Tuesday, 8 July 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 8,2025




Magazetini





Share:

Monday, 7 July 2025

EXPLORE THE WILD WONDERS OF SERENGETI – UNFORGETTABLE DAY TRIP FROM BUNDA!




TECTO COMMUNITY COMPANY LTD (TECTO TOUR & TRAVEL)

Your Gateway to Wildlife, Culture & Conservation in Tanzania

🌍 SERENGETI NATIONAL PARK TOUR – WESTERN SERENGETI (Day Trip)
Date: 08/08/2025 (Friday)
Route: Via Ndabaka Gate (Only 20km from Bunda)
Group Offer: Tsh 880,000 for 5 Adults & 2 Children


Package Includes:
✔️ Lunch Box
✔️ Soft Drinks
✔️ T-shirt
✔️ Park Entry Fees
✔️ Guide Fees
✔️ Wildlife Photography Opportunities

Welcome / Karibu Sana!

🚌 STAFF & GROUP TOUR OPTION (30 Tourists)
Travel by Bus (TATA or Coaster)
Cost per Person: Tsh 85,000
Includes:
✔️ Transport
✔️ Lunch Box
✔️ Soft Drinks
✔️ T-shirt
✔️ Park Entry Fees
✔️ Guide Fees

📍Visit Our Lake Victoria Zone Office:
Sarakwa Road, Opposite Diamond, Bunda - Mara, Tanzania

📞 Contact Us Today:
WhatsApp/Call: +255 746 988 397
Call: +255 785 064 024
📧 Email: tectocampany2020@gmail.com



Share:

WAHITIMU WA DARASA LA SABA 2002 MITWERO WAKABIDHI MADAWATI, WAMEOMBA WADAU KUJITOKEZA KUSAIDIA

baadhi ya wahitimu wa darasa la saba mwaka 2002 wakiwa pamoja na walimu na wanafunzi wa shule ya msingi Mitwero mkoani Lindi baada ya kukabidhi madawati shuleni 

Na Regina Ndumbaro-Lindi 

Baadhi ya wahitimu wa darasa la saba mwaka 2002 kutoka Shule ya Msingi Mitwero, iliyopo Kata ya Rasibula, Manispaa ya Lindi, wamekabidhi msaada wa madawati 8 yenye thamani ya Shilingi 780,000 kwa shule yao ya zamani. 

Wahitimu hao walikabidhi madawati hayo kama njia ya kurudisha shukrani kwa jamii na kusaidia kutatua changamoto ya uhaba wa madawati shuleni hapo. 

Mwenyekiti wa umoja huo, Mosses Verisi, amesema wameanza na kidogo lakini wana dhamira ya kuendelea kusaidia zaidi kila mwaka.

Mwalimu  mkuu  msaidizi wa shule ya msingi Mitwero, Amina Mohamedi, amesema shule hiyo ilikuwa na uhaba wa madawati 45 na msaada huo wa madawati 8 umepunguza pengo hilo hadi 37. 

Amewataka wahitimu wengine pamoja na wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia ukarabati wa madarasa chakavu ambayo yanavuja, akisisitiza kuwa shule hiyo bado inakabiliwa na changamoto nyingi za miundombinu.

Kwa upande wa wanafunzi wa sasa, akiwemo Yasini Steven na Agnes Raymond, wameeleza furaha yao kwa kupokea madawati hayo, wakisema yatasaidia kupunguza msongamano darasani na kuongeza hamasa ya kuhudhuria masomo. 

Wametoa wito wa kupatiwa msaada zaidi kama vitabu na vifaa vingine vya kufundishia

Akizungumza wakati wa hafla ya makabidhiano, Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva, amewapongeza wahitimu hao kwa moyo wao wa kujitolea na kuwasihi wahitimu wengine wa shule za serikali kufuata mfano huo.

Pia Kaimu Afisa Elimu Msingi na Awali, Selemani Mgeleka, ameahidi kushirikiana na wadau hao na kuwataarifu pindi shughuli za ukarabati zitakapoanza ili waweze kushiriki kikamilifu.


Baadhi ya wanafunzi wakiwa wamekaa juu ya madawati hayo baada ya kuletwa na wanafunzi waliohitimu darasa la saba mwaka 2002 shuleni hapo 




Share:

Sunday, 6 July 2025

NILISHINDWA KUJIFUNGA VIATU KWA TUMBO KUBWA LAKINI BAADA YA DAWA HII YA ASILI, WATU HUNIPITA WAKIDHANI MIMI NI MWANAFUNZI WA SEKONDARI



Nilikuwa nimezoea watu kunishangaa kila nilipoingia kwenye daladala au sehemu yenye viti vya plastiki. Wengine walifanya mzaha, wengine walinicheka, lakini wengi waliongea kwa sauti ya chini kana kwamba siwezi kusikia.

Ukweli ni kwamba nilikuwa na uzito kupita kiasi. Tumbo langu lilining’inia mpaka hata kujifunga viatu ilikuwa kazi nilihitaji kukaa kwenye kitanda, kuinama kwa muda mrefu huku nikivuja jasho. Na hata hivyo, viatu vingine nilivivaa tu bila kufunga.
Share:

KATIBU TAWALA WILAYA YA KAHAMA AWAPONGEZA WASHIRIKI WA MAONESHO YA SABASABA 2025 KUTOKA MKOA WA SHINYANGA

Katibu Tawala wa Wilaya ya Kahama, Bi. Glory Absalum, amewapongeza wafanyabiashara kutoka Mkoa wa Shinyanga wanaoshiriki Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba, yanayoendelea katika Viwanja vya J.K Nyerere, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mara baada ya kutembelea mabanda ya washiriki hao yaliyopo ndani ya Banda la Sadan, mkabala na Banda la TANESCO, Bi. Glory amepongeza ubunifu mkubwa unaofanywa na wafanyabiashara hao, hususan katika kuongeza thamani ya bidhaa mbalimbali walizonazo.

“Nawapongeza kwa dhati wafanyabiashara wote kutoka Halmashauri zote za Mkoa kwa ushiriki wenu mzuri. Maonesho haya ni fursa adhimu ya kuuza bidhaa zenu, kutangaza huduma mnazotoa pamoja na kuonesha fursa zilizopo katika maeneo yenu. Huu ni wakati muafaka wa kushirikiana na wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi,” alisema Bi. Glory.

Aidha, ameeleza kuwa kiwango cha maandalizi na ubora wa bidhaa zinazotolewa na washiriki kutoka Mkoa wa Shinyanga ni ushahidi wa uwezo mkubwa walionao na utayari wa kushindana katika masoko ya Kitaifa na Kimataifa.

Mabanda ya Mkoa wa Shinyanga yamekuwa kivutio kikubwa kwa wageni mbalimbali wakiwemo viongozi wa Serikali, wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi pamoja na wananchi, kutokana na ubunifu, nidhamu ya kazi na bidhaa zenye viwango vya juu vinavyoendana na mahitaji ya soko.

Maonesho ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba ni jukwaa muhimu kwa wafanyabiashara na taasisi mbalimbali kuonesha bidhaa, huduma na teknolojia mpya, huku yakihamasisha uwekezaji ndani ya Mkoa wa Shinyanga na ushirikiano wa kibiashara kati ya Tanzania na mataifa mengine.

Share:

DIB YAENDELEA KUTOA ELIMU KATIKA MAONESHO YA 49 YA SABASABA


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Bodi ya Bima ya Amana (DIB) inaendelea kutoa elimu kwa wananchi na wadau mbalimbali katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa maarufu kama SABASABA, yanayoendelea kufanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Barabara ya Nyerere, Jijini Dar es Salaam.

Wananchi wote wanakaribishwa kutembelea banda la DIB ili kupata elimu kuhusu majukumu ya Bodi, umuhimu wa ulinzi wa amana zao kwenye taasisi za fedha, pamoja na nafasi ya DIB katika kuhakikisha usalama na uthabiti wa mfumo wa fedha nchini.

Kwa sasa, DIB ipo katika mchakato wa kuboresha muundo wake wa kisheria na kiutendaji, hatua inayolenga kuimarisha mchango wake katika sekta ya fedha na kuhakikisha inajitegemea kwa ufanisi zaidi.

Mabadiliko haya yanatarajiwa kuongeza ufanisi wa DIB katika kutekeleza majukumu yake ya msingi, ikiwemo kulinda haki za wateja wa taasisi za fedha na kuimarisha imani ya wananchi katika mfumo wa kifedha wa Tanzania.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JULAI 6,2025

Magazeti
Share:

Saturday, 5 July 2025

Tanzia : BINGWA WA MASHAIRI, MWANDISHI WA HABARI SHOMARI BINDA AFARIKI DUNIA


 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger