Sunday 28 August 2016
Saturday 27 August 2016
Angalia Picha 30: ASKARI WA JESHI LA POLISI SHINYANGA WAKIFANYA MAZOEZI KUJIANDAA KUKABILIANA NA UHALIFU
Leo Jumamosi,Agosti 27,2016 Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga
limeendelea kufanya ya mazoezi ya utayari wa kukabiliana na vitendo vya
kihalifu.
Akiongoza mazoezi hayo,Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro
Jumanne Muliro amesema mazoezi hayo aliyoyataja kwa jina la Kiingereza
““Route Match” ni ya kawaida kwa ajili ya kujiweka tayari kukabiliana na
uhalifu unaoweza kujitokeza.
Kamanda Muliro amesema wamekuwa wakifanya mazoezi mara kwa mara lakini
kilichofanyikani kubadilisha muda wa kufanya mazoezi na wataendelea
kufanya kila siku za Jumamosi.
“Huu ni mfumo huu ni wa kawaida kwa mujibu wa sheria na kanuni
zinazolisimamia jeshi la polisi..tumefanya matembezi yanayohusiana na
ukakamavu,yanayojenga ujasiri kwa askari kumsaidia katika utekelezaji wa
majukumu yake,kwa hiyo kwa wananchi wanaoishi karibu na kambi ya jeshi
siyo wageni wa mambo haya ambayo huwa tunayafanya siku za Jumamosi
”,alieleza Muliro.
“Kilichofanyika leo tumepita mtaani asubuhi/mchana badala ya
usiku/alfajiri (saa 11 hadi saa 1.30) kama vile tumekuwa tukifanya
lakini lengo ni moja tu,watambue kuwa jeshi lao la polisi liko imara
katika kuwalinda raia na mali zao,kusimamia sheria za nchi na askari
mzuri ni yule mkakamavu,mwepesi ana uwezo wa kufikiri haraka kujua kile
anachokitekeleza kimesimamia sheria gani”,aliongeza Muliro.
Alisema mazoezi hayo ni ya kawaida na kusisitiza kuwa kwa wananchi ambao siyo wahalifu na walio wema wamefurahia mazoezi hayo.
Askari polisi wakiongozwa na kamanda Muliro walipita katika maeneo
mbalimbali mjini Shinyanga na maeneo huku wakiwa na vifaa mbalimbali vya
jeshi hilo ikiwemo magari,silaha na magari ya maji ya kuwasha.
Mwandishi mkuu wa Malunde1 blog,Kadama Malunde alikuwepo maeneo
mbalimbali walikopita askari polisi mjini Shinyanga,ametuletea picha
31…Shuhudia hapa chini
Hapa ni katika kambi ya jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga-Kulia ni
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro
akitoa maelekezo kwa askari wa jeshi hilo kabla ya kuanza mazoezi mtaani
leo majira ya saa tatu asubuhi
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akieleza kuhusu mazoezi ya "Route Match"
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akisisitiza jambo kabla ya kuanza kufanya mazoezi
Askari polisi wakiwa kambini kabla ya kuanza kufanya mazoezi mtaani
Askari polisi wakijiandaa kuanza kufanya mazoezi
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro
akifanya mazoezi na askari polisi wa jeshi hilo mjini Shinyanga
Askari polisi wakiendelea na mazoezi mtaani
Askari polisi wakiwa katika gari la maji ya kuwasha
Mazoezi yanaendelea katika eneo la Phatom mjini Shinyanga
Gari la maji ya kuwasha likiwa barabarani
Magari ya polisi yakiwa barabarani
Mazoezi yanaendelea
Askari polisi wakiwa ndani ya gari
Wananchi wakiendelea na shughuli zao huku askari polisi wakiendelea na mazoezi yao
Wananchi wakiendelea na safari zao
Askari polisi wakiendelea na mazoezi yao
Askari wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga wakiwa kambini baada ya kumaliza kufanya mazoezi
Askari polisi wakiwa kambini baada ya kumaliza kufanya mazoezi mtaani
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro
akizungumza kambini ambapo aliwaambia askari polisi kuwa watakuwa
wanafanya mazoezi ya namna hiyo kila siku za Jumamosi
Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga ACP Muliro Jumanne Muliro akisisitiza jambo
Maafisa wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga wakiwa kambini baada ya kumaliza kufanya mazoezi
Askari polisi wakiwa kambini
Askari polisi wakimsikiliza kamanda Muliro
Kamanda Muliro akizungumza na waandishi wa habari baada ya kumaliza kufanya mazoezi
Waandishi wa habari wakiwa kambini
Askari polisi wakijiandaa kutawanyika baada ya kumaliza kufanya mazoezi.
Picha zote na Kadama Malunde-Malunde1 blog
Picha: JESHI LA POLISI LAONGEZA ASKARI WENGINE 80 KUSAKA MAJAMBAZI VIKINDU MKOANI PWANI
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limeongeza nguvu kwa
kutuma askari wengine 80 katika oparesheni ya kusaka majambazi
inayoendelea katika maeneo ya Vikindu, wilayani Mkuranga mkoani Pwani.
Akizungumza na vyombo vya habari leo katika kituo kikuu cha Polisi Dar
es Salaam, Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo Kamishna Simon Sirro,
amesema Jeshi hilo limeanza rasmi oparesheni hiyo usiku wa kuamkia jana,
ikiwa na lengo la kusaka watu wanaoshukiwa kuwa ni majambazi wanaodaiwa
kufanya matukio kadhaa ya ujambazi likiwemo lile la kuuawa kwa askari
wanne waliokuwa wakienda lindoni, katika benk ya CRDB, Mbade jiji Dar es
Salaam.
Amesema kuwa katika oparesheni hiyo kuna watu waliouawa na wengine
wanashikiliwa na jeshi hilo, lakini amekataa kutaja idadi yoyote ile ya
waliouawa au waliokamatwa kwa sababu za kiusalama kwa kuwa oparesheni
hiyo bado inaendelea.
“Itakuwa ni kinyume cha utaratibu nikieleza kinachoendelea kwenye
operesheni, niwahakikishie silaha zilizochukuliwa
zinarudi,kinachoendelea nitawajulisha jumanne ili wananchi wajue kitu
gani kinaendelea,” amesema.
Ameongeza kuwa; “Mapambano ni ya kawaida sana, na ndio maana askari
polisi akifa kwa silaha ni jambo la kawaida sana. Operesheni tutaifanya
maeneo ya Vikindu, Pwani Dar es Salaam, sababu hii network (mtandao) ipo
na lazima tutaisafisha.Kama walidhani wataitawala DSM wamejidanyanya
lazima tutarudisha heshima ya jiji.”
Katika hatua nyingine, Sirro amesema amepata taarifa kuwa wapo baadhi ya
watu wanapewa fedha kwa ajili ya kufanya maandamano Septemba Mosi mwaka
huu ambapo ametoa onyo kwa watakaoshiriki kuwa watachukuliwa hatua kali
za kisheria kwa kuwa maandamano hayo hayajaruhusiwa.
“Wote tunajua madhara ya fujo, wazalendo naomba msishiriki, Wanaotaka
kujionesha wanapambana na polisi waje barabarani, ” amesema.
Usiku wa kuamkia jana, hali ya taharuki iliwakumba wakazi wa Vikindu
baada ya kikosi maalum cha askari kuvamia nyumba moja iliyoko eneo hilo,
na kisha kuzuka kwa majibizano ya risasi kati ya polisi na wanaodaiwa
kuwa ni majambazi waliokuwa katika nyumba hiyo.
Baadhi ya askari wakiwa tayari kwenye magari yao wakati wa kujiandaa kuelekea Vikindu kwenye mapambano
Vikosi hivyo vikitoka makao makuu ya kanda maalum ya Dar kuelekea kwenye mapamban
LOWASSA AKUTANA USO KWA USO NA RAIS MAGUFULI KANISA LA MTAKATIFU PETRO JIJINI DAR ES SALAAM
Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William Mkapa leo tarehe 27
Agosti, 2016 ameadhimisha Jubilei ya Dhahabu ya Miaka 50 ya Ndoa yake na
Mama Anna Mkapa katika kanisa la Mtakatifu Petro lililopo Oysterbay
Jijini Dar es Salaam.
Hafla ya Jubilei hiyo imefanyika nyakati za mchana katika ukumbi wa
Kardinali Rugambwa uliopo kando ya kanisa la Mtakatifu Petro-Oysterbay
na imetanguliwa na Misa ya shukrani iliyofanyika katika kanisa hilo
majira ya asubuhi.
Jubilei hiyo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Mkewe Mama
Janeth Magufuli, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais Mstaafu
wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais Mstaafu wa Awamu ya
Sita wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid Karume, Mke wa Baba wa Taifa Mama
Maria Nyerere, Mawaziri Wakuu Wastaafu Mhe. Cleopa Msuya, Dkt. Salim
Ahmed Salim, Jaji Joseph Warioba na Mhe. Edward Lowassa.
Misa Takatifu ya Shukrani imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu
Katoliki la Arusha Mhashamu Askofu Josephat Lebulu na kuhudhuriwa na
Maaskofu na Maaskofu Wakuu saba akiwemo Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu
Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo.
Akizungumza baada ya kumalizika kwa Misa Takatifu Rais Magufuli
amempongeza Rais Mstaafu Benjamin William Mkapa kwa kutimiza miaka 50 ya
ndoa na ameeleza kuwa ndoa hiyo iliyowaunganisha wanandoa wanaotoka
katika madhehebu tofauti ya Kikristo imetoa fundisho kubwa kuwa binadamu
wanapaswa kuwa wamoja hata kama wana tofauti mbalimbali zikiwemo za
kimadhehebu ya dini, siasa na kanda.
Rais Magufuli amesema miaka 50 ya ndoa ya Mhe. Benjamin William Mkapa
ambaye ni Muumini wa Kanisa Katoliki na Mkewe Mama Anna Mkapa ambaye ni
Muumini wa Kanisa la Kilutheri inawafundisha watanzania wote hususani
wanasiasa kuishi kwa upendo na kuilinda amani waliyonayo na ametoa wito
kwa viongozi dini kuendeleza juhudi zao za kuliombea taifa na
kuwaunganisha wananchi licha ya tofauti walizo nazo.
Kwa upande wake Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Mhe. Benjamin William
Mkapa pamoja na kuwashukuru Viongozi wote, ndugu, jamaa na marafiki
waliohudhuria Misa ya Shukrani na Jubilei hiyo ya miaka 50 ya ndoa yake
amemshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuijaalia ndoa yake umri mrefu.
Rais Mstaafu Mkapa pia ametoa wito kwa watanzania kupenda na
kushirikiana huku akibainisha mafunzo aliyoyapata kutoka kwa viongozi wa
dini kuwa "Kila mmoja ni zawadi kwa mwenzake"
Nae Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Dar es Salaam Mwadhama Polycarp
Kardinali Pengo amempongeza Rais Mstaafu Mkapa na Mkewe Mama Anna Mkapa
kwa kuadhimisha miaka 50 ya ndoa na amewasihi watanzania kuiga mfano
mwema uliooneshwa na wana ndoa hao ambao wamedumu katika imani bila
kuyumba.
Kardinali Pengo amesema ndoa ya Rais Mstaafu Mkapa anaifundisha jamii kuwa tunaweza kuishi kwa imani zetu bila kubadili dini
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es Salaam
27 Agosti, 2016