Wednesday, 30 April 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 30, 2025


 

Magazeti ya leo


















Share:

Tuesday, 29 April 2025

WAZIRI MKUU : SERIKALI ITAENDELEA KULINDA UHURU WA HABARI KWA VITENDO, WAANDISHI TUMIEMI AKILI MNEMBA KWA UWAJIBIKAJI


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, akizungumza jijini Arusha leo Aprili 29, 2025 wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani- Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, akizungumza jijini Arusha leo Aprili 29, 2025 wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani
Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, akizungumza jijini Arusha leo Aprili 29, 2025 wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani

***

👉Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Asisitiza Akili Mnemba Isaidie, Isiwe Kikwazo kwa Uhuru wa Habari 

👉Serikali Kulinda Uhuru wa Vyombo vya Habari kwa Vitendo

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, amesema Serikali itaendelea kulinda uhuru wa vyombo vya habari kwa vitendo na si kwa maneno, akisisitiza matumizi sahihi ya akili mnemba (Artificial Intelligence) kama chachu ya uwajibikaji na si kikwazo kwa waandishi wa habari.

Akizungumza jijini Arusha leo Aprili 29, 2025 wakati akifungua rasmi maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani (World Press Freedom Day 2025) ,yenye kaulimbiu ya mwaka huu isemayo “Uhabarishaji katika Dunia Mpya: Mchango wa Akili Mnemba kwenye Uhuru wa Vyombo vya Habari”, Mhe. Majaliwa ametoa wito kwa wanahabari kutumia akili mnemba kwa weledi na kuzingatia ukweli wa taarifa wanazotoa.

“Akili Mnemba itumike kama nyenzo kwa waandishi wa habari na siyo kikwazo. Mjitahidi kuitumia vizuri kwa uwajibikaji, kutoa taarifa sahihi na zenye kuzingatia maadili ya taaluma. Serikali kwa kushirikiana na Wadau tunaendelea na mchakato wa kutengeneza sera kuhusu Akili Mnemba ”, amesema Waziri Mkuu.

Katika kuelekea Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, Mhe. Majaliwa ametaka vyombo vya habari kuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha uchaguzi unakuwa huru, haki na wa uwazi akihimiza utoaji wa taarifa sahihi, zinazojenga amani na mshikamano.

"2025 huu ni mwaka wa uchaguzi, sisi kama serikali, kama wadau wa uchaguzi, pindi tume huru ya uchaguzi watatoa ratiba tunatarajia nyie ndiyo mtalieleza taifa (Wanahabari) na sisi ushiriki wetu ni kuhakikisha kwamba yale yaliyo muhimu ya kuufanya uchaguzi huu kuwa wa usalama, na kila mmoja atakwenda kushiriki kwa usalama wake.. Na watu wa tume huru ya uchaguzi wametuambia kwamba uchaguzi huu watausimamia kwa uhuru na haki na uwazi. Na sisi serikali kama wadau wa uchaguzi tunataka tuwahakikishie kuwa uchaguzi huu utakuwa ni wa amani na utulivu", amesema Waziri Mkuu.

“Uchaguzi huu utakuwa wa amani na utulivu. Ninyi waandishi wa habari mtakuwa sehemu ya walinzi wa amani. Toeni taarifa zinazohamasisha kulinda tunu zetu za kitaifa,” amesisitiza.

Aidha, amevitaka vyombo vya habari kuendelea kuelimisha na kuhabarisha jamii kuhusu maendeleo ya taifa, kwa kuzingatia ukweli na uadilifu.

Waziri Mkuu ameeleza kuwa, Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan itaendelea kulinda uhuru wa vyombo vya habari kwa vitendo siyo maneno, ikiwa ni pamoja na kuweka mazingira rafiki ya upatikanaji wa taarifa na uhuru wa kujieleza.


Maelezo TV LIVE tola ARUSHA📍

🎈SIKU YA UHURU WA VYOMBO HABARI DUNIANI 2025

Share:

Monday, 28 April 2025

RAIS SAMIA SULUHU AHAMASISHA HUDUMA BURE ZA SARATANI KWA WANANCHI WA KILWA


Madaktari Bingwa kutoka Hospitali ya Ocean Road wakiwa katika picha ya pamoja na Watumishi wa Wilayani Kilwa Mkoani Lindi katika hatua ya kupeleka huduma ya ugonjwa wa Saratani kutokana na maagizo ya Mheshimiwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan Mkoani Lindi

Na Regina Ndumbaro Kilwa-Lindi.

Timu ya Madaktari Bingwa kutoka Hospitali ya Ocean Road, wakitimiza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, wametembelea Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilwa na kufanya mazungumzo na viongozi pamoja na watumishi wa halmashauri hiyo. 

Mazungumzo hayo yamehusu maandalizi ya zoezi la utoaji wa huduma za uchunguzi na matibabu ya magonjwa ya saratani kwa wananchi wa Wilaya ya Kilwa, zitakazotolewa katika Hospitali ya Wilaya ya Kinyonga kwa muda wa siku tatu kuanzia leo, tarehe 28 hadi 30 Aprili 2025.

Huduma hizo, ambazo zitatolewa bure, zinalenga kupambana na kuikomboa jamii dhidi ya magonjwa hatari ya saratani kama vile saratani ya mlango wa kizazi, saratani ya tezi dume, saratani ya ngozi na aina nyinginezo. 

Zoezi hili ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha huduma za kibingwa zinawafikia wananchi wa maeneo ya vijijini bila gharama, huku pia likiwa na lengo la kutoa rufaa za moja kwa moja kwa wagonjwa wanaohitaji matibabu ya ngazi ya juu zaidi katika hospitali kubwa nchini.

Akizungumza na madaktari hao, Katibu Tawala wa Halmashauri ya Kilwa, Ndg. Yusuf Mwinyi, ametoa shukrani kwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa msukumo huo muhimu wa afya kwa wananchi. 

Amesisitiza kuwa msaada huo utawezesha jamii kupata huduma za kibingwa bila malipo, tofauti na hapo awali ambapo ilihitajika kuwa na  safari ndefu na gharama kubwa kupata huduma hizo. 

Ameahidi ushirikiano wa ofisi yake kuhakikisha wananchi wengi zaidi wanapata huduma hizo.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, Ndg. Hemedi Magaro, amewapongeza madaktari hao kwa kujitokeza kutoa huduma kwa wananchi wa Kilwa.

 Amewataka watumishi wa umma na wananchi wote wa Wilaya ya Kilwa kujitokeza kwa wingi kutumia fursa hiyo adhimu ya kupima afya zao bure. 

Aidha, ameeleza kuwa viongozi wa Wilaya wapo tayari kushirikiana kikamilifu na timu ya madaktari kuhakikisha zoezi hilo linafanikiwa kwa kiwango cha juu.

 

Share:

ELIMU YA GESI ASILIA KWENYE MAGARI YAWAVUTIA WENGI MAONESHO YA WIKI YA USALAMA MAHALA PA KAZI, SINGIDA.

Katika kuadhimisha Wiki ya Usalama Mahala pa Kazi, kampuni ya GASCO imeendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya matumizi salama na nafuu ya gesi asilia, hasa kwenye vyombo vya moto. 

Katika banda la GASCO, wananchi walijitokeza kwa wingi kujifunza zaidi kuhusu teknolojia ya kutumia Gesi Asilia iliyoshindiliwa (CNG) kama mbadala wa mafuta ya petroli na dizeli. 

Akizungumza mbele ya wageni mbalimbali waliotembelea banda hilo, Mhandisi Hassan Temba alifafanua faida nyingi za matumizi ya gesi asilia kwenye magari ikiwemo kuokoa gharama.

"Gesi asilia ni salama zaidi kwa mazingira, inapunguza gharama za uendeshaji wa magari kwa zaidi ya asilimia 50, na inapunguza uzalishaji wa gesi chafu kwa mazingira," alisema Temba. 

Aidha Temba, alisisitiza kuwa usalama wa matumizi ya gesi asilia umepewa kipaumbele, ambapo magari yanayofungwa mifumo ya gesi hupitia taratibu za ukaguzi wa kina na zinazozingatia viwango vya juu vya usalama vya kitaifa na kimataifa. 

Mhandisi Temba akitoa ufafanuzi  wa matumizi ya gesi kwenye magari kwa wannachi waliotembelea banda la GASCO

Wananchi wamehimizwa kutokuwa na hofu juu ya upatikanaji wa gesi asilia kwa magari yao, kwani TPDC imejipanga vizuri kuhakikisha huduma hii inapatikana kwa uhakika ikiwa ni pamoja na kushirikisha  sekta binafsi na taasisi nyingine ili kupanua mtandao wa vituo vya kujaza gesi nchini.

Katika hatua muhimu ya kuendeleza matumizi ya nishati safi na salama nchini, Afisa Maendeleo ya jamii Bw. Oscar Mwakasege ameeleza kuwa TPDC  imekamilisha ujenzi wa kituo mama cha gesi asilia eneo la Chuo kikuu Dar es salaam kwa ajili ya kuhakikisha upatikanaji wa gesi asilia kwa ajili ya matumizi ya vyombo vya moto.  

‘‘Kituo hiki kitaongeza unafuu kwa watumiaji hali itakayochochoea kukua kwa uchumi na kuongeza tija kwa wananchi katika sekta ya usafirishaji.

Kituo hicho chenye uwezo wa kuhudumia magari zaidi ya 1000 kwa siku na kusambaza bidhaa hiyo kwa vituo vingine ni dhahiri kitasaidia kupunguza kero waliyokuwa wanapata watumiaji wa vyombo vya moto. Ujenzi wa kituo hiki ni sehemu ya mkakati wa kitaifa wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi ikiwemo gesi asilia kama mbadala wa nishati ya mafuta. Alisema Oscar. 

Muonekano wa Kituo mama cha gesi asilia kwenye Vyombo vya moto, eneo la Chuo kikuu Dar es salaam.

 Hatua hii ni fursa kwa wananchi, wafanyabiashara, na sekta ya usafirishaji kupunguza gharama za uendeshaji na kuchangia katika kupunguza uchafuzi wa mazingira. 

Kwa sasa, TPDC inaendelea na ujenzi wa kuongeza idadi ya vituo vidogo vinavyopokea gesi kutoka kituo hiki mama na kusambaza kwa watumiaji katika maeneo mbalimbali ya mijini na pembezoni, hivyo kuongeza urahisi wa kupata huduma hiyo popote walipo.

Share:

WAZIRI KIKWETE AIPONGEZA BARRICK KWA MATUMIZI TEKNOLOJIA ZENYE USALAMA MIGODINI


Waziri wa Nchini Ofisi ya Waziri Mkuu (Ajira , Kazi na Watu wenye Ulemavu) Ridhiwani Kikwete akipata maelezo moja ya kifaa cha kukaa kinavyofanya kazi kwenye migodi ya Barrick North Mara
Mtaalamu wa Afya na Mazingira kutoka Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Aristides Medard (Kushoto) akifafanua jinsi mgodi huo wa Barrick unavyofanya shughuli za uchimbaji kwa kutumia teknolojia ya hali ya juu , vifaa na mitambo ya kisasa na akili mnemba kwa Waziri wa Nchini Ofisi ya Waziri Mkuu (Ajira, Kazi na Watu wenye Ulemavu) Ridhiwani Kikwete ambaye alikuwa Mgeni Rasmi wa Maonesho yanayoendelea na Afya na Usalama mahali pa kazi yanayoratibiwa na Wakala wa Afya na Usalama wa Mahali pa kazi (OSHA) katika viwanja vya Mandewa mjini Singida
Mrakibu Mwandamizi wa Usalama wa Mgodi wa North Mara, Bw. Meshack Issack (kushoto) akitoa maelezo na ufafanuzi kuhusu akili mnemba inavyotumika kwenye uchimbaji wa madini kwenye migodi ya Barrick kwa Waziri wa Nchini Ofisi ya Waziri Mkuu (Ajira , Kazi na Watu wenye Ulemavu) Ridhiwani Kikwete kwenye maonesho ya usalama mahali pa kazi yanayoendelea kwenye viwanja vya Mandewa mjini Singida

***
Waziri wa Nchini Ofisi ya Waziri Mkuu (Ajira, Kazi na Watu wenye Ulemavu) , Mhe Ridhiwani Kikwete ameipongeza migodi ya Barrick yenye ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga nchini kwa kuboresha utendaji kazi wake kwa kutumia Akili Mnemba (AI) na vifaa, mitambo ya kisasa ya kijiditali na kulinda usalama na afya za wafanyakazi wake mahali pa kazi.

Amesema hayo alipotembelea banda la Barrick kwenye maonesho ya OSHA yanayoendelea kwenye viwanja Mandewa mjini Singida na kusisitiza umuhimu wa kuweka mfumo madhubuti wa teknolojia ili kulinda afya za wafanyakazi kwenye sehemu zote za kazi kama vile migodi, viwandani na sehemu zingine.

“Huko nyuma mlikuwa mnakwenda wenyewe chini kwenye uchimbaji wa dhahabu chini ya ardhi lakini sasa mnatumia mitambo ili kuweza kufanikisha kazi hii, hongereni sana kwa kuboresha mazingira ya kufanyia kazi,” amesema Kikwete alipokuwa kwenye Banda la Barrick Bulyanhulu.

Mhe. Kikwete aliongeza kwamba juhudi za Barrick nchini kwa kushirikiana na Wakala wa Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA) zimefanikisha kuwepo mazingira rafiki ya ufanyaji kazi ambayo ni chachu katika kuleta mabadiliko Chanya katika sekta ya uchimbaji wa madini,

“Natoa wito kwamba elimu hii ya afya na usalama mahali pa kazi inayoendelea kutolewa kupitia maonesho haya iendelee kutolewa nchini nzima ili kupanua wigo wa uelewa kwa watanzania hasa wafanyakazi katika sekta mbalimbali hapa nchini katika kukabiliana na ajali na majanga sehemu za kazi,” amesisitiza.

Kwa upande wake, Aristides Medard, Mtaalam wa Afya na Mazingira kutoka mgodi wa Barrick Bulyanhulu amemweleza Waziri Kikwete na ujumbe wake kuwa kwa kutumia akili mnemba mgodi huo unaendesha shughuli zake kwa ufanisi na usalama zaidi hali ambayo inawapa motisha wafanyakazi kufanya kazi kutokana na mazingira kuwa rafiki.

Naye Mrakibu Mwandamizi wa Usalama, Bw. Meshack Issack kutoka Mgodi wa North Mara amesema mgodi huo ni kinara wa matumizi ya kidigitali na akili mnemba na mifumo ya kimataifa katika uchimbaji wa madini na afya na usalama nchini.

Ameongeza kwamba mgodi huo na migodi mingine yote ya Barrick inatekeleza program ya “Journey to Zero” ambayo inalenga kuhakikisha kila mfanyakazi anakuwa salama kazini hadi anaporudi nyumbani na kupaza sauti kunapokuwepo na viashiria vya mazingira hatarishi kwenye maeneo ya kazi.

“Hii programu ya “Journey to Zero” ni DNA ya kampuni inawahusu pia wakandarasi wa Barrick ,wageni wanaotembelea migodi yetu na jamii nzima kwa ujumla”, amesisitiza.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger