Saturday 14 September 2024

WATAFITI WATAKIWA KUTAFSIRI KWA LUGHA RAHISI MATOKEO YA TAFITI ZAO KUHUSU MTO MARA

 
Na Mwandishi Wetu-  Narok Kenya
Wanasayansi na watafiti wanaofanya tafiti kuhusu faida za uhifadhi wa bonde la mto Mara wametakiwa kutafsiri kwa lugha rahisi matokeo ya tafiti zao ili ziweze kueleweka  kwa jamii husika hatua ambayo itakuwa na mchango chanya kwenye uhifadhi wa bonde hilo.

Akizungumza kwenye kongamano la pili la  wanasayansi leo Septemba 14,2024 katika Kaunti ya Narok nchini Kenya kujadili utunzaji wa bonde la mto Mara ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya Mara,Profesa Patrick Lumumba kutoka chuo Kikuu cha Nairobi amesema matokeo ya tafiti nyingi yameandikwa kwa lugha ngumu ambazo hazieleweki hasa kwa jamii zinazozunguka bonde la mto huo.

Amesema Bonde la Mto Mara linakabiliwa na changamoto kubwa za uharibifu wa mzingira pamoja na mabadiliko ya tabia nchi na kwamba ili changamoto hizo ziweze kupatiwa ufumbuzi wa kudumu suala la ushiriki wa  jamii ni la muhimu.

"Ni lazima tuwe na maneno ya kueleweka,tuwe na misamiati inayotamkwa na kueleweka katika mitaa na vijiji vinavyozunguka bonde,tutafsiri  manneo magumu hata kwa kilugha cha jamii husika ili yaeleweke  kuna maneno mengi mfano neno baianua, ikolojia, na mengine mengi," amesema .

Amesema wananchi wakielewa kwa kina madhara na nini cha kufanya kwaajili ya ulinzi wa bonde hilo upo uwezekano mkubwa wa wao kushiriki kwa  kiwango kikubwa katika ulinzi wa bonde hilo hivyo kuwa  na matokeo chanya.

Profesa Lumumba amesema  mamlaka husika pia zinatakiwa kujihoji kama zinafanya wajibu wao kikamilifu katika ulinzi wa bonde hilo kufuatia uwepo wa shughuli za kibinadamu zinazotishia  uhai wa bonde la mto Mara. 

"Tujihoji kabla ya kutoa vibali vya uwepo wa viwanda na hata kufanya utafiti kujiridhisha juu ya viatilifu vinavyotumika kwenye kilimo kando ya bonde hilo kama vitu hivyo ni rafiki  kwa uhai wa bonde na hili linapaswa kufanywa kwa pamoja  baina ya nchi zetu mbili yaani Kenya na Tanzania na Afrika Msahariki jwa ujumla," ameongeza 


Mkuu wa mkoa wa Mara, Evans Mtambi amesema jukumu la ulinzi wa rasilimali hiyo ni la kila mdau hivyo suala utekelezaji  wa makubaliano ya midahalo ya wanasayansi ambayo imeanza kufanyika mwaka jana inatakiwa kusimamiwa na kutekelezwa kwa pamoja.

"Kesho ya bonde la mto Mara iko kwenye mikono yetu,na hili linawezekana tukiamua kwani tuna wajibu wa pamoja wa kulinda ustawi na uendelevu wa bonde hili kwa manufaa ya watu wetu kutoka nchi zote mbili," amesema Mtambi

Mtambi amesema madhara ya mabadiliko ya tabia nchi na shughuli za kibinadamu ni katoka bonde hilo makubwa lakini  yanaweza kuepukika endapo ushauri wa tafiti za kisasanysi zilizowasilishwa  utafanyiwa kazi kwa pamoja na kwa wakati.


Amesema serikali mkoani Mara itahahkilisha inashirikiana na wanachi na wadau wengine katika ulinzi  bonde hilo kwa maelezo kuwa uharibifu wa mazingira kwa ujumla ni  sawa na hukumu ya kifo kwa kizazi kijacho.


Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Bonde la ziwa Victoria,  Dk Masinde Bwire amesema ustawi wa  bonde la mto Mara  una mchango wa moja kwa moja kwa uchumi wa watu na uendelevu wa sekta ya utalii kwa nchi zote  zote mbili.

Amesema changamoto zinazokabili bonde hilo zinapaswa kujadiliwa kwa pamoja kwa kushirikisha watafiti, watunga sera pamoja watejelezaji na wadau wote kushiriki ili kuja na makubaliano ya pamoja juu ya namna ya ulinzi wa bonde hilo.

"Bonde la mto Mara sio rasilimali muhimu kwa ikolojia pekee bali  pia ni nguzo muhimu ya kiuchumi kwa mamilioni ya watu wa nchi zetu wanaolitegemea kama rasilimali muhimu katika maisha yao hivyo ulinzi wake ni jambo la lazima," amesema Dk Bwire


Akiwasilisha mada katika kongamano hilo, Brian Ndungu kutoka Chuo Kikuu cha Maasai Mara amesema bonde la mto Mara linakabiliwa na changamoto kubwa ya uharibifu wa mazingira kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo kutokuwepo kwa mikakati ya kutosha ya utunzaji wa mazingira ya bonde  pamoja na ushiriki hafifu wa wadau.

Amesema changamoto hizo zinahusu  uharibifu wa uoto wa asili katika bonde hilo unaofanywa kwa upande wa Tanzania na Kenya pamoja na changamoto ya mabadiliko ya tabia nchi mambo ambayo yanahitaji ushiriki wa pamoja kutoka kwa wadau wote.
   



Share:

Video Mpya : SURA YA KAZI - MBINA

 

Share:

Friday 13 September 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 14,2024

Share:

BoT, AZAKI WAJADILI KUBORESHA HUDUMA JUMUISHI ZA FEDHA KWA JAMII


Mchambzi Mwandamizi wa Masuala ya Fedha, Idara ya Huduma Jumuishi za Fedha, Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dastan Massawe, Akizungumza katika mdahalo wa kujadili Biashara Jumuishi kati ya Sekta Binafsi na Asasi za Kiraia uliofanyika leo Septemba 12, 2024 Jijini Arusha.
 
Mkuu wa Programu kutoka Shirika la Foundation For Civil Society (FCS) Nasim Losai,akizungumza alipokuwa akitoa maelezo ya awali kuhusu mdahalo huo.

Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano (TCRA - CCC) Mary Msuya, (kulia), akizungumza namna taasisi yao inavyotekeleza majukumu yake kwa mujibu wa sheria.

PICHA NA; FCS Na; Hughes Dugilo, ARUSHA

Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imesema itaendelea kufanya jitihada mbalimbali za kusaidia ukuaji wa huduma za malipo kidigitali kwa kuweka miundombinu rafiki ili kuhakikisha inamlinda mwananchi katika shughuli za uchumi ikiwemo kuwa na unafuu wa kutuma miamala ya fedha.

Akizungumza Jijini Arusha katika mdahalo wa kujadili Biashara Jumuishi kati ya Sekta Binafsi na Asasi za Kiraia, Mchambzi Mwandamizi wa Masuala ya Fedha, Idara ya Huduma Jumuishi za Fedha, Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Dastan Massawe, amesema kuwa Benki hiyo inatambua umuhimu wa huduma za fedha kama chachu ya ukuaji wa biashara na uchumi nchini.

Massawe amesema BoT inaendelea na jitihada za kuwezesha biashara ya ndani na nje ya nchi pamoja na kuangalia usalama wa fedha ili kuondokana na changamoto zinazojitokeza ikiwemo uwepo wa matapeli mtandaoni.

Amesema kuna sera wezeshi ambazo haziingiliani na sera nyingine zenye ubunifu katika mifumo inayoimarisha usalama wa miamala baina ya wafanyabiashara mbalimbali.

“Wafanyabiashara wengi bado hawajafikiwa na huduma rasmi za kifedha, asilimia kubwa wanafanya biashara nje ya mifumo, hivyo kuwakosesha fursa ya kupata mitaji” Amesema Massawe.

Kwa upande wake Mkuu wa Programu kutoka Shirika la Foundation For Civil Society (FCS) Nasim Losai, amesema kuwa Shirika hilo linatekeleza mradi wa miaka mitatu wenye lengo la kuyawezesha makundi matatu ambayo ni wanawake, vijana na watu wenye ulemavu ili kuwajengea uelewa mpana wa kuzitambua haki zao za msingi za masuala ya biashara na fedha.

"Kuna fursa na faida nyingi ambazo watu wanazipata lakini sio makundi yote ambayo wanaweza kupata, ndiomaana FCS tumekuja na mradi huu ili kuyafika makundi yote” Amesema Lasai.

Akizungumza katika mdahalo huo, Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Mawasiliano (TCRA - CCC) Mary Msuya, amesema kuwa matumizi ya teknolojia yamerahisisha huduma jumuishi za fedha kupitia miamala ya simu tofauti na ilivyokuwa awali.

Msuya amesema kuwa kwa mujibu wa takwimu zilizotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Juni 2024 zinaonesha kuna laini za simu milioni 76.6 zinazotumika, ambapo akaunti za fedha kwa njia ya ni simu milioni 55.7, huku watumiaji wa huduma ya internet wakiwa milioni 39.3.

Amesisitiza kuzingatia umuhimu wa kutoa na kulinda taarifa binafsi kwa watoa huduma za fedha wakati wa kujisajili, kwani baadhi yao wamekuwa sio waaminifu katika utekelezaji wa zoezi hilo.

Naye mwakilishi wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Perodius Makubi, amesema licha ya faida zinazopatikana katika biashara za mtandaoni kuna madhara ambayo yanajitokeza ikiwemo baadhi wa watu kwenda kinyume na malengo yaliyokusudiwa na kuleta usumbufu kwa wengine.
Share:

Thursday 12 September 2024

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA SEPTEMBA 13, 2024

Share:

HAKIELIMU YAZINDUA MRADI WA MAJARIBIO KUWEZESHA WALIMU KUFUNDISHA KWA VITENDO


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la HakiElimu Tanzania limezindua mradi wa majaribio ambao umelenga kukuza ufundishaji wa walimu,kupitia teknolojia ambayo itamwezesha Mwanafunzi kupata picha halisi ya kitu anachofundishwa.

Akizungumza leo Septemba 12,2024 Jijini Dar es salaam Mkuu wa Programu Shirika la HakiElimu Bw.Godfrey Boniventura wakati wa uzinduzi wa mradi huo amesema kuwa mradi huo umekusudia kumfundisha mwanafunzi kwa vitendo na sio nadharia pekee ambapo wanafunzi watafundishwa kwa kutumia vitu katika picha na maumbo yake halisi.

"Hata kama unataka kumfundisha mtu awe makenika (fundi wa gari) labda kufunga mguu wa gari(shock up) unamfundisha kwa maumbo halisi na kumuonesha inapofungwa ambapo anapata picha halisi kwa namna ya kufanya". Amesema.

Aidha Boniventura amesema baada ya mradi huo wa majaribio kukamilika wanatarajia kutanua wigo kwa kushirikisha taasisi mbalimbali za elimu nchini.

Aidha Boniventura amesema Taasisi ya Hamk ,Save the Children na taasisi 5 za kitaaluma zimeshiriki katika kuhakikisha utekelezaji mzuri wa mradi huo wa majaribio ili kufikia malengo yaliyokusudiwa ambapo itakuwa njia nzuri ya kupima ufanisi na umuhimu wake katika mazingira ya Kitanzania.

Kwa upande wake kutoka Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Dkt. Abdalah Ngodu ametoa shukrani zake kwa waandaaji wa mradi huo ambapo anatarajia kuona ubunifu na mipango yenye matokeo kwenye maisha ya wanafunzi kwa kuzalisha ujuzi wenye kuleta tija kwa jamii.

Aidha amesema kuwa ukuaji wa kasi wa teknolojia,unachangia uhitaji wa zana za kisasa kama teknolojia ya VR na XR ambao pia ni sehemu ya maudhui ya mradi huo ambapo inatoa mwanya kwa wakufunzi na wanafunzi kujifunza mtandaoni kwa pamoja kabla ya kufanya vitendo katika ulimwengu halisi.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mafunzo ya Amali (VTA), Dkt. Bakari Ali Silima amesema uingizwaji wa mfumo wa kidijitali wa maudhui ya mafunzo katika teknolojia ya vipimo vitatu na matumizi ya miundombinu ya TEHAMA, kutawezesha kutumia mwalimu mmoja kutoa mafunzo kwa wanafunzi wengi katika maeneo tofauti kwa wakati mmoja.

Mradi huo wa majaribio unatarajiwa kufanyika kwa miaka miwili ambapo umefadhiliwa na kampuni ya 3D BEAR na kuratibiwa nchini na Chuo kikuu Cha Hamk,Shirika la Save The Children,HakiElimu pamoja na vyuo vikuu Vitano.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger