Monday, 27 January 2020

Nyota wa zamani wa LA Lakers Kobe Bryant amefariki dunia katika ajali

Nyota wa mpira wa vipaku nchini Marekani Kobe Bryant amefariki dunia pamoja na wenzake wanne kwenye ajali ya helikopta iliyotokea California usiku wa leo tarehe 26 Januari 2020.

Taarifa kutoka Marekani zimeeleza kuwa Kobe Bryant alikuwa akisafiri kwa helikopta binafsi kabla haijalipuka na kuteketea kwa moto huko Calabasas.

Kwa mujibu wa Mamlaka jijini Los Angeles wameeleza kuwa jumla ya watu watano walikuwa kwenye helikopta hiyo na hakuna aliyenusurika katika ajali hiyo.

Kobe Bryant amefariki akiwa na umri wa miaka 41 akiwa na ameichezea timu ya mpira wa kikapu ya Los Angeles Lakers nchini Marekani kwa takribani miaka 20, hadi alipostaafu mwezi Aprili mwaka 2016


Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama ni  miongoni mwa watu wa awali mashuhuri waliotuma salamu za rambirambi kufuatia kifo  hicho.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu January 27

















Share:

Sunday, 26 January 2020

YANGA SC YAIPIGA TANZANIA PRISONS 2-0 NA KUTINGA 16 BORA AZAM SPORTS FEDERATION CUP


Na Asha Said, DAR ES SALAAM
TIMU ya Yanga SC imeungana na vigogo wenzao, Simba SC kutinga hatua ya 16 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Tanzania Prisons jioni ya leo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Kwa ushindi huo, Yanga SC watamenyana na Gwambina FC ya Daraja la Kwanza ambayo jana iliitoa Ruvu Shooting kwa penalti 7-6 baada ya sare ya 1-1 Uwanja wa Gwambina, Misungwi.

Katika mchezo wa leo Yanga SC inayofundishwa na kocha Mbelgiji, Luc Eymael kwa ushirikiano na gwiji wa klabu, mzawa Charles Boniface Mkwasa ‘Master’ wakisaidiwa na Riedoh Berdien kutoka Afrika Kusini ambaye ni kocha wa mazoezi ya utimamu wa mwili na Manyika Peter, kocha wa makipa ilipata bao moja kila kipindi.

Alianza kiungo mpya Mghana, Bernard Morrison kufunga bao la kwanza dakika ya tisa kwa penalti baada ya beki Michael Ismail wa Tanzania Prisons kuunawa mpira kwenye boksi katika harakati za kuokoa krosi ya Balama Mapinduzi.

Akafuatia mchezaji mwingine mpya, mshambuliaji Yikpe Gislain Gnamien kutoka Ivory Coast aliyefunga bao la pili kwa kichwa dakika ya 64 kwa kichwa akimalizika pasi ya kiufundi ya Bernard Morrison. 

Mechi nyingine za leo, Lipuli FC imekuwa timu nyingine ya Ligi Kuu kutolewa baada ya Mtibwa Sugar na Ruvu Shooting kufuatia kufungwa kwa penalti 5-4 baada ya sare ya 2-2 na Kitayosa Uwanja wa Samora mjini Iringa.

Nayo Namungo FC imeifunga Biashara United 2-1, Kagera Sugar imeifunga Mighty Elephant 2-0 Stand United imesonga mbele kwa ushindi wa penalti 5-4 baada ya sare ya 1-1 na Maji Maji FC Uwanja wa Maji Maji mjini Songea.

Kitayosa, Namungo FC, Kagera Sugar, Stand United na Yanga SC zinaungana na Alliance FC, Ndanda SC, Ihefu FC, JKT Tanzania, Simba SC, Gwambina FC na Sahare All Stars, KMC, Panama na Mbeya City kuingia raundi ya tano ya michuano hiyo ambayo bingwa wake hucheza michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika.

Hatua ya 32 Bora itahitimishwa kesho kwa mabingwa watetezi, Azam FC kumenyana na Friends Rangers Dar es Salaam.

Kikosi cha Yanga SC kilikuwa; Metacha Mnata, Juma Abdul, Jaffar Mohamed, Lamine Moro, Said Juma ‘Makapu’, Abdulaziz Makame, Deus Kaseke/Patrick Sibomana dk82, Haruna Niyonzima, David Molinga/Yikpe Gislain dk57, Mapinduzi Balama na Bernard Morrison/ Feisal Salum dk98.

Tanzania Prisons: Jeremiah Kisubi, Michael Ismail, Benjamin Asukile, Vedastus Mwihambi, Nurdin Chona, Adilly Buha, Salum Kimenya/Samson Mbangula d68, Ezekia Mwashilindi, Jeremiah Juma/ Hamid Mohammed dk89, Paul Peter na Aziz Ismail/Cleophace Mkandala dk80.

Chanzo - Binzubeiry  blog
Share:

WAZIRI KAIRUKI APONGEZA JUHUDI ZA BRELA



Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Mhe. Angellah Kairuki akisikiliza kwa makini jambo katika Warsha ya kwanza ya Wanawake wa Kiislamu katika ujasiriamali na Tanzania ya viwanda iliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.
 Msaidizi wa Usajili Mkuu kutoka BRELA, Bw. George Chuwa akiwasilisha mada kuhusu nafasi ya BRELA kufanikisha Tanzania ya Viwanda katika Warsha ya kwanza ya Wanawake wa Kiislamu katika ujasiriamali na Tanzania ya viwanda iliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam

***
Waziri wa Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Mhe. Angellah Kairuki amepongeza juhudi zinazofanywa na Wakala ya Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) katika kuhamasisha urasimishaji wa Biashara.

Hayo yamebainiswa leo alipohudhuria kama Mgeni rasmi kwa niaba ya Makamu wa Rais Mama Samia Suluhu Hassan katika Warsha ya kwanza ya Wanawake wa Kiislamu katika ujasiriamali na Tanzania ya viwanda iliyofanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika Warsha hiyo Mhe. Kairuki amesema ni muhimu sana kwa Wajasiriamali kurasimisha Biashara kwa kuwa itafungua fursa nyingi sana.

“Kurasimisha Biashara ni muhimu sana, na ninafurahi sana kuwaona BRELA hapa, kwa sababu, urasimishaji wa biashara unakuja na fursa mbalimbali ambazo zinazaidia ukuaji na kuongeza kipato”.Alisema Mhe. Kairuki.

Naye Msaidizi wa Usajili Mkuu kutoka BRELA, Bw. George Chuwa ametoa wito kwa wanawake wote wajasiriamali kusajili majina ya Biashara zao, Alama za Biashara au huduma, Usajili wa Kampuni na pia huduma zingine za BRELA.

“Natoa rai kwa wanawake wajasiriamali wote kutumia huduma za BRELA ambazo zote zinapatikana kwa njia ya mtandao. 

Huduma hizo ni pamoj na Usajili waa Majina ya Biashara, Usajili wa Alama za Biashara au Huduma, Usajili wa Kampuni, Kutoa Hataza, Kutoa Leseni za Biashara Kundi A pamoja na kutoa Leseni za Viwanda”.


Aidha Bw. Chuwa ameeleza kuwa ili kuweza kufungua huduma katika mfumo wa ORS hitaji la kwanza ni kuwa na namba ya utambulisho wa Taifa kisha kutembelea www.brela.go.tz ili kupata huduma zote. 
Share:

Waziri Mkuu: Wafanyabiashara Wa Madini Wanaofuata Sheria Walindwe

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameviagiza vyombo vya Ulinzi na Usalama vihakikishe vinawalinda wafanyabiashara wa madini wanaofanya kazi zao kwa kufuata sheria na kujiepuka kamata kamata zisizo na tija.

“Katika kipindi cha hivi karibuni kumejitokeza malalamiko mengi kutoka kwa wawekezaji na wadau wa madini kuhusu kukamatwa au kubughudhiwa bila sababu za msingi. Kutokana na hali hiyo, natumia nafasi hii kukemea suala la ukamataji holela wa wawekezaji au wadau wa madini pasipo kufuata taratibu.”

Ametoa agizo hilo leo (Jamapili, Januari 26, 2020) wakati akifunga semina ya ushiriki wa vyombo vya Ulinzi na Usalama katika usimamizi na udhibiti wa rasilimali madini katika ukumbi wa Mtakatifu Gaspar jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amesema kwamba vyombo vya Ulinzi na Usalama vinatakiwa vitumie Sheria, Kanuni na Miongozo mbalimbali iliyowekwa mahsusi kwa ajili ya kuimarisha usimamizi wa sekta ya madini.

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuviagiza vyombo vya Dola kusimamia na kudhibiti utoroshwaji wa madini na kuhakikisha kuwa masoko yote ya madini  nchini yanalindwa.

“Nyote mtakubaliana nami kwamba kila taasisi ina utaalamu na wataalamu wake. Kwa hivyo, hatunabudi kufanya kazi kwa kuheshimu na kutambua utaalamu ama taaluma za wengine tunaoshirikiana nao.”

“Sasa ni vema tukaondoa tofauti zetu na kuwa kitu kimoja kwa lengo la kuimarisha udhibiti na usimamizi wa rasilimali madini. Aidha, tutambue kuwa kuna nyakati hatuhitaji kutumia nguvu nyingi bali ushauri tuu ili kutatua changamoto husika.” 

 Waziri Mkuu ameelekeza kwamba kuanzia sasa  wadau wote wanaopatikana na madini wapewe utaratibu wa kuelekea sokoni kuuza madini hayo badala ya kuwakamata wakiwa wanaenda sokoni.

Waziri Mkuu amesema Wizara ya Madini kupitia Tume ya Madini ina ofisi mikoa yote ya Tanzania Bara, hivyo hakuna sehemu ambayo wanaweza kusema walikosa msaada wa kitaalamu. “Ni wajibu wetu sote kama watumishi wa umma kujenga mazingira rafiki ya kazi, kuaminiana na kufanya kazi kwa ushirikiano.”

Wakati huo huo,Waziri Mkuu amesema kuazia sasa suala la migodi kutegemea bidhaa mbalimbali kutoka nje ya nchi lifikie ukomo kwa kuhakikisha kuwa, kila huduma inayohitajika migodini, inapatikana nchini.

Waziri Mkuu amesema nchi inawajibu wa kutoa huduma zinazokidhi mahitaji ya wadau wa madini kwa maana ya kutoa huduma kwa ubora stahiki na kwa wakati muafaka.

Amesema sekta ya madini inazalisha ajira ila kuna changamoto ya ubora wa ajira, mishahara na stahiki katika kazi zinazofanana na suala la unyanyasaji wa wafanyakazi.

Waziri Mkuu amesema masuala mengi hapo yanaweza kuonekana haraka kwenye maeneo yao ya kazi, hivyo ni vyema wakawa na taarifa hizo kwa wakati na kuwasilisha kwa wahusika ili mambo yawekwe sawa na kuipeleka sekta mbele. 

Akizungumzia kuhusu suala la unyanyasaji wa wafanyakazi wazalendo amesema si suala la kufumbiwa macho kama ilivyo suala la usalama wa watenda kazi katika migodi. 

Kadhalika, suala la udhibiti wa wageni kufanya kazi ambazo zinaweza kufanywa na Watanzania wenzetu pia ni jukumu letu na hivyo ni wajibu wetu kusimamia mikataba tuliyoingia na wawekezaji hususani eneo  la urithishaji wa madaraka na ujuzi kwa wazawa.

Kwa upande wa Wizara ya Madini na Tume ya Madini, Waziri Mkuu amewaagiza watafute suluhu ya changamoto ya usalama wa wafanyakazi kipindi wakiwa kazini na baada ya kumaliza muda wa kazi kwa hiari au kwa kustaafu au kumaliza mkataba. “Tumepokea malalamiko mengi sana katika eneo hilo.”

“Hivyo, ni wajibu wetu kushirikisha wadau wote wanaohusika na masuala ya ajira, bima za wafanyakazi, afya za wafanyakazi na usimamizi wa stahiki za wafanyakazi kukaa kwa pamoja na kutatua changamoto hii ili isiendelee kukomaa.”

Vilevile, Waziri Mkuu ameagiza suala la utunzaji wa mazingira liwekewe mkazo wa kipekee maana nje ya mazuri yote yaletwayo na Sekta ya Madini, uharibifu wa mazingira unaweza kugharimu maisha ya binadamu, wanyama na mimea.

Waziri Mkuu amesema “mazingira yetu ndio uhai wetu sisi na vizazi vijavyo, hivyo ni wajibu wetu kama Wizara kuhakikisha wawekezaji wetu ni watu wema kwa mazingira yetu.”

Pia, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kumpongeza na kumshukuru Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa uthubutu mkubwa alioufanya ambao umeleta mageuzi makubwa katika Sekta ya madini.

“Hili linadhihirishwa na kitendo cha utiaji saini makubaliano ya uanzishwaji wa Kampuni ya Twiga Minerals uliofanywa juzi Jijini Dar es Salaam tarehe 24 Januari 2020 ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Sheria Mpya ya Madini ya mwaka 2017.”

Awali, Waziri wa Madini Doto Biteko alisema lengo la semina hiyo ni kujenga uelewa wa pamoja kwenye masuala ya usimamizi wa sekta ya madini nchini.

Alisema suala la kudhibiti utoroshwaji wa madini linafanyika kwa kushirikiana kati Wizara ya Madini na vyombo vya Ulinzi na Usalama na kwamba wanaendelea kushirikiana katika kutatua changamoto zinazojitokeza.

Waziri Biteko ametumia fursa hiyo kutuma salamu kwa wafanyabiashara wanaojihusisha na utengenezaji na uuzaji wa madini bandia pamoja na wanaotaka kuuza madini nje ya mfumo kuwa zama zao zimekwisha.


Share:

Rais Xi asema virusi vya corona ni changamoto kubwa....56 Wafariki Dunia

Rais wa China Xi Jinping amesema nchi yake inakabiliwa na "hali mbaya," wakati ambapo virusi vya corona vinaendelea kuenea huku watu wapatao 1,975 wakiliripotiwa kuwa wameambukizwa.

China mnamo siku ya Jumapili ilizidisha vizuizi vya usafiri ili iweze kupambana na virusi vya corona ambavyo Rais Xi Jinping amesema ni tishio kubwa. Kwa mujibu wa shirika la habari la taifa, serikali ya China imesimamisha shughuli  za kuwatembeza watalii kutoka mataifa ya nje, pia hakutakuwepo na safari za mabasi yanayotoka na kwenda mikoani kuanzia Jumapili katika juhudi za kupunguza kuenea kwa ugonjwa unaosabbabishwa na virusi vya corona.

Mlipuko huo unaaminika kuwa ulianzia katika eneo la mashariki mwa China katika mji wa Wuhan na umesambaa hadi katika nchi zingine kadhaa kama Marekani, Ufaransa, Japan na Australia.

Watu wapatao 1,975 wanaaminika kuwa wameambukizwa, na takriban vifo 56 vimeripotiwa. Taarifa ya serikali  imesema watu 324 wamo katika hali mbaya. Wakati huo huo serikali ya China imechukua hatua ya kuweka marufuku ya kuingia au kutoka kwenye mkoa wa Hubei ulio katikati mwa nchi hiyo ambao pia umeathiriwa vibaya, hii ikiwa ni katika juhudi za kudhibiti maambukizi zaidi.
 
Kiongozi wa Hong Kong, Carrie Lam, ametangaza hali ya dharura kuhusu virusi vya corona katika jiji hilo na serikali yake imetangaza kufungwa shughuli za usafiri, shule na vyuo vikuu. Visa vitano vya maambukizi ya virusi vya corona vimeripotiwa katika jiji la  Hong Kong na watu zaidi ya 122 wanadhaniwa kuwa na virusi hivyo.

-DW


Share:

Serikali Yaandaa Mkakati Wa Miaka Mitano Wa Kukuza Zao La Pamba

Serikali imesema imetengeneza mkakati wa miaka mitano kuhusu sekta ndogo ya pamba ili kukidhi mahitaji ya soko na upatikanaji wa pembejeo kwa wakulima nchini.

Kauli hiyo Imetolewa na Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe Hussein Bashe wakati akifungua mkutano wa kamati ndogo ya wadau wa kilimo iliyokutana jijini Dodoma.

Mkutano huo ulihudhuriwa na Wakuu wa mikoa inayolima zao la pamba nchini ambao wamepokea na kujadili taarifa ya kamati ndogo iliyoundwa kuchunguza changamoto zinazoikabili tasnia na kutoa mapendekezo ya utatuzi wake.

Kamati ndogo ya wadau iliundwa Octoba mwaka jana jijini Mwanza kwa lengo la kuja na mapendekezo ya utatuzi wa changamoto za zao hilo nchini.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo Mh Bashe amesema kikao hicho ni uhimu ili kutengeneza mustakabali mzuri wa tasnia ya pamba kwenye mikoa 17 inayolima zao hilo.

Bashe amesema msimu ujao wa kilimo cha pamba unapaswa uwe mzuri na usiwe na matatizo licha ya mikoa michache bado ina takribani asilimia 20 ya pamba isiyonunuliwa hadi sasa.


Share:

Profesa Lipumba Akamatwa na Jeshi la Polisi

Jeshi la Polisi wilayani Handeni mkoani Tanga, limemkamata Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi CUF, Profesa Ibrahimu Lipumba, kwa madai ya kufanya ziara bila kuwa na kibali. 

Profesa Lipumba amekamatwa leo Jumapili Januari 26, 2020 Kijiji cha Segera wilayani Handeni na kupelekwa kituo kikuu cha polisi wilayani humo kilichopo mjini Handeni.

Mkurugenzi wa Usalama wa CUF, Masoud Mhina amesema mwenyekiti huyo amekamatwa wakati akijiandaa kufungua tawi la chama hicho Kijiji cha Segera.

Amesema ameshangazwa na kitendo hicho cha polisi kumkamata Profesa Lipumba wakati tayari chama kilishawasilisha jeshi la polisi taarifa ya ziara hiyo.


Taarifa zaidi zitafuata, juhudi za kumtafuta RPC Tanga zinaendelea.


Share:

RAS Tabora Awataka Maofisa Tarafa Kuhakikisha Kero Za Wananchi Zinatatuliwa Katika Maeneo Wanayosihi

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imewataka Maofisa Tarafa kutatua kero na migogoro inayowakabili wananchi katika maeneo yao badala ya kuwaacha bila usaidizi na kuwafanya kukimbilia kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ili kutafuta haki zao.

Kauli hiyo imetolewa  na Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu alipokuwa na Kikao kazi cha siku moja na Maofisa Tarafa wa Tarafa zote za wilaya zote za Mkoa huo.

Alisema ni jukumu la Maofisa hao kuhakikisha wanashughulikia migogoro ya ardhi, kuondoa madai ya wananchi kuombwa rushwa, mauaji na matumizi mabaya ya madaraka inayofanywa na Watendaji walioko chini yao ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma nzuri na wanayotarajia.

Katibu Tawala huyo wa Mkoa wa Tabora alisema ni vema wakasimama vema katika nafasi zao za uongozi ili kuwaondolea adha ya kusafiri umbali mrefu kutoka wanapoishi hadi Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kutafuta haki zao.

“Sifurahishwi kuona wananchi wengine ni wazee sana wameshindwa kusaidia kule wanapoishi na kuamua kuja katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ili kumuona Mkuu wa Mkoa au mimi ili niwasikilize kero zao ambazo kimsingi zilitakiwa kutatuliwa na viongozi walio karibu nao ambao wengine wao ni ninyi Maofisa Tarafa ” alisema.

Makungu alisema kuwa Maofisa Tarafa ndio kiungo kati ya Serikali Kuu na Serikali za Mitaa ni vema wakahakikisha kuwa shughuli zote zinazofanyika katika maeneo yao ya utawala yanazingatia Sheria za Nchi na zinatolewa kwa haki kwa wananchi wote.

Aidha Katibu Tawala huyo wa Mkoa wa Tabora amewataka Maofisa Tarafa kuhakikisha mapato ya Serikali yanakusanywa na kudhibiti Wafanyabiashara wanaokwepa kodi za Serikali.

Alisema kuna baadhi ya wafanyabiashara bado wanaendesha shughuli bila kulipa kodi zinazotakiwa kwa mujibu wa Sheria.

Mwisho


Share:

Waziri Ummy:maambukizi Mapya Ya Ukoma Yapungua Kutoka Watu 43 Hadi Watu 26

Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma
Katika kuelekea Maadhimisho ya siku ya Ukoma Duniani leo,Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto ,Mhe.Ummy Mwalimu amesema kiwango cha maambukizi mapya ya ugonjwa wa ukoma umepungua kutoka watu 43 kati ya watu milioni  Moja  2014 hadi watu kufikia wagonjwa 26 kati ya watu milioni Moja mwaka 2019.

Amezungumza hayo jana jijini Dodoma alipokuwa akizungumza na wazee ambao ni waathirika wa ugonjwa wa ukoma katika kijiji cha Samaria Kata ya Hombolo bwawani.

Amesema kupungua kwa maambukizi hayo ni kutokana  na juhudi zaa serikali za kuhakikisha  wanapima na kutoa matibabu bure kwa aathirika wa ugonjwa wa huo.

Pia Waziri Ummy amesema maambukizi mapya Ukoma kwa watoto takriban asilimia 41 % ambapo mwaka 2014 kulikuwa na watoto 90  na wamepungua hadi watoto  53 mwaka 2019.

Kwa upande wake mkurugenzi wa progamu  wa elimu vijini (CHEP) Ruteni Kanal  Msaafu Daudi Tandila  amesema  Kulingana na Takwimu hizo,na msimamo wa shirika la afya Duniani (WHO) yakuwa Kati ya wagonjwa elfu kumi akipatikana Mgonjwa Mmoja,italeta ripoti ya kuwa hakuna ugonjwa wa ukoma.

Hivyo Wizara ya afya ikusanye taarifa upya kupata Takwimu zinazotolewa na WHO za udhibitisho wa Kutokuwepo kwa ugonjwa huo.

Sambamba na hayo Waziri Ummy amekabidhi sukari kilo 50,Mchele kilo 100,maharage kilo 50,unga kilo 50 na viatu pea 48 kwa waathirika wa Ukoma  kama ishara ya kuwathamini huku  akishikana mikono nao  katika kupinga dhana potofu  ya kwamba ugonjwa huo unaambukiza   kwa njia ya kushikana.

Kuhusu changamoto ya miundombinu ya barabara iliyopo katika eneo hilo Waziri Ummy amemwagiza mkuu wa wilaya alifanyie kazi kwani imekuwa kero na changamoto kubwa ambapo ilisababisha msafara wake kukwama mara kwa mara hali iliyomsababisha kutembea kwa miguu.


Share:

Tanzania, India Zaahidi Kuendeleza Uhusiano Wa Kidiplomasia, Kukuza Maendeleo

Tanzania na India zimeahidi kuendeleza uhusiano wa kidiplomasia pamoja na  kushirikiana katika kuhakikisha kuwa na maendeleo endelevu baina ya nchi hizo mbili.   

Akihutubia sherehe za maadhimisho ya 71 ya Jamhuri ya India, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amesema kuwa Tanzania na India ni ndugu na nchi hizo zitaendelea kushikiana katika kuhakikisha kuwa maendeleo ya diplomasia ya uchumi baina ya nchi hizo yanakuwa kila wakati. 

"Nchi ya Tanzania na India zina uhusiano mzuri, imara na wa muda mrefu ulianzishwa na baba wa Taifa Mwl. Julias Nyerere pamoja na Mahatma Gandhi. Na uhusiano huu umekuwa ukisaidia kuimarisha maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa" alisema Dkt. Ndumbaro   

Dkt. Ndumbaro aliongeza kuwa "sisi Tanzania na India ni ndugu, kwa hiyo basi tunawatakia sana kila la kheri katika kuiletea India maendeleo…lakini pia tukumbuke kuwa maendeleo ya India ni maendeleo ya Tanzania pia,"   

Kwa sasa uchumi wa India na Tanzania umezidi kukuwa na kuendelea kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia baina ya mataifa hayo. India imekuwa msharika mzuri wa maendeleo nchini Tanzania katika sekta mbalimbali ikiwemo utalii, maji, afya, teknolojia na elimu. Msaada wa India katika sekta ya maji hadi sasa, imeweza kusaidia kusambaza maji safi na salama katika kwa jiji la Dar es Salaam pamoja na upanuzi na uboreshaji wa mitambo ya maji Zanzibar.  

Aidha, kwa upande wa sekta ya elimu, Tanzania na India zimeshasaini makubaliano ya kushirikiana kujenga kituo cha ufundi na pia msaada wa kuendeleza vyuo vikuu vya Zanzibar ambavyo vinatoa ujuzi unaolengwa kuwaendeleza wanawake walio na elimu ndogo au isiyo rasmi. 

Kwa upande wake, Balozi wa India chini Tanzania, Mhe. Balozi Shri Sanjiv Kohli ameishukuru Serikali ya Tanzania kwa umoja na mshikamano ambao imekuwa ikionesha kwa India na kusema kuwa umoja huo umekuwa ni chachu ya maendeleo kwa Tanzania na Taifa la India. 

"Napenda kuwafahamisha kuwa umoja na mshikamano wetu umekuwa chachu ya maendeleo baina ya mataifa haya mawili…..tukumbuke kuwa umoja ni nguvu na dhamira yetu ni kushirikiana na mataifa yote duniani. Na dhamira yetu ni kuishi kwa amani umoja na mshikamano ili kukuza uchumi wetu," Alisema Balozi Kohli 

Aidha, Balozi Kohli amebainisha kuwa Tanzania itaendelea kuwa ya kipekee kwa taifa la India kutokana na mshikamano ambao imekuwa ikionesha kwa nchi ya India kijamii, kisiasa na kiuchumi. 

"India inajivunia kuwa na uhusiano na mzuri na Tanzania ambao umewezesha mataifa haya kufanya biashara, uwekezaji, kujenga uwezo, ujenzi wa miundiombinu pamoja na maendeleo ya kiuchumi," ameongeza Balozi Kohli. 


Share:

Naibu Waziri Mabula Azitaka Halmashauri Kutenga Bajeti Za Mabaraza Ya Ardhi Ya Kata Na Vijiji

Na Munir Shemweta, WANMM ILEJE
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewataka wakurugenzi wa Halmashauri nchini kutenga bajeti kwa ajili ya Mabaraza ya Ardhi ya Kata na Vijiji sambamba na kufuatilia tozo zinazotozwa na Mabaraza hayo ili yafanye kazi kwa ufanisi.

Dkt Mabula alitoa agizo hilo mwishoni mwa wiki wilayani Ileje na Mbozi wakati akizungumza na viongozi pamoja na watendaji wa sekta ya ardhi akiwa katika ziara yake ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi na ujenzi wa miradi inayofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) mkoani Songwe.

Naibu Waziri Mabula alisema, Wakurugenzi wa Halmashauri nchini wamekuwa hawatengi bajeti kwa ajili ya Mabaraza ya Ardhi ya Kata na Vijiji jambo linalosababisha Wajumbe wake kujifanyia mambo wanavyotaka ikiwemo kuweka viwango tofauti vya tozo za kwenda uwandani.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, Mabaraza ya Ardhi ya Kata na Vijiji yanapaswa kusimamiwa na Wakurugenzi wa Halmashauri kwa kuyapatia kwa kuyatengea bajeti za kuendesha ofisi kama vile Shajala sambamba na kujua yanayofanyika ikiwemo tozo zake ili kuepuka uonevu unaoweza kujitokeza kwa wananchi wanaoshitakiana.

‘’Katika Mabarza ya Ardhi ya Kata na Vijiji watu wanalipa tozo kulingana na sura kama mtu kavaa tai basi anapigwa shilingi elfu hamsini jambo linalowaumiza wananchi’’ alisema Mabula

Alizitaka ofisi za Wakurugenzi wa halmashauri nchini kuyasimamia Mabaraza hayo na kutoa semina kwa wajumbe wake na kuyapangia viwango vya tozo na kusisitiza kuwa hayo yasipofanyika kuna hatari wajumbe wake kufanya maamuzi kwa matakwa ya wenye uwezo.

Amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri kubadilika katika kuyasimamia mabaraza ya ardhi ya kata na vijiji na kubainisha kuwa Mabaraza hayo yakifanya vizuri yatapunguza mlundikano wa kesi za ardhi zinazokwenda Mabaraza ya ardhi ya nyumba  ya Wilaya.

Awali Afisa Mipango Miji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ileje mkoa wa Songwe Dismas Ndinda alimueleza Naibu Waziri  Mabula kuwa halmashauri hiyo pamoja na kuwa Mabaraza ya  Ardhi ya Kata na Vijiji sabini na moja lakini haina Baraza la ardhi la wilaya jambo linalowafanya wananchi wanaoshindwa kupata suluhu kusafiri hadi Mbeya kupata huduma za Baraza la Ardhi la Wilaya.

Wakati huo huo, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alikagua maendeleo ya ujenzi wa Ofisi na nyumba ya Meneja ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) unaofanywa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika shamba la Miti la Iyondo Msimwa wilaya ya Ileje mkoa wa Songwe.

Akikagua maendeleo ya ujenzi huo, Dkt Mabula mbali na kuridhishwa na maendeleo ya mradi huo alisema mradi wa ujenzi wa ofisi na nyumba ya Meneja wa TFS utasaidia ufuatiliaji wa msitu huo kwa kuwa Meneja wake atakuwa akiishi karibu na msitu huo. Aidha, ameuelezea mradi huo kuwa umesaidia pia kutengeneza ajira ya muda kwa wakazi wa eneo hilo na kuwawezesha kupata kipato cha mahitaji madogomadogo.

Kwa upande wake, Kaimu Meneja wa NHC mkoa wa Mbeya Pauline Kamaghe alisema mradi huo unaojengwa na Shirika lake unatarajiwa kugharimu kiasi cha milioni 426.8 na kukamilika mwezi April mwaka huu wa 2020 na kubainisha kuwa kwa sasa mradi umefikia asilimia 38 ya ujenzi.


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili January 26
















Share:

Saturday, 25 January 2020

Country Representative at PSI

Job title: Country Representative (CR) Department: Anglophone Africa Market Based in Dar es Salaam, Tanzania Reports to the Deputy Director, Anglophone Africa Who we are We’re Population Services International (PSI), the world’s leading non-profit social marketing organization. We work to make it easier for people in the developing world to lead healthier lives and plan the families they… Read More »

The post Country Representative at PSI appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Admin Officer at Seedspace

Job Title: Admin Officer Location: Dar es Salaam, Tanzania Are you looking to join a fast-growing international and impact-driven startup, work in a flexible environment, and be surrounded by a young and diverse team? Who We Are Seedstars is a global organization with headquarters in Switzerland and a presence in 70+ emerging markets. We are on a mission… Read More »

The post Admin Officer at Seedspace appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Admission officerat SUMAIT University

Admission officer  The Abdulrahman Al-Sumait University (SUMAIT University) was built on the foundation of the former University College of Education Zanzibar (CEZ) established in 1998 by a Kuwait based charity organization, Direct Aid. As part of our expansion programme, SUMAIT University invites qualified Tanzanians and non Tanzanians to fill various academic and administrative vacant posts as follows: Job… Read More »

The post Admission officerat SUMAIT University appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

TBS YAENDESHA MAFUNZO KWA WAFANYABIASHARA KAHAMA...DC MACHA ATAKA TBS KUSIMAMIA UBORA WA CHAKULA NA VIPODOZI


Na Adela Madyane- Malunde 1 blog Kahama
Katika kuhakikisha kuwa Watanzania wanatumia bidhaa zenye viwango vya ubora unaotakiwa kwa matumizi ya binadamu, mkuu wa Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga, Anamringi Macha amelitaka Shirika la Viwango Tanzania kuhakikisha linasimamia ubora wa Bidhaa na si vinginevyo.

Macha alitoa agizo hilo juzi wakati akifungua Mafunzo ya siku moja kwa wafanyabiashara mbalimbali wa Wilaya ya Kahama wanaojihusisha na masuala ya ujasiliamali wa bidhaa mbalimbali yaliyoandaliwa na Shirika la Viwango Tanzania TBS yaliyofanyika mjini Kahama na kujumuisha washiriki 100 wakiwemo wauza chakula na wauzaji wa vipodozi.

Macha amesema kuwa hapa nchini Wafanyabiashara wengi wa Vipodozi wamehatarisha afya za Watanzania kwa kusambaza bidhaa ambazo hazina viwango vya Ubora unaotakiwa katika matumizi ya binadamu hali ambayo itaendelea kusababisha madhara iwapo hali hiyo haitadhibitiwa.

Macha amesema kuwa eneo hilo la vipodozi bado lina shida kubwa na kwamba linafanya ukatili wa wazi wazi kwa Watanzania kutokana na kuwauzia bidhaa ambazo hazijahakikiwa na Shirika la viwango Tanzania TBS na hivyo kusababisha madhara ya mara kwa mara kwa watumiaji.

Aidha amewataka TBS kuhakikisha kuwa wanafanya uchunguzi wa kina kwa wafanyabiashara wa vipodozi ambao bidhaa zao hazijahakikiwa na kuwa na kiwango cha ubora unaohitajika hali ambayo itaepusha madhara ya kuathhirika kwa ngozi kwa watumiaji.

Naye mfanyabiashara wa vipodozi Joseph Walioba amesema kuwa Wafanya biashara hawana elimu juu ya vipodozi licha ya hapo awali kutembelewa na maafisa kutoka TFDA na kuahidi kufanyia kazi mafunzo hayo waliyopatiwa na TBS.

“Binafsi nafanya biashara ya vipodozi vya asili na kuchakata asali na siagi vyote hivi pamoja na elimu yangu ndogo bidhaa yangu imehakikiwa na TBS kwakweli hapa nazidi kupata elimu kwakuwa nilisha anzisha biashara nyingine ya vipodozi,” amesema Ebson Muzibila.

Kwa upande wake Afisa Usalama wa Chakula mwandamizi Nuru Mwasulama amesema kwa sasa wanaendelea kutoa mafunzo katika sehemu mbalimbali ili kuwajengea uwezo wajasilamali wadogo ili wafanye biashara zisizoleta athali kwa wananchi.

Amesema kuwa lengo la mafunzo hayo ni kuwataka wajasiliamali wazalishe chakula salama ili kudumisha afya za walaji huku akizungumzia upande wa vipodozi aliwataka wafanyabiashara wa vipodozi kuzingatia kanuni za vipodozi na kuwasisitiza kuacha kuhifadhi bidhaa nje jambo ambalo linasababisha kuondoa uhalisia wake.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger