Friday, 21 July 2023

NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA MAJI AFANYA UKAGUZI WA UTOAJI HUDUMA ZA MAJI SHINYANGA, ATOA MAAGIZO KWA MAMLAKA ZA MAJI

Na Mwandishi wetu - Malunde 1 blog 
Naibu Katibu Mkuu wizara ya Maji nchini Mhandisi Cyprian Luhemeja amefanya ziara yake ya kikazi Mkoani Shinyanga kwa ajili ya ukaguzi wa utoaji wa huduma za maji mkoani humo.


Ziara hiyo imefanyika jana Julai 20, 2023 ikiwa ni muendelezo wa ziara yake ya kikazi ya siku 21 yenye lengo la kukagua ufanisi katika utekelezaji wa miradi ya maji, uendeshaji wa mamlaka za maji na ubora wa utoaji wa huduma kwa wateja mkoani Shinyanga.


Ziara hiyo ilihusisha kutembelea kwenye miradi mitatu ya maji inayotekelezwa ndani ya wilaya ya Kishapu kupitia Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Vijijini RUWASA ambayo ni mradi wa maji ya bomba Seseko - Ngundangali, uliogharimu bilioni 2.73 fedha kutoka serikali kuu unaotarajia kuhudumia wananchi wapatao 15,500 kutoka kwenye vijiji vya Seseko, Mpumbula, Ngundangali, Kakola na Dugushilu, mradi wa pili ni mradi wa maji Masanga - Ndoleleji wenye unaogharimu kiasi cha bilioni 2.3 fedha kutoka serikali kuu kupitia Program ya malipo kwa matokeo (Payment for Result) uliousisha ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji lenye ujazo wa lita 100,000 unaotarajia kuhudumia wakazi 12,768 kutoka vijiji vya Ndoleleji, Masanga, Mwampolo na Ng’wang’halanga, mradi wa tatu ni mradi wa ziwa Victoria Iganga - Isagala wenye gharama ya shiringi bilioni 6.62 unaotarajia kuhudumia takribani watu 49,965 katika vijiji 13.


Mara baada ya kutembelea miradi hiyo mitatu Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji ameipongeza RUWASA kwa kusimamia utekelezaji wa miradi hiyo kikamilifu na kusema kuwa amelizishwa na ujenzi wa miradi hiyo inayotekelezwa na kuwasihi wakandarasi kuongeza kasi ya ujenzi ili kuharakisha huduma ya maji kwa wananchi.


“Hongereni sana RUWASA kwa kazi hii nzuri mnayoifanya kwa kuendelea kusimamia utekelezaji wa miradi ya maji kupitia fedha za serikali ya awamu ya sita ya Rais Samia Suluhu Hasani ambapo kwa sasa ametoa Shiringi Bilioni 7 kwaajili ya utekelezaji wa miradi ya maji kwenye wilaya ya Kishapu, tunataka kuona mkoa wa Shinyanga ufike 90% ya upatikanaji wa huduma ya maji ni vyema kulipa madeni ya wakandarasi ili kuwawezesha kumaliza miradi hii ndani ya wakati”, amesema Naibu katibu mkuu Mhandisi Cyprian Luhemeja.


Mbunge wa jimbo la Kishapu Boniphace Butondo ameipongeza serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutenga kiasi kikubwa cha fedha ili kusogeza huduma ya maji karibu na wananchi.

 “Naipongeza sana serikali ya awamu ya sita kwa kuleta fedha nyingi kwaajili ya utekelezaji wa miradi ikiwemo miradi ya maji kutoka ziwa victoria ambapo itakapokamilika tutakwenda kuwa na zaidi ya 90% za upatikanaji wa maji kutoka kwenye 50% zilizopo kwa sasa, ukiangalia katibya vijiji 122 ni vijiji 70 tu ndio vimefikiwa na huduma ya maji safi na salama ndani ya wilaya hii”, amesema Mbunge Butondo.


Awali akipokea taarifa za mamlaka za maji kwenye kikao cha uwasilishaji wa taarifa za uendeshaji wa huduma za maji mkoni humo KASHWASA, SHUWASA, RUWASA ambapo meneja wa RUWASA mkoa wa Shinyanga Mhandisi Julieth Payovela alisema hadi sasa mkoa wa shinyanga una Vyombo vya watoa huduma ya maji ngazi ya jamii (CBWSOs) vipatavyo 34 ambapo kwa wilaya ya kahama ni 11, Kishapu 9 na Shinyanga 14 ambapo kufikia mwezi Disemba wanatarajia kukamilisha miradi yote inayotekelezwa.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maji nchini Mhandisi Cyprian Luhemeja akiwasili kuanza ziara yake Mkoani Shinyanga.
Naibu Katibu Mkuu wizara ya Maji nchini Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza wakati wa ziara yake
Mradi wa Tanki la maji Igaga - Isagana.
Mradi wa Tanki la kuhifadhia maji Masanga - Ndoleleji.
Mradi wa maji ya bomba Seseko - Ngundangali.
Meneja RUWASA Wilayani Kishapu Mhandisi Dickson Kamazima akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi wilayani humo.
Mbunge wa Jimbo la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo Akizungumza.
Meneja wa RUWASA Mkoa wa Shinyanga Mhandisi Julieth Payovela.
Meneja RUWASA Wilayani Kishapu Mhandisi Dickson Kamazima akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi wilayani humo.
Naibu Katibu Mkuu wizara ya Maji nchini Mhandisi Cyprian Luhemeja akizungumza mara baada ya kupokea taarifa.
Mkurugenzi wa KASHWASA Mhandisi Patrick Nzamba akiwasilisha taarifa ya utekelezaji na uendeshaji.

Share:

MSIKUBALI UPOTOSHAJI WA WAZUSHI, BANDARI HAIUZWI _ MBUNGE DKT. CHAYA


Mbunge wa Manyoni Mashariki Mhe. Dkt. Pius Chaya, amewataka wananchi wake kupuuza upotoshaji unaoendelea mitandaoni kuhusu suala la Bandari, na kuzuka kauli za kwamba Mhe. Rais Samia ameuza nchi.

Mhe. Dkt. Chaya ameyasema hayo leo  Julai 20, 2023 wakati wa ziara yake Katika Kata ya Chikola na Sasilo, Wilayani Manyoni ambapo amefanya Mikutano ya hadhara, baada ya kuulizwa Maswali na Wananchi juu ya maswali waliyonayo kuhusu ukakasi uliopo juu ya Bandari   

Amefanya Ziara Katika Vijiji vya Ipululu, Mwitikila, Chidamsulu na Chikola

Mhe. Chaya ameeleza kuwa kinachokwenda kufanyika ni Ubia kati ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Dp World ya Nchini Dubai na haina tofauti na ilivyokuwa kwa Kampuni ya Ticts ambayo imetekeleza Mkataba wake kwa Miaka 25.

"Kinachokwenda kufanywa na Rais Samia ni Ubia sio ubinafsishaji, sasa kuna watu wanaanza kupotosha, mara tunauza bandari, huyu anapokuja tunakuja kukubaliana nae kwamba wewe unachukua sehemu gani na unatekeleza kwa asilimia kadhaa, na asilimia kadhaa atatekeleza Tanzania yaani TPA, na hicho ndo kinachofanyika"

Akiendelea kuwaasa wananchi wake, Mhe. Dkt. Chaya amesema wengi wanapotosha kwamba Mama Samia ameuza Bandari, jambo ambalo wao kama Wabunge hawawezi kukubali, ni lazima wangepiga kelele kupinga.

"Ubia ni makubaliano kwamba nachukua sehemu hii, wewe chukua sehemu hii baadae mnaweka utaratibu mzuri wa mgao, hakuna tofauti kabisa Kati ya anachokuja kufanya Dp World na Ticts"

Amesema anashangaa kumekuwa na Siasa nyingi kwenye jambo hilo, na kuwaomba Watanzania kumuunga Mkono Mhe. Rais na wao kama Viongozi Vijana wanapaswa kuaminiwa na Wananchi kwani hawawezi kukubali jambo ambalo linaihatarisha nchi.


"ninachofurahi kote huko nilikopita sijakutana na upotoshaji wa aina yoyote, wengi wanasimama kwakweli wanakiri kabisa kwamba huyu Mama anafaa, anatosha na chenji inabaki" amesema Dkt. Chaya


Mbunge huyo amewaambia wananchi hao kuwa, hakuna sehemu ambayo ilikuwa na Madudu mengi kama Bandarini, hata enzi za  Hayati Rais Magufuli wengi walifukuzwa katika bandari.

Ameongeza kuwa, watu wengi wametajirika kupitia Bandari ya Dar es salaam na ukifuatilia wanaopinga wengi ni wale wanaofanya Kazi katika Bandari hiyo na wanajua kwa sababu wananufaika.

 "Niwaombe kama kuna maeneo mazuri ya kuboresha, toeni mawazo yenu tuboreshe huu uwekezaji ambao Rais wetu anataka kuufanya, tunataka tupate Fedha ili tutekeleze miradi mingi ya maendeleo"

Amesema, maendeleo yanayofanyika katika Jimbo lake yanatokana na mapato, na mojawapo ikiwa ni ya Bandari kwani ni eneo ambalo mapato mengi yanatoka huko,  hivyo uwekezaji huo utakaokwenda kufanyika utaongeza utekelezaji wa miradi katika Taifa.

"Ukicheza na bandari usipoweka uwekezaji mzuri hautavuna chochote mapato ,Mimi nimetembelea pale bandarini, hatuna uwezo wa kushusha mizigo kwa muda muafaka, mizigo ikifika inakaa muda mrefu sana na matokeo yake wawekezaji wengi wanahama"

Ametaka Rais Samia aungwe mkono kuhusu suala la Bandari kwani ana nia njema na hapaswi kukatishwa tamaa

"Ndugu zangu wana Chikola na sisi tusiwe watu wa kufuata mkumbo, tusikubali kupotoshwa na Wazushi" Mbunge Dkt. Chaya.

Aidha, Mbunge Dkt. Chaya alipopita Katika Vijiji hivyo, ameeleza Miradi ambayo Serikali inatekeleza, na itaendelea kutekeleza Katika maeneo yao.

Ziara ya Mhe. Mbunge Dkt. Chaya bado inaendelea katika Vijiji mbalimbali Jimbo la Manyoni Mashariki.
Share:

MAFUNZO MAALUMU YA MATIBABU YA UTAPIAMLO MKALI KWA WATOTO YATOLEWA KWA WATUMISHI HOSPITALI YA RUFAA YA BOMBO

 

 Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Mohamed Salehe wa tano  kulia mwenye koti akifuatilia kwa umakini  Mafunzo Maalumu yanayohusu matibabu ya utapiamlo mkali kwa watoto yametolewa kwa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo

Sehemu ya washiriki wa mafunzo wakifuatilia 
Daktari wa Wodi ya Watoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga -Bombo Dkt Mwalimu Khalid



Na Oscar Assenga,TANGA.

MAFUNZO Maalumu yanayohusu matibabu ya utapiamlo mkali kwa watoto yametolewa kwa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo huku yakielezwa kuwa yatakuwa na umuhimu mkubwa kwao.

Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo ya siku mbili,Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Mohamed Salehe alisema mafunzo hayo yatawasaidia kuongeza ufanisi wakati wa utoaji wa huduma kwa wagonjwa.

Dkt Mohamed ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Watoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga alisema baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo anaimani kwamba washiriki wanakwenda kuwa chachu katika utoaji wa huduma.

Mafunzo hayo yamewashirikisha wataalamu mbalimbali wakiwem kutoka Ustawi wa Jamii, Madaktari, Manesi na maafisa lishe ambayo yanatajwa kwamba yatakuwa chachu katika utoaji wa huduma

Alisema mafunzo hayo yanatolewa kwa natharia na vitendo huku washiriki wakionekana kuwa na uelewa mzuri na walimu wamekuwa wakitoa mafunzo ya kuwaezesha kutoa matibabu kwa watoto wenye utampiamlo.

“Unampomtibu mtoto mwenye tatizo la utapiamlo linahitaji watu wote waweze kusaidiana na chimbuko la hasa na sababu kuweza kujulikana na kumtibu ndio moja njia pekee ya kuweza kumuondolea huyo mtoto tatizo hilo”Alisema

Dkt Mohamed alisema akiwa ametibiwa Hospitali lakini pia akirudi nyumbani awe ametibika moja kwa moja ikiwemo kupewa matunzo wanaporudi nyumbani baada ya kumaliza matibabu.

“Pamoja na kwamba wanatibiwa Hospital wanahitaji matunzo huko nyumbani watoto wanakaa na wazazi hivyo ni kuwapa mafunzo ya namna ya kuwalea watoto kama hao kwani wanaweza kuwa kama wengine na ndoto zao ila mafunzo kwa wazazi ni jambo la muhimu”Alisema

Awali akizungumza wakati wa mafunzo hayo Afisa Lishe wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga –Bombo Imakula Mwamrefu alisema wapo kwenye mafunzo maalumu yanayohusu matibabu kwa watoto wenye utapiamlo mkali wanaozaliwa katika hospitali hiyo.

Alisema kwamba kwenye hospitali hiyo wana kitengo ndani ya wodi ya watoto 13 na 14 kinachohusika kwa matibabu ya utapiamlo mkali kwa watoto hivyo kutokana na hilo wameona wawe na mafunzo ya kujengeana uwezo namna ya kuwatibu watoto wanapofika hospitalini.

Hata hivyo alisema kwamba mafunzo hayo yatakuwa kwa njia ya kuelekezana na vitendo kuona namna ya kutambua utapiamlo mkali

Naye kwa upande wake Daktari wa Wodi ya Watoto katika Hospitali hiyo Dkt Mwalimu Khalid alisema kwamba mafunzo hayo ya matibabu kwa watoto wenye utapiamlo mkali ni muhimu kutokana na kwamba wanakuwa na miili yenye mabadiliko hivyokuna na utofauti jinsi ya kuwatibu ukilinganisha na wale wa kawaida.

Alisema hiyo kuna umuhimu wa madaktari na manesi wanaopokuwa na wajibu wa kuwaangalia hao watoto wanatakiwa kueleza mafunzo hayo kutokana na watoto hao wanatibiwa tofauti na wengine hivyo daktari anaweza kuwa mzuri sana kutibu watoto lakini akimpata mtoto kama huyo kama hajapata mafunzo anaweza kumtibu tofauti.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULAI 21,2023





























Share:

NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AGAWA MITUNGI YA GESI ROMBO


Mbunge wa Viti maalumu Mhe Ummy Nderiananga ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu)
 

Na Mathias Canal, Rombo-Kilimanjaro

Mbunge wa Viti maalumu Mhe Ummy Nderiananga ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) ameunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuviwezesha vikundi vya wanawake kutumia nishati safi ya kupikia kwa kutoa Mitungi ya gesi.

Naibu Waziri Mhe Nderiananga ametoa mitungi hiyo wakati akiwa katika ziara ya kikazi Wilayani Rombo Mkoani Kilimanjaro huku akisisitiza umuhimu wa nishati hiyo mbadala.

Mhe Nderiananga amesema kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan imelenga kuhakikisha inapunguza matumizi ya kuni, mkaa na mabaki ya mazao ili kulinda afya za wananchi.

Amesema kuwa I licha ya athari za kimazingira zinazotokana na ukataji wa miti unaofanywa na Wananchi Matumizi ya nishati chafu yamekuwa na athari zaidi za kiafya.

“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt.Samia Suluhu Hassan anatoa fedha nyingi kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo programu ya kumtua mama ndoo kichwani lakini akasema wakina mama wanapata shida wao ndio wapishi sasa ni wakati wa kuwatua kuni kichwani kwa kuwasaidia kupata nishati ya gesi na mimi nimekuja kutekeleza adhma yake ya kumtua mama kuni kichwani” Amekaririwa Mhe Ummy

Pia amesema kuwa dhumuni la Mheshimiwa Rais ni kuona namna ya kuwakomboa wanawake hususani vijijini hutumia saa nne hadi tano kutafuta kuni, hivyo wanakutana na majanga mbalimbali ikiwemo kung’atwa na wanyama wakali na kutumia muda mwingi kutafuta kuni porini.


Aidha, ameahidi kuendelea na programu hiyo wakinamama kuwatua kuni kichwani na kusaidia kulinda mazingira.







Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger