Monday, 28 July 2025
WAFANYAKAZI WA BARRICK WALIVYOSHIRIKI NBC DODOMA MARATHON 2025
Sunday, 27 July 2025
UCHAGUZI MKUU 2025: WANAWAKE WAMEJITOKEZA, VYAMA VIWATEUE

Wadau wa masuala ya wanawake na uongozi wamevitaka vyama vya siasa nchini kuhakikisha vinawateua wanawake waliokidhi vigezo kugombea nafasi za uongozi katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025, hususan kwenye nafasi za uwakilishi, ubunge na udiwani zinazoshindaniwa majimboni.
Wakizungumza katika taarifa yao kwa vyombo vya habari, wadau hao wameeleza kuwa kwa muda mrefu wanawake wamekuwa wakipewa nafasi za viti maalum pekee, hatua inayowanyima nafasi ya kushindana moja kwa moja na wanaume na kuonesha uwezo wao katika siasa za ushindani.
Katika kipindi hiki cha mchakato wa chaguzi za ndani ya vyama kuelekea uchaguzi mkuu, wanawake wengi wamejitokeza kuchukua fomu, licha ya kuwa idadi yao bado ni ndogo kulinganisha na wanaume.
Kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuhusu Zanzibar, wanachama 1,640 wamechukua na kurejesha fomu za kugombea Ubunge, Uwakilishi na Udiwani, ambapo kati yao wanawake ni 406, sawa na asilimia 24.7.
Chama cha ACT Wazalendo kwa upande wake kimeripoti kuwa kati ya wanachama 435 waliotangaza nia ya kugombea nafasi hizo visiwani humo, wanawake ni 40 pekee, sawa na asilimia 9.2.
Vyama hivyo vinasubiri vikao vya Kamati Kuu na Kamati Maalum kupitisha rasmi majina ya wagombea, mchakato unaotarajiwa kukamilika mwishoni mwa Julai hadi Agosti 2025.
Wadau wametoa pongezi kwa wanawake hao kwa ujasiri wa kujitokeza lakini wakasisitiza kuwa hatua hiyo haitoshi iwapo hawatapewa nafasi halisi ya kugombea majimboni.
Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020, Zanzibar ilifanikiwa kupata wanawake wanane pekee (sawa na asilimia 16) katika Baraza la Wawakilishi na wabunge wanne (asilimia 8), kupitia siasa za ushindani.
“Tunaomba wajumbe wa vikao vya uteuzi kwenye vyama mbalimbali kuwapigia kura wanawake wakati wa mchakato wa kuwapata wagombea wa mwisho. Huu ni wakati wa kufanya mabadiliko halisi ya kisiasa na kijamii kwa kuzingatia usawa wa kijinsia,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.
Wadau wamesisitiza kuwa uwepo wa wanawake kwenye nafasi za juu za uongozi ni chachu ya maendeleo ya taifa, kwani tafiti mbalimbali zinaonesha kuwa wanawake ni viongozi waadilifu, wanaoweka mbele maslahi ya familia na jamii, na ni wasikivu na wenye kujitoa.
Wakirejea Mkataba wa Kimataifa wa Kuondoa Aina Zote za Ubaguzi Dhidi ya Wanawake (CEDAW) wa mwaka 1979, wadau hao wamekumbusha wajibu wa Tanzania kama nchi mwanachama kuhakikisha inachukua hatua za kuongeza ushiriki wa wanawake katika vyombo vya maamuzi.
Taarifa hiyo imetolewa kwa ushirikiano wa taasisi kadhaa za wanawake zikiwemo Jumuiya ya Wanawake wenye Ulemavu Zanzibar (JUWAUZA), Jumuiya ya Wanasheria Wanawake Zanzibar (ZAFELA), Jumuiya ya Mazingira, Jinsia na Utetezi Pemba (PEGAO) na Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania – Zanzibar (TAMWA ZNZ), kwa kushirikiana na Ubalozi wa Norway.
Wamewatia moyo wanawake waliotia nia wasikate tamaa bali waendelee kuwa imara na waaminifu kwa dhamira ya uongozi kwa maslahi ya jamii na taifa kwa ujumla.
MRADI WA SEQUIP WAJENGA SHULE 6 MPYA IRAMBA-DC MWENDA
KONGAMANO LA WANAWAKE WA KIISLAMU LATOA TUMAINI KWA WATOTO YATIMA NA WAJANE SONGEA
Kongamano la wanawake wa Kiislamu wakiwa katika kituo cha watoto yatima cha Luhila kwa Mangoma Manispaa ya Songea Mkoani Ruvuma wakiburudika kwa pamoja Na Regina Ndumbaro Songea-Ruvuma
Kongamano maalum la wanawake wa Kiislamu kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara na Zanzibar limefanyika katika kituo cha watoto yatima cha Luhila kwa Mangoma, Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, likiwa na lengo la kusaidia watoto yatima, wanaoishi katika mazingira magumu pamoja na wajane.
Kongamano hilo limeandaliwa kwa ushirikiano wa taasisi mbalimbali na kikundi cha Umoja wa Wanyonge kinachosaidia jamii kwa moyo wa kujitolea.
Akizungumza katika kongamano hilo, Bi Aziza Issa, mwanzilishi wa kituo cha watoto yatima cha Luhila, amesema kuwa kituo hicho kinahudumia watoto 59 na kwa sasa kinakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa nyumba ya mwalimu na fensi kwa usalama.
Ameeleza kuwa jumla ya shilingi milioni 56 zinahitajika kukamilisha ujenzi huo wa nyumba ya mwalimu pamoja na fensi amewaomba wadau kujitokeza kuchangia chochote walichonacho.
Kwa yeyote atakayeguswa, anaweza kuwasiliana naye moja kwa moja kupitia namba 0784 856 649.
Bi Zena Mtamba kutoka wilaya ya Masasi, ambaye ni amirathi wa kanda ya kusini na muhamasishaji wa kulea watoto yatima na wasiojiweza.
Amekabidhi mchango wa shilingi milioni 1 na laki moja kwa kituo hicho na kusisitiza kuwa malezi ya watoto si jukumu la serikali pekee bali kila mwanajamii anapaswa kushiriki.
Aidha, ametangaza kuwa kongamano lijalo litafanyika wilayani Masasi mwezi Oktoba au Novemba.
Kwa upande wake, Bi Lulu Ramadhani, mjane mwenye watoto wanne, ameeleza kwa hisia namna kituo hicho kilivyomsaidia baada ya mume wake kufariki dunia akiwa mjamzito wa miezi saba.
Amemshukuru Bi Aziza kwa moyo wake wa huruma na kujitolea, akisema kuwa kupitia msaada wa kituo hicho, yeye na mke mwenzie wameweza kulea watoto wao kwa heshima na utu pamoja na kupatiwa mahitaji muhimu.
Kongamano hili limekuwa jukwaa muhimu la kujadili changamoto mbalimbali zinazowakumba watoto yatima na wajane, huku likiwaunganisha wanawake wa dini tofauti kwa lengo la kusaidia jamii.
Wanawake hao wametoa wito kwa viongozi wa serikali, vyama vya siasa na wananchi kwa ujumla kujitokeza kusaidia kundi hilo lenye uhitaji mkubwa, ili kuepusha watoto kuingia katika mazingira ya hatari na ukatili wa kijinsia.
Mjane aliesaidiwa na kituo cha Luhila kwa Mangoma Bi Lulu Ramadhani pichani akiwa na mwanae ambaye aliachwa na mumewe akiwa na ujauzito wa miezi saba pindi mume wake anafariki dunia
Saturday, 26 July 2025
KATIBU MKUU MKOMI AKAGUA MAENDELEO YA MRADI WA UJENZI WA MAKAZI YA WATUMISHI KIJIJI CHA KIJIWENI
AGNESS SULEIMAN 'AGGY BABY' AANDIKA HISTORIA MPYA: ASHINDA TUZO MBILI KWENYE AFRICA ARTS ENTERTAINMENT AWARDS 2025
Tuzo hizo zilitolewa rasmi tarehe 25 Julai 2025 katika hoteli ya kifahari ya Protea Hotel Courtyard, jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Aggy Baby ameshinda katika vipengele viwili vinavyothibitisha mchango wake mkubwa ndani na nje ya sanaa:
✅ Best Inspirational Youth Icon / Motivator
✅ Fastest Rising Foundation of Excellence (kupitia taasisi yake ya kijamii – Tupaze Sauti Foundation)
Ushindi huu si wa kawaida. Ni uthibitisho wa jitihada zake si tu kwenye muziki na burudani, bali pia kwenye kuhamasisha maendeleo ya vijana wa Kitanzania kupitia elimu, maadili na miradi ya kijamii.
Mashabiki wake na Watanzania kwa ujumla wanahimizwa kuendelea kumuunga mkono msanii huyu wa kipekee, ambaye kwa sasa ni nembo ya ubunifu, kipaji na uzalendo wa kweli.
Aggy Baby si msanii tu – ni kielelezo cha matumaini, uthubutu na mabadiliko chanya kwa kizazi kipya.
🔗 Fuata kurasa rasmi za tuzo hizi kwa taarifa zaidi:
@eaea_tanzania na @eaea_awards_inc
#AggyBabyFahariYaTanzania 🇹🇿
#EAEATanzania2025
#TalantaZaKikwetu
#EAEACountryLevelAwards2025


BANDARI KAVU YA KWALA KUZINDULIWA RASMI JULAI 31
Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame MbarawaNa Sheila Ahmadi – Dar es Salaam
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuzindua rasmi Bandari Kavu ya Kwala, mkoani Pwani, tarehe 31 Julai 2025.
Uzinduzi huo utahusisha pia upokeaji wa mabehewa ya mizigo, pamoja na safari za treni za mizigo ya SGR kati ya Dar es Salaam na Dodoma. Hii ni hatua muhimu katika kuboresha usafirishaji wa mizigo nchini na kuongeza ufanisi wa shughuli za bandari.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa, amesema kuwa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA), kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa sekta ya bandari, inaendelea kuboresha miundombinu kwa wakati ili kuchochea ukuaji wa uchumi na biashara nchini, hasa katika maeneo ya Dar es Salaam na Pwani.
“Bandari Kavu ya Kwala itasaidia kupunguza msongamano mkubwa wa magari katika barabara ya Mandela, sambamba na kuongeza ajira kwa wakazi wa maeneo ya jirani,” amesema Prof. Mbarawa.
Ameongeza kuwa serikali inatarajia pia ongezeko la viwanda katika eneo hilo, hali itakayoongeza mapato ya serikali kwa kiwango kikubwa.
Aidha, Prof. Mbarawa amefafanua kuwa serikali haijaitelekeza reli ya zamani ya MGR, ambapo katika hafla hiyo ya uzinduzi, Rais Dkt. Samia atapokea mabehewa mapya 50 kati ya 100 yaliyonunuliwa na Shirika la Reli Tanzania (TRC). Vilevile, mabehewa 20 ya MGR yamefanyiwa ukarabati na Wakala wa Uwezeshaji wa Ushoroba wa Kati.
Kwa mujibu wa Waziri huyo, usafirishaji wa mizigo kati ya Dar es Salaam na Dodoma ulianza rasmi Juni 27, 2025 ambapo makontena 10 yenye jumla ya tani 700 za bidhaa mchanganyiko kutoka Kampuni ya Azania yalisafirishwa.
Bandari hiyo ya Kwala inatarajiwa kuhudumia makasha 823 kwa siku, sawa na makasha 300,395 kwa mwaka, ambayo ni asilimia 30 ya makasha yote yanayohudumiwa kwa sasa na Bandari ya Dar es Salaam. Pia, bandari hiyo itakuwa kituo muhimu cha kusafirisha shehena ya makasha kwenda nchi jirani.
“Tunatoa wito kwa wadau wote wa usafirishaji, wafanyabiashara na wawekezaji kuchangamkia fursa ya gharama nafuu na usafiri wa uhakika kupitia Bandari Kavu ya Kwala,” amesema Prof. Mbarawa.





































