Sunday, 30 July 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JULAI 31,2023































Share:

GGML YATOA MSAADA WA MADAWATI 8,823 MKOANI GEITA


Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Terry Strong (kulia) akimkabidhi Mkuu wa mkoa wa Geita, Martin Shigela baadhi ya madawati hayo. Kushoto kwa mkuu huyo wa mkoa ni Mkuu wa wilaya ya Geita, Cornel Maghembe.
Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Terry Strong, Mkuu wa mkoa wa Geita, Martin Shigela baadhi ya viongozi wengine wa mkoa huo, wakiwa wamekaa katika madawati hayo pamoja na wanafunzi mkoa huo kama ishara ya furaha ya makabidhiano ya madawati kwa shule mbalimbali za Geita.
Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Terry Strong akizungumza katika hafla hiyo ya makabidhiano ya madawati kwa shule mbalimbali za Geita.

NA MWANDISHI WETU

KATIKA kutimiza dhamira ya kuimarisha sekta ya elimu na kuwezesha mazingira ya utoaji elimu nchini kuwa ya usawa, Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa msaada wa madawati 8,823 kwa shule mbalimbali za Geita ili kuweka mazingira mazuri ya kujifunzia kwa wanafunzi wa mkoa huo.

 

Katika hafla ya makabidhiano hayo iliyofanyika juzi Mjini Geita kwa ushirikiano na mamlaka za serikali za mitaa kupitia mpango wa GGML wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR), Mkuu wa Mkoa wa Geita, Martin Shigella, aliishukuru kampuni hiyo kwa kuwa msaada huo umekuja wakati muafaka.

 

Alisema kadiri shule nyingi zinavyoendelea kujengwa ndivyo hitaji la madawati linavyozidi kuonekana jambo ambalo GGML inajitahidi kutatua changamoto hiyo.

 

Shigella alipongeza GGML kwa kuwa na mipango ya muda mrefu ya kuinua sekta ya elimu mkoani Geita na Tanzania nzima kwa ujumla.

 

"Ni furaha yangu kwamba tangu GGML ianze shughuli za uchimbaji hapa mkoani Geita, imekuwa ikishirikiana kwa karibu na Serikali kutekeleza miradi kadhaa ya elimu, hasa ujenzi wa madarasa na shule".

 

Mkuu huyo wa mkoa alikiri kuwepo kwa uhaba wa madawati katika shule mbalimbali hivyo kuwaomba wadau wengine mkoani humo kufuata nyayo za GGML katika kuboresha mazingira ya kujisomea kwa wanafunzi.

 

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Terry Strong, alisema ni muhimu kuboresha mazingira ya utoaji elimu nchini ili kufikia lengo namba 4 la Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa.

 

"Kutoa elimu bora kwa wote ni msingi wa kujenga dunia yenye amani na ustawi. Elimu huwapa watu maarifa na ujuzi wanaohitaji ili kuwa na afya njema, kupata ajira. GGML inafurahi kuboresha maisha ya Watanzania katika sekta mbalimbali ikiwemo sekta ya elimu," alisema.

 

Akielezea malengo ya GGML katika kuboresha maisha ya Watanzania hususani kupitia uboreshaji wa sekta ya elimu, Strong alieleza kuwa tangu kuanzishwa kwa kampuni hiyo mwaka wa 2000, GGML imeendelea kuwekeza katika nyanja mbalimbali zinazoboresha maisha ya jamii nzima ya Geita na Tanzania kwa ujumla.

 

Alisema GGML imewekeza kwa kuzingatia masuala muhimu kama vile afya, elimu, maji, barabara na miradi ya kuzalisha kipato cha kaya na kukuza uchumi wa Taifa.

 

"GGML imewekeza katika utekelezaji wa miradi endelevu ambayo inainufaisha jamii inayouzunguka mgodi. Kwa hiyo mchango huu wa madawati unadhihirisha jukumu la GGML kama mwananchi anayehitaji elimu bora kubadilisha maisha yake," alisema na kuongeza;

 

"Juhudi za GGML kujitolea kutekeleza miradi mbalimbali zinaendelea kuacha alama isiyofutika na kusaidia kuboresha maisha ya jamii kupitia uwepo wa kampuni hii mkoani Geita."


Share:

ORYX GAS YATOA MITUNGI 500, MAJIKO YAKE KWA MAMA LISHE ILEMELA

Meneja Masoko wa Kampuni ya Oryx Gas Tanzania Peter Ndomba akitoa elimu ya matumizi salama ya mtungi wa gesi ya Oryx kabla ya mitungi hiyo kukabidhiwa kwa wanawake wajasiriamali wilayani Ilemela mkoani Mwanza.

***************

Na Mwandishi Wetu, Mwanza

MKURUGENZI Mtendaji wa Kampuni ya Oryx Gas Tanzania Araman Benoite, amesema kaampuni hiyo imegawa bure mitungi ya gesi 500 pamoja na majiko yake kwa mamalishe wilayani Ilemela, kuunga mkono juhudi za Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Oryx Gas imegawa mitungi na majiko hayo jana kwa wanawake wajasiriamali wa Mama Lishe waliopo katika Kata 19 za Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza, kuwaongezea nguvu katika shughuli zao na kuzifanya kisasa.

Akizungumza mbele ya viongozi wa Wilaya ya Ilemela wakiongozwa na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk. Angelina Mabulla, Benoite amesema kuwa wameendelea kuunga mkono juhudi za serikali katika kulinda na kutunza mazingira kwa kuhamasisha nishati safi ya kupikia.

“Katika mwendelezo huo wa kuhimiza matumizi ya nishati safi na salama kwa kupikia, Kampuni ya Oryx Gas Tanzania Limited imekuwa mstari wa mbele kufikia azma hiyo, leo (jana) kampuni yetu imevitupia macho vikundi vya wafanyabiashara wa vyakula (Mama Lishe) wilayani Ilemela kwa kuwakabidhi bure mitungi 500 ikiwa na gesi yake.

“Utoaji huu wa mitungi ya Oryx umefanikiwa kwa ushirikiano mkubwa kutoka kwa Waziri wa Dk. Mabula. Malengo ya kampuni ni kuona mabadiliko katika matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia kwa jamii zote za Watanzania,” amesema.

Aliongeza kuwa hatua hiyo inaendana na mpango wa serikali wa miaka 10 wa matumizi salama ya nishati safi ya kupikia huku akifafanua wanafahamu kundi la Mama Lishe kila siku linahudumia chakula kwa wananchi lakini wengi wao wameathirika kwa namna mbalimbali kutokana na matumizi ya kuni na mkaa.

“Mwanza na mikoa ya Kanda ya ziwa imeharibiwa kwa kiasi kikubwa na ukataji miti kwa matumizi ya kuqndaa chakula, hivyo juhudi kubwa inahitajika kulinda afya na kuokoa mazingira ya ukanda huu na maeneo mengine nchini,” Amesema.

Aliongeza Oryx Gas inawekeza katika siku zijazo kwa kutekeleza mipango ya kukabiliana na kaboni kupitia elimu ya upishi safi, uchangiaji wa vifaa vya kuanzisha LPG bila malipo kwa baadhi ya mikoa, uhamasishaji wa matumizi ya LPG kupitia uuzaji mkubwa wa mitungi ya gesi kwa bei nafuu.

WAZIRI DK. MABULA APONGEZA

Kwa upande wake Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk. Angelina Mabulla amesema hatua ya Kampuni ya Oryx Gas kutoa hamasa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia inapaswa kuungwa mkono kwa inaisadia serikali kuhanasisha utunzaji mazingira nchini

Dk. Mabula akizungumza katika hafla ya kukabidhi majiko hayo, Ilemela jijini Mwanza, Waziri Dk. Mabula ambaye pia ni Mbunge wa Ilemela amesema yatagawanywa katika kata zote 19 za wilaya hiyo kulingana na shughuli zinazofanywa na Mamalishe wilayani humo.

“Tunaona namna ambavyo akinamama wanapata shida katika kutekeleza shughuli zao kwa haraka, katika mazingira mazuri, lakini tunahitaji kutunza mazingira yetu. Rais Dk. Samia Suluhu Hassan amedhamiria kuhakikisha huduma zote anazotoa kaanzia kwenye huduma za uchumi, kaja kwenye elimu lakini uwekezaji ameupa kipaumbele.

“Ukija katika huduma za jamii akina mama wengi wamekuwa wakihanagika kutafuta kuni na mkaa, wanakwenda kufyeka misitu.Tumetajiwa hadi kiwango cha uharibifu ambacho kimefanyika. Sasa tunapopata kampuni kama hizi ambazo ziko tayari kuwekeza katika afya na utunzaji bora wa mazingira yetu, lazima tuwashukuru,” ameema.


Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ilemela mkoani Mwanza (kulia) akijadiliana jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Oryx Gas Tanzania Araman Benoite.

Mkurugenzi Mtendaji wa Oryx Gas Tanzania Araman Benoite akizungumza wakati wa tukio la ugawaji mitungi ya gesi 500 pamoja na majiko yake kwa Mama Lishe waliopo katika Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza



Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JULAI 30,2023















Share:

Saturday, 29 July 2023

Tazama Picha : MWENGE WA UHURU UKITOKA SHINYANGA MJINI

Tazama picha Mwenge wa Uhuru ukitoka Halmashauri ya Manispaa ya Shinyanga kwenda Halmashauri ya Shinyanga leo Jumamosi Julai 29,2023 - Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger