Saturday 29 March 2014

UFAFANUZI WA MASWALI MBALIMBALI YA WADAU WA ELIMU KUHUSU MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2013


 

BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA


UFAFANUZI WA MASWALI MBALIMBALI YA WADAU WA ELIMU KUHUSU MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2013



Imetolewa Na:


KAIMU KATIBU MTENDAJI

29 MARCH, 2014


UFAFANUZI WA MASWALI MBALIMBALI YA WADAU WA ELIMU KUHUSU MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2013
Baraza la Mitihani la Tanzania lilitangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) 2013 tarehe 21/02/2014. Baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Baraza limekuwa likipokea maswali mbalimbali yanayoashiria kuwa baadhi ya wadau wa elimu hawakuelewa vizuri kuhusu Viwango vya Ufaulu (grade ranges), alama ya chini ya ufaulu (pass mark) na Ufaulu wa jumla wa mtahiniwa (overall performance). Baraza la Mitihani linapenda kutoa ufafanuzi katika mambo hayo kama ifuatavyo:
1.        Viwango vya ufaulu (grade ranges) ni makundi ya alama yanayopangwa ili kuwaweka pamoja watahiniwa wenye uwezo unaofanana katika somo husika na kuwatofautisha na watahiniwa waliopo katika kundi jingine. Makundi haya hupangwa ili kuwawezesha wadau kutambua namna watahiniwa walivyotawanyika katika viwango mbalimbali vya umahiri wa somo husika. Baraza la Mitihani la Tanzania, limekuwa likitumia makundi Matano (5) kwa kipindi kirefu hadi mwaka 2012. Aidha, Kuanzia Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) 2013, Baraza limeanza kutumia utaratibu wa Makundi Saba (7) ambayo ni A, B+, B, C, D, E na F. Utaratibu huu umelenga kupunguza mlundikano mkubwa wa alama katika kundi moja. Mgawanyo wa makundi hayo ni kama inavyoonekana kwenye Jedwali la 1.

Jedwali Na 1: Viwango vya ufaulu vilivyotumika katika Matokeo ya CSEE 2013.

Kundi
Gredi
Alama
Idadi ya Pointi
1
A
75 - 100
1
2
B+
60 - 74
2
3
B
50 - 59
3
4
C
40 - 49
4
5
D
30 - 39
5
6
E
20 - 29
6
7
F
0 -  19
7

Aidha, Idadi ya makundi ya ufaulu hutofautiana kati ya nchi na nchi kulingana na mahitaji ya nchi husika.  Kwa mfano; Kenya wana makundi Kumi na mbili (12), Malawi Tisa (9), Uganda Tisa (9), Nchi za Afrika magharibi (Nigeria, Ghana, Siera Leone na Liberia) makundi Tisa.

2.        Kwa kuzingatia viwango vya ufaulu vilivyoainishwa katika makundi saba yaliyopo kwenye Jedwali na 1, kiwango cha chini cha ufaulu ni gredi D na kiwango cha juu cha ufaulu ni Gredi A. Mtahiniwa atakuwa amefaulu somo husika iwapo atapata gredi D na kuendelea. Aidha, mtahiniwa aliyepata gredi E na F atakuwa hajafaulu somo husika.

3.        Madaraja ya ufaulu yamepangwa kwa mujibu wa kifungu cha 20 (1)-(6) cha Kanuni za Mitihani kinachoelekeza kuwa Ufaulu katika daraja la Kwanza hadi la Tatu upangwe kwa kuzingatia jumla ya alama (Points) na Ufaulu katika Daraja la Nne unapangwa kwa kuzingatia ufaulu wa chini aliopata mtahiniwa ambao ni gredi D katika masomo yasiyopungua mawili au ufaulu kwa kiwango kisichokuwa chini ya Gredi C katika somo moja. Hivyo, madaraja yaliyotumika ni kama yanavyoonekana kwenye Jedwali la 2.

Jedwali 2: Madaraja yaliyotumika katika CSEE 2013

Daraja
Pointi
I
7 – 17
II
18 – 24
III
25 – 31
IV
1.      Ufaulu katika somo moja kwa kiwango kisichokuwa chini ya Gredi C au
2.      Ufaulu katika masomo yasiyopungua mawili katika Gredi D
0
Alama chini ya D mbili

4.        Kwa mujibu wa Kanuni za Mitihani, ufaulu wa somo katika Gredi A hadi C utakuwa ni ufaulu wa “Credit” na Gredi D itahesabika kuwa ni “pass”. Aidha Gredi E na F zitakuwa alama za kufeli.

5.        Baraza la mitihani la Tanzania linapenda kutoa taarifa kwamba ufafanuzi wa sifa za kujiunga na mafunzo katika ngazi mbalimbali kwa kutumia mfumo huu mpya wa madaraja utatolewa na mamlaka husika ambapo Kamishna wa Elimu atalitolea ufafanuzi zaidi.




Imetolewa Na:


KAIMU KATIBU MTENDAJI
Share:

TANGAZO KWA CSEE 2014 KUTOKA NECTA





                       BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA

TANGAZO
Kaimu Katibu Mtendaji, Baraza la Mitihani la Tanzania anapenda kuwatangazia watu wote wanaotaka kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT)  mwezi Novemba,  2014  kama Watahiniwa wa Kujitegemea kwamba kipindi cha usajili kwa malipo ya  ada ya kawaida (Shilingi 50,000/=kwa wanaojisajili CSEE na Shilingi 30,000/= kwa wanaojisajili QT ) kimeongezwa kutoka tarehe 28 Februari, 2014 hadi tarehe   31 Machi, 2014. Watahiniwa watakaojisajili  kuanzia tarehe 1 Aprili, 2014 hadi tarehe 30 Aprili, 2014 watatakiwa kulipa ada ya kawaida pamoja na faini mpaka usajili utakapofungwa rasmi tarehe 30 Aprili, 2014.
Waombaji wote wanasisitizwa kuhakikisha wanajisajili mapema kwa njia ya mtandao kupitia tovuti ya Baraza la Mitihani ya www.necta.go.tz. Kabla ya kujisajili kwenye mtandao, waombaji wanapaswa kwenda kwenye vituo vya mitihani kuchukua namba rejea (reference number) zinazotolewa bure na kulipa ada ya mtihani kwa njia ya Posta au Mpesa.

Imetolewa na:
KAIMU KATIBU MTENDAJI
BARAZA LA MITIHANI LA TANZANIA.
Share:

KANGA MOJA:WAFANYA KUFURU

TAZAMA VIDEO HII HAPA CHINI


Share:

RODGERS:NO PRESSURE ON US













The Anfield outfit have won their last seven games on the bounce, putting them in contention for the title

Liverpool head into Sunday's game on the back of Wednesday's 2-1 success over Sunderland, a result that left Rodgers' side just one point behind Premier League leaders Chelsea.







The Merseyside club have won their last seven league games and are unbeaten in the Premier League in 2014, but that run has not prevented Sherwood from questioning Liverpool's ability to keep pace with Chelsea and fellow title rivals Manchester City.

However, Rodgers has been quick to dismiss Sherwood's comments, insisting that his players are calm ahead of the final run-in.

"We're very relaxed," Rodgers told reporters. "We're focused. There was no expectation on us being where we are, so there's certainly no pressure."

Rodgers also hit back at Sherwood, indicating that Tottenham - who sit seven points adrift of the top four in sixth - have performed below expectations this season.

"I suppose the likes of Tottenham are a team who were maybe looking to be challenging for the league this season. You spend £100m-odd - it's a group that's set up to challenge," he added.

"There's certainly no pressure on ourselves, and I think we've shown that over the course of the season. We're playing with no fear.

"We're very hungry to succeed and that can give you a real advantage. We've proved that already this season. Experience isn't everything.

"We're looking to make sustainable success. That's our objective. We're looking to build something here."
Share:

VIDEO:BUNGE LA KATIBA KUHUSU MARIDHIANO YA KANUNI JANA


ANGALIA VIDEO :

Share:

CHAMPIONI JUMAMOSI, JIPATIE NAKALA YAKO LEO

Share:

NO PRESSURE ON US-RODGERS

The Anfield outfit have won their last seven games on the bounce, putting them in contention for the title

Betare feeling the pressure in the title race.


Liverpool head into Sunday's game on the back of Wednesday's 2-1 success over Sunderland, a result that left Rodgers' side just one point behind Premier League leaders Chelsea.







The Merseyside club have won their last seven league games and are unbeaten in the Premier League in 2014, but that run has not prevented Sherwood from questioning Liverpool's ability to keep pace with Chelsea and fellow title rivals Manchester City.

However, Rodgers has been quick to dismiss Sherwood's comments, insisting that his players are calm ahead of the final run-in.

"We're very relaxed," Rodgers told reporters. "We're focused. There was no expectation on us being where we are, so there's certainly no pressure."

Rodgers also hit back at Sherwood, indicating that Tottenham - who sit seven points adrift of the top four in sixth - have performed below expectations this season.

"I suppose the likes of Tottenham are a team who were maybe looking to be challenging for the league this season. You spend £100m-odd - it's a group that's set up to challenge," he added.

"There's certainly no pressure on ourselves, and I think we've shown that over the course of the season. We're playing with no fear.

"We're very hungry to succeed and that can give you a real advantage. We've proved that already this season. Experience isn't everything.

"We're looking to make sustainable success. That's our objective. We're looking to build something here."
Share:

Kura mchanganyiko Bunge la Katiba

Kura mchanganyiko Bunge la Katiba

Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Profesa Abdul Shariff (kulia) akipiga kura ya siri wakati Bunge hilo jana lilipokuwa likipitisha utaratibu wa kupiga kura za aina mbili (siri na wazi). . 
Kwa ufupi
Mjumbe Vuai Ali Vuai alisema, wamefikia maridhiano hayo, ili kuwezesha kuendelea na mchakato wa katiba mpya kwani kila upande uliendelea kutetea msimamo wake hata katika kikao cha maridhiano.


Dodoma.Wajumbe wa Kamati ya Maridhiano jana walinusuru Bunge Maalumu la Katiba kuvunjika, baada ya kukubaliana kutumika kwa utaratibu wa upigaji kura wa wazi na siri kama ilivyopendekezwa na Kamati ya Kanuni na Haki za Bunge.
Wajumbe hao walitangaza uamuzi huo bungeni kutokana na makubaliano yaliyofikiwa katika kamati ndogo ya maridhiano iliyofanyika jana asubuhi baada ya kushindwa kuafikiana katika kikao cha awali kilichofanyika juzi kuanzia saa 3:00 usiku hadi usiku wa manane ili kunusuru kukwama kwa Bunge hilo.
Kabla ya uamuzi huo, Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samuel Sitta alisema juzi usiku walikutana hadi usiku wa manane baada ya hapo, walikabidhi kamati ndogo yenye mchanganyiko wa wajumbe kutoka Kamati ya Kanuni na Kamati ya Maridhiano.
“Baada ya kukamilisha kazi, wajumbe wa kamati ndogo watatoa taarifa hapa ambao ni John Mnyika, Profesa Ibrahimu Lipumba, Vual Ali Vual na Askofu Donald Mtetemela,”alisema Sitta.
Akitoa taarifa ya maridhiano hayo, kwa niaba Freeman Mbowe, Mjumbe John Mnyika alisema, alianza kwa kunukuu kitabu kilichoandikwa na Mwalimu Nyerere, mwaka 1962 chenye ujumbe mahususi kwa Chama cha TANU akisema ujumbe huo kwa sasa ni sahihi kwa watu wengi na taasisi ikiwamo CCM.
Mnyika pia alisema Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) hawana nia yoyote ya kuvuruga mchakato wa katiba kama ambavyo imeelezwa katika siku za karibuni na viongozi, kwani wazo la kutaka Katiba Mpya imekuwa ni kilio chao cha muda mrefu.
Naye Profesa Lipumba alisema suala ambalo tumekuwa tukisimamia kwa muda mrefu suala ambalo lina utata, kati ambao wanapenda kura za uwazi na wale wa siri.
Alisema: “Tuliletewa mchanganyiko wa uwazi na siri, lakini maana yake ni kura ya uwazi, wenzetu wamekuwa na msimamo mkali hata hili la kufanya uamuzi ilikuwa tufanye kwa siri, lakini hata hivyo hawakukubali.”
“Tulifanya uamuzi ili tusonge mbele, basi tulipendekeza upigaji kura wa kuamua tupige kura kwa mfumo wa siri, lakini pia wenzetu walikataa,”alisema Profesa Lipumba.
Alisema kwa kuzingatia kutokwama kwa zoezi la kuanza kujadili rasimu, wameamua kukubali kutokubaliana.
“Ili kusonga mbele tunahitaji kusonga mbele tuanze kujadili Katiba, natoa wito kwa wenzangu wa chama tawala kwa kuwa mpo wengi mnadhamana kubwa, ni vyema mkawa na utaratibu wa kuwasikiliza wachache,” alisema.
Mjumbe Vuai Ali Vuai alisema, wamefikia maridhiano hayo, ili kuwezesha kuendelea na mchakato wa katiba mpya kwani kila upande uliendelea kutetea msimamo wake hata katika kikao cha maridhiano.
Share:

DUDE APATA AJALI LOLIONDO

DUDE APATA AJALI LOLIONDO


STAA wa sinema za Kibongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’ amepata ajali ya gari wakati akielekea Loliondo, Arusha kupata dawa ya kikombe inayotolewa na mchungaji mstaafu, Ambilikile Mwaisapila.
Staa wa sinema za Kibongo, Kulwa Kikumba ‘Dude’
Dude ameiambia Bongowood kuwa, hivi karibuni walikuwa na gari aina ya Toyota Prado wakimpeleka mama yake kupata tiba ya ganzi mwilini ndipo tairi lilipopasuka na gari kuangukia gema.
“Ilipoteza muelekeo, likayumba lakini nashukuru Mungu hatukuumia, tukasaidiwa kunyanyua, tukaenda kupata tiba ya babu,” alisema Dude.
Share:

Friday 28 March 2014

VIDEO: TAZAMA AJALI HII KUBWA YA NDEGE ILIVYOTOKEA


Share:

MAPIGANO MAKALI DHIDI YA M23


Share:

VIDEO:25TH MATCH BETWEEN MAN CITY AND MAN UNITED


Share:

VIDEO:KAMATI YA MARIDIANO YA KANUNI ZA BUNGE IKIJADILI KUHUSU KANUN HIZO


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger