Tuesday, 12 May 2020

AMUUA MKE WAKE KISHA KUMUUNGUZA MOTO KWA KUNYIMWA TENDO LA NDOA



Jeshi la polisi mkoa wa Mara limamshikilia Mokiri Wambura (46) mkazi wa Kengesi wilaya ya Serengeti mkoani Mara kwa tuhuma za kumuua mke wake Mwise Kyobe(38) kwa kumkata mapanga na kisha kumuunguza kwa moto ndani ya nyumba kwa madai ya kunyimwa tendo la ndoa kwa zaidi ya miaka miwili.

 Bwana huyo pia amemjeruhi kwa kumkata mapanga mtoto wake wa kike mwenye umri wa mwaka mmoja.
Share:

WANAODAIWA KUWA MAJAMBAZI WAVAMIA NA KUPORA MATAIRI YA GARI LA KAMANDA WA POLISI GEITA


Jeshi la polisi mkoani Geita linawashikilia watu wawili waodaiwa kuwa ni majambazi huku likiendelea kuwasaka watu kadhaa kwa tuhuma za kuvamia usiku wa manane eneo lililokuwa limehifadhiwa gari la kamanda wa polisi mkoa huo na kuiba matairi yake yote manne kisha kutokomea pasipojulikana.

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita Mponjoli Lotson anasema katika hali isiyo ya kawaida watu hao kwa kushirikiana na walinzi walifanya uporaji huo kwa kufungua matairi hayo kisha kutokomea nayo huku jeshi hilo likiendelea na msako ili wahusika wote wakamatwe na kuchukuliwa hatua. 
Share:

Spika Ndugai Atoa Masharti Ya Kumtimua Bungeni Cecil Mwambe

Spika wa Bunge la Tanzania Job Ndugai, amewataka wale wote wanaotaka amfukuze Ubunge Mbunge wa Ndanda Cecil Mwambe, basi wamshauri amuandikie Spika barua ya kujiuzulu kwake, halafu waone kama ataendelea kukaa bungeni.

Spika Ndugai ameyabainisha hayo leo Mei 12, 2020 na kusema kuwa maamuzi hayo yote ya kumrejesha Mwambe bungeni, yamekuja kutokana na yeye kupata barua ya upande mmoja.

"Nimeeleza Mwambe amewahi kuniandikia barua lini?, hivi wewe ungekuwa Spika ungefanyaje, huna barua ya mtu kujiuzlu ungefanyaje?, unamfukuza tu!, lazima mchunguze na muangalie mzani uko wapi, Mwambe yupo hajafa, mwambieni aandike barua anikabidhi mimi, akishanikabidhi muone kesho yake itakuwaje" amesema Spika Ndugai.

Aidha Spika Ndugai amesema kuwa leo jioni atatolea ufafanuzi kuhusu tamko lililotolewa na CHADEMA, kwamba Wabunge wake waliojiweka karantini kwa sasa hawatorudisha posho kwa sababu wao siyo wezi


Share:

MAMA AUA MTOTO WAKE WA MIAKA MIWILI ILI APATE UTAJIRI KISHIRIKINA ALIVYOELEKEZWA NA SANGOMA WA SUMBAWANGA

Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Ulrich Matei

Na Esther Macha,Mbeya
WATU wanne wanashikiliwa na Polisi mkoani Mbeya kwa tuhuma za mauaji ya mtoto, Tamali Simon (2), ambapo miongoni mwa watuhumiwa ni mama mzazi wa mtoto huyo akidaiwa kushirikiana na watu hao kufanya unyama huo.

Kamanda wa Polisi mkoani Mbeya, Ulrich Matei amesema jana kwamba watuhumiwa hao walikamatwa wakati wa msako maalum uliofanywa na Polisi Mei 6, mwaka huu saa 4.00 usiku katika Kijiji cha Iwindi Kata ya Utengule Usongwe Mji Mdogo Mbalizi.

Kamanda Matei amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Rehema Kasela (36) ambaye ni mama mzazi wa mtoto, Riziki Muhema (20) mkazi wa Mtakuja Mbalizi 3, Estar Msongole (52) mganga wa kienyeji mkazi wa Sumbawanga, Mtumwa Haonga (65) mganga wa kienyeji mkazi wa Mtakuja Mbalizi ambao wote wanatuhumiwa kumuua mtoto Tamali mwenye umri wa miaka miwili na miezi mitatu.

Aidha Kamanda Matei amesema chanzo cha tukio hilo ni tamaa za kupata utajiri kwa njia za ushirikina na baada ya mtuhumiwa ambaye ni mganga wa kienyeji kuwapa masharti yaliyopelekea kifo cha mtoto huyo.

Akielezea zaidi Kamanda Matei amesema Mei 4, mwaka huu saa 2.00 usiku katika Kijiji na Kata ya Iwindi Tarafa ya Usongwe mtoto Tamali alikutwa ameuawa kwa kunyongwa shingo na mtu asiyejulikana na mwili wake kutelekezwa.

Amesema baada ya tukio hilo Polisi walifanya msako na kufanikiwa kuwakamata watuhumiwa katika maeneo tofauti na kwamba wakati wa mahojiano watuhumiwa walikiri kuhusika kwenye tukio hilo baada ya kupewa masharti na mganga wa kienyeji.

“Polisi walipofanya upekuzi nyumbani kwa mganga wa kienyeji walikuta vifaa mbali mbali vya uganga na dawa za kienyeji za aina mbali mbali, upelelezi wa tukio hilo unaendelea na mara baada kukamilika watafikishwa mahakamani,”amesema.
Share:

RAIS TRUMP AKATISHA MKUTANO NA WAANDISHI BAADA YA KUKERWA NA SWALI LA MWANDISHI WA HABARI

Rais Trump amekatisha mkutano na waandishi baada ya kukerwa na swali la Mwandishi wa CBS Weijia Jiang aliyemuhoji ni kwanini amekuwa anashindana kwa kujigamba kuwa USA inaongoza kupima corona kuliko wote wakati wana vifo zaidi ya Elfu 81.

Trump alimjibu hapaswi kuulizwa kwanini Wamarekani wengi wanazidi kupoteza maisha wakati sehemu nyingi duniani watu wanapoteza maisha hivyo sio swala la ajabu huku akisisitiza kuwa swali hilo wanapaswa kuulizwa China kwa kuwa wao ndio wameleta Corona na sio Yeye.

Baada ya kuona mwandishi anahitaji kujibiwa swali lake Trump akaona isiwe tabu akaamua kuondoka zake. 

Trump aliulizwa kuwa “Why is this a global competition to you if every day Americans are still losing their lives and we’re still seeing more cases?”
Share:

Kigwangalla: Hatuwezi Kushuhudia Sekta Ya Utalii Ikipigwa na Corona

Na Ahmed Mahmoud, Arusha
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk, Hamis Kingwangalla amesema kuwa hatuwezi kushuhudia  sekta ya utalii ikipigwa na janga la Covid – 19 wakati kunamianya mbalimbali ya kuifungua sekta hiyo kwa kujadili mambo mbalimbali yanayopaswa kuchukuliwa ili watalii waje nchini.

Dk, Kingwangalla aliyasema hayo jana Jijini Arusha wakati alipokuwa akizungumza na wadau mbalimbali wa sekta ya utalii nchini katika maandalizi ya mpango wa kupokea watalii baada ya janga la Covid – 19

Alisema sekta ya utalii itakuwa ni sekta ya kwanza kaamka hivyo kwa tafiti mbalimbali zinazoendelea na ikumbuke sekta hii ni sekta nyeti inayoingiza fedha nyingi za kigeni.

Alisema ni vyema sasa tujadiliane jinsi ya kuweka mambo mbalimbali ili kuifungua sekta ya utalii ingawa si jambo rahisi maana sekta hii imeathirika sana na ugonjwa huu hivyo lazima tujadili ili kuweka mikakati ya kuweka mbele yetu na baadaye tufungue milango ya kibiashara

“Tunakila sababu ya kujenga imani katika soko hili la utalii ikiwemo upimaji wa Corona kwa wageni wetu na jinsi ya kudhibiti sababu hatutaki tumwambukize virusi mtalii na sisi tusiambukizane”

Lazima tuangalie msingi ya afya iliyotolewa na inayotolewa na sekta za afya tuonaona nchi mbalimbali zimeanza kufungua mipaka yake na sisi lazima tuwe na viwango vibavyitakiwa ili kuwahudumia watalii wataokutwa na virusi tutawahudumiaje

Alisisitiza ugonjwa huu upo hivyo ni lazima sasa kutafuta mbinu zaukuhakikisha  tahadhari  mbalimbali za kudhibiti ugonjwa huu ikiwemo kuhakikisha tunajaribu kufanya utalii kwa tahadhari kubwa na kuzingatia maelekezo yote yanayotolewa na wizara husika.

“Haya tutakqyoyajadili lazima tuweke imani na kufuata muongozo itakayokubaliwa na serikali ikiwemo kuweka viwango vinavyotakiwa hivyo ni lazima tujadili jambo hili kwa kina na kisha kesho (jumanne) nitaongea kwa kina na vyombo vya habari ili kusema yale tuliyokubaliana “

Sekta hii imeathirika sana kwa familia zinazotegemea utalii sekta binafsi, mahoteli na sehemu nyingine hivyo lazima tujadiliane na kuyafikisha katika mamlaka zinazohusika

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii,Profesa Adolf Mkenda alisema kikao hicho ni muhimu na ni lazima watu wawe wazalendo katika kuhakikisha sekta ya utalii inanyanyuka tena

Kikao hicho kinashirikisha washiriki kutoka Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania  (Tanapa) , Mamlaka ya Hifadhi ya Njiro (NCAA) , Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori  Tanzania (Tawa)  Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) pamoja na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Uhamiaji.


Share:

WALIOFARIKI KWA CORONA NCHINI MAREKANI WAFIKA 81,795


Kulingana na takwimu zilizotolewa na shirika la habari la Reuters, idadi ya vifo vinavyotokana na janga la Corona imefikia zaidi ya 81,795 nchini Marekani.

Hayo yanajiri wakati hatua ya kulegeza vizuizi vya kudhibiti maambukizi ya ugonjwa huo imeanza kutekelezwa katika majimbo mengi nchini humo.

Idadi ya vifo vinavyotokea ya kila siku imeongezeka kwa wastani hadi 2000 tangu katikati ya mwezi wa Aprili, licha ya hatua zinazotekelezwa kumaliza janga hilo.

Idadi hii iko juu zaidi ya ile ya homa ya msimu kwa miaka yote tangu mwaka 1967, pia inazidi ile ya UKIMWI kwa kipindi cha miaka ya 1981 hadi 1992, ikimaanisha miaka kumi na moja kufuatia kuanza kwa ugonjwa huo.

Kuhusu idadi ya visa vya maambukizi, zaidi ya watu milioni 1.3 wamepata virusi vya Corona na idadi ya jumla ya kila siku inaendelea kuongezeka, hasa huko Mississippi, Minnesota na Nebraska.

Kwa upande mwingine, idadi ya maambukizi imepunguka katika jimbo la New Jersey na Jimbo la New York


Share:

PAKUA APP YA MALUNDE 1 BLOG ...IMEBORESHWA KWA UBORA WA HALI YA JUU KUKUWEZESHA KUPATA HABARI ZOTE KWA WAKATI KIPINDI HIKI CHA CORONA

Kuwa wa Kwanza kupata habari na matukio yanayojiri Tanzania na dunia kwa ujumla kwa kupakua/ kudownload App ya Malunde 1 blog tukuhabarishe masaa 24.


Tembea na dunia kiganjani mwako sasa.

Pakua App mpya ya Malunde 1 blog imeboreshwa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wasomaji wetu. Hii ndiyo mpya kabisa,ina alama hii ↡↡
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.malunde.blog
Ni rahisi sana : Ingia Play store kisha Andika Malunde 1 blog halafu bonyeza Install

https://bit.ly/2Qb7qyF

Tafadhali fuata maelekezo hapo juu... Usikubali kukosa habari kizembe..Pakua app yetu Mpya ya Malunde1 blog Sasa
Share:

FULL POWER, ZATI 50 NI KIBOKO YA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA UUME MDOGO

Zati 50
Full Power
Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume:


⇒Ngiri,

⇒Henia

⇒Kisukari

⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri

⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu

⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi

⇒Msongo wa mawazo 



⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.



FULL POWER



⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.



⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Zati 50

⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

Madereva Wa Tanzania Walalamika Zoezi La Upimaji Corona Mpaka wa Namanga Kwenda Kenya

Madereva wa malori na magari 302 waliokuwa wanasafirisha bidhaa na abiria kwenda nchi jirani ya Kenya, jana walizuiliwa katika mpaka wa Namanga hivyo kushindwa kuingia nchini Kenya hadi hapo watakapopimwa kama wana virusi vya Corona na kusubiri majibu ndani ya masaa 48.

Wakizungumza katika mkutano ulioitishwa na mkuu wa wilaya ya Longido, Frank Mwaisumbe, baadhi ya madereva hao, walilalamikia zoezi hilo la upimaji wa nguvu mpakani na huku wakihofia pia matokeo ya vipimo.

Dereva Audax Ntebe amesema wamekosa Imani na zoezi la upimaji kwa kuwa hakuna tahadhari ya upimaji lakini pia hakuna uwakilishi wa Tanzania huku dereva Kassim Mkali akisema wakati wamezuiwa kuingia kenya, bado wanalipishwa ushuru wa maegesho kwa siku kiasi cha sh 4000 na fedha za ulinzi wa magari sh 3000 kwa siku jambo ambalo linaendelea kuwapa ugumu wa maisha.

Akizungumza na madereva hao, mkuu huyo wa wilaya, Mwaisumbe alisema tayari amewasiliana na mkuu wa wilaya ya Kajiado juu ya kupinga zoezi hilo ambalo amesema haliendi katika hali sahihi kutokana na kukosa uwakilishi kwa upande wa Tanzania.

Kufuatia hatua hiyo Mwaisumbe amesema kuanzia sasa magari na madereva kutoka kenya wanaoingia nchini, pia watatakiwa kupimwa na kusubiri majibu masaa 48 kama wanavyofanya wakenya.


Share:

Mbarali District Council Various Jobs (Watendaji)

Mbarali District is one of the seven districts of Mbeya Region, Tanzania. It is bordered to the north and east by Iringa Region, to the south by Mbeya Rural District and to the west by Chunya District. 



Share:

Monday, 11 May 2020

41 New Government Jobs at MNH, TPRI, NAOT, STAMICO and SUA

Overview:
The Public Service Recruitment Secretariat (PSRS) is a government organ with a status of independent Department established specifically to facilitate the recruitment process of employees to the Public Service. Public Service Recruitment Secretariat was established by the Public Service Act No. 8 0f 2002 as amended by Act No. 18 of 2007, section 29(1)


Public Service Recruitment Secretariat (PSRS) On behalf of the Muhimbili National Hospital (MNH), Tanzania Insurance RegulatoryAuthority (TIRA), Tanzania Tropical Seeds Research Institute (TPRI),The National AuditOffice of Tanzania (NAOT), The State Mining Corporation (STAMICO) and SokoineUniversity of Agriculture (SUA), Public Service Recruitment Secretariat invites qualifiedTanzanians to fill 41 vacant posts as mentioned in the PDF file attached;

 Click link below to download the file:

Deadline for application is 21st May, 2020;

DOWNLOAD PDF FILE HERE


Share:

LHRC WACHANGIA VIFAA KINGA, MAPAMBANO DHIDI YA CORONA

Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Anna Henga (katikati) akiwa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dkt. Rashid Mfaume wakati wa makabidhiano ya vifaa kinga.
***

Katika kukabiliana na mlipuko wa virusi vya corona, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kimeendelea kuchukua hatua mbalimbali ikiwemo kuendelea kutoa elimu kwa umma juu ya namna ya kukabiliana na maambukizi. 

Maambukizi ya virusi vya corona yanaathiri haki za msingi ikiwemo haki ya kuishi, haki ya kufanya kazi na kupata ujira, haki ya kujumuika na hata haki ya kuishi, hii inailazimu LHRC kutoa elimu kwa jamii kwa ujumla na makundi yanayoathirika zaidi kufuatia mlipuko wa COVID-19. 

Sambamba na kutoa elimu na msaada wa kisheria kwa makundi haya, LHRC imeendelea kushirikiana na wadau na mamlaka za serikali ikiwemo Wizara ya Afya katika kukabiliana janga hili.

 Leo Mei 11, 2020, Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu kimechangia kwa serikali vifaa tiba ikiwemo mavazi ya kujikinga (PPE) 300 na barakoa za madaktari 300 vyenye jumla ya thamani ya milioni 21. 

Akizungumza wakati wa makabidhiano ya vifaa hivyo yaliyofanyia jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Wakili Anna Henga amesema LHRC kama watetezi wa haki za binadamu wameguswa na janga la corona na wameamua kuchangia sekta ya afya kwa kuzingatia kwamba sekta hiyo iko mstari wa mbele katika kukabiliana na virusi vya corona. 

“Tumeguswa kuchangia kidogo tulichojaaliwa na tukaona tuchangie vifaa vitakavyowasaidia watoa huduma za afya kuendelea kutoa huduma huku wakilinda haki yao ya afya. LHRC tunafanya utetezi wa haki zote za binadamu na katika hili la haki ya afya tumechukua hatua na tutaendelea kuchukua hatua kukabiliana na corona” – alisema Anna Henga 

Kwa upande wake mwakilishi wa Serikali, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Dkt. Rashid Mfaume amewashukuru LHRC kwa kutoa vifaa hivyo na kuwataka wadau wengine kuendelea kutoa misaada kwa sekta ya afya.‬

‪“Huu ni msaada tuliokuwa tunauhitaji sana, tunafahamu vifaa hivi vina gharama kubwa lakini ninyi mmejitoa kwa kujali umuhimu wa haki ya afya. Tunawashukuru kwa kujitoa na tunawakaribisha wadau wengine wachangie zaidi”. alisema Dkt. Mfaume‬

Katika mapambano dhidi ya virusi vya corona wadau mbalimbai wameungana na serikali kwa namna mbalimbali kuhakikisha wanatokomeza ugonjwa huo hatari nchini. LHRC wanakuwa sehemu ya wadau waliochangia katika utoaji elimu na utoaji wa misaada ya moja kwa moja.
Share:

CHADEMA YAWAFUTA UANACHAMA WABUNGE WANNE


“Kamati Kuu CHADEMA imeazimia Wabunge Anthony Komu na Joseph Selasini pamoja na kuwa wamejipotezea sifa ya uanachama wa CHADEMA, wameendelea kutoka kauli za kejeli, kashfa na kukiuka maagizo ya Chama, hivyo Chama kimeazimia kuwafukuza uanachama” -John Mnyika, Katibu Mkuu CHADEMA.


“Mbunge David Silinde na Wilfred Rwakatare sio tu wamekiuka agizo la Chama bali wamekuwa wakijitokeza kwenye vyombo vya habari kutoa maneno ya kashfa na kejeli dhidi ya maagizo ya Chama na Viongozi wa Chama, Kamati Kuu CHADEMA imefikia uamuzi wa kuwafuta uanachama”- Mnyika

“Mjumbe wa Kamati Kuu CHADEMA,  Mariamu Msabaha, ameshiriki kukiuka maagizo ya Chama, ilitakiwa awe mfano na kwa kuwa amekwenda kinyume, amevuliwa nafasi zake zote ndani ya Chama na kubaki na Ubunge na atatakiwa ajieleze kwanini asichukuliwe hatua zaidi kwa kukiuka maagizo”-Mnyika

“Kuhusu Wabunge wengine ambao wamekwena kinyume na maagizo ya Chama lakini hawajaonesha utovu wa nidhamu kwa kutoa kashfa kwa Chama, watatakiwa wajieleze kwanini wasichukuliwe hatua zaidi kwa kukiuka maagizo” -Mnyika
Share:

Picha : SHIRIKA LA AGAPE LATOA MSAADA WA VIFAA KUKABILIANA NA CORONA VIJIJI VYA KATA YA MWAMALA SHINYANGA


Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la AGAPE ACP, John Myola (kushoto) akimkabidhi ndoo ya kunawia mikono Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko. Shirika limetoa msaada wa ndoo 62, sabuni 62 za maji na barakoa 150 kwa ajili ya kusaidia wananchi wa vijiji vya kata ya Mwamala halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ili kukabiliana na Maambukizi ya Virusi vya Corona.  Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la AGAPE ACP, John Myola (kushoto) akimkabidhi ndoo ya kunawia mikono Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko. 
 Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko (kulia) akijaribishia kufungua ndoo ya kunawia mikono.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la AGAPE ACP, John Myola (kushoto) akimkabidhi sabuni za maji kwa ajili ya kunawia mikono Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko.
Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la AGAPE ACP, John Myola (kushoto) akimkabidhi barakoa Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko.
Kushoto ni Mkurugenzi wa Shirika la AGAPE ACP, John Myola akizungumza wakati wa akimkabidhi Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko mchango wa vifaa  kwa ajili ya kushirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya Corona.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko (kulia) akilishukuru Shirika la AGAPE kwa kutoa mchango wa vifaa  kwa ajili ya kushirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya Corona huku akiwaomba wadau wengine kujitokeza kusaidiana na serikali kukukabiliana na COVID -19. 
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko (kulia) akizungumza wakati akipokea msaada wa ndoo 62,sabuni 62 za maji na barakoa 150 zilizotolewa na Shirika la AGAPE ACP kwa ajili ya kusaidia wananchi wa vijiji vya kata ya Mwamala halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ili kuiunga mkono serikali katika mapambano dhidi ya Virusi vya Corona. 
Muonekano wa sehemu ya ndoo, sabuni na barakoa zilizotolewa na shirika la AGAPE ACP.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Shirika la Agape ACP limetoa msaada wa ndoo 62, sabuni 62 za maji na barakoa 150 kwa ajili ya kusaidia wananchi wa vijiji vya kata ya Mwamala halmashauri ya wilaya ya Shinyanga ili kuiunga mkono serikali katika mapambano dhidi ya Virusi vya Corona. 

Akikabidhi vifaa hivyo kwa Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko leo Jumatatu Mei 11,2020, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la AGAPE ACP, John Myola amesema vitaongeza nguvu katika mapambano dhidi ya Virusi vya Corona. 

“AGAPE ACP kwa kushirikiana na kamati za MTAKUWWA tumekuwa tukitoa elimu kuhusu masuala ya ukatili wa kijinsia na madhara ya mimba na ndoa za utotoni lakini sasa pia tutatoa elimu kuhusu Corona kwani huenda katika kipindi hiki cha Corona kuna vitendo vya ukatili wanafanyiwa watoto”,alieleza Myola. 

“Kwa kuwa tunatekeleza mradi wa Utu wa Msichana kwa ufadhili wa shirika la MUNDO Co-Operante katika kata ya Mwamala tumeona ni vyema tuchangie ndoo za kunawia mikono,sabuni za maji na barakoa ambavyo tutavigawa katika vijiji vinne vya kata ya Mwamala,zahanati na familia duni zitakazotambuliwa na serikali ya kijiji kuwa hazina uwezo wa kununua vifaa vya kupambana na Corona”,aliongeza Myola. 

Akipokea mchango huo, Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko amelishukuru Shirika la AGAPE kwa kushirikiana na serikali katika mapambano dhidi ya Corona huku akiwaomba wadau wengine kujitokeza kusaidiana na serikali kukukabiliana na COVID -19. 

“Tunawashukuru AGAPE ACP kwa mchango huu na upendo wenu kwa wananchi wa Shinyanga. Mkienda Mwamala hakikisheni mnawasisitiza wananchi wanawe mikono kila wanapohitaji kupata huduma za kijamii wasishike kitu bila kunawa”,alisema Mboneko. 

“Wasisitizeni wazazi na walezi kulinda watoto wao wasizurure minadani bali watulie majumbani na wajisomee wasiwaozeshe na wananchi wasitumie barakoa zilizotengenezwa kwa mifuko ya plastiki”,aliongeza Mboneko.
Share:

Waziri Mkuu wa Uingereza alegeza vikwazo kwa mara ya kwanza nchini humo Tangu Janga La Corona Liikumbe Nchi Hiyo

Waziri Mkuu wa Uingereza Boris Johnson kwa mara ya kwanza ametangaza kulegeza vikwazo dhidi ya virusi vya corona. 

Johnson amesema kuanzia leo, watu ambao walikuwa hawawezi kufanya kazi wakiwa nyumbani, wanaweza kurudi kazini. 

Waziri Mkuu huyo pia amesema kuanzia Jumatano watu walio na jamaa zao majumbani wanaweza kutoka nje tena bora tu wadumishe kanuni za umbali wa mtu mmoja na mwingine.

 Amesema kuanzia Juni mosi, serikali yake itatoa tangazo la iwapo maduka yataanza kufunguliwa taratibu na iwapo wanafunzi wa shule za msingi wataweza kurudi shule. 

Johnson vile vile ametoa ruhusa ya watu kufanya mazoezi. 

Uingereza imeshuhudia vifo vya watu 32, 0000 vilivyotokana na mamabukizi ya Corona, huku maelfu wakiambukizwa, ikiwa nchi ya pili baada ya Marekani duniani kuwa na idadi kubwa ya maambukizi.


Share:

Naibu Waziri wa Afya Dkt Faustine Ndugulile Akanusha Taarifa Kwamba Ni Mgonjwa

Naibu Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt Faustine Ndugulile, amekanusha taarifa za kwamba yeye ni mgonjwa na hali yake ni mbaya, zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii.

Dkt Ndugulile amezikanusha taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa Twitter leo Mei 11, 2020, na kusema kuwa taarifa hizo zipuuzwe kwamba yeye ni mzima wa afya.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger