAYEUGUA UGONJWA WA NGOZI MWAKA WA 16 SASA

Share:

NAMNA WAKULIMA WANAVYOPOTEZA FURSA KWA KUTOKUCHANGAMKIA FURSA


Kaimu Mkurugenzi Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dk Fortunatus Kapinga akionyesha maziwa yanayotegenezwa kwa kutumia korosho.
Kaimu Mkurugenzi Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dk Fortunatus Kapinga akionyesha maziwa yanayotegenezwa kwa kutumia korosho.
Mtafiti kutoka kituo cha utafiti wa kilimo Tari- Naliendele, Regina Msoka akinyesha bidhaa zinazotengenezwa kwa kutumia mabibo ya korosho, juisi kusho na kulia ni mvinyo.
Mtafiti kutoka kituo cha utafiti wa kilimo Tari- Naliendele, Regina Msoka akinyesha bidhaa zinazotengenezwa kwa kutumia mabibo ya korosho, juisi kusho na kulia ni mvinyo.
Chupa zenye mvinyo ulio tayari kwa ajili ya kwenda sokoni.

Chupa zenye maziwa yanayotengenezwa kwa kutumia korosho.
****
Mara nyingi wakulima wa korosho hulima zao hilo kwa lengo la kuuza korosho ghafi ambazo kwa kiasi kikubwa husafirishwa kwenda nje nchi na baadhi yao wachache huzibangua ili kuziongezea thamani.
Lakini bado wamekuwa wakipoteza mapato kwa kiasi kikubwa kutokana na kutotumia vyema fursa inayopatikana kwenye korosho.
Kutokana na utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele katika zao hilo mkulima anaweza kuzalisha bidhaa nyingine kwa mbali na ile korosho anayoiuza ikiwa ghafi.
Katika zao hilo kuna tunda la bibo ambalo wakati wa mavuno mkulima hulazimika kutenganisha bibo na korosho ndipo apeleke korosho ghalani. Wakulima wengi huyateketeza kwa moto licha ya kuwa yanafaa kuzalisha bidhaa kama mvinyo, jam na juise’
Mtaalamu kutoka kituo cha utafiti wa kilimo Tari- Naliendele, Regina Msoka anasema mkulima anapopata kilo moja ya korosho ghafi shambani anaacha mabibo kilo tisa huku akiambulia kati ya Sh 2,400 hadi 4,000 kulingana na bei ya mnada.
“Mkulima akipata kilo moja ya korosho  ghafi maana yake ameacha kilo tisa za mabibo shambani unaweza kuona ni jinsi gani anaacha bidhaa ambayo ni muhimu shambani,”anasema Msoka
Anabainisha katika katika kilo tisa ya mabibo yakisindikwa na kutengenezea mvinyo na kuuthaminisha ana uwezo wa kupata Sh 100,000 huku kilo moja pekee ya korosho hazidi Sh 4,000.
“Ukipiga hesabu za haraka katika kilo kumi za korosho ana mabibo kilo 90 maana yake ana Sh 40,000 ya korosho na ambaye anatumia mabibo kutengeneza mvinyo ana Sh 1milioni kwa hiyo hapo unaona ni faida gani iliyopo kwenye mabibo,”anasema Msoka na kuongeza;
“Tumefanya utafiti teknolojia zipo tuna uwezo wa kutengeneza juisi ya mabibo ambayo haina ukakasi, ambapo katika mabibo kilo moja unapata nusu lita ya juisi,wengi wanakimbia bibo sababu ya ule ukakasi wake,sisi tumefanikiwa kuutoa na pia tunapata juisi nzuri, tunapata jam na pia mashine zinapatikana Sido na tunaendelea kutoa mafunzo kwa badhi ya wakulima,”anasema
Kutokana na bibo kutohifadhika kirahisi anasema baadhi ya wakulima huyakausha na kutenegenezea pombe za kienyeji maarufu kama ulaka ambazo hazijathibitishwa kwani kiutaalamu.Anasema kitaalamu yanapaswa kutunzwa sehemu yenye ubaridi (cold room).
Muda wa kupata mvinyo, jam na juisi
Ili kupata mvinyo uliokamilika inahitajika miezi mitatu ili kuyasindika mabibo ili ukomae ambapo kilo moja ya mabibo una uwezo wa kuzalisha lita moja ya mvinyo.
Ili kupata juisi zinahitajika siku mbili ambapo mtengenezaji anahitaji mabibo kilo moja ili kupata nusu lita ya juisi na kwa jam ni siku moja.
Utengenezaji  siagi ya korosho na maziwa
Mtafiti Msoka anasema kwa kutumia  kilo moja ya daraja la mwisho ambalo ni vipande vidogo vya korosho (small pieces WW450) baada ya kubanguliwa na kupangwa katika madaraja unaweza kutengeneza siagi kilo moja ambayo huuzwa Sh 20,000 na korosho hizo thamani yake ni Sh 10,000 kwa kilo.
 “Badala ya kuuza korosho Sh 10,000 natengeneza siagi kilo moja na kuuza Sh 20,000,nikitoa gharama za uzalishaji bado nitakuwa na faida, na nikitumia kilo moja hiyo hiyo ya korosho nina uwezo wa kupata maziwa takribani lita tatu ambazo nitaziuza Sh 25,000,”anasema
Kuhusu madaraja ya korosho,Kaimu Mkurugenzi Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Naliendele, Dk Fortunatus Kapinga anasema kwenye saizi ya mbegu kiutafiti wamefanikiwa kuwa na mbegu ambazo zina ukubwa unaostahili  kwenye soko kwa maana zinazokidhi daraja kubwa na kuvutia wanunuzi kutoka nje.
Anafafanua daraja la mbegu 500 nchini hazipo na badala yake zipo zinazokidhi daraja kubwa la mbegu 180 huku zile za daraja la 450 zikiwa ni chache sana na ndizo hutengenezea maziwa na siag.
“Korosho za Tanzania zina ubora wa kimataifa unaokubalika kwa sababu tuna mbegu ambazo tumezizalisha na tumezigundua zina sifa za soko la kimataifa na ndio maana tunahimiza wakulima wetu wapande mbegu bora kutoka Naliendele il tunapoenda kwenye ushindani soko lolote la kimataifa hakuna anayetushinda,”anasisitiza Dk Kapinga
Anafafanua kutokana na baadhi ya watu kama watoto kushindwa kutafuna korosho au kuwa na mzio (allergy) ya maziwa ya ng’ombe ndio sababu za wao kuwa na utafit wa maziwa ya korosho.
Upatikanaji wa malighafi
Msoka anasema malighafi wanazotumia kutengeneza mvinyo,jam na juisi hupatkana katika mashamba yao ya utafiti huku korosho zinazotengenea ,maziwa na pinetbutter hutokana na korosho zinazobanguliwa katika kiwanda kilichopo kwenye taasisi hiyo kwa ajili ya utafiti.
Mwakilishi wa mkurugenzi mkuu wa Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech) Dk Bakari Msangi anasema kwa kuwa Taasisi ya Utafiti wa kilimo Naliendele imeshafanya utafiti na kuthibitisha teknolojia inayoweza kutumika watu wachangamkie fursa.
Anasema wafanyabiashara wakubwa wanatakiwa kuona fursa na kuweka viwanda katika mikoa inayozalisha korosho kwa kuanzisha viwanda vitakavyozalisha bidhaa zitakazotokana na mabibo.
“Wanachotakiwa ni kuona tayari katika level ya research tumeprove teknolojia kwamba inaweza na tumeshatoa product zinazoingia sokoni, kwa hiyo tunawavutia wawekezaji wa ndani na nje waone umuhimu wa kuweka viwanda,”anasema Dk Msangi
Hata hivyo, anasema kwa kuwa sasa ni uchumi wa viwanda hawawalengi tu wajasiriamali wadogo, bali wafanyabiashara wakubwa na watunga sera wote.
“Watu wote wanaoongelea sera za nchi wajitahidi kuitangaza teknolojia hii ambayo imeshahakikiwa na Naliendele kuhamasisha watu kuwekeza katika maeneo yanayozalisha korosho ili kutumia hii product (bidhaa) ambayo inapotea,ni potential area,”amesema Dk Msangi
Wakulima
Mkulima Elisha Millanzi anasema katika msimu mmoja ana uwezo wa kupata korosho tani mbili hadi tatu na mabibo yatokanayo na korosho hizo hutengeneza juisi ya kunywa wawapo shmbani na yanayosalia ambayo ni mengi huyateketeza kwa moto pindi yanapokauka.
Pia, anasema wapo baadhi ya watu huyatumia kutengenezea pombe maarufu kama ulaka pindi yanapokuwa mabichi na hutumika katika familia na hutumika kama burudani ya familia na wengine huyakaush na kutengenezea pombe ya gongo ambayo hairuhusiwi.
“Unapokula bibo linakuwa na asili ya sukari, mara nyingi tunakamua na kuchuja na kunywa bila hata kuweka sukari wala kuongeza maji, hata kama uko shambani umekosa maji ya kunywa unayakamua na kunywa,”anasema Millanzi
“Kama serikali ikituletea viwanda vya kutengeneza bidhaa nyingine itakuwa imetusaidia kwa sababu tunatupa rasilimali nyingi, mtu akivuna tani kumi ina maana kila korosho moja ilikuwa na bibo lake moja hapo mabibo na yenyewe ni tani kumi au zaidi,”
Mikakati iliyopo
Mbunge wa Tandahimba, Katani Katani anasema baadhi ya wakulima hutengeneza pombe asili ya gongo ambayo haina viango na hairuhisiwi nchini na hivyo kupelekea mabibo mengi kuteketezwa.
Anasema utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa kilimo Naliendele unahitaji mashine zitakazotakiwa kufanya uzalishaji.

“Bahati nzuri waziri wa kilimo tulifika naye Naliendele anajua mabibo yanaweza kutengeneza mvinyo, kwa hiyo tunajaribu kuangalia namna iliyo sahihi tuweke kwenye sera ya kuona hilo jambo linaweza kuwanufaisha wakulima kwa namna nyingine,”anasema Katani

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger