Sunday, 12 January 2025

KIRUSWA AWATAKA MALAIGWANANI KUKEMEA TABIA YA JAMII HIYO KATIKA CHAGUZI



NAIBU Waziri wa Madini na Mbunge wa Longido Mkoani Arusha,Dkt Steven Kiruswa amewataka viongozi wa Milla wa Jamii ya Kimasai maarufu kwa jina la Malaigwanani kukemea tabia ya jamii hiyo kutaka kuchagua viongozi wa kichama na kiserikali kwa kufuata makundi ya Uko na rika na kusema kuwa hiyo itawanyima watu demokrasia ya kuchagua viongozi bora na kutoa mwanya kuchaguliwa viongozi wasiokuwa bora na sifa na hivyo kusababisha makundi na migogoro ndani ya jamii.


Kiruswa alisema hayo wakati akizindua Baraza Kuu la Malaigwani la Wilaya ya Longido lililohudhuriwa na Malaigwanani zaidi ya 60. Viongozi wengine waliohudhuria ni pamoja na Mkuu wa wilaya ya Longido,Salum Kalli, Mwenyekiti wa Wilaya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Papa Nakuta, viongozi wastaafu wa chama na serikali wilaya na Mkoa akiwemo Lekule Laizer, Joseph Sadira na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Longido,Simon Oitesoi.

Alisema Malaigwanani ni kiungo muhimu kati ya serikali na jamii ya kifugaji katika suala la kuhamasisha maendeleo na wanatakiwa kuwa mstari wa mbele kukemea hilo kwani tabia hiyo ikijengeka itazaa viongozi wasiokuwa na sifa na kutapelekea kupata viongozi wasiostahili na kuwa chimbuko kwa jamii kukumbwa na migogoro ya mara kwa mara yanayotokana na makundi ya rika,uko na ukanda, kitu ambacho ni hatari kwa ujenzi wa jamii bora yenye mshikamano na umoja.

Alisema hilo lilijitokeza katika uchaguzi uliopita wa mwaka 2024 wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji wilayani Longido katika baadhi ya maeneo na kuwataka viongozi wa Milla kukemea hilo kwa nguvu zote lisijirudie katika chaguzi zijazo kwani linawagawa wananchi na kuathiri demokrasia kwa kuwa baadhi ya waliochaguliwa walipatikana kupitia mihemuko ya kirika na koo.

Naibu Waziri Kiruswa alisisitiza Malaigwanani kuhakikisha wanahimiza na kuhamashisha wananchi kushiriki kazi za maendeleo ikiwa ni pamoja na kupeleka watoto shule, kusimamia

Nyanda za malisho na kutoa elimu ya mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwa wao ni nguzo ya jamii ya kimasai na wanaheshimika katika jamii hivyo watumie nafasi hiyo kuiongoza vyema jamii na sio vinginevyo.

Alisema huu Mwaka ni mwaka wa uchaguzi Mkuu hivyo viongozi wa Milla wanawajibu wa kutoa elimu kwa jamii kuchagua viongozi bora na waadilifu wanaoweza kuongoza jamii kwa kuhamashisha na kufanya kazi za maendeleo kwani Malaigwanani ni kiungamishi cha serikali na jamii na wana wajibu huo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Longido,Salum Kalli alisema yeye ana miezi minne tu toka amehamia Longido na amepata ushirikiano mkubwa toka biongozi wa Milla hivyo kurahisisha kazi yake ya kusimamia ulinzi wa usalama wa raia na mali zao ndani ya wilaya.

Kalli alisema Malaigwanani wanawajibu wa kusimamia amani na mshikamano kwa kushirikiana na serikali na amewashukuru viongozi hao kuwajibika kwa hilo.

Mwenyekiti wa Baraza la Malaigwani Wilaya ya Longido, Laigwanani Simon Melau Ole Mepurda alisema kikao hicho ni muhimu kwa jamii hiyo kwani kimeshirikisha wajumbe kutoka katika kata zote 19 za jimbo la Longido na akasistiza kuwa baada ya Baraza kuzinduliwa wana wajibu wa kuelimisha jamii inayowazunguka kuheshimu sheria za nchi na milla ya jamii hiyo.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha wafugaji Wilayani Longido,Joseph Sadira aliwataka viongozi wa milla kuhimiza ufugaji bora na kuuza mifugo yao katika kiwanda cha nyama kilichopo Longido kwani ndio kiwanda kinachoingiza mapato katika Halmashauri ya Longido hivyo kinapaswa kuungwa mkoano na sio vinginevyo.


Share:

SIMBACHAWENE ATANGAZA UTARATIBU MPYA USAILI WA KADA ZA UALIMU KUANZIA JANUARI 14 HADI FEBRUARI 24

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. George Simbachawene leo amezungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, na kutangaza kuwa kuanzia tarehe 14 Januari hadi terehe 24 Februari, 2025, usaili wa kada za Ualimu utaendeshwa na Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais (UTUMISHI); Ofisi ya Rais (TAMISEMI); Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia; Wizara ya Afya; Tume ya Utumishi wa Walimu; Ofisi za Wakuu wa Mikoa yote na wataalamu mbalimbali kutoka katika Taasisi za Umma.



"Usaili huu una lengo la kujaza nafasi elfu kumi na nne mia sita na arobaini na nane (14,648) zilizotolewa na Mheshimiwa Rais kwa lengo la kupunguza uhaba wa walimu nchini.
 Ninapenda kuchukua nafasi hii kuwasihi sana wale wote walioitwa kwenye usaili wajiandae vyema kwa usaili huo kwani nafasi hizi ni za ushindani.

"Vilevile, kulingana na mahitaji yetu ya elimu kwa sasa, tutaajiri wataalamu wa fani za Amali. Hivyo, nawasihi sana wale wote watakaopata nafasi ya kuajiriwa, wawe tayari kujiendeleza ili kuweza kukidhi matakwa ya ajira zao katika Utumishi wa Umma." alisema Waziri Simbachawene.

Mhe. Simbachawene amesema kuwa usaili huu wa kada za Ualimu utafanyika katika Mkoa ambao kila msailiwa anaishi. Lengo kuu la utaratibu huu ni kuwapunguzia gharama za kusafiri na mambo mengine. Sekretarieti ya Ajira ilitoa matangazo kumtaka kila msailiwa kuhuisha taarifa zake katika akaunti yake ya Ajira Portal sehemu iliyoandikwa ‘current physical adress’ kwani ndipo tumewapangia vituo vya usaili kulingana na anuani walizojaza.

Aidha Mhe. Simbachawene amesema kuwa Usaili wa awali wa kuandika (Mchujo) kwa kada za Ualimu utafanyika kwa njia ya kuandika kwa mkono kwa kada zote na ngazi zote za elimu. 

"Ninapenda kuwakumbusha wale wote watakaokwenda kwenye usaili wahakikishe wanabeba vyeti vyao Halisi kikiwemo Cheti cha Taaluma na Cheti cha kuzaliwa. alisema Mhe. Simbachawene

Vilevile, wasailiwa wanapaswa kuja na namba zao za usaili walizotumiwa kwenye akaunti zao za ajira portal pamoja na kuzingatia Ratiba kama ilivyopangwa na Sekretarieti ya Ajira.

Kwa wale ambao kwenye vyeti vyao vya kitaaluma wanatumia majina mawili wakati kwenye cheti cha kuzaliwa na kitambulisho cha NIDA kuna majina matatu (3), au wale ambao majina yanatofautiana katika vyeti, wanapaswa kuwa na hati za kiapo (Affidavit au Deed Poll) ili kuthibitisha majina yao na vyeti husika.

Wasailiwa wanapaswa kuwa na kitambulisho halisi kwa ajili ya utambuzi, Kitambulisho kinachotambuliwa ni pamoja na Kitambulisho cha Taifa (NIDA); Hati ya Kusafiria; Leseni ya Udereva; Kitambulisho cha Mpiga Kura; Kitambulisho cha Mkaazi; Kitambulisho cha Kazi; au Barua ya Utambulisho kutoka ofisi ya Serikali ya Mtaa unaoishi au Shehia.

"Ninapenda kusisitiza kwamba ni muhimu sana msailiwa kuhakikisha anakwenda katika kituo alichopangwa kwa ajili ya usaili na si vinginevyo kwani mahitaji yake yatakuwa katika kituo alichopangwa." Alisema Mhe. Simbachawene. 

Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma ilianzishwa kwa mujibu wa Kifungu cha 29 (1) cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Sura ya 298 ambacho kinaelekeza kuwepo kwa chombo maalumu cha kushughulikia mchakato wa Ajira katika Utumishi wa Umma. Pamoja na Sheria hii kutungwa Mwaka 2007, Sekretarieti ya Ajira ilianza utekelezaji wa majukumu yake rasmi tarehe 01 Machi, 2010 baada ya maandalizi muhimu kukamilika. Aidha, iliweza kuendesha usaili wa kwanza Mwezi Juni, 2010.

Share:

Saturday, 11 January 2025

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JANUARI 12,2025

 

Magazetini
 
           
Share:

WAZIRI JAFO ATINGA ENGARUKA KUTANGAZA NEEMA KUTOKA KWA RAIS SAMIA



WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo,akizungumza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika leo Januari 10,2025 katika Kata ya Engaruka wilayani Monduli.

Na.Mwandishi Wetu

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Selemani Jafo,amesema Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 14.48 kwa ajili ya ulipaji wa fidia katika mradi wa magadi soda wa Engaruka ambapo shilingi billion 6.2 zitatumika katika ulipaji fidia kwa wananchi waliopisha mradi huo.


Waziri Jafo,ameyasema hayo leo Januari 10,2025 wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara katika Kata ya Engaruka wilayani Monduli.


Amesema kuwa wananchi 595 kutoka vijiji vinne vya Engaruka Chini, Mbaash, Idonyonado na Irerendeni watanufaika na fidia hiyo ya shilingi bilioni 6.2 huku fedha zingine zilizobaki zikienda katika shughuli mbalimbali za miradi mbalimbali ya huduma za kijamii.


Katika mkutano huo, Dkt. Jafo amewapa habari njema wananchi wa Kata hiyo ya Engaruka kwamba Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan tayari ameshatoa pesa za kuwalipa fidia wananchi hao watakaopisha mradi.


"Mradi huo tayari umetangazwa kwa lengo la kutafuta wawekezaji ambapo hadi sasa Makampuni kadhaa tayari wameonyesha nia ya kuwekeza kwenye mradi huu".amesema Dkt.Jafo


Aidha Dkt. Jafo amesema fedha hizo zimetolewa na Serikali ikiwa ni mkakati wa kuendeleza miradi ya kimkakati yenye tija kwa Taifa.


Dkt. Jafo mradi huo ni muhimu sana kwa uchumi wa Taifa kwani Viwanda vingi nchini vinatumia magadi soda kama malighafi muhimu vikiwemo viwanda vya kutengeneza vioo, sabuni, nguo, nk.


Aidha, Dkt. Jafo amesema kwamba mradi huo utasaidia sana kuokoa matumizi ya fedha za kigeni ambazo kwasasa zinatumia kuagiza Magadi soda kutoka nje ya nchi.


Katika kuweka msisitozo, Jafo amewashauri wananchi hao kuanza kufikiria kujenga hotel na nyumba za kulala Wageni na kubuni biashara mbalimbali za huduma kwani eneo hilo litafikiwa na wageni wengi wanaokuja kufanya kazi katika viwanda vitakavyojengwa eneo hilo.


Naye Naibu Waziri wa Madini, Mhe.Dkt.Stephen Kiruswa amesema mradi huo uwe ni chimbuko la mafanikio kwa wananchi wa wilaya ya Monduli na Longido kwani mradi huu ni mkubwa na unatija Kwa wananchi.
 
Share:

SERIKALI YASISITIZA UMUHIMU WA MAFUNZO YA UFUATILIAJI NA TATHIMINI KWA MAENDELEO YA MIRADI YA SERIKALI





Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) imezitaka halmashauri, taasisi, na wadau mbalimbali wanaonufaika na mafunzo ya ufuatiliaji na tathmini kutumia vyema fursa hizo. Imepongeza ushirikiano uliopo baina ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, ambacho kimeendelea kutoa mafunzo wakishirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu ili kuongeza ufanisi wa kufuatilia na kusimamia maendeleo ya miradi ya serikali.


Kauli hiyo imetolewa leo Januari 10, 2024, na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Ufuatiliaji na Tathmini kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, na Uratibu, John Bosco Quman, wakati wa kufunga mafunzo ya uelewa kwa watumishi wa serikali ngazi ya halmashauri. Quman amehimiza washiriki kushiriki kikamilifu hatua zote tatu za mafunzo ili kuimarisha usimamizi na utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Aidha amekipongeza Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, Quman amesema chuo hicho kimefanya kazi nzuri katika kutoa mafunzo ya ufuatiliaji na tathmini, bila malalamiko yoyote kuhusu utekelezaji wa mpango huo unaosimamiwa na serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu.

Kwa upande wake, mwezeshaji wa mafunzo hayo kutoka Chuo Kikuu Huria, amesema mpango huo unalenga kuwajengea uwezo wafanyakazi wa serikali. Hadi sasa, mikoa yote nchini imefaidika na mafunzo hayo katika ngazi ya kwanza. Ameongeza kuwa washiriki 67 kutoka halmashauri mbalimbali wamepata maarifa ya kutafsiri miongozo, kusimamia utekelezaji wa miradi, na kuandaa miongozo inayosaidia kutatua changamoto za kijamii katika mafunzo yaliyotolewa Mkoani Morogoro .

Naye, Caroline Marila, mshiriki wa mafunzo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa, amesema mafunzo hayo yataboresha utekelezaji wa miradi ya serikali na usimamizi wa rasilimali fedha, hivyo kuleta mabadiliko chanya katika utoaji wa huduma kwa jamii.

Mafunzo haya, yaliyoanzishwa na serikali kupitia Chuo Kikuu Huria cha Tanzania, yalianza mwaka 2024 kwa lengo la kuwajengea uwezo watumishi wa umma katika kufuatilia na kutathmini miradi ya maendeleo ili kuongeza uwajibikaji na ufanisi wa matumizi ya rasilimali.



Share:

Friday, 10 January 2025

WAZIRI BASHUNGWA AZINDUA MIKAKATI SITA YA MAWASILIANO KUONGEZA TIJA KWENYE UTENDAJI KAZI



Na Dotto Kwilasa, Dodoma. 

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Innocent Bashungwa amewaelekeza wasemaji wa vyombo vya usalama na wakuu wa vitengo vya habari na mahusiano  kufanya tathmini ya pamoja ya utendaji kazi wa vitengo vya habari katika Wizara na vitengo vyake vya usalama kwa kuzingatia mpango kazi unaosomana.

Bashungwa ameeleza hayo Januari 9,2025 Jijini Dodoma wakati akizindua mikakati Sita itakayotekelezwa  ili kuweze kutimiza lengo na kuimarisha nguvu za kiutendaji na kueleza kuwa  kuzinduliwa kwa mikakati hiyo kunapaswa kuwa chachu ya kuitekeleza kwa ufanisi ili ilete tija kwa Wizara kwani itasaida kuimarisha suala la Mawasiliano kwa umma.

"Hakikishe kuwa vitengo vyetu vya habari vinatengewa bajeti ili viweze kutelekeza mikakati hii ya mawasiliano kwani inaleta tija na mabadiliko chanya kwenye kuwahudumia watanzania,"amesema. 

Amesema miongoni mwa malengo ya kuangaliwa kwenye mikakati hiyo ya mawasiliano ni kuongeza uelewa na ushiriki wa jamii kwenye kuimarisha usalama wa raia na mali zao sambamba na utunzaji wa amani na utulivu wa nchi. 

Naye Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Daniel Sillo amewahasa washirki kikao kazi cha mwaka cha wasemaji wa vyombo vya usalama na maafisa habari, Mawasiliano na uhusiano wa Wizara hiyo kutumia jukaa hilo kijtathmini walipotoka, walipo na wanakoeleea ili kwa pamoja waweze kupata uzoefu ambao utasaidia kuimarisha sekta ya habari kwa maslahi ya wananchi na taifa kwa ujumla. 

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi Ally Gugu amesena mikakati hiyo inasaidia kuboresha upatikanaji wa habari ambayo ndiyo lengo la Serikali ya awamu ya sita ili kuiwezesha jamii kupata taarifa kwa wakati ambapo ni mapendekezo ya tume ya haki jinai.

"Katika kutekeleza maelekezo ya Serikali Wizara yetu imeanza na uandaaji wa mikakati hii ya mawasiliano ambayo imezinduliwa leo na baada ya hapo tutaenda kuitekeleza kwa vitendo na kwakuwa zipo shughuli mbalimbali ambazo zimepangwa kutekelezwa kwa miaka miwili na baada ya hapo tumepanga kufanya mapitio ili kuona hatua mbalimbali za utekelezaji wa mikakati hiyo, "amesema. 

Awali akitoa taarifa kuhusu mikakati hiyo Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini  Christina Mwangosi amesema mikakati hiyo imeandaliwa kwa kuzingatia miongozo ya Wizara, vyombo ya usalama pamoja na mkataba wahuduma kwa wateja.

"Mikakato hii ni ya miaka mwili na baada ya hapo tutafanya tathmini ya matokeo yatakayokuwa yamepatikana na ndipo tutaanza tena mikakati mingine kulingana na matokeo yatakayokuwa yamepatikana,"amesema.

Hata hivyo Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi imezindua Mikakati Sita ya mawasiliano yenye lengo la kuimarisha upatikanaji wa huduma kwa urahisi kwenda kwa wananchi. 



Share:

USIKU WA WADAU SHUPAVU SHINYANGA KUKUTANISHA VIONGOZI NA WADAU MASHUHURI

 


HolySmile Chini ya Mkurugenzi wake Arnold Bweichum inawaletea hafla ya kipekee inayokusanya wadau mashuhuri kutoka sekta mbalimbali – viongozi wa serikali, wawekezaji, wajasiriamali, wasanii, na wanaharakati wa maendeleo Usiku wa Wadau Shinyanga! Hii ni fursa adhimu ya kusherehekea juhudi na mafanikio ya wale walio mstari wa mbele kuboresha maisha ya wakazi wa Shinyanga.

📅 Tarehe: 1 Februari 2025

📍 Mahali: Ukumbi wa Makindo, Shinyanga

⏰ Saa: 12:00 jioni – 6:00 usiku

Hafla hii itakuwa na hadhi ya kipekee na kuwakutanisha watu mashuhuri wa kada na idara zote – sekta ya afya, elimu, kilimo, biashara, teknolojia, utalii, na sanaa.

Kutakuwa na; 

1. Tuzo za Heshima na Pongezi: Kuwatambua na kuwapongeza wadau shupavu kwa mchango wao mkubwa.

2. Mahusiano ya Kibiashara (Networking): Kukutana na kushirikiana na watu wa maana kwa maendeleo binafsi na ya jamii.

3. Chakula cha jioni na burudani za kiwango cha juu: Furahia usiku wa heshima na burudani za kipekee kutoka kwa wasanii maarufu.

4. Nafasi ya kutangaza chapa yako: Weka chapa yako mbele ya viongozi na mashujaa wa maendeleo.

KIINGILIO

1. VIP Single: TZS 50,000

2. VVIP Single: TZS 100,000

3. Meza ya VVIP (Watu 5): TZS 500,000

4. Meza ya VVIP (Watu 12): TZS 1,000,000


NJIA ZA MALIPO:

✅ Voda Lipa Namba: 57845152

✅ Akaunti ya NMB: 30610057561

(Jina: HOLYSMILE)


MAWASILIANO

📞 Simu: 0756254146

Hii ni nafasi yako kushiriki tukio kubwa la kihistoria, lenye heshima na hadhi ya dhahabu. HolySmile, chini ya uratibu wangu kama Mkurugenzi, inahakikisha tukio hili linakuwa alama ya kumbukumbu kwa Shinyanga na Tanzania kwa ujumla.

Tukutane Usiku wa Wadau Shinyanga – mahali ambapo heshima, mshikamano, na maendeleo vinakutana!

Share:

Thursday, 9 January 2025

WAZIRI KOMBO AAGANA NA BALOZI WA MAREKANI


Tanzania itaendelea kutoa ushirikiano kwa Ubalozi wa Marekani nchini na kuahidi kumpatia ushirikiano wa karibu Balozi ajaye katika utekelezaji wa majukumu yake awapo Tanzania pamoja na kuangazia maeneo ya kuongeza wigo wa ushirikiano kwa manufaa ya nchi zote mbili.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, akimuaga Balozi wa Marekani nchini, Mhe. Michael Battle anayetarajiwa kuondoka nchini hivi karibuni.

Waziri Kombo amemshukuru Balozi Battle kwa ushirikiano mzuri kati ya wizara na ubalozi katika kipindi chote cha uongozi wake pamoja na kufanya kazi kwa karibu na sekta na wizara mbalimbali za kimaendeleo nchini.

Aidha, ametumia fursa hii kutoa salamu za pole kwa msiba wa Rais Mstaafu wa Marekani, Hayati Jimmy Carter aliyefariki Dunia Desemba 29, 2024.

Kwa upande wake, Balozi Battle amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa dhamira yake katika kuleta maendeleo Tanzania lakini pia kwa utayari wake katika shughuli za ushirikiano.

Ameomba pia Wizara kumpa ushirikiano wa karibu Kaimu Balozi atayekuwepo wakati Marekani ikingoja kutuma Balozi mwingine.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger