Sunday 26 June 2016

BREAKING NEWS:RAIS MAGUFULI ATEUA WAKUU WA WILAYA 139 NA NAFASI ZA WAKUU WA MIKOA ZILIZOKUWA WAZI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS IKULU

Simu : +255-22-2114512, 2116898
Faksi : 255-22-2113425
OFISI YA RAIS,
IKULU,
1 BARABARA YA BARACK OBAMA,
11400 DAR ES SALAAM,
TANZANIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya mabadiliko madogo katika safu ya wakuu wa mikoa na amewateua wakuu wa wilaya 139.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika mabadiliko hayo Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Bi. Zainab R. Telack kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.
Bi. Zainab R. Telack anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Bi. Anna Kilango Malecela ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.
Rais Magufuli pia amemteua Dkt. Binilith Satano Mahenge kuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma.
Dkt. Binilith Satano Mahenge anajaza nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Bw. Said Thabit Mwambungu ambaye amehamishiwa Ofisi ya Waziri Mkuu Dar es salaam ambako atapangiwa majukumu mengine.
Aidha, Rais Magufuli amemteua Dkt. Charles F. Mlingwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mara.
Dkt. Charles F. Mlingwa anajaza nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Stanslaus Magesa Mulongo ambaye uteuzi wake umetenguliwa.
Wakuu wapya wa mikoa walioteuliwa wataapishwa tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi Ikulu Jijini Dar es salaam na mara baada ya kuapishwa watakula kiapo cha maadili ya uongozi.
Wakati huo huo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 26 Juni, 2016 amefanya uteuzi wa Wakuu wa Wilaya 139.
Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi amesema katika uteuzi huo Rais Magufuli amezingatia mambo kadhaa ikiwa ni pamoja na umri ambapo kwa wale ambao umri wao ni zaidi ya miaka 60 ameamua wastaafu.
Mhe. Rais amewashukuru sana kwa utumishi wao mzuri na amesema pale ambapo itahitajika, serikali itaendelea kuwatumia katika majukumu mengine.
Katika uteuzi huo, Wakuu wa Wilaya waliopo sasa ambao wamebaki katika nafasi zao ni 39. Pia Rais Magufuli amewateua Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri 22 kuwa Wakuu wa Wilaya kutokana na utendaji wao mzuri.
Aidha, nafasi 78 za uteuzi wa Wakuu wa wilaya zimejazwa na watanzania wengine ambao wameteuliwa kwa mara ya kwanza wengi wao wakiwa ni vijana, wenye elimu ya kutosha na uzoefu katika maeneo mbalimbali.
Walioteuliwa kuwa wakuu wa wilaya ni kama ifuatavyo (Orodha imepangwa kulingana na mikoa)
ARUSHA
  1. Arusha           -           Mrisho Mashaka Gambo
  2. Arumeru        -           Alexander Pastory Mnyeti
  3. Ngorongoro  -           Rashid Mfaume Taka
  4. Longido         -           Daniel Geofrey Chongolo
  5. Monduli         -           Idd Hassan Kimanta
  6. Karatu                        -           Therezia Jonathan Mahongo


DAR ES SALAAM
  1. Kinondoni     -           Ally Hapi
  2. Ilala                -           Sophia Mjema
  3. Temeke         -           Felix Jackson Lyaviva
  4. Kigamboni     -           Hashim Shaibu Mgandilwa
  5. Ubungo          -           Hamphrey Polepole

DODOMA
  1. Chamwino     -           Vumilia Justine Nyamoga
  2. Dodoma        -           Christina Solomon Mndeme
  3. Chemba         -           Simon Ezekiel Odunga
  4. Kondoa          -           Sezeria Veneranda Makutta
  5. Bahi                -           Elizabeth Simon
  6. Mpwapwa      -           Jabir Mussa Shekimweli
  7. Kongwa          -           John Ernest Palingo

GEITA
  1. Bukombe      -           Josephat Maganga
  2. Mbogwe         -           Matha John Mkupasi
  3. Nyang'wale     -           Hamim Buzohera Gwiyama
  4. Geita               -           Herman C. Kipufi
  5. Chato             -           Shaaban Athuman Ntarambe

IRINGA
  1. Mufindi          -           Jamhuri David William
  2. Kilolo             -           Asia Juma Abdallah
  3. Iringa              -           Richard Kasesela

KAGERA
  1. Biharamulo   -           Saada Abraham Mallunde
  2. Karagwe         -           Geofrey Muheluka Ayoub
  3. Muleba          -           Richard Henry Ruyango
  4. Kyerwa           -           Col. Shaban Ilangu Lissu
  5. Bukoba          -           Deodatus Lucas Kinawilo
  6. Ngara             -           Lt. Col. Michael M. Mtenjele
  7. Missenyi         -           Lt. Col Denis F. Mwila

KATAVI
  1. Mlele              -           Rachiel Stephano Kasanda
  2. Mpanda         -           Lilian Charles Matinga
  3. Tanganyika    -           Saleh Mbwana Mhando

KIGOMA
  1. Kigoma           -           Samsoni Renard Anga
  2. Kasulu                        -           Col. Martin Elia Mkisi
  3. Kakonko       -           Col. Hosea Malonda Ndagala
  4. Uvinza                        -           Mwanamvua Hoza Mlindoko
  5. Buhigwe         -           Col. Elisha Marco Gagisti
  6. Kibondo        -           Luis Peter Bura

KILIMANJARO
  1. Siha                -           Onesmo Buswelu
  2. Moshi             -           Kippi Warioba
  3. Mwanga         -           Aaron Yeseya Mmbago
  4. Rombo           -           Fatma Hassan Toufiq
  5. Hai                 -           Gelasius Byakanwa
  6. Same              -           Rosemary Senyamule Sitaki

LINDI
  1. Nachingwea   -           Rukia Akhibu Muwango
  2. Ruangwa        -           Joseph Joseph Mkirikiti
  3. Liwale             -           Sarah Vicent Chiwamba
  4. Lindi               -           Shaibu Issa Ndemanga
  5. Kilwa              -           Christopher Emil Ngubiagai


MANYARA
  1. Babati             -           Raymond H. Mushi
  2. Mbulu                        -           Chelestion Simba M. Mofungu
  3. Hanang'         -           Sara Msafiri Ally
  4. Kiteto              -           Tumaini Benson Magessa
  5. Simanjiro       -           Zephania Adriano Chaula

MARA
  1. Rorya              -           Simon K. Chacha
  2. Serengeti        -           Emile Yotham Ntakamulenga
  3. Bunda                        -           Lydia Simeon Bupilipili
  4. Butiama         -           Anarose Nyamubi
  5. Tarime           -           Glodious Benard Luoga
  6. Musoma        -           Dkt. Vicent Anney Naano

MBEYA
  1. Chunya          -           Rehema Manase Madusa
  2. Kyela              -           Claudia Undalusyege Kitta
  3. Mbeya                        -           William Ntinika Paul
  4. Rungwe          -           Chalya Julius Nyangidu
  5. Mbarali          -           Reuben Ndiza Mfune

MOROGORO
  1. Gairo              -           Siriel Shaid Mchembe
  2. Kilombero     -           James Mugendi Ihunyo
  3. Mvomero       -           Mohamed Mussa Utali
  4. Morogoro      -           Regina Reginald Chonjo
  5. Ulanga                        -           Kassema Jacob Joseph
  6. Kilosa             -           Adam Idd Mgoyi
  7. Malinyi           -           Majula Mateko Kasika

MTWARA
  1. Newala           -           Aziza Ally Mangosongo
  2. Nanyumbu    -           Joakim Wangabo
  3. Mtwara           -           Dkt. Khatibu Malimi Kazungu
  4. Masasi                        -           Seleman Mzee Seleman
  5. Tandahimba -           Sebastian M. Walyuba

MWANZA
  1. Ilemela           -           Dkt. Leonald Moses Massale
  2. Kwimba          -           Mhandisi Mtemi Msafiri Simeon
  3. Sengerema     -           Emmanuel Enock Kipole
  4. Nyamagana    -           Mary Tesha Onesmo
  5. Magu              -           Hadija Rashid Nyembo
  6. Ukerewe        -           Estomihn Fransis Chang'ah
  7. Misungwi       -           Juma Sweda

NJOMBE
  1. Njombe          -           Ruth Blasio Msafiri
  2. Ludewa                      -           Andrea Axwesso Tsere
  3. Wanging'ombe          -           Ally Mohamed Kassige
  4. Makete                       -           Veronica Kessy

PWANI
  1. Bagamoyo      -           Alhaji Majid Hemed Mwanga
  2. Mkuranga      -           Filberto H. Sanga
  3. Rufiji               -           Juma Abdallah Njwayo
  4. Mafia              -           Shaibu Ahamed Nunduma
  5. Kibaha           -           Asumpter Nsunju Mshama
  6. Kisarawe        -           Happyness Seneda William
  7. Kibiti               -           Gulamu Hussein Shaban Kifu

RUKWA
  1. Sumbawanga -           Dkt. Khalfan Boniface Haule
  2. Nkasi              -           Said Mohamed Mtanda
  3. Kalambo        -           Julieth Nkembanyi Binyura

RUVUMA
  1. Namtumbo    -           Luckness Adrian Amlima
  2. Mbinga           -           Cosmas Nyano Nshenye
  3. Nyasa             -           Isabera Octava Chilumba
  4. Tunduru        -           Juma Homela
  5. Songea           -           Polet Kamando Mgema

SHINYANGA
  1. Kishapu         -           Nyambonga Daudi Taraba
  2. Kahama         -           Fadhili Nkulu
  3. Shinyanga      -           Josephine Rabby Matiro


SIMIYU
  1. Busega           -           Tano Seif Mwera
  2. Maswa                        -           Sefu Abdallah Shekalaghe
  3. Bariadi           -           Festo Sheimu Kiswaga
  4. Meatu             -           Joseph Elieza Chilongani
  5. Itilima             -           Benson Salehe Kilangi


SINGIDA
  1. Mkalama       -           Jackson Jonas Masako
  2. Manyoni        -           Mwembe Idephonce Geofrey
  3. Singida           -           Elias Choro John Tarimo
  4. Ikungi             -           Fikiri Avias Said
  5. Iramba           -           Emmanuel Jumanne Luhahula

SONGWE
  1. Songwe           -           Samwel Jeremiah
  2. Ileje                -           Joseph Modest Mkude
  3. Mbozi             -           Ally Masoud Maswanya
  4. Momba          -           Juma Said Irando


TABORA
  1. Nzega             -           Geofrey William Ngudula
  2. Kaliua             -           Busalama Abel Yeji
  3. Igunga                        -           Mwaipopo John Gabriel
  4. Sikonge          -           Peres Boniphace Magiri
  5. Tabora           -           Queen Mwashinga Mlozi
  6. Urambo         -           Angelina John Kwingwa
  7. Uyui                -           Gabriel Simon Mnyele

TANGA
  1. Tanga             -           Thobias Mwilapwa
  2. Muheza          -           Mhandisi Mwanaisha Rajab Tumbo
  3. Mkinga           -           Yona Lucas Maki
  4. Pangani          -           Zainab Abdallah Issa
  5. Handeni        -           Godwin Crydon Gondwe
  6. Korogwe        -           Robert Gabriel
  7. Kilindi                        -           Sauda Salum Mtondoo
  8. Lushoto         -           Januari Sigareti Lugangika

Wakuu wote wa Wilaya walioteuliwa wanapaswa kufika Ikulu Dar es salaam siku ya Jumatano tarehe 29 Juni, 2016 saa tatu kamili asubuhi kwa ajili ya kiapo cha maadili ya uongozi na maelekezo mengine kabla ya kuapishwa na wakuu wa mikoa watakaporejea katika mikoa yao.


Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
26 Juni, 2016

Share:

USHAURI WA BURE NINI CHA KUFANYA KWA WANAFUNZI WOTE MLIOKOSA NAFASI ZA KUJIUNGA KIDATO CHA 5 2016

Image result for ngao ya tanzania 


Habari zenu wadau wa BLOG PENDWA YA MASWAYETU
,namshukuru allah kwa kuniwezesha kuiona siku hii ya leo tena.
Mada ambayo napenda kuiongelea hapa ni kuhusu vijana wote waliokosa nafasi za kuchaguliwa kujiunga na kidato cha tano july 2016,lakini wanasifa za kujiunga na kidato cha tano,Basi kama wewe au ndugu yako ni mmoja wapo fanya yafuatayo kwa kuangalia lipi linakufaa kwa sasa;

1.SUBIRI SECOND SELECTION
Endapo bado una nia ya kwenda kidato cha tano na umefaulu vizuri,mara nyingi serikali yetu imekuwa sikivu katika kuhakikisha kuwa kila kijana aliefaulu anachaguliwa kujiunga kidato cha tano,huwa inatoa second selection kwa wanafunzi wwenye sifa za kujiunga na kidato cha tano,kwa hiyo kama wewe GPA YAKO ni kuanzia 1.6 au div 3 pts 25  na unahamu na kidato cha tano tafadhali subiri utachaguliwa.

NOTE:usibweteke na kusubiri tu hizo second selection fanya yafuatayo kwani kidato cha TANO sio maisha ,maisha ni popote pale,basi fanya yafuatayo;

2.APPLY UALIMU KUPITIA NACTE
Nacte inahusika na vyuo vya ualimu kwa ngazi ya diploma na kushuka chini,basi naomba ufanye hima uombe ualimu haraka mara tu watakaofungua application,Kama una sifa zifuatazo omba ualimu fasta wakifungua.

EDUCATION PROGRAMS 
The Ministry of Education and Vocational Training in collaboration with the National Council for Technical Education (NACTE) would like to inform the public that Central Admission System (CAS) is now open for new applicants into Teacher Training Institutions for academic year 2016/17
Minimum Entry Requirements:

  1. Ordinary Diploma (Pre Service): Division I – III OR GPA of 1.6 in O’Level
  2. Ordinary Diploma (In Service): Grade IIIA Certificate
  3. Higher Diploma: Two (2) principle passes in A’Level or Ordinary Diploma (NTA 6).
  4. Ordinary Diploma in Laboratory Technology: Passes (D) in Physics, Chemistry, Biology and Mathematics
NOTE:KUNA UWEZEKANO MKUBWA NACTE WAKAFUNGUA APPLICATION UPYA,PLEASE WAKIFUNGUA FANYIA KAZI USHAURI WANGU.

MWISHO:
Endapo utaufanyia kazi ushauri wangu nina imani kubwa malengo yako yatafanikiwa mbele kwa mbele,nakutakia mfungo mwema wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.
Wako,
Share:

AJALI: Meli ya mizigo iitwayo HAPPY yazama eneo la Chumbe, Unguja ikitoka Dar kuelekea Zanzibar

Meli ya mizigo iitwayo Happy ikitokea Dar es salaam kwenda Zanzibar imezama eneo la Chumbe, Unguja.

Taarifa zimedai kwamba Meli hiyo ilianza kuzama saa 10 alfajiri baada ya kuingiza maji ndani na kukosekana kwa vifaa kama motor ya kutolea maji hayo kufikia saa 1 asubuhi hii Meli hiyo ilizama kabisa ndani ya maji.


Meli hiyo ilikuwa imebeba Dengu gunia 450 pamoja na Mbao zaidi ya 1000 huku wafanyakazi sita waliokuwa ndani ya Meli hiyo wakiokolewa.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema kuwa ni meli ya mizigo mitupu na mabaharia mpaka sasa imeripotiwa kwamba wote ni wazima.

13502130_1070396369720352_3702524120513408319_n.jpg 13495064_500820163444320_103952615715841024_n.jpg
13529254_500820133444323_9094812653178131848_n.jpg
Share:

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNE TAREHE 26.6.2016


Share:

Saturday 25 June 2016

Share:

AJALI:Joyce Kiria na crew ya Wanawake Live yapata ajali Sumbawanga-VIDEO


Share:

Profesa Mbarawa amteua Mhandisi Kakoko kuwa Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA)

image.jpeg
Share:

MPYA:TAARIFA MUHIMU KWA WANAFUNZI WOTE WA CHUO KIKUU UDOM

Image result for UDOM
This is to inform all registered students that, they are required to fill in their particulars (form four, form six and equivalents index numbers). The CSEE and ACSEE Index numbers should be written correctly and must contain 15 characters eg. S0235/0897/2012 .Please submit your particulars by visiting your account in UDOM-SR THEN EDIT MY INFO not later than Sunday 26th June 2016
All students are required to obey a deadline provided above. Students who will fail to comply with this notice will be held responsible for anything that might happen to them.
Please you are also reminded to provide your response on Students Satisfaction Survey.
ISSUED BY THE OFFICE OF DEPUTY VICE CHANCELLOR (ACADEMICS, RESEARCH AND CONSULTANCY)
Share:

Fanya haya ili usiishie kuzalishwa, kuachwa!


Couple sitting on sofa with arms folded, looking angry
KWA neema na rehema zake Mungu, mimi na wewe tunaendelea kukutana katika safu hii. Jumamosi nyingine ambayo ninaamini nimefumbata jambo kichwani ambalo lina faida. Chukua muda wako, soma na utafakari kwa makini kisha chukua hatua.
Kama mada inavyojieleza hapo juu. Matarajio ya wengi ni kuishi katika penzi salama. Kuishi na mwanaume au mwanamke wa ndoto yake. Lakini bahati mbaya sana, tofauti na matarajio, wengi hujikuta wakianguka katika mikono ambayo si salama.
Wanaishi katika penzi kipofu. Wanajisahau wakiwa penzini na kujikuta baadaye wakijuta. Mtu anawekeza nguvu nyingi kwa mtu ambaye si sahihi. Bahati mbaya sana nguvu ya penzi humfanya mtu awe kipofu. Anaweza kuona kabisa anaangamia lakini hashtuki.
Anauona moto mbele yake lakini anafikiri ni barafu. Matokeo yake anajikuta matatizoni. Wengi sana wamelia baada ya kujikuta wamedumu penzini na matapeli wa mapenzi. Mwanamke amepewa matumaini, ahadi kemkemu kwamba ataolewa lakini kumbe mwanaume ni tapeli.
Anapewa matumaini kwamba ataolewa. Uongo unamuingia kwelikweli. Anaruhusu kubeba mimba ya kwanza, anajifungua. Anabeba mimba nyingine, anajikuta amezaa mtoto wa pili. Mwanaume anaendelea kumpa moyo na matokeo yake hata mtoto wa tatu, mwanaume anaanza visa na baadaye kuingia mitini.
Hapo ndipo mwanamke anatamani kujiua. Anawaona wanaume wote duniani ni maadui. Anajuta kupoteza muda. Analia kwa mengi. Kwanza anaumia kudanganywa na mtu ambaye yeye alimpenda. Anaumia kwa sababu tayari ujana unakuwa umemtupa mkono.
Anajuta kwamba pengine angegundua mapema madhumuni ya mwanaume huyo, angeiahirisha safari mapema. Kwa kuwa umri tayari unakuwa umemtupa mkono, ‘soko’ lake pia linakuwa limepungua. Uwezekano wa kutokea mwanaume mwingine ili aweze kumuoa unakuwa mdogo.
Anaumia kila anapowaangalia wale watoto ambao wote wanahitaji mahitaji kutoka kwake. Ataumia zaidi pale mwanaume huyo anapooa mwanamke mwingine bila kujali kwamba amempotezea muda.
Bahati mbaya sana mateso hayo huwa yanakuwa upande wake. Mwenzake anafurahia maisha mapya ya ndoa na mwanamke mwingine. Akiwa mstaarabu atampa mahitaji, asipokuwa mstaarabu hatatoa mahitaji kwa watoto.
Ameziba milango kwa mwanamke wake wa awali, yeye milango inazidi kufunguka kwa kupata mwanamke mwingine. Tatizo hilo laweza kumtokea pia mwanaume lakini wachambuzi wengi wa masuala ya uhusiano wanasema lina madhara zaidi kwa wanawake.
Mwanaume anaweza kuingia kwenye ndoa akiwa na miaka zaidi ya hamsini lakini kwa mwanamke ni nadra. Mwanamke taa nyekundu inawahi zaidi kumuwakia kulingana na maumbile.
NINI CHA KUFANYA?
Unapaswa kutathmini mwenendo wako kila wakati. Usikubali kuishi na mtu ambaye kuna mahali unamtilia shaka. Ukiwa katika hatua ya awali, jiulize mtu uliye naye ni sahihi kwako? Ana sifa za kuwa baba wa watoto wako?
Ana sifa za kuwa mume? Anahitaji kweli kuishi kwenye maisha ya ndoa na wewe? Si mhuni? Maana wapo watu wana sifa za kuwa wahuni miaka yote. Anaishi maisha ya anasa. Yasiyofikiria kesho yake, asiyefikiria kwamba kuna wakati na yeye atatakiwa kuwa baba.
Kwake yeye ni kujirusha kwenda mbele. Kamwe hawezi kukupa wazo la kimaendeleo. Mtu wa aina hiyo muepuke mapema. Jiulize mtu uliye naye,  si mjanja mjanja? Historia ya maisha yake ipoje? Ana hofu ya Mungu?
Mungu ndiye aliyeweka mpango sahihi wa mwanaume kuwaacha wazazi wake na kwenda kuishi na mkewe, muombe yeye akupe mwenza sahihi wa maisha yako.
Mwenendo wa mtu hauwezi kujificha kwa miaka miwili mitatu. Atabainika tu. Usiruhusu ujauzito wakati mtu uliyenaye una shaka naye. Ikiwezekana mnaweza mkasubiri hadi pale mtakapoingia kwenye ndoa. Muombe Mungu akupe mtu ambaye atakuwa ni sahihi na asije kukutenda!
Share:

Shamsa adaiwa kubanjuka na Chid Mapenzi


SHAMSA
DIVA anayeuza sura kwenye kiwanda cha filamu Bongo, Shamsa Ford anadaiwa kubanjuka kimalavidavi na mfanyabiashara maarufu jijini Dar anayefahamika kwa jina la Chid Mapenzi, kiasi kwamba wameshindwa kujizuia na kulianika penzi lao hadharani kwenye mitandao ya kijamii.
Madai hayo ya Shamsa kubanjuka na jamaa huyo yameibuka baada ya hivi karibuni kupitia Mtandao wa Kijamii wa Instagram, Chid kuposti picha inayomuonesha akiwa uwanja wa ndege amebeba begi na kuambatanisha ujumbe wa mapenzi akimuaga Shamsa ambaye baada ya muda mfupi alijibu pia akimtakia safari njema.
Gazeti hili lilipomtafuta Shamsa na kumbana alisema; “ Jamani yule ni mtu wangu tu wakaribu, tunataniana sana na hakuna lolote linaloendelea. Kwanza hivi karibuni nataka kufungua biashara yangu ya kuuza nguo na yeye atakuwa ananisaidia kuniletea kutoka nje kwa sababu ni mzoefu kwenye biashara hiyo.”
Share:

Nuh Mziwanda: Jike Shupa imetokana na vigodoro


Nuh-mziwanda
WAKATI Naftal Mlawa ‘Nuh Mziwanda’ anaanza safari yake ya muziki miaka kadhaa iliyopita, wengi wetu tulikuwa hatuamini kama ipo siku anaweza kufikia hatua ya kufanya muziki mzuri na kuweza kukubalika.
Wengi waliamini atasikika ndani ya muda mfupi, atapotea kama ambavyo wengi wameibuka na kupotea kabla ya kufikia hatua ya kupata umaarufu.
Hata alipojaribu kutupa karata yake kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwigizaji Zuwena Mohammed ‘Shilole’, bado watu walikuwa hawaelewi anafanya nini mjini.
Wengi waliamini hata suala la mapenzi ni kiki tu za mjini. Hata alipokuja kuachwa, wengi waliamini pale ndiyo ulikuwa mwisho wa safari yake.
Lakini waswahili wanasema Mungu hamtupi mja wake, licha ya kuachwa kwa vitimbi na Shilole, kusakamwa mitandaoni kuwa alikuwa akitembea na mtu aliyemzidi umri, hatimaye amefanikiwa kufanya wimbo mkali wa Jike Shupa akimshirikisha fundi Alikiba Saleh ‘King Kiba’ ambao kwa sasa ni habari ya mjini.
Wimbo huo umekubalika. Unachezeka na video yake ni kali.
Je, Nuh anazungumziaje suala la kuonekana amemuimba Shilole? Kwa nini aliamua kuimba wimbo huo? Idea ilitoka wapi? Hapa chini pana mambo mengi zaidi:
Kwanza tuambie jina la wimbo wa Jike Shupa umelitoa wapi?
Hilo neno Jike Shupa amelitoa Alikiba wakati anaandika chorus yake.”
Unataka kutuambia haukuwa wimbo wako hadi jina alitoe Alikiba?
Hapana ni wimbo ambao nilikwishaurekodi na chorus yangu nilikuwa nimeifanya nikawa nataka niuachie, lakini nilipotafakari nikaona sijashirikiana na mtu, mashabiki wangu hawajanizoea kwenye kolabo sasa hivi ngoja nirudi kitofauti.
Nikaona bora nimtafute Alikiba, nikamsikilizisha wimbo, akaniambia mbona Nuh huu wimbo umeshaisha  halafu hapa ulivyoimba wewe mbona wimbo mkali, nikamwambia bro’mimi nahitaji sauti yako. Naomba unisaidie.
Kiba ana jina kubwa, hakukuringia wakati unamuomba kolabo?
“Nashukuru Mungu hakuchomoa. Akaniambia poa tutaenda studio, baada ya muda kama wiki mbili, tukaenda studio tukarekodi wakatoa chorus yangu ambayo mimi nilisharekodi, Ali akanza kuandika chorus yake ambayo ndiyo ikapatikana Jike Shupa ndani ya hiyo chorus.
Sasa hii Jike Shupa ina maana gani? Imetokana na nini?
“Jike Shupa ni kitu ambacho pia kilitukumbusha zamani mimi na Ali, sababu tulikuwa ni family friend. Tunachezacheza wote zamani tukienda kwenye vigodoro, kuna wale wanawake ambao hawajatulia tulikuwa tunawaita majike shupa tukiendaenda kwenye vigodoro, kwa hiyo vitu kama hivyo tukaona poa tulitumie kwa sababu tunalijua na ndiyo tumekua nalo, kwa hiyo kwa kifupi Alikiba ndiye alitoa idea ya Jike Shupa. Namshukuru kwa kufanya kitu kikubwa kwangu.
Watu wanasema umemuimba Shilole baada ya kukutenda huko nyuma, unalizungumziaje hilo?
“Just idea tu, japo watu wengine wanasema nimemuimbia mtu, lakini mimi niliimba kwa ajili ya jamii na mashabiki wangu na watu ambao wametuzunguka sababu kama mapenzi si mimi tu nimeumizwa, wapo wengi tu ambao wameumizwa. Sikujiangalia mimi tu lakini niliangalia na mashabiki wangu.
Kati ya warembo waliowahi kukuumiza penzini ni Shilole, hukuhisi kwamba atajisikia vibaya pindi atakaposikiliza wimbo huu?
Muziki ni filings. Kuimba kile kitu ambacho umekipitia. Haijalishi mapenzi na maisha magumu uliyopitia. Mimi nanukuu marehemu Remmy Ongala, alipoimba Kifo alifiwa na mtu wake wa karibu.
Kwa hiyo hivyo ni vitu ambavyo unaimba kwa fillings. So hata mimi nimeimba kitu ambacho kimenitokea. Siwezi kuimba tu kila siku vitu ambavyo vimewatokea watu wengine. Nafikiri ni jambo zuri kuwapa hisia zangu ambazo naamini hata wao ‘wamezifili’.
Sasa unafikiri Shilole anafurahia kile ulichokifanya katika video kuigiza matendo yote mliyoishi naye?
Kama yeye imemuumiza, I don’t  care. Mimi sijali kwa sababu mimi nimewapa hisia mashabiki wangu.
DONDOO:
Jina kamili: Naftal Mlawa
Umri: 24
Ngoma zake zilizobamba: Otea Nani, Zima Taa, Msondo Ngoma, Bilima, Ganda la Ndizi na Hadithi.
Share:

Drake ashitakiwa kwa wizi wa mdundo


drakewimbledon2015billboard6501.jpgKIMENUKA! Rapa maarufu kutoka Marekani, Aubrey Graham ‘Drake’ ameingia matatani baada ya kukumbwa na tuhuma za wizi wa mdundo hata kushitakiwa na Prodyuza Noel Fisher ‘Detail’ ambaye ndiye aliyetengeneza Wimbo wa Beyonce uitwao Drunk In Love.
Akizungumzia tuhuma hizo za wizi, Detail alisema Drake alimuibia mdundo huo mwaka 2014 walipokuwa na makubaliano ya kufanya kazi pamoja lakini yakavunjika na kuanzia hapo amekuwa akimtaka rapa huyo asiutumie mdundo huo lakini yeye amekaidi.
“Nimemfikisha mahakamani Drake maana amekaidi makubaliano yetu baada ya kushindwa kufanya kazi pamoja. Kiukweli hakuwa mstaarabu na hili litakuwa fundisho kwa rapa wengine wenye tabia kama yake ambao wanafikiri mkono wa sheria hauwezi kuwagusa kwa vile tu wana majina makubwa,” alisema Detail.
Hata hivyo, Drake na Detail waliwahi kuwa na ugomvi mkubwa mwaka 2014 baada ya kushindwa kufanya kazi pamoja na kupigana huku chanzo haswa cha ugonvi wao kikiwa hakijawekwa wazi.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger