Thursday, 21 January 2021

WATOTO WANING'INIZWA JUU YA MTI KUPIMWA UZITO,WAJAWAZITO WALAZWA KWENYE MADAWATI, SAKAFUNI KUPATA HUDUMA


Na Dinna Maningo,Tarime

Wananchi katika kijiji cha Nyagisya kata ya Kiore wilayani Tarime mkoani Mara wamelazimika watoto wao kupewa huduma ya Kliniki chini ya mti wa muembe huku wakining'inizwa juu ya mti kupimwa uzito na wajawazito nao wakilazwa juu ya meza,madawati,sakafuni ili kupata huduma za afya.

Malunde 1 blog imefika katika kijiji hicho ili kufahamu sababu za huduma ya Kliniki kutolewa chini ya mti ambapo akina mama wakiwa wamebeba watoto wao pamoja na wajawazito walisema kuwa wanalazimika kufanya hivyo kwa kuwa kijiji hakina zahanati na kwamba huduma hiyo ya kliniki hutolewa mara moja kwa kila mwezi.

Pia walisema kuwa wanaepuka umbali wa kilomita 4 kwenda kupata huduma ya Kliniki katika zahanati ya Mtana kata ya Manga,umbali wa km 12 kwenda zahanati ya Gamasara kata ya Nyandoto na hospitali ya wilaya ya Tarime iliyopo umbali wa km14.

Furaha Joseph mkazi wa kijiji hicho alisema,"mimi ni mmoja wa akina mama tunaoteseka kuitafuta huduma ya afya hatuna zahanati ukiugua,au kwenda kupata huduma ya clinic mpaka ujipange uwe na nauli elfu 3,000 ya pikipiki kwenda Mtana,na 5000 kwenda hospitali ya wilaya kama hauna inabidi utembee kwa miguu inachosha".

Happines Johanes alisema kuwa wanapokwenda kwenye zahanati hizo baadhi ya watoa huduma hukataa kuwapa huduma na kuwataka kwenda zahanati ya Gamasara au hospitali ya wilaya jambo ambalo liliwalazimu kuomba kupewa huduma ya kliniki katika kijiji chao ili kuepuka usumbufu.

"Tukienda Mtana nesi wanatuambia nyie nao mnatusumbua si mjenge zahanati yenu? mnakuja tu kurundikana hapa,ukiwa unaanza kliniki wanakusukuma kwenda hospitali ya wilaya. Tunashukuru serikali yetu ya kijiji ilikaa ikaona ni kwanini tuendelee kuteseka tukaona ni bora huduma ya kliniki tuifanye hapa kwetu hata kama ni chini ya mti inatusaidia kupunguza umbali na gharama za nauli na kauli mbalimbali za kukatisha tamaa", alisema Johanes.

Kutolewa huduma hiyo ya kliniki chini ya mti bado ni changamoto kwa akina mama wenye watoto na wajawazito kwa kuwa mvua ikinyesha hutangatanga kutafuta mahali pakufanyia huduma na kujikinga mvua hali ambayo wakati mwingine watoto kupimwa uzito huku nguo ikifungwa juu ya kenchi kwenye madarasa shule ya msingi Nyagisya na Wajawazito kulala juu ya madawati,meza na sakafuni kupata huduma ya cliniki.

"Mwandishi bahati nzuri umekuja siku ya kliniki na umeshuhudia mwenyewe kwa macho yako,huwa tunapima hapa chini ya mti,mvua ikinyesha tunahangaika pakupima na kujikinga ikinyesha tunaenda ofisi ya kijiji nako wakiwa na vikao vyao tunaondoka tena tunaenda shuleni tunaomba tunapewa darasa lakini sasa hivi wanafunzi wamejaa hakuna madarasa inabidi tusubiri wanafunzi wakienda kupata chakula ndiyo tunaingia kama hakuna mvua tunakaa chini ya mti",alisema.

"Nesi anafunga kikoi juu ya kenchi watoto wanapimwa uzito,kwa wajawazito  wanaunganisha madawati au juu ya meza analala anapimwa kuangalia kimo cha mtoto,mlalo,mapigo,kama anacheza huduma anapata zote isipokuwa uzito na wingi wa damu hatupimwi,ofisi ikiwa wazi kuna godoro wananchi tulinunua linawekwa chini ya sakafu mjamzito unalala nesi anapiga magoti chini anakupima,tukiwa nje wanaweka meza mjamzito unalala juu ya meza unapimwa meza tunaazima shuleni",alisema Ester Mwita.

Rhobina Meng'anyi alisema kuwa huduma hiyo wanayoipata chini ya mti ni huruma ya serikali ya kijiji na halmashauri ya wilaya ya Tarime baada ya kuona wajawazito na watoto wanavyoteseka kupata huduma ya Kliniki ambapo Mariam Wambura aliwashukuru wauguzi kuwasogezea huduma karibu licha ya changamoto nyingi wanazozipata lakini hawajakata tamaa kuwasaidia.

Wananchi walisema kuwa adha ya mama na mtoto itapungua endapo ikijengwa zahanati kwani bado kuna huduma hawazipati kiwemo ya mjamzito kutopimwa uzito,baadhi ya vipimo kukosekana ,huduma ya kujifungua na matibabu ya ugonjwa hivyo bado hulazimika kuchapa mwendo kuitafuta huduma ya afya.

Ester Simon alisema"Mama mkwe wangu alikufa njiani akiwa anaenda kujifungua alivuja damu nyingi kutokana na mitikiso ya pikipiki barabara mbuvu alafu umbali mrefu,aliacha watoto sita na mke mwenzangu alipofika hospitali ya wilaya alijifungua lakini mtoto alifariki alizaliwa akiwa kachoka,mama mkewe wangu alifia njiani akienda kujifungua aliacha watoto sita na mimi nawatoto sita wakiugua napata shida sana hakuna zahanati".

Anna Ryoba alisema kuwa ni miongoni mwa wanawake waliojifungulia njiani kutokana na umbali mrefu na kwamba kutokuwepo kwa zahanati bado wanatembea umbali mrefu ambao usababisha baadhi ya wajawazito kujifungulia njiani,naye akiwa miongoni waliojifungulia njiani na wengine kujifungua wakiwa nyumbani jambo linalosababisha wengine kufa na watoto wanauzaliwa kufa kwa kwa kukosa huduma za kitaalamu au wakunga wenye utaalamu wa kuzalisha.

Wanaume nao hawakuwa nyuma kueleza kero zao,Athanas Machera alisema kuwa umbali mrefu wa kwenda kufuata huduma ya afya umekuwa kero kwa watoto wanaoachwa majumbani na wazazi wao kwakuwa ushida njaa bila kula chakula wakisubiri wazazi kufika kuwahudumia,wakati mwingine watoto wadogo wanalazimika kuwasha moto ili kupika chakula jambo ambalo ni hatari kwa usalama wao.

Thomas Wambura ambaye ni mwendesha pikipiki alisema kuwa wajawazito wengi wanajifungua usiku hivyo wakati mwingine waendesha pikipiki hukataa kuwasafirisha usiku na wale wanaokubali huwatoza gharama kubwa na wengine kucheleweshwa kufikishwa hospitali na hivyo kujifungua njiani na nyumbani na wengine kufariki dunia kwa kukosa huduma.

"Ikiwa usiku gharama ni 30,000/= huku ni porini na ni mbali kuna fisi wengi,unakuta unakaa mbali na umelala na mke wako unapigiwa simu wakati mwingine saa saba za usiku au saa nane,hali hii inawashinda mabodaboda wengi mwingine akikupigia simu unaacha kupokea na wakati huo mgonjwa ana hali mbaya anakosa msaada anazidiwa anaamua kuzaa nyumbani wengine wanakufa,au uchungu unazidi anazalia njiani", alisema Wambura.

Rebeka Samson ni miomgoni mwa wauguzi katika zahanati ya Mtana anayetoa huduma ya kliniki chini ya mti kwenye kijiji cha Nyagiswa alisema kuwa ameamua kutoa huduma hiyo kwa kuwa ni sehemu yake ya kazi licha ya kukutana na changamoto nyingi wakati wa utoaji huduma.

"Huwa tunakuja wauguzi watatu leo niko mwenyewe mmoja anaumwa mwingine yuko masomoni,tunatoa huduma ya kliniki tu kwa watoto na wajawazito inayotolewa mara moja kwa mwezi na tunahudumia wagonjwa zaidi ya 50 kama unavyoona niko peke yangu kila kitu nafanya mimi,napima watoto,wajawazito na huduma ya chanjo.

"Isipokuwa uzito wajawazito hatuwapimi mzani wa kuwapimia ni mkubwa kuusafirisha kutoka zahanati ya Mtana ni mbali unaweza kuharibika,huwa tunawashauri waende kupima Mtana,mazingira si rafiki huwezi jua juu ya mti kuna wadudu gani wabaya,wakati mwingine sisimizi wanatusumbua lakini siwezi kukata tamaa maana naipenda kazi yangu na nijukumu langu kutoa huduma,nikiwa sina nauli ya usafiri inanibidi nikope baadae ofisi yangu unilipa", alisema Samson.

Muuguzi huyo alisema kuwa wakati wa mvua anapata shida kuhamahama kutafuta mahali pakutolea huduma  na maeneo ya kutolea huduma siyo mazingira salama lakini hulazimika kufanya hivyo ili kuhakikisha huduma ya kliniki inapatikana kijijini kama njia ya kuwapunguzia umbali lakini wajawazito na watoto hufika kwa wingi kupata huduma.

Kutokana na changamoto ya ukosefu wa zahanati wanakijiji wameamua kuchangishana fedha na nguvu zao kujenga zahanati ambapo wakati wa ziara ya mbunge wa jimbo la Tarime vijijini Mwita Waitara aliwaahidi kuwachangia milioni 5 ya kununua Saruji na baadhi ya vifaa vya ujenzi.

Mkuu wa shule ya msingi Nyagisya Egid Kamala alisema kuwa shule ina eneo zaidi ya ekari 50,kutokana na changamoto ya zahanati ilitoa eneo ekari 6 kujengwa zahanati na ekari 13 kujenga shule ya Sekondari.

Athanas Wambura alimpongeza Diwani wa Kata ya Kiore Rhobi John ambaye ni mwanamke kwa madai kuwa tangu kijiji hicho kianzishwe mwaka 1974 licha ya kuongozwa na viongozi mbalimbali wa serikali ya kijiji na Madiwani wa kata hawakuwahi kuhamasisha ujenzi wa zahanati lakini yeye amekuwa Diwani wa kwanza kuhamasisha ujenzi wa zahanati na ujenzi umeanza.

Mjumbe wa Serikali ya kijiji hicho Bruno Maswi alisema kuwa wameamua kusitisha ujenzi wa sekondari kwa kuwa kata hiyo ina sekondari mbili na kugeukia kwenye zahanati kutokana na kero nyingi ikiwemo wajawazito kufukuzwa zahanati ya Mtana na baadhi ya wagonjwa kunyima huduma.

Kaimu Mwenyekiti wa kijiji cha Nyagisya ambaye pia ni mwenyekiti wa kitongoji cha Senta Ghati John alisema kuwa sababu za wajawazito na watoto kupata huduma chini ya mti ni kutokana na kuwepo mgogoro kati ya kata yao ya Kiore na kata jirani ya Manga kuliko na zahanati ya Mtana kuwataka kujenga zahanati yao nasiyo kwenda kusongamana kwenye zahanati ya Mtana.

"Tukiwa hatuna vikao na hakuna watu wengi tunaowahudumia tunawaachia ofisi wanawahudumia wajawazito,nawapongeza wananchi kwa kujitolea kuhakikisha tunajenga zahanati wagonjwa na Wajawazito wanateseka sana uongozi wa kijiji tulikaa na uongozi wa shule tukashauriana eneo likapatikana la kujenga zahanati nawaomba wadau mbalimbali waguswe watusaidie tukamilishe ujenzi tumechoka kutukanwa na watu wa Mtana", alisema.

Afisa Mtendaji wa kijiji cha Nyagisya Waitara Kemo ambaye ana miezi minne tangu ahamishiwe kwenye kijiji hicho alisema kuwa tayali wananchi wamechimba msingi kwa nguvu zao,wamechanga fedha na tripu 5 za mawe zimenunuliwa,matofali 3,500,tripu nne za mchanga,mifuko 30 ya saruji na kuna kiasi cha milioni 1 na vitatumika kuanzia ujenzi na kwamba lazima ujenzi utakamilika ili kusogeza karibu huduma ya afya.

Diwani wa kata ya Kiore Rhobi John alisema kuwa kwakuwa wajawazito na watoto wanateseka sana akiwa kama Diwani wa kwanza mwanamke kuchagulia ndani ya kata hiyo atazidi kuhamasisha ujenzi wa zahanati baada ya kuona wagonjwa,wajawazito na watoto wanavyoteseka nakwamba Zahanati itakamilika mwaka huu na atashirikiana na wananchi wa kata yake katika maendeleo.





Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS JANUARI 21,2021























Share:

Wednesday, 20 January 2021

Drivers 14 posts at World Vision

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Purpose of the position: To drive WVT vehicles so as to facilitate staff/visitor movements as assigned by Senior Transport Officer and keep the vehicle clean and in good working condition Communicate World Vision’s Christian ethos and demonstrate a quality of spiritual life that is an example to others. To keep vehicle clean, in good condition […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Regional Sales Manager – 5 Positions at StarTimes

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Title: Regional Sales Manager – 5 Positions Department: Sales Locations: Northern Zone, Southern Zone, Central Zone, Lake Zone and Coast Zone Reports To: Zone Manager/ Sales Director StarTimes Group was founded in 1988.  It is the most influential system integrator, technology provider, network operator, and content provider in China’s television broadcasting industry, and it […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Sales Training Manager – 5 Positions at StarTimes

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Title:  Sales Training Manager – 5 Positions Department: Sales Locations: Northern Zone, Southern Zone, Central Zone, Lake Zone and Coast Zone Reports To: Zone Manager/ Sales Director StarTimes Group was founded in 1988.  It is the most influential system integrator, technology provider, network operator, and content provider in China’s television broadcasting industry, and it […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Sales Graduate Trainee-20 Position at StarTimes

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

  Job Title: Sales Graduate Trainee-20 Position Department: Sales Locations: Dar es salaam StarTimes Group was founded in 1988.  It is the most influential system integrator, technology provider, network operator, and content provider in China’s television broadcasting industry, and it is on its way to become a media group with global influence. With a global […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Business Relationship officer at Kilimanjaro Co-operative Bank Limited (KCBL)nship Officer at

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Kilimanjaro Co-operative Bank Limited (KCBL) is the only Co-operative Bank in the country, Headquartered in Moshi – Kilimanjaro, is fully fledged  Bank owned by    Co-operatives and private business entities. The Bank is ambitiously reorganizing its business model and implementing growth strategy to widen nationwide outreach and network expansion to support government    Co-operative movement […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Branch Quality Assurance at Kilimanjaro Co-operative Bank Limited (KCBL)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Kilimanjaro Co-operative Bank Limited (KCBL) is the only Co-operative Bank in the country, Headquartered in Moshi – Kilimanjaro, is fully fledged  Bank owned by    Co-operatives and private business entities. The Bank is ambitiously reorganizing its business model and implementing growth strategy to widen nationwide outreach and network expansion to support government    Co-operative movement […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

BABA MATATANI KWA KUMFINYA AKITUMIA PRAIZI MTOTO KISA HAJUI KUSOMA WALA KUANDIKA

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga linamshikilia mwanaume aitwaye Shija Abdallah (28), mkazi wa kata ya Kambarage Manispaa ya Shinyanga kwa kosa la kumshambulia kwa kumfinya kwa kutumia Praizi mtoto wake wa kiume mwenye umri wa miaka 8 anayesoma darasa la tatu katika shule ya msingi Kambarage.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Debora Magiligimba amesema tukio hilo Januari 15, 2021 saa majira ya saa nane kamili mchana. 

“Tunamshikilia Shija Abdallah kwa kosa la shambulio la kudhuru mwili baada ya kumfinya kwa kutumia praizi mwanae wa kiume, (jina limehifadhiwa) mwenye umri wa miaka 08, mwanafunzi wa darasa la tatu shule ya msingi Kambarage sehemu mbalimbali za mwili wake na kumsababishia maumivu makali”,ameeleza Kamanda Magiligimba. 

“Bibi wa mtoto huyo mwenye umri wa miaka 70 mkazi wa kata ya Ndala, Manispaa ya Shinyanga alibaini mtoto huyo kufanyiwa ukatili huo na baba yake mzazi huyo kwa kufinywa kwa kutumia praizi sehemu mbalimbali za mwili wake chanzo kikiwa ni kumuadhibu mtoto huyo kwa sababu hajui kusoma wala kuandika na mahudhurio shuleni ni hafifu”,amefafanua Kamanda Magiligimba. 

Amesema madhura amepatiwa matibabu katika hospitali ya rufaa mkoa wa Shinyanga na hali yake inaendelea vizuri na kwamba mtuhumiwa atafikishwa mahakamani baada ya upelelezi kukamilika. 

“Natoa wito kwa wazazi na walezi kuacha tabia ya kuwafanyia ukatili watoto wao na watumie njia sahihi ya kuwaadhibu watoto pindi wakoseapo. 

“Jeshi la polisi mkoani Shinyanga halitamvumilia mzazi au mlezi yeyote atakayebainika kufanya vitendo vya ukatili dhidi ya watoto na hatua kali zitachukuliwa dhidi yake na niwatake wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi ili kukomesha vitendo hivi vya ukatili dhidi ya watoto”,amesema.
Share:

JOE BIDEN AAPISHWA KUWA RAIS WA 46 WA MAREKANI..AHUTUBIA TAIFA


Joe Biden amekula kiapo na kuwa rais wa 46 wa taifa la Marekani. Biden amekula kiapo mbele ya jaji wa Mahakama Kuu John Roberts.

Baada ya kula kiapo Biden amelihutubia taifa kwa mara ya kwanza akiwa Rais wa Marekani akisema ''hii ni siku ya kidemokrasia''. Siku ya kihistoria na matumaini.

''Marekani imejaribiwa na kunyanyuka tena dhidi ya changamoto. Leo tunasheherekea ushindi si wa mgombea isipokuwa ushindi wa demokrasia''.

''Ninawashukuru watangulizi wangu wa vyama vyote walio hapa hii leo,'' alisema Rais mpya. Marais wa zamani Clinton, Bush na Obama wamehudhuria sherehe hiyo.

Biden amesema alizungumza kwa njia ya simu na Rais Jimmy Carter- ambaye sasa ana miaka 96, na kumpongeza kwa utumishi wake.

Mtangulizi wake, Donald Trump hajahudhuria tukio hilo muhimu, na hatua hiyo imemfanya kuwa rais wa kwanza kutohudhuria sherehe za kuapa kwa mrithi wake tangu mwaka 1869.
Rais mpya ametangaza msururu wa maagizo yanayolenga kugeuza sera kuu za Bw Trump.

Makamu wa Rais mteule Harris aliapishwa mbele ya Bwana Biden - kuwa mwanamke wa kwanza na mtu wa kwanza mweusi na mwenye asili ya Asia na Amerika aliyeinuliwa kuhudumu katika nafasi ya pili muhimu baada ya Urais.

Shughuli za uapisho zimefanyika wakati kukiwa na ulizi mkali baada ya waandamanaji wanaomuunga mkono Trump kufanya vurugu tarehe 6 mwezi Januari.

Wanajeshi 25,000 wanalinda eneo linalofanyika sherehe hizo, sherehe ambazo zimekosa kuhudhuriwa na maelfu ya watu kama ilivyo desturi yake kwa sababu ya janga la corona.

Kilichofanyika siku ya uapisho
Mapema Jumatano Bw Biden alihudhuria Misa katika kanisa kuu huko Washington - pamoja na viongozi wanne wa baraza kuu la Katoliki, wote wa Democratic na Republican - kabla ya kwenda Capitol.

Akiwa na umri wa miaka 78, Bwana Biden ndiye rais wa Marekani mwenye umri mkubwa zaidi kuwahi kuapishwa.

Makamu wa Rais anayemaliza muda wake Mike Pence pia amehudhuria sherehe hiyo. Hakwenda kwenye hafla ya salamu ya kijeshi ya Bwana Trump katika uwanja wa Andrews.

Awali wasaidizi walisema Bw Biden atatumia hotuba yake kutoa wito wa matumaini wa umoja wa kitaifa baada ya utawala wa mtangulizi wake kutoka chama cha Republican.

Sherehe hizo zilipambwa na watumbuizaji kama vile Lady Gaga- aliyeimba wimbo wa taifa, halikadhalika Jenifer Lopez na Garth Brooks.

Tamasha la jioni litahodhiwa na Tom Hanks na Bruce Springsteen, John Legend, Jon bon Jovi, Justin Timberlake na Demi Lovato.

Je Trump anafanya nini?

Katika hotuba yake katika kambi ya kijeshi ya Andrews Air Force , rais anayeondoka aliangazia kile alichokitaja kuwa ufanisi wa utawala wake kama rais.

Tulichofanya kimefanikiwa kwa kiwango kikubwa, alisema bwana Trump.

Bwana Trump mwenye umri wa miaka 74 aliondoka ili kuanza maisha ya bila urais katika uwanja wa mchezo wa gofu huko Mar-a lago katika ufukwe wa bahari wa Palm Beach.

Katika saa zake za mwisho katika madaraka bwana Trump aliwapatia uhuru zaidi ya watu 140 , akiwemo mshauri wake wa zamani Steve Bannon , ambaye alikabiliwa na mashtaka ya kufanya udanganyifu.

Je historia itamkumbuka vipi Trump?
Matukio ya kisiasa yanayomzunguka hayajaisha. Bunge la Seneti linatarajiwa kumshtaki kufuatia kushtakiwa na bunge la uwakilishi kwa mara ya pili kwa kuchochea ghasia za Capitol.

Siku ya Jumanne , Kiongozi wa Republican katika bunge la seneti Mitch McConell , alisema kwamba waandamanaji hao walichochewa na rais Trump na kuambiwa uongo.

Je Biden atafanya nini katika siku yake ya kwanza?
Bwana Biden ametoa maagizo mengi ya urais. Katika taarifa yake siku ya Jumatano , alisema kwamba atatia saini maagizo 15 baada ya kuapishwa.

Watabadilisha hatua ya rais Trump kuindoa Marekani katika mkataba wa mazingira wa paris.
Kufutilia mbali cheti cha kuruhusu kampuni ya mabomba ya Keystone XL Pipeline , ambayo inapingwa na wanamazingira na makundi ya Wamarekani asilia.

Kufutilia mbali sera ya Trump kuhusu uhamiaji na fedha za dharura zilizosaidia kujenga Ukuta wa Mexico mpakani.

Kuwataka watu wavalie barakoa mbali na kukaa mbalimbali miongoni mwa wafanyakazi wa majimbo, pamoja na ofisi ya Ikulu kutokana na virusi vya corona.Mipango ya uongozi wa Biden huenda ikaathiriwa na idadi ya wabunge alionao katika bunge la seneti pamoja na bunge la uwakilishi.

Siku ya Jumanne , Bwana Biden alitoa hotuba katika jimbo lake la nyumbani huko Delaware , akiwaambia waandishi wa habari kuwa ,'' hizi ni siku mbaya , lakini kuna nuru'' , kabla ya kuelekea Washington .

CHANZO - BBC SWAHILI

Share:

ALIYETENGENEZA KEKI ZENYE MAUMBO YA SEHEMU ZA SIRI AKAMATWA


Mwanamke mmoja nchini Misri ameshikiliwa na polisi kwa muda baada ya kushutumiwa kutengeneza keki zenye maumbo ''yasiyo na heshima'' vyombo vya habari nchini humo vimeeleza.

Keki hizo zilizotengenezwa na peremende laini zilizobuniwa maumbo ya sehemu za siri na maumbo ya nguo za ndani, zililiwa katika sherehe ya kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa katika klabu ya michezo ya Cairo.

Baada ya picha kusambaa kwenye mitandao ya kijamii, mtengenezaji wa keki alikamatwa kisha kuachiwa kwa dhamana ya dola 319 za Marekani. Alikana kuoka keki zenye maumbo yanayochochea ngono.

Chombo cha juu cha kidini kimetahadharisha kuwa bidhaa zinazotengenezwa kwa mtindo huo zinapigwa marufuku katika uislamu.

Dar al-Ifta kiliandika katika mtandao wa Facebook kuwa bidhaa zinazowakilisha masuala ya ngono '' ni ukiukaji wa maadili na udhalilishaji katika jamii''.

Wanawake kadhaa walioshiriki kwenye sherehe hiyo pia wanaripotiwa kuchunguzwa, huku Wizara ya vijana na michezo ikitazama namna klabu hiyo ilikofanyika sherehe ilivyohusika.

Wakili wa haki za binadamu Negad El Borai aliandika katika ukurasa wa twitter kwamba tukio hilo lilithibitisha "kuna sehemu ya jamii, kwa msaada wa serikali, ambayo inataka kuondoa nafasi yoyote ya uhuru wa watu nchini Misri kwa kisingizio cha kulinda maadili ya familia ''.

Alifananisha na kesi za wanawake kadhaa vijana wa Misri wanaotuhumiwa kwa makosa yanayohusiana na maadili kuhusiana na video zilizochapishwa kwenye TikTok na majukwaa mengine ya mitandao ya kijamii

Jumanne iliyopita, mahakama ya rufaa ilifuta hukumu ya miaka miwili ya gerezani iliyotolewa kwa washawishi wawili - Haneen Hossam, 20, na Mawada al-Adham, 22 - ambao walitiwa hatiani mnamo mwezi Julai mwaka jana kwa "kuvunja maadili na kanuni za kifamilia" na kuchapisha picha "zisizo za adabu" na video.

Lakini siku chache baadaye iliibuka kwamba mwendesha mashtaka wa umma alikuwa ameamuru kuendelea kwa kizuizini kwa wanawake kusubiri uchunguzi juu ya mashtaka ya usafirishaji wa binadamu.

Mwendesha mashtaka alidai kwamba walikuwa wamewashawishi wasichana kwa kuwahimiza watume video zinazofanana na zao.

Wakili wa wanawake hao alisema watakata rufaa dhidi ya hatua hiyo.

CHANZO- BBC SWAHILI
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger