Tuesday, 20 July 2021

MAHAKAMA YAAMURU MIILI YA WATU 61 WASIOJULIKAN IZIKWE HARAKA IWEZEKANAVYO

Mahakama Kuu nchini Kenya imeamuru miili 61 ya watu wasiotambulika katika mochwari mbali mbali za hospitali za kaunti ya Kisumu zizikwe haraka iwezekanavyo.

Afisa mkuu wa afya kaunti hiyo Fredrick Olouch ameambia vyombo vya habari kwamba miili hiyo imezikwa katika makaburi ya pamoja katika makaburi mbali mbali ya umma kaunti hiyo. 

Oluoch pia alisema kuna miili mingine 16 ambayo itazikwa endapo familia hazitajitokeza kuwatambua jamaa zao kwa kipindi cha wiki moja.

Afisa huyo alisema kati ya miili hiyo ambayo haijatambulika, 13 imehifadhiwa katika hospitali ya rufaa ya Kisumu na mingine katika hospitali tofauti katika kata ndogo ya Ahero.

Oluach alisema notisi ilikuwa imetolewa kwa umma lakini familia hazijafika kuchukua miili ya jamaa zao na sasa kilichosalia ni kuizika ili kupunguza msongamano kwenye mochwari. 

Serikali awali ilikuwa imeagiza hospitali kutohifadhi miili kwa zaidi ya saa 48 ikiwa ni mojawapo wa masharti yaliowekwa ya kuzuia na kudhibiti maambukizi ya COVID-19. 

Vifo vingi vinazidi kurekodiwa nchini kutokana na maambukizi ya virusi hivyo, kufikia sasa visa vya maambukizi vilivyorekodiwa nchini ni 193,189 na sampo zilizopimwa ni 2,059,193.

CHANZO - TUKO NEWS
Share:

DC KISWAGA ATANGAZA MAONESHO MAKUBWA YA WAWEKEZAJI, WAFANYA BIASHARA NA WAJASIRIAMALI ZAIDI YA 450 KAHAMA

Mkuu wa wilaya ya Kahama , Festo Kiswaga akielezea kuhusu maonesho ya biashara ya kimkakati ya wawekezaji, wafanyabiashara na wajasiriamali yatakayofanyika Mjini Kahama kuanzia Julai 30,2021 hadi Agosti 8,2021
Na Patrick Mabula , Kahama.

Serikali wilayani Kahama imeandaa maonesho ya biashara ya kimkakati ya wawekezaji , wafanyabiashara na wajasiriamali wapatao zaidi ya 450 wa ndani na nje ya nchi kwa lengo ya kukuza uchumi na masoko.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 20,2021 ofisini kwake Mkuu wa wilaya ya Kahama , Mhe. Festo Kiswaga amesema maonesho hayo yatafanyika kwa siku kumi kuanzia tarehe Julai 30  hadi Agosti 8,2021 katika Viwanja vya Kahama Mji Zamani (Nyihogo Mjini Kahama) kwa lengo la kutangaza fursa za kiuchumi na uwekezaji zilizopo wilayani Kahama.

Amesema maonesho hayo makubwa ya uwekezaji na biashara yanayoandaliwa na serikali ya wilaya ya Kahama , pamoja na halmashauri zote tatu zilizopo ambazo ni Ushetu , Msalala na Manispaa ya Kahama yanakidhi vigezo vyote vya kibiashara kutokana na fursa mbalimbali za kiuchumi na masoko zilizopo wilayani Kahama.

Kiswaga amesema wilaya ya Kahama yenye watu wanaokadiriwa kuwa zaidi ya milioni moja kwa mujibu wa sensa ya taifa ina vigezo vyote vya uwekezaji katika swala ya kibiashara kutoka na kuwepo kwa fursa nyingi za kiuchumi kwenye madini , kilimo , mifugo na biashara na ipo katika barabara kuu ya rami inayounganisha nchi za maziwa makuu na kiwanja cha ndege.

Amesema maonesho hayo ya kimkakati mbali na kuhusisha washiriki hao zaidi ya 450 pia yanahusisha taasisi zote za umma na serikali pamoja na wadau mbalimbali wa maendeleo na kwa kuzingatia fursa za kiuchumi zinazopatikana katika sekta ya madini, kilimo, ujenzi wa viwanda, elimu, burudani na michezo lengo kufungua masoko kiuchumi.

"Ndugu zangu waandishi wa habari katika maonyesho hayo kutakuwa na mikutano ya kibiashara , mafunzo mbalimbali ya elimu toka taasisi za umma na binafsi na za kifedha zinazohudumia wafanyabiashara na wajasiriamali ili kuwajengea uwezo wa kuwa tija katika shughuli zao", amesema Kiswaga.

Kiswaga amesema wito wake kwa wawekezaji , wafanyabiashara na wajasiriamali na wananachi wote kujitokeza kushiriki ili kuwa na tija kwa maslahi mapana katika kukuza uchumi wao na taifa.


Amesema pia maonesho hayo yatatoa fursa ya watu kuona wanyama pori wakiwemo simba , chui, fisi , mamba  na kobe wakubwa kwa lengo la kuhamasisha utalii wa ndani.

Kwa upande wao baadhi ya wadau, Simon Cheyo katibu wa TCCIA wa wilaya ya Kahama na Afisa wa kampuni ya GS1 Tanzania  wanaojihusisha na kuweka alama ya utambuzi wa bidhaa , Shabani Mikongoti wamesema maonesho hayo ya kimkakati wa elimu na biashara yatawasaidia sana wawekezaji na wafanyabishara.

Nao baadhi ya wafanyabishara walioshiriki  katika kikao na mkuu wa wilaya akiwemo Charles Daud amesema maonesho hayo yatawasaidia sana kuwa na tija kutokana na fursa mbalimbali zitakazotolewa kwa kile alichodai kuwa siku za nyuma walikuwa wamekata tamaa ya kuendelea na biashara.
Mkuu wa wilaya ya Kahama , Festo Kiswaga akielezea kuhusu maonesho ya biashara ya kimkakati ya wawekezaji, wafanyabiashara na wajasiriamali yatakayofanyika Mjini Kahama kuanzia Julai 30,2021 hadi Agosti 8,2021





Share:

TACH Operations Officer at Absa

TACH Operations Officer     Bring your possibility to life! Define your career with us With over 100 years of rich history and strongly positioned as a local bank with regional and international expertise, a career with our family offers the opportunity to be part of this exciting growth journey, to reset our future and shape […]

This post TACH Operations Officer at Absa has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Programme Coordinator at Prime Minister’s Office

Programme Coordinator    AFDP Programme July, 2021 Ref. No.EA.9.355/02/31 Prime Minister’s Office invites dynamics and suitable qualified Tanzanians to fill various posts in Coordination Unit of Agriculture and Fish­eries Development Programme- AFDP as mentioned below: PROGRAMME COORDINATOR-1 POST Programme Coordinator that will be liaising with the Focal Persons in Ministries of Agriculture, Ministry of Livestock […]

This post Programme Coordinator at Prime Minister’s Office has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

JAJI MKUU PROF. JUMA AKIPONGEZA CHUO CHA UONGOZI WA MAHAKAMA LUSHOTO KUANDAA KITABU CHA MKUSANYIKO WA MASHAURI YA WATOTO


Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma
Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaohudumia Watoto (UNICEF), Bi. Sampathi Perera.

Na Rosena Suka IJA Lushoto
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma ametoa pongezi kwa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto kwa kuandaa Kitabu cha Mkusanyiko wa Mashauri ya Watoto (Compendium of Child Justice Cases) pamoja ripoti ya tathmini ya mafunzo kwa wadau wa haki za watoto (report on the impact assessment of trainings to juvenile justice frontline workers).

Jaji mkuu wa Tanzania. Mhe. Prof. Juma ametoa pongezi hizo kwenye uzinduzi wa kitabu hicho uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam, leo Julai 19, 2021. Kitabu hicho kilichoandaliwa na Chuo cha Uongozi wa Mahakama kwa kushirikiana na Mahakama ya Tanzania kupitia ufadhili wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia masuala ya mtoto (UNICEF).

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mhe. Jaji Prof. Juma amezitaka mamlaka zinazosimamia na kutetea haki za mtoto kufanya kazi kwa kushikiana pamoja na kushiriki katika mafunzo mbalimbali yanayohusu mada za uendeshaji ya mashauri ya mtoto ili kuweza kuboresha mfumo wa ufatiliaji madai ya haki za mtoto kwa kushirikiana na mahakama nchini.

Mhe. Jaji Prof. Juma aliendelea kwa kusema kuwa wadau wa haki ya mtoto wanapaswa kushilikiana katika kutoa kipaumbele kwa masilahi ya haki za mtoto. Profesa IBrahimu amesema kuwa haki ya ulinzi pamoja na ustawi wa mtoto hauwezi kupatikana kwa kuiachia chombo cha mahakama peke yake bali inapatikana katika mfumo jumuishi wa haki ya mtoto ambao ni kivuli katika kuhakikisha usitawi na maendeleo ya mtoto,

Kwa upande mwingine, Mhe. Jaji Prof. Juma alitoa wito kwa Waheshimiwa Majaji Wafawidhi wa kanda zote nchini, Mahakimu Wafawidhi wa Mikoa na Mahakama za Wilaya kuhakikisha kuwa wanapata nakala za kitabu hicho katika ofisi zao kwa ajili ya matumizi yao ili kusaidia kufanya rejea inapotakiwa kufanya hivyo.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto Mhe. Dkt. Paul Kihwelo Jaji wa Mahakama ya Rufani amesema kwa kushirikiana na Mahakama kuu ya Tanzania chini ya ufadhili wa Shirika la kuhudumia watoto dunia UNICEF uongozi wa chuo umekuwa ukiendesha mafunzo mbalimbali yanayohusu namna bora ya usimamizi wa kesi za mtoto mahakamani. 

 Mhe. Dkt. Kihwelo amesema kuwa Chuo cha Uongozi wa Mahakama kimekuwa kikifanya tathimini katika kanda zote za mahaka kuu ili kuhakisha wadau mbalimbali walioshiriki kwenye mafunzo ya haki za mtoto wanaendelea kuwa na uelewa mkubwa katika kujuwa namna ya kusimamia kesi za madai kwa watoto mahakamani.

Mhe. Dkt Kihwelo aliendelea kwa kusema kuwa, hata hivyo kitabu cha mkusanyiko wa kesi za watoto kimetayalishwa kwa lengo la kurahisisha upatikanaji wa maamuzi mengi ya mahakama za juu kuhusu haki za watoto kwa maafisa wa mahakama pamoja wadau wa wengine wa haki za mtoto ili kuweza kuongeza uelewa wa maamuzi mbalimbali yanayohusu haki ya mtoto mahakamani kupitia sheria ya mtoto ya mwaka 2009.

Akitaja faida kadhaa za kitabu hicho, Mhe. Jaji Mkuu alisema kuwa kitabu hiki kinakumbusha kuwa, zipo sheria nyingi zaidi ya Sheria ya Mtoto ya 2009 [Law of the Child Act Na. 21 ya 2009], na kuwa Haki Mtoto haipatikani ndani ya Sheria moja tu bali kuna vifungu vya Katiba, Sheria mbalimbali, Kanuni, Taratibu, Mazoea na vigezo vingi ambazo kwa pamoja vinaleta mtirirko wa kufahamu mapana na marefu ya Haki ya Mtoto.


Kwa upande wake Mwakilishi kutoka Shirika la Umoja wa Mataifa linaohudumia Watoto (UNICEF), Bi. Sampathi Perera alitoa pongezi nyingi kwa Mahakama ya Tanzania na Chuo cha Uongozi wa Mahakama kwa kufanikiwa kuzindua kitabu hicho na kueleza kwamba uzinduzi wa kitabu hiki mafanikio makubwa sana kwani itawawezesha Majaji na Mahakimu kuendelea kutoa maamuzi sahihi kuhusu mashauri ya Watoto.

Uzinduzi huu ni sehemu ya utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama (IJA) 2018/2019-2022/2023 wa kuwajengea uwezo wadau wa sekta ya sheria nchini.

Uzinduzi huo umehudhuriwa na wadau mbalimbali wa sekta ya Sheria nchini wanaohusika na haki za mtoto wakiwemo Majaji wa Mahakama ya Rufani, Majaji wa Mahakama Kuu, Mahakimu wa ngazi mbalimbali, Wawakilishi wa Taasisi za Serikali, Wawakilishi kutoka Mashirika yasiyo ya Serikali na Wawakilishi wa UNICEF.

Share:

Wimbo Mpya: MBOSSO – MTAALAM

 Wimbo Mpya Mbosso – Mtaalam




Share:

KAMANDA MULIRO : USIMILIKI SILAHA KAMA HUNA SIFA


Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam Jumanne Muliro amesisitiza kuwa sio sifa kumiliki silaha endapo huna sifa za kuimiliki.

Amesema umiliki wa silaha una sheria zake na endapo mmiliki anazikiuka hatua za kisheria zinachukuliwa dhidi yake ikiwa ni pamoja na kifungo cha miezi 12 jela au faini ya shilingi milioni moja au vyote kwa pamoja.

Kamanda Muliro ametoa kauli hiyo kufuatia matukio la mauaji yaliyotokea hivi karibuni katika maeneo ya Sinza Mori na Mbezi Makabe mkoani Dar es Salaam, ambapo pia amewataka Viongozi wa Serikali za mitaa na wamiliki wa maeneo ya starehe kushirikiana na jeshi la polisi kuwafichua wahalifu katika maeneo yao ili kuepusha madhara yanayoweza kuwapata Wananchi.

Amewaambia Waandishi wa habari mkoani Dar es salaam kuwa jeshi hilo lina jukumu la kulinda raia na mali zao, hivyo ushirikiano wa Wananchi ni muhimu katika kufanikisha jambo hilo.

Katika tukio lililotokea tarehe 17 mwezi huu katika baa ya Lamax Sinza, mteja anayejulikana kwa jina la Alex korosso maarufu kama simba alimpiga risasi kijana aliyetambuliwa kwa jina la Gift Mushi kabla ya yeye kujipiga risasi shingoni na kufariki dunia papo hapo.

Kuhusu mtu aliyetekeleza mauaji katika eneo la Mbezi Makabe Kamanda Muliro amesema Jeshi la Polisi lipo kwenye hatua za mwisho ili kumfikisha mahakamani mtuhumiwa kwa mujibu wa sheria.



Share:

Evaluation and Knowledge Management Officer at Prime Minister’s Office

Monitoring, Evaluation and Knowledge Management Officer    Prime Minister’s Office -AFDP Programme Ref. No.EA.9.355/02/31 Prime Minister’s Office invites dynamics and suitable qualified Tanzanians to fill various posts in Coordination Unit of Agriculture and Fish­eries Development Programme- AFDP as mentioned below: MONITORING, EVALUATION AND KNOWLEDGE MANAGEMENT OFFICER Under the direct supervision of the Programme Coordinator, the […]

This post Evaluation and Knowledge Management Officer at Prime Minister’s Office has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Procurement Officer at Prime Minister’s Office

Procurement Officer     Ref. No.EA.9.355/02/31 Prime Minister’s Office invites dynamics and suitable qualified Tanzanians to fill various posts in Coordination Unit of Agriculture and Fish­eries Development Programme- AFDP as mentioned below: Procurement Officer should perform his duties by adhering to procurement guidelines set out in the Public Procurement Act. MAIN DUTIES AND RESPONSIBILITIES Undertake or […]

This post Procurement Officer at Prime Minister’s Office has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Halmashauri Zatakiwa Kuandaa Hati Zisizopungua 100 Kila Mwezi


Na Munir Shemweta, SUMBAWANGA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ametoa agizo kwa kila halmashauri nchini kutoa hati zisizopungua mia moja kwa kila mwezi.

Akizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi katika mkoa wa Rukwa tarehe 19 Julai 2021 akiwa katika ziara ya kukagua utendaji kazi sekta ya ardhi nchini, Dkt Mabula alisema halmashauri kupitia idara zao za ardhi zinatakiwa kuandaa hati zisizopungua mia moja kwa mwezi katika yale maeneo ambayo viwanja vyake vimepimwa.

‘’kule ambako viwanja havijapimwa watendaji wake wanaweza kueleweka lakini mtu ana viwanja mia moja halafu anashindwa hati za idadi hiyo na wakati mwingine anatoa hati kumi tu huku akiwa amejiwekea lengo la kutoa hati mia moja’’ alisema Naibu Waziri wa Ardhi.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, hatimiliki za ardhi zisipotoka na kumilikisha kwa wamiliki wa ardhi migogoro haitaisha na matokeo yake ni kuwepo umilikishaji mara mbili (Double allocation).

Alimtaka Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Rukwa Swagile Mfinanga kumpatia taarifa ya uandaaji hati kwa kila halmashauri yake kufikia mwisho wa mwezi wa nane na kusisitiza kuwa, hatu hiyo pia itafika mikoa yote kwa kuangalia idadi ya viwanja vingapi vimepimwa na wamiliki wangapi wameomba lakini hawajapatiwa na kama hawajaomba mara ngapi watendaji wa sekta ya ardhi katika halmashauri husika wamekwenda kuahamasisha ili wamiliki waombe kupatiwa hati.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri wa Ardhi nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula aligawa Ankara za malipo ya kumilikishwa ardhi kwa baadhi ya wananchi wapatao 593 waliopimiwa maeneo yao katika kata ya Momoka Manispaa ya Sumbawanga mkoa wa Rukwa.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliwaambia wakazi wa kata ya Momoka katika manispaa ya Sumbawanga kuwa, wamefanya jambo zuri la kukubali kupimiwa maeneo yao ili baadaye waweze kumilikishwa na Wizara ya Ardhi inawaunga mkono kwa kuwa uamuzi waliofanya utawasaidia kuepukana na migogoro ya mipaka na wakati huo kutumia hati watakazopata katika shughuli za maendeleo kama vile kuchukulia mikopo benki.



Share:

Waziri Biteko Auagiza Mgodi Kulipa Deni La Kijiji Ndani Ya Siku 60


 Na. Steven Nyamiti, Mara
Waziri wa Madini, Doto Biteko ameuagiza uongozi wa kampuni ya uchimbaji wa madini ya Dhahabu MMG GOLD LIMITED unaomilikiwa kwa ubia kati ya Kampuni ya MMG na Polygon kulipa deni la kiasi cha shilingi milioni 36 zinazodaiwa na kijiji kwa mujibu wa mkataba wa uwekezaji.

Agizo hilo amelitoa, Julai 19, 2021 wakati akiwa kwenye ziara ya kukagua shughuli za uchimbaji katika mgodi wa MMG GOLD LTD katika kijiji cha  Seka kata ya Nyamlandililila wilaya ya Musoma Vijijini , Mkoani Mara.

Akizungumza na Mkurugenzi wa mgodi  huo Yury Chernomorchenko, Waziri Biteko ametoa miezi miwili deni hilo liwe limelipwa na kampuni hiyo.

Biteko amesema kuwa, kampuni hiyo ilikuwa inadaiwa zaidi ya shilingi milioni 60 toka mwaka 2018 na Serikali ya kijiji kama ushuru, deni lililoachwa na menejimenti iliyopita ya MMG ambapo walilipa fedha kiasi na hadi sasa deni linalodaiwa ni shilingi milioni 36 na kijiji kwa mujibu wa mkataba wa uwekezaji.

“Niwaombe Serikali za mitaa, Vijiji na Halmashauri, makubaliano yoyote wanayoingia na migodi ili yaweze kuwa na nguvu ya Kisheria kwa msimamizi wa migodi ni lazima wayasajili makubaliano hayo kwenye ofisi ya madini.” amesisitiza Biteko

“Tunataka tuone haya manufaa ya mgodi huu yaweze kuonekana kwenye maisha ya kawaida ya wananchi kwenye miundombinu ya barabara, miundombinu ya elimu na afya”

Pia, amemuagiza Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara Nyaisara Mgaya  kuhakikisha anasimamia malipo hayo yanafanyika ndani ya muda hu ona endapo hayataliwa asimamishe shughuli zote katika mgodi mpaka deni litakapolipwa.

Akiwa kwenye mgodi wa uchimbaji Dhahabu wa Cata Mining Waziri Biteko ameagiza uongozi wa mgodi huo kuzingatia Sheria na Kanuni  za madini zilizopo hapa nchini hususan wanapofanya ununuzi wa bidhaa mbalimbali na wanapotafuta kampuni za kufanyanazo kazi kwenye mgodi.

Msipozingatia sheria za madini mtapigwa faini ya shilingi milioni 50 jambo  ambalo Serikali ya awamu ya Sita haipendi, tunataka kuwalea  ili mkue zaidi siyo kuwarudisha nyuma,” amesema Waziri Biteko.

Akijibu swali la waziri kuhusu ajira kwa wazawa, Mkurugenzi wa Mgodi huo Johann Christoffel amesema hadi sasa wana watumishi 470 ambao ni wazawa jambo ambalo limepongezwa na Waziri Biteko.

Hata hivyo amewashauri wanapoajiri wazawa watoe kipaumbele kwa wakazi wa maeneo yanayozunguka mgodi wa Cata ili kuweka mazingira mazuri ya kiuhusiano na jamii.

Waziri Biteko amefanya ziara ya siku moja Mkoani Mara na kutembelea migodi miwili ya MMG Gold Limited na Cata Mining. Mkoa wa Mara umebarikiwa kuwa na aina nyingi za Madini ambayo ni dhahabu, shaba, Silver, chuma, chokaa, soapstone na madini ya ujenzi. Kati ya hayo madini yanayopatikana kwa wingi zaidi ni madini ya dhahabu.


Share:

Naibu Waziri wa Ardhi aagiza mamlaka za upangaji nchini kuandaa mipango kabambe ya maeneo yao kwa kutumia wataalamu wa ndani


Na Munir Shemweta, SUMBAWANGA
Naibu Waziri wa Ardhi nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ametoa rai kwa mamlaka za upangaji nchini kuandaa mipango kabambe ya maeneo yao kwa kutumia wataalamu washauri au wataalamu wa ndani kadri ya uwezo wa mamlaka husika.

Aidha, amezielekeza halmashauri ambazo zimeanzisha mchakato wa kuandaa Mipangop Kabambe kuongeza jitihada kukamilisha kazi hizo na wataalamu watekeleze majukumu yao kwa weledi.

Naibu Waziri Mabula alitoa rai hiyo tarehe 19 Julai 2021 wilayani Sumbawanga wakati akizindua Mpango Kabambe wa Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa.

Alisema, mipango kabambe inaongeza kasi ya kupanga na kupima miji yetu sambamba na kuondoa changamoto mbalimbali zikiwemo za migogoro ya matumizi ya ardhi , ukuaji wa makazi yasiyo rasmi , uharibifu wa miundombinu  na mazingira,  kukuza fursa za uwekezaji pamoja na kuongeza ajira kwa wananchi wa manispaa ya Sumbawanga.

‘’ kama tunavyojua Tanzania imepimwa kwa kiwango kisichozidi asilimia 25 na kama tumeenda mbali tunasogea asilimia 30 lakini tunavyoendelea kuweka mipango midogomidogo kulingana na mamlaka husika tutajikuta tumepnga nchi nzima na wizara ya ardhi imejipanga katika hilo’’ alisema Dkt Mabula.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Ardhi, kukamilika kwa Mpango Kabambe wa Manispaa ya Sumbawanga kumekuja wakati muafaka maana pamoja na kutumika kama chombo cha kuongoza na kusimamia uendelezaji mji pamoja na kudhibiti  ujenzi holela pia utatoa uhakika wa uwekezaji kwenye halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga..

Alitoa wito kwa halmashauri zote nchini ambazo hazijaandaa Mipango Kabambe ya miji yao kuiga mfano wa Manispaa ya Sumbawanga ili kuongeza kasi ya kupanga na kupima miji yote nchini.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, hadi sasa kuna jumla ya mipango kabambe 26 iliyoandaliwa katika mamlaka za upangaji na kuidhinishwa na wizara na zoezi la kuizindua linaendelea. Hata hivyo, tayari mipango kabambe ya jiji la Dodoma, Manispaa za Mtwara Mikindani, Musoma , Iringa, Singida , Tabora na Miji ya Njombe na Tunduma imekamilika na kuzinduliwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga Jacob Mtalitinya alisema, Mpango Kabambe wa Manispaa yake utekelezaji wake upo katika awamu nne za miaka mitano mitano ambapo jumla ya miradi 12 ilitarajiwa kutekelezwa katika awamu ya kwanza (2015/2020) na baadhi yake ni kituo cha mabasi Katumba, kufungua miji ya pembeni pamoja na mpango wa urasimishaji makazi holela



Share:

Communications Officer at World Vegetable Center

Communications Officer     The World Vegetable Center is a non-profit, autonomous international agricultural research center with headquarters in Taiwan and five regional offices around the globe. The World Vegetable Center conducts research and development programs that contribute to realizingthe potential of vegetables for healthier lives and more resilient livelihoods. For more information, please visit our […]

This post Communications Officer at World Vegetable Center has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Welfare Manager at Unilever

 Welfare Manager – UTT     Purpose of the Role The role exists to ensure the delivery of UTT’s welfare priorities providing advice, guidance and practical support in the implementation of the Company’s Strategy & people agenda in line with our values of respect, pioneering, integrity and responsibility to ensure the safety and wellbeing of all […]

This post Welfare Manager at Unilever has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Food Safety Officer at Agricycle Global Inc

Food Safety Officer     As our Food Safety Officer, you will report to the Food Safety Manager based in Kenya and Operations Coordinator in Tanzania and work closely with a team of  Field Officers and Sourcing Officers. You will be responsible for developing, and managing the Food Safety Management System by ensuring ongoing compliance and […]

This post Food Safety Officer at Agricycle Global Inc has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Database Officer at Agricycle Global Inc

Database Officer     As our Database Officer, you will report to the Impact Coordinator, and will work closely with the department Coordinators and Field Officers. You will be responsible for inputting and managing data regarding our growing network of smallholders and cooperatives across East Africa with reliability, diligence and attention to detail. You will lead […]

This post Database Officer at Agricycle Global Inc has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JULAI 20,2021




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger