Thursday, 14 January 2021
RAIS WA ZANZIBAR DK. MWINYI, MAALIM SEIF SHARIFF HAMAD WATUA CHATO KUZUNGUMZA NA JPM
MCHUNGAJI ALIYEBAKA NA KUWAPA MIMBA BINTI ZAKE ATUPWA JELA MIAKA 140...ASEMA ALIPITIWA NA SHETANI
MTWIVILA CITY (IFUENGA UNITED) YAIFUATA IVAMBINUNGU FC FAINALI YA ASAS SUPER LEAGUE
Bunge Marekani lamshtaki Trump kwa mara ya pili
Baraza la Wawakilishi katika Bunge la Marekani limepiga kura na kupitisha mashtaka ya kumvua madaraka rais wa nchi hiyo Donald Trump, kufuatia mashtaka ya kuchochea vurugu na uvamizi wa majengo ya bunge wiki iliyopita.
Wabunge 10 wa Chama cha Republic ni miongoni mwa waliopiga kura na Wademocrat dhidi ya Trump. Spika wa bunge, Nancy Pelosi amesema hatua hiyo ya baraza la wawakilishi ni ujumbe kuwa hakuna aliye juu ya sheria, akimrejerea Rais Trump.
Trump amekuwa rais wa kwanza katika historia ya Marekani kupigiwa kura ya kutokuwa imani naye mara mbili. Hata hivyo baraza la seneti halitaanza mchakato wa kupitisha au kuzuia hatua hiyo ya baraza la wawakilishi kabla ya kuapishwa kwa rais mteule Joe Biden Januari 20.
Endapo baraza la seneti litamkuta na hatia hata baada ya kuondoka madarakani, huenda atazuiwa kuwania urais tena katika uchaguzi ujao wa mwaka 2024.
WATAALAM WA KILIMO SINGIDA WATAKIWA KUZINGATIA SHERIA YA KILIMO CHA UMWAGILIJI KATIKA KAZI ZAO.
Godwin Mutahangarwa Mwanasheria kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji akiwasilisha mada i nayohusu Sheria ya Kilimo cha Umwagiaji ya mwaka 2013 na kanuni zake katika kikao kazi na wataalam wa kilimo Mkoani Singida.
Mkurugenzi wa Idara ya Uendelezaji Miundo mbinu tokaTume ya Taifa ya Umwagiliaji Mhandisi Senzia Maeda, akigawa makablasha kwa wataalam wakilimo wakati wa kikao kazi kilichofanyika Mkoani Singida.
Warishiriki wakifuatilia kikao kazi kilichohusisha wataalam wa Kilimo na Ushirika Mkoani Singida
Na Mwandishiwetu - Singida
Maafisa Kilimo Ushirika na Umwagiliaji Mkoani Singida, wametakiwa kuzingatia nakutumia kikamilifu Sheria ya Taifa ya Umwagiiaji ya mwaka 2013 na kanuni zake pamoja na Sheria ya usimamizi na uhifadhi wa Mazingira ya mwaka 2004,ilikuweza kunusuru na kulinda vyanzo vya maji,nakutunza Miundombinu ya kilimo cha Umwagiliaji.
Hayo yamesemwa leo na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Daudi Kaali, alipoikuwa akizungumza katika kikao kazi na maafisa kilimo ushirika na wahadisi wa Umwagilijiaji Mkoani Singida.
Bw. Kaali amewataka wataalam hao wazielewe sheria hizo na kuhakikisha zinafanyakazi na kueleweka kwa umma na bila kupepesa macho kuwe na utii washeria bila shuruti na kuwachulia hatua wale wote wanaofanya uharibifu wa mazingira kwa kufanya shughuli za kibinadamu kwenye vyanzo vya maji,ilikulinda miundombinu ya kilimo cha umwagiliaji.
“Ni lazima kuzingatia utunzaji wa mazingira kwa kutokukata miti ovyo,nauchafuzi wa miundombinu ya umwagiliaji, mshirikiane na mamlaka husika ili kuweza kunusuru mazingira na kutunza miundombinu hiyo na mazingira,iko wazi kabisa kuwa, miundombinu mingi iliyoharibika inaonekana kuwa chanzo kikubwa ni uharibifu wa mazingira.” Alibainisha.
Akiongelea suala la Uhabirifu wamazingira litokanalo na mabadiliko ya Tabianchi, Bw. Kaali amesema ili kuhimili na kukabiliana na changamoto hiyo, wamekuwa wakihamasiha matumizi sahihi ya teknolojia nyingine sambamba na kupanga mikakati ya pamoja ya kuelendeleza sekta ya kilimo cha umwagiliaji kwa kushirikiana na sektabinafsi.
Akiongea katika kikao kazi hicho, Bw. Suleiman Musunga Afisa Kilimo,Ushirika na Umwagiliaji toka Wilaya ya Mkalama ameushukuru Mradi wa kurejesha Ardhi iliyoharibika nakuongeza usalama wa chakula katika maeneo kame nchini, (Reversing land Degradation trends and increasing food security in degraded ecosystem in semi-arid areas of Tanzania) Unaoratibiwa na Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira ,Kwa kukamilisha hatua ya awali ya kazi ya upembuzi yakinifu na nakuelekea kwenye hatua nyingine ya ujenzi wa mabwawa.
Mradi ambao utawawezesha wakulima katika eneo hilo kuweza kupata maji salama kwa ajili ya kilimo,na wafugaji kwa ajili ya mifugo na matumizi ya jamii iinayoishi maeneo kame.
Kikao kazi hicho cha siku tatu, kilihusisha wataalam wa sekta ya kilimo na umwagiliaji kutoka katika Manispaa ya Singida na wilayaza Manyoni,Ikungi,Itigi,Iramba na Mkalama.
TAKUKURU YAREJESHA NYUMBA ILIYOPORWA KINYEMELA BAADA YA MMILIKI WAKE KUSHINDWA KULIPA MKOPO WA SHILINGI LAKI TATU KAHAMA
Tigo yaungana na mawakala wa Tigo Pesa kuhitimisha promosheni ya Tigo Pesa Wakala Push, yatoa zawadi kwa mawakala mbalimbali
VUKA LENGO NA USHINDE: “Ili kuwa mshindi, kila wakala alitakiwa kuvuka lengo alilopewa, kulingana na historia ya miamala yake ya kila siku. Zaidi ya mawakala 4,000 walifanikiwa kuvuka malengo yao na kushinda zaidi ya shilingi milioni 400.” Angelica Pesha, Mkuu wa Kitengo cha Tigo Pesa #TigoPesaNiZaidiYaPesa #TigoPesaWakalaPush
TIGO PESA BOOST MTAJI!: “Nawashukuru Tigo kwa kuwa kupitia #TigoPesaWakalaPush wameweza kuniboost mtaji wangu” Piason Baruti, Wakala Tigo Pesa na Mshindi wa Milioni 1.5
#TigoPesaNiZaidiYaPesa
Mkuu Kitengo cha Tigo Pesa-Tz akiwa na katika picha ya Pamoja na washindi
#TigoPesaNiZaidiYaPesa
Kaimu Mkurugenzi Asimamishwa kazi kwa Kusafirisha Maiti Juu ya Gari.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Selemani Jafo amemuagiza Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo Mhandisi Joseph Nyamuhanga kumsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Tarime mkoani Mara Jumanne Yassin ili kupisha uchunguzi, kufuatia kitendo cha halmashauri hiyo kusafirisha mwili wa Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Emmanuel Sizo juu ya Carrier ya gari.
Waziri Jafo ametoa agizo hilo baada ya gari iliyobeba mwili wa Mtumishi huyo.kusambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.
Amesema amesikitishwa na kitendo hicho ambacho ni kinyume na kanuni za utumishi wa Umma, pamoja na mila na desturi za Mtanzania.
Ameagiza Watumishi wote waliohusika na uzembe huo wachukuliwe hatua za kinidhamu kwa mujibu wa sheria, kanuni.na taratibu za utumishi wa Umma.
Waziri Jafo amewataka Watumishi wote wa Umma katika tawala za mikoa na mamlaka za serikali za mitaa kujenga tabia ya kuheshimiana, kupendana na kuthaminiana wakati wote wanapotekeleza majukumu yao.
Sizo alifariki duniani kwa ajali ya gari mkoani Singida Januari 10 mwaka huu.
Watumishi 23 MOI mikononi mwa TAKUKURU
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU), inawachunguza Watumishi 23 wa Taasisi ya Mifupa Muhimboli ( MOI) kitengo cha Famasia, kwa tuhuma ya uchepushaji wa dawa zenye thamani ya shilingi bilioni 1.2.
Akizungumza na Waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU Brigedia JeneraliJohn Mbungo amesema uchunguzi wa kuwabaini Watuhumiwa hao ulianza mwaka 2018 hadi mwaka huu kwa ushirikiano na MOI na TAKUKURU.
Katika hatua nyingine Brigedia Jenerali Mbungo amefanya mabadiliko ya Watendaji ndani ya taasisi hiyo, lengo likiwa ni kuongeza ufanisi.
Pia amewaambia Waandishi wa habari kuwa, wameanzisha kitengo cha TAKUKURU kinachotembea, kitakachokuwa kikisikiliza na kutatua kero za Wananchi poppte walipo.
MITANDAO YA KIJAMII YAZIMWA MKESHA WA UCHAGUZI UGANDA
WAKRISTO WATAKIWA KUPANDA MBEGU BORA WAPATE MAVUNO MENGI
![]() |
| Mtumishi wa Mungu Mwalimu Joyce Mwakalasya baada ya kutoa mafunzo ya upandaji wa mbegu kwa waumini wa Kanisa la Moravian Usharika wa Kijichi jijini Dar es Salaam Jumapili. |
Na Dotto Mwaibale
WAKRISTO wametakiwa kupanda mbegu bora kwa kumtolea Mungu sadaka ili waje wavune mavuno mengi.
Ombi hilo limetolewa na Mtumishi wa Mungu Mwalimu Joyce Mwakalasya wakati akitoa mafunzo ya upandaji wa mbegu kwa waumini wa kanisa la Moravian Usharika wa Kijichi jijini Dar es Salaam Jumapili.
Mwakalasya alisema suala la upandaji wa mbegu ni la muhimu wakati wa kumtolea Mungu sadaka kwani huwezi ukatoa sadaka ndogo wakati unayo kubwa ukategemea kubarikiwa.
"Hata kabla ya kwenda kutoa sadaka yako Mungu anakuwa anaijua hivyo tunapokwenda kuitoa mbele ya madhabahu tutoe kwa uaminifu ili uje uvune mavuno mengi baada ya kuipanda." alisema Mwakalasya.
Alisema kabla ya kupanda mbegu yako hiyo unapaswa kujua unaipanda eneo gani na kwa wakati upi na si kila eneo utakapo ipanda itastawi.
Mwakalasya alitaja uvivu na uzembe kwa mkristo kuwa ni adui mkubwa wa upandaji mbegu hivyo alitoa rai ya kufanya kazi kwa bidii kwani huwezi kumtolea Mungu sadaka bila ya kuwa cha chanzo cha mapato.
Alitaja vitu vingine ambavyo vinakwamisha kupanda mbegu ni mtu kuwa na imani haba, wivu usiofaa, uchoyo, ubinafsi, kutosamehe, kufanya kazi isiyo halali na kutolipa kodi ya serikali.
Alitaja changamoto nyingine zinazo changia kuzolotesha upandaji wa mbegu kuwa ubinafsi, hofu, kutokuwa na moyo wa kuthubutu kufanya jambo, kiburi, ushirikina na kuwaza kinyume cha matokeo.
Alisema mkristo akifanikiwa kuyashinda mambo hayo ni lazima atapata mafanikio Mungu ni zaidi ya yote kwani aliweza kuwa saidia akina Eliya na wengine wengi hivyo ukimtolea sadaka kamilifu kwa kupanda mbegu atakubariki.
Mwakalasya alitumia nafasi hiyo kuwaambia waumini hao kuwa mara baada ya kuvuna mavuno yao yaliyotokana na upandaji mbegu wayatumie kuwa saidia watu wenye uhitaji.
YANGA BINGWA MAPINDUZI CUP, YAICHAPA SIMBA SC KWENYE MIKWAJU YA PENALTI 4-3
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduziu Mhe.Dk. Hussein Ali Mwinyi akimkabidhi Kombe la Ubingwa wa Michuano ya Mapinduzi Cup Nahodha wa Timu ya Yanga Haruna Nyonzima, baada kuifunga Timu ya Simba katika mchezo wa Fainali uliofanyika Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)






































