Friday, 21 November 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 21,2025

Magazeti
 
Share:

Thursday, 20 November 2025

TUWAKATAE WANAONUFAIKA NA VURUGU- KAZAZI



Na Mwandishi Maalum, Dar

Vijana na Watanzania kwa ujumla wametakiwa kujiepusha na kutumika na watu wachache wenye kutanguliza maslahi yao binafsi ambao wamekuwa wakipata kipato kutokana na uharibifu, vurugu na ghasia wanazozihamasisha kufanywa ndani ya Jamii ya Watanzania.

Wito huo umetolewa na Bw. Juma Rashid Kazazi, Mkazi wa Dar Es Salaam wakati akizungumza kuhusu kadhia ya vurugu, wizi na uharibifu uliotokea Oktoba 29, 2025 na baada ya siku ya uchaguzi Mkuu wa Tanzania, akisema wapo wanaonufaika na ghasia hizo huku washiriki wa ghasia hizo wakiathirika.

"Ndugu zangu Watanzania sasa tusifikie Vijana tukawa ni sehemu ya kipato cha watu, mtu anakuja kwa maslahi yake. 

Hilo jambo nawasisitiza Vijana wa Kitanzania mjaribu kukaa, mfikirie na si kila jambo ni la kupokea maana katika matukio haya wanatengenezea watu kipato na sisi tunabaki kuumia, kushinda njaa, kupigwa na hata kufa."

"Wao wanafaidika sisi tunaendelea kuumia na ni muhimu tujifunze kwa tukio lile na kama wana nia njema waje na wao tushirikiane kwenye kuandamana badala ya kututanguliza sisi wakati wao wapo nje ya nchi. Niwaombe Vijana hili jambo tuliangalie kwa ukubwa na tuwakatae watu hawa na kile wanachotuambia." Amesema Bw. Kazazi.

Akieleza kuwa ni mara ya kwanza kushuhudia uharibifu na vurugu zile, amewaomba watanzania pia kukemea jambo hilo jipya nchini, akisema ikiwa Watanzania wote watasimama pamoja watafanikisha kuidumisha amani ya Tanzania na kuruhusu kila mmoja kuendelea na shughuli zake za kiuchumi na kijamii.
Share:

Wednesday, 19 November 2025

MKUU WA WILAYA YA KAHAMA AFANYA KIKAO NA VIONGOZI WA DINI KUJADILI NAMNA YA KUIMARISHA AMANI

  

Mkuu wa Wilaya ya Kahama Frank Nkinda, ameongoza kikao maalum na Viongozi wa Dini pamoja na wajumbe wa Baraza la Amani Wilaya ya Kahama, chenye lengo la kujadili hali ya amani na kuweka mikakati ya kuendelea kuilinda amani katika wilaya hiyo.

Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya, kikihusisha viongozi kutoka madhehebu mbalimbali ya kidini ambao wamekutana kubadilishana mawazo juu ya namna bora ya kudumisha maelewano, mshikamano na utulivu wa jamii.

Akizungumza kwenye kikao hicho, Dc Nkinda amesisitiza kuwa amani ndiyo msingi wa ustawi wa wananchi na maendeleo ya wilaya, akibainisha kuwa Serikali inaiona nafasi ya viongozi wa dini kama ya msingi katika kuhamasisha maadili, uwajibikaji na utulivu wa kijamii.

 "Kahama imekuwa mfano wa maeneo yenye utulivu na mshikamano, Ili tufike mbali zaidi, tunahitaji ushirikiano wa dhati kati ya Serikali na taasisi za dini,  Amani haitokei tu tunaitengeneza na kuilinda kwa pamoja", amesema Mhe. Nkinda.

Kwa upande wao, viongozi wa dini wameipongeza Serikali kwa utaratibu wa kuwaleta pamoja na kuwashirikisha katika masuala muhimu yanayoigusa jamii, huku wakiahidi kuendelea kuwa mstari wa mbele kuhimiza amani, upendo na uvumilivu miongoni mwa waumini na wananchi kwa ujumla.

Baraza la Amani limesema kuwa litaendeleza majadiliano na mikutano ya mara kwa mara ili kuhakikisha changamoto ndogo ndogo zinazoweza kuhatarisha amani zinatambuliwa mapema na kutafutiwa suluhu.

Kikao hicho kimehitimishwa kwa makubaliano ya kuongeza ushirikiano kati ya Serikali, taasisi za dini na wadau wengine, kuhakikisha Kahama inasalia kuwa wilaya salama, yenye utulivu na mwelekeo mzuri wa maendeleo.

Share:

RAIS SAMIA AWAAPISHA MAWAZIRI WAPYA IKULU CHAMWINO, DODOMA



Na Dotto Kwilasa, Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaapisha Mawaziri wa Wizara mbalimbali kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 18 Novemba, 2025.

Hafla hiyo imehudhuriwa na viongozi waandamizi wa Serikali, wawakilishi wa vyombo vya ulinzi na usalama, viongozi wa dini pamoja na wageni mbalimbali, ikiashiria mwanzo mpya wa safari ya kuimarisha utendaji wa Serikali ya Awamu ya Sita.

Katika hotuba yake mara baada ya uapisho, Rais Samia amewataka viongozi hao wapya kufanya kazi kwa kasi, ubunifu na uadilifu ili kuhakikisha Serikali inaendelea kutekeleza mipango ya maendeleo kwa manufaa ya wananchi wote.

Amewakumbusha kuzingatia uwajibikaji, ushirikiano na kusimamia vizuri rasilimali za umma.

Uapisho huu unaendelea kuonesha dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kuleta matokeo chanya, kuimarisha utawala bora na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

Share:

Tuesday, 18 November 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 19,2025




Magazeti ya leo







Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger