Friday, 1 May 2020

FISI AUA MTOTO WA MIAKA MITATU AKICHEZA NA WENZAKE KISHAPU


Kamanda wa polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 
Mtoto aitwaye Sungwa Kulwa mwenye umri wa miaka mitatu (03) mkazi wa kijiji cha Dodoma Kata ya Masanga, wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga amefariki dunia baada ya kushambuliwa na fisi sehemu za kichwani wakati akicheza na wenzake nje ya nyumba yao. 

Kamanda wa polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba amesema tukio hilo limetokea jana Aprili 30,2020 majira ya saa moja usiku katika kijiji cha Dodoma Kata ya Masanga, Wilaya ya Kishapu

“Mtoto huyo alikuwa akicheza na watoto wenzake nje ya nyumba yao umbali wa mita kumi, ndipo fisi huyo alitokea kwa ghafla kutoka vichakani na kumshambulia kisha kumburuza umbali wa mita 100 ambapo alimuachia baada ya kusikia kelele za wananchi waliokuwa wakimfukuza”,ameeleza Kamanda Magiligimba. 

Kamanda Magiligimba ametoa wito kwa wazazi na walezi kuhakikisha watoto wako mazingira salama muda wote, wasiachwe peke yao na kuwataka wananchi kuchukua tahadhari hasa kwa kipindi hiki ambacho fisi wamekuwa wakionekana maeneo mbalimbali ya mkoa wa Shinyanga.
Share:

RAIS UTPC : WAAJIRI KATIKA VYOMBO VYA HABARI WABORESHE MASLAHI YA WAANDISHI WA HABARI KIPINDI HIKI CHA COVID - 19

Rais wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), Deogratius Nsokolo

Leo ni Mei Mosi 2020, tukiadhimisha katika kipindi ambacho tupo katika vita kubwa ya kukabiliana na ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Corona.

Sekta ya Habari nchini Tanzania ni moja kati ya sekta ambazo zimeathiriwa sana na hali hii.

Wito wangu ni kwa waajiri yaani vyombo vya habari kuboresha maslahi ya waandishi wa habari kutoa ajira rasmi na kuwapa mikataba, kuthamini mchango wa waandishi wa haabri katika vyombo vyao, kulipa kwa wakati madai mbalimbali,kuanza kuwalipa waandishi walau kila wiki ili waweze kukabiliana na changamoto za maisha kwa sasa kutokana na kutokuwepo kwa shughuli na baadhi yao kulazimika kukaa nyumbani.

Ni matumaini yangu wakati tukiadhimisha Sikukuu ya Wafanyakazi, waandishi wa habari nchini wanatumia siku hii kutafakari namna ya kuboresha kazi zao, kuongeza juhudi na maarifa, kuzingatia sheria na taratibu za nchi huku waajiri na wamiliki wakitafakari pia kuzingatia sheria za kazi na sheria nyingine ili kumfanya mwandishi na chombo cha habari kutenda haki na kuwajibika kwa umma.

Nawatakia Sikukuu Njema, TUFANYE KAZI KWA UANGALIFU, TUFUATE MAELEKEZO YA WATAALAMU, CORONA NI HATARI, IPO NA INAUA, TUJILINDE NA TUWALINDE WAPENDWA WETU.
Rais wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC).

Share:

CHADEMA Yazuia Wabunge Wake Kwenda Bungeni.....Yawataka Wajiweke Karantini Kwa Siku 14

Chama cha Demokrasia na Maendeleo- CHADEMA kimetoa maelekezo kwa Wabunge wake wote, kutohudhuria tena vikao vya Bunge vinavyoendelea,na wajiweke Karantini kwa muda wa siku 14 na wasiende majimboni kwao kipindi hiki mpaka pale watakapothibitika hawana maambukizi ya Virusi vya Corona

Taarifa iliyotolewa na  Mwenyekiti wa chama hicho Freeman Mbowe leo Ijumaa May 1, 2020  imetoa maelekezo manne kwa wabunge wa chama hicho ambayo ni; Kutohudhuria vikao vya bunge au kamati za bunge,Kutofika eneo la Bunge Dodoma na Dar es Salaam, Wabunge wajiweke karantini kwa muda wa siku 14, wabunge wa chama hicho wasiende mikoani au majimboni bali wabaki Dodoma hadi itakapothibitika hawana maambukizi

Aidha, CHADEMA  pia wameshauri Bunge lisitishwe kwa siku 21 ili kuruhusu wabunge wote kwenda Karantini, Wabunge wote wapimwe pamoja na familia zao na Kamati za Bunge zifanye vikao kwa njia ya mtandao


Share:

TANZIA: Waziri wa Katiba na Sheria , Mh. Balozi Dkt. Augustine Mahiga, amefariki dunia ......Rais Magufuli Atuma Salamu za Rambirambi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anasikitika kutangaza kifo cha Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Philip Mahiga (Mbunge) kilichotokea leo alfajiri tarehe 01 Mei, 2020 Jijini Dodoma.

Mhe. Balozi Mahiga ameugua ghafla akiwa nyumbani kwake Jijini Dodoma na amefikishwa hospitali akiwa tayari ameshafariki dunia.

Mhe. Rais Magufuli ametoa salamu za pole kwa familia ya Marehemu, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Yustino Ndugai, Wabunge, Wafanyakazi wa Wizara ya Katiba na Sheria na wananchi wa Mkoa wa Iringa kwa kuondokewa na mpendwa wao, na amesema anaungana nao katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.

Mhe. Rais Magufuli amemuelezea Marehemu Balozi Mahiga kuwa alikuwa mchapakazi, mwadilifu, mzalendo na Mwanadiplomasia mahiri aliyeiwakilisha na kuipigania Tanzania katika njanya za Kimataifa kwa miaka mingi.

“Pamoja na umri wake mkubwa na uzoefu wa kushika madaraka katika nyadhifa mbalimbali za Kitaifa na Kimataifa, Marehemu Balozi Mahiga alikuwa mnyenyekevu na mtiifu kwa kila jukumu nililomtuma” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Amemuombea kwa Mwenyezi Mungu aipumzishe roho yake mahali pema peponi, Amina.




Share:

Rais Magufuli Awapongeza Wafanyakazi na Kuwatakia Heri katika Siku ya Leo ambayo ni Mei Mosi ( Siku ya Wafanyakazi)




Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa May 1




















Share:

Thursday, 30 April 2020

Bilioni 33 Kutumika Kuimarisha Huduma Za Kijamii Nchini Tanzania

NA WAMJW Dodoma
Wizara ya Afya, kupitia Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii inatarajia kutumia Jumla ya shilingi bilioni 33.195 ili kutekeleza shughuli mbalimbali za kijamii hususani zilizopewa kipaumbele kwa mwaka wa fedha 2020/21.

Akiwasilisha Hotuba ya Wizara ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto  Mhe. Ummy Mwalimu amesema katika mwaka wa fedha 2020/21 Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii inatarajia kutumia kiasi hicho cha fedha kwa lengo la kuimarisha huduma na mafunzo kwenye Taasisi za Ustawi na Maendeleo ya Jamii, kukarabati makazi ya wazee, kujenga mahubusu za watoto na kutokomeza ukatili wa kijinsia.

Alisema kuwa bajeti hiyo itasaidia kuimarisha Kujenga kumbi pacha na hosteli katika Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru ambapo jumla ya shilingi bilioni 2.7 zimetengwa, pia kuboresha utoaji wa mafunzo ya taaluma ya maendeleo ya jamii ili kukidhi mahitaji ya soko sambamba na kukuza ujuzi wa wahitimu ikiwemo kuwajengea uwezo wa kujiajiri na kuajiriwa kwa kutenga jumla ya shilingi bilioni 6.6.

Maeneo mengine yaliyotengewa fedha ni pamoja na ukarabati wa majengo na miundombinu katika makazi ya wazee kwa shilingi milioni 400, ujenzi wa Shule ya Maadilisho katika Mkoa wa Geita shilingi milioni 200, kuimarisha ujenzi wa mahabusu ya watoto katika mikoa ya Kigoma na Mtwara shilingi milioni 700 na kuwezesha Taasisi ya Ustawi wa Jamii kuboresha utoaji wa mafunzo yanayokidhi mahitaji ya soko shilingi milioni 250.

Aidha, jumla ya shilingi milioni 827.95 zimetengwa kwa ajili ya shughuli za kutokomeza ukatili wa kijinsia katika jamii.

“Ili kutekeleza vipaumbele vilivyoanishwa kwa mwaka 2020/21, Wizara kupitia Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii imekadiria kutumia kiasi cha shilingi bilioni 33 kwa ajili ya kutekeleza majukumu mbalimbali ya Wizara ikiwa ni pamoja na uendeshaji wa ofisi na miradi ya maendeleo” alisema.

Mhe. Ummy amesema Wizara imeendelea kukuza ari ya jamii kushiriki katika kujiletea maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa kutumia nguvu kazi na rasilimali zinazowazunguka na kusimamia masuala yote ya ushirikishwaji wa jamii kwenye sekta mbalimbali.


Share:

Safari Za Kwenda Kuwatembelea Ndugu Vijijini Zisubiri Corona iishe:- Dr Subi

Na WAMJW- DSM
Mkurugenzi wa huduma za kinga Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Leonard Subi ametoa wito kwa wananchi kutosafiri kwenda vijijini kwa lengo la kuwasalimia ndugu katika kipindi hiki ili kuzuia maambukizi ya virusi vya Corona kusambaa zaidi nchini.

Wito huo ameutoa leo, wakati akiongea na Waandishi wa habari katika ofisi ndogo za Wizara ya Afya Jijini Dar es Salaam juu ya mwenendo wa kampeni ya “Mikono safi, Tanzania salama” inayolenga kuelimisha wananchi juu ya kujikinga dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

“Kwa wanaotaka kwenda kuwatembelea Wazee kijijini, wasubiri Corona iishe, kwasababu tunaona watu watatoka kwenye miji ambayo inamaambukizi wanaenda vijijini kuwatembelea wazazi ambao umri wao umeenda, inawezekana wana magonjwa ya uzeeni, kunauwezekano mkubwa wakuwaambukiza huko” alisema.

Aliendelea kusisitiza kuwa, katika maeneo yote yenye msongamano hususan maeneo ya biashara na huduma za Afya, waweke utaratibu mzuri, utaosaidia wateja kukaa umbali wa mita moja au zaidi pindi wanaposubiri kupata huduma, hali itayosaidia kukata mnyororo wa maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine.

“Maeneo ya kutoa huduma mbali mbali, ikiwemo Hospitali na vituo vya Afya, waweke utaratibu mzuri, watu wanaokuja kupata huduma wakae katika utaratibu wa mita moja au zaidi ili watu hawa wasiweze kuambukizana maradhi, lengo likiwa kukata mnyororo wa maambukizi kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mtu mwingine ” alisema

Aliendelea kusema, ni muhimu uvaaji wa Barakoa uzingatiwe katika ngazi zote, hasa katika maeneo yenye mkusanyiko wa watu, huku akisisitiza kuwa, ni muhimu kuzichoma moto Barakoa zilizotumika ili kuepusha usambaaji wa magonjwa ya mlipuko yanayoweza kujitokeza.

“Tunasisitiza uvaaji wa Barakoa, hasa unapokuwa kwenye mkusanyiko wa watu, lakini barakoa sio kitu salama baada ya kumaliza kukitumia, kinakuwa kichafu na maambukizi, kwa mantiki hiyo, hakikisha unaitupa sehemu salama na unachoma moto ili mtu mwingine asiweze kuikokota na kuitumia tena ” alisema

Aidha, Dkt. Subi amesema kuwa, bado elimu ya kunawa mikono kwa sabuni na maji safi yanayotiririka haijaeleleweka vizuri, hivyo kuitaka timu ya hamasa kuongeza nguvu katika hatua zote tano za unawaji mikono ili elimu hiyo isaidie katika mapambano dhidi ya maambukizi ya virusi vya Corona.

“Tunaposema kunawa mikono kwa maji safi yanayotiririka na sabuni tunamaana kwamba, unapokwenda kunawa hakikisha sabuni imekolea vizuri kwenye kiganja cha mikono, hakikisha umesugua vizuri, povu la sabuni limeshika vizuri, na hakikisha umenawa vizuri mbele, nyuma, kwenye vidole na kila eneo la mikono vizuri kwa sekunde zisizopungua 20″alisema

Akiwasilisha ripoti ya utendaji kazi wa kampeni ya “mikono safi, Tanzania salama,” Mkuu wa Kitengo cha maji na usafi wa mazingira, Wizara ya Afya, Ndg. Anyitike Mwakitalima ameweka wazi kuwa, mpaka sasa timu hiyo ya uhamasishaji imeshatembelea jumla ya maeneo 145 kati ya 213 yaliopangwa yametembelewa ikiwa ni sawa na asilimia 68.

Mbali na hayo amesema kuwa, licha ya kutoa elimu ya tahadhari, kikosi cha uhamasishaji kimekuwa kikitoa zawadi kwa taasisi na watu ambao wanazingatia maelekezo yanayotolewa na Wizara, vikiwemo vitakasa mikono (Sanitizer), viang’azi (Reflectors) na khanga za Kampeni.


Share:

Serikali Haitopanga Bei Za Mazao Ya Wakulima

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma
Serikali imesisitiza kuwa haitopanga wala kuingilia bei za mazao ya wakulima nchini badala yake wakulima watajipangia bei na kuuza wenyewe ilihali serikali ikisalia kama msimamizi.

Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba (Mb) ameyasema hayo leo tarehe 30 Aprili 2020 wakati akizungumza na viongozi wa TADCOs Co ltd kuhusu hatua iliyofikiwa ya uagizaji wa mbolea katika ukumbi wa KILIMO IV Jijini Dodoma.

Mhe Mgumba amesema kuwa mfumo wa biashara ulivyo unategemea zaidi ujazo wa mazao sokoni, hivyo bei haitolewi kutokana na gharama alizotumia mkulima wakati wa uzalishaji badala yake bei inaendana na soko.

Amesema kuwa wakulima kama wanavyoruhusiwa kuzalisha kadhalika wakulima hao watauza mazao yao popote watakapotaka wao lakini kwa kufuata taratibu na sheria za nchi.

Kuhusu Mfumo wa stakabadhi ghalani Naibu Waziri Mhe Mgumba amesema kuwa mfumo huo ulianzishwa kwa lengo la kumrahisishia huduma za biashara mkulima hivyo utaendelea kutumika kwa mujibu wa matakwa ya kuanzishwa kwake.

Amesema kuwa zipo changamoto nyingi katika utekelezaji wa mfumo huo unaochagizwa na viongozi wanaosimamia hususani wa vyama vya Ushirika kutotekeleza kwa mujibu wa sheria.

“Mtu akipeleka mazao yake ghalani lengo la serikali kwa sababu mazao yote tunategemea msimu wa mvua na upatikanaji wake ni wa wakati mmoja hivyo kuhifadhi kwa pamoja na kupewa stakabadhi itakayomrahisishia kupata mkopo kwa ajili ya kukidhi mahitaji yake wakati akisubiri gharama za mazao zikipanda aweze kuuza kwa bei nzuri” Alikaririwa Mhe Mgumba

Mhe Mgumba ameongeza kuwa mfumo huo ni mzuri endapo utaendelea kusimamiwa vizuri ikiwa ni pamoja na kuendelea kuuboresha zaidi ili uwanufaishe wakulima kote nchini kwani mfumo huo unapunguza gharama za uendeshaji.

Ameeleza kuwa miongoni mwa changamoto waliyokuwa nayo wakulima ilikuwa ni Tija ndogo katika mavuno yao yaliyosababishwa na matumizi madogo ya mbolea hivyo serikali ilitoa elimu ya kutosha kwa wakulima kuhusu matumizi sahihi ya mbolea hivyo katika kipindi cha serikali ya awamu ya tano tija imeongezeka.

Mgumba amesema kuwa matumizi sahihi ya mbolea yameongeza tija katika sekta ya kilimo kwani uzalishaji umeongezeka na wakulima wamekuwa na kipato kikubwa.

Katika kikao kazi hicho Naibu Waziri wa Kilimo Mhe Omary Mgumba amesema kuwa nchi ina mbolea ya kutosha ambapo ina akiba ya zaidi ya Tani 203,000 iliyotokana na uagizaji wa mbolea uliofanywa kwa mwaka mzima wa kiasi cha mbolea Tani 633,197


Share:

Wenye Virusi vya Corona Kenya Wafika 396....Ni Baada ya Wengine 12 Kuongezeka Leo

Idadi ya watu walioambukizwa virusi vya corona nchini kenya, imefikia 396  baada ya wengine 12 kuongezeka leo April 30, 2020

Wizara ya afya nchini humo  imesema kwamba kati hao 12 walioambukizwa, 7 wanatoka Mombasa, 3 Nairobi, Kitui 1 na Wajir 1.

Kwa saa 24 zilizopita, wagonjwa 15 wamepona ikiwa ndio idadi ya juu tangu kutangazwa kwa virusi hivi nchini mno huku wale waliopona wakifikia 144 kwa ujumla.
 
Aidha wawili wamethibitishwa kufariki na kufikisha idadi hiyo kuwa 17.


Share:

Kwanini Baadhi Ya Watu Wana Uzito Mdogo Kupita Kiasi ? ( Kukonda Na Kudhoofu Mwili )

Kuna  idadi  kubwa  ya  watu  ambao wana  kabiliwa  na  tatizo  la kuwa  na  uzito  mdogo kupita  kiasi.

Kwa  mujibu  wa   tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  ni  jambo  linalo weza  kuhatarisha  afya  ya  mhusika.

Kama  ilivyo  kwa  suala  la  kuwa  na  uzito  mkubwa  kupita  kiasi,  suala  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  pia  lina  madhara  mengi  katika  afya  ya  binadamu.

MADHARA   YA KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI  (  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )

Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, yafuatayo  ni  madhara  ya  kiafya  yanayo  weza  kumpata  mtu  mwenye  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi.

1.    Kupungua  na  kudhoofika  kwa  kinga  ya  mwili
2.    Kuwa  katika hatari  ya  kushambuliwa  na  magonjwa  ya  mifupa  kwa  sababu  mwili hushindwa  kupokea  na  kutengeneza  virutubisho  muhimu  vinavyo hitajika  katika  kuimarisha  afya  ya  mifupa
3.    Kuwa na  nywele  zisizo  na  afya  (  Kinyonyoki)
4.    Kuwa  na ngozi  isiyo  na  afya
5.    Kuugua  mara  kwa  mara  kutokana  na kuwa  na  kinga  dhoofu  ya  mwili.
6.    Watu  wenye  uzito  mdogo  kupita  kiasi  huwachukua  muda  mrefu  kupona  hata  magonjwa  ya  kawaida  ambayo  hupona  ndani ya  muda  mfupi
7.    Kujisikia  uchovu  muda  mwingi
8.    Kupungukiwa  damu  ambako  huweza  kusababisha hali   kama  vile  kizungu  zungu na  maumivu  ya  kichwa  ya  mara  kwa  mara.
9.    Kwa  wanawake , tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi  linaweza  kuathiri  mpangilio  wa  hedhi  ambao  unaweza  kupelekea  matatizo  katika  uzazi.

10.  Na  kwa  mwanamke  mjamzito  mwenye  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi, anaweza  kupatwa  na  tatizo la  kujifungua  kabla  ya wakati  yani  kabla  ya  wiki  37.

11.  Tatizo  la  uzito mdogo  kupita  kiasi  huathiri  ukuaji  wa  watoto.  Watoto  wadogo  wanahitaji  kuwa  na  virutubisho  vya  kutosha  ili  waweze  kukua  na  kuongezeka  na kuwa  na  mifupa  yenye  afya.  Ukosefu  wa  vitu  hivyo  maana  yake  ni  kwamba  mtoto  husika  hatoweza  kukua  na  kuongezeka  vizuri .  Vilevile  tatizo  la  uzito  mdogo  kupita  kiasi  linaweza  kusababisha  tatizo  la  mifupa  kwa watoto  jambo  ambalo  ni  hatari kwa  mustakabali  wa  afya  za  watoto  husika

CHANZO   CHA   TATIZO   LA   KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI ( KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )
Kwa  mujibu  wa  tafiti  mbalimbali  za  kitaalamu, zifuatazo  ni  baadhi  ya  sababu  kuu  za  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi ( Kukonda  na  kudhoofu  mwili )

1.    Kuugua  magonjwa  na  matatizo  mbalimbali  ya  kiafya  kama  vile  vidonda  vya  tumbo,presha   na kisukari.

2.    Msongo  wa  mawazo.

3.    Kujinyima  kula  ( Kufanya  diet  ngumu )  au  kukosa  hamu  ya  kula  kwa  muda  mrefu.  Kukosa  hamu ya  kula  kunaweza  kuwa  kumesababishwa  na  eidha  kuugua  magonjwa  na matatizo  mbali  mbali  ya  kiafya  au  kupatwa  na  tatizo  la  msongo wa  mawazo.

SULUHISHO   LA  TATIZO  LA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI( KUKONDA NA  KUDHOOFU  MWILI )
Unaweza  kumaliza  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  kwa  kuzingatia  kula  mlo  kamili  (  Balanced  Diet ) au  kwa  kutumia  DAWA  ZA  ASILI  ambazo  ni  maalumu  kwa  ajili  ya  kumaliza  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi (  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )

DAWA  YA  ASILI INAYO  MALIZA  TATIZO  LA  KUWA  NA  UZITO  MDOGO  KUPITA  KIASI ( TATIZO  LA  KUKONDA  NA  KUDHOOFU  MWILI )
Ipo  DAWA –LISHE  YA ASILI  ambayo  INATIBU  na  KUMALIZA  kabisa  tatizo  la  kuwa  na  uzito  mdogo  kupita  kiasi  ambalo  linaenda  sambamba  na  kukonda  na  kudhoofu  mwili.  Dawa  hii  ni  ya asili  kabisa  isiyo  na  kemikali  yoyote  ya  viwandani  na  inayo  saidia  kutibu  na kumaliza tatizo  hili  na  kuurudisha  mwili  katika  afya  yake  ya  awali  ndani  ya  siku  thelathini.

JINSI  YA  KUPATA DAWA  HII:  Jinsi  ya  kupata dawa  hii, fika  katika duka  la  kuuza  dawa  za  asili  la  NEEMA  HERBALIST.  Tunapatikana  UBUNGO  jijini  DAR  ES  SALAAM   nyuma  ya  JENGO  LA  UBUNGO  PLAZA  jirani  na  SHULE  YA  MSINGI  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Wasiliana  nasi  kupitia  simu  namba  0693  -  005  189.
Na  kwa  taarifa  Zaidi  kuhusu  huduma  zetu  nyingine, tutembelee  kupitia  tovuti  yetu :

https://ift.tt/1u8My9X


Share:

UNICEF JOBS: Sub-Saharan Roster of Consultants in Child Poverty, Public Financial Management and Social Protection, including Emergency Cash Transfers

Sub-Saharan Roster of Consultants in Child Poverty, Public Financial Management and Social Protection, including Emergency Cash Transfers Apply Job Number: 531360 | Vacancy Link Locations: Africa: Angola, Africa: Botswana, Africa: Burundi, Africa: Comoros, Africa: Chad, Africa: Gabon, Africa: Liberia, Africa: Benin, Africa: Burkina Faso, Africa: Central Afr.Rep, Africa: Congo, Africa: Cote d’Ivoire, Africa: Congo, Dem. Rep, Africa: Djibouti, Africa: Equatorial… Read More »

The post UNICEF JOBS: Sub-Saharan Roster of Consultants in Child Poverty, Public Financial Management and Social Protection, including Emergency Cash Transfers appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Makonda Atoa Msaada Wa Mabati Yenye Thamani Ya Shilingi Milioni 476 Kwaajili Ya Kuezeka Nyumba 1,000 Za Wajane Waliokumbwa Na Mafuriko Dar

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda leo April 30, 2020 ametoa msaada wa mabati yenye thamani ya Tsh. 476m kwa ajili ya Kuezeka nyumba 1,000 za Wajane wa mkoa huo ambazo zimeathiriwa na mafuriko. RC Makonda amewataka pia wananchi waliojenga mabondeni kuhama.

RC Makonda amesema hayo wakati wa Ziara ya Kukagua athari za Mvua  na kubaini uwepo wa familia za Wajane ambao Nyumba zao zimechukuliwa na Mafuriko na sasa wanapitia changamoto ya kuhifadhiwa kwa majirani baada ya kukosa makazi ya kuishi hivyo ameona ni busara kutoa msaada huo kama sehemu ya pole kwa adha waliyoipata.

Aidha RC Makonda amewapa siku 10 Wakuu wa Wilaya kuhakikisha wanapitia maeneo ya Mito na Mabonde kukagua athari za mabadiliko ya tabia nchi kwa kuwashirikisha viongozi wa mitaa ili kwa pamoja watoe mapendekezo ya nini kifanyike kisha wampatie ripoti ya kuonyesha hatua za kukabiliana na Mafuriko ya Mara kwa Mara.

Aidha RC Makonda amesema athari zinazoonekana kwa sasa ni matokeo ya Jamii kuwafumbia macho watu wanovunja sheria kwa kujenga mabondeni, kuchimba mchanga na kuziba mikondo ya maji jambo linalopelekea Mafuriko hivyo ametaka kila mwananchi kuwa mlinzi wa mwenzake.

Pamoja na hayo RC Makonda amesema kwa sasa serikali inaendelea kurejesha miundombinu na madaraja yaliyochukuliwa na Mafuriko ikiwemo ujenzi wa madaraja ya muda mfupi ili kuwezesha shughuli za kijamii kuendelea.


Share:

Country Representative – Tanzania | Global Development Incubator

Company Description Aceli Africa is a market-enabling facility to mobilize over $700M in private sector lending for agricultural SMEs in Uganda, Kenya, Rwanda, and Tanzania by 2025. To achieve this goal, Aceli Africa will provide financial incentives to increase the risk appetite of 20+ financial institutions (both global and local) to make loans ranging from USD $25K-$1.5M to… Read More »

The post Country Representative – Tanzania | Global Development Incubator appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Infectious Disease Specialist at Doctors with Africa CUAMM

Doctors with Africa CUAMM is the first NGO in the healthcare area officially recognized in Italy. Deadline Date: Friday, 15 May 2020 Organization: Doctors with Africa CUAMM Country: United Republic of Tanzania City: Shinyanga Founded in 1950 with the aim of training doctors to work in developing countries, CUAMM is working in Angola, Central African Republic, Ethiopia, Mozambique, Sierra… Read More »

The post Infectious Disease Specialist at Doctors with Africa CUAMM appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

WASH Officer-Hygiene Promotion at Danish Refugee council (DRC)

Wash Officer-Hygiene Promotion Categories: WASH Officer-Hygiene Promotion Location: Nduta camp, Kibondo Start Date: ASAP Contract duration: 5 months PURPOSE: The WASH Officer under the management and supervision of the WASH Team Leader will be responsible to implement different activities of DRC related WASH program to ensure the program’s objectives are achieved. The post holder is directly responsible for all Sanitation… Read More »

The post WASH Officer-Hygiene Promotion at Danish Refugee council (DRC) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Tangazo La Nafasi Za Kazi Katika Shirika La IFAD




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger