Thursday, 28 January 2021

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 28,2021



Magazetini leo Alhamis January 28,2021





























Share:

Wednesday, 27 January 2021

VIDEO YA UCHI MCHUNGAJI AKIWA NA WAUMINI WAKE YAVUJA MTANDAONI....MWENYEWE AFUNGUKA


Mchungaji mmoja kutoka eneo la Nkpor, Idemili Kaskazini lililopo katika jimbo la Anambra nchini Nigeria, kwa jina Onye Eze Jesus, ameomba msamaha kwa umma kwa video yake ya utupu iliyosambaa sana mitandaoni ambapo alionekana akiwadondoshea fedhaa baadhi ya waumini wa kanisa lake huku akiwaombea wakati hajavaa nguo wakiwa katika mto.

Onye Eze Jesus ameomba radhi kwa kupeperusha fedha namna ile pamoja na kuonesha watu wakiwa hawajavaa nguo katika mitandao ya kijamii na kusema kuwa hatorudia tena.

"Ninawaomba radhi raia wa Nigeria na kila mtu kwa kosa la kupeperusha fedha kwa namna ile pamoja na kuwaonesha watu wakiwa hawana nguo katika mitandao ya kijamii.

Ilienda mtandaoni kimakosa na haitajirudia tena. Kuna watu wanaweka taarifa katika kurasa yangu na nilipogundua nilifuta haraka lakini kumbe baadhi ya watu tayari walikuwa wameishirikisha kwa wengine."

Mchungaji huyu ameomba radhi mara baada ya mamlaka ya jimbo la Anambra, ambayo imetoa onyo kali dhidi ya kutumia dini katika mambo yasiyo na maadili.
Onye Eze ni mchungaji wa jimbo la Anambra

Kamishina wa jimbo la Anambra ,Don Adinuba alisema alipata madai kuwa mchungaji huyo alikuwa anasaidia watu kuinua uchumi wao kwa njia za miujiza.

Wafuasi wake huwa wanamwagiwa fedha mara kwa mara kwenye mto na wafuasi hao kuoga mtoni wakiwa hawana nguo.

Suala la kuwaweka katika mitandao ya kijamii

Kwa waumini hao kuonekana mtandaoni ni jambo la aibu kwa jimbo hilo kwa ujumla, watu wa Anambra wanajulikana duniani kuwa ni watu wenye kupenda kufanya kazi.

"Onyeze Jesus anahamasisha mambo ya kishirikina, kusadikika na imani za potofu ambazo si nzuri katika jamii; ndugu zangu, marafiki na wafanyabiashara hizi nguvu za giza zinatupeka kubaya.

Masuala ya kishirikina kama haya yanaweza kuleta uadui bila sababu ya msingi na watu wanaweza kugombana hata kuuana bila sababu ya msingi.

Nimelazimika kukemea tabia hii na kuchukua hatua dhidi ya watu wazima waliopiga picha wakiwa hawana nguo na waliosambaza video hiyo,

Mchungaji Onyeze Jesus yuko hatiani kwa kuwanyima wafuasi wake haki ya kulinda utu wao na kukiuka sheria ya Nigeria kwa kuhamasisha mambo ambayo yapo kinyume na maadili."

Mchungaji huyo alikuwa anawahidi wafuasi wake kuwa wanaweza kuwa mamilionea kwa usiku mmoja tu na kutokana na mambo kama hayo serikali itachukua hatua madhubuti.

Onye Eze Jesus aliomba radhi na kuelezea kuwa anafanya kazi tofauti na wachungaji wengine lakini vilevile aliomba radhi kwa kumwaga fedha kwa namna ile.

Aliongeza kusema kuwa tayari video hiyo ameifuta katika kurasa yake ingawa tayari imeshirikishwa na watu wengi.

Chanzo - BBC SWAHILI
Share:

ATUPWA JELA KWA KUMTWANGA CHUPA KICHWANI MWENZAKE DAR

Mahakama ya Wilaya ya Temeke mkoani Dar es Salaam, Tanzania, imemuhukumu kwenda jela miezi sita Mkazi wa Chang'ombe, Oscar Sanga baada ya kukiri kosa la kumshambulia kwa chupa na kumjeruhi kichwani Justa Paskal.

Hukumu hiyo imesomwa leo Jumatano Januari 27, 2021 na Hakimu Mkazi, Amos Rweikiza baada ya mshtakiwa huyo kukiri kosa lake.

Hakimu Rweikiza amesema Desemba 19, 2020 maeneo ya Temeke Sokota, mshtakiwa huyo alimshambulia kwa chupa na kumjeruhi Justa kinyume na kifungu cha 231 cha makosa Sheria namba 16 rejeo ya mwaka 2019.

Amesema kutokana na mshtakiwa kukiri kosa lake, mahakama hiyo imemkuta na hatia.

Via Mwananchi
Share:

NAIBU WAZIRI WA NISHATI ATEMBELEA UJENZI WA KITUO CHA KUPOZA UMEME KIGAMBONI


Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato akiongozana na Meneja wa Usafirishaji Umeme Makao Makuu ya Tanesco, Mhandisi Neema Mushi wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme wa gridi ya taifa kinachojengwa wilayani Kigamboni kikigharimu jumla ya shilingi Bilioni 26. 
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Usafirishaji Umeme Makao Makuu ya Tanesco, Mhandisi Neema Mushi wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme wa gridi ya taifa kinachojengwa wilayani Kigamboni kikigharimu jumla ya shilingi Bilioni 26. 
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Usafirishaji Umeme Makao Makuu ya Tanesco, Mhandisi Neema Mushi  wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme wa gridi ya taifa kinachojengwa wilayani Kigamboni kikigharimu jumla ya shilingi Bilioni 26 kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni Bi.Sarah Msafiri. 
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato akioneshwa transfoma kubwa ya umeme na Meneja wa Usafirishaji Umeme Makao Makuu ya Tanesco,Mhandisi Neema Mushi wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme wa gridi ya taifa kinachojengwa wilayani Kigamboni kikigharimu jumla ya shilingi Bilioni 26. 
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato akioneshwa mitambo mbalimbali ya kupoza umeme iliyofungwa kwenye kituo hicho na Meneja wa Usafirishaji Umeme Makao Makuu ya Tanesco ,Mhandisi Neema Mushi wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme wa gridi ya taifa kinachojengwa wilayani Kigamboni kikigharimu jumla ya shilingi Bilioni 26. 
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato akioneshwa mifumo mbalimbali inayofungwa katika kituo hicho cha kupoza umeme na Meneja wa Usafirishaji Umeme Makao Makuu ya Tanesco, Mhandisi Neema Mushi wakati alipotembelea mradi wa ujenzi wa kituo cha kupoza umeme wa gridi ya taifa kinachojengwa wilayani Kigamboni kikigharimu jumla ya shilingi Bilioni 26. 
Baadhi ya mitambo iliyofungwa katika kituo hicho inavyoonekana. 
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato pia ametembelea mitambo ya kufua umeme wa gesi Kinyerezi II na kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa katika mitambo hiyo. 
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato akipokea taarifa ya uzalishaji katika mitambo hiyo. 
Mhandisi Innocent Luoga akimuongoza Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Stephen Byabato wakati alipokuwa akitembelea mitambo ya kuzalisha umeme ya Kinyerezi II.
Share:

MUME AUA MKE WAKE KWA KUMPIGA NGUMI NA MTWANGIO SHINYANGA

Share:

UMMY MWALIMU : IPO HAJA YA KUZIJENGEA UWEZO HALMASHAURI ZIWE NA USIMAMIZI MZURI WA TAKA KATIKA MADAMPO


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu amesema ipo haja ya kuzijengea uwezo halmashauri zote nchini ili ziweze kuwa na usimamizi mzuri wa taka katika madampo.

Ummy amesema hayo leo Januari 27, 2021 wakati akiwasilisha Taarifa kuhusu muundo wa Ofisi ya Makamu wa Rais na Utekelezaji wa Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo inayosimamia utekelezaji wa majukumu ya uhifadhi na usimamizi wa mazingira mbele ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira katika Ofisi za Bunge jijini Dodoma.

Alisema kuwa kumekuwepo na changamoto ya kutokuwepo na usimamizi mzuri wa taka zinazotupwa katika madampo na badala yake zinaachwa na kurudi kwenye makazi ya watu hali inayohatarisha afya zao.

"Halmashauri zikifanya sorting (kutenganisha) aina za taka kwa mfano chupa za plastiki zinapelekwa viwandani kurejelezwa, taka za mabaki ya chakula zinafanya kuwa mbolea tutakuwa tumefanikiwa kusimamia na kudhibiti taka kwenye madampo", alisema Ummy.

Alitaja mikakati itakayokelezwa kuwa ni pamoja na kuhamasisha usimamizi na udhibiti wa taka kwa kutumia dhana ya Punguza, Tumia tena na Rejeleza kwa lengo kupunguza gharama za usimamizi na udhibiti wa taka katika mamlaka za Serikali za Mitaa.

Pia waziri huyo alisema Serikali itaimarisha usimamizi na hifadhi ya mazingira kwa ajili ya maendeleo endelevu pamoja na uratibu na utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Mazingira.

Kwa upande mwingine Waziri Umya alibanisha kuwa upo utegemezi mkubwa wa matumizi ya mkaa na kuni kama chanzo cha nishati ya kupikia pamoja na shughuli za kilimo zisizo endelevu jail inayosababisha ongezeko la uharibifu wa mazingira nchini.

Kutokana na hali hiyo alisema kuwa Ofisi ya Makamu wa Rais kwa kushirikiana na wadau imeendelea kuhamasisha kampeni ya upandaji miti, matumizi ya nishati mbadala kama gesi na kuweka mikakati ya uhamasishaji wa kilimo kinachozingatia uhifadhi wa mazingira.

Aliongeza kuwa Serikali imeweka mikakati ya kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala kwa ajili ya kupikia katika ngazi ya kaya na taasisi za umma na binafsi hususan taasisi za elimu na mafunzo, Magereza, na Majeshi. 
Share:

BENKI YA EXIM YAMWAGA ZAWADI ADA ZA SHULE, SAFARI ZA SERENGETI KWA WASHINDI WA CHANJA KIJANJA

Mkuu wa Idara ya Kidigitali na Huduma Mbadala wa benki ya Exim Bw Silas Matoi (Katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) wakati wa hafla ya kutangaza washindi wa kampeni ya benki hiyo ijulikanayo kwa jina la ya 'Chanja Kijanja na Exim Mastercard' iliyolenga kuhamasisha wateja wa benki hiyo kutumia kadi katika manunuzi ya mtandaoni au kufanya malipo kupitia mashine za malipo (POS). Wengine ni pamoja na Maofisa waandamizi wa benki hiyo Bw Callist Butinga (Kushoto) na Paritosh Babla.

Na Mwandishi wetu - Dar es salaam
Benki ya Exim hii leo imetangaza washindi wa kampeni yake ya 'Chanja Kijanja na Exim Bank Mastercard', huku ikigawa zawadi mbalimbali kwa washindi hao ikiwemo ada za shule pamoja na safari ya kutembelea hifadhi ya Serengeti kwa washindi wa jumla wa kampeni hiyo.

Kampeni hiyo iliyodumu kwa mwezi mmoja, ilianza Desemba mwaka jana, ikilenga kuhamasisha wateja wake kutumia kadi za MasterCard za benki hiyo wanapofanya manunuzi au malipo ya mahitaji muhimu kwenye maduka (Shopping) pamoja na ununuzi wa bidhaa kimataifa kupitia mtandaoni.

Kati ya washindi watatu wa jumla wa kampeni hiyo, ilishuhudiwa washindi wawili wakichagua zawadi ya kulipwa ada ya shule pamoja na vifaa vyote vya shule kwa mtoto mmoja kwa kila mshindi, wakati mshindi mmoja akichagua zawadi safari ya kutembelea Hifadhi ya Taifa Serengeti akiwa na mwenza wake huku kila kitu kikiwa kimelipiwa. 

“Benki ya Exim inaelewa changamoto ambazo wazazi wanakabiliwa nazo wakati wa kufungua shule. Wafanyakazi wetu wengi ni wazazi pia, kwa hivyo tunaelewa hizi changamoto. Tunaamini zawadi za namna hii zitapunguza mzigo wa kifedha kwa wazazi na walezi katika katika kipindi hiki. "alisema Mkuu wa Idara ya Kidigitali na Huduma Mbadala wa benki hiyo Bw Silas Matoi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kwenye hafla hiyo iliyofanyika makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es Salaam.

Alisema kampeni hiyo imehitimishwa kwa mafanikio makubwa yaliyotokana na muitikio mkubwa kutoka kwa wateja wa benki hiyo hatua ambayo inadhihirisha uhalisia wa huduma zinatolewa na benki hiyo kwa wateja wa benki hiyo.

"Kwa muitikio huu tumebaini ongezeko kubwa la matumizi ya huduma zetu za kidigitali kutokana mwenendo wa mfumo wa maisha wa wateja wetu kitu kinachotupa mrejesho muhimu utakaotusaidia kuendelea kubuni huduma bora zaidi zinazoendana na hitaji hilo la wateja wetu. Zaidi tunashukuru na kujivunia zaidi kuona kwamba wateja wetu wanafurahia huduma zetu kulingana na matarajio yao ambayo ni kupata huduma za haraka, rahisi na salama kwao,’’ aliongeza.

Zaidi Bw. Matoi alihamasisha wateja wa benki hiyo kuendelea kufurahia huduma za kidigitali hata baada ya kuisha kwa kampeni hiyo.

Kwa upande wao washindi Baraka Kimaro, Khamis Mansour na Mustafa Albaghdadi wote walionyesha furaha yao na shukrani baada ya kupokea habari za ushindi huo huku wakielezea kuridhishwa zaidi na uhakika na ubora wa huduma za kibenki ikiwemo zile za mtandaoni na kwenye matawi wanazopata kupitia taasisi hiyo.
Share:

TSC YAWAAGA WASTAAFU WAKE


Katibu Mstaafu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Winifrida Rutaindura (kulia), akipokea zawadi kutoka kwa Mwenyekiti wa TSC, Profesa Willy Komba, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wastaafu wa Tume, iliyofanyika Januari 26, 2021, mjini Morogoro. Wa kwanza kushoto ni Kaimu Katibu wa TSC, Moses Chitama.
Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Profesa Willy Komba, akitoa hotuba ya kufunga Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume, mjini Morogoro, Januari 26, 2021. Kushoto ni Kaimu Katibu wa TSC, Moses Chitama.
Katibu Mstaafu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), Winifrida Rutaindura, akizungumza na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume hiyo, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wastaafu iliyofanyika Januari 26, 2021 mjini Morogoro.
Baadhi ya watumishi wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC), waliostaafu na wanaotarajiwa kustaafu hivi karibuni, wakiungana na Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume, kuimba kwa furaha wakati wa hafla fupi ya kuwaaga wastaafu hao iliyofanyika Januari 26, 2021 mjini Morogoro.   Watumishi mbalimbali wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) waliostaafu na wanaotarajiwa kustaafu hivi karibuni, wakipokea zawadi kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume, Profesa Willy Komba, wakati wa hafla fupi ya kuwaaga iliyofanyika mjini Morogoro, Januari 26, 2021. *******************

Na Veronica Simba - TSC 
Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) imewaaga rasmi watumishi wake 10 waliostaafu na wale wanaotarajiwa kustaafu hivi karibuni, akiwemo aliyekuwa Katibu wa Tume, Winifrida Rutaindura. 

Tukio hilo lilifanyika Januari 26, 2021 mjini Morogoro, wakati wa kuhitimisha Mkutano wa Baraza la Wafanyakazi uliohudhuriwa na Mwenyekiti wa Tume, Profesa Willy Komba, Kaimu Katibu wa Tume, Moses Chitama, Menejimenti na wawakilishi kutoka wilaya zote za Tanzania Bara. 

Akizungumza wakati wa hafla hiyo fupi, Profesa Komba aliwapongeza wastaafu hao kwa utumishi uliotukuka na kuwaomba waendelee kuwa Mabalozi wa Tume kokote watakakokwenda. 

Kwa upande wake, Katibu Mstaafu wa Tume, Bibi Rutaindura, akizungumza kwa niaba ya wastaafu wenzake, alishukuru ushirikiano walioupata kutoka kwa watumishi wote na kuwaasa kuendeleza mshikamano baina yao. 

Akitoa hotuba ya kufunga Mkutano huo wa Baraza la Wafanyakazi, Profesa Komba alibainisha kuwa umekuwa wenye mafanikio makubwa huku akiwakumbusha wajumbe kuzingatia maadili ya kazi na weledi ili kuiwezesha Tume kufikia malengo yaliyowekwa na Serikali. 

“Nawasisitiza muendelee kufanya kazi kwa weledi ili tufikie malengo na kuwa Taasisi ya mfano wa kuigwa kwa kuihudumia vyema kada ya walimu na hivyo kuwezesha kuinua zaidi kiwango cha elimu nchini.” 

Aidha, alitumia fursa hiyo kuwakumbusha kuwa Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kuondoa uzembe na vitendo vya rushwa mahali pa kazi pamoja na kubana matumizi yasiyo ya lazima, hivyo akawataka kujiepusha na vitendo hivyo badala yake kila mmoja atimize wajibu wake ipasavyo. 

Wastaafu wengine walioagwa ni pamoja na Christina Hape aliyekuwa Makao Makuu Dodoma, Corona Maira (Ilemela), Anna Mutungi (Bukoba), Fanuel Edward (Musoma), Rahim Mgongo (Lushoto) na Vicent Shemsanga (Kibaha). 

Wengine ni Matilda Philemon (Kigoma), Elineema Mtaita (Morogoro) na Magdalena Nakitundu (Tabora). 

Mkutano huo wa siku mbili wa Baraza la Wafanyakazi wa Tume ya Utumishi wa Walimu, ulifunguliwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), David Silinde.
Share:

RAIS MAGUFULI AZINDUA SHAMBA LA MITI CHATO - GEITA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas Ndumbaro, Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani, Waziri wa Madini Doto Biteko, Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu TFS Profesa Dos Santos Silayo pamoja na viongozi wengine akizindua shamba la Miti lenye ukubwa wa ekari elfu 69 katika eneo la Butengo Chato mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021. Picha na Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Damas Ndumbaro, Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani, Waziri wa Madini Doto Biteko, Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu TFS Profesa Dos Santos Silayo pamoja na viongozi wengine akizindua shamba la Miti lenye ukubwa wa ekari elfu 69 katika eneo la Butengo Chato mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021. 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Viongozi wengine wakipiga makofi mara baada ya kuzindua shamba la Miti la Chato lenye jumla ya ekari elfu 69 katika eneo la Butengo Chato mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimwagilia maji mti alioupanda kama kumbukumbu mara baada ya kuzindua shamba la Miti lenye ekari elfu 69 katika eneo la Butengo Chato mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwapungia mkono wananchi wa Butengo Chato wakati akiondoka katika shamba la Miti la Chato mara baada ya kulizindua mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Butengo Chato mkoani Geita kabla ya kuzindua Shamba kubwa la Miti lenye jumla ya ekari elfu 69 mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Butengo Chato mkoani Geita kabla ya kuzindua Shamba kubwa la Miti lenye jumla ya ekari elfu 69 mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021
Kamishna wa Uhifadhi wa Wakala wa Huduma za Misitu TFS Profesa Dos Santos Silayo akipiga Saluti mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kutangaza Rasmi kuwa Shamba la Miti la Chato sasa liitwe Shamba la Silayo kama Heshima kutokana na utendaji wake mzuri wa kazi. 

PICHA NA IKULU 



Share:

RAIS MAGUFULI ATOA MSIMAMO CHANJO YA CORONA...."SITEGEMEI KUTANGAZA KUJIFUNGIA NDANI"


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wananchi wa Butengo Chato mkoani Geita kabla ya kuzindua Shamba kubwa la Miti lenye jumla ya ekari elfu 69 mkoani Geita leo tarehe 27 Januari 2021.
**
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Pombe Magufuli amewatahadhalisha kuhusu chanjo ya COVID 19 inayoendelea katika mataifa mbalimbali na kuwasisitiza kusimama imara huku akisisitiza kuwa hategemei hata siku moja kuwatangazia wananchi wajifungie ndani kwa sababu ya Ugonjwa wa Corona.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Jumatano January 27,2021 wakati azindua shamba la miti la Silayo mkoani Geita.

"Mtatishwa sana ndugu zangu Watanzania lakini simameni imara, najua wapo baadhi ya watanzania hata wameondoka ndani ya nchi na kukimbilia maeneo mengine na kwenda kuchanjwa na walikochanjwa huko wamekuja huku wametuletea corona ambayo ni ya ajabu ajabu simameni imara.”

“Chanjo hazifai kama Wazungu wangekuwa na uwezo wa kuleta chanjo, hata chanjo ya Ukimwi ingekuwa imeshaletwa, chanjo ya kifua kikuu ingekuwa kifua ingeshaondoka, hata chanjo ya malaria ingekuwa ishapatikana hata chanjo ya kansa ingekuwa imeshapatikana, lazima watanzania tuwe waangalifu kwa mambo ya kuletewa letewa,” amesema Rais Magufuli.

“Sisi Watanzania hatujajifungia ndani na hatutegemei kujifungia ndani, na wala sitegemei kutangaza hata siku moja kwamba tunajifungia ndani kwa sababu Mungu wetu yupo hai na ataendelea kutulinda Watanzania. Tutaendelea kuchukua tahadhali nyingine za kiafya ikiwa pamoja na kujifukizia, unajifukizia huku unamuomba Mungu unasali..., sali huku unapiga zoezi la kulima mahindi, viazi ili ule vizuri ushibe. Corona ashindwe kuingia katika mwili wako,” ameongeza Rais Magufuli.
Share:

TAKUKURU SINGIDA YAOKOA ZAIDI YA SHILINGI MILIONI 270

 

Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Singida, Adili Elinipenda (katikati) akitoa taarifa ya utekelezaji kwa kipindi cha miezi mitatu Oktoba hadi Disemba 2020.

 Na Dotto Mwaibale, Singida

TAASISI ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Singida imeokoa zaidi ya shilingi 270.7 kutoka maeneo mbalimbali ikiwemo mikopo umiza.

Akitoa taarifa ya utekelezaji kwa kipindi cha miezi mitatu Oktoba hadi Disemba 2020 Mkuu wa Taasisi hiyo Mkoani hapa Adili Elinipenda alisema Takukuru imeokoa shilingi milioni 270,079,600 ndani ya kipindi hicho kutoka maeneo mbalimbali.

Elinipenda alisema shilingi milioni 154,416,000 pekee zimeokolewa kutoka mikopo umiza, shilingi milioni 28,000,000 ziliokolewa kutokana na fidia ya maeneo ya wananchi yaliyotwaliwa kufanya shughuli za uchimbaji madini Wilayani Mkalama,wakati kiasi kingine kikiokolewa kutoka maeneo mengine ikiwemo mahakama ya Manyoni.

"Fedha hizi tulizikabidhi kwa wahusika baada ya kuokolewa ambapo fedha tulizoziokoa kutoka mikopo umiza, Mkuu wa Mkoa Dk Nchimbi aliwakabidhi wananchi hao wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani Manispaa ya Singida." alisema Elinipenda.

Alisema katika kuhakikisha Vitendo vya Rushwa vinaisha Takukuru kwa kushirikiana na wadau wengine imeendelea kutoa Elimu kwa jamii kwa kushirikisha makundi mbalimbali ikiwemo Vijana wa shule za msingi, Sekondari na Vyuo.

Aidha Elinipenda alisema Taasisi hiyo imeanzisha utaratibu wa Takukuru inayotembea (MOBILE PCCB) ambapo itatenga siku moja ndani ya mwezi ili kuwatembelea wananchi kwenye maeneo yao lengo la kufanya hivyo ni kusikiliza na kutatua kero zao.

Hata hivyo Taasisi hiyo inazidi kutoa rai kwa wananchi wa Mkoa wa Singida kujiepusha na Vitendo vya Rushwa huku ikiwataka kushiriki kikamilifu katika kutoa taarifa za Vitendo hivyo pamoja na kutoa ushirikiano kwenye uchunguzi na kutoa ushahidi mahakamani

Share:

WATOTO WAFARIKI KWA KUANGUKIWA UKUTA MVUA IKINYESHA GEITA

Eneo la ukuta wa nyumba walio kuwemo watoto tisa wa familia moja ambao wawili kati yao walipoteza maisha baada ya kuangukiwa na ukuta wa nyumba yao.

***
Watoto wawili wa familia moja wamefariki dunia baada ya kuangukiwa na ukuta wa nyumba chanzo kikitajwa kuwa ni mvua inayoambatana na upepo iliyonyesha wilayani Geita juzi Jumapili Januari 24, 2021.

Waliofariki ni Asheri Malima(4) na Laurencia Malima (2) waliokuwa wakiishi kijiji cha Kasesa kata ya Kaseme.

Baba wa watoto hao, Malima Kengere amesema aliwaacha wanae tisa nyumbani na kwenda kuuza mahindi ya kuchoma lakini mmoja wa watoto wake alimfuata na kumueleza kuwa nyumba yao imeanguka. Amesema wakati ukuta ukianguka watoto hao walikuwa wenyewe nyumbani.

“Walipoona ukuta unaanguka walikimbia lakini hawa wawili walikuwa wadogo hawakuweza, walifukiwa na kifusi,” amesema akibainisha kuwa siku hiyo mvua ilinyesha kuanzia saa nane mchana hadi saa 10 jioni.

Kamanda wa polisi mkoani Geita, Hendry Mwaibabe amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuwataka wazazi kuwa waangalifu hasa nyakati za mvua ili kuepuka majanga yanayoweza kuzuilika.

CHANZO- MWANANCHI

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger