Wednesday, 22 January 2020

T-MARC TANZANIA YATOA MSAADA WA DIAPERS ZA SMILEY HOSPITALI YA MWANANYAMALA, DAR ES SALAAM

Mmoja wa wanawake waliojifungua katika hospitali ya Mwananyamala, Rebecca Nelson akifurahia Diapers mpya za Smiley baada ya kukabidhiwa na balozi wa bidhaa hizo za T-MARC Tanzania, Dinah Marrios (kushoto),wengine pichani ni watumishi waandamizi wa hospitali hiyo na kutoka taasisi yak T-MARC.

Mkurugenzi wa bidhaa za kijamii wa T-MARC Tanzania , Flavian Ngole, (kulia) akikabidhi msaada wa diapers mpya za Smiley zilizozinduliwa katika soko nchini karibuni na T-MARC, kwa mzazi, Rebecca Nelson, katika wodi ya wazazi ya hospitali ya Mwananyamala jijiji Dar es Salaam, wakati wa hafla ya taasisi hiyo kukabidhi msaada wa bidhaa hizo hospitalini hapo , (katikati) ni Balozi wa Smiley , Dinah Marrios, wengine (kutoka kushoto) ni Muuguzi Mkuu wa Hospitali hiyo , Dk.Mussa Wambura na Muuguzi Rosa Moses.
Wauguzi Waandamizi wa hospitali ya Mwananyamala wakipokea msaada wa Diapers za Smiley zlizozinduliwa hivi karibuni kutoka kwa Mkurugenzi wa bidhaa za kijamii wa T-MARC Tanzania, Flavian Ngole (kushoto) na balozi wa bidhaa hizo, Dinah Marrios.
Share:

WAZIRI MPINA AUNDA TIMU UCHUNGUZI UKWEPAJI WA KODI KAMPUNI YA UFUGAJI SAMAKI AINA KAMBAMITI



WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina (katikati) akiangalia namna vifaranga vya samaki aina ya Kambamiti vinavyozalishwa na Kampuni ya Aphakrust alipofanya ziara kukagua uzalishaji wa kampuni hiyo kisiwani Mafia. Kushoto ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Ganeshan Vedagiri na Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Sera na Mipango Wizara ya Mifugo na Uvuvi, James Mganga. Picha na Mpiga Picha Wetu.


WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akivua samaki aina Kambamiti alipotembelea mabwawa ya Kampuni ya Aphakrust kisiwani Mafia. Kwenda kulia ni Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, Ganeshan Vedagiri na Mkurugenzi Ukuzaji Viumbemaji, Dk. Nazael Madala na Mkurugenzi wa Uvuvi, Magese Bulayi. Picha na Mpiga Picha Wetu.
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Alphakrust, Ganeshan Vedagiri (katikati) alipotembelea mabwawa ya ufugaji kambamiti kisiwani Mafia mwingine Mkurugenzi Ukuzaji Viumbemaji, Dk. Nazael Madala. Picha na Mpiga Picha Wetu.



NA MWANDISHI WETU, MAFIA


WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ameunda timu ya wataalamu kufanya uhakiki wa takwimu, mauzo, uzalishaji na uendeshaji wa Kampuni ya Alphakrust inayojishughulisha na uzalishaji wa samaki aina ya Kambamiti pamoja na uhalali wa mapato ya Serikali kufuati kuwepo udanganyifu kwenye biashara hiyo.

Kulingana na takwimu za mauzo ya Kambamiti nje ya nchi kampuni hiyo ilipaswa kulipa shilingi milioni 300 kama ushuru wa huduma kwa Halmashauri hiyo lakini imekuwa ikilipa shilingi milioni 100 kwa mwaka na hivyo kuipunja Serikali kiasi cha shilingi milioni 200 kila mwaka.

Waziri Mpina amebaini njama hiyo inayofanywa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia kwa kushirikiana na Mwekezaji wa Kampuni ya Alphakrust inayofuga samaki aina ya Kambamiti kisiwani humo kwa lengo la kuiibia Serikali mapato yake yanayotakiwa kutozwa kama ushuru wa huduma yaani ‘Service Levy’

Alisema Halmashauri ya Mafia imetengeza makadirio ya kutoza ushuru wa huduma ya shilingi milioni 9 kwa mwezi kutoka Kampuni ya Apha Krust na kuacha Kanuni maalumu iliyowekwa kwa mujibu wa Sheria ya ukokotoaji wa mapato yanayopatikana ya kutakiwa kulipa asilimia 3 ya mapato yote yanayopatikana kwenye biashara husika.

Udanganyifu huo umebainika wakati wa ziara ya Waziri Mpina ya kukagua Kituo cha kutotoleshea vifaranga na Shamba la ufugaji samaki aina ya Kambamiti lilomilikiwa na Kampuni ya Alphakrust kisiwani Mafia.

Waziri Mpina katika ziara hiyo aliambatana na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Pwani, Ramadhani Maneno na Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Mafia ikiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Shaib Nnunduma, Wakurugenzi na Wataalamu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi.

Mpina alihoji iweje Halmashauri ya Mafia itoze ushuru kinyume cha Sheria wakati kanuni za ukokotoaji wa mapato zinajulikana na hivyo kuamini kuwa huo ni mkakati wa siri uliosukwa baina ya Halmashauri ya Mafia na Kampuni ya Apha Krust kwa lengo la kukwepa kulipa mapato stahiki ya Serikali.

“Haiwezekani Halmashauri ya Mafia ikaacha kufuata fumula ya uchukuaji wa ‘service levy’ uliowekwa na Serikali na kutengeneza utaratibu wake yenyewe..mwisho wa siku watu wa nje tunachoweza kukielewa ni njama inayowekwa baina ya Halmashauri na Mwekezaji kuiibia Serikali” alisema Mpina.

“Kwanini mkokotoo huo usizingatie sheria takwimu za makusanyo zipo, bei inayotumika kuuza na masafirisho ya nje ipo kwanini haikutumika kukokotoa..kwanini itumike fumula ya kukubalina nje ya utaratibu uliowekwa kwa mujibu wa sheria”alihoji Waziri Mpina.

Waziri Mpina alisema kama halmashauri inatoza fedha nyingi zaidi za ushuru wa huduma tofauti na iliyowekwa kwenye Sheria ni makosa kwani Serikali haiwezi ikatoza fedha ambazo haziko kwenye utaratibu wa sheria lakini kama halmashauri inakusanya fedha kidogo kuliko sheria inavyosema nalo ni kosa kwa mujibu wa sheria.

“Kwanini uchukue fedha kidogo wakati fomula ya kupata makusanyo halisi kwa niaba ya wananchi ipo..kwanini wewe utumie fumula ya kwako ya kubuni wewe wakati fumula ya kisheria ipo”alihoji Waziri Mpina.

Mbali na dosari hizo za ukwepaji kodi, Waziri Mpina alielezea kusikitishwa kwake na kitendo cha mwekezaji huyo kushindwa kuwashirikisha wananchi wanaozunguka eneo hilo kujifunza teknolojia hiyo ili kukuza sekta ya ukuzaji viumbe maji hasa ufugaji wa Kambamiti.

Alisema Serikali haijapokea maombi yoyote ya upungufu wa wataalamu wenye utaalamu na uzoefu maalum kuendesha mradi kwani wataalamu hao wanazalishwa katika vyuo vyetu kikiwemo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) na Vyuo vya Wakala wa Elimu na Mafunzo ya Uvuvi (FETA).

“Mradi huu unaendeshwa kwa usiri na wivu mkubwa kiasi kwamba wananchi wa kawaida hawawezi kupata utaalamu kupitia mradi huu..kwenye taarifa yenu sikuona mkichukua vijana wanaomaliza vyuo au kuingia makubaliano na vyuo (MOU) kufanya mafunzo ya vitendo kwenye mradi huu na kuwalipa kima cha chini cha mshahara”alihoji Waziri Mpina.

Alisema wawekezaji kutoka nje wanapofika nchini wanalojukumu katika mikataba yao ya kusambaza taaluma katika eneo lao la uwekezaji ili kuwawezesha watanzania wengi kunufaika na uwekezaji wao na kueleza kusikitishwa kwake na kampuni hiyo kuwabagua wazawa na kuwapa nafasi wageni hata kwenye kazi ambazo zingeweza kufanywa na watanzania.

“Toka nimeanza kutembelea miradi hii kuanzia Dar es Salaam nimekuja kwenye shamba la kambamiti na kituo cha kutotoleshea vifaranga mapokezi na utolewaji wa maelezo na ufafanuzi unafanywa na wageni hii ni ishara kwamba uongozi wote umeundwa na wageni au ni sehemu ya kuficha ukweli juu ya undeshaji wa biashara hiyo’ alihoji Waziri Mpina

Mbali na hilo Waziri Mpina alisema Serikali inazo taarifa za vijana wanaokwenda kufanya kazi kwenye uwekezaji huo wanashindwa kufanya kazi kutokana na ujira mdogo wanaolipwa na mwekezaji huyo na kuvunjika moyo na kisha kuondoka.

“Kulipwa mshahara mdogo haijulikani wanalipwa hivyo ili wakate tamaa waondoke na baadae itengeneze nafasi ya ajira kutoka nje ya nchi au tatizo ni nini”alihoji Waziri Mpina.

Kwa upande wake Meneja wa Alphakrust, Ganeshan Vedagiri amelalamikia kukosa wataalamu wenye weledi na pindi watanzania wanapoajiriwa wanakaa muda mfupi na kuondoka huku akilalamikia kudaiwa ushuru kwenye halmashauri zaidi ya moja

Alisema mradi huo wa Mafia una mabwawa 31 ya Kambamiti ambapo kwa mwaka huzalisha wastani wa tani 400 huku asilimia 90 ya samaki hao wakiuzwa nchini ufaransa huku asilimia 10 zikiuzwa hapa nchini. 


Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mafia, Chuchu Silvery licha ya kuwepo kwenye ziara hiyo hakuweza kuzungumzia chochote kuhusiana na dosari hizo.
Share:

Simbachawene Agoma Kufungua Machinjio Ya Msalato jijini Dodoma

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. George Simbachawene hii leo amegoma kufungua machinjio ya Msalato jijini Dodoma kwa kutokidhi vigezo vya ubora vinavyoridhisha ikiwemo ukarabati wa kiwango cha chini na kutoa muda wa wiki ya moja kurekebisha dosari zilizobainika.
 
Ametoa uamuzi huo wakati akitembelea jengo la machinjio ya Msalato jijini Dodoma wakati wa ziara aliyoifanya na kubaini kasoro mbalimbali zinazotakiwa kupatiwa ufumbuzi. “Sifungui hii machinjio kwa sababu hamjajiandaa na ujenzi uko hovyo kwahiyo siwezi kufungua kitu cha hovyo namna hii” Simbachawene alisisitiza.
 
Akiongea katika ziara hiyo amesema amesikitishwa sana na ukarabati wa kurekebisha machinjio hayo kwani haukidhi viwango na ujenzi wake ni wa kiwango cha chini hivyo amemuagiza Afisa Mipango Miji wa Jiji la Dodoma Bwana Shabani Juma kuhakikisha ndani ya wiki ya moja kila kitu alichotolea maelekezo kifanyiwe marekebisho.
 
“Sijafurahishwa kwa kwakweli, majengo ya Serikali yanatakiwa kujengwa na mafundi classic, vitu vya Serikali viwe State of Art” Simbachawene alisisitiza.
 
Waziri Simbachene pia amegiza kuandaliwa kwa taarifa rasmi ya ukarabati huo ikiwa ni pamoja na thamani ya fedha zilizotumika katika zoezi zima la ukarabati na ujenzi wa  mifumo ya maji safi na maji taka.
 
Naye Diwani wa Kata ya Msalato Mheshimwa. Ali Mohamed amesema kuwa amesikitishwa sana kwa kutofunguliwa kwa machinjio hiyo kwani wakazi wengi wa Kata yake wanategemea machinjio kwa shughuli zao za kila siku kwa sababu ni Wafugaji. Pia alisema Maelekezo yote yaliyotolewa na Mheshiwa Waziri Simbachawene wameyapokea na naamini kuwa yatarekebishwa kwa wakati.
 
Machinjio hiyo ya Msalato ilifungwa na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimazi wa Mazingira (NEMC) tarehe 31 Oktoba 2019 kutokana na sababu za mazingira yasiyokua safi na salama, kufuatia ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira.


Share:

Bilioni 23.5 Zaokolewa na TANESCO Kila Mwaka

Na  mwandishi wetu - Dodoma
Shilingi Bilioni 23.5 zinaokolewa kila mwaka baada ya Serikali kupitia Shirika la umeme Tanzania (TANESCO) kuzima mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia mafuta mazito.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Jijini Dodoma kuhusu mafanikio ya Shirika hilo katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya tano, Mkurugenzi mtendaji wa Shirika hilo Dkt. Tito Mwinuka amesema kuwa Shirika hilo limefanikiwa kujiendesha bila kupokea ruzuku  kufuatia hatua zilizochukuliwa na Serikali ikiwemo kuzimwa kwa mitambo ya kuzalisha umeme kwa kutumia mafuta.

“Tumezima mitambo ya kuzalisha umeme kwa mafuta mazito katika maeneo ya  Makambako, Tunduru, Liwale, Namtumbo, Ludewa, Madaba  na kuyaunganisha na gridi ya Taifa hali inayochangia kuongeza kasi ya maendeleo katika maeneo hayo na kupunguza gharama za uendeshaji ;” Alisisitiza Dkt. Mwinuka

Akitaja baadhi ya mitambo iliyozimwa Dkt. Mwinuka amesema kuwa ni  ile ya IPTL, AGRECO, Syimbion na mingine  katika maeneo mbalimbali hapa nchini iliyokuwa ikitumia mafuta katika uzalishaji wa umeme.

Akifafanua amesema kuwa hali hiyo imechangia katika kuongeza mapato ya Shirika hilo kutoka Shilingi takribani trilioni 1.2 mwaka 2012 hadi kufikia zaidi ya trilioni 1.5 kwa mwaka kwa sasa hali inayoliwezesha Shirika hilo kuendelea kuongeza tija katika utoaji wa huduma.

Kwa upande wa wateja waliounganishiwa umeme wameongezeka kutoka milioni 1.6 waliokuwepo kufikia mwaka 2015 hadi zaidi ya milioni 2.7 kufikia mwaka 2019 sawa na ongezeko la wateja zaidi ya milioni 1.05 katika kipindi hicho ambao ni asilimia 63.84.

Akizungumzia miradi ya kimkakati Dkt. Mwinuka amesema kuwa ni pamoja na mradi wa kufua umeme wa Mwalimu Nyerere katika Mto Rufiji megawati 2115 unaotekelezwa na Serikali kwa gharama ya shilingi trilioni 6.55, Rusumo megawati 80, Kakono megawati 87, Mradi wa kuzalisha umeme kwa gesi mkoani Mtwara megawati 300.

Akieleza zaidi, Dkt. Mwinuka amesema kuwa miradi mingine inatekelezwa katika maeneo mengine katika mikoa mbalimbali hapa nchini kwa lengo la kuhakikisha kuwa kila mwananchi anafikiwa na huduma ya umeme.

Kwa upande wa Vijiji vilivyounganishiwa umeme vimeongezeka kutoka 2018 mwaka 2015 hadi Vijiji 8236 kufikia Desemba 2019 ikiwa ni ongezeko la asimia 67 hali inayotokana na jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano kuhakikisha kuwa wananchi wote wanafikiwa na nishati ya umeme katika maeneo yote.

Katika kipindi cha miaka 4 umeme ulioongezwa kwenye gridi ya Taifa ni Megawati 400 zinazotokana na utekelezaji wa miradi ya kimkakati ikiwemo ya Kinyerezi namba 1 na namba 2.

“Kwa upande wa wateja wa viwanda  wameongezeka kutoka 2571 mwaka 2015 hadi  3787 mwezi Desemba 2019;” Alisisitiza Dkt. Mwinuka

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetekeleza miradi mbalimbali ikiwemo ya uzalishaji, usambazaji na uwekezaji katika sekta ya nishati ili kukuza uchumi na ustawi wa wananchi.


Share:

PICHA: Ujenzi Wa Barabara Za Juu Makutano Ya Ubungo (Ubungo Interchange)

Maendeleo ya Ujenzi wa Barabara za Juu katika Makutano ya Ubungo (Ubungo Interchange). Mradi huo wa Ujenzi katika Makutano  ya Barabara za Mandela, Morogoro na Sam Nujoma (Ubungo Interchange) unaendelea kwa kasi kubwa na umefikia asilimia 65 kwa mradi mzima na sehemu ya gorofa ya pili ambayo itapitisha magari yanayotumia barabara ya Morogoro imefikia asilimia 75.

Mradi huo unatarajiwa kuondoa adha ya msongamano mkubwa katika makutano ya barabara hizo pindi utakapokamilika. PICHA NA IKULU


Share:

Je Wewe ni Mwanasiasa, Mfanyabiashara.?....Kutana na Sheikh Omary Mtaalamu wa Nyota

Je Wewe ni MWANASIASA, MFANYABIASHARA, MSANII Maigizo ama MWANAMZIKI ? tunazo PETE za BAHATI zenye uwezo mkubwa.
 
Nakuona Unavyo pata TABU sana katika MAHUSIANO yako ni KERO, SHIDA, DHIKI, TABU na MATESO kila kukicha ni Ugomvi Masimango. Huna hata Chembe ya Furaha kabisa.

Njoo umuone Sheikh Omary  na Ujuwe  yanayo Kusibu ni mtu Mkarimu mpenda Watu

Anatibu kwa Kutumia Qur_an
 
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1..

0746 753 790 Sheikh OMARY.


Share:

KIGWANGALLA: WALIPANGA KUNIANGAMIZA NA WALITAKA NITUMBULIWE UWAZIRI

Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt Hamis Kigwangalla, ameeleza kuwa kwa sasa anaishi kwa hofu na tahadhari kubwa juu ya uhai wake kutokana na kuwepo kwa kundi la watu wanaomuwinda wakitaka kumuangamiza huku wengine wakimfanyia mipango ya kumuharibia ili atumbuliwe uwaziri.


Kupitia akaunti yake ya instagram Kigwangala ameweka wazi kuwa hata alivyopata ajali aliwekewa ulinzi mkali wodini ili wabaya wake wasiweze kummalizia kwa namna yoyote.

Kupitia instagram yake ameandika hivi; Sikusudii kufanya press conference. Watu wengi wamenishauri niishie hapa. 

Team yangu imefanya kazi nzuri, imenipa uthibitisho wa majina ya wanaotaka nichafuliwe ili niondolewe uwaziri. 

Bahati mbaya hakuna cha kunichafua nacho, wanapika hadithi za kitoto na kurudia tu. Walidhani ningekaidi maelekezo ya Mhe. Rais juu ya mgogoro wa ndani ya Wizara yetu ili Rais achukie aniondoe, wakakwama. Sikukaidi. 

Wakaona wafanye mwendelezo kupitia gazeti, sijataka kujibishana nalo, tutakutana mahakamani ambapo mbivu na mbichi zitajulikana, ukweli utawekwa wazi na rekodi itakaa sawa. Sijashangaa kuwa wahusika ni wale wale wa kipindi kilichopita.

Hakuna jipya. Sababu ni deal yao binafsi, ambayo haitekelezeki bila ridhaa ya Waziri, na bahati mbaya kwao Waziri ni mimi; walitamani nisiwepo watafune pesa za serikali vizuri, wamekwama. 

Tutaendelea kudhibiti kimya kimya. Kwa wanaokumbuka wakati nimelazwa ICU na baadaye wodini, ilikuwa ngumu sana kunitembelea na kuniona. 

Paliwekwa ulinzi mkali sana na watu wote walizuiliwa kuingia isipokuwa kwa kibali cha Ikulu, hadi Mawaziri wenzangu hawakuruhusiwa. 

Nilishangaa sana lakini niliambiwa ndiyo hivyo. Baadaye nikaja kujua kuwa kuna watu walipanga njama za kuniua na hiyo ingeweza kuwa fursa kwao kunimalizia. 

Baada ya kuteuliwa tu Wizara hii kulizuka mtafaruku mkubwa sana juu ya usalama wangu, nilifuatiliwa kila kona mpaka serikali ikanipa walinzi, nilibisha kwa kuwa sipendi attention sana lakini nililazimishwa na kuambiwa nipo kwenye ‘threat’! Sikuwa na option. 

Nilianza kuishi kwa hofu na mashaka sana. Hivyo, baada ya ajali na yaliyotokea kutokea nililazimika kuwa makini zaidi. Imani yangu kwa kila mtu ilipungua. Nikawa ‘alert’ wakati wote. 

November 2019 nililetewa taarifa za kutisha, nikaongeza umakini. Team yangu imenisihi nisiweke majina hadharani na kwamba wanawafuatilia wahusika kwa ukaribu na watazijulisha mamlaka kwa hatua stahiki zaidi. Watu wa karibu sana na mimi nimewapa mpango na taarifa zote na wanajua cha kufanya endapo chochote kitanitokea. Kuna mbinu nyingi za mapambano. Tuendelee tu!

Share:

Tanzania Yapangiwa Kundi J Kufuzu Kombe la Dunia Qatar 2022

Timu ya Taifa ya Tanzania imepangwa Kundi J katika mechi za Kufuzu kwa Kombe la Dunia Qatar 2022 hatua ya makundi Afrika



Share:

Wafanyakazi wanne wa kampuni ya uwindaji ya Green Miles Wakamatwa na Polisi

Wafanyakazi wanne wa kampuni ya uwindaji ya Green Miles iliyoondolewa katika kitalu cha Lake Natron(east) wilayani Longido wanashikiliwa na polisi kwa madai ya kukaidi agizo la Serikali  kuondoka wa hiari katika kitalu hicho.

Wafanyakazi hao wamekamatwa na polisi leo Jumatano Januari 22, 2020 waliokuwa wameongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Longodo mkoani Arusha.

Wanatuhumiwa kuendelea na kazi katika kitalu hicho licha ya kutakiwa kuondoka Januari 20, 2020.

Katibu tawala Wilaya ya Longido, Toba Nguvila amesema baada ya wafanyakazi hao kukamatwa, eneo hilo litakuwa chini ya usimamizi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori (Tawa) kwa kushirikiana na polisi.

Ofisa wanyamapori wa kikosi cha kuzuia ujangili Mkoa wa Arusha, Emmanuel Pius amewataja wanaoshikiliwa kuwa ni kaimu meneja wa kambi ya Tandala, Lazaro Lembrise, Moses Sikange, Mohamed Bembe na  Hassan Mahonza.


Share:

Tanzania kujumuishwa kati ya nchi 7 zitakazowekewa vikwazo na Marekani

Serikali ya Marekani ina mpango wa kuziongeza Nchi nyingine 7 ikiwemo Tanzania kwenye orodha ya Nchi ambazo Raia wake wamewekewa zuio/vikwazo vya kuingia Nchini humo ambapo Nchi nyingine kwenye hizo 7 ni Nigeria, Sudan, Eritrea, Myanmar, Belarus na Kyrgyzstan.

Vyombo vya habari Marekani vimeripoti kuwa baadhi ya Nchi VISA zinaweza zisifungiwe kabisa bali zitakua ngumu kupatikana kwa masharti (za biashara na matembezi) Maafisa wamesema bado orodha haijakamilika kwani mpaka J'nne Ikulu ilikua inajadili kuongeza Nchi nyingine 1 au 2.

Ripoti hiyo imesema baadhi ya Nchi hizi 7 Raia wake wameongoza kwa kupitiliza muda wa kukaa Marekani kulingana na VISA walizopewa, kwa mwaka 2018 pekee 24% ya Raia wa Eritrea walipitiliza siku za kukaa Marekani, Raia wa Nigeria kwa asilimia 15, Sudan 12%. 

Leo Jumatano Januari 22, 2020 kaimu balozi wa Marekani, Dk Inmi Patterson akihojiwa na Redio Clouds amethibitisha suala hilo baada ya jana jioni taarifa za Tanzania na nchi hizo kuwekewa vikwazo kuanza kusambaa katika mitandao ya kijamii. 

Soma zaidi :https://www.nytimes.com/2020/01/21/us/politics/trump-travel-ban.html


Share:

Bunge la Seneti Marekani laidhinisha mpango wa kumuondoa madarakani Rais Trump

Baraza la seneti nchini Marekani limepiga kura kwa misingi ya chama na kuidhinisha sheria zitakazotumika katika kesi ya kumuondoa madarakani Rais Donald Trump. 

Baraza hilo lililo na idadi kubwa ya maseneta wa chama cha Republican limezikataa juhudi za Wademocrat za kupata ushahidi na kuhakikisha kwamba mashahidi wanasikilizwa. 

Wakili mkuu wa Trump katika kesi hiyo amesema kesi ya Wademocrat ni juhudi zisizo na msingi kutaka kupindua ushindi wa Trump katika uchaguzi wa mwaka 2016 ingawa mbunge mmoja wa chama cha Democratic amesema kuna ushahidi wa kutosha kuonyesha makosa ya Trump. 

Baraza la wawakilishi la bunge la Marekani lilipiga kura ya kumuondoa madarakani Trump mwezi uliopita kutokana na madai ya matumizi mabaya ya madaraka na kuzuwia mamlaka ya bunge la Congress kwa kuishinikiza Ukraine kumchunguza hasimu wake wa kisiasa ambaye ni makamu wa rais wa zamani Joe Biden wa chama cha Democratic. 

Trump anashikilia hakufanya makosa yoyote.


Share:

TMA yatoa tahadhali ya mvua kubwa katika mikoa mitatu

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania ( TMA) imetoa tahadhali ya mvua kubwa itakayonyesha katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma na kusini mwa Morogoro leo Jumatano Januari 22, 2020.

TMA imetoa tahadhali ya upepo mkali na mawimbi makubwa katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Pwani, Dar es Salaam, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.

Taarifa ya TMA iliyotolewa jana Jumanne Januari 21,2020 inasema mvua hizo  zinaweza kuleta athari ikiwamo uharibifu wa miundombinu na mali na makazi kuzunguukwa na maji.

Athari zingine zinazoweza kutokea hatari kwa maisha ya watu kutokana na maji kutiririka kwa kasi, ucheleweshaji wa usafiri na kusimama kwa baadhi ya shughuli za kiuchumi.

Kwa upande wa tahadhali ya upepo mkali na mawimbi makubwa TMA imesema athari zinazoweza kujitokeza katika mikoa hiyo kuathirika kwa shughuli za uvuvi, ucheleweshaji wa usafiri pamoja na kuanguka kwa majani na matawi ya miti.


Share:

Njombe:Mahakama yakamilisha kusikiliza ushahidi wa kesi ya mwanafunzi kuvunjwa uti wa mgongo

Na Amiri kilagalila-Njombe
Kesi namba 141-2019 inayomkabili mwalimu Focus Mbilinyi anayetuhumiwa kumvunja uti wa mgongo aliyekuwa  mwanafunzi wa shule ya msingi Madeke wilayani Njombe Hosea Manga baada ya kumpa adhabu ya viboko 10 kwa madai ya kukosa hesabu 10 imeendelea kusikilizwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Njombe kwa kukamilisha mahojiano na mashahidi wawili wa mwisho kutoka upande wa utetezi ambao ni wanafunzi wenza wa majeruhi huyo.

Akitoa utetezi mbele ya mahakama,Catheline Hongoli aliyekuwa kiongozi wa darasa la  Hosea Manga anasema machi 21 ,2017 mwalimu wa hesabu aliingia darasani na kuagiza wanafunzi ambao hawajafanya hesabu alizotoa kupita mbele ,ambapo miongoni mwa wanafunzi waliopita alikuwepo Hosea Manga ambaye aliadhibiwa viboko vitatu makarioni kwa kosa hilo.

Baada ya adhabu hiyo mwalimu alitoka darasani na Hosea Manga akaelekea chooni na kurejea akiwa darasani akiwa mzima na kisha baada ya muda mfupi akadondoka na kushindwa kusimama hali ambayo iliwasukuma wanafunzi kumwita mwalimu mkuu ambaye alimtoa na kumlaza nje ya darasa kijana Hosea Manga.

Shahidi wa pili na wa mwisho kwa upande wa uetetezi  Sephania Kyelula ambaye pia ni mwanafunzi mwenza wa kijana Hosea anasema kabla ya kupatiwa adhabu ya viboko vitatu Hosea Manga alikuwa na uwezo wa kutembea huku akidai kuwa na maumivu ya mguu lakini mapema baada ya kuadhibiwa alitoka na kwenda chooni na kisha kurejea darasani na muda mfupi akadondoka na kushindwa kuinuka.

Kesi hiyo inayoendeshwa na hakimu mkazi Ivran Msaki na kusimamiwa na mawakili watatu wa upande wa utetezi ambao ni Liliani Gama,Octavian Mbugwani na Innocent Kibadu imeahirishwa mpaka februali 4 itakaposikilizwa kesi ya majumuisho na kutajwa tarehe ya hukumu.


Share:

STAMICO Kuanzisha Mradi Wa Kusafisha Dhahabu Mwanza

Imeelezwa kuwa, Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) lipo katika hatua za awali za uanzishwaji wa Mradi wa Kusafisha Dhahabu (Gold Refinery) na tayari kampuni ya ubia ijulikanayo kama Mwanza Precious Metals Refinery Company Limited imeanzishwa.

Hayo  yamebainishwa  Januari 21, 2020 na Kaimu Mtendaji Mkuu wa (STAMICO) Dkt. Venance  Mwase wakati  akiwasilisha kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Taarifa  kuhusu Utekelezaji na Hali ya Upatikanaji wa Fedha za Maendeleo ya shirika hilo kwa  Kipindi cha Nusu Mwaka, kwa Mwaka wa Fedha 2019/2020 kwa niaba ya Waziri wa Madini.
 
Dkt. Venance ameileza kamati hiyo kuwa,  mradi huo utaendeshwa kwa ubia ambapo STAMICO itakuwa  na hisa asilimia 25 na mwekezaji asilimia 75, huku ikilelezwa kwamba, mradi huo  utakaojengwa jijini Mwanza utahusisha kujenga mtambo wenye uwezo wa kusafisha wastani wa kilo 200 hadi 500 kwa siku.
 
Ameongeza kuwa, makadirio ya fedha zinazohitajika ni Dola la Marekani Milioni 58.204 ambazo zimepangwa kwa ajili ya ununuzi wa mtambo wa kusafishia dhahabu, gharama za awali za mradi, kununua dhahabu kutoka katika masoko pamoja na gharama zaza uendeshaji na kuongeza‘’ Mheshimiwa Mwenyekiti tumepanga uwe mtambo wa viwango vya kimataifa,’’.
 
Aidha, Dkt. Mwase amesema kwamba katika kipindi cha Julai hadi Desemba, 2019, tayari mradi umetekeleza majukumu kadhaa ikiwemo kupata leseni ya kujenga na kuendesha mtambo huo, kusainiwa mkataba wa ubia pamoja na kuanza taratibu za uanzishwaji wa kampuni ya ubia na kupata eneo la ujenzi wa mtambo chini EPZA. 
 
Ameongeza majukumu mengine yaliyotekelezwa ni pamoja na kufanyika kwa Athari kwa Mazingira (EIA) kwenye eneo la mradi upembuzi yakinifu pamoja na kukusanya taarifa za upatikanaji wa dhahabu katika maeneo mbalimbali yanayokusudiwa.
 
Akizungumzia shughuli nyingine zinazoendeshwa na Shirika hilo amesema linaendelea kutoa huduma za Kibiashara za uchorongaji miamba wa biashara katika sekta ya mafuta na gesi ambapo katika Mwaka wa Fedha 2019/20  ambapo limefanikiwa kupata kandarasi 4 za uchorongaji kupitia zabuni mbalimbali  zenye thamani ya shilingi bilioni 2.2 .
 
Kuhusu Mgodi wa Stamigold ambao ni Kampuni Tanzu ya Shirika hilo ameieleza kamati hiyo kuwa, kuanzia Julai hadi |Desemba, 2019, mgodi huo umezalisha na kuuza wakia 7,133.00 za madini ya dhahabu na wakia 879.19 za madini ya fedha, vyote vikiwa na thamani ya shilingi 24,172,700,255.34.
 
‘’ Mhehimiwa Mwenyekiti, katika kipindi hicho, mgodi umelipa jumla ya shilingi 1,712,455, 550.91 kwa ajili ya malipo ya mrabaha, ada ya ukaguzi na kibali cha kusafirisha madini nje ya nchi,’’ ameeleza Dkt.  Venance.
 
Kuhusu mradi wa makaa ya mawe katika Mradi wa Kabulo na Kiwira, amesema jumla ya tani 4,359.10 ziliuzwa na kulipatia Shirika kiasi cha shilingi 17,558,184.76 na kuongeza kuwa, ‘’ shirika lilifanikiwa kulipa mrabaha, ada ya ukaguzi na tozo ya Halmashauri ya jumla ya shilingi 23,645,000.62
 
Aidha ameongeza kuwa Mgodi umeendelea kutoa ajira kwa Watanzania zaidi ya 400.
 
Kwa upande wake, Waziri wa Madini Doto Biteko wakati akitoa ufafanuzi wa hoja zilizoibuliwa na kamati, amewatoa Hofu Wajumbe wa kamati hiyo kuhusu Maendeleo ya Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) ambapo ameeleza pamoja na changamoto zinazolikabili, linakua na linafanya vizuri.
 
Waziri Biteko ameiomba Kamati hiyo kuendelea kuilea na kuishauri STAMICO  kwa kuwa mwelekeo wake ni mzuri na kwamba hivi sasa lina uwezo wa kuzalisha hadi shilingi Bilioni 20 tofauti na ilivyokuwa awali na kuongeza kuwa, Watendaji na Bodi ya Shirika hilo mara zote wanafanyia kazi ushauri unaotolewa na Kamati pamoja na Wizara.
 
‘’Mheshimiwa Mwenyekiti, itakuwa bahati mbaya sana kulifuta shirika hili. Linakua, wanaendelea vizuri na Wana Bodi nzuri, watendaji wanasikiliza ushauri na kuufanyia kazi na mapungufu yanafanyiwa kazi, naomba muendelee kuilea na kuishauri STAMICO,’’amesisitiza Waziri Biteko.


Share:

Halmashauri Uvinza Yamkera Naibu Waziri Mabula

Na Munir Shemweta, WANMM UVINZA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ameijia juu halmashauri ya wilaya ya Uvinza mkoa wa Kigoma kwa kushindwa kuihudumia idara ya ardhi na kusababisha watumishi wa idara hiyo kugharamia baadhi ya vifaa ili kutekeleza majukumu yao.

Hali hiyo ilibainika jana katika halmashauri hiyo wakati Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi akiwa katika ziara yake ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi katika mkoa wa kigoma.

Akiwa katika Masijala ya Ardhi ya halmashauri ya wilaya ya Uvinza, Dkt Mabula alibaini utunzaji majalada ya ardhi usiofuata taratibu huku baadhi ya hati zikiwa hazijakamilishwa kwa ajili ya kuwapatia wamiliki wa ardhi katika halmashauri hiyo tangu mwaka 2018.

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliwajia juu watumishi wa sekta ya ardhi katika halmashauri hiyo kwa kushindwa kutekeleza majukumu ipasavyo jambo alilolieleza kuwa linachangia uwepo migogoro ya ardhi sambamba na kuwanyima wananchi fursa ya kupata hati.

Dkt Mabula aliagiza hati zote ambazo taratibu zake zishakamilishwa ikiwemo wamiliki wake kusaini hati hizo kupelekwa Ofisi ya Kamishna Msaidizi wa Ardhi Kanda ya Magharibi ndani ya wiki moja  kwa ajili ya kukamilishwa na kupatiwa waombaji.

Hata hivyo, baada ya kuwajia juu watumishi wa sekta ya ardhi katika halmashauri ya Uvinza ndipo Afisa Ardhi wa halmashauri hiyo Manyama Makongo alipomueleza kuwa idara hiyo inashindwa kutekeleza majukumu yake kutokana na kukosa vifaa jambo lililosababisha kuamua kuchukua  ‘Printer’ yake binafsi na kuipeleka kwenye ofisi hiyo kwa ajili ya kusaidia kazi za idara.

Hali hiyo siyo tu ilimshutua na kumshangaza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi bali ilimsononesha kwa kuona watumishi wa sekta ya ardhi katika halmashauri hiyo wanatumia fedha zao za mifukoni kuendesha ofisi jambo alilolieleza kuwa halikubaliki.

‘’Hapa jitihada za ziada zinahitajika, halmashauri ipo inashindwa kuihudumia idara ya ardhi, halafu watumishi wanatumia fedha zao za mfukoni hili halikubaliki lazima niwasiliane na Waziri Jafo kuhusiana na suala hili’’ alisema Dkt Mabula.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri Mabula, idara za ardhi katika halmashauri nyingi nchini zimekuwa kama watoto wa kambo kutokana na wakurugenzi wa halmashauri kutozitengea bajeti ya kutosha jambo linalofanya idara kufanya kazi katika mazingira magumu.

Katika hatua nyingine Mkuu wa wilaya ya Mpanda mkoani Katavi Lilian Matinga na Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Enelia Lutungulu wamewaokoa Maafisa Ardhi wa halmashauri hiyo wasitumbuliwe kutokana na kushindwa kutekeleza majukumu yao ipasavyo ikiwemo kutokamilisha utoaji wa hati za ardhi kwa muda mrefu.

Walionusurika ni Afisa Ardhi Mteule wa Halmashauri ya Manispaa ya Mpanda Spear Mwalukasa ambaye ilielezwa yuko katika mafunzo  na  Afisa Ardhi Ezekiel Bichuro. Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula alisema kutokana na Maafisa hao kuzembea kukamilisha hati kwa muda mrefu basi hawafai kuendelea na nafasi zao kwa kuwa wanakwamisha utoaji hati ambao sasa unaweza kufanyika ndani ya mwezi mmoja pale taratibu zote zinapokuwa zimekamilika.

Hata hivyo, Mkuu wa wilaya ya Mpanda Lilian Matinga na Kaimu Mkurugenzi Enelia Lutungulu waliwatetea kwa kueleza kuwa maafisa hao hawana muda mrefu katika idara hiyo na makosa yanaweza kuwa yalifanywa maafisa waliopita.

Naibu Waziri Mabula alielekeza maafisa hao kupewa barua za onyo kwa kuwa muda wa miezi mitatu waliopo katika idara hiyo wangeweza kuonesha jitihada za kukamilisha hati na kuagiza hati zilizopo zikamilishwe katika kipindi cha mwezi mmoja.

‘’Ikifika tarehe 30 Januari 2020 hati ziwe zimeenda kwa wenyewe, haiwezekani mtu amesaini tangu 2015 halafu mpaka sasa hajapatiwa hati yake, wapo wazembe wachache  wanaochafua Wizara lazima wapewe warning. Alisema Naibu Waziri Mabula.

Naibu Waziri Mabula pia alitembelea wilaya ya Tanganyika ambapo alionesha kutoridhika na kasi ya ukusanyaji mapato yatokanayo na kodi ya pango la ardhi na kuagiza halmashauri ya wilaya ya Tanganyika kuongeza kasi katika makusanyo sambamba na kupanga, kupima na kumilikisha viwanja kwa wananchi.

Kwa mujibu wa Afisa Ardhi wa halmashauri ya wilaya ya Tanganyika Penina Simon kiasi cha shilingi milioni 18,069,179.40 kilikusanywa hadi kufikia nusu ya mwaka wa fedha 2019/2020.


Share:

Rais Magufuli: Uchaguzi ujao wa Tanzania utakuwa huru na wa haki

Rais  Magufuli amesema Serikali imejipanga kuhakikisha uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba, 2020 unakuwa wa amani, uhuru na haki.Amesema utakapofika uchaguzi huo, nchi na taasisi mbalimbali zitakaribishwa Tanzania kushuhudia.

Ametoa kauli hiyo jana Jumanne Januari 21, 2020 alipokutana na mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania katika sherehe za mwaka mpya 2020 na chakula cha jioni zilizofanyika Ikulu, Dar es Salaam.
 
Amebainisha kuwa uchaguzi ni jambo muhimu, Serikali imejipanga kuandaa mazingira mazuri katika uchaguzi huo.

“Oktoba mwaka huu wa 2020 nchi yetu itafanya uchaguzi mkuu, zoezi la uchaguzi ni muhimu kwa nchi yoyote inayofuata misingi demokrasia, Serikali imejipanga kuhakikisha kuwa uchaguzi mkuu unafanyika katika mazingira ya amani, uhuru na haki,” amesema Rais Magufuli.

Amesema ukikaribia uchaguzi huo nchi mbalimbali na taasisi za zitakaribishwa Tanzania kushuhudia

“Kama ilivyo kawaida yetu wakati ukifika tutazikaribisha nchi na taasisi mbalimbali kuja kuangalia uchaguzi wetu ili kujionea jinsi nchi yetu inavyokomaa katika nyanja ya demokrasia,” amesema Magufuli


Share:

Compliance Advisor Job at RTI International Dodoma Tanzania

RTI International is one of the world’s leading research institutes. We work with governments, businesses, foundations, universities, and other clients and partners to improve the human condition by turning knowledge into practice. Our staff of more than 5,000 tackles hundreds of projects to address complex social and scientific challenges facing our clients and the people and communities they… Read More »

The post Compliance Advisor Job at RTI International Dodoma Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger