Sunday 28 April 2019

Rais Magufuli: Nilitamani Kuwa Askofu, Sijui Nini Kilitokea

Rais  Magufuli amesema alipokuwa mdogo alitamani kuwa Askofu lakini hajui ni nini kilitokea akashindwa kuingia katika njia hiyo.

Akizungumza katika ibada ya kuzindua Jimbo Kuu la Kanisa Katoliki Mbeya na kumsimika Askofu Mkuu, Gervas Nyaisonga, Rais Magufuli amesema anashanga hadi sasa pamoja na matamanio yake hayo ameshindwa kuwa hata Katekista au Mwenyekiti wa jumuiya.

“Nilitamani sana kuwa Askofu lakini sijui ni nini kilitokea nikashindwa kuwa hata Katekista lakini au hata mwenyekiti wa Jumuiya.

“Leo nimefurahi na ninawaonea wivu Maaskofu, nilitamani niwe huko lakini niko huku, mlioko huko msitoke ni pazuri, sasa hivi niko huku na bado natamani kuja huko,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli pia aliwakumbusha Maaskofu kuhusu wito wa kazi ya uaskofu kupitia Kitabu cha Biblia cha 1Timotheo 3:1 unaosema “Ni neno la kuaminiwa mtu akitaka kazi ya Askofu atamani kazi njema.”

Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Polycarp Kadinali Pengo, amelitaka Kanisa kutimiza wajibu wake wa kuwasimamia waumini kiroho bila kusahau kutoa ushirikiano kwa serikali katika kuweka mazinga mazuri ya kiutawala.

“Tunahitaji uwepo wa roho mtakatifu katika kuboresha mazingira ya waumini ambao wanatambua vyema wajibu wao katika kuwaongoza vyema waumini, serikali ndiyo inayoweza kulifanya hili katika upeo mpana wa kiutawala, ili roho mtakatifu aweze kutenda kazi tunahitaji kuwa na kanisa linaloshirikiana vyema na serikali,” amesema Kadinali Pengo.


Share:

LIVE: Rais Magufuli Akiwa Kwenye Ibada Ya Kusimikwa Askofu Mteule Mbeya

LIVE: Rais Magufuli Akiwa Kwenye Ibada Ya Kusimikwa Askofu Mteule Mbeya


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521


Share:

Chama cha wenye ulemavu wa Ngozi Tanzania (TAS) chalaani vitendo vya ufukuaji makaburi.

Chama Cha Watu Wenye Ualbino Tanzania kwa masikitiko kinauarifu umma kuhusu tukio la kaburi la marehemu Aman Anywelwisye Kalyembe mwenye Ualbino, aliyezikwa mwaka 2015 kufukuliwa usiku wa kuamkia tarehe 23/4/2019 katika kijiji cha Ibililo kata ya Nkunga wilayani Rungwe ambapo wahusika waliondoka na masalia ya viungo vya marehemu. 

Tukio hili la tatu kwa mkoa wa Mbeya limeibua simanzi na hofu kwa  Watu Wenye Ualbino na familia zao, kwa uzoefu kuwa linahusishwa na imani za kishirikina hasa kipindi hiki tunapoelekea mwaka wa uchaguzi 2020. Ni ishara wazi ya ukatili kwa Watu Wenye Ualbino si tuu wakiwa hai bali hata wakiwa wafu.

Chama cha watu wenye ualbino Tanzania kinaungana na wadau na wote wenye mapenzi mema kukemea vikali tukio hili ovu. 

Ni tukio ambalo limejitokeza wakati baadhi ya wenzetu wako katika vituo maalum, huku kiu yao na jitihada za serikali na wadau wengine ikiwa ni kuona wanarejea kuishi na familia zao, ndugu zao, marafiki na jamii zao katika maeneo yao. 

Tukio hili  linarejesha hofu kwa Watu Wenye Ualbino na familia zao kwani ni tukio la 23 la vitendo ovu vya ukiukwaji wa heshima ya makaburi ya watu wenye ualbino likihusishwa na imani za kishirikina.

Watu Wenye Ualbino na familia zao watafurahi kuona serikali inachukua hatua stahiki kwa wakati ili matokeo mazuri tuliyokuwa tumeyafikia, yakiwemo: watoto wenye ualbino kuanza kuandikishwa shule za kawaida ndani ya maeneo yao na vituo vingi vikiwepo Buhangija (Shinyanga) na Kabanga (Kigoma) kuanza kupunguza idadi ya watoto na watu wazima wenye ualbino, yawe endelevu.

Tunamwomba Mhe. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuingilia kati suala hili, ikiwa ni kutumia nafasi yake kukemea uovu huu na kuwezesha kifedha mikakati iliyopo na itakayokuwepo yenye nia ya kukomesha uovu huu dhidi ya Watu Wenye Ualbino na zaidi  jamii ipate hamasa na kuziacha fikra potofu na matendo ya kishirikina.

 Miongoni mwa mipango tunayoomba iwezeshwe na serikali ni pamoja na:
1.    Mpango kazi wa kutokomeza mauaji na ukatili wa watu wenye ualbino Tanzania uliondaliwa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora kwa kushirikiana na wadau wengine.
2.    ‘Cross-Border Cooperation Plan on Preventing and Combating Trafficking and the Protection of Persons with Albinism in Malawi, Tanzania and Mozambique’ Ulioandaliwa na International Organisation for Migration (IOM), serikali kwa uwakilishi kupitia wizara ya Mambo ya Ndani  na wadau wengine.
3.    ‘Joint Programme for the Protection and Wellbeing of People with Albinism in Tanzania’ Ulioandaliwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa uratibu wa UNESCO kwa ushirikiano na wadau wengine.
4.    ‘ACTION STRATEGY: Minorities and Other Vulnerable Groups’ ulioandaliwa na Tanzania Human Rights Defenders Coalition (THRDC) kwa ushirikiano na wadau wengine.   
5.    ‘Regional Plan of Action on Albinism adopted on May 22, 2017 by the African Commission on Human and Peoples' Rights’ ulioandaliwa na mtaalamu wa kujitegemea wa UN akisimamia haki za watu wenye ualbino.

Tunaitaka serikali katika ngazi zote wakati huu wa kuelekea chaguzi za serikali za vijiji na mitaa na kwenye uchaguzi mkuu mwakani 2020 kuweka ajenda ya hamasa kwa jamii kuhusu ualbino na athari za vitendo vya kishirikina kwenye kampeni zao. 

Jeshi la Polisi limefanya kazi nzuri na ya kupongezwa kwa kipindi cha miaka kadhaa iliyopita. Juhudi zao zimechangia kupungua kwa matukio. Mafanikio haya yamechangiwa pia na jamii kutoa ushirikiano hivyo tunaomba mtu yeyote mwenye taaifa yoyote kuhusiana na matukio haya afikishe jeshi la polisi au awasiliane nasi kwa wakati ili kufanikisha kuwakamata watu hawa waovu. Tunamsihi sana IGP Simon Sirro kuongeza kasi hasa katika upelelezi na kushiriki katika mchakato wa kuelimisha na kuhamasisha jamii kulinda na kuheshimu utu na uhuru wa Watu Wenye Ualbino na familia zao.

Mahakama zina mchango mkubwa kukomesha mauji kupitia adhabu kali ili iwe kama elimu na fundisho kwa jamii. Watu Wenye Ualbino wana imani na Mheshimiwa Jaji Mkuu na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa ujumla wakitarajia kwamba kesi zilizochukua muda mrefu zitashughulikiwa ziishe kwa wakati sanjari na adhabu stahiki kutolewa kwa watakaobainika kuwa na hatia.

Kutokana na matukio haya, Watu Wenye Ualbino na familia zao ni vyema kuendelea kuchukua tahadhari stahiki kwa ajili ya ulinzi wao wakati wote. Toa taarifa polisi na au mamlaka za karibu mapema iwezekanavyo uonapo kiashiria chochote cha uhalifu ili jitihada za kuzuia zifanikiwe.

Vyombo vya habari, viongozi wa dini, serikali kupitia viongozi wa kisiasa, Wizara na taaisi nyingine za kiserikali na za kiraia tuongeze juhudi hasa katika elimu kwa jamii kwa njia mbalimbali ambazo ni endelevu, hii itasaidia sana kuibadili jamii kifikra  ili hatimaye utu wa mtu mwenye ualbino uthaminike.

Mungu ibariki Tanzania

Nemes Colman Temba
Mwenyekiti – Taifa
Chama cha watu wenye Ualbino Tanzania
Aprili 27, 2019

Kwa mawasiliano
Simu (ofisi): 022 2110527
Mob. (Mwenyekiti): 0784 874 592
Email:   info@tas.or.tz




Share:

Rais Magufuli Ataja Sababu za Kutengua Uteuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Chunya

Rais John Magufuli amesema alimtoa aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Chunya, Rehema Madusa kwa sababu alikuwa akichoma mazao ya wananchi kwa madai kuwa wamelima ndani ya hifadhi za wanyamapori.

Rais Magufuli ameyasema hayo jana Aprili 27, 2019  katika mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Sabasaba wilaya ya Chunya mkoani Mbeya ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake mkoani humo.

Alisema licha ya asilimia 32.5 ya eneo lote la Tanzania kuwa na wanyama lakini baadhi ya maeneo hayo yamechukuliwa na kiasi cha pesa kinachopatikana hakijulikani.

“Sasa kama fedha nyingine hatujui zinakokwenda inakuwaje mtu aliyeamua kulima katika eneo la hifadhi wewe umchomee, nilikuwa nimekaa naangalia katika televisheni mtu na rehema zake unamchomea chakula ili akale wapi,” alihoji Magufuli.

“Ukimchomea mahindi yake kesho tena utampelekea mahindi ya kula, kwa hiyo hata msitafute sababu nyingine ni hiyo,” amesema Magufuli

“Yalikuwa mambo ya ajabu sana, nikamuambia mkuu wa mkoa (aliyekuwa- Amos Makala) lakini nikaona na yeye anafanya mambo kidogo kidogo nikaona ngoja nimtoe Mbeya nimpeleke Katavi kwa uangalizi zaidi,”

“Ndiyo maana tukatengeneza timu ya mawaziri waangalie maeneo ambayo zamani yalikuwa hifadhi za wanyama na hayatumiki tutayakata yatakuwa maeneo ya watu.”


Share:

Wanajeshi na wapinzani wa Sudan wafikia makubaliano ya kubuni Baraza la Pamoja

Wanajeshi wanaotawala kwa sasa Sudan na makundi ya upinzani ya nchi hiyo wamefikia makubaliano ya kubuni Baraza la Pamoja kwa ajili ya kuendesha masuala ya nchi hiyo.

Akitangaza habari hiyo, Ahmad ar-Rabii' mmoja wa wakilishi wa makundi ya upinzani amesema kwamba katika kikao chao kilichofayika jana Jumamosi mjini Khartoum, wapinzani na Baraza la Kijeshi wamekubaliani umuhimu wa kubuniwa Baraza la Pamoja la wanajeshi na wapinzani kwa ajili ya kuendesha kwa muda masuala ya Sudan. 

Ar-Rabii' ambaye alihudhuria kikao hicho amesema kwamba mazungumzo yangali yanaendelea kuhusu kuainishwa kwa idadi ya wanajeshi na wapinzani watakaojumuishwa katika baraza hilo la pamoja.

Kikao hicho cha pamoja kati ya wanajeshi na wapinzani kimefanyika siku moja baada ya muungano wa upinzani kwa jina la 'Makundi Yanayopigania Uhuru na Mabadiliko' kutangaza habari ya kubuniwa ujumbe wa wapinzani kwa ajili ya kufanya mazungumzo na wanajeshi. 

Baraza la Kijeshi la Sudan lilibuniwa baada ya Rais Omar al-Bashir wa nchi hiyo kung'olewa madarakani na wanajeshi tarehe 11 Aprili. 

Baraza hilo lilikuwa limetangaza awali kwamba lingetawala kwa muda wa miaka miwili kabla ya kukabidhi madaraka kwa raia. 

Wananchi na makundi ya upinzani wamekuwa wakifanya maandamano na mgomo mbele ya makao makuu ya wanajeshi mjini Khartoum kwa ajili ya kushinikiza raia wakabidhiwe madaraka nchini.


Share:

Naibu Waziri Ikupa Alipongeza Shirika La Compassion International Kwa Kusaidia Watoto Na Vijana Nchini

Na. Mwandishi Wetu
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Stella Ikupa amelipongeza Shirika lisilo la kiserikali la Compassion International Tanzania (CIT) kwa kuwahudumia na kuwapatia watoto na vijana stadi za maisha zinazowawezesha kujitegemea.

Naibu Waziri Ikupa ametoa pongezi hizo wakati wa Maadhimisho ya Miaka 20 ya Shirika hilo yaliyofanyika  jana  Aprili 27, 2019 katika ukumbi wa Kanisa la TAG lililopo Mipango, Jijini Dodoma. Maadhimisho hayo yalikuwa na Kauli Mbiu isemayo; “Wekeza kwa Watoto na Vijana kwa Uchumi Endelevu.”

Alieleza kuwa Shirika la Compassion International Tanzania limekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha watoto na vijana nchini wanahudumiwa na kuondokana na hali ya umasikini kwa kuwa chachu ya maendeleo kwa jamii na Taifa.

“Shirika hili ni la mfano na limeendelea kuunga mkono jitihada za Serikali katika kuwalinda watoto na kuwapa fursa ya kufikia ndoto zao na kuwapatia vijana ujuzi wa stadi za maisha zinazoleta mabadiliko chanya kwao na kuwaletea maendeleo yao binafsi na Taifa kwa ujumla,” alisema Ikupa

Aliongeza kuwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amekuwa akionesha watanzania namna gani nchi yetu imeweza kujitegemea katika kutekeleza shughuli mbalimbali, hivyo Mhe. Rais ni mfano tosha wa kuigwa na vijana nchini kwa kuona wanauwezo wa kujitegemea.

Aidha, Naibu Waziri Ikupa alitoa rai kwa vijana kuacha kukaa kwenye vijiwe bila sababu za msingi na kubadili mitazamo, bali watumie muda wao kutafakari shughuli za kufanya kwa bidii ambazo zitawaletea maendeleo na kuwawezesha kujikwamua kiuchumi.

“Serikali imekuwa ikitoa mikopo kwa vijana ili waweze kuanzisha shughuli mbalimbali zitakazo wawezesha kukua kiuchumi, tumieni fursa ya ujuzi mliopata kupitia shirika hili na ubunifu mlionao kuchangamkia fursa hiyo muhimu itakayowawezesha kuanzisha miradi mbalimbali ikiwemo viwanda,” alisema Ikupa

Pia alitoa wito kwa jamii kuripoti haraka vitendo vya unyanyasaji wa watoto katika madawati ya jinsia na watoto yaliyopo kwenye vituo vya polisi nchini na kwa maafisa ustawi wa jamii ili kutokomeza vitendo hivyo kwa kumjengea mazingira salama motto na kumuonesha jamii yake imejaa upendo.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Taifa wa Shirika la Compassion International Tanzania, Bi. Agness Stanley Hotay alisema kuwa wataendelea kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha wanawatetea na kuwasimamia watoto na kuwapatia nafasi vijana ya kujitambua kwa kuchangamkia fursa ambazo zipo katika jamii na kuleta ufumbuzi wa kimaendeleo.  

“Maono ya shirika ni kuona wanufaika wanatoka katika uhitaji na kujijengea dhana ya kujitegemea, vilevile kuwa wahisani wa watu wengine,” alisema Hotay

Shirika la Compassion International Tanzania (CIT) ni sehemu ya Compassion International ambalo ni shirika la kimataifa la Kikristo linalojihusisha kuhudumia watoto na vijana wanaotoka katika kaya maskini kwa njia ya ufadhili. Shirika hili limekuwa likifanya huduma hii hapa nchini toka mwaka 1999.

Kwa sasa Shirika hilo lipo katika Mikoa 19 ya Tanzania Bara ambayo ni Arusha, Dar es Salaam, Kigoma, Manyara, Pwani, Morogoro, Iringa, Dodoma, Kilimanjaro, Singida, Shinyanga, Mwanza, Mara, Tabora, Lindi, Geita, Mtwara, Simiyu na Kagera.


Share:

Orodha Ya Majina Ya Walimu Walioajiriwa Shule Za Msingi Na Sekondari April, 2019

Serikali kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI) imepata kibali Cha kuajiri jumla ya walimu 4549 Kati ya 91108 walio tuma maombi yao.

 Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Seleman Jafo amesema kuwa Rais Dk.John Pombe Magufuli katika kuhakikisha Serikali inawahudumia vizuri wananchi ameamua kufungua dirisha la ajira kwa walimu.

Jafo alisema jumla ya waombaji 91108 waliojitokeza na kutuma maombi yao katika nafasi mbalimbali na kati ya hayo 43770 sawa na asilimia 48.04 yalikuwa na viambatanisho vyote vilivyohitajika.

Hata hivyo alieleza kuwa maombi 47338 sawa na asilimia 51.96 hayakuwa na vigezo ikiwa ni pamoja na kukosa viambatanisho muhimu vilivyohitajika.

==>>Tazama Hapo chini




Share:

Waziri Mkuu Aagiza Mabango Ya Utalii Yawekwe Uwanja Wa Ndege Wa KIA

*Ni yenye kuonyesha wanyama, milima, fukwe, mambo ya utamaduni

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameuagiza uongozi wa bodi ya KADCO uhakikishe unaweka mabango ya kielektroniki yenye kuonesha vivutio vya utalii kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

“KADCO na Wizara ya Maliasili na Utalii, shirikianeni kuweka utaratibu wa kutangaza vivutio vyetu vya utalii hasa wanyama kwenye viwanja vyote vya ndege. Tunazo mbuga, milima, fukwe za bahari na ngoma za makabila mbalimbali, wekeni mabango yanayobadilisha picha.”

“Screens zenye wanyama wanaobadilikabadilika zinaleta mvuto lakini pia ni fursa ya kutangaza vivutio vyetu. Nimezunguka humu ndani, kuta zote ni nyeupe tu, tumieni fursa hiyo kutangaza tamaduni zetu na vivutio tulivyonavyo," Waziri Mkuu alimweleza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO), Mhandisi Christopher Mukoma.

Alitoa agizo hilo jana mchana (Jumamosi, Aprili 27, 2019) wakati akikagua miundombinu ya uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA) mara baada ya kuwaaga watalii 274 kutoka Israeli wanaowawakilisha wenzao 1,000 walioondoka nchini jana kurejea kwao.

Akiwa uwanjani hapo, Waziri Mkuu alikagua eneo la mapokezi, sehemu ya abiria wanaoondoka na wanaowasili, sehemu ya uhamiaji, mashine za kukagua mizigo ya wanaoondoka na wanaowasili, sehemu za kutolea huduma na maduka.

Pia alimwagiza Mrakibu Mwandamizi wa Uhamiaji kwenye kiwanja hicho cha ndege, Bw. Filbert Ndege awasiliane na makao makuu yake ili waangalie uwezekano wa kuongeza madirisha ya kutolea huduma za uhamiaji (counters) ili huduma hiyo itolewe kwa kasi zaidi.

“Angalieni cha kufanya, ikibidi eneo hili lipanuliwe na counters nyingine ziongezwe ili kufast-track utoaji wa huduma hasa msimu ambao watalii wengi huingia nchini.”

Pia aliwataka KADCO waboreshe eneo la maegesho ya magari kwa kufanya upanuzi na kujenga maturubai ya vivuli (shades) ili kuyakinga na jua kali magari ya wateja.

(mwisho).

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
JUMAPILI, APRILI 28, 2019.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili ya April 28




Share:

Saturday 27 April 2019

REFA KAMBUZI NA WENZAKE WALIOISAIDIA SIMBA SC DHIDI YA KMC JANA KIRUMBA WAFUNGIWA


Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limewaondoa refa Abdallah Kambuzi na wasaidizi wake, Godfrey Msakila na Consolata Lazaro kwenye orodha ya marefa wa Ligi Kuu ya soka Tanzania Bara kwa mechi zilizobaki.

Hatua hiyo inakuja siku moja baada ya watatu hao kuboronga katika maamuzi yao wakichezesha mechi ya Ligi Kuu baina ya KMC na Simba SC, zote za Dar es Salaam Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.

Simba SC iliendeleza wimbi la ushindi katika Ligi Kuu jana baada ya kuwachapa KMC 2-1, hivyo kufikisha pointi 66 baada ya kucheza mechi 26 na kupanda hadi nafasi ya pili ikiizidi kwa wastani wa mabao tu, Azam FC inayoangukia nafasi ya tatu, huku Yanga SC ikiendelea kuongoza kwa pointi zake 74 za mechi 32.

Lakini katika ushindi huo, ilionekana kabisa kulikuwa kuna mbeleko ya marefa, hatua ambayo imeifanya TFF isisubiri hadi Bodi ya Ligi itakapokuja kukaa baada ya muda mrefu na kuingilia kati kuwachukulia hatua waamuzi hao kwa kuutia doa mchezo.

Marefa hao wanadaiwa kuwapa Simba SC penalti mbili za utata jana ambayo moja walikosa, lakini pia kuwanyima KMC penalti na kutoa maamuzi mengine ya ovyo katika matukio ya kuotea.
Share:

Pigo kwa Kenya baada ya China ‘kukataa’ kuipa mkopo wa kujenga reli (SGR)

China imekataa kwa mara ya pili kutoa mkopo kwa ajili ya kufadhili awamu ya tatu ya ujenzi wa reli ya kisasa nchini Kenya (SGR) kutoka Naivasha hadi Malaba.

Uamuzi huo wa China wa kukataa kuipa Kenya mkopo huo ambao imekuwa ikiomba kwa muda sasa, unaziweka katika sintofahamu awamu mbili za ujenzi wa reli hiyo (Mombasa hadi Nairobi, na Nairobi hadi Naivasha).

Badala ya kupata mkopo wa kujenga SGR, Kenya imeweza kupata mkopo wa TZS bilioni 906.8 kwa ajili ya kukarabati reli ya zamani (meter gauge) ambayo sasa italazimika kuunganishwa na SGR ili kuwezesha usafirishaji wa mizigo kutoka Mombasa kwenda Uganda.

Kenya ilikuwa inahitaji mkopo wa TZS trilioni 8 kwa ajili ya kukamilisha awamu hiyo ya mwisho ya ujenzi wa reli hiyo, na kuiunganisha na Uganda.

Kufuatia uamuzi wa China, baadhi ya wataalamu wa uchumi wamesema kuwa sasa Kenya imebakiwa na reli ambayo haiendi popote (a railway to nowhere), huku mkopo uliotumika kutengeneza awamu mbili za kwanza ukitakwa kuanza kurejeshwa.

Waziri wa Usafiri wa Kenya, James Macharia  alisema kuwa wameafikiana na China waikarabati kwanza reli ya zamani, ili SGR kutoka Nairobi hadi Naivasha itakapokamilika mwezi wa 8, mizigo inayotoka Mombasa iweze kufika Malaba kwa wakati.

Hata hivyo imeelezwa kuwa masharti magumu ndiyo yaliyosababisha Kenya kushindwa kupata mkopo huo, ambapo China ilikata kutoa sehemu za fedha hizo kama ruzuku, lakini pia iimetaka kuwepo na maelezo ya namna reli hiyo itakavyozalisha faida kabla ya kufadhi ujenzi huo wa Naivasha.

Reli hiyo ya Kenya tayari imekamilika katika sehemu ya Mombasa hadi Nairobi huku kipande cha Nairobi hadi Naivasha kikitarajiwa kukamilika Agosti mwaka huu.

Tangu kuzinduliwa kwa reli ya Mombasa hadi Nairobi Juni 2017, tayari abiria milioni 2.6 wameshatumia usafiri huo huku mizigo yenye tani 3.6 ikiwa imesafirishwa.

Katika mwaka wake wa kwanza wa kutoa huduma, reli hiyo ilipata hasara ya TZS bilioni 227, ambapo waziri mwenye dhamana alisema hasara hiyo ilitarajiwa kutokana na uelewa mdogo wa wananchi kuhusu usafiri huo.


Share:

Rais Magufuli Akemea Vitendo Vya Ubakaji na Ulawiti Jijini Mbeya

Rais Dk John Magufuli amekemea vikali vitendo vya ubakaji vinavyoendelea jijini Mbeya, amewataka viongozi na wananchi kushirikiana kwa pamoja kutokomeza tatizo hilo kwa kuwachukulia hatua wanaohusika na vitendo hivyo.

Ametoa kauli hiyo Jumamosi Aprili 27, wakati akizungumza na Wananchi wa wilaya ya Chunya mkoani humo katika ziara yake ya kikazi ya siku nane ambapo ameshazindua barabara ya Mbeya – Chunya yenye urefu wa kilomita 72 na kuweka Jiwe la msingi la ujenzi wa Barabara ya Chunya – Makongorosi.

Dk Magufuli amewataka viongozi hao kuiga mfano wa marehemu Abbas Kandoro kwa namna alivyosaidia kwenye hukumu ya mwanaume aliyehukumiwa kifungo cha maisha kutokana na kupatikana na  hatia ya kulawiti mtoto ambaye hadi sasa yupo katika hali mbaya.

“Tatizo la ubakaji linaonekana linataka kuwa ugonjwa katika maeneo haya, jana kuna mama alijitokeza katika mkutano wetu akaeleza shida yake kwamba ana mtoto wake ambaye alilawitiwa akiwa na miaka sita kukawa na ujanja ujanja na baadaye alienda kumuona aliyekuwa Mkuu wa Mkoa, Abbas Kandoro akaishughulikia kesi hiyo vizuri na hakimu akatumia sheria zote na mtuhumiwa akahukumiwa kifungo cha maisha.

“Nitoe wito kwa viongozi kuiga mfano wa Mzee kandoro maana alisimamia haki popote palipokuwa hakuna haki, hivyo yeyote atakayefanya vitendo vya ajabu apelekwe kwenye vyombo vya dola na nina imani tukilisimamia hili kwa pamoja tutazaa matunda mazuri,” amesema.

Aidha ametoa agizo kwa viongozi mkoani huo kuhakikisha wanafungua soko la madini katika Wilaya ya Chunya ndani ya siku saba na kwamba hilo ndilo litakuwa jaribio lao kubwa licha ya kuwa na utendaji mzuri mkoani humo.


Share:

Waziri Mkuu Awaaga Watalii 1,000 Kutoka Israel

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watalii kutoka Israel wakawe mabalozi wazuri wa kuitangaza Tanzania pindi wakirudi  huko kwao.

Ametoa wito huo leo mchana (Jumamosi, Aprili 27, 2019) kwenye uwanja wa ndege wa Kilimanjaro (KIA) wakati akiwaaga watalii 274 walioondoka nchini leo mchana kurejea kwao.

Watalii hao ni miongoni mwa watalii 1,000 waliowasili nchini tangu Aprili 20, mwaka huu na kutembelea maeneo kadhaa ya vivutio kwenye ukanda wa Kaskazini.

Kundi la kwanza liliondoka jana usiku, la pili leo mchana, la tatu litaondoka leo saa 10 jioni na la mwisho litaondoka leo saa 2 usiku.

Waziri Mkuu amewaomba watalii hao wapange muda wao na watafute fursa nyingine ya kuja Tanzania kutembelea mbuga nyingine za ukanda wa Kusini pamoja fukwe nzuri za Zanzibar.

"Tumefarijika sana na ujio wenu na tunaamini mtaenda kutangaza mazuri mliyoyaona kwa wengine. Tunazo mbuga nyingine za Rubondo, Katavi, Ngorongoro, Ruaha, Selous, fukwe nzuri za Zanzibar na mlima Kilimanjaro," amesema.

Pia amewashukuru mawakala wa utalii nchini pamoja na Mkurugenzi wa kampuni wakala wa utalii ya Another World kutoka Israel Bw. Carmel Shlomo kwa kuamua kuitangaza Tanzania kama kivutio namba moja cha utalii barani Afrika.

Kwa upande wake, Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla aliwashukuru watalii hao kwa kuamua kuitembelea Tanzania licha ya kuwa wangeweza kwenda maeneo mengine yaliyo jirani na Israel.

"Natambua uchovu mlionao sababu ya urefu wa safari kutoka Israel hadi hapa, lakini nawashukuru kwa uamuzi wenu wa kuja Tanzania katika kipindi hiki ambacho tunafanya maboresho kwenye sekta ya utalii ili tuweze kutoa huduma bora zaidi," alisema.

Alisema Tanzania ina vivutio vingi vya utalii na hii inawezekana kwa sababu iliamua kutenga zaidi ya robo ya ardhi yake kwa ajili ya mbuga na hifadhi za taifa za wanyama.

Pia alizishukuru kampuni za utalii za Tanzania na Israeli kwa kushirikiana kuleta watalii wengi kiasi hicho. Alizitaja kampuni hizo kuwa ni Excellent Guides, Mauly Tours and Safaris, Matembezi, Leopard Tours and Safaris, African Queen Adventures na TAWISA zote za kutoka Tanzania. Kamuni za kutoka Israeli ni Another World, My Trip, Camel na Safari Company.

Kwa upande wao, baadhi ya watalii kutoka Israel wamesema wamevutiwa na waliyaona hapa nchini na wameahidi kurudi tena ili watembelee vivutio vingine zaidi.

Bibi Naomi Peer Moscovich na mabinti zake Dana na Lihi wamesema wamevutiwa na wingi wa wanyama waliowaona lakini pia wameguswa na ukarimu wa watu waliokutana nao.

"Tunaondoka na neno moja kubwa nalo ni kwamba hatutaisahau Tanzania (we say Unforgettable Tanzania) na tutarudi tena hivi karibuni," alisema Dana Peer Moscovich ambaye ni dada yake Lihi.

Hafla ya kuwaaga watalii hao ilihudhuriwa pia na Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii nchini, Jaji Thomas Mihayo, Katibu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Adolf Mkenda na Wakuu wa Mikoa ya Kilimanjaro na Arusha. Mama Anna Mghwira na Bw. Mrisho Gambo.

(mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


Share:

JINSI WANAUME NAO WANAVYOPATA HEDHI


Imezoeleka kuwa wanawake pekee ndiyo wameumbiwa kuingia period kila mwezi mara pale wanapovunja ungo, kudhihirisha kuwa sasa wako tayari kuweza kubeba ujauzito na kuzaa.

Lakini ni kitu cha ajabu kusikia kuwa hali hiyo hutokea kwa mwanaume. Nikujuze tu kuanzia sasa unatakiwa ufahamu kuwa hata wanaume wanaingia hedhi, lakini sio kama ile ya wanawake ambapo wao hutoka damu sehemu zake za siri (baada ya yai kutorutubishwa na kutoka).

Jinsi wanaume wanavyopata hedhi

Kwa wanaume kitendo hiki huwa tofauti kabisa. Kwa mujibu wa mtaalamu wa psychotherapist na mwandishi wa kitabu cha Male Syndrome (IMS), Jed Diamond, PhD. Diamond, amedhirisha hili na kusema kwamba wanaume nao huingia period lakini ni tofauti na ile ya wanawake.

Kwa wanaume wao hukutana na mabadiliko ya homoni za testosterone ambazo husababisha mabadiliko ya kiafya, ikiwemo kuwa na msongo wa mawazo, uchovu na kubadilika kwa hali kila mara.

Hali hii pia huwatokea wanawake pale wanapoingia hedhi na muda mwingine huwaletea maumivu makali ya tumbo kutokana na mabadiliko ya mwili katika via vyake vya uzazi, lakini kwa wanaume haina madhara makubwa na wala hawawezi kupata damu kama wanawake, zaidi ya kuhisi mabadiliko kutokana na kutotulia kwa homoni.

Source: Health Line
Share:

Serikali Yaajiri Walimu Wapya 4,549

Serikali kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI) imepata kibali Cha kuajiri jumla ya walimu 4549 Kati ya 91108 walio tuma maombi yao.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo 27 Mei 2019 Magogoni, Dar es Salaam, Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Seleman Jafo amesema kuwa Rais Dk.John Pombe Magufuli katika kuhakikisha Serikali inawahudumia vizuri wananchi ameamua kufungua dirisha la ajira kwa walimu.

Jafo alisema jumla ya waombaji 91108 waliojitokeza na kutuma maombi yao katika nafasi mbalimbali na kati ya hayo 43770 sawa na asilimia 48.04 yalikuwa na viambatanisho vyote vilivyohitajika.

Hata hivyo alieleza kuwa maombi 47338 sawa na asilimia 51.96 hayakuwa na vigezo ikiwa ni pamoja na kukosa viambatanisho muhimu vilivyohitajika.

" Kutokana na mahitaji makubwa kwa walimu katika shule za msingi na sekondari kwa masomo ya sayansi, Tamisemi imefanya uchambuzi na kutoa vipaumbele katika ajira za walimu daraja la tatu (A) cheti kwa ajili ya kufundisha shule za msingi.

"Walimu daraja tatu (B) stashahada wa masomo ya sayansi kwa ajili ya kufundisha shule za sekondari( kidato cha kwanza hadi nne); na walimu daraja la tatu (C)shahada, wa masomo ya sayansi kwa ajili ya kufundisha kwa kidato cha tano na sita," alisema Jafo.

Pia walimu daraja la tatu (C) shahada, wa masomo ya elimu maalum , biashara, uchumi, kilimo na maarifa ya nyumbani kwa ajili ya kufundisha shule ya sekondari.

" Mchakato wa kupitia maombi ulijumuisha uhakiki wa uhalali wa vyeti vya elimu ya taaluma vya waombaji na ukamilishaji wa nyaraka zilizohitajika," alisema Jafo.

Aidha Jafo alieleza kuwa waombaji wa masomo ya sayansi na sanaa waliotimiza vigezo na hawakufanikiwa kupata nafasi kwa kipindi hiki, maombi yao yamechambuliwa na yamehifadhiwa kwenye kanzidata ya Tamisemi.

Alisema kwa walimu hao pindi fursa za ajira zitakapojitokeza utaratibu wa ajira utatolewa dhidi yao.

"Jumla ya walimu 4549 wamepangiwa moja kwa moja kufundisha shule zilizo na uhitaji wa walimu ambapo 3059 shule ya msingi na 1490 kwa sekondari," alisema.

Jafo alisema kuwa walimu wote waliopata ajira wanatakiwa kuripoti kwa wakurugenzi wa Halmashauri zenye shule walizopangiwa kwa ajili ya kuhakikisha vyeti vyao na kujaza mikataba ya ajira Kisha kuripoti kwenye vituo vyao kuanzia Mei 7, mwaka huu.

Jafo alisema walimu wapya ambao hawataripoti katika vituo vyao ifikapo Mei 21, 2019 nafasi zao zitajazwa moja kwa moja na walimu walio na sifa ambao hawakupangiwa bila kuwataarifu.

" Wakurigenzi wa Halmashauri wasikubali kubadilisha vituo vya kazi vya walimu bila kibali Cha katibu mkuu wa OR-TAMISEMI. Walimu Hawa tumewapangia kulingana na mahitaji ya sehemu husika.

Hata hivyo alisema kwa mwajiriwa atakayeripoti nakuchukua posho ya kujikimu Kisha akaondoka katika kituo chake cha kazi alichopangiwa atachukuliwa hatua kali za kisheria.


Share:

Ufahamu Ugonjwa Wa Ngiri Na Tiba Yake

Tatizo la Ngiri Linavyosababisha Upungufu wa Nguvu za Kiume na Maumbile Kusinyaa.
 
Ngiri au Hernia ni aina ya ugonjwa ambao unampata mtu baada ya misuli au kuta za tishu mwilini zinazoshikiria au kubeba viungo (organs) fulani mwilini kupoteza uimara wake au kuwa na uwazi (Opening) na hivyo kusababisha viungo hivyo kutoshikiriwa ipasavyo katika sehemu vinapostahili kuwepo.

Katika mwili wa binadamu, maeneo ambayo tatizo hili hutokea mara kwa mara ni maeneo ya tumboni, katika eneo la kinena, eneo la paja kwa juu na pia ngiri inaweza kutokea katika eneo ambalo mtu alifanyiwa upasuaji (operesheni).

Dalili za Ngiri
Tumbo kuunguruma, kiuno kuuma, kupata choo kama cha mbuzi, kushindwa kufanya tendo la ndoa, mishipa ya uume kulegea, kutokuwa na hamu ya kurudia tendo la ndoa, korondani moja kuvimba, mgongo kuuma.

Dalili zingine za ugojwa wa ngiri ni pamoja na;

Uvimbe unaoteremka kuingia ndani ya korodani unaojulikana kitaalamu kama Direct Scoratal inguinal Hernia.
Uvimbe unaojitokeza tumboni na kuteremka hadi ndani ya korodani, uvimbe huu hauumi na unaweza kurudishwa kwa urahisi iwapo mgonjwa atalala chali na kusukuma kwa vidole, uvimbe huu.
Na pindi ukikubali kurudi ndani ndipo unapoitwa Reduible direct scrotal inguinal hernia.
Na pia endapo utashindikana kurudi tumboni ndipo unapoitwa Irreduible direct scrotal inguinal hernia.

Tiba ya Ngiri
Tiba yake ni kufanyiwa upasuaji , ama kutumia dawa za asili ili kupona kabisa tatizo hilo. Wasiliana Nami Kwa Ushauri zaidi wa Tatizo hili. Simu: 0714006521


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger