Wednesday, 25 March 2020

Auditor II (2 Positions) – NMB Bank

Auditor II (2 Positions) Reporting Line: Audit Manager Job Purpose To maintain an independent Internal Audit that adds value and improves the operations of the Bank through systematic and disciplined approach in evaluating and improving the effectiveness of risk management, control and governance processes. Main Responsibilities • Coordinate audit plans (of small audits) for assigned projects by ensuring… Read More »

The post Auditor II (2 Positions) – NMB Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

1000 Job vcancies at the Ministry of Health 2020 – Medical doctors

Share:

TAMISEMI : How to change Combination Form four graduates in 2019 for 2020/2021 form five selection

Form four graduates in 2019 to change Combination for 2020/2021 selection How to change form five Combination – Students who wish to join Form Five and Colleges for 2020/2021 The Government has provided opportunities for students who passed the Form four exam in 2019 and who are expecting to joining Form Five and varous colleges in 2020 to… Read More »

The post TAMISEMI : How to change Combination Form four graduates in 2019 for 2020/2021 form five selection appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

New Government Job vacancies – Doctors / Dentist ( 610 Post )

Doctor Grade II / Dentist Grade II APPLY HERE

The post New Government Job vacancies – Doctors / Dentist ( 610 Post ) appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Taarifa kwa Umma kuhusu utaratibu wa wanafunzi waliohitimu kidato cha Nne mwaka 2019 kufanya mabadiliko ya machaguo (Combination)




Share:

AIR TRAFFIC MANAGEMENT OFFICERS II – 30 POST – TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY

POST AIR TRAFFIC MANAGEMENT OFFICERS II – 30 POST POST CATEGORY(S) EDUCATION AND TRAINING ENVIRONMENTAL SCIENCES AND GEOGRAPHY LAND MANAGEMENT RESEARCH,SCIENCE AND BIOTECH STATISTICS AND MATHEMATICS TRANSPORT AND LOGISTICS WATER, MINING AND NATURAL RESOURCES EMPLOYER TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY APPLICATION TIMELINE: 2020-03-24 2020-04-06 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i.    To plan, execute and monitor the control of… Read More »

The post AIR TRAFFIC MANAGEMENT OFFICERS II – 30 POST – TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

AERONAUTICAL INFORMATION OFFICERS II – 30 POST AT TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY

POST AERONAUTICAL INFORMATION OFFICERS II – 30 POST POST CATEGORY(S) IT AND TELECOMS LAND MANAGEMENT EMPLOYER TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY APPLICATION TIMELINE: 2020-03-24 2020-04-06 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i.    To assist in accepting, processing and disseminating Flight Plans to all Air Traffic Management units designated Authorities, Search and Rescue units, including those along aircraft flight routes… Read More »

The post AERONAUTICAL INFORMATION OFFICERS II – 30 POST AT TANZANIA CIVIL AVIATION AUTHORITY appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Rais wa DRC atangaza hali ya dharura nchini kote kupambana na virusi vya Corona

Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokraisa ya Kongo DRC ametangaza hali ya dharura nchini kote, ikiwa ni juhudi za kupambana na virusi vya Corona.

Rais Tshisekedi amesema, uamuzi huo umetokana na hatari kubwa ya virusi hivyo, na kutangaza hatua nyingine kadhaa ikiwemo kusimamisha safari zote za kuingia na kutoka katika mji mkuu wa Kinshasa na mikoa mingine ili kuuweka mji huo kwenye karantini.

Rais Tshisekedi amelitaka jeshi la polisi na vikosi vya usalama kufanya dora ya pamoja ili kuhakikisha hatua hizo zinatekelezwa kwa manufaa ya watu wote.

Pia rais Tshisekedi ametangaza kufunga mipaka na kuruhusu malori, meli na ndege za mizigo muhimu tu kuingia nchini humo.

Mpaka sasa, kuna jumla ya kesi 48 za maambukizi ya virusi vya Corona nchini DRC.


Share:

Godbless Lema afikishwa mahakamani

Mbunge wa jimbo la Arusha Mjini, Godbless Lema amefikishwa mahakamani mkoani Singida na kusomewa mashitaka 15.

Tarehe mbili mwezi huu, Lema alikamatwa na polisi mkoani Arusha na kusafirishwa hadi mkoani Singida ili ahojiwe, baada ya kutuhumiwa kutoa taarifa za uongo kuhusu mauaji ya watu 14 wilayani Manyoni kati ya mwaka 2019 na mwaka huu.

 
Kati ya mashtaka hayo moja ni la kusababisha taharuki kwa jamii na 14 ya kupotosha jamii.

Amesomewa mashtaka hayo leo Jumatano Machi 25, 2020 na mawakili wa Serikali, Monica Mbogo, Rose Cholongola, Michael Ng’hoboko na Caren Malando mbele ya hakimu mfawidhi wa mahakama hiyo, Consolata Singano.

Lema  anadaiwa kutenda  makosa hayo  Februari 29, 2020 mjini Manyoni mkoani Singida katika mazishi ya kiongozi wa Chadema.

Anadaiwa siku hiyo na katika mitandao ya kijamii alisambaza taarifa za uongo kwa nia ya kupotosha jamii kuwa watu 14 wameuawa kwa kupigwa mkoani Singida.

Lema alikana mashtaka yote yanayomkabili na shauri hilo kuahirishwa hadi Aprili 15, 2020 huku mbunge huyo akiachiwa kwa dhamana.


Share:

Mwanamfalme Charles apata maambukizi ya Virusi vya Corona

Mtoto wa Malkia Elizabeth, Mwanamfalme Charles (71) amepata maambukizi ya COVID19, Mke wake aitwaye Camilla (72) ‘Duchess of Cornwall’ amepimwa na kuthibitika hana maambukizi.

Kwa mujibu wa taarifa, Mwanamfalme alionesha baadhi ya dalili za Virusi hivyo Jumapili. Vipimo vilichukuliwa siku inayofuata na leo vimethibitisha kuwa ana maambukizi ya CoronaVirus.

Haijafahamika ni wapi Mwanamfalme Charles amepata maambukizi hayo lakini amekuwa akikutana na watu mbalimbali katika wiki zilizopita, kama sehemu ya majukumu yake.

Taarifa iliyotolewa imesema anaendelea vizuri na yupo karantini nyumbani huko Scotland huku akiendelea na kazi zake.

Alikutana na Malkia Elizabeth kwa mara ya mwisho Machi 12 na imeelezwa kuwa afya ya Malkia huyo ni nzuri.


Share:

FULL POWER , ZATI 50 SULUHISHO LA KUDUMU NGUVU ZA KIUME NA UUME MDOGO



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume


⇒Ngiri,

⇒Henia

⇒Kisukari

⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri
⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu
⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi
⇒Msongo wa mawazo 

⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.

FULL POWER

⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.

⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa
⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.

Zati 50

⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4

⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

Tanzania Yapokea Msaada Wa Vifaa Tiba Vya Corona Toka Kwa Mfanyabiashara wa China Jack Ma

Vifaa tiba vilivyotolewa na mfanyabiashara kutoka China, JackMa kwa ajili ya kupambana na virusi vya Corona nchini Tanzania vimewasili usiku wa kuamkia leo Machi 25, 2020, na ndege ya shirika la Ethiopia.

Katika taarifa yake aliyoiandika kupitia ukurasa wake wa  Twitter Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, amemshukuru mfanyabiashara huyo pamoja na Serikali ya China kwa ujumla.

"Jana usiku sisi Tanzania tulipokea mchango wa vifaa tiba, ambavyo vitasaidia katika mapambano yetu dhidi ya COVID-19, shukrani zetu za dhati kwa mfanyabiashara JackMa na taasisi yake ya AlibabaGroup na Serikali ya Ethiopia" Ameandika Waziri Ummy.

Vifaa hivyo ni barakoa 100,000, vipimo 20,000, na mavazi ya kujilinda (protective suits) 1,000.


Share:

Video Mpya : KISIMA 'NYANDA MAJABALA' - MBATE

Hii hapa ngoma mpya ya Msanii Kisima 'Nyanda Majabala' inaitwa Mbate
Share:

MAHAKAMA YAJIPANGA KUKABILIANA NA CORONA.....KESI AMBAZO UPELELEZI HAUJAKAMILIKA HAZITAPOKELEWA


Mahakimu wa Mahakama ya Hakimu Mkazi na Wilaya nchini, wameagizwa kuzingatia maelekezo ya tangazo la serikali namba 296 la mwaka 2002 linaloeleza kesi zote zilizokamilika upelelezi zipokelewe mahakamani na kuanza kusikilizwa mara moja.

Kadhalika, kesi ambazo upelelezi wake haujakamilika wasizipokee wazingatie tangazo hilo kufuatia agizo la serikali kuzuia mkusanyiko kupunguza maambukizi ya ugonjwa wa corona.

Rai hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Jaji Kiongozi wa Mahakama ya Tanzania, Dk. Eliezer Feleshi, katika mkutano wake na waandishi wa habari, kuhusu mhimili huo unavyounga mkono juhudi za serikali.

"Imefika wakati sasa mahakimu wafawidhi wa Mahakama za Hakimu Mkazi na Wilaya wafanye kazi kwa kuzingatia tangazo hilo na kama kesi upelelezi haujakamilika, basi ziishie hukohuko na si kupelekwa mahakamani kufuatia agizo la serikali kutoka kwa Rais Dk. John Magufuli, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na Waziri wa Afya, Jinsia na Watoto, Ummy Mwalimu," alisema Jaji Kiongozi.

Alisema mahakama imeongeza kasi ya matumizi ya mifumo hiyo kwa kanda ya Dar es Salaam kwa kesi zote za jinai zinazoahirishwa kutokana na sababu mbalimbali, watuhumiwa waliopo katika Gereza la Keko na Segerea watasikiliza, yataendelea kuahirishwa kwa njia ya Mahakama Mtandao (Video Conference) ili kuepuka msongamano na mkusanyiko wa mahabusu na wafungwa mahakamani.

Pia, alisema Kanda ya Mbeya na Bukoba zina vifaa vya mahakama mtandao, utaratibu unakamilishwa kwa uwekaji wa vifaa hivyo katika Magereza yaliyopo katika kanda hizo ili huduma hiyo ianze mara moja.

"Juhudi za kuweka vifaa hivyo kwa kanda zingine zilizosalia zinaendelea na baada ya muda mfupi huduma kama hizo zitatolewa, utumiaji wa mfumo wa usajili wa kesi kwa njia ‘E-Filing’ (kielektroniki). Mahakama inaimarisha na kuwasisitiza wadau wote (wananchi, mawakili wa serikali na mawakili wa kujitegemea) kusajili kesi kwa njia hii ya mitandao ili kupunguza msongamano na mchanganyiko wa watu katika maeneo ya mahakama," alisema Jaji Kiongozi, Dk. Feleshi.

Alisema muhimili huo utaongeza wigo wa matumizi ya Tehama kwa njia ya barua pepe na simu za mkononi kwa kutumia mfumo wa 'SMS notification' na 'USSD' katika usambazaji na upatikanaji wa taarifa za mashauri ambao hautawalazimu wadaiwa kufika mahakamani kupata taarifa hizo.

Mahakama itakuwa ikiendesha programu ya elimu ya namna ya kusajili mashauri, kupata taarifa pamoja na kutoa msaada wa usajili wa kesi kwa njia ya kielektroniki kwa kuanza na mahakama zenye kesi nyingi ambazo zinaweza kusababisha mkusanyiko wa watu wengi.

Naye Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Dar es Salaam, Lameck Mlacha, alisema wanatumia Mahakama Mtandao kwa lengo la kupunguza maambukizi ya corona.

Vile vile, ameshawaagiza mahakimu kupunguza idadi ya watu wakati wa usikilizwaji kesi katika vyumba vya mahakama na badala yake zitumike kumbi za wazi.



Share:

Mbowe Athibitisha Mwanae Kupata Virusi Vya Corona

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amethibitisha mtoto wake Dudley amepata maambukizi ya Corona

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mbowe,  Jumanne Machi 24, Dudley amethibitika kuwa na virusi vya corona baada ya kupata homa za vipindi, kuumwa kichwa mfululizo na kukohoa kwa siku tano.

“Mama yake ambaye ni daktari alibaini hali hiyo na alizitaarifu mamlaka za Serikali zinazoshughulikia janga hili nazo zilimtaka kijana apelekwe Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam kwenye vipimo zaidi ambapo ilithibitika rasmi kuwa ana virusi vya corona.

“Aidha, timu ya Serikali imeendelea kutoa ushirikiano na ufuatiliaji wa karibu kwa familia yote ikiwamo ushauri nasaha kwa wanafamilia na marafiki wengine waliokutana na Dudley katika mikusanyiko mbalimbali ikiwamo kuweka wengine karantini,” amesema Mbowe.

Aidha, amesema familia yake inakiri kupokea ushirikiano wa kiwango kilichowezekana kutoka kwa mamlaka husika za Serikali wakiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, Katibu Mkuu wake, Mganga Mkuu wa Serikali na wataalam wao wote.

‘Hali ya Dudley sasa imeimarika. Homa zimekwisha. Kichwa kimepona. Bado anakohoa kiasi na yuko chini ya uangalizi maalum.

‘Dudley hajasafiri nje ya nchi mwaka huu. Maambukizi haya kayapata ndani ya Mkoa wa Dar es Salaam. Ugonjwa huu haupaswi kuwa siri japo kuna miiko inayoongoza utoaji wa taarifa za wagonjwa. Tatizo ni kubwa kuliko tulivyojiandaa na tunavyojiandaa.

‘Wengi wameitafuta familia kutaka kujua ukweli na undani wa jambo hili. Pengine kupitia ushuhuda wangu, tutaweza kuokoa wengi katika nchi yetu. Hakika leo kila mmoja anastahili kujua janga hili liko mlangoni mwake,” alieleza Mbowe kwenye taarifa yake.

Pamoja na mambo mengine, ametoa rai kwa Rais John Magufuli, kuunda timu ya kumsaidia na ashirikishe wadau wengine nje ya Serikali  kwani yako mengi ya kufanya nje ya mikakati ya kitabibu inayosimamiwa na Waziri Mkuu na Waziri Ummy Mwalimu.

“Tusiiachie serikali pekee. Tutajuta. Tusiilaumu tu, tuishauri nayo iwe tayari kuupokea ushauri na ishirikishe. Ni janga la dunia na hakika tutaumizwa kuliko tunavyowaza.

“Katika maisha maandalizi hayajawahi kuwa hasara, bali hasara iliyo majuto ni kutokujiandaa na kupuuza yanayofanywa na walioyapitia kama ilivyo nchi za wenzetu zilizoendelea na hata majirani zetu" Alisema


Share:

Ahukumiwa Kunyongwa Hadi Kufa Baada ya Kumbaka na Kisha Kumnyonga Binti wa Miaka 7

Mtuhumiwa  anayedaiwa kubaka mtoto wa umri wa miaka 7, kisha kumnyonga shingo hadi kumuua amehukumiwa na Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Musoma kunyongwa hadi kufa.

Aliyehukumiwa kifo, ni Matiko Chanduru (20) mkazi wa Kijiji cha Maburi wilayani Serengeti mkoani Mara,aliyekuwa anakabiliwa na kesi ya mauaji ya kukusudia namba 27/2019 ambayo iliharishwa kutolewa hukumu kutokana na utata wa umri ambao sasa umethibitishwa na daktari kwamba ni mtu mzima.

Kabla ya kutolewa hukumu hiyo, Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Musoma, John Kayohoza alimkumbusha mshtakiwa shtaka lililokuwa linamkabili la kubaka kwamba alitenda kosa hilo Juni 30, 2018 nyakati za jioni Kijiji cha Maburi eneo la Mlima Ujerumani,akilinda shamba kuzuia wanyama waharibifu kwa kumbaka Munira Frahimu(7).

Binti huyo,ambaye anamuita mshtakiwa mjomba, alimbaka na kumsababishia maumi vu makali sehemu za siri baada ya kufanyiwa ukatili huo,alijikokota kwenda kwa bibi yake anapoishi na kumweleza mjomba mkubwa Asante Chanduru kuhusu kitendo alichofanyiwa.

Mjomba wake, aliamua kwenda kumhoji akiwa na binti huyo, lakini mtuhumiwa alikataa

Baada ya muda inadaiwa mtoto  aliondoka kurejea nyumbani ,akiwa njiani kurudi kwa bibi yake, mshtakiwa alimfuatilia kwa nyuma na kumkamata kwa nguvu,kisha kumvutia vichakani na kumnyonga shingo na kumvua nguo zote na kubakisha nguo ya ndani ambayo aliiteremsha hadi kwenye ma goti na kutupa mwili porini.

Ilielezwa Julai mosi,2018, mtuhumiwa baada ya kubanwa na uongozi wa kijiji pamoja na ndugu, alikiri kutenda kitendo hicho na kuwapeleka hadi alipotelekeza mwili  wa mpwa wake, kisha kufikishwa mahakamani.

Mahakama baada ya kumkumbusha mshtakiwa kosa na kuthibitisha, alihukumiwa kunyongwa hadi kufa na si vinginevyo na kusema mtuhumiwa anaweza kukata rufaa ndani ya siku 30 kama hakuridhika na hukumu hiyo.

Credit: Mtanzania


Share:

Wizara Ya Afya Yatangaza Nafasi 1000 za Madaktari

Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imetangaza nafasi mpya elfu moja za ajira kwa kada ya madaktari daraja la pili.

Tangazo hilo la nafasi za ajira limetolewa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo Dkt Zainab Chaula, ambapo kati ya nafasi hizo madaktari 610 watakwenda kufanya kazi katika hospitali za wilaya zilizo chini ya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI).

Madaktari 306 ni kwa ajili ya hospitali za mikoa na zile za Rufaa, arobaini watapelekwa katika hospitali ya Taifa ya Muhimbili jijini Dar es salaam na wengine Ishirini katika hospitali ya Benjamin Mkapa iliyopo jijini Dodoma.

Katika mgawanyo wa nafasi hizo mpya za madaktari, Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (MOI) itapata madaktari kumi, Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete madaktari saba na Taasisi ya Saratani ya Ocean Road nayo pia madaktari saba.

Februari Ishirini mwaka huu wakati akihutubia kwenye maadhimisho ya siku ya madaktari kitaifa kwa mwaka huu, Rais John Magufuli aliahidi kutangaza nafasi za ajira mpya elfu moja za madaktari, madaktari ambao baada ya kuajiriwa watapangiwa kufanya kazi kwenye maeneo yenye upungufu.

==>>Kwa Nafasi Mbalimbali za Kazi  <<bofya hapa>> 


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger