Monday 29 August 2016

MAGAZETI YA LEO JUMATATU AGOSTI TAREHE 29.8.2016





Share:

Sunday 28 August 2016

CHADEMA: TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

 
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Kuhusu picha zinazoashiria shari.
Yanayowakuta Chama cha Chadema Tanganyika Ndio hayo hayo yanayo endelea kuwakuta Chama cha CUF na Wafuasi wao tokea miaka 20 ya Vyama Vingi ianzishwe Zanzibar. CCm wamekuwa wakitumia uniform za CUF kwakufanya shari na mauwaji, uharibifu wa Mali n.k.. Ili wapate Justification yakuwazuia Wazanzibari kudai haki zao.
Ndugu Watanzania kutoka Zanzibar na Tanganyika, lazima tuwe makini sana na kuwajuwa Maadui zetu nini lengo lao la ku.post Picha zinazoashiria SHARI, VITA kwakutumia Bendera na Uniform za Chama cha Democratic na Maendeleo (CHADEMA). Hii ni njia moja yakuonyesha kwamba Watawala hawa Haramu ( Vidiktetor Uchwara) wanajaribu Kutumia UV-CCM na Jeshi la Wananchi kufanya mazoezi ya SHAri ambayo yanaonyesha Watu/ mtu amevaa uniform akiwa na silaha za jadi. Lengo la picha hizi Ni kwamba Serikali haina Ushahidi wowote ule ambao wanawasingizia Vyama vya Upinzani kwamba ni Wachochezi. Sasa wanachokifanya nikujaribu Kujenga Twaasira yakuonyesha kwamba wanaofanya Mazoezi ya kivita ni Wanachama wa Chadema na wanataka kuhatarisha Amani ya Inchi ili Wa-JUSTIFY Kamata kama ya Wananchi wa vyama vya Upinzani vya Siasa na Viongozi wao. Kwataarifa zaidi hebu someni habari hii iliopo hapo chini:
Jioni hii zimeonekana picha za mtu ambaye anadhaniwa kuwa ni mwanamke ameshika silaha za jadi mikononi mwake, panga, upinde na mishale huku akiwa amevalia nguo zenye rangi na nembo za CHADEMA.
Mtu huyo ameonekana pia akifanya mazoezi huku nyuma yake kukiwa na bendera ya CHADEMA ambayo imeshikwa na watu ‘wanaoficha’ sura zao nyuma ya bendera hiyo.
Kwa mtazamo wa haraka picha hizo zinamuonesha mtu huyo akijiandaa kwa ‘shari’ ambayo bila shaka anaijua mwenyewe au na wenzake walioshirikiana naye kupiga hizo picha.
Tungependa kutaarifu umma kuwa picha hizo zisihusishwe kwa namna yoyote ile na Operesheni UKUTA na maandalizi ya Septemba 1 kwa ajili ya mikutano ya hadhara na maandamano ya amani kwa mujibu wa Sheria za Nchi, ambayo inatarajiwa kufanyika katika kutimiza wajibu na haki za kikatiba za Watanzania.
Tumeona ni vyema kuweka sawa jambo hili baada ya watu mbalimbali wapenda haki ambao wangependa kuona Operesheni UKUTA na Septemba 1, zikifanyika na kuendelea kwa amani ili kufikisha ujumbe mzito na muhimu unaokusudiwa kwa maslahi na matakwa ya Watanzania, kuanza kuhoji kuhusu picha hizo.
Lakini pia tumeamua kutozipuuzia picha hizo baada ya kuona dalili za maadui wa demokrasia na watetezi wa uvunjifu wa Katiba na Sheria za Nchi unaoendelea kufanywa na watawala kupitia kauli, matamko na vitendo, wakilenga kuzitumia picha hizo kuwatisha watu na bila shaka kujazia jazia vinyama kwenye vihoja vyao na propaganda nyepesi za kupindisha maudhui na madhumuni ya Septemba 1 na UKUTA kwa ujumla.
Chama kinalaani vikali matumizi ya nembo za chama yaliyofanywa na watu hao kwa namna inayoashiria shari na vurugu huku ikihusishwa na Operesheni UKUTA na Septemba 1. Waliozipiga na kuzisambaza mitandaoni wanajua makusudi yaliyowatuma kufanya hivyo na bila shaka watapaswa kuwajibika kwa walichofanya.
Tunapenda kusisitiza tena, kama ambavyo Chama kupitia kwa viongozi wakuu kimesema mara kadhaa sasa, Operesheni UKUTA na maandalizi ya Septemba 1, vitatekelezwa kwa misingi inayothamini na kuzingatia uwajibikaji kwa maslahi mapana ya Watanzania wote, ikiwa ni pamoja na kudai HAKI na KUPINGA UVUNJAJI WA KATIBA na SHERIA za Nchi kwa njia za AMANI.
Tumaini Makene
Mkuu wa Habari na Mawasiliano CHADEMA
Share:

JESHI LA KUJENGA TAIFA(JKT):TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KUKANUSHA VIJANA WA KUJITOLEA KURIPOTI KAMBINI



  TAARIFA KWA UMMA

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) linapenda kukanusha taarifa potofu zinazosambazwa kwa njia ya ujumbe mfupi kwenye baadhi ya simu za mkononi na mitandao ya kijamii inayoeleza kuwa” JKT linawataka vijana waliochaguliwa kujiunga na mafunzo ya JKT kwa Kujitolea mwaka 2016, waripoti ofisi za wakuu wa mikoa kati ya terehe 03 – 07 Septemba 2016, tayari kwa kupelekwa kwenye Makambi ya mafunzo ya JKT”.

Taarifa hiyo siyo sahihi na wananchi wanatakiwa kuzipuuza. Utaratibu utakapokamilika wa kuwachukua Vijana hao, JKT itawatangazia kupitia vyombo rasmi vya habari na siyo kwa njia ya simu za mkononi.

Aidha JKT kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Nchini inafuatilia kujua ni mtu gani au kikundi gani kimehusika na upotoshaji huo wa taarifa ili hatua kali za kisheria kuchukuliwa.

Imetolewa na:
Kurugenzi ya Habari na Uhusiano
Makao Makuu ya JKT
27 Agosti 2016

Share:

Mwalimu Mbaroni kwa Kuwapa mimba Wanafunzi Watano

 
Mwalimu wa Shule ya Sekondari ya Nyakabungo wilayani Nyamagana mkoani Mwanza, anatuhumiwa kuwapa ujauzito wanafunzi watano wa shule hiyo.
Wanafunzi hao wamebainika kuwa na ujauzito, baada ya uongozi wa shule hiyo kuona mabadiliko kwenye miili yao na kuamua kuwapima afya.
Mkuu wa shule, Boniphace Mjuli amesema baada ya kujiridhisha kuwa wana ujauzito, waliwaandikia barua wazazi wao kuwaita shuleni kwa ajili ya kuwaeleza matokeo ya vipimo na kuchukua hatua stahiki.
Wakizungumzia tukio hilo, baadhi ya wazazi wa watoto waliokutwa na ujauzito wameiomba Serikali ichukue hatua kwa wanaume wote wanaokatisha ndoto za wanafunzi wa kike.
Mzazi Yusuph Yusuph amesema ili kuwajengea mazingira mazuri wanafunzi wa kike, lazima Serikali itekeleze sheria ya kuwakamata wanaume wenye tabia za kutongoza wanafunzi na wahukumiwe kifungo cha maisha jela ili iwe fundisho.
Share:

Wakurugenzi Watano Tpdc Wasimamishwa Kazi Kupisha Uchunguzi

Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI AGOSTI TAREHE 28.8.2016






Share:

Saturday 27 August 2016

Angalia Picha 30: ASKARI WA JESHI LA POLISI SHINYANGA WAKIFANYA MAZOEZI KUJIANDAA KUKABILIANA NA UHALIFU



Leo Jumamosi,Agosti 27,2016 Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limeendelea kufanya ya mazoezi ya utayari wa kukabiliana na vitendo vya kihalifu.
Akiongoza mazoezi hayo,Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro amesema mazoezi hayo aliyoyataja kwa jina la Kiingereza ““Route Match” ni ya kawaida kwa ajili ya kujiweka tayari kukabiliana na uhalifu unaoweza kujitokeza. 
Kamanda Muliro amesema wamekuwa wakifanya mazoezi mara kwa mara lakini kilichofanyikani kubadilisha muda wa kufanya mazoezi na wataendelea kufanya kila siku za Jumamosi. 
“Huu ni mfumo huu ni wa kawaida kwa mujibu wa sheria na kanuni zinazolisimamia jeshi la polisi..tumefanya matembezi yanayohusiana na ukakamavu,yanayojenga ujasiri kwa askari kumsaidia katika utekelezaji wa majukumu yake,kwa hiyo kwa wananchi wanaoishi karibu na kambi ya jeshi siyo wageni wa mambo haya ambayo huwa tunayafanya siku za Jumamosi ”,alieleza Muliro. 
“Kilichofanyika leo tumepita mtaani asubuhi/mchana badala ya usiku/alfajiri (saa 11 hadi saa 1.30) kama vile tumekuwa tukifanya lakini lengo ni moja tu,watambue kuwa jeshi lao la polisi liko imara katika kuwalinda raia na mali zao,kusimamia sheria za nchi na askari mzuri ni yule mkakamavu,mwepesi ana uwezo wa kufikiri haraka kujua kile anachokitekeleza kimesimamia sheria gani”,aliongeza Muliro. 
Alisema mazoezi hayo ni ya kawaida na kusisitiza kuwa kwa wananchi ambao siyo wahalifu na walio wema wamefurahia mazoezi hayo. 
Askari polisi wakiongozwa na kamanda Muliro walipita katika maeneo mbalimbali mjini Shinyanga na maeneo huku wakiwa na vifaa mbalimbali vya jeshi hilo ikiwemo magari,silaha na magari ya maji ya kuwasha. 
Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde alikuwepo maeneo mbalimbali walikopita askari polisi mjini Shinyanga,ametuletea picha 31…Shuhudia hapa chini 
Hapa ni katika kambi ya jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga-Kulia ni Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akitoa maelekezo kwa askari wa jeshi hilo kabla ya kuanza mazoezi mtaani leo majira ya saa tatu asubuhi
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akieleza kuhusu mazoezi ya "Route Match"
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akisisitiza jambo kabla ya kuanza kufanya mazoezi
Askari polisi wakiwa kambini kabla ya kuanza kufanya mazoezi mtaani
Askari polisi wakijiandaa kuanza kufanya mazoezi
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akifanya mazoezi na askari polisi wa jeshi hilo mjini Shinyanga
Askari polisi wakiendelea na mazoezi mtaani
Askari polisi wakiwa katika gari la maji ya kuwasha
Mazoezi yanaendelea katika eneo la Phatom mjini Shinyanga
Gari la maji ya kuwasha likiwa barabarani
Magari ya polisi yakiwa barabarani
Mazoezi yanaendelea
Askari polisi wakiwa ndani ya gari 
Wananchi wakiendelea na shughuli zao huku askari polisi wakiendelea na mazoezi yao
Wananchi wakiendelea na safari zao
Askari polisi wakiendelea na mazoezi yao
Askari wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga wakiwa kambini baada ya kumaliza kufanya mazoezi 
Askari polisi wakiwa kambini baada ya kumaliza kufanya mazoezi mtaani
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akizungumza kambini ambapo aliwaambia askari polisi kuwa watakuwa wanafanya mazoezi ya namna hiyo kila siku za Jumamosi
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akisisitiza jambo
Maafisa wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga wakiwa kambini baada ya kumaliza kufanya mazoezi
Askari polisi wakiwa kambini
Askari polisi wakimsikiliza kamanda Muliro
Kamanda Muliro akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza kufanya mazoezi
Waandishi wa habari wakiwa kambini
Askari polisi wakijiandaa kutawanyika baada ya kumaliza kufanya mazoezi.
Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger