Tuesday, 25 July 2023

DC SAMIZI AWATAKA WATANZANIA KUWAENZI MASHUJAA KWA KULIPIGANIA TAIFA NA KUDUMISHA AMANI


Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi akipokea Silaha za Jadi ambazo zilitumika na Mashujaa katika kupigania uhuru wa nchi.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi akiweka silaha za Jadi katika Mnara wa Mashujaa.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi akipiga picha kwenye Mnara wa Mashujaa.

Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko akipokea silaha za Jadi kwa ajili ya kuweka kwenye Mnara wa Mashujaa.
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko akienda kuweka silaha za Jadi kwenye Mnara wa Mashujaa.
Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko akiweka Silaha za Jadi kwenye Mnara wa Makumbusho wa Mashujaa.
Chief Kidola Njange akiweka Silaha  za Jadi kwenye Mnara wa Makumbusho wa Mashujaa.
Silaha za Jadi zikiendelea kuwekwa kwenye Mnara wa Mashujaa.
Silaha za Jadi zikiendelea kuwekwa kwenye Mnara wa Mashujaa.
Viongozi wa Kamati ya Maridhiano Mkoa wa Shinyanga wakiweka Mashada kwenye Mnara wa Mshujaa.
Viongozi wa Kamati ya Maridhiano wakiwa kwenye Kumbukizi ya Mashujaa.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi akiwa na viongozi mbalimbali kwenye kumbukizi ya Mashujaa.
Kumbukizi ya Mashujaa ikiendelea.
Kumbukizi ya Mashujaa ikiendelea.
Kumbukizi ya Mashujaa ikiendelea.
Kumbukizi ya Mashujaa ikiendelea.
Kumbukizi ya Mashujaa ikiendelea.
Picha za pamoja zikipigwa katika Mnara wa Mashujaa.
Picha za pamoja zikipigwa katika Mnara wa Mashujaa.
Picha za pamoja zikipigwa katika Mnara wa Mashujaa.
Picha za pamoja zikipigwa katika Mnara wa Mashujaa.
Mnara wa Mshujaa.

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

MKUU wa wilaya ya Shinyanga Johari Samizi, amewataka Watanzani kuwa enzi mashujaa kwa kulipigania Taifa pamoja na kudumisha Amani ya nchi.


Amebainisha hayo leo Julai 25, 2023 kwenye Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Mashujaa, ambayo Mkoani Shinyanga yamefanyika katika Mnara wa Mashujaa uliopo eneo la Makumbusho Mazingira Center.

Amesema Mashujaa walipigania Uhuru wa Taifa hili, tena wakitumia silaha za Jadi na kuwasihi Watanzia kuendelea kuwaenzi Mashujaa hao kwa kulipigania pia taifa pamoja na kudumisha Amani na utulivu.

“Nawaomba Watanzania tuendelee kulipigania Taifa letu ikiwamo kudumisha Amani na utulivu, pamoja na kulisemea vizuri taifa, sababu hakuna Mbadala wa Tanzania na historia hii ya mashujaa Ibaki vizazi na vizazi,”amesema Samizi.
Share:

JUMUIYA YA WAZAZI CCM WILAYA YA TANGA YAHIMIZA JAMII KUTUNZA MAZINGIRA

 

KATIBU wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tanga Urassa Nanyaro kulia akipokea miti kwa ajili ya kuupanda wakati Jumuiya hiyo iliposhiriki kwenye kampeni inayoendeshwa na Taasisi ya Tea inayojishughulisha na mazingira ikiwemo upandaji wa miti katika maeneo mbalimbali kwenye Jiji hilo ambapo miti hiyo ilipandwa kituo cha Afya Mwakidila
KATIBU wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tanga Urassa Nanyaro kulia akipanda miti  wakati Jumuiya hiyo iliposhiriki kwenye kampeni inayoendeshwa na Taasisi ya Tea inayojishughulisha na mazingira ikiwemo upandaji wa miti katika maeneo mbalimbali kwenye Jiji hilo ambapo miti hiyo ilipandwa kituo cha Afya Mwakidila


Viongozi wa Jumuiya ya Wazazi wakiwa kwenye picha ya pamoja  mara baada ya kumalizika zoezi la kupanda miti wa pili kutoka kulia ni Mjumbe wa Wazazi wilaya ya Tanga Pamela Chaula


Na Oscar Assenga,TANGA.


KATIBU wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Tanga Urassa Nanyaro ameshiriki kwenye kampeni ya upandaji wa miti katika kituo cha Afya Mwakidila Jijiji Tanga huku akiitaka jamii kuendelea kutunza mazingira.

Nanyaro aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati Jumuiya hiyo iliposhiriki kwenye kampeni inayoendeshwa na Taasisi ya Tea inayojishughulisha na mazingira ikiwemo upandaji wa miti katika maeneo mbalimbali kwenye Jiji hilo.

Alisema kwamba wananchi na jamii kwa ujumla wanapaswa kutunza mazingira kwa mustakabvali wa kuimarisha vyanzo vya maji na uchumi wa Taifa letu kwa sababu maji ndio chanzo kikubwa cha nishati ya umeme.

Aidha alisema na nishati ya umeme inapatikana kutokana na utunzaji mazingira na unapandwaji wa miti na hivyo kupatikana mvua za kutosha zinazopelekea mitambo ya kuzalisha umeme kutokana na uwepo wa mvua za kutosha.

“Niipongeze taasisi ya Tea kwa kuendesha kampeni hii kwani miti inapopandwa inasaidia kupata lishe,kivuli na matunda na kuwasaidia kuwezesha kupata mvua ya kutosha itakayowezesha kuendesha mitambo na kuzalisha nishati ya umeme inayotumika hospital viwanda na kuinua uchumi wa Taifa letu”Alisema Nanyaro.

Akiwa katika shule ya Msingi Mwakidila Katibu huyo aliwapongeza walimu wa shule hiyo kutokana na utunzaji wa mazingira na wana hifadhi ya mazingira ambayo ndio chanzo za utunzaji huo

“Sisi Jumuiya ya Wazazi wilaya ya Tanga majukumu yetu ni kushrikiana na shule za msingi ,awali,sekondari vyuo Lengo kuhamasisha vijana wapate malezi bora kulingana na tamaduni ya kitanzania tupo hapo leo wanapoanda miti ya matunda na kwa hali hiyo tuliokuta tunaamini miti itakuwa kwa muslakabali wa viumbe hali na kutunza vyanzo vyetu na vya maji “Alisema

Hata hivyo alisema licha ya utunzaji wa vyanzo vya maji lakini pia mwisho wa siku kupitia mazingira mazuri Taifa liweze kusonga mbele kiuchumi likiwa na watu wenye afya na siha njema.
Share:

MSITOE DAWA KWA WAGONJWA KAMA HANA CHETI CHA DAKTARI-DKT SHEKALAGHE


KATIBU Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt Seif Shekalaghe akizungumza  wakati akifungua kongamano la mrejesho wa Tafiti za Kukinga na kudhibiti Maambukizi na Usugu wa dawa za Antibiotic lililofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa NIMR Prof. Said Shehe Aboud  na kulia ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Prof. Said Shehe Aboud  akizungumza wakati wa  kongamano la mrejesho wa Tafiti za Kukinga na kudhibiti Maambukizi na Usugu wa dawa za Antibiotic lililofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo 
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo Dkt Naima Yusuf akizungumza wakati wa kongamano hilo
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo Dkt Naima Yusuf akizungumza wakati wa kongamano hilo
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt Seif Shekalaghe akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Prof. Said Shehe Aboud  mara baada ya kuwasili katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo kushoto wa kwanza ni Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa mkoa wa Tanga Bombo Dkt Naima Yusuf 



Na Oscar Assenga,TANGA

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt Seif Shekalage amewataka wenye maduka ya dawa nchini wafuate taratibu zilizowekwa na Serikali wasitoe dawa kwa wagonjwa kama hawajakwenda na cheti kilichoandikwa na daktari.

Dkt Seif aliyasema hayo Jijini Tanga wakati akifungua kongamano la mrejesho wa Tafiti za Kukinga na kudhibiti Maambukizi na Usugu wa dawa za Antibiotic lililofanyika katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo.

Alisema jambo hilo ni la msingi na Serikali wameweka sheria kali mtu akimakatwa anachukuliwa hatua lakini sasa wanazungumza wanaofanya kwa njia za siri ambao hawajagundulika wanasababisha tatizo linakuwa kubwa.

“Katika hili napenda kusisitiza hili kwa wenye maduka ya dawa nchini wafuate taratibu zilizowekwa na Serikali wasitoe dawa kwa wagonjwa kama hawajakwenda na karatasi iliyoandikwa daktari”Alisema

Alisema jambo jingine ni wenzao wanaoshirikiana nao wanaouza dawa za mifugo mtu anakwenda anasema kuku wake anatatizo fulani anatoa dawa lakini ushauri unatolewa kwa wahusika kwamba huyo kuku anaumwa nini na anapaswa kutibiwa vipi.

Katibu Mkuu huyo alisema wanahitaji waandishi wa habari kutumia kalamu zao kuweza kutoa elimu kwao waandihi wa habari kila mkoa kuewaeleza athari za dawa na mambo mengine na kuifikisha jamii na hivyo kuweza kuondosha kasumbua hiyo kwa jamii.

Alisema zipo dawa ambazo mtu anajisikia anaumwa na kichwa kununua panado kwa sababu ya kutuliza kichwa iili uende kwa daktari akakupe dawa hilo ndio jambo la msingi sana

Alisema waanajua zipo dawa muhimu zilizowekwa kwenye maduka lakini dawa za antibayotiki wananchi wasitumie tu kwa sababu wanapotumia dawa bila kupata ushauri kwa daktari dawa za aina gani kwa sababu kufanya hivyo wanatengeneza mwili wao kuwa na usugu vimelea vinavyokupata kuweza ku kutibiwa na zile dawa ambazo ni sahihi kwa sababu umeshatengeneza usugu wa kuweza kutrumia tu dawa,

Awali akizungumza Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) Prof. Said Shehe Aboud alitoa wito kwa wananchi wasiende kwenye duka la dawa kununua bila cheti cha daktari kwani kumekuwa na mazoezi wananchi kwenda kujinunulia dawa bila kujua kama kweli wanahitaji kutumia hizo au la.

Alisema pia vilevile wanapoandikiwa dawa za daktari wahakikishe wanatumia dozi kamili na wanatumia kwa mujibu ilivyoandikwa na Daktari.

Aidha aliwataka pia kuhakikisha kwamba pale wanapokwenda kununua kwenye duka la dawa na mambo ya kujitibu wenyewe wanapopata tatizo la kiafya waende hospitalini waonwe madaktari wapimwe wapate vipimo vya maabara na vikapaporudi kwa daktari ndio wanaweza kujua wanapaswa kutumia dawa ya aina gani.

Naye kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Dkt Naima Yusuf alisisitiza wananchi kuacha kutumia dawa bila kujua wanaumwa na nini kwani kufanya hivyo zinaweza kuwasababishia madhara mbalimbali.

Alisema katika utafiti huo walichofanya walichukua sampuli kutoka kwa mama na mtoto aliyezaliwa na kama amezaliwa kwa njia ya kawaida au upasuaji na vifaa vilivyotumika.

“Tupo hapa kwa ajili ya kusisitiza wananchi wasitumie dawa bila kujua wanaumwa na nini kwani kuna tabia unaumwa kidogo unakwenda duka la dawa unachukua dawa mwishowe zile dawa zinaacha kufanya kazi”Alisema

Dkt Naima alisema kwa sababu utakwenda kununua kwa hela ulionayo anunua dozi ambayo haijakamilika na unanunua dawa hujui unaumwa na nini ni vijidudu gani vimesababisha hali hiyo”Alisema

Share:

VIFAA VYA MAWASILIANO 108,395 VYAFUNGWA


Na Mwandishi Wetu - Dodoma

JUMLA ya simu na vifaa vingine vya mawasiliano 108,395 vimezuiliwa kupokea na kutoa mawasiliano katika kipindi cha mwaka mmoja, kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo kujihusisha na ulaghai, vitendo vya udanganyifu, kuibiwa, wizi, na kuripotiwa kuibiwa.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt. Jabiri Bakari, aliwaambia waandishi wa habari jijini Dodoma wiki iliyopita kuwa, TCRA imekuwa macho katika kutambua vifaa vya mawasiliano vinavyotumiwa nchini kwa kuhakikisha vinatumika katika huduma za mawasiliano kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo iliyowekwa.


“TCRA imesimamia zoezi la kuzuia matumizi ya simu zilizoripotiwa kuibiwa, kupotea au kuharibika pamoja na kuzuia matumizi ya simu zisizokuwa na viwango. Usimamizi huu unawezesha kubaini na kufungia namba tambulishi za vifaa vya Mawasiliano zilizonakiliwa (Duplicate International Mobile Equipment Identity-IMEIs), namba tambulishi za vifaa vilivyotumika kwenye udanganyifu pamoja na namba tambulishi zilizotolewa taarifa ya kupotea au kuibiwa,” alisisitiza Dkt Jabiri katika ukumbi wa Idara ya Habari-MAELEZO jijini Dodoma.


Alisisitiza kuwa, kuanzia Julai 2022 hadi Juni 2023 jumla ya namba tambulishi zilizofungiwa na mfumo wa utambuzi wa namba hizo ni 108,395 ambazo ziliripotiwa kupotea, kuibiwa au kuhusika katika matukio ya kihalifu, hivyo kuwezesha kupunguza matukio ya wizi na kusaidia upatikanaji wa vifaa vya Mawasiliano vyenye ubora kwenye soko.


Kuhusu kubainisha simu za ulaghai Mkurugenzi Mkuu Jabiri alisema kuwa, TCRA imeendelea kubaini simu za ulaghai zinazoingia hapa nchini na hatua stahiki zimekuwa zikichukuliwa. “Kutokana na hatua hiyo, idadi ya simu za udanganyifu imeendelea kupungua kuanzia mwaka 2020 hadi Juni 2023. Hata hivyo, tulibaini matukio machache ya simu za ulaghai yalitokea mwezi Septemba, 2022 kama inavyoonekana kwenye Jedwali hapo chini,” alisema.


Kuhusu Usimamizi wa simu za ndani na kimataifa Jabiri alisema Idadi ya dakika za simu za kimataifa zinazoingia nchini (International Incoming) zimepungua kutoka dakika 3,136,692 mwezi Julai 2022 hadi kufikia 2,900,165 mwezi Juni 2023 ambayo ni sawa na asilimia 7.54%, idadi ya dakika za simu za kimataifa zinazotoka nchini (International Outgoing) zimepungua kutoka dakika 2,405,522 mwezi Julai 2022 hadi kufikia dakika 2,226,071 mwezi Juni 2023 ambayo ni sawa na asilimia 7.46%.


“Kupungua kwa simu za kimataifa kunasababishwa na mabadiliko ya teknolojia na upatikanaji wa chaguzi mbadala za kupiga simu kupitia mitandao ya intaneti kama vile Whatsap, Facebook, Telegram, Zoom nakadhalika,” alibainisha.


Alibainisha kuwa idadi ya dakika za simu za kitaifa ndani ya mtandao mmoja (onnet) zimeongezeka kutoka dakika 6,172,696,579 mwezi Julai 2022 hadi dakika 7,012,574,045 mwezi Juni 2023 ambayo ni sawa na 13.61%.


“Hivyo hivyo idadi ya dakika za simu za kitaifa nje ya mtandao mmoja (offnet) zimeongezeka kutoka dakika 4,879,102,325 mwezi Julai 2022 hadi kufikia dakika 5,064,800,480 kufikia mwezi Juni 2023 ambayo ni sawa na 3.81%. Ongezeko la simu za kitaifa linasababishwa na ukuaji wa sekta ya mawasiliano nchini,” aliongeza.


Mamlaka hiyo yenye jukumu la kusimamia huduma za mawasiliano nchini ilianzishwa mwaka 2003 kwa Sheria namba 12 ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania, ikianzishwa baada ya kuunganishwa kwa zilizokuwa Tume ya Mawasiliano na Tume ya Utangazaji nchini. TCRA inasimamia sekta ndogo za simu na Intaneti, huduma za Utangazaji na Posta, ambapo hutoa taarifa ya mwenendo wa sekta kila Robo ya Mwaka wa Fedha na Mwaka mzima ambapo zamu hii Mkurugenzi Mkuu Bakari alikuwa akiwasilisha taarifa ya Maendeleo ya Usimamizi wa Sekta ya Mawasiliano nchini kwa mwaka mmoja uliopita yaani 2022/2023.
Share:

CRDB WAKALA : MUONGO MMOJA WA KUWEZESHA JAMII NA KUBORESHA MAISHA NCHINI

Mkuu wa Kitengo cha CRDB Wakala, Ericky Willy (wapili kushoto) akimkabidhi mshindi wa mwezi wa tano wa kampeni ya “CRDB Wakala 10 na Kitu”, Joshua Lembeli Loketa kadi ya Bajaj baada ya kuongoza kwa Idadi ya miamala katika kampeni hiyo. Wengine pichani ni baadhi ya wafanyakazi wa Benki ya CRDB, pamoja na wake wa mshindi huyo.
Mshindi wa mwezi wa kampeni ya “CRDB Wakala 10 na Kitu”, Joshua Lembeli Loketa akiwa katika Bajaj aliyoshinda baada ya kuongoza kwa Idadi ya miamala katika kampeni hiyo. Waliokaa nyuma ni wake wa mshindi huyo.


========= ======== ========


Katika wilaya ya Kilosa, mkoa wa Morogoro, Joshua Lembeli Loketa amesimama huku akitabasamu huku akiwa ameshikilia funguo za Bajaji yake mpya kabisa. Akiwa CRDB Wakala, Joshua ameibuka mshindi katika Kampeni inayoendelea ya CRDB Wakala ‘10 na Kitu’, ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 10.


Furaha ya Joshua inaonekana wazi wakati akitoa shukrani zake za dhati kwa Benki ya CRDB kwa zawadi hiyo ya bajaj. Kwa furaha anaeleza jinsi Bajaji itakavyo saidia kwa kiasi kikubwa maisha yake, hasa katika kuwasafirisha watoto wake shuleni. Hapo awali, Joshua alilazimika kutenga Shilingi 60,000 kila mwezi kwa ajili ya gharama zao za usafiri.


Lakini safari ya Joshua na CRDB Wakala ni zaidi ya kushinda tu zawadi. Ana hadithi ya kipekee ambayo inamtofautisha na wengine. Joshua ni mfugaji na pia ni Mhasibu wa kampuni ya ulinzi. Kilichomsukuma kuwa CRDB Wakala ni fursa ya ajabu iliyotolewa na Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR), Chuo cha Afya, na jamii ya Wamasai ambayo ni kiongozi.


Kwa ujuzi wake wa kibiashara, Joshua aliona uwezekano wa kutoa huduma za kifedha kwa wafanyakazi wa miradi ya SGR, wafanyakazi na wanafunzi wa Kituo cha Afya, pamoja na jamii. Aliamini katika kutoa huduma bora kwa wateja, na hii inamtofautisha na wengine.


Weledi wake katika utoaji huduma na kufanya kazi kunaonekana katika idadi ya wateja ambao anawapatia huduma — tayari amefungua zaidi ya akaunti 1,000 katika vituo 12 vya mradi wa SGR. Lakini hana mpango wa kuishia hapo. Maono yake ni kuongeza mtaji na kupanua biashara yake, kuongeza wateja wapya na kufungua ofisi nyingi katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Morogoro.


Kamisheni anazopata kwa kuwa CRDB Wakala haijamwezesha Joshua tu kutimiza mahitaji muhimu ya familia yake bali pia imemjengea heshima katika jamii na miongoni mwa mawakala wengine. Amekuwa mfano wa kuigwa na wengi wanaotamani kufikia ndoto zao kwa bidii na kujituma.


Kampeni ya ‘10 na Kitu’ inapoendelea, hadithi za mafanikio na mabadiliko zinaendelea kujitokeza. Safari ya Joshua Lembeli ni mfano mmoja tu wa mapinduzi ambayo CRDB Wakala imekuwa nayo kwa maisha ya mawakala na jamii wanazohudumia. Kwa kila huduma na akaunti inayofunguliwa, Benki ya CRDB inachukua hatua nyingine kuelekea dira yake ya kukuza ushirikishwaji wa kifedha na kuboresha maisha ya Watanzania.


CRDB Wakala imefanya mapinduzi makubwa katika namna huduma za kifedha zinavyotolewa nchini Tanzania. Tangu kuanzishwa kwake mwaka 2013, imekuwa na ukuaji wa ajabu, na kuleta ufanisi mkubwa kwa Benki ya CRDB na kuchukua jukumu muhimu katika kuchochea ujumuishi wa kifedha kote nchini.


Ikiwa na mtandao mpana zaidi wa mawakala zaidi ya 30,000, Benki ya CRDB inaongoza kwa uwakala wa benki nchini Tanzania na inashikilia nafasi tatu kwa ukubwa Afrika Mashariki. Mtandao huu mkubwa unahudumia zaidi ya Watanzania milioni 3 kila mwezi. Ripoti za utendaji zinaonyesha zaidi ya miamala milioni 80 yenye thamani ya zaidi ya TZS 50 trilioni.


Mafanikio hayo yasingewezekana bila jitihada za CRDB Wakala na uhusiano thabiti walioujenga na jamii wanazozihudumia. Kwa kuadhimisha miaka 10 ya CRDB Wakala, Benki ilizindua kampeni ya miezi minne yenye lengo la kuongeza kasi ya ufikishaji wa huduma za benki kwa wananchi walio wengi zaidi.


Kampeni hiyo inachukua mtazamo kamili wa ujumuishaji wa kifedha kwa kurahisisha upatikanaji wa huduma za kibenki, zikiwemo bidhaa na huduma za benki zinazofuata misingi ya sharia chini ya mwamvuli wa CRDB Al Barakah. Aidha, kwa kutambua umuhimu wa bima katika kuhakikisha ustawi wa jamii, hivi karibuni Benki ya CRDB imewawezesha mawakala kutoa huduma za bima ya vyombo vya moto.


Ili kuhamasisha mawakala, kampeni ya ‘10 na Kitu’ inatoa zawadi za kusisimua. Kila mwezi, mawakala walio na idadi kubwa zaidi ya miamala kutoka kanda mbalimbali wana nafasi ya kushinda pikipiki kumi, huku mshindi wa kwanza wa kila mwezi akiondoka na Bajaj. Mwishoni mwa kampeni wakala mmoja atakayeongoza katika kampeni nzima atajinyakulia zawadi ya gari aina ya Toyota Alphard.


Motisha hizi sio tu kwamba zinatambua mafanikio ya CRDB Wakala na mchango wao katika ushirikishwaji wa kifedha bali pia zinawatia moyo kuendelea na kazi yao muhimu, kuhakikisha kwamba huduma za benki zinapatikana kwa wote, na kuhakikisha hakuna anayeachwa nyuma.


Kujitolea kwa mawakala kama Joshua Lembeli ni muhimu katika kubadilisha maisha na kuleta mabadiliko chanya katika jamii yoyote. Mchango wao katika kukuza ujumuishi wa kifedha haupimwi tu kwa idadi ya watu wanaowahudumia, bali pia katika namna ambavyo wamekuwa wakisaidia kuboresha maisha ya wateja wanaowahudumia.--
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 25,2023



































Share:

Monday, 24 July 2023

BABA KAIKIMBIA FAMILIA NA KWENDA KUOLEWA!


Naitwa Blessing, mzawa wa Kondoa, nina umri wa miaka 26, nimehitimu masomo ya Secondary mwaka 2015 ila sikuweza kupata nafasi ya kujiunga na masomo ya high school kutokana na hali ngumu ya maisha nyumbani kwetu.

Mwaka 2014 mama yetu aliondoka nyumbani na kurudi kwao Iringa kutokana na tabia ya baba yetu ya ulevi na kuwa na wanawake wengine nje ndoa bila kujali yake inahitaji matunzo.


Baada ya mama kuondoka maisha ya nyumbani yalibadilika sana, baba akawa anakunywa pombe hadi anamaliza siku bila mbili kurejea nyumbani.

Hatimaye tulipata habari kuwa baba kaolewa na mwanamke mwenye Baa alipokuwa anakunywa pombe mara kwa mara, basi nilibeba jukumu la kuwalea wadogo wangu.


Maisha ambayo tulikuwa tunapitia tulitambua kuwa chaguo baya zaidi maishani ni kuchagua mume au mke asiye kuwa na sifa nzuri na ndicho kilichomgharimu mama yetu hadi kuja kutufikia sisi.

Kutokana na hilo, nilikuwa makini sana na wanaume ambao walikuwa wanaomba kunioa ila mimi nilikuwa nimeandaa sifa tatu muhimu ambazo mwanaume yoyote atakayetaka kunioa lazima awe nazo kuepuka kuwapatia tabu na shida watoto wangu.


Nilipofikisha miaka 24 shangazi yangu akaniambia kuwa natakiwa kuolewa kwa sababu umri unaenda, mimi sikujali kwa sababu niliona bora nisiolewe kuliko kuolewa kisha nikaanza kujutia.

Siku moja nikiwa nyumbani rafiki yangu Rita alikuja kunijulia hali na wadogo zangu, Rita ni rafiki yangu tangu tukiwa shule ya msingi hivyo alikuwa anajua mengi sana kunihusu.


Katika stori zetu aliweza niambia kuwa alimfunga Boyfriend wake asiweze kumpenda msichana mwingine zaidi yake hadi wakimaliza Chuo na kufunga pingu za maisha. Nilipomuuliza alimfunga kivipi ndio akanipatia namba hizi +254 769 404965 na kuniambia ni za African Doctors.

Akanieleza kuwa African Doctors anaweza nisaidia kumpata mwanaume mwenye sifa nizitakazo kwa muda mfupi tu, siku kadhaa zilizipita nikaamuua kutembelea tovuti yao www.african-doctors.com na kuona kweli wana huduma hiyo.

Nikiwa bado katika tovuti yao niliona namba ile niliyopewa na Rita kisha nikatuma ujumbe WhatsApp kwa ajili ya kuomba msaada, African Doctors alinijibu vizuri kisha akaniambia kuwa nimtumie sifa za mume ambaye namhitaji.


Nilituma kisha akaniomba nisubiri kwa masaa 48 tu nitaweza mtambua mtu sahihi kwangu, masaa 48 kabla ya kuisha aliweza kujitokeza kijana kutoka Kondoa mjini kisha kuniomba kuwa mke wake. Nilipotazama kila sifa niliyotaka alikuwa nayo, hatimaye tulifunga ndoa na kwa sasa tunaishi wote kwa amani na furaha.

Wasiliana na African Doctors kwa namba; +254 769 404965, tembelea tovuti yao; www.african-doctors.com au watumie email; africandoctorheals@gmail.com.

Mwisho.



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger