Friday, 14 April 2023

WAMILIKI WA KUMBI ZA STAREHE WATAKIWA KUFUATA SHERIA KUDHIBITI KELELE NA MITETEMO

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla akizungumza katika Mkutano na Wadau wa Mazingira kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira leo Aprili 14,2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Samuel Gwamaka akizungumza katika Mkutano na Wadau wa Mazingira kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira leo Aprili 14,2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Mwanahamisi Mnkunda akizungumza katika Mkutano na Wadau wa Mazingira kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira leo Aprili 14,2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya akiwa katika Mkutano na Wadau wa Mazingira kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira leo Aprili 14,2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
Wadau mbalimbaali wa Mazingira wakiwa kwenye mkutano kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira leo Aprili 14,2023 katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

(PICHA NA EMMANUEL MBATILO)


******************

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla ameongoza Mkutano na Wadau wa Mazingira kujadilia suala la viwango vya udhibiti wa kelele na mitetemo pamoja na katazo la mifuko ya plastiki leo tarehe 14 April 2023, uliohudhuriwa na wadau mbalimbali wa mazingira katika ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika Mkutano huo, Mhe.Makalla amesema kuna umuhimu mkubwa viongozi wa dini wakapatiwa elimu kusimamia katazo na zuio la mifuko ya plastiki pamoja na udhibiti wa makelele kwenye maeneo ya makazi ya watu ili kuondoa changamoto hizo ambazo zimekuwa zikitokea katika maeneo mbalimbali kwenye Jiji la Dar es Salaam.

Mhe. Makala amesisitiza juu ya changamoto ya viwango vya juu vya kelele katika kumbi za starehe na nyumba za ibada pamoja na kupiga marufuku matumizi ya mifuko ya plastiki akiwaasa wanajamii kuepuka matumizi ya mifuko hiyo kwani ni chanzo cha uharibifu wa mazingira na kutoa muda wa wiki moja kwa NEMC na TBS kuweka ratiba ya kupita katika wilaya za jiji la Dar es salaam kufanya ukaguzi wa kutoa elimu ya matumizi sahihi ya mifuko ya plastiki.

Amesema "Dar es salaam bila mifuko ya plastiki na kelele zilizodhidi viwango inawezekana na ni wakati wa kila mmoja kuwajibika na kuhakikisha haki inatendeka bila kupepesa macho na kwa wazalishaji kusalimisha mifuko ya plastiki waliyoizalisha katika ofisi za NEMC bila kuchukuliwa hatua."

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) Dkt. Samuel Gwamaka amewataka wananchi kufuata Kanuni na Sheria za Uhifadhi wa Mazingira kwa kudhibiti viwango vya kelele na mitetemo katika maeneo mbalimbali hususani kumbi za starehe na makanisa pamoja na kupunguza matumizi ya mifuko ya plastiki iliyopigwa marufuku kwani ni chanzo cha uchafuzi wa mazingira.

Amesisitiza kuwa "wazalishaji, wasambazaji na wauzaji wa mifuko ya plastiki wahakikishe kuwa viwanda vyao vinasajiliwa na Baraza na kupata cheti cha Tathmini ya Athari kwa Mazingira kabla ya kuanza uzalishaji na kufuata matakwa ya Sheria na viwango sahihi vilivyowekwa."

Pia ametoa angalizo kwa wazalishaji na wasambazaji wa mifuko ya plastiki kunisalimisha kwani Baraza litatoa donge nono kwa yeyote atakaye toa taarifa juu ya uwepo wa kiwanda au wasambazaji wa mifuko na vifungashio visivyokidhi viwango.

Aidha Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Athuman Ngenya amesema "wale wote wanaomiliki viwanda vya kuzalisha plastiki ambao wana leseni ya TBS endapo watahitaji kuhuisha leseni au kuchukua leseni mpya lazima wawe na Cheti cha Mazingira kutoka NEMC.

Nao wadau wa mazingira walitoa maoni yao juu ya udhibiti wa viwango vya kelele na mitetemo kwa kuomba kupatiwa vifaa vya kupimia sauti, kuboreshaji njia za utoaji elimu kwa wananchi ili kuwezesha kudhibiti kelele chafuzi pamoja na kupewa vibali maalum ili kuwezesha viongozi katika ngazi za mtaa kuchukua hatua stahiki kwa wanaokiuka Sheria.

Kwa upande wa katazo la mifuko ya plastiki wadau wameisihi Serikali kuhakikisha kuwa wananchi wanapata taarifa sahihi juu ya mifuko iliyopigwa marufuku na pia kuboresha njia bora za kuwadhibiti wale wote wanaozalisha mifuko ya plastiki kwa kuwachukulia hatua za Kisheria ili kuweza kutokomeza tatizo hili.
Share:

SEKTA YA MAKAA YA MAWE YATAKIWA KUZINGATIA SHERIA NA MIONGOZO YA USALAMA NA AFYA

Meneja wa OSHA Kanda ya Kusini Bw. Wilbert Ngowi akitoa elimu ya masuala ya usalama na afya katika uchimbaji na uchukuzi wa makaa ya mawe kwa wafanyakazi na viongozi wa kampuni za BECCO na ARIA Commodities Mkoani Ruvuma.
Viongozi na Wafanyakazi wa Kampuni za ARIA Commodities na BECCO Limited wakifuatilia mada ya masuala ya usalama na afya mahali pa kazi kutoka kwa Meneja wa OSHA Kanda ya Kusini Bw. Wilbert Ngowi (hayupo pichani)
Meneja wa OSHA Kanda ya Kusini Bw. Wilbert Ngowi akijibu swali kutoka kwa mfanyakazi wa BECCO Limited aliyeuliza kuhusu namna sahihi ya kujikinga dhidi ya vumbi la makaa ya mawe katika maeneo ya ofisi na mgodi.
Mfanyakazi wa Kampuni ya uchimbaji wa Makaa ya mawe ya JITEGEMEE Limited akiuliza swali kwa Meneja wa OSHA Kanda ya Kusini Bw. Wilbert Ngowi (hayupo pichani) kuhusu njia sahihi za kuzuia na kudhibiti vihatarishi katika maeneo yao ya migodi.

************************

Na Mwandishi wetu

Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) umetoa wito kwa wawekezaji na waajari wa sekta ya makaa ya mawe kuhakikisha wanazingatia ipasavyo sheria na miongozo ya usalama na afya ili kuwalinda wafanyakazi wao dhidi ya ajali na magonjwa yanayoweza kuwapata katika maeneo yao ya kazi.

Wito huo umetolewa kupitia kwa Meneja wa OSHA Kanda ya Kusini, Bw.Wilbert Ngowi alipokuwa akihitimisha programu maalumu ya siku nne ya mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi kwa Viongozi na Wafanyakazi wa sekta ya makaa ya mawe Wilayani Mbinga Mkoani Ruvuma.

“Sekta ya makaa ya mawe inakabiliwa na vihatarishi mbalimbali kama ilivyo kwa sekta zingine za madini mfano mfanyakazi anapovuta vumbi la makaa kwa muda mrefu anaweza kupata ugonjwa wa nimonia ya mapafu meusi (coal worker’s pneumoconiosis), ugonjwa huu hauna dalili za haraka wala tiba hivyo mfanyakazi akiathirika na huu ugonjwa utakuwa ndio ulemavu wake wa maisha na pengine unaweza kumsababishia kifo,”

“Hivyo basi kutokana na sekta hii kukabiliwa na vihatarishi vingi na vinavyoweza kuhatarisha Maisha ya wafanyakazi tumeona tuanze kuchukua tahadhari mapema kwa kuendesha programu maalumu ya mafunzo kwa lengo la kuwapa elimu wafanyakazi hawa ili waweze kuepukana na vihatarishi hivi vya ajali na magonjwa vinavyoweza kuwapata katika maeneo yao ya kazi ikiwa ni pamoja na kuepukana na vumbi la makaa ya makaa ya mawe”. Alisema Bw. Ngowi akiongeza kwa kutoa wito kwa wawekezaji.

“Nitoe wito kwa Waajiri na Wawekezaji wa Sekta ya Makaa ya Mawe wahakikishe kwamba wanazingatia taratibu zote za usalama na afya katika maeneo yao yote ya kazi kwa kuchukua tahadhari zote stahiki ikiwa ni pamoja na kuhakikisha vumbi linapungua katika maeneo yao pia wahakikishe vifaa vyote vinavyotumika katika shughuli mbalimbali vinamkinga mfanyakazi dhidi ya vihatarishi vya ajali na magonjwa.” aliongeza Bw. Ngowi.

Aidha kupitia progamu hiyo ya mafunzo, Mkurugenzi wa Oparesheni wa Kampuni ya uchimbaji wa Makaa ya mawe ya Jitegemee Holdings, Bw.Boscow Mabena ameeleza namna ambavyo kampuni hiyo imehamasika katika kuimarisha mifumo ya usalama na afya katika Kampuni yake.

“Tunawashukuru sana OSHA kwa kutupatia elimu hii ya usalama na afya katika sekta yetu ya makaa ya mawe, wamekuwa wakitutembelea na kutupa miongozo mbalimbali ya namna sahihi ya kuboresha mazingira ya kazi hivyo tumehamasika kwa kiasi kikubwa sana na tayari tumetenga bajeti ya mafunzo ya usalama na afya, tutapeleka wafanyakazi wakahudhurie mafunzo hayo yanayotolewa na OSHA” alisema Bw. Mabena.

Kwa upande wao washiriki wa mafunzo hayo kutoka kampuni mbalimbali wanaeleza namna ambavyo elimu hiyo itawaongezea tija katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

“Nime elimika kwa kiasi kikubwa sana na kama kiongozi itanisaidia kuwasimamia vyema wafanyakazi wenzangu katika eneo letu la kazi ikiwemo kuwalinda dhidi ya vumbi la makaa ya mawe linaloweza kusababisha ugonjwa wa nimonia ya mapafu meusi vivilevile tunaahidi kutekeleza mambo yote yaliyoagizwa na sheria ya usalama na afya ikiwemo kuhakikisha wafanyakazi wote wana tekeleza majukumu yao wakiwa wamevaa vifaa kinga.” Alisema Rajabu Miraji

Kwa upande wake Bi. Merce Gerald ambaye ni Mhandisi kutoka Kampuni ya Jitegemee ameeleza kuwa mafunzo haya yataleta mabadiliko ya kiusalama kwa kiasi kikubwa sana katika maeneo yao ya kazi.

“Elimu hii itatusaidia sana kujikinga na vihatarishi mbalimbali tunavyokabiliana navyo katika maeneo yetu ya kazi hivyo niombe OSHA waendelee kutoa mafunzo haya kwa migodi mingine ili waweze kuokoa Maisha ya wafanyakazi wengine wa sekta hii.”alisema Bi. Merce Gerald.

Programu hii maalumu ya mafunzo ya usalama na afya mahali pa kazi katika sekta ya uzalishaji wa makaa ya mawe imefanyika kuanzia tarehe 11 – 14/04/2023 na jumla ya wafanyakazi 400 kutoka kampuni za TANCOAL, RUVUMA COAL, JITEGEMEE HOLDINGS, ARIA COMMODITIES na BECCO LTD wamefikiwa na elimu hiyo.
Share:

DKT RWEZIMULA: TUJIPANGE MIKOPO KWA WANAFUNZI 'SERA YA ELIMU BILA ADA

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk.Franklin Rwezimula akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Abdul-Razaq Badru wakati Naibu Katibu Mkuu huyo alipotembelea HESLB jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Abdul-Razaq Badru (mwenye miwani) akizungumza wakati Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk.Franklin Rwezimula alipotembelea HESLB jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dk.Franklin Rwezimula akipokea zawadi kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Abdul-Razaq Badru wakati Naibu Katibu Mkuu huyo alipotembelea HESLB jijini Dar es Salaam.


**********************





Na Mwandishi Wetu

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) imetakiwa kujiandaa kwa ongezeko kubwa la wanafunzi wahitaji wanaotokana na sera ya elimu ya msingi na sekondari bila ada ambao wanatarajia kujiunga na taasisi za elimu ya juu kuanzia mwaka 2026/2027.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Franklin Rwezimula amesema kuwa ni muhimu kwa HESLB kuwa na mipango inayoendana na mageuzi makubwa ya elimu yanayofanywa na Serikali ikiwemo kuwawezesha watoto kupata elimu ya msingi na sekondari bila malipo ya ada.

“Bajeti ya mikopo kwa mwaka huu wa 2022/2023 ni TZS 654 bilioni, na mwakani tutarajie itaongezeka zaidi … sasa ni vema mipango yenu (HESLB) iendane na ongezeko linalokuja kuanzia mwaka 2026/2027 ambapo matunda ya sera ya elimu bila ada yataanza kwenda elimu ya juu,” amesema Dkt. Rwezimula.

Dkt. Rwezimula ameyasema hayo alipokutana na Menejimenti ya HESLB katika ofisi za taasisi hiyo jijini Dar es salaam alipofika kujitambulisha na kubadilishana uzoefu baada ya kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan tarehe 26 Februari mwaka huu.

Akizungumza katika kikao hicho, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru amesema Menejimenti ya HESLB imejipanga na kuandaa mapendekezo ya kuhimili ongezeko la wanafunzi wahitaji wa mikopo katika miaka ijayo.

“Hivi karibuni, tumefanya utafiti kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Uchumi (HEET) kuhusu matokeo ya elimu bila ada katika ugharimiaji wa elimu ya juu miaka ijayo … taarifa ipo na tutawasilisha kwa ajili ya ushauri na maandalizi,” amesema Badru.

HESLB ilianzishwa mwaka 2005 ikiwa na majukumu makuu mawili – kutoa mikopo kwa wanafunzi wahitaji wa elimu ya juu na kukusanya fedha za mikopo zilizoiva zilizotolewa kwa wanafunzi tangu mwaka 1994/1995.
Share:

KAILIMA AMPONGEZA WAZIRI MHAGAMA KWA BAJETI KUPITA BUNGENI


Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa akiwa Bungeni pamoja nae ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama (wapili kushoto), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Prof. Joyce Ndalichako (wapili kulia) na Naibu Waziri ,Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobas Paschal Katambi.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama akichangia hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya mwaka 2023/24 Bungeni Jijini Dodoma leo Aprili 13,2023. Kulia ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Prof. Joyce Ndalichako
Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Ramadhani Kailima akimpongeza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama pamoja na viongozi wengine wa Wizara baada ya kuhitimishwa kwa Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya mwaka 2023/24 Bungeni Jijini Dodoma leo Aprili 13,2023.




Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista Mhagama na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Prof. Joyce Ndalichako pamoja na manaibu Waziri na Makatibu wakuu wa Wizara zao wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Taasisi mbalimbali zilizo chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu baada ya kuhitimishwa kwa bajeji ya ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha wa 2023/24 Bungeni jijini Dodoma Aprili 13,2023.
***************


Waziri wa Nchi Ofisi ya waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera Bunge na Uratibu Mhe. Jenista Mhagama amesema Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu imezingatia vipaumbele muhimu katika maeneo yote yanayoratibiwa na Ofisi hiyo ili kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na tija kwa Taifa.

Ametoa kauli hiyo mapema leo wakati akichangia Hotuba ya Bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu ya Mwaka wa fedha 2023/24 wakati wa Kikao cha Bunge la 12 Mkutano wa 11 Kikao cha sita Mjini Dodoma.

Waziri Mhagama amesema pamoja na mambo mengine, Bajeti ya Mwaka huu ya Ofisi ya Waziri Mkuu imezingatia masuala muhimu ikiwemo la Uratibu wa shughuli za Serikali kwa kueleza tayari ofisi hiyo umeunda Idara ya ufuatiliaji na Tathimini ya utendaji wa serikaliambapo itawezesha kuwa na taarifa sahihi za utekelezaji wa Shughuki za Serikali.

Akizungumzia kuhusu Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Waziri Mhagama amesema, Mamlaka imefanya kazi ya kutosha katika maeneo yote manne ya kimkakati ya kupambana na dawa za kulevya, kupunguza uingizaji wa dawa za kulevya, kufanya ukaguzi katika maeneo yanayofanya biashara ya kemikali bashirifu na kufanya maboresho ya sheria na kuteketeza mashamba mengi ya bangi nchini.

Aliongeza kwa kusema kuwa, Mamlaka imefanya vizuri katika kutoa elimu ya uelewa kuhusu matumizi ya madawa ya kulevya.

“Tumefanya vizuri katika kupunguza athari za madhara ya dawa za kulevya kwa waathirika, na huduma ya za kutibu urahibu wa dawa za kulevya na bado tunaendelea kufanya mashirikiano ya nchi, kikanda na kimataifa ili kukabiliana na jambo hili mtambuka.”Alisisitiza

Kwa Upande wa suala la Sera ya lishe, Waziri amesema Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu, itakuja na Mkakati wa kuwa na Sera ya lishe, UKIMWI na Janga la matumizi ya Dawa za kulevya.

Pamoja na hilo, Waziri alieleza kuwa ofisi yake inasimamia Dawati la Afya Moja linaloshughulikia uratibu wa magonjwa ya mlipuko yanayoambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu, ili kuweza kukabiliana nayo na kuangalia usalama wa wananchi.

Aidha alitumia nafasi hiyo kumpongeza Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan, kwa kwa falsafa yake ya kuliwezesha Taifa kuwa na ustahimilivu na kuleta mabadiliko makubwa ya kiuongozi, kidemokrasia, kiuchumi na mahusiano ya kimataifa na kuwataka wabunge kuunga mkono falsafa hiyo.
Share:

CCM MKOA WA IRINGA WAIONGEZA NGUVU YA TSH MILIONI 2 MKWAWA QUEENS KWENDA KUIVAA SIMBA QUEENS



Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Daud Yassin akikabidhi kiasi Cha Tsh Milioni 2 Kwa uongozi wa Timu ya Mkwawa Queens inayocheza Ligi kuu ya Soka la wanawake Tanzania inayotarajia kusafiri jumapili kwenda Dar,Kucheza na Simba Queens kiasi Cha TshMilioni 3.4 zinahitajika ambazo zilikuwa zikihitajika Kwa ajili ya safari hiyo .

Akikabidhi msaada huo Leo Kwa uongozi wa timu hiyo ,Yassin alisema chama Cha Mapinduzi kinatambua mchango mkubwa wa Timu ya Mkwawa Queens na Timu nyingine Katika michezo na kuwa kutokana na changamoto ya timu hiyo .

Hivyo alisema Katika kuunga mkono jitihada za Timu hiyo na jitihada za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan Katika kuendelea michezo nchini wao kama CCM mkoa wa Iringa wataendelea kuuunga mkono jitihada hizo ikiwa ni pamoja na kusaidia sekta ya michezo ndani ya mkoa wa Iringa.

Alisema jitihada za Mkwawa Queens wanaziona na kuwa ili Timu hiyo kutimiza vema majukumu yake ni vema wadau kuendelea kuunga mkono Timu zote ndani ya mkoa .

"Niwapongeze Sana Uongozi wa Mkwawa Queens Kwa kuendelea kuwakilisha mkoa Katika soka la wanawake na sisi kama chama tupo pamoja "

Aidha Yassin alimpongeza mkuu wa mkoa wa Iringa Halima Dendego pamoja na Viongozi wengine wa mkoa huo Kwa kuendelea kusaidia Timu .

Afisa habari wa Mkwawa Queens Francis Godwin alipongeza mchango huo wa chama na kuwa huo ni mchango mkubwa Kwa Timu kupokea .

Alisema Kwa Sasa Timu hiyo inasafari ya kwenda Dar es salaam kucheza na Simba Queens siku ya Jumanne na kuwa timu itaondoka Iringa Jumapili safari ambayo itaigharimu Timu Tsh Milioni 3.4 baada ya hapo inajiandaa Kwa mchezo wake Dodoma na Mkoani Lindi ambako ili kufanikisha Mzunguko uliobaki zaidi ya Tsh Milioni 10 zinahitajika .

Hivyo aliwaomba wadau kuendelea kuisaidia Timu hiyo na kumpongeza jitihada za Mkuu wa mkoa wa Iringa Halima Dendego na uongozi wa CCM mkoa chini ya Mwenyekiti Daud Yassin na wote ambao wameendelea kuichangia Timu hiyo .

Godwin pia alimpongeza mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati Kwa mchango wake wa Tsh 200,000 na wote wanaondelea kujitolea Kwa ajili ya Timu akiwemo katibu wa Chadema Kanda ya Kaskazin Jackson Mnyawami kuchangia Timu namba hii 0715621222 jina la mpokeaji Maryam Swaleh
Share:

Thursday, 13 April 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRILI 14,2023





















Share:

MBUNGE MTATURU AIKUMBUSHA SERIKALI KULIPA WASTAAFU


MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu ,ameendeleza kilio chake cha kucheleweshwa kwa mafao ya wastaafu ambapo safari hii ameikabidhi serikali barua yam zee Simon Albert Makiya kwa ajili ya utekelezaji.

Mei 2022,katika swali lake la msingi Mtaturu aliihoji serikali lini itamaliza changamoto ya kucheleweshewa mafao kwa wastaafu ambapo serikali ilieleza jitihada zake ikiwemo kulipa deni la mfuko wa PSSSF ikiwa ni pamoja na kutoa hatifungani ya Shilingi Trilioni 2.17 ambazo zitaimarisha mtiririko wa mapato na kuwezesha kutoa mafao kwa wakati.

Aidha,Mei 2020,akichangia mjadala wa bajeti ya wizara ya fedha na mipango,Mtaturu aliiomba serikali kuwalipa mapema wastaafu mafao yao na kuwataja wazee wawili wa Ikungi Mohammed Ntandu na Gamilliel Massawe suala ambalo serikali iliahidi kulishughulikia.

Leo April 13,2023,ni mara ya tatu kutoa kilio hicho,“Eneo hili limekuwa likilalamikiwa sana na wabunge wamepata malalalmiko hayo,kuna mzee wangu mmoja ambaye barua yake ninayo ameniletea kama mbunge wake Simon Albert Makiya kutoka Siuyu,

“Barua hii nitaomba niikabidhi kwa waziri,mzee huyu amekuwa akilalamika anasubiri fedha zake za kustaafu na amekuwa akija hapa bungeni akifanya juhudi za kumuona waziri ili asikilize kilio chake,naomba watu wa aina hii watendewe haki ,”amesisitiza.
Share:

HUAWEI CALLS FOR A 'NON-STOP' DIGITAL FUTURE FOR AFRICA'S BANKING INDUSTRY

[Cape Town, ] Huawei today announced its ‘Non Stop Banking’ initiative. Unveiled at the Huawei Intelligent Finance Summit for Africa 2023, the initiative calls for hand-in-hand collaboration between the ICT and banking industries and facilitate a digital future of ‘non-stop’ services, ‘non-stop’ development, and ‘non-stop’ innovation.


In a keynote speech announcing the initiative, Leo Chen, president of Huawei Sub-Saharan Africa Region spoke about why going digital has become such a major imperative for the banking industry. Not only does it make it easier for banks to broaden their customer base, he said, it also saves operational costs, allows them to develop new products, and deepen the customer relationship, thus generating revenues for banks.



In Africa, he added, there’s an even greater imperative for banks to embrace digitization, as it allows for greater financial inclusion. While Chen lauded the innovative work done by many African banks in embracing digitization, he pointed out that all players in the industry need to go further if they’re to embrace the ‘non-stop’ approach that will characterise the future of banking.



Huawei has already served more than 2500 financial customers in over 60 countries and regions, including 50 of the world's top 100 banks. Numerous Huawei technologies, Chen said, are helpful on this front. Over the years, it has provided the foundation and backbone for the digitalization of the banking industry in Africa by supporting the construction of the continent’s ICT infrastructure and digital connectivity in rural areas. Its extensive focus on research and development (R&D), meanwhile, means that it’s well-poised to help the industry shape its future too.



From a technical perspective, he pointed to Huawei's strength in storage, fibre optic networks, IP networks and data communication, which enable ‘multi-domain collaboration’ solutions for banks. For example, its ‘storage and optical connection coordination (SOCC)’ solutions can reduce system switchover time from two minutes to two seconds after a network breakdown, ensuring zero transaction interruptions. The multilayer ransomware protection (MRP) technology, meanwhile, can provide 6-layer protections, from storage, to network, to applications and other layers. It enables a reliable and secure ‘end-to-end’ protection to the whole system. Finally, Huawei’s intelligent network O&M solutions enable faults to be detected in one minute, diagnosed in three minutes, and rectified in five minutes.



Huawei Cloud, the world's fastest-growing major cloud service provider, can additionally support the hybrid multi-cloud service required by banks. Huawei’s digital energy solutions, meanwhile, can help to provide an uninterrupted and green power supply for the banking sector. This effectively addresses power deficit issues and supports ‘non-stop’ banking.


That kind of technological innovation will be important because, as Jason Cao, CEO of Huawei Global Digital Finance pointed out, financial services are becoming mobile and intelligent at a blistering pace.


“The financial industry should pay acute attention to users and their demands, embracing changes,” he said. “Huawei is dedicated to helping its African financial customers address challenges and accelerate changes across six fields: shifting from transaction to digital engagement, cloud-native and agile businesses, data democratization, secure and reliable infrastructure, hybrid multi-cloud and Lego-style modular services, and automated and predictable operation.”


“In this way, Huawei will facilitate financial digitalization and innovatively improve productivity in Africa. Revolving around stability, agility, and intelligence, Huawei aims to build ‘non-stop’ financial services, and achieve ‘non-stop’ development alongside ’non-stop’ innovation,” he added.


Beyond technology, Huawei issued a call for all parties in the industry to come together and build more robust ICT infrastructure, facilitate more measures and policies to encourage digital finance innovation, cultivate a sound innovative ecosystem, and train more digital talent for the industry.


Huawei is particularly active on the last two points. Huawei Cloud’s Spark programme, for example, has pledged to assist 1 000 SMEs over the next three years. And having already trained more than 80 000 digital talents in Africa, it has launched the ‘LEAP’ digital talent training programme in Sub-Saharan Africa region, aiming to train another 100 000 people in the next three years.


The Huawei Intelligent Finance Summit for Africa 2023 brought together more than 200 attendees, including key industry opinion leaders, as well as executives from major banks across Africa.
Share:

MBUNGE CHIKOTA ASHAURI IUNDWE TUME YA KUCHUNGUZA KUSHUKA KWA UZALISHAJI KOROSHO


Na Mwandishi Wetu, DODOMA

Mbunge wa Nanyamba (CCM), Abdallah Chikota, ameomba kuunda Tume huru ya kuchunguza kushuka kwa uzalishaji wa zao la korosho ndani ya miaka mitatu mfululizo licha ya jitihada za kupanua wigo wa kilimo cha zao hilo kwenye mikoa mbalimbali.

Akichangia jana mjadala wa makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu na taasisi zake kwa mwaka 2023/24, Mbunge Chikota alisema pamoja na jitihada za serikali za kuratibu upatikanaji wa pembejeo kuna mdondoko wa zao hilo.



“Napongeza serikali ya awamu ya sita kwa kazi kubwa anayoifanya katika kuwekeza katika tasnia ya korosho, tumeona kwa miaka mitatu mfululizo, Serikali ikitoa pembejeo bure kwa wakulima wa korosho, tunaendelea kuishukuru Serikali.”

“Mwaka huu kuna mikataba yenye thamani ya Sh bilioni 340 ambayo imetolewa na nina matumaini pembejeo hizi zitafika kwa wakati na wakulima wa korosho watanufaika na pembejeo,”alisema Chikota.

Kadhalika, alisema pamoja na uwekezaji ulifanywa na serikali kwenye tasnia ya korosho bado kuna anguko la uzalishaji wa korosho nchini ambapo kwa kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2017/18, Tanzania ilifikisha uzalishaji wa tani 320,000.

“Lakini kwa masikitiko makubwa katika msimu uliopita uzalishaji umepungua hadi kufikia tani 160,000 pamoja na uwekezaji mkubwa uliofanywa, ukiuliza Bodi ya Korosho hawana majibu ya uhakika na hata taasisi ya utafiti ya TARI Naliendele hawana majibu ya kutoshereza ya anguko kubwa na uzalishaji wa korosho,”alisema.



Alisisiza “Haiwezekani mikoa ya uzalishaji wa korosho imeongezeka, serikali imefanya uwekezaji wa kutosha lakini uzalishaji unazidi kuwa mdogo.”

Chikota alisema malengo ya Bodi ya Korosho mwaka huu ilikuwa ni kufikisha tani laki nne na Ilani ya Chama cha Mapinduzi na kufikisha tani 700,000 ifikapo mwaka 2025.

“Kwa anguko hili kuna kazi kubwa inayopaswa kufanywa ili kufikia malengo nashauri serikali kuunda tume hii huru yenye wataalamu kutoka nje ili kupata mawazo mapya,”alisema.

Aliomba watumie wataalamu wa nje na SUA ili kuangalia mfumo wa uagiziaji na udhibiti wa pembejeo kwa kuangalia ubora wake.

“Tusiendelee kuwatumia wataalamu wale wale wa TARI na Bodi ya Korosho watatuletea majibu yela yale tuliyoyazoea. Tupate timu mpya, ikiwezekana tuchukue uzoefu kutoka huko,”alisema.

Pamoja na hayo, Chikota aliishauri Serikali kuimarisha miundombinu ya barabara na reli ili kufungua mikoa ya kusini.

Pia alishauri Serikali kutekeleza mradi wa maji kutoka Mto Ruvuma ili kuweza upatikanaji wa maji hatua ambayo itavutia wawekezaji.
Share:

WIZARA YA ARDHI KUWAFIKISHA MAHAKAMANI WADAIWA SUGU


Kamishna wa Ardhi msaidizi mkoa wa Dodoma Jabir Singano.
Mkuu wa Kitengo cha kodi wa Wizara ya Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Denis Masami akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dodoma kuhusu ukusanyaji wa madeni ya pango la ardhi.


Na Dotto Kwilasa,DODOMA.

SERIKALI kupitia Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi imesema itawafikisha mahakamani watu wote wanaodaiwa malimbikizo ya kodi ya pango la ardhi pamoja na kukamata mali zao na kubatilisha hati zao mara baada ya kuisha kwa kipindi cha msamaha wa Rais Aprili 30, 2023.

Hayo yameelezwa leo Jijini Dodoma na Mkuu wa Kitengo cha kodi wa wizara hiyo Denis Masami,wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ukusanyaji wa madeni ya pango la ardhi katika kipindi ambacho serikali ilitoa msamaha kwa wadaiwa kulipa bila riba.

Denis amesema,"Mheshimiwa Rais alitoa msamaha kwa waliolimbikiza malipo ya kodi ya pango la ardhi katika kpindi cha kuanzi mwezi Julai hadi Desemba mwaka jana ambapo watu 6,000 walijitokeza kutumia fursa hiyo na kulipa bila riba.

Cha kushangaza watu wengi waliomba muda uongezwe na serikali kutoa msamaha kwa awamu ya pili ya kuanzia mwezi Machi hadi Aprili mwaka huu, ambapo hadi sasa ni watu 8,725 wamejitokeza kulipa bila riba”,amesema.

Amesema hadi sasa kiasi cha malimbikizo ya kodi ambacho kimeshalipwa ni Sh. bilioni 31.5 na kiasi cha riba ambacho kimesamehewa ni Sh. bilioni 21.3.

“Hivyo basi niwasihi wananchi kutumia fursa hii ya msamaha wa Rais wetu Samia Suluhu Hassan, kulipa malimbizo ya madeni yao kodi ya pango la ardhi bila riba kwani muda ukifika mwisho wote walishindwa kulipa tutawachukulia hatua ikiwemo kuwafikisha mahakamani na kushikilia mali zao na kubatilisha hati zao”,amesema.

Kwa upande wake Kamishna wa Ardhi msaidizi mkoa wa Dodoma Jabir Singano, amesema katika kipindi cha msamaha wa Rais watu zaidi ya 1,200 wamejitokeza kulipa madeni yao.

Amefafanua kuwa kwa mkoa wa Dodoma pekee watu zaidi ya 1,200 wamejitokeza kulipa na kiasi cha Sh. bilioni 1.2 kimeshalipwa hadi sasa na kwamba wanaendelea kuhimiza wote ambao bado wanadaiwa kulipa katika muda huu uliobaki.

Amesema katika jitihada za kuongeza makusanyo mkoa umeendelea kutatua kero zilizokuwepo ikiwemo kukwama kwa malipo ya miamala ya maombi ya wateja.

“Lakini pia kulikuwepo na shida ya upatikanaji wa namba za malipo (contral numbar) hili pia tumelifanyia kazi ambapo tumetoa namba za malipo zaidi ya 4,050 kwa wateja kupitia timu yetu tuliyoiunda kulifanyia kazi suala hili lililokuwa kikwazo kwa wananchi wetu”,amesema
Share:

Wednesday, 12 April 2023

CHIKOTA:NANYAMBA KUNA UPUNGUFU WA WATUMISHI WA AFYA 610




Na Mwandishi Wetu, DODOMA

SERIKALI imeombwa kupeleka watumishi wa kada za afya kwenye Halmashauri zinazokabiliwa na uhaba mkubwa ikiwamo Halmashauri ya Mji wa Nanyamba yenye upungufu wa watumishi wa kada hiyo 610.

Akiuliza maswali bungeni leo, Mbunge wa Nanyamba (CCM), Abdullah Chikota, amesema upungufu watumishi huo upo kwenye Kituo Cha Afya Majengo, Jinyecha, Kilomba na Hospitali ya Halmashauri hiyo.

"Serikali Ina mpango gani wa dharura wa kupunguza tatizo la watumishi Nanyamba. pia Wizara ya Afya imetoa mwongozo wa wanafunzi waliomaliza masomo kada za afya wajitolee kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, je serikali haioni ni wakati muafaka wa kutenga fedha kwasasa waanze kufanya kazi kwenye maeneo yenye upungufu mkubwa,"amesema.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Dk.Festo Dugange, amekiri kuwapo na upungufu huo na kwamba mpango wa serikali ni kuajiri na kupeleka kwenye maeneo yenye upungufu.

"Nikuhakikishie katika ajira zilizotangazwa Halmashauri zenye upungufu mkubwa zitapewa kipaumbele,"amesema.

Katika swali la msingi, Mbunge huyo alitaka kujua mkakati wa Serikali wa kupeleka watumishi na vifaa tiba katika Kituo cha Afya Majengo.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri huyo alisema katika miaka mwili ya mwaka 2020/21 na 2021/2022 Serikali iliajiri Watumishi wa Kada za Afya 10,328 na kati ya hao Halmashauri ya Mji Nanyamba ilipata Watumishi 51 wa kada mbalimbali za afya.

Dk. Dugange alisema Serikali inatambua changamoto ya uhaba wa wataalam wa afya katika vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Aidha, alisema Kituo cha Afya Majengo kilipangiwa watumishi nne ambao ni Mteknolojia Maabara, Tabibu Msaidizi na Wauguzi wawili.

Dk. Dugange alisema katika mwaka wa fedha 2022/23, Serikali imepeleka vifaa na vifaa tiba katika Halmashauri ya Nanyamba vyenye thamani ya shilingi milioni 300 kwa ajili ya vituo vya huduma za afya.

Share:

RAIS MSTAAFU WA MSUMBIJI CHISANO MGENI RASMI UTOAJI TUZO YA UANDISHI BUNIFU JIJINI DAR ES SALAAM



Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Joaqium Alberto Chissano amewasili nchini kushiriki hafla ya utoaji tuzo ya Kitaifa ya Mwl. Nyerere ya Uandishi Bunifu inayotarajiwa kufanyika Aprili 13, 2023 jijini Dar es Salaam.

Akizungumzia ujio wa Kiongozi huyo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe.Prof. Adolf Mkenda amesema Rais Mstaafu Chissano anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmi katika utoaji wa Tuzo hizo ambazo zinatolewa kwa mara ya kwanza nchini.

Prof. Mkenda ameongeza kuwa Kamati maalum ya Tuzo ilimpendekeza Rais Chissano kuwa mgeni rasmi kutokana na ukweli kwamba ni Rais wa kwanza kuhutubia kutumia lugha ya kiswahili katika Mkutano wa Wakuu wa nchi za Afrika.

"Tunayo furaha kuwa na Mgeni Rasmi Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Joaquim Alberto Chissano ambaye mbali na kuongea lugha ya kiswahili vizuri lakini pia ni Mkuu wa nchi wa kwanza kutumia lugha ya kiswahili katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika," amesema Prof. Mkenda

Ameongeza kuwa mshindi wa Tuzo hiyo mbali ya kupata zawadi ya fedha taslimu, vitabu vyake vitachapishwa na kusambazwa katika shule pamoja na maktaba kwa gharama za Serikali.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Tuzo ya Kitaifa ya Mwl. Nyerere Prof. Penina Mlama amesema Kamati ilipokea miswada 283 ya riwaya na mashairi tuzo ambayo ilishindanishwa na kupata washindi watakaotangazwa Aprili 13, 2023.

Prof. Mlama ameongeza kuwa katika hafla hiyo waandishi nguli na maarufu watashiriki akiwemo Prof. Abdallatif Abdalla, Prof. Farouk Taban, Ida Hadjivayanis na Moyez Vassanji.

Aidha Mwenyekiti huyo amesema kumalizika kwa hafla ya utoaji tuzo za Mwaka 2023 ndio kuanza kwa maandalizi ya tuzo za Mwaka 2024 ambapo Miswada itaanza kupokelewa kuanzia Juni 1, 2023

Tuzo ya Taifa ya Mwl. Nyerere ya Uandishi Bunifu inatolewa kwa lengo la kuhamasisha uandishi Bunifu, usomaji vitabu, kutunza utamaduni ,kukuza matumizi ya lugha ya Kiswahili na kuimarisha Uchapishaji.
Share:

LHRC YAZINDUA RIPOTI YA HAKI ZA BINADAMU YA MWAKA 2022, YAIPONGEZA SERIKALI


*********************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) wameipongeza Serikali kwa kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari ikiwemo kwa kuvifungulia vyombo vinne vya habari vilivyokuwa vimefungiwa.

Pongezi hizo zimetolewa leo Aprili 12,2023 uzinduzi wa Ripoti ya Haki za Binadamu ya mwaka 2022 ambayo imefanyika kwa njia ya mtandao kwa kuwajumuisha waandishi wa habari mbalimbali.

Amesema licha ya Serikali kufanya vizuri kwenye suala hilo lakini bado kuna sheria mbalimbali ambazo zina vifungu vinavyominya uhuru wa vyombo vya habari, ikiwemo Sheria ya Huduma za Habari ya mwaka 2016.

"Tunafurahi pia kuondolewa kwa katazo la mikutano ya kisaisa ya hadhara hivi karibuni, ambalo lilikuwa linakiuka uhuru wa kujumuika na kukuanyika kwa muda mrefu, ikiwemo mwaka 2022.

Aidha amesema katika upande wa vitendo vya ukatili, tathmini walioifanya inaonyesha watoto walikuwa ni wahanga wakuu wa vitendo hivyo (47%), wakifuatiwa na wanawake (33%), na wazee (10%), watu wenye ulemavu (4%), na wengine, ikiwemo wanaume, (6%), hivyo kukiuka haki ya uhuru dhidi ya ukatili.

Amesema Matukio ya wananchi kujichukulia sheria mkononi yameendelea kuwa mwiba kwa haki ya kuishi, ambapo kwa mwaka huu LHRC imekusanya matukio 40, ambayo ni 18 zaidi ukilinganisha na mwaka 2021.

Hata hivyo amesema kuwa matukio ya mauaji yanayotokana na imani za kishirikina yamepungua, lakini bado ni changamoto, hasa kwa wanawake, ambao walikuwa ni 52% ya wahanga.

"Mashambulio na mauaji ya watu wenye ualbino pia yameibuka upya miaka ya hivi karibuni, na mwaka 2022 lilitokea tukio jingine la mauaji ya mtu mwenye ualbino mkoani Mwanza, ambaye alifariki baada ya kukatwa mkono. Mauaji ya mwenza yanayofanywa na mwenza pia yameendelea kuathiri haki ya kuishi yakisababishwa na wivu wa kimapenzi". Amesema

Amesema Haki ya usawa mbele ya sheria imeandelea kuwa mojawapo ya haki zinazokiukwa zaidi kwa sababu ya vikwazo mbalimbali vya upatikanaji haki na changamoto katika mfumo wa haki jinai.

"Mojawapo ya vikwazo vikubwa vya upatikanaji haki kwa mtazamo wa wanajamii ni rushwa (82%), ikifuatiwa na kesi kuchukua muda mrefu na uelewa mdogo kuhusu sheria (54%)". Amesema
Share:

PURA, EACOP WABADILISHANA UZOEFU USHIRIKI WA WATANZANIA

Meneja wa Ushiriki wa Wazawa wa Kampuni ya EACOP, Bw. Olivier Foulonneau (wa kwanza kushoto), Mkuu wa Masuala la Kujenga Uwezo, Bi. Martha Makoi (wa pili kushoto), Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa Wazawa na Uhusishwaji wa Wadau kutoka PURA, Bw. Ebeneza Mollel (wa pili kulia) na Bw. Hakeem Mwaruka kutoka PURA katika picha ya pamoja mara baada ya kikao.

****************

Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli (PURA) imekutana na kufanya mazungumzo na Kampuni ya Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) - upande wa Tanzania kwa lengo la kubadilishana uzoefu katika eneo la kuongeza ushiriki wa wazawa kupitia programu za kujenga uwezo. Mazungumzo hayo yalifanyika tarehe 11 Aprili 2023 katika Ofisi za EACOP Jijini Dar es Salaam. Miongoni kwa waliohudhuria kikao hicho ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ushirikishwaji wa Wazawa na Uhusishwaji wa Wadau kutoka PURA, Bw. Ebeneza Mollel na Meneja wa Ushiriki wa Wazawa kutoka Kampuni ya EACOP, Bw. Olivier Foulonneau.

Akiongea katika kikao hicho, Bw. Ebeneza alieleza kuwa, miongoni mwa mikakati inayotumiwa na PURA kuongeza ushiriki wa watanzania katika shughuli za mkondo wa juu wa petroli ni kuwafikia na kuwashirikiana na wadau mbalimbali wa sekta hiyo. Kupitia mashirikiano hayo, PURA hupata mawazo ya wadau juu ya jinsi ya kuongeza ushiriki wa watanzania na kupata kusikia changamoto zinazowakabili wadau hao wakati wa utekelezaji wa matakwa ya kisheria ya ushiriki wa watanzania.

“PURA inaamini kuwa, suala la kuongeza ushiriki wa watanzania linahitaji juhudi shirikishi ili kufikia matokeo yanayotarajiwa. Kwa kuwa EACOP ni mmoja wa wadau wenye mchango mkubwa katika kuongeza ushiriki wa watanzania, PURA iliona ipo haja ya kukutana na kampuni hii kubadilishana uzoefu katika suala hili” aliongeza Bw. Ebeneza.

Kwa upande wake, Bw. Oliver alisema ni heshima kubwa kuwa na mazungumzo na PURA kama mmoja wa wadau kujadili suala la ushiriki wa watanzania ikiwemo jitihada zinazofanywa na Kampuni ya EACOP katika eneo hilo.

“Kampuni ya EACOP, mbali na kuhakikisha kuwa wakandarasi wakuu wa mradi wanazingatia matakwa ya ushiriki wa watanzania kama yalivyoainishwa katika Mkataba wa Nchi Hodhi na Kanuni za Ushiriki wa Watanzania za mwaka 2017; Kampuni imekuwa ikifanya programu mbalimbali za kuwajengea uwezo watanzania na watoa huduma wakitanzania” aliendelea bwana Olivier.

Akifafanua zaidi kuhusu mikakati inayotekelezwa EACOP Tanzania katika kuwajengea uwezo watanzania, Afisa anayehusika na masuala ya kujenga uwezo, Bi.Martha Makoi alisema kuwa kampuni hiyo inashirikiana na vyuo mbalimbali vya ufundi stadi kama vile Chuo cha Ufundi Arusha na Taasisi ya Teknolojia Kilimanjaro (KIITEC). Mashirikiano haya yatawezesha vyuo hivyo kuwa na uwezo wa kuzalisha wataalamu watakaohitajika katika Mradi wa EACOP (upande wa Tanzania).

Mradi wa EACOP unahusu ujenzi wa bomba la mafuta lenye urefu wa kilomita 1,443 litakalosafirisha mafuta ghafi kutoka maeneo ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania ambapo mafuta hayo yatauzwa katika masoko ya nje. Kwa upande wa Uganda, bomba litapitia wilaya 10 na kaunti 25 na litakuwa na jumla ya kilomita 296. Nchini Tanzania, bomba litakuwa na urefu wa kilomita 1,147 na litapita katika mikoa 8 na wilaya 25. Utekelezaji wa mradi huu utaleta na fursa nyingi zikiwemo ajira na ugavi wa bidhaa na huduma.
Share:

DART KUPANDA MITI 1,000 KWENYE MIUNDOMBINU YAKE DAR ES SALAAM

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba, Mwenyekiti wa Bodi DART Dkt. Florens Turuka,Mkurugenzi wa DART, Dkt. Edwin Mhede pamoja na viongozi wa NMB wakiwa katika uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023

Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba akipanda mche wa mti katika kando ya barabara ya mabasi yaendayo kasi wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023



Mwenyekiti wa Bodi DART Dkt. Florens Turuka akipanda mche wa mti katika kando ya barabara ya mabasi yaendayo kasi wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023
Mkurugenzi wa DART, Dkt. Edwin Mhede akipanda mche wa mti katika kando ya barabara ya mabasi yaendayo kasi wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023
Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba akizungumza wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023
Mwenyekiti wa Bodi DART Dkt. Florens Turuka akizungumza wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023.
Mkurugenzi wa DART, Dkt. Edwin Mhede akizungumza wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti 1000 kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo. Uzinduzi huo umefanyika leo Aprili 12,2023

************


WAKALA wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART), imepanga kupanda miti zaidi ya 1,000 kwenye kilomita 154 ambayo miundombinu ya mabasi yake inapita jijini hapa.


Hayo yalisemwa leo Aprili 12,2023 jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa DART, Dkt. Edwin Mhede, wakati wa uzinduzi wa upandaji wa miti hiyo kwenye kituo cha mabasi ya mwendo kasi Ubungo.


Hafla hiyo pia ilihudhuriwa na Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba na viongozi mbalimbali wa mkoa wa Dar es Salaam wamiwemo wa benki ya NMB.


Dk. Mhede alisema kabla ya ujenzi wa miundombinu ya mwendokasi kulikuwa na uoto wa asili na miti ya aina mbalimbali hivyo DART inawajibika kuirejesha hali ilivyokuwa.


“Sisi tunapojenga barabara kwa kiasi kikubwa tunaharibu uoto wa asili na miti kwasababu kama kulikuwa na mti tunaukata na nyinyi mliokuwa Dar es Salaam wakati huo naamini mnakumbuka hali ilivyokuwa hapa Ubungo kabla ya ujenzi huu, ile hali haipo tena ndiyo sababu tunaona tunawajibika kuirejesha,” alisema Dk. Mhede


Alisema asilimia 45 ya wakazi wa Dar es Salaam wanatumia njia za kwenda kwa miguu (shoroba), ambazo kwa sasa hazina miti ambayo zamani iliwasaidia kupita kivulini hali ambayo alisema lazima irejelezwe.


“Nitoe wito kwa watumiaji wa hizi njia za kwenda kwa miguu waitunze hii miti kwasababu itakuwa msaada mkubwa kwao tumeanza kupanda miti leo lakini tutaendelea mpaka kufikia miti zaidi ya 1,000,” alisema


Naye Mkuu wa Wilaya ya Ubungo, Hashim Komba, alisema uzinduzi wa upandaji miti hiyo ni jambo kubwa na la kihistoria kwa wakazi wa Ubungo na jijini Dar es Salaam kwani itasaidia kwa kiwango kikubwa kurejeleza mazingira yaliyoharibiwa kutokana na shughuli mbalimbali za ujenzi.


“Mazingira ni uhai hivyo ukiyahifadhi mazingira na yenyewe yatakuhifadhi ukiyaharibu na yenyewe yatakuadhibu kwa hiyo natoa wito kwa wananchi wa Ubungo waunge mkono kampeni hii kwa kutunza miti itakayopandwa, kila mtu ambaye miti hii itapandwa mbele ya nyumba yake au eneo lake la biashara atawajibika kuitunza” alisema


Mkuu huyo wa Wilaya alisema alishatoa maelekezo kwa viongozi wa mitaa na kata kuitambua miti hiyo na kuitunza kwa hali na mali itakapopandwa na DART na wafanyabiashara ndogo ndogo wafanye biashara zao sehemu ambazo hazina miti.


“Wafanyabiashara ndogo ndogo lazima wajue umuhimu wa kutunza mazingira kwaajili yao na vizazi vijavyo na wakumbuke kwamba ukiyalinda mazingira na yenyewe yatakulinda kwa hiyo kila mmoja wetu awe mlinzi wa mazingira kwa kuhakikisha miti hii inastawi,” alisema


Aliwataka watanzania kuona fahari ya kupanda miti kwa kushiriki vyema kwenye kampeni ya upandaji miti kwa Mkoa mzima akisema kuwa hata yeye binafsi amekabidhiwa mti ambao ameupanda na kuuwekea alama kwaajili ya kuhakikisha anafuatilia ukuaji wake.


“Huu mti ambao nimeupanda leo nimeagiza wauwekee alama ili niwe naupitia mara kwa mara kuumwagilia na kuuwekea mbolea na mti huu utakapokuwa nitakuwa nimetoa mchango mkubwa kwa taifa katika kuhifadhi mazingira,” alisema


Alisema viongozi wa kitaifa, Rais Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais, Dk. Phillip Mpango na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, wamekuwa mstari wa mbele kuhamasisha upandaji wa miti kwaajili ya kuhifadhi mazingira hivyo wananchi wanapaswa kuiga mfano huo na kupanda miti.




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger