Friday, 21 July 2023
NAIBU KATIBU MKUU WIZARA YA MAJI AFANYA UKAGUZI WA UTOAJI HUDUMA ZA MAJI SHINYANGA, ATOA MAAGIZO KWA MAMLAKA ZA MAJI
MSIKUBALI UPOTOSHAJI WA WAZUSHI, BANDARI HAIUZWI _ MBUNGE DKT. CHAYA
MAFUNZO MAALUMU YA MATIBABU YA UTAPIAMLO MKALI KWA WATOTO YATOLEWA KWA WATUMISHI HOSPITALI YA RUFAA YA BOMBO
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Mohamed Salehe wa tano kulia mwenye koti akifuatilia kwa umakini Mafunzo Maalumu yanayohusu matibabu ya utapiamlo mkali kwa watoto yametolewa kwa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo
Na Oscar Assenga,TANGA.
MAFUNZO Maalumu yanayohusu matibabu ya utapiamlo mkali kwa watoto yametolewa kwa watumishi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo huku yakielezwa kuwa yatakuwa na umuhimu mkubwa kwao.
Akizungumza wakati akifungua mafunzo hayo ya siku mbili,Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Mohamed Salehe alisema mafunzo hayo yatawasaidia kuongeza ufanisi wakati wa utoaji wa huduma kwa wagonjwa.
Dkt Mohamed ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Watoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga alisema baada ya kumalizika kwa mafunzo hayo anaimani kwamba washiriki wanakwenda kuwa chachu katika utoaji wa huduma.
Mafunzo hayo yamewashirikisha wataalamu mbalimbali wakiwem kutoka Ustawi wa Jamii, Madaktari, Manesi na maafisa lishe ambayo yanatajwa kwamba yatakuwa chachu katika utoaji wa huduma
Alisema mafunzo hayo yanatolewa kwa natharia na vitendo huku washiriki wakionekana kuwa na uelewa mzuri na walimu wamekuwa wakitoa mafunzo ya kuwaezesha kutoa matibabu kwa watoto wenye utampiamlo.
“Unampomtibu mtoto mwenye tatizo la utapiamlo linahitaji watu wote waweze kusaidiana na chimbuko la hasa na sababu kuweza kujulikana na kumtibu ndio moja njia pekee ya kuweza kumuondolea huyo mtoto tatizo hilo”Alisema
Dkt Mohamed alisema akiwa ametibiwa Hospitali lakini pia akirudi nyumbani awe ametibika moja kwa moja ikiwemo kupewa matunzo wanaporudi nyumbani baada ya kumaliza matibabu.
“Pamoja na kwamba wanatibiwa Hospital wanahitaji matunzo huko nyumbani watoto wanakaa na wazazi hivyo ni kuwapa mafunzo ya namna ya kuwalea watoto kama hao kwani wanaweza kuwa kama wengine na ndoto zao ila mafunzo kwa wazazi ni jambo la muhimu”Alisema
Awali akizungumza wakati wa mafunzo hayo Afisa Lishe wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga –Bombo Imakula Mwamrefu alisema wapo kwenye mafunzo maalumu yanayohusu matibabu kwa watoto wenye utapiamlo mkali wanaozaliwa katika hospitali hiyo.
Alisema kwamba kwenye hospitali hiyo wana kitengo ndani ya wodi ya watoto 13 na 14 kinachohusika kwa matibabu ya utapiamlo mkali kwa watoto hivyo kutokana na hilo wameona wawe na mafunzo ya kujengeana uwezo namna ya kuwatibu watoto wanapofika hospitalini.
Hata hivyo alisema kwamba mafunzo hayo yatakuwa kwa njia ya kuelekezana na vitendo kuona namna ya kutambua utapiamlo mkali
Naye kwa upande wake Daktari wa Wodi ya Watoto katika Hospitali hiyo Dkt Mwalimu Khalid alisema kwamba mafunzo hayo ya matibabu kwa watoto wenye utapiamlo mkali ni muhimu kutokana na kwamba wanakuwa na miili yenye mabadiliko hivyokuna na utofauti jinsi ya kuwatibu ukilinganisha na wale wa kawaida.
Alisema hiyo kuna umuhimu wa madaktari na manesi wanaopokuwa na wajibu wa kuwaangalia hao watoto wanatakiwa kueleza mafunzo hayo kutokana na watoto hao wanatibiwa tofauti na wengine hivyo daktari anaweza kuwa mzuri sana kutibu watoto lakini akimpata mtoto kama huyo kama hajapata mafunzo anaweza kumtibu tofauti.
NAIBU WAZIRI NDERIANANGA AGAWA MITUNGI YA GESI ROMBO
![]() ![]() |
| Mbunge wa Viti maalumu Mhe Ummy Nderiananga ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) |
Na Mathias Canal, Rombo-Kilimanjaro
Mbunge wa Viti maalumu Mhe Ummy Nderiananga ambaye pia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) ameunga mkono jitihada za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuviwezesha vikundi vya wanawake kutumia nishati safi ya kupikia kwa kutoa Mitungi ya gesi.
Naibu Waziri Mhe Nderiananga ametoa mitungi hiyo wakati akiwa katika ziara ya kikazi Wilayani Rombo Mkoani Kilimanjaro huku akisisitiza umuhimu wa nishati hiyo mbadala.
Mhe Nderiananga amesema kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan imelenga kuhakikisha inapunguza matumizi ya kuni, mkaa na mabaki ya mazao ili kulinda afya za wananchi.
Amesema kuwa I licha ya athari za kimazingira zinazotokana na ukataji wa miti unaofanywa na Wananchi Matumizi ya nishati chafu yamekuwa na athari zaidi za kiafya.
“Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt.Samia Suluhu Hassan anatoa fedha nyingi kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo programu ya kumtua mama ndoo kichwani lakini akasema wakina mama wanapata shida wao ndio wapishi sasa ni wakati wa kuwatua kuni kichwani kwa kuwasaidia kupata nishati ya gesi na mimi nimekuja kutekeleza adhma yake ya kumtua mama kuni kichwani” Amekaririwa Mhe Ummy
Pia amesema kuwa dhumuni la Mheshimiwa Rais ni kuona namna ya kuwakomboa wanawake hususani vijijini hutumia saa nne hadi tano kutafuta kuni, hivyo wanakutana na majanga mbalimbali ikiwemo kung’atwa na wanyama wakali na kutumia muda mwingi kutafuta kuni porini.
Aidha, ameahidi kuendelea na programu hiyo wakinamama kuwatua kuni kichwani na kusaidia kulinda mazingira.






































.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)

.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)
.jpeg)







