Sunday 12 February 2017

MPYA:HAYA HAPA MAJINA YA WANAFUNZI WALIOPATA MKOPO BAADA YA KUKATA RUFAA BODI YA MIKOPO 2016/2017



Bodi ya Mikopo imetangaza majina ya wanafunzi waliofanikiwa kupata mkopo baada ya kukata rufaa,kiukweli ni wanafunzi wengi waliopata mkopo awamu hii ukilinganisha na miaka iliyopita.
Maswayetu blog tumekuwekea hapa taaarifa hiyo,

Ukitaka kuangaliziwa jina lako ,au la mwanao au ndugu yako kama limepata mkopo baada ya kukata rufaa, fanya yafuatayo;

1.TUMA JINA LAKO KAMILI,MFANO (JUMA PAUL-HESLB 2017)
2.HUDUMA HII UTALIPIA TSHS 1000 TU AMBAYO UTAITUMA KWENDA NAMBA 0652740927

3.KAMA UNATUMIA AIRTEL,TIGOPESA AU MPESA  TUMA KWENDA NAMBA 0652740927

4.UTAJIBIWA BAADA YA DK MOJA

5.TAFADHALI TUMA KWANZA PESA NDIO UJIBIWE.

Share:

Askofu Gwajima Kaachiwa Huru na Jeshi la Polisi


Askofu Josephat Gwajima wa kanisa la Ufufuo na Uzima ameachiwa na Polisi leo jioni baada ya mahojiano yaliyodumu toka Alhamisi mchana kwenye kituo cha Polisi kati Dar es salaam kufuatia sakata la dawa za kulevya.

Baada ya kuachiwa Askofu huyo aliandika yafuatayo kwenye mitandao yake ya kijamii “FREE AT LAST: Mungu awabariki wote mlioomba kwa ajili ya jambo hili, kesho nitakuwepo kwa ajili ya Ibada ya Jumapili, Kanisa la Ufufuo na Uzima Dar es Salaam. Mungu awabariki sana nawapenda nawaombea wote mlioomba kwaajili ya hili”
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI FEB TAREHE 12.2.2017

Share:

Saturday 11 February 2017

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEB TAREHE 11.2.2017

Share:

Friday 10 February 2017

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa Ya February 10

Share:

Agizo wa Rais Magufuli uwanja wa ndege Dar laanza kutekelezwa

Shughuli za ujenzi wa jengo jipya la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam (Terminal 3) jana tarehe 09 Februari, 2017 zimeendelea kama ilivyoagizwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aliyefanya ziara ya kushtukiza jana tarehe 08 Februari, 2017.

Wafanyakazi 850 wameendelea na kazi mbalimbali za ujenzi wa uwanja huo ikiwa ni pamoja na ujenzi wa njia za kuingia na kushuka kwenye ndege, mifumo ya ujazaji wa mafuta ya ndege, maeneo ya kuegeshea ndege, sehemu ya kuingia na kutoka jengoni, mifumo ya viyoyozi na ujenzi wa nguzo.

Pia, timu ya wataalamu wanaosimamia ujenzi huo imefanyiwa mabadiliko ambapo wataalamu wengine 9 kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano wamepelekwa na kuanza kazi mara moja.

Mkandarasi ambaye ni kampuni ya BAM International ya Uholanzi, Mhandisi Mshauri ambaye ni kampuni ya ACE ya Misri na wafanyakazi walioajiriwa katika mradi huo wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa hatua alizochukua zilizowezesha shughuli za ujenzi kuendelea.

Katika ziara ya juzi, Mhe. Rais Magufuli alielezea kusikitishwa na utekelezaji wa mradi huo uliopangwa kugharimu Shilingi Bilioni 560 kiasi ambacho ni kikubwa mno ikilinganishwa na jengo linalojengwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa Mnyaa alikiri kuwepo kwa dosari na kuahidi kuchukua hatua.

Mhe. Rais Magufuli ameahidi kuwa Serikali inafanya juhudi za haraka kutoa malipo ya Mkandarasi na Mhandisi Mshauri yaliyosababisha kusitishwa kwa ujenzi.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
Share:

Thursday 9 February 2017

TANGAZO:TUNAFANYA USAJILI WA VYUO VYA NACTE KWA WANAFUNZI WALIOMALIZA FORM 4 NA 6

Habari zenu,
Je,wewe ni mhitimu wa kidato cha nne 2016 na kurudi nyuma?

Nacte imefungua application kujiunga na vyuo katika ngazi ya cheti na diploma mwaka wa masomo 2017/2018 March intake.

Maswayetu blog tutakusaidia kuomba kozi unayoipenda pamoja na kukupa ushauri kuhusu kozi ya kusoma nzuri yenye soko kwa sasa.

Ada ya maombi ni kama ifuatavyo:
  1. Kwa eneo la Afya na Sayansi Shirikishi ada ya maombi ni Tshs 30,000/=.
  2. Kwa eneo moja kati ya maeneo mengine yaliyobaki, ada ni Tshs 20,000/=.
  3. Kwa zaidi ya eneo moja la taaluma, mfano; Afya pamoja na Biashara, ada ni Tshs 30,000/=, ambapo muombaji anaruhusiwa kuchagua maeneo yote.
Mwisho wa kutuma maombi haya ni tarehe 06/03/2017.

KAMA UNAHITAJI HUDUMA YETU TAFADHALI TUPIGIE/AU TUTUMIE SMS KWENYE SIMU NAMBA 0652740927

 KUMBUKA KUWA NAMBA YAKO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE.

MPE TAARIFA NA MWENZAKO
Share:

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI YA FEBRUARI 9,2017

Share:

UFAFANUZI JUU YA UVAAJI WA SARE ZA JWTZ NA SHUKRANI KWA VYOMBO VYA HABARI


Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania linapenda kutoa ufafanuzi kuhusu uvaaji wa sare za Jeshi kwa viongozi wanajeshi wanaoteuliwa na kupewa madaraka mbalimbali nje ya Jeshi. Hivi karibuni kumekuwa na mjadala juu ya uhalali wa uvaaji wa sare hizo.
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania linapenda kuwataarifu wananchi kuwa kulingana na kanuni za Majeshi ya Ulinzi juzuu ya kwanza, viongozi hao wanaruhusiwa kisheria kuvaa sare za Jeshi wanapokuwa wakitekeleza majukumu maalum, hivyo wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa viongozi hao waliopo katika maeneo yao.
Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P 9203, Dar es Salaam, Tanzania.
Kwa Mawasiliano zaidi: 0756-716085
source: Fullshangweblog
Share:

MZAZI ATAKAYEMRUHUSU MTOTO WAKE KUSHIRIKI KAMARI KUSHTAKIWA


Mtu yeyote atakaye ruhusu mtoto chini ya miaka 18 kushiriki, kuingia au kukaa karibu na eneo la mchezo wa kubahatisha (kamari) anahesabiwa kufanya kosa.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji ameyasema hayo leo Bungeni, Mjini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge Viti Maalum Asha Abdullah Juma juu ya kuongezeka kwa maduka ya kucheza Kamari yanayojulikana kama Jack Pot katika miji mingi hapa nchini hivyo kusababisha uvunjifu wa maadili na nguvu kazi ya vijana.
“Michezo yote ya kubahatisha ikiwemo kamari (slots machines) inaendeshwa kwa mujibu wa sheria ya Bodi ya Michezo ya kubahatisha namba 4 ya mwaka 2003, sura 41 pamoja na Kanuni zake,” alifafanua Dkt. Kijaji.
Aliendelea kwa kusema kuwa, kwa mujibu wa sheria hiyo hakuna mtu au taasisi inayoruhusiwa kuendesha biashara ya michezo ya kubahatisha bila kuwa na leseni kutoka Bodi ya Michezo ya kubahatisha pamoja na vibali vingine vinavyotolewa na mamlaka nyingine za biashara.
Vile vile sheria hiyo inakataza watoto wenye umri chini ya miaka 18 kushiriki, kuingia, kukaa au kuzururazurura karibu na maeneo ya michezo ya kubahatisha.
Aidha mtu yoyote ambaye atamruhusu mtoto chini ya miaka 18, kushiriki, kuingia au kukaa karibu na eneo la mchezo wa kubahatisha anahesabika kufanya kosa na anastahili kulipa faini ya shilingi 500,000 au kifungo kisichopungua miezi mitatu au vyote kwa pamoja.
Dkt. Kijaji amesema kuwa ikiwa kosa hilo litafanywa na mwendesha mchezo wa kubahatisha, Bodi inamamlaka ya kumfutia leseni.
Hivyo basi, wajibu wa Serikali ni kuzuia watoto na vijana walio chini ya miaka 18 kucheza michezo ya kubahatisha.
Pia, Dkt. Kijaji ametoa rai kwa wazazi na walezi kuwazuia vijana wao kucheza michezo ya kubahatisha pale wanapoona kuwa uchezaji wao unakuwa na matokeo hasi.
Hata hivyo amesema kuwa, michezo hiyo inaendeshwa kwa mujibu na sheria kama shughuli nyingine. Jambo la msingi ni kuhakikisha kuwa, wanaoendesha michezo hiyo wanazingatia sheria na kanuni zilizowekwa pamoja na wazazi, walezi na jamii kuhakikisha vijana wanazingatiia mila na desturi zinazolinda maadili ya Kitanzania wanapokuwa wanajishughulisha na shughuli halali za kiuchumi.
Share:

Vita dhidi ya dawa za kulevya DSM Watu maarufu wakiwemo wanasiasa waguswa


Sakata la dawa za kulevya katika jiji la dsm limeendelea kutikisa watu maarufu,wakiwemo wafanyabiashara na wanasiasa Pamoja na Kiongozi maarufu wa dini ambao wametakiwa kwenda kituo cha polisi cha kati siku ya ijumaa kwa ajili ya mahojiano.
Mkuu wa Mkoa wa dsm Paul Makonda akizungumza na vyombo vya habari ametangaza Orodha mpya ya watu 65 ambao wanadaiwa kujihusisha kwa namna moja au nyingine katika kuuza au kusaidia kuingiza dawa za kulevya hapa nchini au nje ya nchi.
Baadhi ya watu maarufu wanaotakiwa kuripoti kituo cha polisi cha kati Siku ya Ijumaa ni pamoja na Mbunge mstaafu wa kinondoni Iddi Azzan,Mfanyabiashara Yusuph manji,Mbunge wa hai Freeman Mbowe,mchungaji Josephat Gwajima,huku wafanyabiashara maarufu akiwemo Hussein pamba kali ,mwinyi machapta pamoja na boss Chizenga wakazi wa kinondoni.
Aidha makonda amewataka wamiliki wa hotel wakiwemo Cassino sea cliff,Parm beach casino,Sleep way ,Yatch Club pamoja na Viongozi wa makampuni ya mafuta yakiwemo GBP,Tanga Petrolium,na Nas Hauleg nao kujisalimisha Polisi siku ya ijumaa.
Share:

RAIS DKT MAGUFULI AFANYA ZIARA YA GHAFLA KUTEMBELEA UJENZI WA UWANJA WA NDEGE WA JULIUS NYERERE (TERMINAL III) DAR ES SALAAM LEO



Share:

Monday 6 February 2017

HIZI HAPA HABARI KALI SIKU YA LEO JUMATATU FEB 6 2017

HIZI HAPA HABARI KALI SIKU YA LEO JUMATATU FEB 6 2017

MAGAZETI YA LEO JUMATATU FEBRUARI TAREHE 6.2.2017,SOMA HAPO>>>>>>>>https://goo.gl/870nRt

Serikali yatangaza ‘Diploma’ ndiyo kigezo cha chini cha elimu kwa waandishi wa habari,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>https://goo.gl/dXaecr

 

VIDEO | MAdada Sita-TMK-MKUBWA NA WANAWE - Matobo | Watch/Download,DOWNLOAD HAPO>>>>>>>> https://goo.gl/tjX7pO

 

Watoto wote wanaweza kupatiwa vyeti vya kuzaliwa -Mwakyembe,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>>https://goo.gl/EBMoQV

 

Mbowe awakutanisha mameya sakata la UDA,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>>https://goo.gl/au0m8z

Vyakula Muhimu Kwa Waja Wazito,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>https://goo.gl/f1uG5D

Cameroon yatawazwa mabingwa wa Afcon 2017,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>https://goo.gl/hj3H8A

Serikali yashauriwa kupiga marufuku viroba,SOMA ZAIDI HAPO IMEKUAJE>>>>>>>>https://goo.gl/43vERh

Uporaji kwenye maduka, bodaboda wazua hofu,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>>>>https://goo.gl/G25KvW

Ukata kuchelewesha utoaji wa haki,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>>https://goo.gl/7tsesX

Kulala chali kwa mjazito ni hatari kwa mtoto,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>>>>>https://goo.gl/HtPDQ0

Chakula cha mtu mwenye Vidonda vya Tumbo,SOMA ZAIDI HAPO>>>>>>>>>https://goo.gl/jxdi2d

 TAFADHALI WATUMIE WENZAKO TAARIFA HIZI

MASWAYETU BLOG TEAM

 

 

 

 

 

 

 

Share:

Chakula cha mtu mwenye Vidonda vya Tumbo

Hapo kabla tulisoma kwa kirefu kuhusu vidonda vya tumbo kisha tukasoma kuhusu dawa mbadala ya vidonda vya tumbo na leo tunaendelea kuangalia chakula cha mgonjwa wa vidonda vya tumbo.

Katika kutibu vidonda vya tumbo, mara nyingi ni lazima kupunguza uzalishaji wa asidi tumboni au mwilini kwa ujumla.

Matibabu ya vidonda vya tumbo hujumuisha lishe na kubadilisha mitindo ya maisha na kutumia dawa maalumu.

Ikiwa matatizo kama kuvuja damu au vitobo sehemu ya kidonda yatatokea, basi hapo upasuaji huwa ni muhimu.

Vidonda vya tumbo kwa ujumla hupona ndani ya wiki 4 mpaka 6 za matibabu.
Mtu mwenye vidonda vya tumbo ni mtu mwenye asidi nyingi mwilini kuliko alkalini, hivyo anatakiwa kupendelea zaidi kula matunda na mboga za majani. Anahitaji zaidi ukijani mwilini mwake. Pia apendelee kula ugali wa dona kuliko ugali wa sembe na inashauriwa pia kupunguza kula wali.

Kitu kingine mhimu kwa mgonjwa wa vidonda vya tumbo ni maji. Hakikisha unakunywa kila siku maji glasi 8 hadi 10.

MAZOEZI MAALUMU KWA ANAYESUMBULIWA NA MIGUU KUWAKA MOTO AU ASIDI KUZIDI MWILINI
Unalala chali, nyoosha mikono chini. Kisha nyanyua mguu mmoja juu unyooke, shusha chini mguu na unyanyuwe wa pili hivyo hivyo juu kisha chini. Endelea hivyo hivyo kwa mara kumi kumi kwa round 5. Zoezi lichukuwe dk 10

Nyanyuka na ujipigie saluti mwenyewe ukianzia mkono wa kulia mara 15 hamia mkono wa kushoto mara 15 tena kwa round 5

Kisha simama, chuchumaa simama, chuchumaa simama, hivyo hivyo mara 15 kwa round 5

Pia unasimama wima, nyoosha mikono yote juu na uishushe mabegani. Hivyo hivyo mikono juu mikono mabegani mara 15 kwa round 5

Fanya hivi mara 4 mpaka 5 kwa wiki.
Hapa chini nimekuwekea jedwali la jumla la vyakula na vinywaji vyenye asidi sana, asidi ya kati na alkalini sana, vile vya kuviepuka ni vile vyenye asidi sana, orodha itaendelea kuboreshwa;

Mayai na bidhaa za maziwa

  • Alkaline: mtindi
  • Neutral: mtindi mtupu (plain Yogurt ),
  • Acid: siagi, krimu, mayai, jibini ngumu (Hard Cheese), Ice Cream, jibini ya kiwandani (Processed Cheese), maziwa

Vyakula jamii ya maharage

  • Alkaline: Lima, njegere, Snap, String
  • Neutral: Soya
  • Acid: Black, Garbanzo, Kidney, dengu

Vyakula jamii ya karanga

  • Alkaline: lozi, Nazi freshi (fresh)
  • Neutral:
  • Acid: Brazil, korosho, Nazi kavu (dried coconut), Macadamia, karanga, Pecan, Pistachio, Walnut

Mboga za majani

  • Alkaline: asparaga (Asparagus), kiazisukari (Beets), brokoli (broccoli), kabeji, karoti, Koliflawa (aina ya kabichi – Cauliflower), figili (Celery), tango, mwani (Kelp), saladi (Lettuce), uyoga, vitunguu, kotimiri (Parsley), Bell Peppers, viazi ambavyo havijamenywa (with skin), boga (Squash), nyanya
  • Neutral: Horseradish, Rhubarb, Sauerkraut
  • Acid: Spinachi iliyopikwa, viazi ambavyo vimemenywa (no skin Potato), achali

Matunda

  • Alkaline: tufaa (Apple), parachichi, tende, mtini, zabibu, balungi, Kiwi, Limau, ndimu, embe, tikiti maji, chungwa, mpichi, Pears, Stroberi
  • Neutral:
  • Acid: Blueberry, Cranberry, plamu (Plum), plamu kavu (Prune)

Vinywaji

  • Alkaline: Maji ya limau, Chai ya tangawizi
  • Neutral: Maji
  • Acid: Chai ya rangi, Bia, kahawa, vinywaji vyenye kafeina, juisi za viwandani (processed), Liquor, Soda, Wine

Viongeza utamu

  • Alkaline: Asali mbichi (Raw Honey), sukari mbichi (Raw Sugar), Stevia
  • Neutral:
  • Acid: Viongeza utamu vyote vya kutengenezwa (Artificial Sweeteners)

Nyama

  • Alkaline:
  • Neutral:
  • Acid: Nyama ya ng’ombe, kuku, Samaki, mbuzi, batamzinga, nyama ya nguruwe, Sungura

Mafuta

  • Alkaline: mafuta ya mbegu za katani
  • Neutral: mafuta ya lozi, Canola, mafuta ya nazi, mafuta ya mahindi, Margarine, mafuta ya zeituni, Safflower, mafuta ya ufuta, mafuta ya Soya, mafuta ya alizeti
  • Acid:

Vitafunwa & nafaka

  • Alkaline: Amaranth, Millet, Quinoa
  • Neutral:
  • Acid: Barley, Buckwheat, Oats, mchele, Rye, Spelt, ngano, Pasta (vyakula jamii ya tambi), biskuti

Mbegu

  • Alkaline: Alfalfa (sprouted), chia (sprouted), Sesame (sprouted)
  • Neutral:
  • Acid: boga, alizeti, ngano
Share:

Kulala chali kwa mjazito ni hatari kwa mtoto


Wanawake wajawazito wanaopenda kulala chali  wapo kwenye hatari  ya kuzaa mtoto mfu(stillbirth),kulingana na wanasayansi.

Katika utafiti  uliofanyika nchini Ghana, wanawake wajawazito ambao walipenda kulala chali wakati wa ujauzito  walikuwa  kwenye hatari mara tano zaidi ya kuzaa watoto wenye uzito mdogo na  kwa wanawake wengine walizaa watoto wafu.

Utafiti huu ulifanyika nchini Ghana kutokana na kuwa kati ya watoto 1000 wanaozaliwa 20 hadi 50 kati yao huwa ni watoto wafu.Hata hivyo, utafiti mpya uliofanyika nchini New Zealand pia umehusisha kulala chali kwa mwanamke mjamzito na idadi kubwa ya  watoto wafu wanaozaliwa  katika nchi zenye raia wenye kipato kikubwa.

Mkuu wa utafiti huu,Louise O'Brien  kutoka chuo kikuu cha Michigan, nchini Marekani amesema kama kutokulala chali wakati wa ujauzito hupunguza uwezekano wa kuzaa mtoto mfu basi ni vizuri kuhamasisha kina mama wajawazito kutolala chali kwani hii ni njia rahisi na isiyokuwa na gharama yoyote ile.

Tabia hii ya kulala chali wakati wa ujauzito inaweza kuepukika kwa kuwashauri  kina mama wajawazito madhara yanayopatikana kwa kulala chali.

Matokeo ya utafiti huu yanaonyesha ya kwamba zaidi ya robo ya idadi ya watoto wanaozaliwa wafu inaweza kuepukika kwa kubadilisha staili ya kulala tu kwa wanawake wajawazito.

Siku zote madaktari wanashauri kina mama wajawazito kulala ubavu mmoja hasa upande wa kushoto ili kuepuka kuzaa mtoto mfu au mtoto mwenye uzito mdogo kwa sababu mwanamke mjazito anapolalia ubavu wake wa kushoto huongeza mzunguko wa damu kwa kiumbe kilichomo ndani yake.

Utafiti huu uliofanyika nchini Ghana unaunga mkono utafiti uliofanyika hivi karibuni nchini Australia unaojulikana kama Sydney Stillbirth Study ambao ulisema ya kwamba wanawake wanaolala chali wakati wa ujauzito wako kwenye hatari ya mara sita zaidi ya kuzaa watoto wafu.Utafiti huu wa Australia ulifanyika kwa miaka mitano na ulihusisha wanawake wajawazito 295 kutoka katika hospitali nane nchini Australia.

Naye mtafiti mkuu katika utafiti huu Dr. Adrienne Gordon, kutoka Sydney's Royal Prince Alfred Hospital amesema “Tafiti za awali zilionyesha ya kwamba wanawake wanaolala chali wakati wa ujauzito, hupunguza mzunguko wa damu unaotakiwa kwenda kwa mtoto.Lakini  pia ni vizuri kwa wanawake ambao ni wajawazito  kutotaharuki kama wakati mwingine watalala chali.’’Kutokana na idadi ndogo ya wanawake wajawazito waliohusishwa kwenye utafiti huu sisi wana Tanzmed tunachelea kusema ya kwamba ni vigumu kusema utafiti huu umetoa mapendekezo sahihi ya  namna ya kulala kwa wanawake wajawazito.

Pia kutokana na kutoangalia muda ambao wanawake hao walilala wakiwa chali (mfano kama walilala masaa 4,6 au 8 kwa siku na kwa siku ngapi) na tofauti ya hatari kati ya wanawake wajawazito waliolala muda mfupi na mrefu, hivyo tunawaambia wanawake wajawazito kutohofu kama watalala chali lakini ni bora kuchukua tahadhari mapema.Tafiti hii inatoa changamoto kwa watafiti wetu wa afya kuangalia jinsi ya kufanya tafiti kama hizi katika mazingira ya kwetu.
Share:

Ukata kuchelewesha utoaji wa haki

Bukoba.  Ukata katika Mahakama Kuu Kanda ya Bukoba umesababisha majaji kutoendeleza vikao vya kusikiliza mashauri 24 ya kesi za mauaji, hali itakayosababisha haki kutokutolewa kwa wakati.

Jaji Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Salvatory Bongole akizungumza wakati wa kilele cha siku ya sheria nchini, alisema hadi Desemba mwaka jana hakuna kesi iliyokuwa imezidi miezi sita katika mahakama zote za mwanzo.

Alisema wamejitahidi kumaliza mashauri mengi kwa wakati pamoja na kupunguza malalamiko,  huku kesi 81 zikizidi mwaka mmoja katika mahakama za wilaya kwa kuwa korti hizo hazikuwa na uwezo nazo.

Oktoba 27 mwaka jana katika kesi ya jinai namba 67/2015, Mahakama Kuu chini ya Jaji Firmini Matogolo ilitoa uamuzi baada ya  miaka minane kwa  kuwatia hatiani wanandoa Lameck Bazil na Pancras Minago kwa mauaji ya mlemavu wa ngozi, Magdalena  Andrea yaliyotokea mwaka 2008 wilayani Biharamulo mkoani Kagera.
Share:

Uporaji kwenye maduka, bodaboda wazua hofu

Mbeya. Wamiliki wa maduka, bodaboda na glosari jijini hapa wameingiwa hofu baada ya kuibuka kundi la watu wanaodaiwa kuwa majambazi wanaopora fedha na pikipiki tangu mwishoni mwa Januari.

Mitaa iliyoonja adha ya wavamizi hao ni ya Mafiati, Mwanjelwa, Mabatini, Soweto na Mabanzini ambako vikundi hicho vilivunja maduka matano.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari alisema  wanawashikilia watu watatu wakituhumiwa kuhusika na matukio hayo.

Kidavashari alisema upelelezi wa awali unaonyesha kundi hilo la watu hutoka Tunduma mkoani Songwe na hupokewa na wenyeji ambao huwaongoza katika uporaji.

 Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Bodaboda Kanda ya Soweto, Joseph Patrick alisema hivi karibuni kuna watu waliofika eneo hilo saa 3:00 usiku waliowavamia madereva na kuwapora fedha na baadaye walivamia Mtaa wa Block Q walikopora pikipiki mbili.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger